Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mbunge CHADEMA Asema Wizara Ya Mifugo Ni Hewa.....Aahidi Kuifadhili Kama Serikali Imeshindwa

$
0
0
Mbunge wa Serengeti, Marwa Chacha (Chadema) amedai Wizara ya Mifugo na Uvuvi ni Wizara hewa ambapo pia amehoji ni kwanini Serikali imekuwa ikiwanyanyasa wavuvi kwa kuwanyang’anya nyavu zao.

Akichangia bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi bungeni jijini Dodoma jana Mei 17, wizara hiyo ilitengewa fedha za maendeleo Sh bilioni nne lakini hakuna fedha waliyopewa.

“Najiuliza kwanini wameiweka hii wizara peke yake na kuitenganisha na Kilimo au ilikuwa kuwatafutia ‘washkaji’ ulaji, maana yake ni kwamba hamtaki kusikia biashara ya wavuvi nchi hii.

“Ng’ombe 300 wamepigwa mnada ila tembo akila shamba la ekari tano mhusika analipishwa faini ya Sh 100,000 kwa ng’ombe mmoja.

“Wafugaji wetu wanapata shida mtapata hela wapi Ulega (Abdallah, Naibu Waziri wa Kilimo) mwaka uliopita hamkupewa hata 100 afadhali mje hata mimi naweza kuwafadhili,” amesema Marwa.

Waitara Amtaka Spika Kuwapatia Wabunge Laptop

$
0
0
Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), amemuomba Spika wa Bunge, Job Ndugai alieleze bunge ni lini atawagawia wabunge kompyuta mpakato (laptop) ili wasiendelee kutumia nyaraka za makaratasi wakati wa shughuli za bunge.

Amesema ugawaji wa laptop hizo kwa wabunge ni moja ya ahadi iliyotolewa na Spika Ndugai kama sehemu ya mkakati wake wa kuliboresha bunge.

Waitara ametoa hoja hiyo bungeni leo Mei 18, alipokuwa akiomba mwongozo wa Spika akitumia kanuni ya 68 (7).

Akijibu mwongozo huo, Spika Ndugai amesema atalitolea majibu suala hilo baadaye.

Bulembo: Mpina Ana Mpango Wa Kuiondoa CCM Madarakani

$
0
0
Mbunge wa kuteuliwa, Abdallah Bulembo (CCM), amesema Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ana mpango maalumu wa kuiondoa Chama Cha Mapinduzi (CCM), madarakani.

Akichangia bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2018/19, Bulembo amesema kama operesheni sangara inayofanyika katika Ziwa Victoria ikiendelea CCM itakuwa na wakati mgumu wa kuwaomba kura wananchi katika Uchaguzi Mkuu na Serikali za mitaa unaotarajia kufanyika mwakani.

“Kuna haja operesheni hiyo isimame ili kuwaokoa wavuvi ambao wanaathiriwa na operesheni hiyo,” amsema Bulembo.

Bulembo amemwomba Spika wa Bunge, Job Ndugai kuunda Tume ya kwenda kuchunguza operesheni hiyo kwani wavuvi wanaishi nchini kama watumwa.

 “Wizara hii kwa kweli tuna majonzi sana, nashukuru Mheshimiwa Spika umekaa hapo mbele, ni vyema ukaunda tume ya Bunge kwenda kuangalia matatizo na madhara yaliyowakuta wafugaji na wavuvi.”

Bulembo akichangia kwa hisia  amesema: “Wavuvi wa Tanzania wako katika utumwa kwa sababu ukienda Ukerewe (anataja na visiwa mbalimbali)  maisha yao ni uvuvi, hawa watu leo ni kilio, si kilio kidogo ni kikubwa, watu wamejinyonga, wamepigwa risasi.

“Wana CCM wenzenu, tutakwenda kuomba kura, tutakwendaje kuomba kura, haiwezekani utu wa mtu ukaharibika kwa sababu Mpina ni waziri, katika hili tume haipukiki, CCM ni ya watu, Rais anaongelea wanyonge, wanyonge wa Mafia, Mtwara, kanda ya ziwa.

