Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Sababu za bajeti Wizara ya Afya kupungua

$
0
0
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema bajeti ya wizara hiyo mwaka 2018/19 imepungua kwa asilimia 19.6 ikilinganishwa na ya 2017/18 kutokana na dhamira ya Serikali kutumia fedha za ndani kuitekeleza.

Akijibu hoja zilizoibuka wakati wa mjadala wa hotuba ya bajeti ya wizara hiyo, Ummy alisema mwaka jana wabunge waliishauri Serikali kupunguza utegemezi kutoka wa wafadhili katika kutekeleza bajeti ya afya.

Bajeti ya wizara hiyo mwaka 2018/19 ni Sh898.3 bilioni tofauti na mwaka 2017/18 unaoishia Juni ya Sh1.07 trilioni.

“Waheshimiwa wabunge, mwaka jana wakati nawasilisha bajeti hapa mlieleza wazi kwamba bajeti inategemea wafadhili. Kilichotokea bajeti Wizara ya Afya kwa mwaka huu fedha za ndani zimeongezeka kutoka Sh628 bilioni hadi Sh681 bilioni lakini fedha kutoka kwa wafadhili zimeshuka,” alisema Ummy.

“Hii imeonyesha dhamira ya Rais John Magufuli kutaka kupunguza utegemezi wa wadau wa maendeleo katika kupunguza changamoto za Watanzania.”

Alisema lengo ni nchi kuanza kujipima yenyewe katika utekelezaji wa bajeti ili kuona ni kwa namna gani inaweza kutatua changamoto zilizopo.

Juzi, Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii ilieleza kuwa bajeti ya wizara hiyo imepungua kwa asilimia 19.6 na kwamba kutaleta athari katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Peter Serukamba alisema katika bajeti ya mwaka 2017/18, fungu la fedha za maendeleo, wizara ilitengewa Sh785 bilioni na hadi kufikia Februari Sh385.77 bilioni, kiasi ambacho ni sawa na asilimia 49 kilipokewa na ili kutekeleza miradi.

Alibainisha kuwa kati ya fedha hizo za maendeleo, Sh336.3 bilioni ni za kutoka vyanzo vya ndani na Sh449.5 bilioni kutoka vyanzo vya nje.

“Kamati imebaini fedha zilizopokewa kutoka vyanzo vya ndani ni Sh64.7 bilioni sawa na asilimia 19 ya fedha zilizoidhinishwa. Fedha za nje zilizopokewa ni Sh321 bilioni sawa na asilimia 71,” alisema.

Magufuli apokea ujumbe wa kamisheni ya amani AU

$
0
0
Rais John Magufuli amefanya mazungumzo na kamishna wa amani na usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Balozi Smail Chergui aliyewasilisha ujumbe wa mwenyekiti wa kamisheni hiyo, Moussa Faki Mahamat.

Chergui amesema jana  Aprili 20, 2018 katika mazungumzo na Rais Magufuli yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Taarifa ya Ikulu imesema viongozi hao wawili wamejadili masuala ya amani na usalama barani Afrika na hasa ukanda wa maziwa makuu.

Amesema pia wamejadili masuala ya wakimbizi, huku akimshukuru Rais Magufuli kwa ushauri, mchango wa mawazo na uzoefu katika kuimarisha amani na usalama.

Wakati huohuo, Rais Magufuli amekutana na msaidizi wa Rais wa Misri na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo, Ibrahim Roshdy Mahlab aliyewasilisha ujumbe kutoka kwa Rais wa Taifa hilo, Abdel Fattah el-Sisi.

Baada ya mazungumzo, Mahlab amesema wamejadili namna ya kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya Tanzania na Misri, ikizingatiwa kuwa zipo fursa nyingi ambazo nchi hizi mbili rafiki zinapaswa kuzifanyia kazi.

Mahlab amebainisha kuwa utekelezaji wa makubaliano yaliyowekwa wakati wa ziara ya Rais wa Misri, Abdel Fattah el-Sisi nchini umeanza ambapo tume ya pamoja ya ushirikiano kati ya nchi hizi imeshakutana nchi Misri na kuainisha maeneo yenye fursa na yanayopaswa kufanyiwa kazi.

Aliyemtukana Rais Magufuli Ahukumiwa Miaka Mitatu Jela

$
0
0
Wakili wa Kujitegemea Leonard Kyaruzi amehukumiwa kulipa faini ya Sh. 5,000,000  au kwenda jela miaka mitatu.
 
