Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Msukuma: Wanaolisema Vibaya Jeshi la Polisi Wanakosea....Siku Likiacha Kazi Watu Watabakana bila Kutongozana

0
0
Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Musukuma, amesema kwamba watu wanaomsema Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kuhusu watu wasiojulikana na wanao likashifu jeshi la polisi na kulituhumu kwa mambo yasiyofaa wanalikosea jeshi hilo, kwani bila wao tusingekuwa salama.

Musukuma ameyasema hayo jana alipokuwa akiongea na East Africa Television, na kusema kwamba iwapo jeshi la polisi likiacha kazi kufanya kazi hata kwa siku moja hakutakuwa na amani, kwani watu watafikia hatua ya kubakana bila kutongozana.

“Ilitengenezwa tu chuki kuwa watu wasiojulikana wanatumwa na Makonda, sijui na nani!! Mara polisi, hii dhana si nzuri, haya matukio yametokea sehemu nyingi, Kibiti huko, sijui wapi huko, ila mnalichafua tu jeshi la polisi , Siku jeshi la Polisi likisema liache kufanya kazi, hali itakuwa mbaya, hatutatongozana tutabakana.”, alisema Musukuma.

Sambamba na hilo Musukuma amesema watu wanaofanya hivyo hawako sahihi, kwani badala yake wanapaswa kulishukuru jeshi hilo kwa jukumu la kuwalinda wao na mali zao.

Msukuma: Kuna Baadhi ya Wizara Zinatia Kichefuchefu na Kila Nikiwaona Mawaziri Wake Natamani Kukimbia

0
0
Mbunge wa Geita Vijijini Mh. Joseph Musukuma amesema baadhi ya Wizara ni kichefuchefu na kuna Waziri hata akifumba macho akifumbua akamuona anakimbia kutokana na anavyofanya kazi zake katika Wizara anayoongoza ndio maana baadhi wamepata taabu kupitisha Bajeti zao Bungeni.

Akiongea jana Mei 23, kwenye kipindi cha Kikaangoni cha EATV , Musukuma aliwataja baadhi ya Mawaziri wanaozitendea haki Wizara zao kuwa ni Waziri William Lukuvi wa Ardhi na Ummy Mwalimu wa Afya.

''Unajua sio kila Wizara unachangia tu zingine zimekamilika hata Mawaziri wake waliposimama kusoma Bajeti zao ili zipitishwe hakuna aliyepinga, lakini kuna Waziri hata ukinifumba macho nikifumbua tu nikamuona nakimbia'', amesema.

Musukuma alisema baadhi ya Mawaziri wamekuwa wakifanya kazi kwa mihemuko ndio maana wao kama wabunge wanajitahidi kuwashauri wanapokuwa wameenda tofauti.

Aidha ameeleza kuwa kitendo cha Wabunge kushauri vitu kadhaa Bungeni hawamaanishi lazima wasipitishe bajei ila wanachofanya ni kushauri kisha kupitisha ili serikali ikafanyie kazi ushauri wao.

Wanawake 40 Kunyongwa Iraq

0
0
Serikali inatarajia kuwanyonga wachumba 40 wa wanamgambo wa Dola ya Kiislamu (IS) kulipiza kisasi kwa wapiganaji hao wa jihadi kuikalia kwa miaka mitatu ardhi ya Iraq wakati wa mapigano yaliyosababisha maelfu ya watu kuuawa kikatili.

Wanawake hao ambao ni wa kigeni walikiri mahakamani kwamba na wao ni waathirika wa IS, walipewa dakika 10 kila mmoja kutetea uhai wao kabla ya majaji kufikia uamuzi wapewe adhabu kali.

Wanawake hao walishutumiwa na mahakama ya Iraq na raia wa kawaida kwa kuwapa msaada waume zao wapiganaji waliosababisha maafa katika eneo walilokuwa wanakalia kuanzia mwaka 2014 hadi 2017.

Mwanamke mmoja mwenye uraia wa Ufaransa aitwaye Djamila Boutoutao, 29, alidai kuwa alidhani alikuwa anaolewa na mwanamuziki wa miondoko ya rap.

“Ni baada ya kuwasili Uturuki kwa ajili ya ‘mapumziko’ ya wiki moja ndipo nilipogundua ya kuwa mume wangu ni mpiganaji wa kijihadi,” alisema Djamila.

“Mimi ni mwathirika. Mume wangu alinipiga na kunifungia kwenye pango na watoto wangu nilipokataa kumfuata (hadi Iraq).’

Djamila ni mmoja wa raia wa Ufaransa wapatao 1,900 na wasafiri wa kigeni wanaokadiriwa kuwa 40,000 waliosafiri hadi Syria na Iraq kujiunga na miliki ya khalifa.

Katika hukumu yake ya hivi karibuni, ambako aliomba asitenganishwe na binti yake, Djamila aliwaambia waandishi wa habari wa gazeti la The Guardian: “Nachanganyikiwa hapa. Nakabiliwa na adhabu ya kifo au kifungo cha jela maisha. Hakuna anayeniambia chochote, si balozi wetu wala watu ndani ya gereza.”

“Jamani nawasihi msiwaache waondoke na binti yangu. Niko tayari kuwapa fedha endapo mtawasiliana na wazazi wangu. Tafadhali niokoeni.”