“Mnakwendaje kuomba, Mtanzania anakuwa mtumwa, wafanyakazi wanalia, wakulima wanalia, itawezekanaje, Mpina huwatendei haki.”

Bashe: Bajeti Ya Mifugo Iondolewe, Imejaa Kasoro

$
0
0
Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), ameitaka serikali iiondoe bungeni Bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya mwaka 2018/19, kwa sababu imejaa kasoro zinazotakiwa kurekebishwa kabla haijapitishwa.

Amesema bajeti hiyo inatakiwa kurekebishwa kabla haijapitishwa kama ilivyo kawaida ya wabunge kupitisha bajeti zenye kasoro kama ilivyofanyika juzi katika bajeti ya Wizara ya Kilimo iliyokuwa na kasoro mbalimbali.

Bashe ameyasema hayo bungeni leo Mei 18, alipokuwa akichangia bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya mwaka 2018/19 iliyowasilishwa juzi na Waziri wa Wizara hiyo, Luhaga Mpina.

Amesema hoja za baadhi ya wabunge zinazohusu maisha ya wananchi zinafia katika vikao vya vyama vya siasa.

“Naweza kuonekana mbaya kila ninapokuwa nikiikosoa serikali  lakini nitaendelea kusema ukweli kwa kuwa nilianza kuwa na kadi ya CCM kabla sijawa mbunge,” amesema Bashe.

Bashe alieleza jinsi Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye alivyowahi kuitwa na Kamati ya Bunge ya Uongozi baada ya kutaka kuwasilisha hoja ambayo haikuwafurahisha baadhi ya watu.

Wabunge Wahoji Unyanyasaji Wa Wavuvi

$
0
0
Wabunge wamehoji ni kwanini serikali haiweki utaratibu wa upatikanaji wa nyavu za kuvulia kwa wavuvi na badala yake imekuwa ikiwanyanyasa kwa kutokujua ni aina gani ya vyavu wanatakiwa kutumia wakati wa kuvua.

Mbunge wa Geita, Costantine Kanyasu (CCM), amesema kwa sasa kilio cha wavuvi ni kunyanyaswa na serikali kuhusiana na aina ya nyavu wanazotakiwa kuzitumia.

“Kwa sasa kilio cha wananchi ni unyang’anyi mkubwa unaofanywa na wizara hii, kuna bahati mbaya tunatumia nguvu kubwa lakini majibu ya serikali ni mepesi.

“Kwa sasa hakuna nyavu madukani, wavuvi wameacha kununua nyavu za Tanzania kwa sasa wananunua za Kenya na Uganda, kwanini Waziri anazuia nyavu, unataka watu wavulie nini, siungi mkono hoja waziri atuambie ni kwanini tunateseka,” amesema Kanyasu.

Naye Mbunge wa Ukerewe, Joseph Mkundi (Chadema) alihoji kuhusiana na operesheni Sangara kuwadhulumu wavuvi.

“Uchumi wa taifa unategemea mtu mmoja mmoja na uvuvi unachangia pato la taifa asilimia 2.2 lakini sioni kama kuna umakini katika hili.

“Uvuvi Kanda ya Ziwa ni siasa mfano operesheni Sangara ni uonevu na udhulumati mkubwa, wavuvi wanafanyiwa vitendo vya ajabu kabisa.

“Operesheni Sangara inawanyima uhuru Wavuvi watu wahuni tu wanawachomea nyavu zao,” amesema.

Waziri: Wahitimu Elimu ya Juu ni wengi kuliko ajira

$
0
0
Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi, ajira na watu wenye ulemavu Mh. Antony Mavunde amesema kuwa Serikali inatambua kuwa wahitimu wa Elimu ya juu ni wengi kuliko mafasi za ajira.

Waziri Mavunde ametoa kauli hiyo bungeni leo wakati akijibu swali la Hadija Ally Mbunge viti maalum (CCM) lililohoji serikali imepanua fursa kwa kuongeza vyuo vikuu nchini, je ni kiasi gani mfuko wa vijana unaweza kuwanufaisha walengwa ikizingatiwa kuwa tatizo la ajira ni hali halisi inayowakabili vijana.

