Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
MAKANGA 3 POWER; DAWA BORA NGUVU ZA KIUME
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.
 
Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.
 
Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.
 
Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.
 
Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.
 
Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.
 
Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.
 
Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Je Wajua Saa Zenye Moyo Kama Wa Binadamu

$
0
0
NDio najua bado kichwani mwako unajiuliza saa zenye moyo wa binadamu kivipi? basi mwandishi wa makala hii ndo kazi yangu kukupa majibu na elimu kuhusu saa zenye moyo...


Tuanzie hapa msomaji saa zenye moyo kwa lugha sahihi ya kiswahili ni saa ambazo hazitumii battery yaani kiingereza automatic watch/mechanical watches....katika ulimwengu huu wa saa basi saa hizi ndo zilikuwa za kwanza kugunduliwa saa hizi ziligunduliwa na peter henlein wa mji wa nuremberg ujerumani....wakati saa za mabattery ziligunduliwa mwaka 1955 yaani quartz watch huko japani ..... baada ya historia fupi hiyo ngoja sasa tuone uchawi wa mzungu huyu peter henlein alifanyaje saa hizi hazitumii battery tutamia lugha nyepesi kila mtu asomae makala hii aelewe na video nitaweka
 
1.SAA HIZI HUPATA NGUVU UNAPOTIKISA MKONO WAKO
chazo kikubwa cha nguvu za saa hizi huwa mtu alivaa saa hii akiwa anatembea anavyotikisa mkono basi saa hizi kama unajua wana fikia hapa wataelewa saa hii huchukua motion energy na kuifadhi nguvu hii kwenye spiringi kuu (main spring)yaani saa hii uko zako mishe mishe zako unatembea ..na yenyewe inakuwa bize inachaji jinsi unavyotisa mkono.....
 
2. INA GIA
mi ndo maana nasemaga wazungu bwana kwenye ugunduzi ni watu hatari saa hizi bwana zina mfumo wa gia ...gia hizi bwana zinafanya kazi kwa waledi wa hali ya juu yaani kubadilisha nguvu ya mtetemeko wa mkono wako na kuziifadhi kwenye spiring kuu yaaani huu sasa NDO HUITWA MOYO wa saa yaani ukizima na saa inasimama kana kwamba binadamu moyo ukizima nae anakufaaa....lakini saa hizi moyo huu wa saa ni kwamba ukitisaa tu mkono na moyo wa saa unaanza kufanya kazi ...ngoja niwekee mfano saa ya kampuni t winner ambayo nayo ni moja ya SAA AMBAYO INA MOYO
basi ndugu msomaji hii kwenye video hapo juu ni moja kati ya mfano saa nyingi ambazo hazina mabattery ..kama utakuwa ni mdadisi wa mambo utakuwa umeangalia vizuri umeona kama kitu kama cha mvirigo kinatikisika kwa spidi basi ule ndo moyo sasa wa saa
 
3.HAZIINGII MAJI
basi saa hizi bwana ili kutunza ule moyo wake yaani springi kuu usichoke kufanya kazi hizi saa bwana huwa ni rafiki na maji yaani ukupita mvuani sawa tu hazina shida .....pia saa hizi wafanyakazi hasa wa POSTA huzipenda sana koz zinaongezea muonekano hata mimi hapa kama mwandishi wa habari hii saaa ni ninayo ina skeleton mechanical watch bofya jina hapo kuiona unaweza nunua hapo pia niliko nunua mimi mwandishi wako
 
4.UTAPATA WAPI SAA HIZI NA KWA SIFA ZIPI ILI UPATE ORIGINAL
ili upate original sifa ya kuangalia ni muda gani springi kuu ina uwezo wa kutunza chaji muda mara nyingi huwa ni masaa 48 bila kuguswa mara nyingi watu huagiza kwenye mitandao kama AMAZON wa marekani au pia POSTA kuna maduka huuza saa hizi za automatic pia kuna njia nyepesi kuna HUU mtandao wa daresalaamshop.com ambao personally nakurecommend ukanunue hawa unagiza na unaletewa ulipo TANZANIA nzima hawa majamaa huwa ni original na utalipia mzigo ukifika kitu umekiona usikose utamu wa saa hizi pia ndugu msomaji kuna link chini hapo bofya buy now kuweka order,,, mpaka siku nyingine kwenye makala zingine ASANTE
 
IMEANDIKWA NA
robnson kayaula kutoka twigaz news

Swali La Kwanza Alilouliza SUGU Leo Bungeni

$
0
0
Leo May 21, 2018 Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amesimama na kuuliza swali Bungeni kwa mara ya kwanza tangu atoke gerezani Ruanda, Mbeya May 10 alipokuwa akitumikia kifungo cha miezi mitano.

Sugu aliuliza swali lake mara baada ya Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa  kujibu swali la msingi la  Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea (Chadema) lililohusu sheria za makosa ya mtandao.

Mwenyekiti wa Bunge, Chenge alimruhusu Sugu aulize swali la nyongeza ambapo alisema: “Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti, niwatakie mfungo mwema ndugu zangu Waislamu, ndani ya bunge na nchi nzima kwa wale ambao ni viongozi wautumie mwezi huu kujitathmini.

