Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ofisa Mauzo Kizimbani Kwa Kuchapisha Taarifa za Uchochezi Telegram

$
0
0
Ofisa Mauzo wa Kampuni ya Aggrey&Clifford, Razack Hamad (26) amefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na kosa la kuchapisha taarifa za uchochezi kupitia mtandao wake wa Telegram.

Wakili wa serikali, Patrick Mwita amedai mbele ya Hakimu Mkazi, Martha Mpazi kuwa mshtakiwa anakabiliwa na kosa la kuchapisha taarifa ya uchochezi kinyume na kifungu cha 53(1)(c) na 52(1)(a) cha Sheria ya Habari Namba 12, ya mwaka 2016.

Inadaiwa mshtakiwa ametenda kosa hilo, Machi 9, mwaka huu akiwa jijini Dar es Salaam ambapo alitumia mfumo wa kompyuta katika simu yake kupitia mtandao wake wa Telegram kwa kuandika; “Nimepata wazo kwa group jingine huko tunaweza kukwepa gharama pia kuandika hata kwenye kuta za wazi #April 26 Magufuli Out, Pinga Dictator” Maneno ambayo yangeibua chuki kwa Watanzania.

Mshtakiwa amerudishwa rumande kwa kushindwa kutimiza masharti yaliyomtaka kuwa na wadhamini wawili watakaosani bondi ya Sh milioni tano. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Mei 24, mwaka huu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 13

Mbunge: ''Serikali imeshindwa kuzuia bidhaa feki''

$
0
0
Mbunge wa Wawi (CUF), Ahmed Ngwali ameitaka serikali kukiri wazi kwamba imeshindwa kuzuia uingizwaji wa bidhaa bandia nchini licha ya jitihada ambazo serikali inatangaza kuzifanya lakini bado bidhaa hizo zimeeendela kuingia  nchini.

Mbunge huyo amesema hayo Bungeni Mei 11, 2018 wakati wa kuchangia hoja bajeti ya Wizara ya viwanda, biashara na uwekezaji kwa mwaka wa fedha 2018/2019 na kuongeza kuwa polisi ndiyo watuhumiwa wakubwa katika uingizwaji wa bidhaa hizo.

“Serikali iseme tu kama imeshindwa kuzuia bidhaa bandia nchini,  lakini polisi ambao unasema katika kitabu chako,  mnataka kutumia mpaka Interpol katika kuzuia bidhaa feki, polisi hao wenyewe ndiyo wanashiriki katika mambo hayo ya kuingiza bidhaa feki, sasa hiyo Interpol gani mnataka kutumia? Mheshimiwa Mwijage hilo mlirekebishe” alisema Ngwali.

Mbunge huyo ameongeza kwamba serikali imekua inatumia mifumo mbalimbali ikiwemo ukaguzi wa mizigo bandarini lakini tatizo la uingizwaji wa bidhaa bandia umeendelea kuwa mkubwa.

Kwa upande mwingine Mbunge Ngwali amesema mahitaji ya gypsum nchini ni makubwa kuliko uwezo wa uzalishaji wa viwanda vya ndani ambavyo vipo vinne tu na vinauweo wa kuzalisha gypsum milioni tano tu wakati mahitaji ya gypsum nchini ni zaidi ya milioni 10 hadi 12.

Mradi wa Stiegler’s Gorge kuanza Julai Mwaka Huu

$
0
0
Waziri  wa Nishati, Dk Medard Kalemani amesema kazi ya ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme kwa nguvu za maji ya Mto Rufi ji eneo la Stiegler’s Gorge, unatarajiwa kuanza Julai mwaka huu.

Dk Kalemani alisema jijini hapa jana kuwa hatua hiyo ya kuanza kwa mradi inatokana na kazi ya tathmini ya kumpata mkandarasi wa ujenzi kukamilika. 

Akizungumza wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Dk Kalemani alisema mradi huo utaanza baada ya taratibu zote za kiutendaji kukamilika, ambako mradi huo mkubwa wa umeme utaongeza megawati 2,100, zaidi ya megawati 560 zinazozalishwa katika miradi mingine ya maji. 