Mavunde amesema “Nafasi za ajira zinazotengenezwa kwa mwaka zimekuwa ni chache kuliko wingi wa vijana hivyo basi serikali imeanza kuwabadili mitazamo kuwa sio wote wanaoweza kukaa maofisini bali wanaweza kutumia uwezo wao na kujiajiri katika sekta za kilimo na shughuli nyingine halali zinazoweza wapatia kipato”.

Waziri mavunde ameongeza kuwa Mfuko wa Maendeleo ya vijana umeweza kufikia vikundi 397 ambapo zaidi ya Bilioni nne zimekwisha tumika kuwezesha vijana kiuchumi.

Mbunge Ahoji Serikali ‘kung’ang’ania’ Ng’ombe Jimboni Kwake

$
0
0
Mbunge wa Itilima, Njalu Silanga (CCM), amehoji ng’ombe 339 katika Jimbo lake kuendelea kushikiliwa na Serikali wakati mahakama iliamuru waachiwe huru.

Akichangia bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Silanga amesema wafugaji wameteseka hususani wa kando kando ya hifadhi huku akitaka miundombinu katika minada iboreshwe ili iwasaidie wafugaji kusafirisha mifugo.

“Kwenye Wilaya yangu ya Itilima ng’ombe 339 wa wafugaji wanashikiliwa na serikali waKati mahakama iliamuru  waachiwe, mambo haya yapo kisheria lakini tunadhulumiwa baadhi ya vyombo vinazuia ng’ombe zetu Waziri tusaidie kwanini jambo hili linaendelea.

“Ukiachilia mbali suala la ng’ombe, katika maeneo yetu hatuna miundombinu mizuri nia yetu ni ya dhati lakini lazima msaidie wafugaji lakini pia nikupongeze Waziri kwa mipango yako ya kuhakikisha Kiwanda cha Shinyanga kinafanya kazi,” amesema Silanga.

Spika Ndugai Awashauri Vijana Wagombee Udiwani na Ubunge Kukabiliana na Tatizo la Ajira

$
0
0
Spika wa Bunge la Tanzania mheshimiwa Job Ndugai amewataka vijana nchini kugombea nafasi mbalimabali  za uongozi ikiwemo udiwani na ubunge ili kutatua tatizo la kukosa ajira kutokana na kukosa uzoefu.

Spika Ndugai amesema hayo Bungeni leo, Mei 18, 2018 baada majibu ya Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Bunge, Jenista Mhagama, kutokana na swali la mbunge wa viti maalumu Zainab Katimba aliyetaka kujua mkakati wa Serikali katika kutatua tatizo la ajira kwa vijana wasomi wasikuwa na uzoefu.

“Asante sana Waziri wa nchi kwa majibu ya nyongeza, Vijana wasomi, zipo kazi nyingine hazihitaji uzoefu, mnaweza mkagombea Udiwani, mkagombea Ubunge, nawatangazia vita waheshimiwa hapa” amesema Spika Ndugai.

Awali Naibu Waziri, Sera, Bunge, kazi, vijana, ajira  na walemavu Anthony Mavunde amesema kwamba serikali imeendaa utaratibu wa kuwapa vijana nafasi za kujitolea katika makampuni na mashirika mbalimbali ili kupata uzoefu wa kuweza kuajiliwa

“Kupitia mpango huu utawasaidia sana vijana wasomi  wa nchi yetu ambao walikuwa wakipata tabu na kikwazo cha uzoefu, kwa hivi sasa atapata nafasi ya kujifunza katika kampuni kwa muda huo wa mwaka mmoja na badae tutampatia cheti cha kumtambua ili iwe kama kiambatanisho chake” amesema Naibu Waziri Mavunde.

PICHA: Lowassa na RC Gambo katika mazishi ya DC Mstaafu Molloimet

$
0
0
 Aliyewahi kuwa Mbunge wa Monduli na Mkuu wa wilaya Mstaafu Luteni Mstaafu Lepilal Ole Molloimet aliyefariki dunia Jumapili iliyopita amezikwa leo wilayani Longido.

Luten Molloimet amefariki dunia kwa ugonjwa wa shinikizo la damu, moja ya viongozi waliohudhuria mazishi hayo ni mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA, Edward Lowasa pamoja na Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.