Kutokana na maelezo hayo ya Sugu, Chenge alimkatisha Sugu na kumtaka kuuliza swali moja kwa moja.

Sugu aliendelea kwa kusema: “Sheria hii pamoja na sheria nyingine mbovu za habari si tu zinawabana wananchi kupata habari bali zinatumika pia kufunga watu jela hovyo kisiasa…

“Mfano mimi nilifungwa kwa kujadilina na wananchi wangu taarifa za watu kupigwa risasi, watu kutekwa, maiti kuokotwa kwenye viroba, watu kutokuwa na uhuru wa kuongea….

Chenge alimkatisha Sugu kwa mara ya pili akimtaka kuuliza swali: “Mheshimiwa uliza swali.”

Sugu aliendelea: “Kitu ambacho si mimi tu najadili kwani kilishajadiliwa  ndani ya Bunge hili na pia Maaskofu wa Katoliki…

Chenge aliingilia tena: “Uliza swali,Uliza swali Mheshimiwa, hapana, hapana sina muda, uliza swali.”

Sugu: “Ni lini sheria hizi zitafutwa ili kulinda Katiba ya hususani Ibara ya 18 mfano maslahi  mapana ya demokrasia  nchini,”.

Chenge alimkatisha kwa kumwambia; “umeeleweka Mheshimiwa…”

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na  Mawasiliano, Kwandikwa alitumia muda huo kumkaribisha Mbunge huyo bungeni kwa mara nyingine.

“Kwanza nimkaribishe Mheshimiwa Sugu ndani ya nyumba Mheshimiwa karibu sana, lakini napenda kumjibu kuwa sheria zote Serikali inazitazama, na kama kuna maeneo yanahitajika marekebisho hufanya hivyo mara moja kwa kutumia Bunge.

“Labda kama kuna eneo mahususi kwa sababu Mheshimiwa Sugu umekuja tuonane ili na mimi nipate kwa upana kile ambacho unakizungumza, halafu sisi baadaye kama Serikali tutaangalia kwa nia nzuri ili sheria bora zaidi,” amesema.

PICHA: Wasafi Tv Wazindua Kipindi Cha Mwezi Mtukufu Wa Ramadhani

$
0
0
Kituo cha televisheni cha Wasafi Tv kinachomilikiwa na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, siku ya jana kimetangaza ujio wa kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Siku ya jana Wasafi Tv walifanya uzinduzi wa kipindi hiko kitakachoitwa Nyumba ya Imani ambacho kitakuwa maalumu kabisa kwa waislamu wote katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani kitakachorushwa Wasafi Tv.

Hafla hiyo ilifanyika katika makao makuu ya Wasafi Tv Mbezi beach na kuhudhuriwa na mastaa mbali mbali walioalikwa kwa ajili ya kupata futari.

Hizi ni baadhi ya picha za hafla hiyo:

Serikali Yasisitiza Kutowapa Mikopo Wanafunzi Waliosoma Shule Binafsi....Vipaumbele Vyake ni Kwa wasio Na Uwezo

$
0
0
Serikali imesema kuwa mwanafunzi aliyemaliza shule binafsi inachukuliwa moja kwa moja kuwa anauwezo wa kulipa ada ya chuo kikuu hivyo wanafunzi wasiona na uwezo watapewa vipaumbele.

Hayo yameelezwa leo,Mei 21 Bungeni, Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Ole Nasha ambapo amesema kuwa bajeti ya mikopo kwaajili ya wanafunzi wanaoenda vyuo vya Elimu ya Juu kwa mwaka ni sh. Bilioni 427.

“Kuhusu wasiwasi wa wazazi kwa wanafunzi ambao wamesoma kwenye shule za binafsi kupata mikopo ya kwenda katika elimu ya juu naomba niendelee kuweka wazi jambo ambalo tumekuwa tukizungumza, bajeti ya mikopo kwaajili ya wanafunzi wanaoenda vyuo vya Elimu ya Juu kwa mwaka ni sh. bilioni 427 wakati wanafunzi ambao tunategemea kuomba kwa mwaka ni kama elfu 70 mwaka huu wa fedha unaoisha tuliweza kuwachuku wanafunzi elfu 30 na kwa mwaka unaokuja tunategemea idadi hiyo kufikia wanafunzi elfu 40,” amesema Nasha.

Ameongeza kuwa “Katika hali ambayo fedha iliyopo inaweza kuwachukua wanafunzi kiasi fulani ni lazima tufanye uchaguzi, uchaguzi wetu utaangali uwezo wa wazazi kulipa.

"Kwahiyo mwanafunzi aliyemaliza shule binafsi aliyesoma katika shule binafsi inachukuliwa moja kwa moja kuwa anauwezo wa kulipa chuo kikuu.

"Mfano shule nyingi za binafsi ada  kuna zingine zinafika mpaka milioni 30 na nyingine unaweza kuta za chini kabisa milioni 1 na laki 5, kwahiyo tunachoomba wale watoto ambao hawana uwezo kabisa tuwape nafasi kwanza kabla hatujawachukua wale ambao historia yao inaonyesha wanauwezo wa kulipa. 

