Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Okoa Ndoa Yako Sasa : Je Umepungukiwa Na Nguvu Za Kiume Au maumbile Au Mpenzi Wako Hakutimizii Utakacho?

$
0
0
Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sabubu ya kutokuwa na nguvu za kiume au uume wako mdogo dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA;
 1 KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA YA MWENZI WAKO
2 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA 
3 UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE 
4 KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

MAKAKANUA; HII NI dawa ya maumbili madogo...hufusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba, dawa za uzaz,Mi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo 

FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU. KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA. piga simu 0743362017. 0789234653 DR AGU

KKKT yawatenga Maaskofu wake watatu kwa Kuupuza Waraka

$
0
0
Maaskofu watatu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ‘wametengwa’ na kanisa hilo kwa tuhuma za usaliti unaohusishwa na masuala ya kisiasa.

Mbali na Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dkt Alex Malasusa aliyeripotiwa jana na vyombo vya habari kwamba ametengwa, wengine ni Dkt Solomon Massangwa wa Dayosisi ya Kaskazini Kati na Dkt Lucas Mbedule wa Dayosisi ya Kusini Mashariki.

Hatua ya kuwatenga maaskofu hao ilifikiwa katika mkutano wa Baraza la Maaskofu wa KKKT uliofanyika Aprili 24 na 25 jijini Arusha kujadili masuala mbalimbali ikiwamo kufanya tathmini ya waraka wake wa Sikukuu ya Pasaka lililoutoa Machi 24. 
 
Habari za uhakika kutoka ndani ya Baraza hilo zinasema kwamba pia limewapa maaskofu hao watatu muda wa kuandika barua kueleza kama wanakubali au kukataa waraka huo ambao lilisema walishiriki kuuandaa na ikiwa hawatafanya hivyo hatua zaidi dhidi yao zitachukuliwa.

Kwa hatua hiyo waumini wa dayosisi zao hawatakuwa na uwakilishi kwenye Baraza ka Maaskofu hivyo kupoteza fursa ya kujadiliwa kwa masuala yanayowahusu.

Pia , maaskofu waliotengwa hawataruhusiwa kufanya shughuli za kiroho nje ya dayosisi zao wala maaskofu wengine 24 waliobaki hawatashiriki masuala yoyote ya kiimani katika dayosisi hizo tatu na uamuzi wa mwisho kuhusu nafasi zao umeachwa kwa waumini wao.

Waraka huo walioutoa baada ya kikao kilichofanyika Arusha Machi 15 mwaka huu, mbali ya kuzungumzia masuala ya kiroho, umetaja changamoto tatu na kuzifikisha kwa waumini wake “ili ziongeze mzigo wa kuliombea taifa letu na viongozi wake.”

Changamoto zilizotajwa katika waraka huo uliopewa jina ‘Taifa Letu Amani Yetu’ na kusainiwa na maaskofu wote 27 wa kanisa hilo nchini ni hali ya kijamii na kiuchumi, maisha ya siasa na masuala mtambuka ikiwamo Katiba Mpya.

Baraza hilo liliagiza maaskofu wote kuusimamia ili usomwe katika sharika zote nchini. swahilitimes.com. Hata hivyo, imeelezwa kuwa maaskofu 25 kati ya 27 waliokutana mkoani Arusha, katika tathmini, walibaini wenzao hao kuwasaliti ikielezwa kuwa baada ya kuupokea hawakusimamia kuhakikisha unasomwa kama walivyokubaliana Machi 15 wakiuhusisha na siasa.

“Unajua ule waraka walioutoa maaskofu ulikuwa mzito na kishindo chake mlikiona, sasa kabla ya kusomwa kuna watu waliwafuata baadhi ya maaskofu na kuwatishia wasiusome na wao wakakubali bila kujua wanachokifanya ni makosa,” kilidokeza chanzo na kuongeza:

“Ndiyo maana kama unakumbuka, Askofu Mkuu wa KKKT, Frederick Shoo alitoa kauli ya kuwaonya wanaoupinga.”

Alipoulizwa jana kwa simu kuhusu kutengwa, Askofu Mpedule alisema, “aaa, siyo kweli muulize huyo aliyekupa taarifa atakuwa na majibu mazuri.”

Alipoulizwa kama alisimamia waraka huo kusomwa kama walivyokubaliana alijibu kwa kifupi, “Hapana sina jibu.”

