Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

China Yaipatia Tanzania Msaada Wa Bilioni 146

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM-Dar es Salaam
Serikali ya Tanzania imetiliana saini na Serikali ya China mkataba wa msaada wa kiasi cha Shilingi Bilioni 146.47. Mkataba huo umesainiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dotto James na Balozi wa China nchini Wang Ke  Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo Katibu Mkuu alisema kuwa fedha hizo ni msaada na siyo mkopo na zitatumika katika miradi miwili ya miundombinu. Mradi wa kwanza ni ujenzi wa Chuo Kikuu cha Usafirishaji cha Taifa (NIT) ambacho kitajengwa Mabibo Jijini Dar es Salaam kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 62 sawa na takriban Shilingi bilioni 138.3.

Mradi wa pili ni kwa ajili ya kusaidia upembuzi yakinifu na upembuzi sanifu wa mradi wa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa (SGR), ambapo kiasi cha Sh. bilioni 3.2 kimetengwa kwa ajili hiyo.

Bw. Doto James alisema kwa sasa mradi wa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha Kimataifa umeanza kwa awamu mbili ambazo moja ni kuanzia Dar es Salaam hadi Morogoro, na kuanzia Morogoro hadi Makutopora-Dodoma, upembuzi yakinifu utakaofanywa na Serikali ya China ni kwa maeneo mengine ya ujenzi wa Reli hiyo kuanzia Dodoma, Tabora hadi Mwanza na Kuanzia Kaliua hadi Kigoma.

"China imetusaidia miradi mingi ikiwemo mradi wa maji Chalinze, Ujenzi wa uwanja wa Michezo wa Taifa, Mradi wa teknolojia za Kilimo mkoani Morogoro, Kituo cha upasuaji wa moyo na mafunzo, Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Nyerere pamoja na misaada ya dawa na vifaa tiba" alieleza Bw. James

Kwa upande wake Balozi wa China hapa nchini, Wang Ke, Alisema kuwa China inategemea kuona kuwa msaada huo utasaidia kuimarisha maendeleo na kuisaidia Tanzania kupata maendeleo haraka.

Aidha alisema China itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo ambayo itawasaidia Watanzania na kuendeleza urafiki uliopo kati ya nchi hizi mbili.

Balozi Wang Ke, amesema Pia Serikali ya China na Tanzania zinaendelea majadiliano kuhusu ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, na kuongeza kuwa majadiliano hayo yatakapokamilika nchi yake itasaidia ujenzi wa bandari hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Usafirishaji Taifa (NIT) Prof. Zacharia Mganilwa ameishukuru Serikali ya China kwa msaada huo na kusema kuwa msaada huo utaisaidia chuo hicho kuweza kutoa wataalamu wa kutosha kuweza kushiriki katika ujenzi wa miundombinu ikiwemo sekta ya anga.

Amebainisha kuwa Chuo hicho Kikuu kitatoa mafunzo kwenye fani muhimu na zinazohitajika ikiwemo ufundi wa reli, masuala ya anga na sekta nyingine mtambuka kwa kutoa wataalamu waliobobea watakao changia kufanikisha azma ya Serikali ya uchumi wa viwanda.

Kwa upande wake Kaimu Naibu Mkurugenzi Uendeshaji wa Shirika la Reli Tanzania-TRC, Bw. Focus Msasani ameeleza kuwa msaada huo wa shilingi bilioni 3.22, utasaidia kuipunguzi serikali gharama ilizokuwa izitumie kwa kazi hiyo kenye mradi mkubwa wa kihistoria wa ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Sababu za Nondo Kutokata Rufaa Baada ya Hakimu Kugoma Kujitoa

$
0
0
Wakili wa Mwanafunzi wa mwaka wa tatu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Abdul Nondo, Jebra Kambole amefafanua kuwa sababu kubwa ya kutokata rufaa baada ya Hakimu wa kesi ya mteja wake kugoma kujitoa kwenye kesi hiyo ni kutokana na kuwa huo  ulikuwa ni uamuazi mdogo ndani ya kesi kuu.