Dk Kalemani alisema kwenye mradi huo wa Mto Rufiji, kinachofanyika sasa ni maandalizi kwa taasisi za serikali zinafanya kazi ya kumpata mkandarasi.

Alisema kazi ya sasa ni kila taasisi kutengeneza miundombinu wezeshi ikiwamo kupeleka umeme kwenye vijiji vitatu ambako mradi unapita. Alisema matayarisho ya mradi huo yalishaanza muda mrefu. 

“Kazi ya tathmini ya kumpata mkandarasi imekamilika, baada ya kumpata mkandarasi kazi za ujenzi zinatarajiwa kuanza Julai mwaka huu,” alisema Dk Kalemani. 

Alisema eneo la mradi huo limo ndani ya Pori la Akiba la Selous katika mipaka ya mikoa ya Morogoro na Pwani, ambalo linachukua eneo lisilozidi asilimia tatu ya mradi.

Akiwasilisha mada katika mkutano huo, Mhandisi John Mageni alisema mradi huo wa maji katika maporomoko ya mto Rufiji uliasisiwa na Rais wa Kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere katika miaka ya 1960, na mwaka 1972, Serikali ya Tanzania na Serikali ya Norway kupita iliyokuwa Mamlaka ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Rufiji (RUBADA) walifanya upembuzi yakinifu kama maandalizi ya kuendeleza mradi. Mageni alisema mradi huo ungezalisha umeme wenye uwezo wa megawati 850, na kiasi cha nishati ya umeme GWh 5,420.

Alisema Julai 2017, Rais John Magufuli aliamua kuanza utekelezaji wa mradi huo ili kuzalisha umeme wa angalau megawati 2,100 ndani ya miaka mitatu ambapo iliundwa kamati ya wataalamu kutoka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) ili kufanya maandalizi ya utekelezaji wa mradi, na baadaye kusimamia ujenzi baada ya mkandarasi kupatikana. 

Alisema hali ya sasa ya mradi ni ujenzi wa usanifu wa awali, tuta kuu la bwawa aina ya Gravite Roller Compacted Contrece (RCC), njia mbili za kuchepusha maji wakati wa ujenzi pamoja na matuta mawili ya kuzuia maji kwenda sehemu ya ujenzi na tuta kuu la bwawa.

Alitaja sababu za kuwapo kwa mradi huo ni kupatikana kwa umeme wa uhakika na wa bei nafuu utakaosaidia maendeleo na ustawi wa jamii pamoja na kuvutia uwekezaji katika sekta ya viwanda. 

Aidha, kupata umeme wa ziada kiasi cha kuuza nchi jirani pamoja na kuhamasisha ukuaji wa uchumi kwa ujumla na wa mwananchi mmoja mmoja kutokana na kuongezeka kwa uwekezaji katika sekta mbalimbali za kiuchumi, pia kupunguza athari za mafuriko katika Mto Rufiji kwa vijiji na miji iliyo chini ya eneo la mradi. 

Alisema bwawa hilo litakuwa na eneo la kilometa za mraba 914, urefu wa kilometa 100, na upana wa bwawa hadi kilometa 25. Alisema kutazalishwa ajira za kudumu na za muda hadi kufikia 10,000 wakati wa mradi wa miezi 36.

Waziri wa Afya: Upimaji UKIMWI baa sio lazima

$
0
0
Waziri  wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema upimaji wa Kifua Kikuu (TB) na Ukimwi kwenye baa hautakuwa wa lazima.

Akizungumza wakati wa maadhimisho wa miaka 30 ya Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi (NACP), Mwalimu alisema baada ya kutolewa taarifa ya kuwapo mpango huo watu wengi wamekuwa na hofu. 

“Tutatekeleza mpango wa kusogeza huduma za upimaji TB na ukimwi kwenye baa, ila hautakuwa wa lazima, tutachofanya ni kuwashawishi wananchi kutumia fursa ya kusogezewa huduma hiyo,”alisema.

Aidha, alisema kwa sasa wizara yake iko katika mkakati wa kufanyia marekebisho ya Sheria ya Ukimwi kwa lengo la kuruhusu watu kujipima mwenyewe, kutoa fursa kwa vijana kuanzia miaka 15 kwenda kupima ukimwi bila kupata ridhaa ya wazazi au walezi. 