Askofu Masanhwa kwa upande wake alisema, “Sina barua inayosema nimetengwa,” Alipoulizwa kama alisimamia waraka huo kusomwa alijibu, “Ulisomwa katika makanisa Mengi.”

Hata hivyo, mawasiliano ya simu yalikatika katikati ya mazungumzo na alipopigiwa tena hakupokea na kutuma ujumbe mfupi wa maandishi akisema yupo kikaoni.

Jitihada za kumpata Dkt Malasusa ziligonga mwamba kutokana na simu yake ya mkononi kutopatikana.

Juzi jioni alipopigiwa simu kuzungumzia suala hilo hakuwa tayari kuzunguzia kwani baada ya mwandishi kumweleza kuhusu hatua hiyo aliomba apigiwe kwa simu ya ofisi na alipofanya hivyo hakupokea.

Jana, Dkt Shoo ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini hakupatikana kuzungumzia suala hilo.

Machi 25, Askofu Shoo akiwa katika Usharika wa Masama Kati, Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro baada ya Mchungaji Kiongozi wa Usharika huo, Pray Usiri kuusoma waraka huo, aliwaomba Wakristo na Watanzania kuutafakari kwa makini huku akiwaonya wanasiasa kuepuka kuwagawa Watanzania akisema hawatakaa kimya.

Waraka huo uliokuwa a kurasa nane ulipongeza jitihada zinazofanywa na Serikali katika ukusanyaji kodi  huku ukitaka kuwapo kwa jitihada za mara kwa mara baina ya sekta binafsi na Serikali za kuimarisha uhusiano mwema.

Huo ni waraka wa pili kutoka kwa viongozi wa dini baada ya Februari mwaka huu, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), kutoa ujumbe wa Kwaresma uliosainiwa na maaskofu wake 35 uliozungumzia masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Chanzo: Mwananchi

Kikwete Ammwagia Sifa Rais Magufuli

$
0
0
Mbunge wa Chalinze kupitia CCM, Mh. Ridhiwani Kikwete ameonesha kuridhishwa na kazi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli hususani katika kuboresha miundombinu nchini.

Ridhiwani ameyasema hayo baada ya kujionea ub ora wa daraja la Kelema wilayani Chemba mkoani Dodoma, alipopita eneo hilo ikiwa ni sehemu ya safari yake kuelekea kwenye maadhimisho ya siku ya Muungano yaliyofanyika jijini humo.

Kupitia mtandao wa Twitter Mh. Ridhiwani ameandika, ''Nikiwa na mke wangu, kuangalia uzuri wa nchi yetu. Hakika ni nchi nzuri yenye kuvutia. Hongera sana Rais wangu @MagufuliJP kwa kusimamia Miundombinu, pia Asante @WorldBankAfrica kwa kusaidia maendeleo''.

Aidha katika ujumbe huo wa Ridhiwani pia ameishukuru Benki ya Dunia kwa misaada inayotoa hususani ujenzi wa barabara ambao ndio umekuwa kipaumbele chake katika nchi zinazoendelea ikizisaidia kwa mikopo ya masharti nafuu.

April 27 Rais Magufuli alizindua barabara ya Kondoa-Babati, yenye urefu wa Km 251. Katika uzinduzi huo aliwataka wananchi kutunza miundombinu hiyo, haswa alama za barabarani kwani hiyo ndio barabara kuu kwa upande wa Kaskazini.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0753471612, 0623386305, 0715249530 -DR KUZENZA

Ummy atoa onyo juu ya chanjo ya Saratani ya Mlango wa uzazi

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, ametoa onyo kwa wataalamu wa Afya nchi nzima kutothubutu kutoa chanjo ya Saratani ya Mlango wa uzazi  kwa watoto wenye umri wa miaka 14 bila ridhaa za wa wazazi.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa chanjo ya Saratani ya mlango wa uzazi kwa watoto wenye umri wa miaka 14, akiwa mkoani Tanga ambapo pia ameshauri  wanawake kupima kama wana tatizo hilo.

"Naomba kutoa rai nikiwa hapa Tanga , mtoto achanjwe pale ambapo mzazi wake akiwa ameridhia. Msimchanje mtoto bila ridhaa. Hili ni agizo kwa nchi nzima," Ummy.

Pamoja na hayo Waziri Ummy amesema kwamba mpaka sasa wagonjwa wengi hufika hospitalini wakiwa na asilimia 80 za ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi.

