Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tibaijuka: Kwa Hili Serikali ni Lazima Iwajibike.....Utawala wa Sheria Uheshimiwe

0
0
Mbunge wa Muleba Kusini(CCM), Profesa Anna Tibaijuka ameitaka serikali ya awamu ya tano iwajibike kuwanunulia ng'ombe wafugaji walioshinda kesi zao Mahakamani kama sheria inavyosema nasio vinginevyo.

Prof. Tibaijuka ametoa kauli hiyo jana  Mei 22, 2018 Bungeni Jijini Dodoma kwenye kikao cha 34 mkutano wa 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akichangia bajeti ya Wizara ya Maliasiri na Utalii ya mwaka 2018/19 ambayo ni shilingi 115.8 bilioni baada ya kuwepo tatizo la muda mrefu kwa wafugaji kuporwa mifugo yao na watu wa maliasili pindi wanapokuwa wamevamia hifadhi kwa lengo la kulisha mifugo yao.

"Serikali hii ya awamu ya tano naishukuru sana walitoa miezi 10 kwa Mawaziri humu ndani Bungeni kutafuta ardhi za wafugaji lakini hiyo kazi haikufanyika kilichotokea watu walikuja kuondolewa kwenye hifadhi kama operesheni na kwa kweli yalikuwa mateso makubwa sana. Mhe. Spika ni utawala wa sheria kama mtu ameshinda mahakamani na anatakiwa arudishiwe mifugo yake ni lazima afanyiwe hivyo na kama haipo lazima inunuliwe, serikali hapo inatakiwa kuwajibika", alisema Tibaijuka.

Pamoja na hayo, Prof. Tibaijuka aliendelea kwa kusema "kuwajibika hakuwezi kuwa sehemu ya wananchi pekee yake bali na serikali yenyewe lazima iwajibike pale ambapo kosa limefanywa na watendaji wake".

Kwa upande mwingine, Profesa Anna Tibaijuka amesema hawezi kuiunga hoja iliyokuwa mezani mpaka pale suala lake litakapopatiwa majibu yenye kuridhisha.

Je Wajua Saa Zenye Moyo Kama Wa Binadamu

0
0
NDio najua bado kichwani mwako unajiuliza saa zenye moyo wa binadamu kivipi? basi mwandishi wa makala hii ndo kazi yangu kukupa majibu na elimu kuhusu saa zenye moyo...


Tuanzie hapa msomaji saa zenye moyo kwa lugha sahihi ya kiswahili ni saa ambazo hazitumii battery yaani kiingereza automatic watch/mechanical watches....katika ulimwengu huu wa saa basi saa hizi ndo zilikuwa za kwanza kugunduliwa saa hizi ziligunduliwa na peter henlein wa mji wa nuremberg ujerumani....wakati saa za mabattery ziligunduliwa mwaka 1955 yaani quartz watch huko japani ..... baada ya historia fupi hiyo ngoja sasa tuone uchawi wa mzungu huyu peter henlein alifanyaje saa hizi hazitumii battery tutamia lugha nyepesi kila mtu asomae makala hii aelewe na video nitaweka
 
1.SAA HIZI HUPATA NGUVU UNAPOTIKISA MKONO WAKO
chazo kikubwa cha nguvu za saa hizi huwa mtu alivaa saa hii akiwa anatembea anavyotikisa mkono basi saa hizi kama unajua wana fikia hapa wataelewa saa hii huchukua motion energy na kuifadhi nguvu hii kwenye spiringi kuu (main spring)yaani saa hii uko zako mishe mishe zako unatembea ..na yenyewe inakuwa bize inachaji jinsi unavyotisa mkono.....
 