Alikutwa na hatia ya kumkashifu Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Dk. John Magufuli kwa kumwita Zuzu.

Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Godfrey Mwambapa, baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi wanne wa Jamhuri na utetezi wa mshtakiwa.

Katika hukumu hiyo, hakimu aliegemea katika maelezo yake ya onyo ambayo yamepita bila kupingwa kama kielelezo cha upande wa Jamhuri mahakamani hapo.

"Mahakama hii bila kuacha shaka imepitia ushahidi wa mashahidi wanne wa upande wa Jamhuri, imekuona una hatia, utalipa faini ya Sh. milioni tano ukishindwa utakwenda jela kutumikia kifungo cha miaka mitatu," alisema hakimu Mwambapa.

Katika kesi ya msingi, ilidaiwa kuwa Juni 2, 2016 katika jengo la Tanzanite lililopo Barabara ya Sam Nujoma, jijini Dar es Salaam,  mshtakiwa alichapisha taarifa kwenye mtandao wa Whatsapp kwa lengo la kumkashifu Rais Magufuli.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa alichapisha taarifa kwamba "Hivi huyu Pombe ni kwamba hana washauri? Hashauriki? Au zuzu? Bwege sana huyu jamaa, he doesn't consider the law in place before opening his mouth! Au na yeye anaumwa ugonjwa wa Mnyika" alinukuliwa mshtakiwa.

TCRA kuanza usajili wa wamiliki wa Blogu, Online Forums, Redio na Televisheni za Mtandaoni leo Aprili 21

$
0
0
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imetangaza kuanza zoezi la usajili wa wamiliki wa Blogu, Majukwaa ya Mtandaoni (Online Forums), Redio pamoja na Televisheni za mtandaoni kuanzia leo Jumamosi Aprili 21, 2018.

Taarifa ya TTCL kuhusu kuhusika kwenye tangazo lenye lugha isiyo na maadili

Korea Kaskazini yatangaza kuachana na makombora ya nyuklia

$
0
0
Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un ametangaza kusitisha majaribio ya makombora ya nyuklia kuanzia leo, ikiwa ni hatua ya kutengeneza mazingira bora zaidi ya mazungumzo kati yake na Korea Kusini.

Uamuzi huo wa Kim Jong-un umetangazwa na Shirika la Habari la Kikorea (KCNA). Kwa mujibu wa taarifa hizo, Kiongozi huyo amesitisha majaribio hayo ikiwa ni siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano mkubwa wa mazungumzo kati yake na viongozi wa Korea Kusini yenye lengo la kutatua mgogoro wa kinyuklia katika eneo hilo.

KCNA imeeleza kuwa Pyongyang inaweza kufunga kabisa vituo vyake vya utengenezaji wa mabomu hayo ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha uchumi wake na kutafuta amani katika eneo hilo.

“Hatuhitaji tena mpango wowote wa kufanya majaribio ya makombora ya nyuklia yanayoishia katika eneo hili au yanayovuka bara, na kwa sababu hiyo vituo vya kutayarisha makombora hayo vya kaskazini vimemaliza mpango wake,” KCNA imemkariri Kim Jong-un.

Kwa mujibu wa KCNA, Korea Kaskazini imeahidi kuunga mkono juhudi za kimataifa za usitishwaji wa majaribio ya nyuklia na kwamba haitatumia silaha za kinyuklia kwakuwa hakuna tishio tena dhidi ya nchi hiyo.

Kiongozi huyo pia anajiandaa kukutana kwa mara ya kwanza na rais wa Marekani, Donald Trump katika juhudi za kutafuta suluhu ya mgogoro wa kinyuklia kati ya nchi hizo na washirika wao.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

TEMBELEA KATIKA BLOG YETU HAPA>>>;

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Tundu Lissu Amvaa Spika Ndugai Baada ya Kudai Hakufuata Taratibu

$
0
0
Mbunge Tundu Lissu amefunguka na kudai sheria ya uendeshaji wa Bunge halijaweka masharti yeyote ya kupatiwa fedha za matibabu kama alivyo tangaza Spika wa Bunge Job Ndugai hivi karibuni na wala hakuna kifungu chochote kinachozungumzia kibali cha Hospitali ya Muhimbili au cha Rais Magufuli.