Mbali na hayo Waziri huyo ameweka wazi kwamba vituo vyote vya afya vinavyomilikiwa na serikali vimejengewa uwezo na kupewa vifaa vya ajili ya matibabu ya saratani ili kupunguza tatizo la wagonjwa.

Mwanafunzi Chuo cha Pasiansi Mwanza ahofiwa kufa maji Mto Grumeti

$
0
0
Mwanafunzi wa Chuo cha Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi kilichopo jijini Mwanza, Wambura Otaigo (19) anahofiwa kufa maji baada ya kuzama ndani ya Mto Grumeti wilayani hapa mkoani Mara wakati wanachota maji ya matumizi kambini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Juma Shija alisema tukio hilo lilitokea Aprili 23 na hadi sasa mwanafunzi huyo hajaonekana.

Mto Grumeti unamwaga maji Ziwa Victoria, hivyo kuibua hofu ya mwili wa mwanafunzi huyo kutopatikana kutokana na wingi wa maji unaotokana na mvua za masika zinazonyesha sehemu mbalimbali nchini.

Kamanda Shija alisema wakati wa tukio hilo mwanafunzi huyo aliyekuwa kwenye mafunzo kwa vitendo katika Kituo cha Mazoezi cha Fort Ikoma wilayani Serengeti, alikuwa na wenzake ambao walijaribu bila mafanikio kumsihi asiingie majini kutokana na mto kufurika na maji kutiririka kwa kasi.

Mto Grumeti unadaiwa kuwa na idadi kubwa ya mamba, hali inayozidisha hofu ya mwanafunzi huyo kupatikana licha ya juhudi za askari polisi, wanafunzi wenzake pamoja na wananchi za kumtafuta.

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO 0754372325/ 0689013109/ 0620806813 

HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Rais Magufuli kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Iringa

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli anatarajia kufanya ziara ya kikazi mkoani Iringa kuanzia leo  tar 29 mwezi huu hadi tar 4 mwezi ujao.

Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, ambapo alisema kuwa wanatarajia kumpokea rais Dkt. Magufuli leo  tar 29 mwezi huu.

Alisema kuwa mara baada ya kupokelewa Rais Dkt. Magufuli atazindua barabara ya kijiji cha Migori kwenda Fufu kupitia Iringa mjini.

“Siku ya Mei Mosi Rais Dkt. Magufuli atakuwa mgeni rasmi, ambapo kitaifa yatafanyika mkoani hapa ambapo kutakuwepo na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri Mkuu, Spika wa bunge na viongozi wengine,”alisema Masenza

Mkuu huyo wa mkoa wa Iringa amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi ambapo zimepangwa kufanyika mkoani humo.

Hata hivyo, ameongeza kuwa Rais Magufuli akiwa ziarani mkoani humo atazindua miradi mbalimbali ya kimaendeleo vikiwemo viwanda.

Serikali kuendelea kukomesha ajira hatarishi za watoto

$
0
0
Serikali imedhamiria kuendelea kukomesha ajira hatarishi za watoto ili kuhakikisha kuwa watoto wanalindwa na kuwapa nafasi stahiki kulingana na sheria na kanuni zilizopo nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama alipohudhuria katika kilele cha Siku ya Afya na Usalama Mahali Pa Kazi Duniani inayoadhimishwa kila mwaka Aprili ambapo Kitaifa ilifanyika Mkoani Iringa.

Amesema kuwa katika mapambano hayo ya ajira hatarishi kwa watoto ni moja ya utekelezaji wa kampeni zinazolenga kuharakisha utekeleezaji wa vipaumbele vilivyomo kwenye lengo namba (8) la maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa ambalo ni kuboresha mazingira ya wafanyakazi na kukomesha ajira mbaya kwa watoto.

“Tuendelee kupiga vita ajira mbaya kwa watoto kwa kuzingatia kampeni zilizopo hasa ile ya kuboresha mazingira ya wafanyakazi ifikapo mwaka 2030 pamoja na kukomesha ajira mbaya za watoto ifikapo mwaka 2025,” amesema Mhagama

Aidha, amesema kuwa katika kuhakikisha watoto wanakuwa na mazingira salama, lazima kuwe na mikakati  ya pamoja baina ya utatu katika masuala ya kazi na ajira ikiwemo na kujenga utamaduni wa kujikinga na vihatarishi sehemu za kazi vinavyoweza kusababisha kuhatarisha afya na usalama wa wafanyakazi.