2. INA GIA
mi ndo maana nasemaga wazungu bwana kwenye ugunduzi ni watu hatari saa hizi bwana zina mfumo wa gia ...gia hizi bwana zinafanya kazi kwa waledi wa hali ya juu yaani kubadilisha nguvu ya mtetemeko wa mkono wako na kuziifadhi kwenye spiring kuu yaaani huu sasa NDO HUITWA MOYO wa saa yaani ukizima na saa inasimama kana kwamba binadamu moyo ukizima nae anakufaaa....lakini saa hizi moyo huu wa saa ni kwamba ukitisaa tu mkono na moyo wa saa unaanza kufanya kazi ...ngoja niwekee mfano saa ya kampuni t winner ambayo nayo ni moja ya SAA AMBAYO INA MOYO
basi ndugu msomaji hii kwenye video hapo juu ni moja kati ya mfano saa nyingi ambazo hazina mabattery ..kama utakuwa ni mdadisi wa mambo utakuwa umeangalia vizuri umeona kama kitu kama cha mvirigo kinatikisika kwa spidi basi ule ndo moyo sasa wa saa
 
3.HAZIINGII MAJI
basi saa hizi bwana ili kutunza ule moyo wake yaani springi kuu usichoke kufanya kazi hizi saa bwana huwa ni rafiki na maji yaani ukupita mvuani sawa tu hazina shida .....pia saa hizi wafanyakazi hasa wa POSTA huzipenda sana koz zinaongezea muonekano hata mimi hapa kama mwandishi wa habari hii saaa ni ninayo ina skeleton mechanical watch bofya jina hapo kuiona unaweza nunua hapo pia niliko nunua mimi mwandishi wako
 
4.UTAPATA WAPI SAA HIZI NA KWA SIFA ZIPI ILI UPATE ORIGINAL
ili upate original sifa ya kuangalia ni muda gani springi kuu ina uwezo wa kutunza chaji muda mara nyingi huwa ni masaa 48 bila kuguswa mara nyingi watu huagiza kwenye mitandao kama AMAZON wa marekani au pia POSTA kuna maduka huuza saa hizi za automatic pia kuna njia nyepesi kuna HUU mtandao wa daresalaamshop.com ambao personally nakurecommend ukanunue hawa unagiza na unaletewa ulipo TANZANIA nzima hawa majamaa huwa ni original na utalipia mzigo ukifika kitu umekiona usikose utamu wa saa hizi pia ndugu msomaji kuna link chini hapo bofya buy now kuweka order,,, mpaka siku nyingine kwenye makala zingine ASANTE
 
IMEANDIKWA NA
robnson kayaula kutoka twigaz news

Rais wa TLS, Fatma Karume akutana na kufanya majadiliano na IGP Sirro

0
0
Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Fatma Karume amemtembelea mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro ofisini kwake akieleza wamejadiliana mambo manne yanayohusu masuala ya sheria na haki.

Wakati Fatma akieleza hayo jana, msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa alisema: “Alikuja kujitambulisha kuwa yeye ni rais wa TLS. Ilikuwa ziara ya kawaida na binafsi, hapa tunapokea wageni wa kila aina.” 

Fatma ameyataja mambo waliyojadiliana kwakina na IGP Sirro kuwa ni wanasheria kutobughudhiwa wanapokuwa kwenye vituo vya polisi, hali ya usafi na usalama wa mahabusu wawapo rumande, haki ya maandamano na uhuru wa polisi kufanya uamuzi bila kushinikizwa na wanasiasa.

Fatma ambaye ni wakili wa kujitegemea alichaguliwa kuongoza TLS Aprili 14, akichukua mikoba ya Tundu Lissu aliyemaliza muda wake wa uongozi.

Alisema wanasheria wamekuwa hawatendewi haki wanapokuwa katika vituo vya polisi kutetea wateja wao.

Fatma alisema ni haki ya kila raia kuwa na mwanasheria anapopata tatizo la kisheria na ni haki ya wanasheria kutimiza majukumu yao bila kuingiliwa.

Pia, alisema walijadiliana kuhusu usafi wa mahabusu na kutojaza watuhumiwa kwenye vyumba vidogo.