Wakili Kambole amesema kuwa ingawa hakimu huyo amegoma kujitoa kwenye kesi hiyo watasubiri mpaka mwisho wa shauri hilo ili kuona kama maamuzi hayatakuwa ya haki ndipo watakapokata rufaa ya shauri zima.

"Sheria zetu zinaruhusu kwamba hakimu ndiye mwenye kuamua kuendelea kuwepo au kujitoa. Lakini Hakimu Mpitanjia amesema kwamba atatenda haki. Sisi tumekubali na atujakata rufaa kwa sababu ni mjaamuzi madogo kwenye kesi kuu. Kama tutakata rufaa kwenye kesi kuu na haya manung'uniko pia tutayajumisha kwenye rufaa ya kesi kuu," Kambole.

Pamoja na hayo Kambole amesema sababu kuu iliyompelekea Nondo kuandika barua ya kutokuwa na imani na Hakimu ni kutokana na ukaribu aliokuwa nao Hakimu pamoja na Mkuu wa upelelezi kitu ambacho kinatia wasiwasi wa haki kutendeka.

Tochi Za Trafiki Pwani Zakaguliwa Ubora Wake

$
0
0
Wakala wa Vipimo Tanzania  (WMA),  umekagua vifaa vya kubidhiti mwendo maarufu kama tochi zinazotumiwa na Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, kuhakiki ubora wake.

WMA imefanya ukaguzi huo mapema leo katika Mkoa wa Pwani ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Vipimo Duniani ambayo hufanyika Mei 20, kila mwaka.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ukaguzi huo Mkurugenzi wa Ufundi wa WMA Tanzania, Stella Kahwa amesema hatua hiyo imelenga pia kuhakiki usalama wa vifaa hivyo katika kudhibiti mwendo.

“WMA hapo awali tulikuwa tunapima ubora wa vipimo kama vile mizani lakini sasa tumeendelea kuongeza wigo wa kazi zetu tunapima vipimo vya sekta ya biashara,  afya na mazingira,” amesema.

Amewahakikishia watumiaji wa barabara hususan madereva wasiwe na wasiwasi kwani ubora wa vifaa hivyo ni wa uhakika.

“Wawe makini wanapokuwa barabarani kwa sababu akienda mwendo wowote uwe kasi ama la, kifaa hiki kinaweka taarifa zake, ukienda speed 70 ni 70 na kama ni 80 kinaonesha hivyo hivyo 80 ” amesema.

Naye, Mrakibu wa Polisi na Mkuu wa Kitengo cha Usalama Barabarani wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Makao Makuu, Abel Swai amewahimiza madereva kuendelea kuzingatia na kutii sheria za usalama barabarani.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

TEMBELEA KATIKA BLOG YETU HAPA>>>;

Wanahisa Wamgomea Dk Kimei .....Wataka Asiondoke CRDB

$
0
0
Baadhi ya wajumbe waliohudhuria mkutano mkuu wa mwaka wa Benki ya CRDB unaofanyika leo Mei 19, 2018 jijini hapa, wamemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Dk Charles Kimei kuendelea kuitumikia benki hiyo.

Kauli za wanahisa hao waliohudhuria mkutano mkuu wa 23 wameeleza hayo baada ya Dk Kimei kuwajulisha kuwa kwenye mkutano mkuu ujao, atawaaga rasmi.

"Hotuba yangu ya leo si ya mwisho. Tutakutana tena mwakani nitakapowaaga. Mkataba wangu unaisha Mei, 2019,” amesema  Dk Kimei alipokuwa akitoa hotuba ya mwenendo wa benki hiyo ambayo mwaka 2017 imepata faida ya Sh36 bilioni ambayo imepungua kutoka Sh70 bilioni iliyopata mwaka 2016.

Kwenye michango yao, baadhi ya wanahisa hao wamesema kipindi hiki ni kigumu kiuchumi hivyo CRDB inahitaji mtu mwenye uzoefu wa kutosha kukabiliana na changamoto zilizopo.