“Haya ni maeneo ambayo kama tutayafanyia marekebisho tutaweza kusaidia kuongeza kasi ya kudhibiti maambukizi ya Ukimwi,” alisema.

Katika hatua nyingine, Mwalimu aliagiza kuanzia Julai mosi mwaka huu, watu wanaoishi wa virusi vya Ukimwi kupewa dawa za miezi mitatu badala ya sasa ya kupewa kwa miezi mwili. 

Agizo alilitoa kutokana na Mwenyekiti wa Baraza la Watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi, Justin Mwinuka kudai kuwa utaratibu wa kupewa dawa za miezi miwili umekuwa ukiongezea gharama, kwani wamekuwa wakitakiwa kupima afya zao kila baada ya miezi mitatu. 

Waziri huyo alisema utaratibu huo wa kuwapa dawa kwa miezi mitatu mitatu uanze haraka isipokuwa kwa wale ambao wanaonekana hawataweza kutunza dawa hizo au ambao ndio kwanza wanaanza kutumia dawa hizo.

Baba Diamond Agombaniwa na Warembo Kirabuni

$
0
0
Warembo wawili ambao walifahamika kwa majina ya Ashura na Zubeda, wamedaiwa kuzichapa kavukavu chanzo kikitajwa kuwa ni kumgombea baba wa msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Abdul Juma.

Tukio hilo lililokusanya watu lilitokea hivi karibuni katika baa moja maarufu kwa jina la Suma iliyopo maeneo ya Magomeni-Kagera jijini Dar ambayo baba wa msanii huyo anadaiwa kuwa anakwenda mara kwa mara kupata ‘kinywaji’.

Taarifa zaidi zinaarifu kuwa, warembo hao walitangulia kufika katika baa hiyo na kupiga stori pamoja huku wakipata kilevi lakini baadaye alipotokea baba Diamond na kujumuika nao, kila mmoja alianza kujitapa kuwa ni wake. 

“Yani walianza kubishana. Ghafla wakaanza kushikana na ndipo watu walipowawahi na kuwaamua. Baba Diamond kukwepa soo akaamua kutoweka eneo hilo,” kilidai chanzo

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 14

ACT Wazalendo Yataka Wanafunzi Waruhusiwe Kufanya Siasa Vyuoni

$
0
0
 Chama cha ACT Wazalendo kimeitaka Serikali kuwaruhusu wanafunzi wa vyuo vikuu wafanye siasa vyuoni kwa taratibu zilizowekwa kwa sababu vyuo ni kitovu cha mabadiliko ya jamii.

Wito huo umetolewa jana Mei 13 na Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa chama hicho, Ado Shaibu ambaye anapinga kauli ya Rais John Magufuli aliyoitoa alipotembelea Chuo cha Kilimo cha Sokoine (Sua) kuwataka wanafunzi wasifanye siasa vyuoni.

Shaibu alisema historia inaonyesha kwamba viongozi wengi wa taifa hili walishawahi kuwa viongozi wa serikali za wanafunzi walipokuwa vyuoni. Amesisitiza kwamba maisha ya siasa wakiwa vyuoni ndiyo yaliwapa ujasiri wa kuingia kwenye ulingo wa siasa.

"Kupiga marufuku siasa vyuoni ni kujenga taifa la vijana waoga, wasiokuwa na uwezo wa kuhoji. Vijana msiache kuhoji mambo ya msingi kwa jamii zenu, hiyo ndiyo maana ya usomi," alisema Shaibu.

Katibu huyo alitoa mifano ya baadhi ya viongozi waliokuwa viongozi vyuoni kuwa ni pamoja na Waziri Mkuu wa zamani, Joseph Warioba ambaye amesema mwaka 1965 alikuwa mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi wa vyuo vikuu hapa nchini.

Alimtaja pia Spika wa zamani, Samuel Sitta ambaye pamoja na wenziwe walifukuzwa chuo mwaka 1966 kwa kufanya mgomo kupinga matabaka hapa nchini, ajenda ambayo Mwalimu Nyerere aliibeba kwenye Azimio la Arusha.