Aidha kama Taifa lazima tuoneshe umuhimu wa kuhakikisha kampeni hii inakuwa na matokeo chanya na kuendelea kuwa na Taifa lenye maendeleo.

Hata hivyo, ameongeza kuwa kulingana na matokeo ya Utafiti wa Mtakwimu Mkuu wa Serikali uliofanyika mwaka 2014 na matokeo yake kuchapishwa mwaka 2016 ulibainisha kuwa, hali ya ajira  hatarishi za watoto kuzidi kuwa mbaya zaidi katika sehemu za mashambani, sekta ya madini, misitu na uvuvi.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Makamu Wa Rais Ahani Msiba Wa Kandoro

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha kumbukumbu ya maombelezo ya Marehemu Abbas Kandoro aliyefariki jana kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpa pole mke Marehemu Abbas Kandoro, Mariam Kandoro nyumbani kwa marehemu Mbweni jijini Dar es salaam.
Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

Makala: Wizara Ya Maliasili Na Utalii Inavyoimarisha Sekta Ya Uhifadhi Na Utalii Nchini

$
0
0
Na Hamza Temba-WMU
………………………………………………..
Wakati huu tunapoadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ni takriban miaka miwili sasa na miezi kadhaa tangu Serikali ya awamu ya tano, inayoongozwa na Mhe. Rais, Dk. John Pombe Joseph Magufuli iingie madarakani.

Itakumbukwa kuwa katika hotuba yake ya kwanza ya kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa mjini Dodoma, Mhe. Rais Magufuli alitoa vipaombele kadhaa vya kutekelezwa na wizara zake huku Wizara ya Maliasili na Utalii akiipa vipaombele vikuu vitatu ambavyo ni kukabiliana na ujangili, kutatua migogoro ya mipaka kwenye maeneo ya hifadhi na kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Wizara ya Maliasili imeendelea kutekeleza vipaombele hivyo pamoja na jukumu lake la msingi la kuhifadhi na kusimamia matumizi endelevu ya rasilimali za maliasili na malikale, na kuendeleza Utalii kwa faida ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho.

Ujangili
Wizara imefanikiwa kuanzisha mikakati mbalimbali ya kukabiliana na ujangili na biashara haramu ya wanyamapori ambayo imeanza kuzaa matunda.

Mikakati hiyo ni pamoja na kuanzishwa kwa Kikosi Kazi Maalum cha Kudhibiti Uhalifu wa Misitu na Wanyamapori nchini ambacho kilianzishwa mwezi Julai, 2016 sambamba na kuimarishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) ambayo ilianza majukumu yake rasmi tarehe 1 Julai, 2016.

Mikakati mingine ni mabadiliko ya mfumo wa utendaji kutoka ule wa kiraia kwenda wa Jeshi Usu, matumizi ya teknolojia ya ndege zisizokuwa na rubani (drones) kwa ajili ya doria, ushirikishwaji wa wananchi kwenye uhifadhi na matumizi ya mbwa maalum wa kunusa ili kutambua nyara katika viwanja vya ndege na bandari.

Kupitia mikakati hiyo, mwaka 2016/2017 Wizara kupitia taasisi zake iliendesha doria mbalimbali ndani na nje ya maeneo yaliyohifadhiwa na kufanikiwa kukamata watuhumiwa 7,085 kwa makosa mbalimbali. Aidha, meno ya tembo 129 na vipande 95 vyenye uzito wa jumla ya kilo 810.03 vilikamatwa.

Vielelezo kadhaa pia vilikamatwa ikiwemo silaha za kivita 48, silaha za kiraia 150, risasi 1,058, magobore 406, silaha za jadi 22,307 na roda 120,538.

Jumla ya kesi 2,097 zilifunguliwa katika mahakama mbalimbali na kesi 802 zilimalizika. Watuhumiwa 472 katika kesi 262 walifungwa jela jumla ya miezi 42,153 na watuhumiwa 79 katika kesi 43 waliachiwa huru huku watuhumiwa wengine 469 katika kesi 276 wakilipa faini ya jumla ya shilingi  milioni 452.1.