Mmoja wa wanahisa hao, Lemburis Sirikwa (76) wa Arusha amesema endapo mkurugenzi huyo ataondoka na kuiacha benki hiyo, ndani ya miaka miwili ya kutokuwa naye lazima ufanisi utapungua.

"Kimei shall remain until further notice (aendelee kuwepo mpaka taarifa nyingine itakapotolewa). Kama bodi haitaki kufanya hivyo, tutachagua wajumbe wengine," amesema Sirikwa.

Sirikwa amesema wapo wakurugenzi wenye umri wa miaka 90 lakini wanaendelea kuziongoza taasisi zao hivyo haoni sababu ya Kimei kustaafu.

"Kimei ni mdogo sana. Mimi nina miaka 76, namzidi mbali sana. Asiondoke sasa hivi," amesema.

Mwanahisa mwingine kutoka mjini Sumbawanga, Kapteni mstaafu Noel Nkoswe amesema suala la kumpata mkurugenzi ni gumu.

"Tulipoanza, tulitafuta mtu anayefaa lakini hatukupata. Mwishowe tukaenda kuiomba  Benki Kuu ambayo ilitupatia Dk Kimei. Tunaishukuru Benki Kuu kwa kutupa mtaalamu huyu, napendekeza aendelee kuwepo walau miaka miwili au mitatu zaidi," amesema.

Mfumo wa mshine za kielektroniki za kutolea risiti (EFDs) wakumbwa na tatizo.

Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume....Huna Sababu ya Kuaibika Tena

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MALUNA:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUPER MORISIS:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr LALIMBO mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR LALIMBO ATAKUSAIDIA SM NO :- 0653182109, 0744391089.

Taarifa ya BOT Kuhusu Kuongezeka Kwa Deni la Taifa

$
0
0
Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imesema kuwa imeshtushwa na taarifa zilizoandikwa na Gazeti la Mwananchi tarehe 17 Mei taarifa hizo si za kweli na zinapaswa kupuuzwa.

Taarifa ya BOT imeeleza kuwa Gazeti hilo lilidai kwamba   imeongezeka Trilioni 12 katika deni la Taifa kati ya Disemba 2017 na March 2018 takwimu ambazo sio sahihi.

RC Makonda Apokea Vifaa Vyenye Thamani Milion 400 Kwaajili Ya Ujenzi Wa Ofisi Za Walimu

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo amekabidhiwa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi Million 400 kutoka kiwanda cha MMI Steel ltd kwaajili ya kampeni ya ujenzi wa ofisi 402 za walimu Dar es salaam.

Vifaa alivyokabidhiwa ni Mabati 15,000 yenye thamani ya shilingi Million 360, Nondo Tani 22 zenye thamani ya million 40 ambapo kiwanda hicho kimemuahidi tena kumpatia RC Makonda vifaa vingine ikiwemo Rangi, Nondo na Mabati.

Akipokea vifaa hivyo RC Makonda ameshukuru kiwanda cha MMI Steel chini ya mkurugenzi wake Subhash Patel kwa kuwa mdau mkubwa wa kampeni ya ujenzi wa ofisi za walimu na kuwasihi wadau na wananchi kujitokeza kuchangia kampeni hiyo ili kutoa heshima kwa walimu.

Aidha RC Makonda amesema kampeni ya ujezi wa ofisi za walimu inaendelea vizuri ambapo hivi karibuni atapokea kontena nyingine 16 za furniture kutoka Marekani, Kontena 10 za Vitabu kwaajili ya Maktaba ya jamii kutoka Marekani, Kontena 10 za vifaa tiba kutoka uingereza na kontena 10 za Maziwa kutoka China kwaajili ya watoto waliojitokeza wakati wa Zoezi la kutafuta haki ya watoto waliotelekeza Kama sehemu ya msaada.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kiwanda cha MMI Steel Ltd Bwana Subhash Patel amesema wameamua kutoa vifaa hivyo kama sehemu ya kutambua umuhimu wa elimu na kuunga mkono jitiada za RC Makonda katika uboreahaji wa elimu kupitia mazingira bora ya walimu kufanya kazi.

Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari,

$
0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:

KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1. MKEBE NO.1 Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo la kwanza bila kuchoka naitakufanya uwe na hamu ya kuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER
MKEBE NO 2 ni dawa ya kuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,

KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,
Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake, humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa pia ana pete za bahati ambazo zimetajilisha wengi.

SUPER POWER,
Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI

SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Serikali Yasaini Mkataba Wa Kuwakopesha Watumishi Wa Umma Mitungi Ya Gesi Na Vifaa Vyake

$
0
0
Serikali imesaini mkataba na Kampuni ya Gesi ya Mihan Gas wa kukopesha mitungi ya gesi na vifaa vyake kwa watumishi wa umma.

Hatua hiyo inakuja ikiwa ni juhudi za Serikali za kutaka  kupunguza matumizi ya mkaa pamoja na kuni kwa lengo la kutaka kuhifadhi misitu ambayo imekuwa ikitumika  kama nishati.

Mkataba huo ulisainiwa jana  Jijini Dodoma na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu  Tanzania (TFS),Profesa Dos Santos Silayo na   Mkurugenzi Mtendaji wa Mihan Gas,Hamisi Ramadhan na huku Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Mej. Gen. Gaudence Milanzi akishuhudia tukio hilo.

Mbali na kusaini mkataba huo, TFS na Kampuni ya Mihan Gas zilizindua kampeni ya kukopesha mitungi ya gesi na  vifaa vya vyake kwa Watumishi wa Umma.

Awali, Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Milanzi  aliwahimiza watumishi kuchangamkia fursa hiyo ya  kukopa mitungi na vifaa hivyo kwani itasaidia katika kuokoa misitu.

“Hili ni tukio kubwa hasa kwa wale ambao ni watunzaji wa mazingira katika kuwezesha jamii kuanza kutumia  nishati mbadala.’’ Alisema

Naye, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Misitu  zaTanzania (TFS),Profesa Dos Santos Silayo,alisema upatikanaji wa huduma hiyo ni jitihada za kuhakikisha matumizi ya mkaa yanapungua

Aliongeza kuwa nishati mbadala ndo njia pekee itakayosaidia jamii kuachana na  matumizi ya mkaa na kuni.

Kwa upande wake, Mkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni hiyo,Hamisi Ramadhani aliishukuru Serikali kwa kuikubalia kampuni hiyo kusambaza gesi kwa watumishi. 

Akizungumzia namna watumishi watakavyonufaika na mpango huo,  Mkurugenzi Mtendaji , Ramadhani alisema kampuni imetenga fungu ambalo litarahisisha ukopeshaji wa vifaa hivyo na kila Mtumishi atapewa nafasi ya kuweza kulipia mwezi mmoja mara baada ya kuanza kuitumia gesi.

Mahakama Yaiagiza TFF Kupitia Upya Swala la Wambura

$
0
0
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam imekubali maombi yaliyopelekwa na aliyekuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Michael Wambura ya kutaka kurudia maamuzi ya kamati hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana Ijumaa na wakili wake, Emmanuel Muga, hukumu kwenye shauri No.20/2018 iliyotolewa Mei 18, mwaka huu na Jaji Wilfred Ndyasobera baada ya kuridhika na hoja zilizotolewa na mawakili wa Wambura, Dr Masumbuko Lamwai na Muga.

Maamuzi hayo, yanatokana na maombi yaliyowasilishwa Mahakama Kuu wiki mbili zilizopita yakiomba mahakama imruhusu Wambura afungue kesi ya msingi kuomba kutengua maamuzi ya kamati ya TFF.

Mahakama imetamka kuwa Wambura kesi yake ina msingi na inafaa isikilizwe. Mahakama imeridhika kuwa maombi yaliletwa ndani ya muda na Wambura ana maslahi mapana ya kuleta maombi, hivyo mahakama imempa ruhusa ya kuleta kesi ya msingi ya kuomba kutenguliwa kwa maamuzi ya kamati za TFF.