Takriban wanawake 40 ndio wamehukumiwa kifo na watu wengine 300 wenye mafungamano na IS wameshauawa.

Babu Tale Apelekwa mahabusu kwa muda usiojulikana

0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imemwamuru mkurugenzi wa kampuni ya Tiptop Connections Company Limited, Hamis Shaban Taletale maarufu kwa jina la Babu Tale, kukaa mahabusu katika kituo cha Polisi akisubiri amri ya kupelekwa kifungoni.

Mahakama hiyo katika uamuzi uliotolewa na Naibu Msajili, Wilbard Mashauri Februari 16, iliamuru Babu Tale na ndugu yake Idd Shaban Taletale wakamatwe na kupelekwa kifungoni baada ya kushindwa kutekeleza hukumu yake.

Hukumu hiyo iliyotolewa na Jaji Agustine Shangwa Februari 18, 2016, iliwaamuru ndugu hao kumlipa fidia ya Sh250 milioni, Mhadhiri wa Dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde kwa makosa ya kutumia mahubiri yake kibiashara bila ridhaa yake.

Kutokana na amri hiyo ya kuwakamata, Babu Tale alitiwa mbaroni juzi na jana alipelekwa mahakamani hapo kwa ajili ya amri ya kumpeleka kifungoni, lakini alilazimika kurudishwa mahabusu Kituo Kikuu cha Polisi kwa kuwa Naibu Msajili aliyetoa amri ya kuwakamata hakuwepo.

Amri hiyo ya kumrejesha rumande ilitolewa na naibu msajili wa mahakama hiyo, Ruth Massam hadi hapo Naibu Msajili Mashauri aliyetoa amri ya kuwafunga atakaporejea kutoka Dodoma alikokwenda kikazi.

Kwa kuwa haijulikani ni lini atarejea, Babu Tale ambaye pia ni meneja wa msanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya, Abdul Nassib maarufu kama Diamond Platnum, atalazimika kukaa mahabusu kwa muda usiojulikana mpaka atakaporejea.

Hati ya kuwakamata Babu Tale na ndugu yake ilitolewa April 4, mwaka huu kutokana na maombi ya Sheikh Mbonde kupitia wakili wake Mwesigwa Muhingo.

Sheikh Mbonde aliwasilisha maombi hayo baada ya Babu Tale na nduguye kushindwa kutekeleza hukumu hiyo, yaani kumlipa kiasi hicho walichoamriwa na Mahakama wala kubainisha mali za kampuni yao, au zao binafsi, ili zipigwe mnada kulipia fidia hiyo.

Katika kesi ya msingi, Sheikh Mbonde aliieleza Mahakama kuwa Juni 6, 2013 aliingia makubaliano na kampuni hiyo ili irekodi mawaidha yake na kuziuza kisha wagawane faida, lakini baada ya kurekodi masomo saba, walimwambia kuwa walikuwa wameachana na mpango huo.

Alieleza kuwa baadaye alibaini kuwa mikanda ya video ya mfumo wa DVD zenye mawaidha yake zilikuwa zikiuzwa katika mikoa mbalimbali huku zikiwa na majina na namba za simu za wakurugenzi wa kampuni hiyo, ndipo akafungua kesi hiyo.

Baada ya Sheikh Mbonde kuwasilisha maombi ya kuwafunga jela Babu Tale na nduguye, mahakama ilimwelekeza Sheikh Mbonde kuwalipia wafungwa hao watarajiwa pesa za chakula mahakamani na kumtaka pesa kwa ajili ya matumizi mengine kuziwasilisha gerezani.

Kwa mujibu wa Mahakama, gharama za kuwahudumia wafungwa hao wakiwa gerezani ni kama ifuatavyo:

Vifaa ambavyo ni taulo ya kuogea Sh12,000; godoro Sh40,000; mto wa kulalia Sh10,000; chandarua Sh13,000; mashuka manne Sh48,000; kandambili (malapa) Sh3000; mswaki na dawa ya meno Sh2,000 ambazo jumla ni Sh128,000 kwa mtu mmoja na kwa watu wote wawili ni Sh256,000.

Chakula, kifungua kinywa Sh7,000; chakula cha mchana Sh8,000; maji lita tatu 3,000, jumla Sh18,000 kwa mtu mmoja kwa siku na kwa wote wawili ni Sh36,000. Wote kwa mwezi ni Sh1,080,000.

Pia, kuna fedha za tahadhari kiasi cha Sh800,000 kwa kila mfungwa na kwa wote wawili jumla ni Sh1,600,000.

Sheikh Mbonde alisema kuwa tayari ameshawalipia wafungwa hao fedha za chakula ya mwezi mmoja kiasi cha Sh1,080,000 na kusema ataendelea kuwalipia kiasi kama hicho kila mwezi.

Alisema fedha za matumizi mengine kama yalivyoainishwa na mahakama, ziko tayari na kwamba hizo ataziwasilisha kwa uongozi wa gereza baada ya wafungwa hao kufikishwa huko.

Musukuma amkana Bashe Sakata la Kutekwa na Usalama wa Taifa

0
0
Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma Kasheku, amefungukia madai yaliyowahi kutolewa na Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe, kwamba walitekwa na watu wa usalama wa Taifa ni ya uongo na kwamba kilichotokea walikamatwa na askari na mbinu zilizotumika ni zile wanazofundishwa bungeni.