Katika kuelekea kwenye Mfumo wa Jeshi Usu, Wizara imeendesha mafunzo kwa watumishi 661 kuhusu ukakamavu, uongozi na ukusanyaji wa taarifa za kiintelijensia kuhusu Ujangili. Watumishi walioshiriki mafunzo hayo ni 139 kutoka TAWA, 388 kutoka TANAPA, 117 kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro na 17 kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania.

Kutokana na jitihada hizi hali ya ujangili imepungua kwa kiasi kikubwa. Kwa mfano, katika Pori la Akiba Selous idadi ya Tembo waliouwawa imepungua kutoka tembo 17 mwaka 2015/16 hadi tembo 7 mwaka 2016/17.

Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni, wanyamapori hasa tembo wameanza kuonekana katika maeneo mbalimbali ambayo kwa kipindi kirefu hawakuwa wakionekana, mfano hivi karibuni tembo kadhaa walionekana katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Aprili 18 mwaka huu, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na Balozi wa Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke ofisini kwake mjini Dodoma, alinukuliwa akisema kuwa ujangili hapa nchini umepungua kwa zaidi ya asilimia 50.

Alisema katika kipindi cha miezi sita iliyopita hadi kufikia mwezi huu wa Aprili hakuna mauaji mapya ya wanyamapori yaliyoripotiwa kuhusiana na ujangili na kwamba nyara zinazokamatwa hivi sasa ni masalia ya zamani ambayo yanatafutiwa masoko.

Alisema mafanikio hayo yametokana na juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama sambamba na kuwashirikisha wananchi kwa kuimarisha ulinzi na doria za mara kwa mara za kiitelijensia katika maeneo ya hifadhi.

Utalii
Katika kuongeza idadi ya watalii nchini, Wizara imeendelea kutekeleza shughuli mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuimarisha ulinzi kwenye maeneo ya hifadhi, kuboresha miundo mbinu kwenye maeneo ya vivutio, kuanzisha huduma mpya za utalii pamoja na utangazaji.

Juhudi hizo zimewezesha ongezeko la watalii wa kimataifa kutoka 1,284,279 mwaka 2016 hadi kufikia 1,327,143 mwaka 2017 sawa na ongezeko la asilimia 3.2.

Aidha, mapato yanayotokana na utalii yameongezeka kutoka Dola za Marekani bilioni 2.1 mwaka 2016 hadi Dola za Marekani bilioni 2.2 mwaka 2017.

Sekta hii ya utalii imetoa ajira takriban 500,000 za moja kwa moja na ajira nyingine milioni moja zisizo za moja kwa moja kwa mwaka.

Sekta hii pia inachangia takriban asilimia 17.5 ya Pato la Taifa na wastani wa asilimia 25 ya fedha zote za kigeni.

Aidha, Wizara imedhamiria kupanua wigo wa vivutio vya utalii nchini kwa kufungua utalii wa Kanda ya Kusini ili kuongeza idadi ya watalii na mapato ya Serikali.

Kupitia dhamira hiyo Serikali imesaini mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia wa Dola za Marekani milioni 150, sawa na takriban shilingi bilioni 340 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa Kusimamia Maliasili na Kuendeleza Utalii wa Ukanda wa Kusini –REGROW.

Mradi huu ambao maandalizi yake yalianza mwezi Novemba 2014 ulizinduliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan tarehe 12 Februari, 2018 katika viwanja vya Kihesa Kilolo Mjini Iringa huku Kauli Mbiu yake ikiwa “Utalii kwa Maendeleo Endelevu- Karibu Kusini”.

Mama Samia alisema lengo la mradi huo ni kuongeza mchango wa sekta ya maliasili na utalii katika uchumi wa taifa kwa kuboresha vivutio vya utalii, miundombinu, usimamizi wa vivutio na kuongeza faida za kiuchumi kwa jamii zinazoishi jirani na maeneo ya hifadhi katika ukanda huo wa kusini.

Katika kuongeza jitihada za kutangaza utalii ndani na nje ya nchi, Wizara imeendelea kuongeza bajeti ya utangazaji ambapo Bodi ya Utalii Tanzania kwa mwaka wa fedha 2017/18 imeongezewa bajeti kufikia shilingi bilioni 6.6 ikilinganishwa na shilingi bilioni 4.1 mwaka 2016/2017 na bilioni 4.3 mwaka 2015/16.

Aidha, katika kufungua masoko mapya ya utalii nje ya nchi, Wizara inaangazia masoko mapya katika nchi za China, Israel, Urusi, Australia na nchi nyingine za Skandinavia.