Kwa mujibu wa Muga, Mahakama imeamuru kuwa kesi ya msingi ifunguliwe ndani ya siku 14 kuanzia jana. Maombi ya mapitio yaani ‘Judicial Review’ ni haki ya msingi inayotafutwa pale chombo kilichotoa maamuzi kilivunja sheria au kukiuka misingi ya haki kama haki ya kusikilizwa.

“Tunaamini hii haitachukuliwa kama Wambura amepeleka mpira mahakamani, kwani, hii ni ‘judicial review’ ya maamuzi ambayo yalivunja sheria ya TFF wenyewe, pia hayakufuata misingi ya haki ya kusikilizwa.

“Mahakama ipo kwa mujibu wa sheria za nchi, na TFF inafuata sheria hizo, ndiyo maana wamesajiliwa kwa sheria za BMT, na pia waliapishwa na msajili wa vyama vya michezo kwa mujibu wa sheria hiyo,” alisema Muga ambaye amewahi kuwa mwandishi wa michezo wa BBC.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Waziri Jafo Atoa Siku Tano Kwa Halmashauri 10 Kujieleza Kuhusu Matumizi Ya Fedha Za Miradi Ya Afya

$
0
0
 Zulfa Mfinanga na Magdalena Stanley
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Seleman Jafo ametoa siku tano kwa wakurugenzi na waganga wakuu wa halmashauri 10 nchini kutoa maelezo ya kina kwa nini halmashari hizo hazijafika asilimia kumi ya matumizi ya fedha za miradi ya afya.

Jafo ameyasema hayo leo wakati akifungua kikao kazi juu ya utekelezaji wa miradi ya afya inayotekelezwa chini ya Mamlaka za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kilichowajumuisha Makatibu Tawala kutoka mikoa yote nchini.

Amesema halmashauri hizo zimeshindwa kutumia fedha zilizotolewa kwa ajili ya miradi ya afya kama inavyotakiwa ambapo matumizi yake yanaonekana kuwa chini ya kiwango, huku akizitaja halmashauri hizo kuwa ni halmashauri ya wilaya ya Karatu, Mpimbwe, Mbulu Dc, Songwe, Simanjiro, Mkinga, Mkuranga, Namtumbo, Nzega TC pamoja na Kilindi.

“Halmasharu hizi zina kila dalili ya kupata hati chafu, naagiza hadi kufika siku ya Jumatano niwe nimepata majibu ya kuridhisha ni kwanini hawajatumia fedha walizopewa kama maelezo yanavyotaka, tukiacha kufanya kazi kwa mazoea tutapata matokeo mazuri, lakini kwa hali hii tusitegemee matokeo mazuri kwa baadhi ya maeneo” Alisema Jafo

Kuwa upande mwingine Waziri Jafo aliwaagiza Makatibu Tawala hao kuwaelekeza wakurugenzi wa halmashauri nchini kuwekeana malengo na watumishi wao kwa kuwafanya tathmini ya uwajibikaji kila mwaka ili kuongeza ufanisi na uwajibikaji kazini kwani bado wapo baadhi ya watumishi wanafanya kazi kwa mazoea.

Amesema kuwa iwapo mtumishi wataonekana amefanya kazi chini ya kiwango cha alama 50 kama ni mkuu wa idara atawajibishwa kwa kushushwa cheo, na yule ambaye ataonekana kufanya vizuri zaidi alishauri anastahili kupewa zawadi ya mfanyakazi bora wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani-Mei Mosi.

Aidha Waziri Jafo amesema kwa sasa kipaumbele cha utoaji wa fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo zitatolewa kwa kuzingatia kipimo cha matokeo mazuri kwa halmashauri husika, kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kuongeza uwajibikaji.

Wakati huo huo Waziri huyo aliagiza halmashauri zote nchini kuweka mfumo wa matumizi ya mfuko wa afya ya jamii wa CHF iliyoboreshwa sambamba ya kuhimiza matumizi ya ukusanyaji wa mapato wa njia ya kimtandao ili kuepuka upotevu wa fedha za serikali.