Alisema alizungumzia haki ya wananchi kuandamana na umuhimu wa kufanya hivyo.

Kuhusu uhuru wa polisi kufanya kazi bila kuingiliwa alisema: “Natambua kuwa sheria ya mfumo mzima wa Jeshi la Polisi haijakaa sawa, ingekuwa amri yangu ingebadilishwa ili kuwe na usawa katika utendaji na wao wafanye kazi zao bila kuingiliwa na wanasiasa.”

“Nchi zilizoendelea wakuu wa polisi wanateuliwa na kamati, lakini sheria za nchini wanateuliwa na Rais, jambo ambalo linawawia vigumu kufanya kazi kwa kujitegemea,” alisema Fatma.

Alisema anatambua hilo lipo nje ya uwezo wa Polisi, hivyo kitu pekee wanachopaswa kufanya ni kuhakikisha wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria.

Fatma alisema IGP Sirro aliwaomba kuelimisha wananchi kuhusu sheria, kutambua haki zao na wajibu wao katika kuzitekeleza.

“Nimelichukua hili, tutatafuta majukwaa kuhakikisha tunatoa elimu kwa jamii kuhusu sheria, namna ya kuzitekeleza na wajibu wao,” alisema Fatma.

Zanzibar Yaagiza Walimu 300 Wa Sayansi kutoka Nigeria

0
0
Serikali ya Zanzibar imeagiza zaidi ya waalimu 300 wa masomo ya Sayansi kutoka nchini Nigeria ambao tayari wameanza kuwasili visiwani humo.

Kwa mujibu wa serikali ya Zanzibar, waalimu hao wanaoingia kwa awamu, na wanatarajiwa kuziba pengo la uhitaji wa zaidi ya waalimu 300 wa masomo hayo.

Naibu waziri wa Elimu Zanzibar Mmanga Mjengo amesema ujio huo utasaidia kuamsha pia morali ya waalimu wengine wa masomo ya sayansi visiwani humo.

Ameongeza pia wameamua kwenda Nchini Nigeria kwa sababu kuna wingi wa waalimu na wenye ubora na haikuwa rahisi kuchukua kutoka nchi za karibu kwa sababu na wao pia wana tatizo la uhaba wa waalimu.

''Mchakato wa upatikanaji wa waalimu hawa hufanywa kwa kutegemea uwezo wao katika ufundishaji na pia ubora wa kazi zao.'' alisema waziri Mjengo.

Serikali ya Zanzibar imesisitiza kuwa sio mara ya kwanza kwa ujio kama huu kwani katika miaka ya nyuma waalimu hawa wamekua wakija kwa kujitolea.

Ujio wa waalimu hawa ambao watakuwepo kwa kipindi cha miaka miwili unatajwa kupunguza uhitaji wa zaidi ya waalimu 300 visiwani humo.

Mashine Ya CT-Scan Muhimbili Yaharibika

0
0
Hospitali  ya Taifa Muhimbili (MNH), imekiri kuharibika kwa moja ya mashine zake za CT-Scan hali inayolazimu wagonjwa kupimwa kwa kutumia mashine moja ambayo ni mpya.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja wa Muhimbili, Aminiel Aligaesha alithibitisha kuharibika kwa mashine hiyo jana.

“Ni kweli mashine yetu moja ya CT Scan, ile ambayo ilikuwa inatumika kwa muda mrefu hapa hospitalini imeharibika si chini ya miezi mitatu sasa,” alisema.

Eligaesha alisema hivi sasa madaktari wanalazimika kuwafanyia uchunguzi wagonjwa katika mashine mpya iliyonunuliwa na Serikali miaka miwili iliyopita.

“Hii mpya haina tatizo lolote, MOI (Taasisi ya Mifupa Muhimbili), wanatarajia kufunga CT-Scan mpya, tutakuwa tunashirikiana nao kuwachunguza wagonjwa,” alisema.