"Siasa za vyuo vikuu zimewekewa utarabitu wake, sasa tukianza kuwadhibiti hata vijana walio vyuoni tunatengeneza taifa la namna gani?" Alihoji Shaibu na kusisitiza kwamba serikali ina wajibu wa kuhamasisha vijana kujitosa kwenye siasa ili Taifa lipate viongozi bora siku zijazo.

Ng'ombe 12 Vibudu Wakamatwa Jijini DAR....Ni Waliokufa, Walikuwa Wakichinjwa Ndani ya Lori

$
0
0
Ngombe 12 wanaosadikiwa kufa jana wamekutwa wakichinjwa ndani ya lori eneo la mtaa wa Wazo kwa ajili ya kusambazwa kwenye mabucha ya ngo’mbe.

Mmoja wa mashuhuda  Issa Ibrahim amesema wakati anaelekea msikitini  jana saa 10 alfajiri aliliona gari aina ya lori limesimama pembezoni mwa barabara na alipolisogelea aliwaona watu wakiwachuna ng’ombe waliokufa.

Amesema aliwahoji na kuwakataza wasiendelee kuwachuna ngombe hao kwa kuwa dini hairuhusu kula vibudu lakini watu hao walikaidi na kuendelea kazi yao.

“Wale watu walikuwa wengi kila mmoja alikuwa na kisu chake huku wakichuna ngombe hao, kwa kuhofia usalama wangu nilipiga simu msikitini ndipo walikuja eneo hili ili tuungane tuweze kuwakamata lakini wote walikimbia na kuacha nyama zao kwenye gari,” amesema Ibrahim.

Katibu wa Kamati ya Afya na Mazingira mtaa huo, Ally Kitokos amesema matukio ya kuchinjwa ng’ombe waliokufa hujitokeza mara kwa mara na ndiyo maana  hivi karibuni mmiliki wa machinjio ya Wazo alimfukuza kazi mchinjaji mkuu baada ya kupingana na kitendo cha kuchinja ngombe waliokufa.

“Leo hii tunaona ng’ombe 12 wamekufa kibudu na wanaendelea kuwachuna kwa ajili ya kupelekwa kwenye mabucha, wakati mchinjaji mkuu wa mwanzo alifukuzwa kwa kosa hilo,” amesema.

Serikali Yaagiza Tani 70,354.35 za Sukari Kutoka Nje ya Nchi.....Tizeba Asema Hakutakuwa na Upungufu

$
0
0
Na Bashiri Salum, Dodoma
Serikali imeagiza sukari kiasi cha tani 70,354.35 kutoka nchi za nje lengo likiwa ni kujipanga ili kuhakikisha kuwa hapatokei upungufu wa bidhaa hiyo hapa nchini.

Akizungumza na vyombo vya habari hivi karibuni waziri  wa kilimo Mhe. Dkt. Charles Tizeba amesema kuwa tani 60,539.35 ya sukari itaanza kuingia hapa nchini katikati ya mwezi Mei 2018 ambapo kiasi kilichobaki cha tani 9,815 kitaingia mwezi  June mwaka 2018.

Aidha  Dkt. Tizeba amefafanua kwamba hakutarajiwi kuwa na upungufu wa sukari hapa nchini  kwa sababu hadi kufikia tarehe 10 mei 2018 katika maghala ya wazalishaji na wafanyabiashara kulikuwa na tani 78,147.67 za sukari na kiasi kingine  tani 25,441.25 kipo Bandarini .

Kwa kiasi cha sukari ambacho tayari kipo hapa nchini kikijumlishwa na kiasi ambacho kitaingia hivi karibuni kutoka nje ya nchi ni dhahiri kwamba  nchi haiwezi kupata upungufu wa bidhaa hiyo, alisema Mhe.Waziri.

Awali Dkt.Tizeba  alisema kwamba mahitaji ya sukari nchi nzima ni tani 630,000 ambapo kati ya hizo, tani 145,000 ni kwa ajili ya matumizi ya viwandani na tani 485,000 ni kwajili ya matumizi ya kawaida.