Musukuma ametoa kauli hiyo jana  wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha Kikaangoni kinachorushwa na  EATV , ambapo alifafanua kwamba walikuwa wakidhaniwa kufanya uhalifu.

Musukuma alisema kwamba "Mara ya kwanza kulala polisi nimelala nikiwa mwana- CCM, mara ya kwanza Dodoma, mara ya pili ni Geita, na nilikubali kwa sababu wala hatukutekwa, nilikuwa na kina Bashe, nilimsikia rafiki yangu Hussein Bashe alisema tumetekwa, hatukutekwa".

"Tulikamatwa tukapelekwa polisi, tukapekuliwa, tulipoonekana hatuna hatia tukaachiwa , hatukutekwa. Sikumjibu Hussein Bashe aliposema tumetekwa kwa sababu sikuwepo, nasema hapa hatukutekwa," Musukuma.

Aprili 11, 2017 Mbunge wa Nzega Mjini(CCM) Hussein Bashe aliwataka wabunge kuacha unafiki kuhusu Usalama kuwateka watu na kwamba yeye ni mmoja wa watu waliokamatwa wakati wa mkutano Mkuu wa CCM.

"Mimi nimekamatwa na kuteswa na Usalama wa Taifa. Nimenyanyaswa sana nchi hii. Ikibidi mnifukuze CCM - " alisema Bashe wakati Waziri wa Tamisemi,(kabla hajaenguliwa katika nafasi hiyo) George Simbachawene kumtaka Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuthibitisha kuwa matukio ya ukamataji yanafanywa na usalama wa Taifa.

Sugu Ampongeza Mwandosya kwa Kumtembelea Gerezani

0
0
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu Sugu (Chadema), ameliambia Bunge kuwa wakati akiwa gerezani, alipokea salamu kutoka kwa viongozi na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) huku akimpongeza Prof. Mark Mwandosya kwa kuwa mwana CCM pekee aliyekwenda kumsalimia gerezani.

Akichangia bungeni jijini Dodoma jana mjadala wa makadirio ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka ujao wa fedha, Sugu aliwapongeza viongozi na wabunge wa CCM kwa kumtumia salamu gerezani huku akidai wengi wao waliogopa kwenda kumjulia hali.

Hata hivyo, Sugu alisema CCM waliwakilishwa vizuri na waziri wa zamani Prof. Mwandosya ambaye ndiye pekee wa chama tawala hicho aliyefika gerezani kumjulia hali.

Mbunge huyo ambaye jana alikuwa wa kwanza kuchangia mjadala huo, pia alitumia fursa hiyo kutoa pole kwa wananchi wa Mbeya ambao alidai waliungana naye kutumikia kifungo hicho.

"Nawashukuru watu wote waliopaza zauti zao kulaani kifungo dhidi yangu," alisema Sugu katika maneno yake ya utangulizi kabla ya kujikita katika hoja iliyokuwa bungeni.

Mbunge huyo mwanzoni mwa mwaka huu alihukumiwa kifungo cha miezi mitano gerezani baada ya kukutwa na hatia kisha kuachiwa wiki mbili zilizopita kwa msamaha wa Rais.

Katika mchango wake jana, Sugu alisema matukio ya uhalifu na vifungo dhidi ya wanasiasa kama yeye yanayotokea nchini yanawafanya baadhi ya wawekezaji kuogopa kuja kuwekeza nchini.

Alisema pamoja na kwamba Tanzania inaweza kuwa na jitihada za kuwashawishi wawekezaji kutoka nje kuwekeza nchini, mkakati huo huenda usifanikiwe kwa kuwa wawekezaji wanapenda kuwekeza katika nchi zenye usalama kuliko nchi zenye vurugu na mauaji.

Sugu pia alimshauri Rais aanze kusafiri kwenda nje ya nchi akisisitiza kuwa safari za nje zina faida kama ilivyokuwa enzi za uongozi wa Rais mstaafu Jakaya Kikwete aliyekuwa akisafiri mara kwa mara.

“Pamoja na hayo, serikali haiwatendei haki Watanzania wanaoacha kazi nje na kuja kufanya kazi nchini kwa sababu inataka iwalipe mishahara midogo kama ilivyotokea kwa bosi mmoja wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)," Sugu alisema.

Mwanamke Amuua Mumewe kwa Kisu...Ni Baada ya Kugoma Kumpikia Chakula Kisha Ugomvi Ukaibuka

0
0
Sophia  Salehe, mkazi wa Kata ya Namiongo, Newala mkoani Mtwara, anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo, kwa tuhuma za kumuua mume wake kwa kumchoma kwa kisu.

Mauaji hayo yalitokana na ugomvi baina ya mtuhumiwa ambaye inadaiwa kuwa alikataa wito wa mumewe kupika chakula baada ya kutokushiba.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Lucas Mkondya, amesema tukio hilo lilitokea juzi mkoani humo.

Kwa mujibu wa Mkondya, mwanamume huyo alikufa papo hapo baada ya kuchomwa kisu na mke wake.

Alisema siku ya tukio majira ya saa 1:30 usiku, mwanamke huyo alimwandalia mume wake chakula na kumpatia.

“Kile chakula kilikuwa kidogo, mume wake, Ahmed Salim, alimtaka arudi jikoni kwa ajili ya kupika tena chakula kwa kuwa hakikumtosha. Hapo ndipo palitokea ugomvi wakalumbana na wakaendelea kugombana na mkewe akachukua kisu na kumchoma kifuani,” alisema Kamanda Mkondya.