Alipoulizwa iwapo pamoja na ushirikiano huo, Muhimbili itanunua mashine mpya nyingine ya CT-Scan, alisema hawana mpango huo kwa sasa.

“Mashine hizi ni gharama kubwa mno, ni kati ya Sh. bilioni mbili hadi tatu hivi, kwa kuwa MOI watafunga, tutaendelea kushirikiana nao pamoja na yetu kusaidia wagonjwa,” alisema.

Kim Jong-un azidi kumvuruga Trump

0
0
Rais wa Marekani, Donald Trump ametilia shaka kuhusu kufanyika kwa mkutano na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un mwezi june mwaka huu huko Singapore.

Ameyasema hayo mara baada ya Korea Kaskazini kutishia kujiondoa katika mkutano huo endapo Marekani itaendelea kusimamia msimamo wake wa kuiwekea vikwazo nchi hiyo.

Aidha, Rais Trump hakuweka wazi ni masharti gani ambayo yamewekwa kwa ajili ya mkutano huo,na alipoulizwa na waandishi wa habari juu ya masharti aliyoiwekea Korea Kaskazini amesema kuwa suala la kuachana na silaha za nyuklia ni lazima litekekelezwe na Korea Kaskazini.

Mkutano kati ya rais Trump na Kim Jon-un uanatarajiwa kufanyikwa June 12 nchini Singapore ukitanguliwa na mkutano wa marais wa Korea hizo mbili uliofanyika mwezi April.

Hata hivyo, ameongeza kuwa mwelekeo wa Kim Jong-un umebadilika baada ya ziara yake ya pili mwezi huu nchini China.

Bajeti Maliasili na Utalii yapita, mradi wa Stigle’s Gorge watikisa

0
0
Sakata la mradi wa umeme wa Stigler’s Gorge ambao utekelezaji wake unafanyika katika pori la akiba la Hifadhi ya Selous, liliibuka tena bungeni jana jioni Mei 22, 2018 na kuzua mvutano  huku Spika Job Ndugai akieleza kutoridhishwa na majibu ya Waziri wa Maliasili na Utalii.

Suala hilo lilitikisa Bunge jana mchana baada ya wabunge kadhaa kuhoji utekelezaji wa mradi huo, kueleza athari za kimazingira zinazoweka kujitokeza.

Selous ni miongoni mwa mapori yanayotambuliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu na Utamaduni (Unesco) kama sehemu ya urithi wa dunia, lakini uamuzi wa Serikali kuzalisha zaidi ya megawati 2,100 ikitumia zaidi ya Dola 2bilioni (zaidi ya Sh4.5trilioni) unaelezwa kuwa huenda ukaliondoa pori hilo kwenye orodha hiyo.

Bunge lilipokaa kama kamati jana jioni kupitisha bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii mwaka 2018/19 ya Sh115bilioni, mbunge wa Ulanga (CCM), Godluck Mlinga alianza kwa kuhoji kama Serikali itakuwa na mkakati mzuri wa kuwasaidia wananchi wanaoishi katika maeneo hayo.

Hoja ya Mlinga iliungwa mkono na Ndugai aliyeitaka Wizara ya Nishati kuwa makini na kutengeneza utaratibu wa kupanda miti katika maeneo mbalimbali yanayoanzishwa miradi ya umeme.

Ndugai amesema katika maeneo mengi Wizara hiyo imekuwa na utaratibu wa kukata miti mingi katika utekelezaji wa miradi lakini inakosa usimamizi wa upandaji miti mingine.

“Mheshimiwa Mlinga  naamini kuwa wamekuelewa lakini na ninyi Nishati lazima muwe na mipango mizuri ya kupanda miti katika miradi yenu. Haiwezekani unakata miti lukuki lakini hakuna mpango wa kuipanda hiyo haikubariki kabisa,” amesema Ndugai.