Hata hivyo mapitio yanaonesha kwamba  msimu wa mwaka 2017/18  viwanda vya ndani vilizalisha tani 306,226  za sukari kwa matumizi ya kawaida  ambapo mwisho wa msimu huu uzalishaji umefikia tani 307,481.76 aliongezea Dkt. Tizeba.

Akimalizia taarifa yake Mhe. Tizeba amebainisha kuwa kwa kiasi ambacho sukari imeagizwa kutoka nje Pamoja na viwanda vya ndani inadhihirisha kwamba hakutakuwa na upungufu wa aina yeyote ya sukari hapa nchini na ikizingatiwa  kuwa viwanda vitaanza uzalishaji mwingine mwezi mei ambapo ukarabati (services ) itakuwa imekamilika .

Kigwangalla amteua mlimbwende wa Miss Tanzania kuwa balozi wa utalii wa Pori la Akiba Selous

$
0
0
Na Hamza Temba-WMU-Dodoma
.............................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amemteua mshindi wa taji la Miss Journalism Tanzania, 2018, Witness Teddy Kavumo (21) kuwa balozi wa utalii wa Pori la Akiba Selous.

Amefanya uteuzi huo mwishoni mwa wiki Jijini Dodoma baada ya mazungumzo na mwanamitindo huyo aliyemtembelea ofisini kwake kwa ajili ya kuomba ufadhili wa kuandaa  mradi wa kijamii ambao ni sehemu ya shindano atakaloshiriki la taji la Dunia la Miss Journalism 2018 litakalofanyika Oktoba 27 Jijini Arusha.

Kufuatia uteuzi huo, Dk. Kigwangalla amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania, Devotha Mdachi kuandika barua ya uteuzi kwa balozi huyo mpya sambamba na kumkabidhi hati ya uteuzi ili pamoja na mambo mengine aweze kunadi vivutio vya utalii vya pori hilo.

Wakati huo huo, Dk. Kigwangalla amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA, Dk. James Wakibara kuandaa safari maalum ya balozi huyo mteule aweze kutembelea Pori la Akiba Selous kwa ajili ya kuona na kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu hifadhi hiyo kwa ajili ya utangazaji.

Sambamba na pori hilo atatembelea pia mapori mengine ikiwemo BBK (Burigi, Biharamulo na Kimisi) mkoani Kagera na Mpanga Kipengele mkoani Njombe ambapo  atatumia fursa hiyo kufanya mahojiano na wasichana wa vijiji jirani na hifadhi hizo kwa ajili ya mradi wa kijamii wa kuwainua ikiwa ni sehemu yenye alama muhimu kwenye shindano hilo la Dunia la Miss Journalism 2018.

Awali akiwasilisha ombi lake kwa Waziri Kigwangalla la ufadhili wa safari yake ya ushiriki wa mashindano hayo, Witness pia aliomba kupewa fursa ya kuwa balozi wa Tanzania kwenye moja ya sekta ikiwemo Misitu, Nyuki au Utalii.

Mbali na kushikilia taji la Miss Journalism Tanzania 2018, Witness amesema amewahi kushinda mataji mengine manne makubwa ya kimataifa ya ulimbwende nchini Afrika ya Kusini anakosomea urubani kwa sasa.

Anasema, "Miongoni mwa mataji hayo ni Miss Garden Route 2017, ambalo ni taji la kitaifa la kuhamasisha na kukuza sekta ya Maliasili na Utalii nchini humo, licha ya kuwa ugenini nilitumia fursa hiyo kunadi vivutio vya utalii vya Tanzania.

"Mashindano haya yalihusisha washiriki 600 na wote walikuwa na asili ya kizungu, mimi peke yangu nilikuwa na asili ya kiafrika na niliibuka mshindi".

Aliyataja mataji mengine kuwa ni Miss Bees Cape Town 2017 kwa ajili kuhamasisha uhifadhi wa sekta ya nyuki na mataji mawili ya kimkoa ambayo ni Miss Asla Capetown 2017 na Miss Carnival Mosselbay 2017.

Mataji mengine ya kitaifa aliyowahi kushinda Witness hapa nchini ni pamoja na Miss Arusha Higher Learning 2014 na Miss Northern Zone 2014.