"Hata hivyo kama itadhihirika kama kuna mwanafunzi ambaye alipata msaada wa kulipiwa shule binafsi tunahitaji tu ushahidi naye atapata ufadhili.”

Alichokisema Hamisa Mobetto Kuhusu Kupigwa na Mama Diamond

$
0
0
Mwanamitindo Hamisa Mobetto amefunguka kuhusu taarifa zilizodai kuwa amepigwa na mama mzazi wa Diamond Platnumz, Sanura Kassim ‘Sandra’.

Hapo jana katika uzinduzi wa kipindi cha Nyumba ya Imani cha Wasafi TV, Hamisa alipata time ya kuzungumza na waandishi wa habari na kusema jambo hilo ni binafsi zaidi ila kugombana kwa binadamu ni kitu cha kawaida.

“Hilo siwezi kuliongelea, yeah!. is too person, is too private, is too family. Hata vikombe kwenye kabati vinagong’ana, so sisi binadamu vinaweza kutokea,” amesema.

Alipoulizwa iwapo kwa sasa yeye na mama Diamond wana maelewano mazuri, alijibu; ‘Sina kinyongo na mtu, sina bifu na mtu, mimi am just fine, may be yeye mwenyewe sio upande wangu wa kuweza kuelezea,’.

Taarifa za Hamisa kupigwa na mama Diamond zilianza kusambaa Jumatatu ya wiki iliyopita, May 14, 2018 ambapo usiku ya jana yake Hamisa na Diamond walihudhuria katika uzinduzi wa filamu ya Aunt Ezekiel ‘Mama’ na baada ya hapo anadaiwa waliongozana hadi Madale kwa kina Diamond ambapo ndipo kisa hicho kinadaiwa kutokea.

Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari,

$
0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:

KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1. MKEBE NO.1 Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo la kwanza bila kuchoka naitakufanya uwe na hamu ya kuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER
MKEBE NO 2 ni dawa ya kuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,

KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,
Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake, humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa pia ana pete za bahati ambazo zimetajilisha wengi.

SUPER POWER,
Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI

SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Mwanaheri: Mimi Sio Kikojozi

$
0
0
Muigizaji wa filamu Bongo Mwanaheri Afcely kwa mara ya kwanza amefunguka juu ya tuhuma za kuwa kikojozi.

Mwanaheri amesema tuhuma hizo hazina ukweli wowote na watu walioanzisha hizo habari wana wivu juu ya ndoa yake.

“Hakuna ukweli wowote, sijawahi kujikojolea hata siku moja, mimi ni msanii huwa nalala kambini, wapigie simu kina JB waulize kama kuna siku nimewahi kukojoa, jamani hii ndoa watu imewauma, mpaka kunizushia habari za uongo!! Sio kweli mimi sio kikojozi, ila nina tatizo la pumu tangu utotoni”, amesema Mwanaheri.

Taarifa za mlimbwende huyo aliyejaliwa shepu ya kiafrika kutoka zilitolewa na  mmoja wa watu wake wa karibu, na kusema kwamba msichana huyo ana tatizo la kujikojolea kitandani alilokuwa nalo tangu utotoni.

Zitto Ahoji Uhalali Wa Mkuchika Kukaimu Uwaziri Mkuu

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amehoji ni kwanini Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi, George Mkuchika akaimu nafasi ya Waziri Mkuu bungeni wakati kanuni za bunge haziruhusu.

Amesema kwa mujibu wa kanuni za bunge, mwenye sifa ya kukaimu nafasi hiyo ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi ambaye ndiye ana muda mrefu bungeni.

“Uwepo wa Mkuchika katika nafasi hiyo umechangiwa na nafasi yake ya udhamini katika Klabu ya Yanga kwa kuwa viongozi wa Yanga wanapenda sana madaraka,” amesema.

Kutokana na hali hiyo, Zitto alitaka Waziri Mkuchika aachie nafasi hiyo kwa kuwa uwepo wake katika nafasi hiyo anakiuka kanuni za bunge.

Akijibu hoja hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alisema Mkuchika alikaimishwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati Dk. Mwinyi akiwa na shughuli nyingine nje ya bunge.

“Kutokana na hali hiyo, Mkuchika ataendelea kushika nafasi hiyo hadi Waziri Mkuu atakapofanya mabadiliko mengine,” amesema Jenista.

Msigwa Amtaka Dk. Kigwangala Kutoa Ushahidi Wa Ufisadi Wake

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amemtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, atoe ushahidi bungeni juu ya ufisadi wake pamoja na aliyekuwa waziri wa wizara hiyo Lazaro Nyalandu.

Msigwa amesema hayo bungeni leo Mei 21, alipokuwa akichangia bajeti ya wizara hiyo, kwa mwaka wa fedha 2018/19 iliyowasilishwa na Dk. Kigwangala.

Kwa mujibu wa Msigwa, tuhuma dhidi yake na Nyalandu zilizotolewa na Dk. Kigwangala miezi michache iliyopita haziwezi kufumbiwa macho kwa sababu zilichafua majina yao katika jamii.