Wananchi wanavyonufaika na uhifadhi
Wizara ya Maliasili inaendelea na juhudi za kuhakikisha wananchi wanaoishi jirani na maeneo ya hifadhi wananufaika na rasilimali zilizopo. Kupitia Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori, jamii zinanufaika kwa kupata ajira, kitoweo, elimu, miradi ya kijamii na kuongeza kipato.

Hadi hivi sasa jumla ya Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori 38 zimeanzishwa. Aidha, wananchi wanaoishi jirani na misitu wananufaika kupitia miradi ya ufugaji nyuki ambapo kupitia uwezeshaji wa Mfuko wa Misitu Tanzania miradi 254 ya kuboresha kipato cha jamii zinazoishi pembezoni mwa misitu imetekelezwa.

Miradi hiyo ni ya ufugaji nyuki ambapo vikundi vya ufugaji nyuki 399 na watu binafsi 27 wamewezeshwa kupata mizinga ipatayo 11,730.

Udhibiti wa migogoro baina ya wananchi na hifadhi
Katika kudhibiti migogoro ya mipaka kati ya wananchi na maeneo jirani na hifadhi, Wizara kwa kushirikiana na Taasisi za Serikali na Wadau imeendelea kuhakiki mipaka yote ya maeneo ya hifadhi na kuweka alama za kudumu na mabango ya tahadhari.

Hadi kufikia mwezi Mei, 2017 vigingi 14,755 vimesimikwa sawa na asilimia 62.4 ya vigingi 23,638 vinavyohitajika katika Hifadhi za Misitu, Mapori ya Akiba, Hifadhi za Taifa na Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro.

Aidha, kupitia program ya Panda Miti Kibiashara, Wizara imewezesha vijiji 48 kuandaa Mipango ya Matumizi Bora ya Ardhi katika Wilaya za Ludewa, Madaba, Makete, Mufindi, Njombe Mjini, Njombe Vijijini, Kilolo na Nyasa.

Mikakati mipya chini ya Waziri wa Maliasili, Dk. Hamisi Kigwangalla

Aidha chini ya Uongozi Mpya wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ipo baadhi ya mikakati yake mipya inayolenga kutoa uelekeo mpya wa kuimarisha sekta Maliasili na Utalii nchini.

Dk. Kigwangalla anaeleza mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kuanzisha kwa mwezi maalum wa Urithi wa Mtanzania (Tanzania Heritage Month) ambao utaadhimishwa mwezi Septemba kila mwaka, kuanzishwa kwa Makumbusho ya Marais Wastaafu waliotawala Tanzania mjini Dodoma na Kuboresha na kuendeleza utalii wa fukwe kwa kuanzisha Mamlaka ya Fukwe.

Mikakati mingine ni pamoja na kujenga makumbusho ya meno ya tembo katika miji ya Dar es Salaam, Dodoma, Arusha na Iringa pamoja na kutambua barabara iliyokuwa ikitumika katika biashara ya utumwa wakati wa ukoloni ili iweze kutumika kiutalii.

Akizungumzia migogoro ya mipaka iliyopo baina ya wananchi na maeneo ya hifadhi, Dk. Kigwangalla amesema Serikali itatatua migogoro hiyo kwa kushirikisha wananchi sambamba na kuwasaidia kutatua changamoto za msingi ambazo ni kuimarisha maeneo ya malisho ya mifugo, upatikanaji wa maji kwa ajili ya wananchi na mifugo, mpango bora wa matumizi ya ardhi na uendelezaji wa kilimo na ufugaji.

Kwa upande wa vitalu vya uwindaji wa kitalii, Dk. Kigwangalla amesema Serikali itafanya mabadiliko katika mfumo wa ugawaji vitalu vya uwindaji wa kitalii kutoka mfumo unaotumika hivi sasa wa Kamati “Administrative Allocation” na kutumia mfumo wa mnada “Auction”.

Lengo ikiwa ni kuongeza uwazi na kuruhusu nguvu ya soko kuamua bei ambapo mapato ya Serikali nayo yatatarajiwa kuongezeka maradufu. Ili kutekeleza hilo, sheria na kanuni zinafanyiwa marekebisho.