Kamanda Mkondya alisema Salim alifariki dunia papo hapo baada ya kutokwa na damu nyingi kwenye jeraha.

Aidha, alisema katika tukio hilo wanamshikilia na mwanaume mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe kutokana na uchunguzi unaoendelea.

Alisema wanamshikilia kijana huyo kwa kuwa katika tukio hilo alikuwapo, hivyo watakapopata maelezo yatakayojiridhisha kutohusika ataachiwa.

“Bado huyu kijana tunamhoji ni kwa nini hakutoa msaada wa kuamua ugomvi huo. Hapa tunataka kujua na yeye amehusika au la na kwa huyu mwanamke taratibu zikikamilika atafikishwa mahakamani,” alisema.

Aidha, Kamanda alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Newala kwa ajili ya kusubiri taratibu za mazishi.

Uhusiano Kati Ya Punyeto Na Kusinyaa/kudumaa Kwa Maumbile Ya Kiume.

0
0
Wanaume  wanao  jihusisha  na  upigaji  wa  punyeto  kwa  muda  mrefu  husalia  kuwa  na  maumbile  ya  kiume  yaliyo sinyaa  na  kudumaa.

Kwa mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  huathiri  na  kuharibu  mishipa  na  misuli  ya  uume na  hivyo kusababisha  kujengeka  kwa  mafuta na  tishu  zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri na  hivyo  kuzuia  mishipa ya  ateri  kupanuka na  kuongezeka  pamoja  na  damu  kutiririka  kwenda  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili yanapotokea  huathiri  uzalishaji  wa homoni muhimu  zinazo  husika  na ukuaji wa misuli ya  uume, na hatimaye  hufanya  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa, kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama wa  mtoto.

 Homoni  hizo hujulikana   kitaalamu kama  HGH  na  huzalishwa  kwenye  ini.

Sababu nyingine   inayo  tajwa  na  wataalamu  ni kwamba, mtu  anaye fanya punyeto   hutumia  akili,  nguvu na  nishati  nyingi sana, jambo ambalo  huathiri utendaji  wa  ogani  nyingine  muhimu  katika  mwili , likiwemo  ini.

Na kwamba  ini  linapo kosa  nishati   ya kutosha  hushindwa  kufanya kazi  zake  vizuri  na  moja  kati  ya  kazi kubwa  za  ini  ni  pamoja  na  uzalishaji  wa  homoni  zijulikanazo  kitaalamu kama  HGH  ambazo  kama  ilivyo andikwa  hapo juu, zinahusika na  kuchochea  ukuaji  wa  sehemu mbalimbali  katika  mwili  wa  mwanadamu  ikiwemo   misuli  ya  uume.

Mbali na  kuathiri  utendaji  wa  ogani  nyingine  mwilini, upigaji  punyeto  husababisha  athari nyingine  kwenye  mwili wa  mwanadamu  kama  vile uchovu  sugu  wa mwili  pamoja na kunyonyoka kwa  nywele.

Athari nyingine  za  upigaji punyeto  ni  pamoja  na  kupoteza  kumbukumbu, kuwahi  kufika  kileleni  ambako  husababishwa  na  kulegea  kwa  mishipa  ya  ateri, kushindwa  kurudia  tendo  la  ndoa, kukosa  hamu  ya  tendo  la  ndoa, uume  kusimama  katika  hali  ya  ulegelege,   maumivu  wakati  wa  tendo  la  ndoa  husuani  wakati  wa  kurudia  tendo  la pili na    mara  baada  ya  tendo  la  ndoa  la  kwanza.

KWANINI   WATU WENGI  WANAO  JIHUSISHA  NA  UPIGAJI  PUNYETO  WANA  MAUMBILE  MADOGO  YA  KIUME YALIYO  DUMAA, SINYAA  NA  KURUDI NDANI.

Uzeofu  unaonyesha  kuwa,  asilimia  kubwa  ya  wanaume  ambao  wamewahi  kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu, wanakabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  maumbile  ya  kiume yaliyo dumaa, sinyaa  na  kurudi ndani.

SABABU  KUBWA   NI  HII  HAPA
Sababu  kubwa  ni kwamba   vijana wengi  wa  kiume, huanza  kujihusisha  na  punyeto   wakiwa  na  miaka  kumi  na sita , kumi na  saba  au  chini  ya  hapo.

Hiki ni  kipindi  ambacho  vijana  hawa  ndio  wanakuwa  wamebalehe.

Na kwa mujibu  wa  tafiti  za kisayansi, katika  kipindi  hiki cha  balehe  ndio  kipindi  ambacho  homoni za  HGH  ambazo huhusika  na  ukuaji  wa  sehemu  mbalimbali  za  mwili  ikiwemo  maumbile ya  kiume, huzalishwa  kwa wingi.

Kama  tulivyo ona  hapo  juu, upigaji  punyeto  huathiri  uzalishwaji  wa   homoni  hizo.

Mwisho wa  siku  maumbile  ya  kiume  ya  wahusika, hushindwa  kukua  na  kuishia  kudumaa na  kusinyaa.