Mgombea CCM Akamatwa Akigawa Rushwa

$
0
0
Mgombea wa nafasi ya Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Kilangala, Halmashauri ya Wilaya ya Lindi, Jenga Mohamedi  na wajumbe saba wa Mkutano Mkuu wa kata wa chama hicho wamekamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wakidaiwa kupokea na kutoa rushwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 18, Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Lindi, Steven Chami amesema watu nane wamekamatwa akiwamo Mgombea ukatibu aliyekutwa akitoa rushwa kwa wajumbe ili achaguliwe.

Kwa mujibu wa Chami, tukio hilo limetokea jana saa mbili asubuhi kwenye eneo la uchaguzi huku watuhumiwa wakiwa  na fedha Sh 2,000  kila mmoja huku mpambe wa mgombea huyo alikutwa na bulungutu kiasi hicho cha fedha zenye thamani ya Sh 50,000 na orodha ya majina ya wajumbe wa mkutano huo.

Alisema watuhumiwa wanashikiliwa  na Taasisi hiyo hadi mahojiano yatakapo kamilika na hatua zingine za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Mbunge Aishauri Serikali Kusitisha Ulaji Samaki

$
0
0
Mbunge wa Kahama Mjini, Jumanne Kishimba (CCM), amesema kuna haja ya serikali kusitisha ulaji wa samaki nchini kama uvuvi wa samaki hautakiwi.

Amesema pamoja na kwamba serikali inapiga vita kupitia operesheni sangara katika Ziwa Victoria, operesheni hiyo haiwezi kukubaliwa kwa sababu inaumiza wavuvi.

Kishimba ameyasema hayo bungeni leo alipokuwa akichangia bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya mwaka wa fedha wa 2018/19.

“Mji wa Mwanza umejengwa kupitia pamba na madini, na hao samaki wanaopigwa marufuku kuvuliwa nao wamechangia kwa sehemu kubwa ukuaji wa mji huo naiomba serikali iwagawie wavuvi vifaranga wa samaki ili zao la samaki liweze kuinufaisha serikali na wananchi kwa ujumla,” amesema.

Kubenea: Mbunge CCM Akikwamisha Bajeti Hii Nisilipwe Mshahara

$
0
0
Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema), amesema kama atatokea Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi CCM) akakwamisha bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ataruhusu mshahara wake asilipwe.

Amesema pamoja na kwamba baadhi ya wabunge wa CCM wanaonyesha kutoridhishwa na baadhi ya bajeti za wizara lakini hawana uwezo wa kuzuia bajeti kwa kuwa wanazuiwa na chama chao kufanya hivyo.

Kubenea ameyasema hayo bungeni leo alipokuwa akichangia bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2018/19.

Katika hatua nyingine kubenea ameliambia bunge kwamba anatarajia kuwasilisha hoja binafsi bungeni akitaka bunge liunde kamati maalumu kuchunguza operesheni sangara inavyotekekezwa katika Ziwa Victoria.

“Operesheni hiyo lazima ichunguzwe kwa sababu imeumiza wavuvi na wananchi kwa ujumla,” amesema.

Naye Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa (CCM) amesema matatizo yaliyoko nchini yamesababishwa na baadhi ya wataalamu ikiwamo kupiga chapa mifugo huku wakijua wanaharibu ngozi.

Mpina Awaomba Wabunge Kumuunga Mkono

$
0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amelieleza bunge jinsi operesheni sangara ilivyofanyika kwa mafanikio katika Ziwa Victoria licha ya malalamiko juu ya utekelezaji wake.

Kutokana na hali hiyo Mpina pia amewataka wabunge kumuunga mkono kwa kuwa kazi wanayopambana nayo ni nzito na inahitaji ushirikiano.

Amesema mafanikio yaliyopatikana katika operesheni hiyo ni pamoja na idadi ya samaki kuongezeka.

Akihitimisha bajeti ya wizara yake aliyoiwasilisha bungeni jana jijini Dodoma leo, Mpina amesema wakati wa utekelezaji wa operesheni hiyo wamefanikiwa kukamata nyavu haramu 555431, kilo 181217, mabondo kilo 5147,pikipiki 269, na pia magari 564 yalikamatwa.