Mashindano hayo ya Dunia ya Miss Journalism 2018 yanahusisha pia uhamasishaji wa maendeleo ya utalii, utamaduni wa amani, uandishi wa habari na kupiga vita ugonjwa wa ukimwi na Malaria.

Pori la akiba Selous ndio hifadhi kubwa kuliko zote nchini ikiwa na ukubwa wa kilomita za mraba takriban 50,000 katika mikoa ya Pwani, Morogoro, Lindi, Mtwara na Ruvuma. Mwaka 1982, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Uneso) lilitangaza eneo hilo kuwa moja ya eneo la Urithi wa Dunia na kuanza kuhifadhiwa.

Fisi Avamia Wapenzi na Kuua Mmoja......Mwingine Kajeruhiwa Vibaya

$
0
0
Mkazi wa wilayani Igunga, mkoani Tabora ameuawa na fisi na mwingine kujeruhiwa baada ya kushambuliwa na mnyama huyo katika Kata ya Ziba, wakati wakirejea nyumbani kutoka kwenye klabu ya pombe.

Azizi Kombe, Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ziba, alimtaja aliyeuawa ni Mwajuma Masanja (37), mkazi wa Kijiji cha Iduguta wilayani Nzega na Shija Maneno (35), mkazi wa Kitongoji cha Ipuli Kijiji cha Igumila Kata ya Ziba ambaye amelazwa katika Hospitali ya Rufani Nkinga na hali yake ni mbaya.

Mtendaji huyo alifafanua watu hao walikuwa ni mtu na mpenzi wake ambao walikuwa wakinywa pombe za kienyeji kwenye klabu iliyopo Kata ya Ziba na kuongeza kuwa baada ya kufika saa 3 usiku waliamua kuondoka kurudi nyumbani.

Hata hivyo, Kombe alibainisha wakati wakiwa njiani kurejea nyumbani walishambuliwa na fisi eneo la vichaka ambapo alimng’ata Mwajuma sehemu za makalio na tumboni, hali iliyomlazimu Shija amsaidie huku akipiga kelele za kuomba msaada.

Mtendaji huyo alisema wakati mwanaume huyo akitoa msaada kwa mpenzi wake, ndipo fisi alimng’ata usoni na ndipo aliposhindwa kutoa msaada na fisi huyo aliendelea kumshambulia mwanamke huyo hadi alipopoteza maisha papo hapo.

Kwa mujibu wa mtendaji huyo, muda mfupi wananchi walifika eneo hilo wakiwa na baadhi ya askari wa kituo kidogo cha polisi Ziba kisha kufanikiwa kumuua fisi huyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Willibrod Mutafungwa, alithibitisha kuuawa kwa mwanamke huyo kwa kushambuliwa na fisi na kwamba fisi huyo aliuawa.

Kwa mujibu wa Kamanda Mutafungwa, majeruhi alikimbizwa Hospitali ya Rufani ya Nkinga ambako alilazwa na kutoa wito kwa wananchi mkoani Tabora kuwa makini na wanyama hatari kwa kutotembea usiku kwenye maeneo hatarishi kwa ajili ya usalama wao.

Raia wa Senegal ateuliwa Kuwa Makamu wa Rais Benki ya Dunia

$
0
0
Makhtar Diop, raia wa Senegal ameteuliwa kuwa makamu wa rais wa Benki ya Dunia (WB) atakayekuwa anasimamia miundombinu.

Diop alitangazwa kushika nafasi hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita na hivyo kumfanya kuwa miongoni mwa maofisa wa ngazi za juu wa taasisi hiyo muhimu duniani.

Taarifa iliyotolewa na benki hiyo inasema Diop anayaanza majukumu hayo mapya baada ya kuwa Makamu wa Rais anayesimamia Afrika katika miaka sita iliyopita akifanikisha kutolewa kwa mikopo yenye thamani ya Dola 70 bilioni za Marekani.

Ndani ya miaka hiyo sita, Diop alisimamia miundombinu ya usafiri na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), nishati na madini, fedha na ushirikiano wa sekta ya umma na binafsi (PPP).