Na  hii ndio  sababu  kubwa  wanaume  wanao  kabiliwa  na  tatizo hili  husalia  kuwa  na  maumbile yenye  ukubwa  ule  ule  walio kuwa  nao wakati wa  kubalehe

NINI  TIBA  ASILIA  YA  TATIZO  LA  KUDUMAA, KUSINYAA  NA  KURUDI NDANI KWA  MAUMBILE  YA  KIUME.

Kama uume wako  umedumaa, sinyaa, legea, nywea  na  kurudi ndani  kwa  sababu  ulifanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  na  unataka  kuondokana  na  hali  hiyo. HII  NI HABARI NJEMA  SANA  KWAKO!

Ipo dawa  ya ASILI   ambayo  HUTIBU  na  KUPONYESHA  KABISA  tatizo la  KUDUMAA, KUSINYAA, KUNYWEA  NA  KURUDI NDANI  KWA MAUMBILE  YA  KIUME kunako  tokana  na  ufanyaji  punyeto  wa  muda  mrefu.

Ni  dawa  ya  asili  kabisa ambayo  hutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la kudumaa  na  kusinyaa  kwa  uume  ndani ya siku thelathini.

JINSI YA  KUPATA  TIBA  HII : Kupata  tiba  hii  fika  ka6ika  duka  la  kuuza  dawa  za  aslili  la  NEEMA  HERBALIST. Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

Kwa wateja  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam  ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  ofisini  kwetu  watapelekewa  dawa mahali  walipo  ( HOME & OFFICE  DELIVERY )  na kwa  wateja  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar  Es  Salaam watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  mabus  au  boti  kwa  waliopo  Zanzibar.

Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  :  0766  53 83 84  au  0693  005 189.

Na  kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee  kila  siku  kupitia  blogu yetu :


Mwigulu Aagiza BodaBoda Zilizokamatwa na Polisi Ziachiwe Mara Moja

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ameagiza pikipiki zote (bodaboda) ambazo zinashikiliwa na polisi kwa makosa madogo ziachiwe mara moja na wahusika wapewe nafasi ya kwenda kutafuta faini wakiwa na vyombo vyao.

“Naagiza kuanzia leo na nitapita kuangalia maeneo mbalimbali pikipiki ambazo hazihitajiki kwenda mahakamani kwa ajili ya kutolea ushahidi nataka ziachiwe mara moja ili kuwapatia wenye mali,” amesema Dk Mwigulu.

Awali, Spika Job Ndugai alimtaka Waziri huyo kufanya sensa ya kutosha na kujionea namna ambavyo vijana wengi wamekuwa wakipoteza mali zao kwa kukamatwa na polisi katika maeneo mbalimbali katika makosa madogo tu.

Ndugai amesema Serikali inapoteza fedha nyingi kupitia kwa waendesha bodaboda na kuwafanya wengi kuwa maskini huku akitolea mfano wa kituo kikuu cha polisi cha mkoa wa Dodoma ambapo amesema kuna pikipiki zaidi ya 300 zinashikiliwa lakini hazina makosa makubwa.

Awali, Mbunge wa Mpwapwa (CCM) George Lubeleje aliomba mwongozo wa Spika kuhusu suala la faini kwa madereva wa bodaboda na kumtaka kutoa maagizo kwa jeshi la polisi ili kupunguza kamatakamata hiyo.

Lubeleje amesema polisi wamekosa huruma kwa vijana wa Tanzania ambao wamekuwa wakilia kwa kushilikiliwa vyombo vyao bila makosa makubwa na hivyo akaomba waruhusiwe kwenda kutumia pikipiki hizo kutafuta faini wanazodaiwa na polisi.

Spika Ndugai: Wizara Ya Fedha Ijitathmini

0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai ameitaka Wizara ya Fedha na Mipango, ijitathmini baada kushindwa kupeleka kwa wakulima wa korosho fedha za tozo za mauzo ya nje ya zao hilo.

Akizungumza bungeni jijini Dodoma leo Mei 24, amesema kinachofanywa na wizara hiyo hakiwezi kukubaliwa kwa sababu kinaathiri zao la korosho nchini alipokuwa akijibu mwongozo wa kutaka kuahirisha bunge ulioombwa na Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye (CCM) aliyetaka bunge lisitishe shughuli zake na kujadili suala la serikali kutotoa fedha hizo kwa wakulima wa korosho.

Nape amesema: “kutopelekwa fedha hizo kumesababisha bei ya mbolea aina ya sulphur kupanda kutoka Sh 16,000 hadi 75,000”.

Akiunga mkono hoja hiyo Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo) amesema kutopelekwa kwa fedha hizo kunatokana na utaratibu wa serikali ya awamu ya tano kutofuata sheria zinazopitishwa na bunge.

Akijibu miongozo hiyo, Spika Ndugai amesema suala hilo liachwe ili alifikishe kwa Waziri Mkuu kwa hatua zaidi.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Hawa Ghasia amesema hatua zilizochukuliwa na kamati yake juu ya hoja hiyo ya Nape.

Lakini pia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri , Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama alisema hoja hiyo ya Nape inahitaji mjadala zaidi ingawa serikali imeshatoa Sh bilioni 10 kwa ajili ya zao la korosho.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

0
0
MAKANGA 3 POWER; DAWA BORA NGUVU ZA KIUME
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.
 
Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.
 
Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.
 
Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.
 
Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.
 
Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.
 
Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.
 
Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Bilioni 53.8 zatengwa kwaajili ya mikopo ya wanawake na vijana

0
0
Serikali imetenga shilingi bilioni 53.8 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ikiwa ni fedha kwa ajili ya Mfuko wa Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu katika Halmashauri zote nchini ambazo zitagawiwa kwa njia ya mikopo kupitia vikundi mbalimbali.

Hayo yameelezwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri TAMISEMI, Joseph Kakunda alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Handeni, Omar Abdallah Kigoda aliyehoji juu ya kiasi gani Serikali inasimamia suala la asilimia 5 ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya Vijana na Kinamama.

“Serikali imeendelea kuhakikisha Halmashauri zote nchini zinatenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu. Katika mwaka wa fedha 2016/2017 jumla ya shilingi bilioni 56.8 zilitengwa na Halmashauri zote nchini, jumla ya shilingi bilioni 17.5 sawa na asilimia 31 zilitolewa kwa vikundi vya Wanawake na Vijana” amesema Mhe. Kakunda.

Kakunda ameendelea kusema kuwa, katika mwaka 2017/2018 jumla ya shilingi bilioni 15.6 sawa na asilimia 27 zilikuwa zimetolewa ambapo jumla ya vikundi 8,672 vya wanawake na vijana vilipatiwa mikopo.

Aidha amesema kuwa, ili kuongeza uwajibikaji katika kutenga na kupeleka fedha za mfuko wa Wanawake na Vijana kwa vikundi husika, Serikali itaweka utaratibu katika sheria ya fedha (Finance Bill) ya mwaka 2018/2019 utakaohakikisha kwamba Halmashauri zote zinatekeleza kikamilifu agizo hilo.

Mzee wa Upako: Nampenda Diamond kwa sababu ni mnyenyekevu, simpendi Alikiba Ana kiburi

0
0
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo maarufu kwa jina la Mzee wa Upako, amemtaja msanii ambaye anamkubali kati ya Alikiba na Diamond pamoja na kutoa sababu zake.

Akiongea na kipindi cha Maisha Mseto cha Times FM, Mzee huyo wa Upako amesema anampenda sana Diamond kwa sababu ni mnyenyekevu lakini Alikiba ni kiburi.

“Mimi nampenda sana Diamond kwa sababu ni mnyenyekevu, Simpendi Alikiba kwa sababu ana kiburi, nadhani kwa sababu amekaa Kariakoo,” amesema Lusekelo.

Mchungaji huyo ameongeza kwa kusema, “Ukipigia simu Diamond anapokea kwa unyenyekevu ila Alikiba anapokea kwa maringo. Ndio maana Diamond amefika mbali.”

Jambazi Anayetumia Bunduki FEKI Asakwa na Polisi

0
0
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma limesema siku za kumkamata mtuhumiwa wa ujambazi anayeteka watu na kuwapora kwa kutumia bunduki bandia na kisu,  zinahesabika.

 Limesema kuwa mtuhumiwa huyo amenusurika kukamatwa mara mbili baada ya kuwekewa mtego na polisi.

 Akizungumza leo Alhamisi Mei 24, 2018 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Martin Ottieno amesema mtuhumiwa huyo  ambaye jina lake halisi halijulikani, anafanya uhalifu kwa kuteka watu na kuwapora mali zao katika barabara ya Kisili-Buhigwe kwenye pori la Kwitanga.

 Pori hilo lipo katikati ya kijiji cha Mahembe na Gereza la Kwitanga katika wilaya ya Kigoma.

 "Tunaendelea kumsaka na polisi wamemkurupusha mara mbili ikabidi adondoshe bunduki yake chini, kumbe ni ya bandia na ndio anayotumia kupora watu," amesema Ottieno.

 “Bunduki hizo bandia zimechongwa kwa kutumia mbao kiasi kwamba mtu akiitazama kwa mbali bila kuichunguza hawezi kutambua kama ni bandia.”

 Mtuhumiwa huyo anadaiwa kupora watu wanaopita barabarani wakiwa kwenye magari, pikipiki, baiskeli na watembea kwa miguu ambapo hunyang'anya simu za mkononi na fedha.

 Ottieno ameomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano wa dhati kwa askari ili iwe rahisi kumkamata jambazi huyo.

Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari,

0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:

KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1. MKEBE NO.1 Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo la kwanza bila kuchoka naitakufanya uwe na hamu ya kuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER
MKEBE NO 2 ni dawa ya kuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,

KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,
Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake, humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa pia ana pete za bahati ambazo zimetajilisha wengi.

SUPER POWER,
Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI

SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Bulaya Aitupia Lawama Serikali....Adai Imesababisha TANESCO Ifiilisike

0
0
Mbunge Bunda Mjini (Chadema), Ester Bulaya amesema Serikali ya Awamu ya Tano tangu ilipoingia madarakani Novemba 5, 2015 imelifanya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kushindwa kujiendesha kwa faida, kutaka ligawanywe.

Bulaya ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Mei 24, 2018 bungeni mjini Dodoma katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Nishati mwaka 2018/19.

Amesema kwa muda mrefu ripoti mbalimbali za kamati za Bunge, ikiwamo ya mashirika ya umma, zinaeleza namna Tanesco inavyojiendesha kwa hasara.