“Pamoja na wabunge kulalamikia operesheni sangara hakuna mbunge hata mmoja aliyewahi kunipa ushahidi wa jinsi wavuvi wanavyonyanyaswa kupitia operesheni hiyo,” amesema Mpina.

Akithibitisha jinsi operesheni hiyo inavyofanyika vizuri amesema wakati wa ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa hivi karibuni wilayani Ukerewe, hakukuwa na malalamiko yaliyotolewa na wananchi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya May 19

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Jeshi la Magereza Lamjibu Sugu

$
0
0
Jeshi la Magereza nchini limekanusha taarifa zilizoibuliwa na Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi kuhusu kukosekana kwa sare za wafungwa zaidi ya 600, katika gereza la Ruanda alipokuwa amefungwa.

Msemaji wa Jeshi hilo Lucas Mboje, amesema kwamba sio kweli kwamba wafungwa hawana sare na hakuna kitu kama hiko, isipokuwa kuna mahabusu ambao wapo mule wakiendelea kusubiri kesi zao, na ndio huenda ambao aliwaona bila sare.

“Hiko kitu hakipo, halafu asichanganye mambo, kuna mahabusu ambao wao wanajulikana kwa mujibu wa sheria hawavai sare, sasa asichanganye, mtu akishafungwa inajulikana lazima avae sare, sasa kuna mahabusu pia, sio kweli kama kuna tatizo la sare hakuna mtu anakosa sare, hebu fikiria wafungwa karibia 600 kwenye gereza moja wakose sare ni kitu ambacho hakiwezekani, hiyo itakuwa ni issue nyingine”, amesema Lucas Mboje.

Mbunge Joseph Mbilinyi (Sugu) alipotoka jela kwa msamaha wa Rais alisema kwamba alilazimishwa kuvaa sare za jela wakati kuna watu amewakuta gerezani zaidi ya mia 6 wamekosa sare na wapo mule ndani.

Wanaume Waliokaidsi Wito wa Makonda Waanza Kusakwa

$
0
0
Jeshi la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limeanza kuwasaka wanaume zaidi ya 1,000 waliokaidi wito wa kufika kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, baada ya kudaiwa kutelekeza watoto.

Wanaume hao ni miongoni mwa waliotajwa na wanawake waliofika kwa Makonda kuomba msaada wa kisheria baada ya kudai kutelekezwa na wenzi wao.

Jumla ya wanawake 17,000 walifika katika ofisi hizo kwa ajili ya kuomba msaada wa kisheria, lakini kutokana na wingi huo ni 7,000 waliohudumiwa.

Makonda aliwaita wanawake na wanaume wenye watoto ambao walitelekezwa na wenza waliozaa nao kwa siku 15 katika ofisi zake jijini Dar es Salaam na wanaume 2008 waliridhia kulea watoto wao.

Mkuu wa Mkoa aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam, wakati akitangaza kamati aliyoiunda kuchunguza tatizo la watoto kutelekezwa, iliyohusisha wanasheria, maofisa ustawi wa jamii na wadau wengine, inayoongozwa na Mwanasheria na Wakili wa Kujitegemea, Albert Msando.

Kamati hiyo yenye wajumbe 11 imepewa mwezi mmoja na itawahoji wananchi waliofika katika ofisi hizo kupata msaada wa kisheria ili kujua wanavyohudumia kwenye ngazi ya Ustawi wa Jamii kabla ya kufika hapo, namna kesi za watoto zinavyoendeshwa na kama sheria iliyopo ina upungufu.

Makonda alisema kati ya idadi ya wanaume hao wapo waliokamatwa kutoka ndani na nje ya mkoa wa Dar es Salaam na kwamba kazi hiyo inaendelea.

“Zoezi la kuwakamata wanaume ambao walikaidi agizo la kuitikia wito wangu linaendelea na tayari nimeshakabidhi majina zaidi ya 1,000 kwa Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa na wengine wameshaanza kukamatwa na wapo kutoka mikoa mbalimbali,” alisema Makonda.

Alisema wapo wanaume waliojitokeza kuitikia wito katika siku ambazo walishafunga kutoa huduma ili nao wasikilizwe.