“Namuomba Dk. Kigwangala alieleze bunge amenufaika kiasi gani kupitia kwa mfanyabiashara OBC aliyeko Loliondo kwa kuwa hivi karibuni alionekana akipokea magari kwa ajili ya kukabiliana na majangili,” amesema Msigwa

Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Yatoa Ushauri Mzito Kwa Serikali

$
0
0
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, imeitaka serikali isiwe inatenga bajeti kubwa za wizara wakati haina uwezo wa kupeleka katika wizara fedha zote zinazopitishwa na bunge.

Ushauri huo ulitolewa bungeni jana na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Nape Nnauye alipokuwa akiwasilisha maoni ya kamati yake baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kigwangallah kuwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/19.

Hoja ya nape ilikuja baada ya kuona bajeti ya wizara hiyo imepungua kwa asilimia 22.1 ikilinganishwa na bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka uliopita.

“Kutokana na kasoro hiyo, kuna uwezekano kwa baadhi ya miradi ya wizara hii kutotekelezwa kutokana na uhaba wa fedha.

“Kamati inaishauri serikali isitishe zoezi la uwekaji wa vigingi vya mipaka katika mipaka ya hifadhi ili kuondoa malalamiko yaliyopo miongoni mwa wananchi wanaoishi jirani na maeneo hayo ya hifadhi,” amesema Nape.

Serikali Yasema Haitapanga Ada kwa Shule Binafsi....yawashauri wazazi kuchagua shule kulingana na uwezo Wao

$
0
0
Serikali imeshauri wazazi na walezi kuchagua shule kulingana na uwezo wa kulipa ada kutokana na tofauti ya viwango vya ada na huduma zitolewazo kwenye shule binafsi.

Ushauri huo umetolewa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, William Tate Ole Nasha alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum,Mariam Nassor Kisangi aliyehoji juu ya kwa nini Serikali isikae na wadau husika ili kupanga ada elekezi kwenye shule binafsi.

“Serikali haitajihusisha na upangaji wa ada kwa shule binafsi, bali itaendelea kusimamia viwango vya ubora, taratibu, kanuni na sheria za uendeshaji wa shule zote nchini,” amesema Mhe. Ole Nasha.

Ameendelea kusema, lengo la Serikali ni kuhakikisha watoto wote wa Kitanzania wanapata elimu bora kwa manufaa yao na Taifa kwa ujumla.

Aidha amesema, Serikali inatambua na kuthamini mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya elimu nchini ambapo hadi sasa, jumla ya shule ya msingi 1,432 kati ya shule 17,583 zinamilikiwa na sekta binafsi.

Amesema jumla ya shule za Sekondari 1,250 kati ya shule 4,885 zinamilikiwa na sekta binafsi. 

Vile vile Serikali inatambua utofauti wa viwango vya ada kati ya shule za umma na shule binafsi pamoja na utofauti wa viwango hivyo kati ya shule moja na nyingine za binafsi.

Waziri Mkuu Azindua Umeme Wa Gridi Lindi, Mtwara

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya kote nchini wahakikishe wanafikisha umeme kwenye vituo vya kutolea huduma za kijamii zikiwemo shule na hospitali.

Ametoa agizo hilo leo (Jumatatu, Mei 21, 2018) wakati akizungumza na mamia ya wananchi na viongozi wa mikoa ya Lindi na Mtwara baada ya kuzindua kituo cha kuunganisha umeme wa gridi ya Taifa katika kijiji cha Mahumbika, wilaya ya Lindi mkoani Lindi.

"Wakati tukizindua miradi kama hii, niwasihi Wakurugenzi wa Halmashauri wahakikishe kuwa umeme unapelekwa kwenye taasisi za kutolea huduma zikiwemo shule zote za msingi na sekondari. Wakurugenzi tekelezeni hilo," amesema.

"Tunataka umeme huu upelekwe kwenye hospitali, vituo vya afya na zahanati. Na kama kuna visima vya maji katika maeneo yenu, navyo pia vipelekewe umeme. Hatutaki kusikia wananchi wanakosa maji eti kwa sababu dizeli imekwisha, " amesisitiza.

Waziri Mkuu amesema malengo ya Mhe. Rais Dk. John Pombe Magufuli na Serikali yake ni kutaka Watanzania watumie umeme huo kukuza uchumi wao kupitia biashara za saluni, kuuza maji baridi au vinywaji baridi.

Amewataka wakazi wa mikoa hiyo washikamane kulinda miundombinu ya umeme ili iweze kuwa endelevu na isaidie vizazi vijavyo. "Kuna baadhi ya watu wanajihusisha na biashara ya vyuma chakavu, na wanang'oa vifaa ili wakauze bila kujali ni hasara gani wanasababisha. Ninawasihi wananchi wenzangu, kila Mtanzania awe mlinzi wa mwenzake kwenye miundombinu ya umeme. Ukiweza pita pale kwa wauzaji na uchungulie aina ya vifaa anavyouza kama ni vipya au ni chakavu kweli. Ukikuta kuna vifaa vyetu vya umeme vinauzwa huko, toa taarifa polisi naye atachukuliwa hatua kwa sababu sheria zipo,” amesema.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na hadhara hiyo, Waziri wa Nishati,  Dk. Medard Kalemani alisema miezi mitatu iliyopita hapakuwa na nyaya wala nguzo za umeme kutoka Lindi kwenda Mtwara lakini mafundi wa TANESCO wamejitahidi na kuifanya kazi hiyo ndani ya muda mfupi.