#MWISHO#

Askofu KKKT awaomba radhi waumini na maaskofu wenzake kwa kutousoma Waraka

$
0
0
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kusini Mashariki, Dk Lucas Mbedule amewaomba radhi waumini wa dayosisi hiyo na Baraza la Maaskofu kwa kutokusoma waraka uliotolewa wa sikukuu ya Pasaka.

Askofu Mbedule ameomba radhi leo Aprili 29, 2018 wakati wa Ibada ya iliyofanyika kanisa la Mtwara Mjini, amesema licha ya salamu hizo kutokusomwa, anaunga nazo na yupo pamoja na maaskofu wenzake.

Akisoma barua ambayo ameituma kwa Mkuu wa KKKT, Askofu Dk Fredrick Shoo na maaskofu wote wa kanisa hilo, Askofu Mbedule amesema baraka za mababa maaskofu zilishindwa kusomwa kwa sababu zilizojitokeza wakati huo.

“Kwa njia ya barua hii, kwanza napenda kuwaombeni radhi kwa kuwakosesha baraka za mababa maaskofu,” amesema Askofu Mbedule.

Amesema yeye alishiriki kuuandaa na kutia saini na yupo pamoja na maaskofu wenzake.

Kilimo cha Bangi Charuhusiwa Rasmi Zimbabwe

$
0
0
Nchi ya Zimbabwe imehalalisha uzalishaji wa bagi kwa matumizi ya kiafya na kisayansi.

Zimbabwe itakuwa nchi  pili kufanya hivyo barani Afrika baada ya Lesotho, ambayo ilitoa leseni yake ya kwanza kwa kilimo cha mmea huo mwaka uliopita.

Waziri wa afya David Parirenyatwa amechapisha sheria zinazowaruhusu watu na kampuni kupewa leseni ya kufanya kilimo cha bangi ambayo hufahamika nchini humo kama mbanje, na kwamba watu wa nchi hiyo sasa wanaweza kutuma maombi ya kulima bangi, na leseni yake itakuwa inaombwa upya kila baada ya miaka mitano, na itawaruhusu wakulima kumiliki, kusafirisha na kuuza bangi.

Watuma maombi watatakiwa kueleza ni wapi watafanyia kilimo chao, kiwango ambacho wataweza kuzalisha na kuuza na wakati wa kuzalisha bangi hiyo.

Nchini Zimbabwe ilikuwa ni haramu kupanda, kumiliki au kutumia mmea huo nchini Humo, na iwapo mtu atapatikana na makosa hayo anaweza kuhukumiwa kifungo cha hadi miaka 12 jela.

Msafara wa Rais Magufuli Wasimamishwa Barabarani.,.......Atoa Ujumbe Mzito Kwa Wakazi Iringa

$
0
0
Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, umesimamishwa na wananchi wa eneo la Migori mkoani Iringa ili kutoa kero zao zinazowakabili, kwa kiongozi huyo mkubwa wa nchi.

Msafara huo ambao ulikuwa ukipita kuelekea mkoani Irnga kwa ajili ya tukio la uzinduzi wa barabara ya Iringa Migori  yenye urefu wa km 189, umelalamikiwa kero mbali mbali zinazowakabili wananchi wa eneo hilo pamoja na changamoto zinazoikabili shule ya sekondari Nyerere iliyopo mkoani Iringa, na kutoa fedha taslim shilingi milioni 5 ili kusaidia ujenzi wa madarasa na nyumba za walimu.

Baada ya Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Walend Manga kuelezea hatua walizofikia za ujenzi wa nyumba za walimu wanazojenga kwa nguvu yao na wananchi, pamoja na kumshukuru Rais Magufuli kwa fedha zinazopelekwa mashuleni, Rais Magufuli alisikika akisema ..."Ahsante sana Mwalimu Mkuu, shule yenu ina jina zuri, jina la Nyerere, na mimi nitawaongezea milioni 5, sina milioni tano hapa!!? Hebu nisaidie hapa hapa kabisa, bahati nzuri nina milioni 5 hapa, nakupa hapa hapa, kazitumie vizuri, mimi huwa nafuatilia, siku moja nitapita hapa nicheki hizi milioni tano zimetumika wapi.

Sambamba na hilo Rais Magufuli amemtaka Mkandarasi aliyepewa jukumu la kusambaza miundombinu ya umeme kwenyye eneo hilo kukamilisha mapema, ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Aidha,  Rais Magufuli amewataka wanakijiji hao kuchapa kazi na kutumia barabara ya lami ya Iringa-Dodoma kujitajirisha.