Ndugai ambaye pia aliungwa mkono na mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe kwa pamoja walipingana na majibu ya Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani kuhusu upandaji wa miti katika eneo hilo.

Wakati wawili hao wakitaka kusikia majibu ya Serikali kuhusu utunzaji wa mazingira katika eneo hilo, ikiwa ni sambamba na kupanda miti baada ya kuikata iliyopo, Dk Kalemani hakuwa akitoa majibu ya kina kuhusu hoja yao hiyo.

Katika majibu yake Dk Kalemani alisema miradi inayoanzishwa itakuwa na mipango mizuri hata ya uhifadhi wa mazingira, huku akijikita zaidi kueleza mpango wa kuongeza nguvu ya uzalishaji umeme nchini.

“Yaani Waziri hujatuelewa kabisa tunachotaka sisi ni hii  miti mingi mnayokata halafu mnakusanya na hampandi mingine, hivi hamjui habari ya uhifadhi kweli basi nimemaliza, nimemaliza waziri usisimame tena,” alisema Ndugai baada ya waziri huyo kuomba kujibu tena huku wabunge wakipinga.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Kangi Lugola alisema mradi huo hauna madhara kwa wananchi na Taifa kwa ujumla, akijitokeza mtu akaupinga atafungwa  bila huruma.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

TEMBELEA KATIKA BLOG YETU HAPA>>>;

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

0
0
MAKANGA 3 POWER; DAWA BORA NGUVU ZA KIUME
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.
 
Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.
 
Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.
 
Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.
 
Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.
 
Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.
 
Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.
 
Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Dawa Lishe Ya Kuongeza Na Kunenepesha Mwili

0
0
Je  umekonda  na  kudhoofu  mwili  wako  kwa  sababu  ya  kuugua  maradhi  mbalimbali  au  kwa  sababu  ya  msongo  wa mawazo  ?

Unataka  kurejesha   mwili  na  afya  yako  katika  hali  yake  ya  awali ?  Kama  jibu  lako  ni  NDIO  basi  HII  NI HABARI  NJEMA  SANA  KWAKO.

Tunayo  DAWA  LISHE  YA  ASILI  ambayo  inasaidia  kurejesha   afya  na  mwili  wa  mtu  alie  dhoofu    kwa sababu  ya kuugua  magonjwa  na  maradhi  mbalimbali  au  kwa  sababu  ya  msongo  wa  mawazo.

Dawa  hii  ya  asili  itarejesha  afya  na  mwili  wako  ndani  ya  muda  wa  siku  thelathini.

Na  kama  wewe  ni   MWEMBAMBA   na  unataka   KUONGEZA  MWILI  na  KUNENEPA  basi  DAWA  LISHE  hii ndio  JAWABU  LAKO.  Dawa  hii  itafanya  mwili  wako  uongezeke  na  kunenepa  ndani  ya  siku  thelathini.

Ni  dawa  ya  asili  kabisa ( pure  herbal ) isiyo  na  kemikali  yoyote  ya  viwandani  na  inapatikana  kwa  gharama  utakayo weza  kuimudu.

Kupata  dawa  hii  fika  katika  duka  la  NEEMA  HERBALIST  linalo patikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA  jirani na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL   HOUSING.

Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba    0766  53  83  84    au  0693 00 51 89.

Kwa  wateja  wasio  na  nafasi  ya  kufika  ofisini  kwetu, tunayo  huduma  ya  kuwapelekea  dawa  mahali  popote  walipo ndani  ya  jiji  la  DAR  ES  SALAAM.

Na kwa  taarifa  zaidi kuhusu  dawa  mbalimbali za  asili  pamoja   na huduma  zetu  kwa ujumla  , tutembelee  kupitia  blogu yetu:

Gigy Money Aomba Radhi Baada Ya Kumchana X Wake Hadharani

0
0
Mwanamuziki wa Bongo fleva Gift Stanford maarufu kama Gigy Money ameomba radhi baada ya ugomvi wake na Baba mtoto wake Mo J.