Akizungumzia mafanikio ya mfuko huo Mratibu wa mfuko wa afya ya jamii TAMISEMI, Nkinda Shekalaghe amesema kuwa hadi sasa mfuko huo haujafikia lengo lililowekwa na serikali la kuunganisha wananchi kwa asilimia 30 hadi kufikia mwaka 2015, kwani kwa mwaka 2016/2017 wamefikia asilimia 24.

Alitaja baadhi ya changamoto zinazoukabili mfuko huo kuwa ni pamoja na utayari wa wananchi kujiunga na mfuko, huduma duni za afya, kutokuwepo kwa mfumo rasmi wa utoaji wa taarifa pamoja na kiwango kidogo cha uchangiaji ambapo amesema tayai wameshachukua hatua mbalimba katika kukabiliana na changamoto hizo.

Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwapima watu wanaoingia kutoka DRC

$
0
0
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imetoa wito kwa nchi wanachama kuchukua tahadhari ya mlipuko wa ugonjwa wa ebola ambao umethibitishwa kulipuka katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Mkuu wa Idara ya Mawasiliano kwa Umma wa EAC, Richard Owora imesema Wizara ya Afya ya DRC ilitangaza mlipuko wa ugonjwa huo katika majimbo matatu ya nchi hiyo.

Amesema hadi May 15 matukio 44 ya Ebola yalitolewa taarifa na vifo vya watu 19 wakiwemo watoa huduma za afya watatu.

Amesema nchi za EAC ambazo ni Tanzania, Kenya, Burundi, Uganda, Rwanda na Sudan Kusini zimeweka hatua za kiusalama ikiwa ni pamoja na kuwapima afya wanaoingia kutoka DRC kwenye mipaka yote iwapo wataonyesha dalili za ugonjwa huo sanjari na kutoa elimu kwa wananchi juu ya kujinga na ugonjwa huo.

Taarifa hiyo imesema wagonjwa wapya wametambuliwa katika mji wa Mbandaka ulio umbali wa kilomita 150 kutoka mji wa Bikoro unaosadikiwa kuwa chanzo.

“Nchi tano kati ya sita wanachama wa EAC zinapakana na DRC, pia zimekuwa na uhusiano wa kibiashara wa karibu sana kwa kuwa na idadi kubwa ya wananchi wanaovuka mipaka kila mara, zikiwemo safari za moja kwa moja  za ndege kati yetu. Hali hii inatufanya tuchukue tahadhari kubwa,” amesema Owora

Kashfa ya ngono yawalazimu Maaskofu 34 wa Kikatoliki kujiuzulu

$
0
0
Maaskofu 34 wa Kanisa katoliki nchini Chile wamemuomba Baba Mtakatifu, Papa Francis kuridhia kujiuzulu nafasi zao kutokana na kashfa iliyowaandamana ya udhalilishaji wa kingono uliodaiwa kufanyiwa vijana wadogo wa kiume nchini humo.

Kabla ya kufikia uamuzi huo, maaskofu hao waliwaomba radhi waathirika wa vitendo hivyo pamoja na kanisa kwa “makosa makubwa waliyoyatenda”.

Bado haijafahamika mara moja iwapo Papa amekubaliana na ombi hilo la kujiuzulu ama la.

Amekuwa katika kukosolewa nchini Chile kwa uamuzi wake wa kumteua askofu ambaye alishutumiwa na kamati ya makasisi kuhusika na kulinda vitendo vya udhalilishaji wa kingono nchini humo.

Alipofanya ziara nchini Chile, Papa aliuambia umma wa wakatoliki walifika kumlaki kuwa anajisikia “maumivu na aibu” juu ya kashfa hiyo iliyolikumba Kanisa la Katoliki nchini Chile.

Zari Asema Hawezi Kumpeleka Diamond mahakamani kwa Sababu ya Matunzo ya Watoto

$
0
0
Mwanamama Zari the Bossy Lady ambae alibahatika kupata watoto wawili na msanii Diamon Platinumz lakini baadae wawili hao walikuja kutengana hivyo Zari kuondoka na watoto na kwenda nao afrika kusini amefunguka na kusema kuwa hata siku moja hawezi na hajawahi kufikiria kwenda kumpeleka mwanaume huyo mahakamani kwa sababu ya matunzo ya watoto.