Amesema kabla ya Serikali hiyo haijaingia madarakani, Tanesco ilikuwa ikipata hasara ya Sh124 bilioni lakini baada ya kuingia madarakani Tanesco inapata hasara ya Sh346 bilioni inayotokana na upugufu wa maji na gharama za uendeshaji.

“Tanesco ina madeni ambayo yamepanda kwa asilimia 23. Kabla Serikali hii haijaingia madarakani, Tanesco walikuwa na madeni ya Sh738 bilioni lakini baada ya kuingia yamefikia Sh958 bilioni na haya si maneno ya Bulaya. Ukiangalia ripoti ya CAG, inasema madeni hayana uhusiano kati ya Tanesco na mali, kwa maana nyingine Tanesco imefirisika,” amesema Bulaya.

Amesema wakati madeni haya yanatokea, kulikuwa na ushauri na mikakati mbalimbali ya kuligawanya shirika hilo ili kutenganisha usambazaji na uzalishaji.

“Leo hii tusingekuwa tunazungumza umeme wa vibaba wakati tunataka Tanzania ya viwanda. Wakati haya yanafanyika, Tanesco inashindwa kukusanya madeni makubwa, Tanesco inaidai Hospitali ya Tumaini Dola milioni 9.4 za marekani sawa na Sh18 bilioni na ni kodi ya pango,” amesema.

“Kodi hii ni tangu mwaka 1998 haijawahi kulipwa, kulikuwa na kesi mahakamani na Tanesco ikashinda na mahakama imeitaka kuondoka lakini mpaka sasa haijachukua hatua zozote.”

Mbunge huyo pia alihoji kitengo cha wizara hiyo kutenga Sh700 bilioni kwa ajili ya mradi wa umeme wa Stiegler’s Gorge badala ya fedha hizo kuzipeleka Rea (Wakala wa Umeme Vijijini) na Tanesco.

“Mkiona wengine tunasema hivi mjue yametuchosha timizeni wajibu wenu acheni mbwembwe ndogondogo,”amesema.

Jaji Mkuu Awataka Viongozi na Watendaji wa Mahakama Kutenda Haki

0
0
Na Beatrice Lyimo- MAELEZO, DODOMA
Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma amewataka viongozi mbalimbali wa mahakama ikiwemo Naibu Wasajili, Mahakimu, Watendaji, Wakuu wa Idara na Vitengo kutenda haki kwa watumishi walio chini yao.

Jaji Mkuu ameyasema hayo leo Mkoani Dodoma wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa baraza la wafanyakazi wa mahakama Tanzania.

“Sisi kama wasimamizi wakuu wa haki nchini tunawajibu mkuu wa kutenda haki kwa watumishi kwa vitendo, ni ukweli usiopingika kwamba kimbilio la mtumishi yeyote aliyefikwa na matatizo ni kwa kongozi wake katika sehemu yake ya kazi, hivyo basi kila kiongozi anapaswa kufungua milango kwa watumishi waliopo chini yake” amesema Jaji Mkuu.

Jaji Mkuu ameongeza kuwa, ubora wa viongozi unapimwa kwa namna wanavyosaidia wafanyakazi walio chini yao, hivyo kuwataka viongozi hao kutokufunga milango yao kwa watumishi wanaowaongoza.

Aidha, Jaji Mkuu amebainisha baadhi ya mafanikio ya kushirikisha wafanyakazi kwa lengo la kukuza motisha na kuleta ufanisi katika maeneo ya kazi na kuongeza tija katika uzalishaji.

“Umihimu wa kushirikisha wafanyakazi usilenge tu katika mabaraza haya ya wafanyakazi bali uwe endelevu ili wafanyakazi wajione ni sehemu ya mabadiliko yanayoonekana” amebainisha Jaji Mkuu.

Hata hivyo Jaji Mkuu ametoa rai kwa viongozi hao kufanya kazi kwa upendo, kutoa taarifa mbalimbali kwa wafanyakazi hali itakayopelekea kupunguza baadhi ya migogoro katika maeneo ya kazi.

Mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa Mahakama Tanzania umewashirikisha wajumbe kutoka kanda zote na menejimenti ya Mahakama Tanzania.

Mapori Matano Ya Akiba Mkoani Kagera Na Geita Kupandishwa Hadhi Ya Kuwa Hifadhi Za Taifa (National Parks)

0
0
Wizara ya Maliasili na Utalii imetangaza kuanza mchakato wa kuyapandisha hadhi Mapori ya Akiba ya Burigi, Kimisi, Biharamulo, Ibanda na Rumanyika kuwa Hifadhi za Taifa.

Mchakato huo tayari umeungwa mkono na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Hayo yameelezwa juzi bungeni Jijini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla wakati akihitimisha mjadala wa bajeti wa makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

“Mheshimiwa Spika, ninaomba kulitaarifu Bunge lako tukufu kuwa  Mhe. Rais ameridhia ombi letu la kupandisha hadhi Mapori ya Akiba ya Burigi, Kimisi, Biharamulo, Ibanda na Chief Rumanyika kuwa Hifadhi za Taifa, kipekee namshukuru sana Mhe. Rais kwa kuridhia ombi letu hilo” amesema Dkt. Kigwangalla.