Gigy Money alimtolea maneno makali Ex wake ikiwemo kuweka wazi kwenye Interview aliyofanya na Millard Ayo kuwa mtoto wake Myra sio wa Mo J kwani alikuwa na mwanaume mwingine.

Gigy Money na Ex wake Mo J walirushiana maneno makali baada ya Gigy kumtuhumu kuwa hakuwa akimtunza kipindi cha ujauzito na kudai alihama na kila kitu baada ya kuachana.

Baada ya sakata hilo Mo J aliongea na vyombo vya habari na kudai kuwa ana uhakika kuwa mtoto wao ni wa kwake ingawa Gigy kwa ajili ya hasira anampa  mtoto mpenzi wake wa sasa.

Baada ya povu hilo Gigy Money ameibuka na kuomba radhi kwa maneno aliyoongea huku akidai ilikuwa ni hasira ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram ameweka ujumbe huu:

Mzee wa Upako Ampigia Simu Q-Chief ,Ni Baada ya Kusikia Anaacha Muziki.

0
0
Baada ya kuweka wazi dhamira yake ya kuacha muziki, msanii Q Chief amesema amepigiwa simu na watu wengi mmoja wapo ni Mchungaji Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’

Muimbaji huyo amesema kuwa Mzee wa Mpako alionyesha kuguswa na hatua hiyo aliyoamua kuichukua.

“Nimepokea simu kutoka kwa mtu kama Anthony Lusekelo, usiku saa tisa, unaweza kuona ni jinsi gani mchungaji anaweza kuguswa na kusema mwanangu nimetaka kama kulia hivi, nimepigiwa simu na maostadhi wakubwa sana Tanzania hii,” Q Chief ameiambia Clouds TV.

Ameongeza kuwa amefikia maamuzi hayo na hana kinyongo chochote na mtu ila kwa sasa ameona mapenzi makubwa sana kutoka kwa watu kwenda kwa Q Cheif.

Waziri Makamba Awatoa Hofu Watanzania mradi wa umeme wa Stiegler’s Gorge

0
0
Baada ya mradi wa umeme wa Stiegler’s Gorge katika Pori la Akiba la Hifadhi ya Selous kutikisa Bunge, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba amewataka Watanzania kutulia na kubainisha kuwa tathmini ya mradi huo inafanyika.

Makamba ametoa kauli hiyo leo Jumatano Mei 23, 2018 wakati akihojiwa katika kipindi cha Power Breakfast kinachorushwa na Redio Clouds.

Jana bungeni mjini Dodoma mradi huo ulikuwa gumzo wakati wabunge wakijadili bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii ya mwaka wa fedha 2018/19, ambapo baadhi ya wawakilishi hao wa wananchi akiwemo Nape Nnauye (Mtama) na Zitto Kabwe (Kigoma Mjini), walitaka tathmini ifanyike kabla ya kuanza kwa mradi huo.

Wamehoji kitendo cha Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kutangaza tenda ya kukata miti katika pori hilo, tenda inayohusisha ukataji miti zaidi ya mita za ujazo 3,495 na kwamba idadi ya miti inayokatwa ni sawa na ukubwa wa Mkoa wa Dar es Salaam huku ikijulikana  wazi kuwa tathmini bado haijakamilika.

Katika maelezo yake ya leo, Makamba amesema  tathmini inafanyika ili kujua athari  na namna ya kukabiliana nazo, “lazima sheria ifuatwe ikiwamo kufanya tathmini ya athari ya mazingira, ndicho kinachofanyika hivi sasa kuhusu mradi huo.”

“Tanesco walikuja NEMC (Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira)  kusajili mradi wa Stigle’s Gorge ili kufanya tathmini ya mazingira. Baada ya kuandikisha Tanesco walimchagua mshauri ambaye ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa sababu ni kazi ya kisayansi.”