Aidha alisema katika usikilizaji huo jumla ya familia 4,644 ziliruhusiwa kumaliza kesi zao katika ngazi za manispaaa huku watu 10,000 wakikosa huduma kutokana na ofisi yake kuelemewa na idadi ya watu.

“Sikuweza kuhudumia watu wote waliojitokeza kwasababu walikuwa wengi kuliko uwezo wangu, hivyo watu 10,000 hawakupata huduma na ndiyo sababu ya kuunda kamati hii ili kupata ufumbuzi wa kudumu,” alisema Makonda.

Pia alisema alizisaidia kupata mawakili ambao hawatawatoza fedha familia zaidi ya 100 ambazo ziliamua kumaliza matatizo hayo mahakamani.

“Wanawake wanapata shida na watoto hata wakitaka kudai haki zao mahakamani hawawezi kupata kwa sababu mawakili wanataka fedha kwa hiyo wanawake 100 waliamua kwenda mahakamani nimewatafutia mawakili wa kuwatetea bure,” alisema Makonda.

Aidha, alisema kutokana na kuwapo kwa wimbi la wazazi kutelekeza watoto, kuna ongezeko la zaidi ya watoto 5,000 wa mitaani katika Jiji la Dar es Salaam.

Alisema ili kukabiliana na changamoto hiyo ndiyo sababu amekuwa akitafuta mbinu mbalimbali za kulitatua na si kupunguza tatizo.

“Watu wanasema Makonda anaanzisha mambo na kuyaacha bila kumalizika, mimi nawaeleza kuwa si kweli, suala hili nilianza nalo kwa kuwaondoa watoto wanaoomba omba barabarani na hii ni sehemu ya nne ya mwendelezo wake,” alisema Makonda.

Pia Makonda alisema baada ya kamati hiyo kukamilisha kazi yake, wataiwasilisha ripoti hiyo kwa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto na Wizara ya Katiba na Sheria ili mapendekezo yake yaweze kufanyiwa kazi.

Naye Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Wakili Msando, aliahidi kuwa ataifanya kazi hiyo kwa uaminifu na uadilifu mkubwa kuanzia jana ingawa ni kazi ngumu.

Waziri Mkuu awapa onyo wakadiriaji majengo nchini

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi wajiepushe na vitendo vya rushwa ili kuhakikisha miradi inayotekelezwa inalingana na thamani ya fedha inayotumika.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana  wakati akifungua semina endelevu ya 29 ya Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, iliyofanyika Jijini Dodoma.

’’Epukeni vitendo vya rushwa ambavyo huisababishia Serikali hasara kubwa na kuleta usumbufu kwa wananchi. Ni matumaini yangu kuwa mtafanya kazi kwa weledi na kufuata maadili ya taaluma zenu’’ Majaliwa.

Alisema wataalamu hao ni vema wakahakikisha majengo wanayobuni yanakuwa bora katika muonekano na mandhari yake iwe yenye kuvutia na yenye kuzingatia utunzaji wa mazingira na matumizi bora na endelevu ya nishati.

Aidha Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuipongeza Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi kwa kuchagua mada inayohusu jukumu la wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi katika kuendeleza viwanda hapa nchini.

Alisema anatambua kuwa ujenzi wa viwanda unaendana na ujenzi wa miundombinu kama majengo, barabara, madaraja, miundombinu ya nishati na viwanja vya ndege, ambayo ni muhimu katika kuimarisha uchumi wa viwanda.

"Hivyo, wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi mna mchango mkubwa sana katika kufikia uchumi wa viwanda. Nitoe rai kwa Bodi ihakikishe kuwa miradi yote ya majengo pamoja na miundombinu mingine inashirikisha wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi katika ubunifu na usimamizi wa ujenzi wake.’’

Mwanafunzi Afariki Kwa Kulipukiwa na Betri ya Simu

$
0
0
Mwanafunzi wa darasa la nne katika shule ya msingi Sabasaba jijini Mwanza, Dotto Baraka (13) amefariki dunia baada ya kulipukiwa na betri ya simu aliyokuwa akiiunganisha na radio chakavu.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amethibitisha tukio hilo ambapo amesema limetokea Mei 17, mtaa wa Igoma Mashariki jijini Mwanza.