Lissu amebainisha hayo usiku wa kuamkia leo kupitia ukurasa wa kijamii zikiwa zimepita takribani siku tatu tokea Spika wa Bunge, Job Ndugai kutoa ufafanuzi juu ya matibabu ya Mbunge huyo kuwa Bunge haliwezi kuidhinisha fedha kwa ajili ya matibabu yake kwa kuwa halijapata vibali vitatu ambavyo vingemuwezesha kupata fedha za matibabu kutoka Bungeni.

"Ukweli ni kwamba kauli ya Spika Ndugai inathibitisha jinsi ambavyo Bunge limepoteza mamlaka na hadhi yake chini ya uongozi wake dhaifu. 

"Hata masuala ambayo Sheria haijampa Rais mamlaka, Spika Ndugai ameyakabidhi. Kauli hiyo ni uthibitisho pia wa jinsi ambavyo Bunge linaendeshwa bila kufuata sheria, kwa chuki na upendeleo wa kisiasa", amesema Lissu.

Pamoja na hayo, Lissu ameendelea kwa kusema "yeye amekwenda India mara nyingi kutibiwa kabla na baada ya kuwa Spika kwa gharama za Bunge. Mimi mbaya wao niliyepigwa risasi nikiwa nahudhuria vikao vya Bunge ninakataliwa matibabu kwa sababu zisizokuwa na msingi wowote. Sio kweli kwamba sikufuata utaratibu, kama maana ya neno hilo ni utaratibu uliowekwa na sheria.
 
"Kusema nisubiri kibali cha Bunge au cha Muhimbili au cha Rais Magufuli ilikuwa ni kunitakia kifo cha wazi. Katika mazingira ya jaribio la mauaji dhidi yangu, utaratibu pekee uliokuwa unawezekana ulikuwa ni kunihamisha nchini kwa dharura. 

"Nilikuwa nimeumizwa vibaya, mifupa imevunjwa kila mahali, nimepoteza damu nyingi na risasi zimejaa tumboni. Kusema nisubiri kibali cha Bunge au cha Muhimbili au cha Rais Magufuli ilikuwa ni kunitakia kifo cha wazi".

Aidha, Lissu amedai uamuzi wa yeye kupelekwa Nairobi nchini Kenya umetokana na makubaliano ya kikao kilichofanyika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma ambapo Spika Ndugai na Naibu wake walikuwepo kwenye kikao hicho pamoja na viongozi wengine wa nchi akiwemo Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu na Katibu Mkuu wake Dkt. Ulisubisya Mpoki na Mwenyekiti Mbowe na wabunge kadhaa walihudhuria pia.

"Baada ya kukubaliana kwamba napelekwa Nairobi, ndege ililetwa Dodoma saa sita za usiku. Uwanja wa Ndege wa Dodoma hauruhusu ndege kuruka au kutua baada ya saa 12 jioni. Nani aliyeruhusu ndege iliyonichukua kutua na kuruka saa sita usiku kama hakukuwa na kibali cha Bunge?", amehoji Lissu.

Waziri Mwakyembe amlilia Msanii wa bendi ya Mzee King Kiki

$
0
0
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe amepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha aliyekuwa mwanamuziki wa dansi, Kalambay Bisongo aliyekua akifanya kazi kwenye bendi ya Wazeee Sugu ya Mzee King Kiki.

Bisongo alifariki April 18 ya mwaka huukatika Hospitali ya Mloganzila iliyopo maeneo ya Kibamba jijini Dra es Salaam. 

Msanii huyo amewahi kufanya kazi kwenye bendi tofauti tofauti ikiwemo Tanzania One, Achingo na baadae bendi ya King Kiki.

Soma taarifa hiyo ya Mhe. Mwakyembe hapa chini:

Magufuli kuzindua tawi la NMB, jengo la PSPF....Tazama Hapa Ratiba Nzima Ya Rais Magufuli

$
0
0
Rais John Magufuli kesho kutwa (Jumatatu) atazindua jengo la Mfuko wa Pensheni wa PSPF na tawi jipya la Benki ya NMB lililopo Mtaa wa Barabara ya Chimwaga mjini Dodoma.

Akizungumza leo  na waandishi wa habari, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge amesema Rais Magufuli atawasili kesho mjini hapa.

“Siku ya Jumanne Aprili 24, Rais atakuwa mgeni rasmi kulihutubia Bunge la Afrika Mashariki ambalo linafanyika Tanzania Bara hapa Dodoma,”amesema.

Amesema Alhamisi Rais atakuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zitakazofanyika katika uwanja wa Jamhuri.