Makamba amesema tayari shirika hilo limeshapeleka ripoti katika ofisi yake baada ya kufanya tathmini hiyo na kinachofuata ni NEMC  kutuma timu kwa ajili ya kujiridhisha kuhusu yaliyoandikwa katika mradi na yanayoonekana kama ni kweli.

Amesema baada ya hapo kamati ya ufundi ya ushauri itazungumza  na wadau wote katika eneo la mradi na kuthibitisha taarifa zilizopo kuhusu mradi husika.

Halima Mdee ataka wenye vyeti feki kuonewa huruma

0
0
Mbunge wa Kawe (Chadema),  Halima Mdee ameitaka Serikali kuwa na huruma na watumishi wake iliowaondoa kazini baada ya kubainika kuwa na vyeti feki.

Mdee ametoa kauli hiyo bungeni mjini Dodoma leo Jumatano Mei 23, 2018 wakati akiuliza swali la nyongeza, kubainisha kuwa  kuna watumishi waliotumia vyeti vya watu wengine kujiendeleza kielimu na wamefanya kazi kwa uadilifu mkubwa.

Hata hivyo, Waziri wa Nishati, Angellah Kairuki ambaye wakati wa uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma ukianza alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora) amesema hakuna malipo wala huruma yoyote itakayotolewa kwa wafanyakazi hao.

" Mdee mdogo wangu na dada yangu wewe ni mwanasheria lazima ujue kuwa hakuna kitu kama hicho kwa hiyo Serikali haiwezi kuwalipa au kuwapa msamaha," amesema Kairuki.

Amesema kwa kuzingatia maelezo hayo, mjadala huo utakuwa umefungwa kwani waliostahili kurudi kazini walisharudishwa.

Mahiga: Watanzania Waishio Nje Hutuma Fedha Nyingi

0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Augustine Mahiga amesema Watanzania waishio nje ya nchi wanatuma zaidi ya Sh trilioni moja nchini kwa mwaka.

Waziri Mahiga ametoa taarifa hiyo bungeni jijini Dodoma leo Mei 23, wakati akiwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/19.

“Watanzania hao wamekuwa na mchango mkubwa katika uchumi wa taifa kwa kuwa baadhi yao wamenunua nyumba zenye thamani ya Sh bilioni 29.7 kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

“Aidha, katika sekta ya afya, timu ya madaktari wa Kitanzania waishio Marekani kupitia taasisi ya afya, elimu na maendeleo ilitoa huduma ya afya bila malipo na vifaa tiba,” amesema.

Pamoja na mambo mengine, Waziri Mahiga amesema Tanzania kama nchi huru haiwezi kuchaguliwa maadui na marafiki duniani na kwamba itaendelea kushirikiana na mataifa mbalimbali duniani kulingana na jinsi itakavyoona inafaa.

Sugu: Matukio Ya Uhalifu Yanakimbiza Wawekezaji

0
0
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu, amesema matukio ya uhalifu yanayotokea nchini yanawafanya baadhi ya wawekezaji wasije kuwekeza nchini.

Amesema pamoja na kwamba Tanzania inaweza kuwa na jitihada za kuwashawishi wawekezaji kutoka nje waje kuwekeza nchini mkakati huo unaweza usifanikiwe kwa kuwa wawekezaji wanapenda kuwekeza katika nchi zenye usalama kuliko katika nchi zenye vurugu na mauaji.

Sugu amesema hayo bungeni jijini Dodoma leo Mei 23, wakati akichangia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, iliyowasikishwa na Waziri wa Wizara hiyo Augustine Mahiga.

Sugu alimtaka rais aanze kusafiri kwenda nje kwa sababu safari za nje zina faida kama ilivyowahi kutokea enzi za Rais Mstaafu Jakaya Kikwete aliyekuwa akisafiri mara kwa mara.