Amesema kufuatia hatua hiyo, wizara yake inaanzisha mchakato rasmi wa kukamilisha taratibu  za kupandisha hadhi mapori hayo ili kupanua wigo wa vivutio vya utalii katika kanda ya Kaskazini Magharibi na hivyo kufikia azma ya Serikali kuongeza idadi ya watalii kufikia milioni 8 na mapato ya dola za kimarekani bilioni 16 katika kipindi cha miaka 7 ijayo.

Inaelezwa kuwa mchakato huo utapitia hatua mbalimbali ikiwemo kuwashirikisha wadau husika kupata maoni yao, mapendekezo kuwasilishwa baraza la mawaziri kabla ya kujadiliwa bungeni na hatimaye kuwasilishwa kwa Mhe. Rais kwa ajili ya kuidhinishwa kuwa Sheria kamili ya kupandisha hadhi mapori hayo.

Akizungumzia mikakati mingine mipya ya kuboresha sekta ya maliasili na utalii itakayotekelezwa, Dkt. Kigwangalla amesema ni pamoja na kuanzisha mamlaka ya usimamizi na uendelezaji wa utalii wa fukwe nchini, kuhuisha maeneo ya vivutio vya Mambo ya Kale na kuviunganisha katika ‘package’ moja ya utalii na vivutio vya wanyamapori.

Mikakati mingine ni kuunda mfumo mmoja funganishi wa TEHAMA uitwao “MNRT Portal” kwa ajili ya kutoa leseni na vibali, ukusanyaji wa takwimu na mapato kutoka vyanzo mbalimbali vya sekta ya maliasili na utalii, ambapo utaunganishwa na mifumo mingine ya Serikali iliwemo GePG, NIDA, TIRA, BRELA, TRA na NBS.

Amesema mikakati mingine ni kuanzisha Jeshi Usu, Utambulisho wa Utalii wa Tanzania Kimataifa ujulikanao kama “Tanzania, Unforgettable”, kufungua utalii wa kanda ya kusini, kuanzisha mwezi wa maadhimisho ya Urithi wa Mtanzania “Urithi Festival”  (Septemba), kuhuisha sheria za TANAPA, TAWA na TFS, pamoja na kuunda kanuni mpya za kusimamia vizuri sekta hizo.

Pori la Akiba Burigi lina ukubwa wa kilomita za mraba 2,941 katika wilaya za Karagwe, Muleba na Ngara mkoani Kagera, wakati Pori la Kimisi likiwa na ukubwa wa kilomita za mraba 1,030 katika wilaya za Ngara na Karagwe mkoani humo.

Pori la Akiba Biharamulo lina ukubwa wa kilomita za mraba 731 katika wilaya ya Muleba mkoani Kagera na wilaya ya Chato mkoani Geita, huku Pori la Akiba Ibanda likiwa na ukubwa wa kilomita za mraba 200 na Pori la Akiba Rumanyika kilomita za mraba 800 katika wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera.

Mapori haya yapo katika ukanda muhimu wa kuunganisha watalii kutoka ikolojia za Magharibi na Mashariki ambapo uwanja wa ndege wa Chato utakuwa muhimu katika kutoa mawasiliano.

Mapori hayo ambayo yanasimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – TAWA sasa yatakuwa chini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania – TANAPA punde baada ya mchakato wa kuyapandisha hadhi kukamilika.

Bunge limeidhinisha Sh. bilioni 115.794 kwa ajili ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo Sh. bilioni 85.816 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Sh. bilioni 29,978 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya May 25

Wakili wa Seth, Rugemalila Aulalamikia Upande wa Mashitaka kwa Kuchelewesha Upelelezi

0
0
Wakili wa utetezi katika kesi inayowakabili Harbinder Seth na James Rugemalira, ameutaka upande wa mashtaka ufanye kazi kwa mujibu wa sheria, taratibu na Katiba kwa kujali haki za washtakiwa ili kesi iendelee na kwamba ndani ya siku 14 ueleze upelelezi umekamilika, kama haujakamilika; washtakiwa waachiwe huru.

Wakili Didas Respicius, amesema hayo wakati akiwasilisha malalamiko katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa washtakiwa hao wamefikisha mwaka mmoja gerezani na upelelezi wa kesi inayowakabili bado haujakamilika.

Wakili huyo ameyasema hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Iman Mizizi kueleza upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Didas amedai kuwa washtakiwa hao walifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani Juni 19, 2017 wakiwa na mashtaka ambayo yanadhaminika lakini wakiwa katika kuwasilisha maombi ya dhamana, walibadilishiwa mashtaka ambayo hayana dhamana.

Amesema tangu mwaka jana hadi sasa upande wa mashtaka unadai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika, kwamba kuwa kwa mujibu wa hati ya mashtaka washtakiwa hao wanadaiwa kutenda makosa hayo, mwaka 2013.

Pamoja na hayo Wakili Mizizi amesema Katiba ndiyo inayotumika kutunga sheria na ndiyo iliyotumika kuwafunguliwa mashtaka washtakiwa .

Baada ya kusikiliza hoja zote, Hakimu Shaidi amesema amezingatia hoja zote na akashauri upande wa utetezi kupeleka maombi Mahakama Kuu kwa ajili ya kupata maelekezo ya sheria ambazo zinalalamikiwa na zile zinazowafunga mikono.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 7, 2018 kwa ajili ya kutajwa.

Sethi na Rugemarila wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu , kughushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kusababisha hasara ya Dola 22 milioni za Marekani.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images