‘Katika majukumu yake mapya, Diop atasimamia ufadhili wa miundombinu ya fedha katika ufanikishaji wa maendeleo endelevu hivyo kupunguza tofauti iliyopo kati ya nchi zilizoendelea na zinazoendelea,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Uteuzi wa Diop anayetajwa kuwa miongoni mwa Waafrika 100 wenye ushawishi zaidi duniani utaanza Julai Mosi.

Alipokuwa akiisimamia Afrika, inaelezwa alisimamia upatikanaji wa fedha za kufanikisha miradi ya aina tofauti akihamasisha zaidi ubunifu na uvumbuzi wa kisayansi.

Alihakikisha Afrika inapata umeme wa uhakika na nafuu huku ikiunganishwa kwa barabara zinazopitika wakati wote.

Ndani ya benki hiyo, Diop ameshahudumu kama mkurugenzi wa fedha, sekta binafsi na miundombinu Amerika Kusini na Visiwa vya Caribbean.

Kati ya mwaka 2009 na 2012 alikuwa mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia, Brazil ambako alisimamia utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo.

Alishawahi kuwa Mkurugenzi Mkazi katika nchi za Kenya, Eritrea na Somalia.

Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini, (TMA) Yatoa Tahadhari ya Mvua Kubwa Hadi May 17

$
0
0
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imetoa tahadhari ya kunyesha mvua kubwa kwa siku tano kuanzia jana, ambazo zinaweza kuleta mafuriko katika maeneo ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara na Visiwa vya Unguja na Pemba.

Katika taarifa ya TMA iliyotolewa jana Mei 13, mvua hizo zilizoanza kunyesha  zitaendelea mpaka Mei 17 mwaka huu.

TMA imesema athari zinazinaweza kutokea ikiwemo mafuriko ambayo yanaweza kusababisha kuvurugika kwa usafiri, barabara kubwa kutopitika na maisha ya watu kuwa hatarini  kutokana na maji kujaa au kupita kwa kasi.

Pia imetoa wito kwa wakazi wa maeneo hayo kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa pamoja na tahadhari zitakazotolewa.

Anusurika kifo baada ya kujifungia kwenye kontena bandarini

$
0
0
Mkazi wa Miembeni mjini Unguja, Hassan Juma amenusurika kifo baada ya kutolewa ndani ya kontena alikojifungia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Hassan Nassri Ali alithibitisha tukio hilo na kwamba wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo.

Msimamizi wa makontena katika Bandari ya Malindi, Ibrahim Abdallah jana alisema chanzo cha Hassan anayekadiriwa kuwa na miaka 30 kuingia kwenye kontena na kujifungia hakijajulikana.

Abdallah alisema wakiwa katika kazi zao za kila siku eneo hilo juzi saa moja asubuhi walisikia sauti ikitoka ndani ya kontena lililopo juu ya jingine na kuzua taharuki miongoni mwao ikidaiwa ‘nakufaa’.

Alisema mtu huyo aliashiria kuomba msaada na walimuuliza yeye ni nani na alijitaja jina.

“Baada ya kutaja jina tulifungua kontena hilo ambalo alikuwa amelifunga na kumtoa akiwa na hali mbaya kiafya, tulimpeleka Hospitali ya Mnazi Mmoja na kupatiwa huduma ya kwanza,” alisema.

Naye msemaji wa hospitali hiyo, Hassan Makame alisema katika hatua za awali wamempatia huduma ya kwanza ili kuhakikisha hali yake inarejea kawaida. Alisema hajafanyiwa vipimo kutokana na hali yake kuonekana kudhoofu.

“Tumemtia dripu ili apate nguvu ili kuendelea na huduma nyingine za vipimo,” alisema Makame.

Kuli katika bandari hiyo, Mohamed Khamis Makame alisema ni mara ya kwanza kutokea tukio la aina hiyo eneo hilo, hivyo wanapaswa kuimarisha ulinzi.

Jibu la Hamisa Mobetto kuhusu kufunga ndoa na Diamond

$
0
0
Mwanamitindo Hamisa Mobetto amejibu iwapo yupo tayari kufunga ndoa Diamond Platnumz mara baada ya muimbaji huyo kuweka wazi atafanya hivyo mwaka huu.