"Lazima tuwapongeze vijana kwa sababu wamefanya kazi kubwa na nzuri na wala  hatujatumia washauri waelekezi (consultants). Ndani ya miezi mitatu, wamejenga laini yenye urefu wa km. 80 kutoka Mtwara hadi Mahumbika. Na kutoka hapa, watajenga laini yenye urefu wa km. 120 kwenda Ruangwa ambayo pia itaunganishwa kwenda Liwale na Nachingwea," alisema.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Lindi,  Bw. Erasto Zambi alisema tukio la uzinduzi wa mradi wa kuunganisha umeme wa gridi ya Taifa kwa mikoa ya Lindi na Mtwara ni la kihistoria.

"Uzinduzi wa leo ni hatua kubwa ya maendeleo, kwani sasa hivi tukizungumza na wawekezaji tuna uhakika na nishati ya umeme. Nitumie fursa hii kuwakaribisha wawekezaji mkoani Lindi. Na huu ni uthibitisho wa Serikali kuamua kuondoa kero kwa Watanzania," alisema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Serikali Yahimiza Halmashauri Kubuni Miradi Ya Kimkakati Ili Kujiongezea Mapato

$
0
0
Serikali imeeleza kuwa Uchukuaji wa baadhi ya vyanzo vya mapato katika halmashauri ulifanyika kwa mujibu wa Sheria ya Bajeti iliyoridhiwa na Bunge ya mwaka 2015 kifungu namba 58 ikiwa na lengo la kuongeza ufanisi wa ukusanyaji na matumizi ya mapato hayo.

Hayo yameelezwa Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) alipokuwa akijibu swali la Msingi la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Suzana Mgonukulima, aliyependekeza itungwe sheria ya kuibana serikali ikiwa haitarejesha fedha zilizotokana na vyanzo vya mapato vilivyopo kwenye Miji, Halmashauri, Manispaa na Majiji zitakazokusanywa na kuwekwa kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali.

Akijibu swali hilo Dkt. Kijaji alisema kuwa  kwa mujibu wa kifungu cha 44 cha Sheria ya Bajeti, mgao wa fedha kutoka katika Mfuko Mkuu wa Serikali utazingatia  bajeti iliyoidhinishwa, upatikanaji na mtiririko wa fedha, utekelezaji mpango wa ununuzi na mpango wa kuajiri hivyo hakuna Fungu litakaloruhusiwa kufanya matumizi ya aina yoyote mpaka kuwe na fedha za kulipa matumizi husika.

“Usimamizi wa  Mapato hayo kwa mujibu ya Sheria ya Bajeti ya Mwaka 2015 Kifungu namba 58  unazingatia mapato kuingizwa kwenye Sheria ya Kuidhinisha Matumizi ya Fedha za Serikali, aliyepewa mamlaka ya kukusanya mapato ya Serikali atawajibika katika ukusanyaji wenye ufanisi, utunzaji wa hesabu, utoaji wa taarifa na kuzuia ufujaji wa mapato”, alisema  Dkt. Kijaji. 

Alisema Usimamizi wa mapato na matumizi umebainishwa vizuri na hivyo hakuna haja ya kutunga sheria nyingine ya kuibana Serikali ikiwa haitapeleka fedha kwenye, Miji, Halmashauri, Manispaa na Majiji.

Aidha akijibu swali la nyongezai la Mhe.  Mgonukulima  kuhusu kutokuwa na usawa katika utoaji wa fedha za maendeleo katika Wilaya, Dkt. Kijaji alisema kuwa tarehe 5 Mei, 2018 Serikali ilizindua Mkakati wa kuziwezesha Mamlaka za Serikali za Mitaa kutekeleza miradi yenye kuchochea upatikanaji wa Mapato ili ziweze kujitegemea  hivyo ni vema Halmashauri zikabuni miradi ya maendeleo itakayoongeza mapato.

Akieleza kuhusu utaratibu wa malipo ya Kodi ya Majengo kutoka katika Halmashauri nchini Naibu Waziri Dkt. Kijaji, alisema kuwa Majengo yasiyofanyiwa tathimini yanatakiwa kutozwa kiwango sawa cha Sh. 10,000 na majengo ya juu (ghorofa) yanatakiwa kutozwa kiwango sawa cha Sh. 50,000.

Alisema majengo yaliyofanyiwa tahimini ndiyo yanayoweza kulipiwa kodi zaidi ya kiasi hicho, hivyo wakurugenzi wa Halmashauri wanapaswa kuzingatia utaratibu huo uliowekwa katika ukusanyaji wa kodi hiyo, alieleza Dkt. Kijaji.