“Lakini pamoja na hayo, serikali haiwatendei haki Watanzania wanaoacha kazi nje na kuja kufanya kazi nchini kwa sababu inataka iwalipe mishahara midogo kama ilivyotokea kwa bosi mmoja wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) (aliyemtaja kwa jina la Kairuki),” amesema Sugu.

Zitto Amshutumu Waziri Mahiga kwa Kushirikiana Na Israel

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo), ameshutumu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Augustine Mahiga kushirikiana na Israel wakati nchi hiyo inawanyanyasa Wapalestina.

Amesema kwamba uamuzi wa Waziri Mahiga kushirikiana na nchi hiyo haukubaliwi kwa sababu unakwenda kinyume na misingi ya kuwapenda wanyonge iliyoasisiwa na hayati Mwalimu Julius Nyerere.

“Hivi karibuni Waziri Mahiga alionekana akinywa mvinyo na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, wakati Afrika Kusini wamemuondoa Balozi wao nchini Israel baada kutoridhishwa na mauaji dhidi ya Wapalestina yaliyofanywa na Israel.

“Naishauri serikali irudi katika misingi ya kuwapenda wanyonge kwa upendo na amani kama ilivyoasisiwa wakati wa kupandisha Mwenge katika Mlima Kilimanjaro,” amesema Zitto.

Hakuna Mtu Aliyethibitika Kuwa Na Ugonjwa Wa Ebola Na Hakuna Ugonjwa Huu Tanzania

0
0
NA WAMJW-DAR ES SALAAM.
NAIBU Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto dkt. Faustine Ndugulile amethibitisha kuwa hakuna mtu aliyethibitika kuwa na ugonjwa wa EBOLA hapa nchini wala hakuna ugonjwa huo hapa Tanzania.

Hayo ameyasema leo jijini Dar es salaam mbele ya waandishi wa habari wakati akitoa tamko kuhusu ugonjwa wa EBOLA kama ilivyodaiwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwepo kwa ugonjwa huo hapa nchini.

“Napenda kuwatoa hofu watanzania kwamba hakuna ugonjwa wa EBOLA na wala hakuna mtu aliyethibitika kuwa na ugonjwa huo, hivyo tuendelee na shughuli za kujenga Taifa ila tunatakiwa tuchukue tahadhari za kujikinga juu ya ugonjwa huu” alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha, Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa EBOLA usiingie nchini Serikali imeweka vifaa vya kupima joto la mwili (themo scaner) pia wapo wataalamu wa Afya ambao  wanauliza hali ya wageni wanaoingia katika mipaka yote inayoizunguka nchi yetu ili kuzuia ugonjwa huo kuingia.

Dkt. Ndugulile amesisitiza kuwa, Serikali haijafunga mipaka ya nchi kwa sababu ya kujikinga na EBOLA.

“Tanzania hatujafunga mipaka na hatuwezi kufunga biashara za mipakani ila tumeimarisha ufuatiliaji wa watu wanaoingia nchini hususani maeneo ya viwanja vya ndege na mipaka mingine yote.”

Mbali na hayo Dkt. Ndugulile ameitaka mikoa yote iliyo mipakani kudhibiti watu wote wanaoingia nchini kwa njia za panya ili kuepusha uingizaji wa ugonjwa huo kwa wananchi  huku akiwataka wafanyabiashara wa mipakani kutoa ushirikiano ili kudhibiti ugonjwa huo usiingie nchini.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani ambaye pia ni Afisa wa kushughulikia magonjwa ya kuambukiza Dkt. Grace Saguti amesema kuwa Wananchi wanatakiwa kupata elimu juu ya kujikinga na ugonjwa huo.

“Elimu inahitajika ya kutosha kwa wananchi wote hasa katika kufichua wagonjwa wa Ebola kama watagundulika hasa wanaotoka nje ya nchi ili kupata msaada kutoka kwa watoa huduma za afya walio yao juu ya kujikinga na ugonjwa huo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images