Akizungumza katika uzinduzi wa Filamu ya Mama kutoka kwa Aunt Ezekiel, Hamisa alipoulizwa iwapo yupo tayari kuolewa na Diamond alijibu kwa sasa huwezi kuzungumzia hilo.

“Siwezi kujibu hilo swali,” aliongea Hamisa kwa kifupi.

Katika hatua nyingine Hamisa alidai kuwa yeye sio single mother kwani wazazi wenzie wanamsaidia katika malezi ya watoto.

“You can’t call your self Single Mother kama unasaidiwa kulea mtoto na baba watoto wako, so facts is mababa watoto wangu wote wananisaidia kulea watoto vizuri, kwa hiyo siwezi nikasema single mother sababu nasaidiwa kulea watoto,” alisema Hamissa.

Hamisa ni mama wa watoto wawili ambao wa kwanza alizaa na Majay na wapili alizaa na Diamod Platnumz.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

TEMBELEA KATIKA BLOG YETU HAPA>>>;

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Wananchi Watishia 'Kumuua' Mwalimu Mkuu, Wanamtuhumu Kuwachapa Wanafunzi na Kuwalimisha Shamba Lake

$
0
0
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wazazi wa kata tatu wilayani hapa Mkoa wa Mara, wamemtaka mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Nyanungu, Otieno Nicholaus kuchagua kuhama au kupoteza maisha.

Kauli hiyo ilitolewa wakati wa mkutano wa wazazi uliofanyika hivi karibuni shuleni hapo.

Wazazi hao walimtuhumu mwalimu huyo kwa kuwapiga watoto hadi kuwajeruhi wanapokataa kulima shambani kwake.

Mmoja wa wazazi wa watoto wanaodaiwa kupigwa, Muniko Sibora alisema Mei 7 mwalimu huyo alimpiga mwanaye baada ya kuvaa yeboyebo kutokana na kuwa na kidonda mguuni.

Pia, alisema aliwapiga watoto wa Mwita Nyasongo na Ngocho Matiku kwa kuwa hawakwenda na majembe kupalilia mahindi yake.

“Huyu mwalimu anachofanya siyo sahihi, anatakiwa ahame vinginevyo mambo yatamharibikia,” alisema.

Kaimu ofisa elimu wilaya, Hawamu Tambwe alikiri kupata taarifa hizo na kwamba amemtuma mratibu elimu kata kufuatilia undani wa suala hilo na kupata taarifa ya maandishi.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Nyanungu, Turuka Magabeu alikiri kupokea malalamiko ya wazazi kuhusu mwalimu huyo kuwapiga watoto. 

“Inaelezwa katika tukio la mwisho aliwapiga na kuwaumiza watoto watatu kiasi cha kupelekwa hospitali,” alisema Magabeu.

Naye mjumbe wa kamati ya shule hiyo, Museti Mwikwabe alisema Aprili 30 aliitisha kikao cha kamati lakini wajumbe walikataa wakiwamo wazazi wote.

“Mei 4 aliwapeleka shambani watoto wakati wa masomo na tukamweleza, akaja juu na Mei 7 akaamua kuwapiga na kuwaumiza watoto huku akiwaambia waje watueleze wazazi,” alisema.

Mwalimu Otieno hakuweza kupatikana shuleni hata simu yake ilikuwa haipatikani kwa kile kilichodaiwa kuwa anaishi kwa kujificha.

Akizungumza suala hilo, diwani wa Kyambahi, Mtoni Manyaki alikiri kupata taarifa hizo na ameitisha kikao cha kamati ya maendeleo kata Mei 21 ili kulijadili.

Naye mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya, Juma Hamsini alisema baada ya kupata taarifa ameagiza timu yake kuchukua hatua haraka na tayari wamepiga marufuku kuwatumia wanafunzi kulimia walimu.

“Hivi karibuni katika Shule ya Msingi Mlimani kulikuwa na kesi kama hiyo niliandika barua ya kupiga marufuku, wanafunzi wanaweza kulima shamba la shule tena si wakati wa masomo,”alisema.

Polisi wilayani hapa wanadai wanaendelea kumsaka mwalimu huyo kuhusiana na tuhuma zilizowasilishwa.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images