Imetolewa na;
Benny Mwaipaja
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango

Serikali Yatoa Bilioni Kumi Kuboresha Reli Ya Tazara

$
0
0
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa shilingi bilioni kumi kwa ajili ya kuboresha reli ya TAZARA nchini ili iweze kujiendesha kwa kusafirisha mizigo na abiria kati ya Tanzania na Zambia, kuzalisha faida na kuchangia ukuaji wa uchumi na pato la taifa kwa nchi mbili.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua njia ya reli ya TAZARA na miundombinu yake katika eneo la Mlimba, Morogoro hadi Makambako, Iringa lenye umbali wa kilomita 163.

Mhandisi Nditiye amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ametoa fedha hizo ili kuhakikisha kuwa Tanzania tunafanya majukumu yetu kwa upande wetu ambapo reli ya TAZARA inaendeshwa na nchi mbili.

Ameongeza kuwa fedha hizo zitatumika kununua traction motors saba zenye gharama ya shilingi bilioni saba kwa ajili ya kufunga kwenye injini 42 za vichwa vya treni ili kuhakikisha kuwa treni inasafiri kwa usalama na kwa uhakika kutoka eneo moja kwenda lingine bila kuharibika njiani na kuchelewesha safari za abiria au mizigo ya wateja ambapo itaboresha utendaji kazi wa TAZARA na hivyo kuongeza makusanyo ya mapato yake.

Amefafanua kuwa, fedha nyingine kiasi cha shilingi bilioni tatu zitatumika kukununua mtambo na vitendea kazi kwa ajili ya kiwanda cha kutengeneza kokoto cha TAZARA ambapo kokoto hizo zinatumika kuimarisha njia ya reli ya TAZARA na miundombinu yake, kuzuia mmomonyoko wa udongo, kuota kwa nyasi na kupunguza mtetemo wakati wa safari.

Wakati wa ziara yake, Mhandisi Nditiye amebaini wizi wa vyuma kwenye njia za reli, madaraja na miundombinu yake ambapo vinaibiwa na hivyo kuhatarisha usalama wa safari na kuharibu miundombinu hiyo. “Naitaka TAZARA mshirikiane na SUMATRA na muwe walinzi wa reli hii na miundombinu yetu”, amesema Nditiye.  

Pia, ametoa rai kwa wanunuzi wa vyuma chakavu kuwa waangalifu wasinunue vyuma vya reli. Ameilekeza TAZARA kwa kutumia kitengo chake cha Polisi kufanya ziara za kushtukiza kwa wanunuzi na wafanyabiashara wa vyuma chakavu, wakibainika na kuthibitika wananunua vyuma hivyo, wakamatwe na sheria ichukue mkondo wake.

Vile vile ameilekeza SUMATRA kuendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye njia ya reli ili kuhakikisha usalama wa usafiri wa njia ya reli.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TAZARA, Dkt. Befram P. Kiswaga ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha hizo ambazo zitawawezesha kufanya ununuzi wa traction motors hizo na mitambo ya kiwanda cha kutengeneza kokoto ili TAZARA iweze kujiendesha kwa faida kama ilivyokuwa hapo awali badala ya kuitegemea Serikali kulipa mishahara ya wafanyakazi wake kama inavyofanyika hivi sasa.

Mkaguzi Usalama wa Reli wa SUMATRA, Mhandisi Hanya Mbawala amemweleza Mhandisi Nditiye kuwa nia yao ni kulinda usalama wa usafiri wa njia ya reli ambapo ripoti ya SUMATRA ya hivi karibuni imeonesha kuwa hakuna hali hatarishi yoyote kwenye njia hiyo ambayo itazuia reli ya TAZARA kwa sasa kusafirisha abiria na mizigo. Aidha, amemhakikishia Mhandisi Nditiye kuwa, wataendelea kufanya ukaguzi huo mara kwa mara na kuielekeza TAZARA hatua stahiki za kufuata pale inapohitajika kuhusu usalama wa reli na miundombinu yake.

Reli ya TAZARA ina jumla ya kilomita 1,860 kutoka Dar es Salaam, Tanzania hadi Kapirimposhi, Zambia. Kati ya kilomita 1,860, jumla ya kilomita 975 zipo nchini Tanzania kati ya Dar es Salaam na Tunduma, mpakani mwa Tanzania na Zambia. Pia, reli ya TAZARA ina jumla ya madaraja 318 ambapo madaraja 272 yapo nchini Tanzania na 46 yapo upande wa Zambia. Aidha, ina mahandaki yapatayo 23, na 22 kati ya hayo yapo Tanzania na handaki moja lipo mpakani mwa Tanzania na Zambia na kati ya hayo, mahandaki 18 yapo katika eneo la Mlimba, Morogoro hadi Makambako, Iringa.