“Siku ya Ijumaa Rais atazindua barabara ya Dodoma hadi Babati yenye urefu wa Kilometa 231.8 na sherehe ya uzinduzi wa barabara hii zitafanyika kwenye wilaya ya Kondoa eneo la Bicha,”amesema.

Amesema uzinduzi wa barabara hiyo ni kichocheo kikubwa cha shughuli za uzalishaji na uchumi wa ukanda wote wa Bahi, Chamwino, Chemba na Kondoa.

“Nisisitize kuwa barabara hii ni sehemu ya Barabara kuu ya kaskazini (Great North Road) inayoanzia Cape Town Afrika Kusini hadi Cairo Misri hivyo ina umuhimu wa kipekee kwetu wananchi wa Dodoma upande wa shughuli za uzalishaji viwanda na uchumi,”amesema.

Dk Mahenge amesema Jumapili Rais ataondoka kulekea mkoani Iringa kwa ajili ya Sherehe za Mei Mosi kitaifa mwaka huu ambazo zinafanyika kitaifa mkoani humo.

“Kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Dodoma namshukuru Rais Magufuli kwa heshima hii ya kipekee anayoendelea kutupatia sisi Mkoa wa Dodoma ambayo ni Makao makuu ya nchi,”amesema.

Amewataka wakazi wa Dodoma na mikoa ya jirani kujitokeza kwa wingi kuhudhuria kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano na uzinduzi mwingine.

Zamaradi Mketemea Asimulia Alivyoumizwa na Kifo Cha Agness Masogange

$
0
0
Mtangazaji Maarufu wa Televisheni na redio, Zamaradi Mketemea amefunguka na kueleza alivyoguswa na msiba wa msanii Agnes Gerard Masogange aliyefariki dunia jana kwa matatizo ya pumu katika Kituo cha Huduma za Afya cha Mamama Ngoma kilichopo Mwenge jijini Dar es Salaam.

Zamaradi amesema alimfahamu Masogange zaidi ya maisha yake ya kwenye mitandao ya kijamii huku akiweka wazi kwamba kuna kipindi Zamaradi alikwenda Afrika Kusini na kupokelewa na Masogange ambaye aliishi kwake kwa zaidi ya wiki moja, hivyo alikuwa kama mwanafamilia.

Mtangazaji huyo amesema amesikitishwa sana na kifo cha ghafla cha Masogange na kusema wamependekeza aagwe Leaders Club ili watu wengi wapate fursa ya kumuaga na kwamba atasafirishwa kwenda kuzikwa kwao, Mbeya.

Aliyekuwa mpenzi wa Masogange, afunguka siri kubwa

$
0
0
Msanii wa filamu bongo Rammy Galis ambaye alishawahi kuwa kwenye mahusiano na Agnes Masogange aliyefariki hapo jana, ametoa siri ambayo wengi walikuwa hawaijui kuhusu maisha ya Agnes.

Kwenye ukurasa wake wa instagram Rammy Galis ameandika ujumbe akionesha kuhuzunishwa na kifo cha mrembo huyo ambaye alibarikiwa na Muumba kwa urembo wake, na kusema kwamba walipokuwa kwenye mahusiano aliwahi kucheza filamu yake ambayo kama ilitabiri kifo chake, kwa kuigiza kufa mwisho wa kisa hiko kilichopewa jina la 'hukumu'.

“Tulikesha usiku na mchana ili ucheze filamu yetu kwa hisia, ukasema hii iwe kumbukumbu yako kama niliwahii hata kwenye kazi zako kukusaidia, sasa kwanini filamu yetu tulitunga jina liitwe #hukumu? ilikuwaje story ya filamu mwisho unafariki? kwani tulikua tunatungia iwe kweli hukumu yako? Mungu ndio hakimu wa viumbe vyote katika dunia , umeondoka ghafla sanaa , na hii pia ni funzo umeniachia”, ameandika Rammy Galis akiambatanisha picha ya wawili hao pamoja.

Kutokana na kauli hii ya Rammy Galis, tunaweza sema Masogange naye amepitia kifo ambacho muigizaji nguli wa filamu za bongo Steven Kanumba alifariki, kwa kuigiza kifo kwenye filamu yake ya mwisho, na kweli kabla ya filamu kutoka alipatwa na mauti.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Naibu Waziri: Jeshi la Polisi Halina Muda wa Kulinda Maandamano Yasiyo na Tija

$
0
0
BUNGE limeelezwa kuwa Jeshi la Polisi halina muda wa kulinda taasisi au chombo chochote kitakachotaka kufanya mikutano au maandamano yasiyo na tija.