“Baada ya kutoka shuleni, marehemu akiwa na watoto wenzake alianza kutengeneza radio chakavu kwa kuchukua betri ya simu na kuunganisha kwenye nyanya za radio hiyo akitumia mdomo ndipo mlipuko ulipotokea na kusababisha kifo chake," amesema Kamanda Msangi.

Aidha Kamanda Msangi ameongeza kuwa wakati tukio hilo linatokea, wazazi wa watoto hao walikuwa safarini huko wilayani Kahama mkoani Shinyanga. Hata hivyo katika tukio hilo hakuna mtoto mwingine aliyejeruhiwa.

Makonda ayakana makontena Yaliyoko Bandarini

$
0
0
Utata umeendelea kuandama umiliki wa makontena 20 yaliyotajwa na Mamlaka ya Mapato (TRA), kuwa miongoni mwa yale yatakayopigwa mnada kwa kukaa bandarini muda mrefu, baada ya mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kukana kuwa sio ya kwake.

Awali, TRA ilitoa tangazo katika gazeti la Daily News, ikisema mtu aitwaye Paul Makonda bila kubainisha kama mtajwa ni mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam au la, anamiliki makontena 20 yenye bidhaa mbalimbali zikiwamo samani katika bandari kavu ya DICD.

Hata hivyo, akizungumza jana wakati akizindua kamati ya mapendekezo kuhusu wanawake waliotelekezwa na wenza wao, Makonda alisema hajui chochote na amesikia habari hizo kwenye magazeti kama walivyozisikia watu wengine.

“Sidhani kama nahusika na jambo lolote lile na sijui chochote, hilo unalolisema hata mimi nimesoma kwenye magazeti kama ulivyosoma wewe. Nafikiri zilikuwa ni habari za jana na leo nimesoma nyingine,” alisema.

Makonda alisema Serikali hufanya kazi zake kwa maandishi na yeye hana nakala yoyote inayohusiana na mzigo huo.

“Sio suala la kwangu kabisa, nimekusikia wewe kama mimi nilivyosikia jana (juzi) na ninafikiri tutaendelea kusikia hivyo hivyo na ndio maana katika hizo habari hakuna sehemu yoyote umeona nimenukuliwa kusema kama ni mali zangu,” alisema Makonda.

Hata hivyo, Februari 16, Makonda alikaririwa na  gazeti la Serikali la HabariLeo kuwa alipokea makontena 20 yenye samani zitakazotumika katika ofisi za walimu zinazoendelea kujengwa ukiwa ni sehemu ya shehena ya makontena 36.

Ilielezwa kuwa samani hizo za ofisini zilizokuwa na thamani ya Sh2 bilioni, zilitolewa na Watanzania wanaoishi Marekani wanaojulikana kama Six Region Diaspora Council.

Mei, 12 kaimu kamishna wa Forodha na Ushuru wa TRA, Ben Asubisye alisema wamiliki wa mizigo hiyo wanatakiwa kuikomboa ndani ya siku 30 kuanzia siku hiyo. Katika tangazo hilo lenye orodha ya makontena zaidi ya 800, jina la Paul Makonda limejitokeza mara 20 akiwa mpokeaji wa makontena 20 yakiwa na bidhaa kadhaa, zikiwamo samani.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo alisema juzi kuwa mamlaka hiyo imetoa notisi ya siku 30 kwa waagizaji wa mizigo ambayo imekaa bandarini kwa zaidi ya siku 90.

“Tangazo lililotolewa ni notice (taarifa) kwa wahusika ili wakomboe mizigo yao ndani ya siku 30. Isipokombolewa itanadiwa. Mizigo hiyo inaweza kuwa ni ile ambayo haijalipiwa kodi au hata ile iliyolipiwa lakini haijaondolewa,” alisema.

Alipoulizwa kama shehena hiyo ni mali binafsi ya Makonda au ya ofisi yake, Kayombo alisema: “Majina yaliyoandikwa kwenye magazeti ndiyo taarifa za consignees (wapokeaji) zilizopo kwenye nyaraka.”
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images