Kwa upande wa Tanzania, reli ya TAZARA ina daraja refu kuliko yote, daraja Na. 117 la Ruipa lililopo kati ya eneo la Mlimba na Makambako lenye urefu wa mita 502. Pia, katika eneo hilo, kuna daraja Na. 190 lenye kina kirefu cha mita 50 kwenda chini lililopo eneo la Kitete. Vile vile, kuna handaki refu kuliko mahandaki yote, handaki la Iganga lenye urefu wa mita 817. Reli ya TAZARA inaendeshwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Zambia ambapo ilikamilika ujenzi wake na kuanza kutumika mwaka 1970.

Mapato Yatokanayo na Utalii Yaongezeka kwa Asilimia 5.6

$
0
0
Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.
Mapato yatokanayo na utalii yameongezeka kutoka Dola za Marekani milioni 2,131.57 kwa mwaka 2016 hadi kufikia Dola za Marekani 2,250.3 kwa mwaka 2017 ikiwa ni sawa na asilimia 5.6.

Hayo yameelezwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Waziri wa MaliAsili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla alipokuwa akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019.

“Idadi ya watalii walioingia nchini imeongezeka kutoka watalii  1,284,279 kwa mwaka 2016 hadi kufikia watalii 1,327,143 kwa mwaka 2017, ikiwa ni ongezeko la asilimia 3.3. Watalii kutoka Marekani wameongoza katika kuitembelea Tanzania wakifuatiwa na nchi za Uingereza, India, Uholanzi na Uswisi,” amesema Dkt. Kigwangalla.

Ameendelea kusema, mafanikio hayo yanatokana na ujenzi wa miundombinu ya barabara, kuongezeka kwa kasi ya kuboresha na kutangaza vivutio vya utalii, kuimarishwa kwa mifumo ya ukusanyaji madhuhuli na kudhibiti matukio ya ujangili na matumizi yasiyo endelevu ya maliasili na malikale.

Vile amesema, katika juhudi za kutangaza utalii, Wizara imeendelea kutekeleza mikakati mabalimbali ikiwemo kuandaa utambulisho wa Tanzania Kimataifa (Destination Branding). Lengo ikiwa ni kuitambulisha Tanzania kama kituo mahsusi cha utalii Duniani.

Aidha, Wizara hiyo inashirikiana na Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo kuanzisha chaneli maalum katika Televisheni ya Taifa (TBC 1) kwa ajili ya kutangaza utalii ambapo kwa sasa Wizara inaendelea na maandalizi ya kuanzisha studio ya kutangaza utalii kwa njia ya teknolojia ya habari na mawasiliano.

Pia amesema, Wizara imeanza kutengeneza mfumo mmoja funganishi wa TEHAMA unaoitwa “MNRT Portal” kwa kutoa leseni na vibali, ukusanyaji wa takwimu na mapato kutoka vyanzo mbalimbali vya sekta ya Maliasili na Utalii.

“Mfumo huo utaunganishwa na mfumo wa Serikali wa malipo ya kielektroniki na kuhuishwa na mifumo mingine ya Serikali kama vile Uhamiaji, NIDA, TIRA, BRELA, TRA na NBS. Mfumo huo utaiwezesha Wizara kufuatilia watalii wa nje na wa ndani, kukusanya na kuchambua takwimu za sekta ya maliasili na utalii kwa wakati, kuimarishsa utoaji wa huduma kwa wateja na kufanikisha ukusanyaji udhibiti wa mapato,” amesema Dkt. Kigwangalla.

Mfumo huo ambao utatumiwa na Wizara, Taasisi na wadau mbalimbali unatarajia kuanza kutumika rasmi mwaka ujao wa fedha.

Wakati huohuo Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Nape Nnauye ameipongeza Serikali kwa kuboresha miundombinu ya utalii hususan barabara, huduma za maji na umeme ambavyo vimeendelea kuvutia watalii wengi kutembelea vivutio vya utalii na kuongeza idadi ya watalii hapa nchini.

“Kamati inaipongeza Serikali kuwezesha kujengwa kwa uwanja wa ndege wa Chato  Uwanja huu utasaidia kufungua fursa nyingi za utalii hasa vivutio vilivyopo katika kanda za ziwa. Vivutio hivyo ni pamoja na Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda, Rumanyika, Hifadhi za Taifa za Saanane na Rubondo,” amesema Mhe. Nape.

Amesema, ili kuupa thamani uwanja wa ndege wa Chato ni muhimu Serikali ikawekeza vya kutosha katika kuviendeleza vivutio vya utalii vya ukanda huo, kujenga na kuimarisha miundombinu ya barabara, maji, umeme pamoja na kuvutia wawekezaji kujenga mahoteli ili kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea vivutio hivyo katika kanda ya ziwa.

Wizara ya MaliAsili na Utalii imeliomba Bunge kuidhinisha jumla ya shilingi Bilioni 115,794,740,000 kwa matumizi ya fungu 69 – Wizara ya MaliAsili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2018/2019.  Kati ya fedha hizo shilingi 85,816,658,000 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na shilingi 29,978,082,000 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya May 22

Wambura analipwa Mil.7.....Kasema watia saini TFF walighushiwa

$
0
0
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura (49) ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa anapokea mshahara wa Shilingi Milioni 7 kwa mwezi.