“Barabara imekamilika mnaiona, itumieni ili mtajirike, limeni mazao kwa bidii na msafirishe kwenda sehemu mbalimbali za nchi,” amesema Rais Magufuli.

Aliwataka kutumia mvua zinazoendelea, kulima na kufuga ili waweze kunufaika.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0766340868

Serikali yabeba jukumu la kumtibu Mzee Majuto

$
0
0
Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amemtembelea msanii nguli wa filamu, Amri Athuman maarufu mzee Majuto na kueleza kuwa Serikali inabeba jukumu la matibabu yake.

Mzee Majuto alilazwa Aprili 23 baada ya kuzidiwa ghafla kutokana na kidonda cha operesheni ya henia aliyofanyiwa Julai mwaka jana jijini Tanga.

Akizungumza katika tukio hilo jana Aprili 28, 2018 Dk Mwakyembe amesema Serikali imeamua kumpeleka mzee Majuto nchini India kwa ajili ya matibabu zaidi.

 "Kwa kuanzia, tumeamua kumhamishia mzee Majuto katika hospitali ya Muhimbili ili kukamilisha maandalizi muhimu kabla ya safari ya India," amesema Dk Mwakyembe.

Amesema matibabu atakayopata mzee Majuto akiwa Muhimbili na akiwa nchini India yatagharamiwa na Serikali.

Katika hatua nyingine, kampuni zilizowahi kufanya kazi na mzee Majuto zimeitikia wito wa kumchangia huku Dk Mwakyembe akitoa wito kwa wadau mbalimbali kuendelea kumchangia ili kuwezesha familia yake kujikimu katika kipindi hiki ambacho anapatiwa matibabu.

Serikali kupiga marufuku uagizwaji wa Mita za Luku kutoka nje ya nchi

$
0
0
 Waziri wa Nishati, Dr. Medard Kalemani amesema kuanzia July 1,2018 serikali itasitisha rasmi uagiziaji wa mita za Luku ya umeme kutoka nje ya nchi ili kutoa fursa kwa wawekezaji wa ndani.

Dr. Kalemani ameyasema hayo wakati akizindua kiwanda cha kutengenezea mashine za Luku maeneo ya Mbezi, ambapo amesema uwepo wa wawekezaji wa ndani utaokoa muda na kupunguza gharama hasa katika sekta hiyo ya nishati.

Amesema kuwa usitishwaji huo ulitanguliwa na ule wa awali ambapo walisitisha uingizaji wa nguzo za umeme kutoka Afrika Kusini na Transformer kutoka India.

Amesema kuwa kuna faida nyingi kwa Mita hizo kutengenezwa nchi ikiwemo kuokoa muda wa uagiziaji na kupunguza gharama.

“June 2017 tulisitisha rasmi uingizaji wa nguzo kutoka Afrika Kusini, ambapo nguzo moja tulikuwa tunanunua Laki 3 hadi Laki 4, wakati ukinunua nguzo za hapa ndani ni Laki 2” amesema Kalemani

” Shirika la Tanesco limekuwa na mizigo mikubwa kwa sababu ya gharama ya kuagizia vifaa kutoka nje ya nchi,”-Kalemani

Pia Dr. Kalemani amesema kuna tatizo la ubora, kwani kuna baadhi ya nchi zina majina makubwa lakini bidhaa zao feki, kwani mwaka jana ziliungua transformer 100 kutoka India kwa wakati mmoja.

Adhabu ukikamatwa umetupa uchafu Dodoma

$
0
0
kiwa ni siku kadhaa zimepita tangu Rais John Magufuli kutangaza kuipa hadhi Dodoma kuwa jiji, Mkurugenzi wa jiji hilo Godwin Kunambi ameanzisha mpango wa kuwapatia bima za afya bure wafagiaji wa maeneo yanayozunguka jiji hilo ili kuweza kuwasaidia .

Kunambi kwa kushirikiana na Mkuu wa mkoa huo Dr Bilinith Mahenge wametangaza adhabu kwa watu wote watakaokutwa wanatupa uchafu katika maeneo yanayozunguka jiji hilo.

”Mtu akitupa uchafu Dodoma anaandikiwa kulipa na anaandikwa kwenye mtandao jina lake linabaki humo, makosa yakifika matano hadi manne tunatoa majina yao kwenye magazeti”. Amesema Kunambi
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>