Akiongea na waandsihi wa habari nchi Kenya, Zari amesema kuwa anatengeneza pesa zake mwenyewe ambazo zinamtosha kwa ajili ya matunzo yake na watoto wake kwahiyo hawezi kuhangaika kumpeleka Diamond mahakamani kwa sababu  hiyo kama wanawake wengine.

Katika historia, Diamond alishawahi kupelekwa mahakamani na Hamisa Mobeto kutokana na kushindwa kutoa matunzo ya mtoto .

Zari ambae ana watoto watano huku watatu wakiwa wa mwanaume mwingine ambae pia alishafariki, amekuwa akionekana kuwalea watoto wake kwa starehe bila shida yoyote kutokana na kusadikika kuwa mwanamke huyo ni tajiri na hana shida ya kuomba misaada.

Mimi Mars Awataka Mashabiki Wake Kufuatilia Muziki Wake sio Muonekano.

$
0
0
Mwanadada kutoka Mdee muziki Mimi Mars amefunguka na kusema kuwa anawaomba sana mashabiki wake kufuatilia zaidi muziki wake na sio mwili wake kwa sababu kipindi cha nyuma alikuwa mnene sana na alikuwa haupendi kabisa mwili wake lakini kadri siku zilivyozidi kwenda aliona ni bora kuanza kupungua ili kukaa sawa lakini kitu cha ajabu kuna baadhi ya watu wamekuwa wakimsema vibaya kuhusu kupungua kwake.

Mimi Mars anasema kuwa aliamua kupunguza mwili wake ili kujiongezea kujiamini zaidi lakini pia kwa sababu mwili wake aliokuwa nao hapo awali alikuwa haumpendezi sana.

"Nilikuwa sijafurahishwa na nilchokuwa nina kiona , na klikuwa kikininyima confidence sana,so ilibidi nijitengeneze na kujibadilisha zaidi ili kuweka kuwa na ile confidence maana hilo ni swla muhimu zaidi katika industry tuliona yao sasa.

"Najua wengi hawajafurahishwa sana na , hawajakipenda  na wamekuwa wakilalamika sana lakini is me, ninafanya kile ninachokipenda mimi,waendelee kuupenda muziki wangu na kuendelea kuusikiliza lakini mwili wangu waniachie mimi."

Vanessa Mdee Azidi Kupata Mafanikio na Albamu Yake Ya ‘Money Mondays’

$
0
0
Mwanamuziki wa Bongo fleva Vanessa Mdee amezidi kufanya vizuri na albamu yake ya ‘Money Mondays’ kwani albamu hiyo imetajwa kuwa ndio inaongoza Afrika Mashariki nzima.

Kupitia mtandao wa Boomsplay ambao unahusika na upakuaji wa nyimbo kadhaa umeweka wazi kuwa Albamu hiyo ndio kinara kupitia mitandao yao ya kijamii ambapo wameandika ujumbe huu:

"Hongera nyingi sana kwake @vanessamdee kwa kuwa na albamu namba moja kwa mauzo na kusikilizwa, ukanda wa Afrika Mashariki nzima ! Wewe kama shabiki wake mkubwa uliyewezesha hili, tunakupa pongezi pia na endelea kuipa support “Money Mondays” kila siku!”.

Vanessa Mdee alionyesha kufurahishwa na taarifa hiyo kwani alitumia ukurasa wake wa Instagram kushukuru mashabiki zake kwa kuweza kupakua wimbo mpaka kufanya uwe namba moja:

"Thank you Asante Sana for making #MoneyMondaysTheAlbum the NO 1 ALBUM in East Africa @mdeemusicofficialmmetishaaaaaa @boomplaymusic_tz@boomplaymusicke @boomplaymusicngwith over a million plays/streams. #SwimmingInJesusJuice #BestFansInTheWorld.”
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images