Wambura ameyaeleza hayo wakati akitoa ushahidi katika kesi ya utakatishaji fedha inayomkabili, aiyekuwa rais wa TFF Jamal Malinzi na wenzake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri.

Akiongozwa na wakili wa utetezi, Richard Rweyongeza kutoa ushahidi wake, Wambura amebainisha kuwa aliwahi kuwasilisha maombi ya kutaka kuongezwa mshahara kutoka Shilingi Milioni 2 hadi 7 wakati wa utawala wa Malinzi.

Alipoulizwa na wakili Rweyongeza kwamba Malinzi alikataa kumuongeza mshahara, Wambura alidai kuwa si kweli, lakini alipeleka maombi hayo tena wakati wa utawala wa Rais wa sasa wa TFF, Walles Karia ambapo ameidhinisha alipwe Shilingi Milioni 7 tangu August 2017 hadi sasa.

Awali akiongozwa na Wakili wa serikali, Shadrack Kimaro, Wambura alidai kuwa muhtasari wa June 5,2016 uliokuwa na ajenda ya kubadilisha watia saini wa akaunti za Benki za TFF zilizopo Stanbic ni wa kughushi na kwamba yeye haufahamu.

Wambura amedai anasema hayo kwa sababu alikuwepo katika kikao hicho cha June 5,2016 na hakukuwepo na ajenda ya kubadilisha watia saini wa benki wa TFF kwa kumtoa Edgar Masoud na kumuingiza Nsiande Mwanga.

Baada ya kueleza hayo, kesi hiyo imeahirishwa hadi May 28 na 29 , 2018 kwa ajili ya kuendelea kusikiliza kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka.

Katika kesi hiyo washtakiwa wengine ni Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine, Mhasibu wa TFF, Nsiande Mwanga. Pia Meneja wa Ofisi wa (TFF),Miriam Zayumba na Karani wa TFF, Flora Rauya.

Kwa pamoja washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka 30 ikiwemo kula njama, kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji wa fedha wa USD 173,335 na Sh 43,100,000.

Joshua Nassari: Serikali Inawarudisha Watanzania Enzi za Ukoloni

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema) Joshua Nassari amesema Serikali imewarudisha Watanzania katika kipindi cha ukoloni ambako waliporwa ardhi yao bila sababu za msingi.

Nasari amesema kitendo cha kuwachomea nyumba wananchi wa Meru kinawakumbusha miaka ya 1950, ambapo walilazimika kuchanga fedha na kumtuma Japhet Kilila Nguro kwenda Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kutetea ardhi yao.

Akichangia katika hotuba ya Wizara ya Maliasili na Utalii, jana Mei 21, mbunge huyo alizungumza kwa hisia kali kuwa jambo kama hilo linawakumbusha mbali Watanzania na kuona kuwa bado wako katika kipindi cha ukoloni walipokuwa wakiporwa ardhi bila hata kusikilizwa.

“Mimi sijui tunawasaidia akina nani Tanzania yetu hii, wafanyabiashara wanalia, wavuvi wanalia, wananchi wanalia na mnawapora ardhi hivi mnataka kutawala nani lakini?” Alihoji Nasari

Alisema mali walizoachiwa Watanzania na Mungu zimeshindwa kuwa baraka tena na badala yake zimegeuka kuwa laana kwa Watanzania na kuwafarakanisha.

“Mnatutonesha kidonda sisi watu wa Meru, angalia picha hizi zinaonyesha haya ni maganda ya risasi na hizi ni picha za mifugo ambayo imedhoofu sana iliyosababisha wananchi kubaki maskini kabisa,” alisema Nasari

Ndugai aitaka Serikali kuhakiki mikataba yake na wawekezaji

$
0
0
Spika wa Bunge Job Ndugai ameitaka Serikali kuhakiki mikataba yake na wawekezaji badala ya kusubiri kuwaadhibu wanaohusika na mikataba mibovu.

Akifungua semina ya Chama cha Wabunge walio katika mapambano dhidi ya rushwa (APNAC) bungeni jana Mei 21, Ndugai alisema wabunge wanafahamu namna ambavyo mikataba ilivyoigharimu nchi.

“Eneo hili la mikataba hasa kwa kampuni za nje ya nchi katika madini, nishati za gesi, umeme imekuwa mibovu sana.  Tumeliwa sana katika mikataba hii,” alisema.

Alitaka eneo hilo kuangaliwa kwa umakini ili kuwa na mikataba safi.

“Lazima tuhakikishe tumeziba mianya yote. Sasa hivi inaaminika kuwa rushwa imepungua sana, japo kuna wengine wanasema imebadili sura na imekuwa rushwa kubwa zaidi ya zile za zamani. Sasa hatujui lipi ni kweli inabidi tulifanyie kazi.

“Tusije tukaenda likizo tukidhani imepungua ama imeisha kumbe bado iko huko iliko. Bunge linapambana sana na masuala ya rushwa kupitia kamati zote za Bunge lakini zinazoshika bendera ni zile za usimamizi,” alisema.

Awali akimkaribisha Spika Ndugai, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika alisema inaonyesha kuwa rushwa inapungua nchini.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images