Aidha, amesema hakuna idadi kubwa ya kutosha kwa askari polisi wa kulinda mikutano ya vyama vya siasa.  

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuf Masauni, alisema hayo jana alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mkoani (CUF), Twahir Awesu Mohamed. 

Katika swali lake, mbunge huyo alihoji ni kwa nini polisi waliwalinda wanachama wa CCM waliofanya maandamano makubwa hivi karibuni visiwani Zanzibar. 

“Kumekuwa na katazo la kufanya mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa lakini  Aprili 8, mwaka huu, CCM mikoa miwili ya Pemba waliandamana chini ya ulinzi mkali  wa Jeshi la Polisi wakiwa wamebeba mabango wakiimba nyimbo za kuhalalisha amani na uchochezi. Hili katazo linahusu vyama vya upinzani pekee au vyama vyote?” alihoji. 

Aidha katika swali la msingi, mbunge huyo alihoji ni lini jeshi la polisi litafanya kazi zake kisayansi zaidi na kuondokana na kutumia nguvu zisizo za lazima wakati wa kutekeleza majukumu yake

 “Suala la weledi kwa watendaji wa polisi linasimamiwa vipi ili polisi waweze kupambana na uhalifu unaokuwa kitaalam kila siku,”alihoji. 

Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri Masauni alisema suala la kuandamana kama yameruhusiwa lazima jeshi la polisi litoe ulinzi. 

“Kipindi hicho ambacho serikali ina shughuli nyingi za kiuchumi, jeshi la polisi haliwezi kuendekeza kutoa ulinzi katika maandamano au mikutano kwa kuwa hatuna askari wa kutosha wa kufanya shughuli hizo,”alisema. 

Alisema kwa taasisi au chombo chochote kitakachohitaji kufanya maandamano au mikutano jeshi la polisi halina muda huo. 

Alisisitiza kuwa sheria ni msumeno inakata kote kote hivyo ni vyema sheria zikafuatwa. 

Alifafanua kuwa katika kutekeleza kazi zake polisi anaruhusiwa kutumia nguvu inayoendana na mazingira ya tukio 

Aidha alisema serikali imekuwa ikiwajengea uwezo wa kiutendaji askari kwa kutoa mafunzo mbalimbali sehemu za kazi yenye lengo la kuwakumbusha taratibu za kazi. 

Alifafanua kuwa katika kuhakikisha linafanya kazi kwa weledi jeshi la polisi limekuwa likiajiri wasomi wenye taaluma mbalimbali kama vile teknolojia ya habari na mawasiliano (Tehama), maabara, uchunguzi wa nyaraka na taaluma zingine zinazohusisna na makosa yanayosababishwa na ukuaji wa teknolojia.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0753471612, 0623386305, 0655283534 -DR KUZENZA

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0766340868

Makonda sasa kuwapima wanaume saratani ya tezi dume nyumba kwa nyumba

$
0
0
Wakati chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wote wenye umri wa miaka 14 ikitarajiwa kuanza kutolewa Jumatatu wiki ijayo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema ana mikakati ya kupita nyumba kwa nyumba ili kuwapima wanaume saratani tezi ya dume.

Makonda ameyasema hayo leo Aprili 21 wakati akifungua rasmi warsha ya chanjo hiyo iliyowashirikisha waandishi wa habari, wataalamu wa afya, viongozi mbalimbali wa dini na siasa.

Amesema wakati saratani ya mlango wa kizazi ikiwaathiri wanawake nchini, tezi dume inaumiza zaidi akina baba ambao hata hivyo hakuna mwamko wa kulizungumzia jambo hilo katika jamii.

"Kuna kasumba kuwa saratani ya tezi dume inapimwa kwa kidole jamani siyo kweli, kuna kipimo cha damu na ni rahisi hivyo nina mkakati wa kupita nyumba kwa nyumba katika mkoa wangu kuhakikisha hii kasi ya vifo kwa kinababa inapungua kwa kuwagundua mapema na kuwaanzishia matibabu," amesema Makonda.

Pia, ametoa wito kwa viongozi wote wa serikali za mitaa na viongozi wa dini kuhakikisha wanatoa elimu kwa jamii ili wasichana wote wenye umri huo wafike kwenye vituo kwa wingi kupata chanjo.

Makonda amesisitiza pia kuzingatia kupata chanjo kamili kwa kurudi mara ya pili ili kuikamilisha.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images