Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli awahoji CAG, Katibu Mkuu kuhusu Sh1.5 trilioni Zinazodaiwa Kupotea

$
0
0
Rais Joh Magufuli amewanyanyua Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali(CAG),  Profesa Mussa Assad na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James kueleza kama kuna upotevu wa Sh 1.5 trilioni kama inavyodaiwa.

Rais Magufuli aliwataka watendaji hao waeleze hilo leo Ijumaa Aprili 20, Ikulu wakati akizungumza baada ya kumaliza kuwaapisha majaji wapya kumi aliowateua hivi karibuni.

“Kuna watu wanaposti posti vitu kwenye mitandao kwamba kuna upotevu wa shilingi trilioni 1.5 mimi nimefuatilia hilo sijaona upotevu huo. Niliposikia taarifa hizo nikampigia CAG mbona kwenye ripoti yako uliyoniletea hapa Ikulu hukuonyesha hilo eneo la upotevu hilo akaniambia hakuna... maana angeniambia tu siku ile ile hata kama ni waziri ningemtimua,” amesema.

Baada ya kueleza hivyo, Rais Magufuli alianza kuwahoji watendaji hao akitaka wathibitishe kama kweli upotevu huo umetokea.

“Bahati nzuri CAG yuko hapa... embu tuthibitishie kama fedha hizo kweli zimepotea,” amesema Rais Magufuli kabla CAG kusimama na kujibu; “mheshimiwa hapana... hakuna upotevu uliokuwepo.” Baada ya CAG kutoa majibu hayo Rais Magufuli akamhoji Katibu Mkuu Wizara Fedha na Mipango asimame kujibu swali hilo hilo.

“ Hakuna upotevu huo mheshimiwa Rais...Hazina tuko salama,” alisema Dotto. Rais Magufuli aliendelea kusisitiza kutokuwepo kwa opotevu huo huku akionyesha kusikitishwa namna watu wanavyotumia uhuru wa mitandao kutuma yale wanayoyapenda.

“Kwa vile hii mitandao hatukontro sisi basi watu wanapostiposti vitu wavitakavyo hata kama siyo vya kweli,” amesema.

Katibu Mkuu CHADEMA : Sharti la kuripoti kwa RPC ni gumu

$
0
0
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dr. Vincent Mashinji amesema sharti la kuripoti kituo Kikuu cha Polisi Central ni gumu kulingana na kazi wanazozifanya.

Dr. Mashinji ameyasema hayo leo April 20, 2018  baada ya yeye na Viongozi wenzake wa chama hicho kuripoti kituoni hapo ikiwa ni sehemu ya sharti la dhamana walilopewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Akizungumza na waandishi wa Habari, Dr. Mashinji amesema, “Iliamuriwa na mahakama kila siku ya Ijumaa turipoti kwa RPC hapa Central Polisi ikiwa kama sehemu ya sharti la dhamana tulilopewa mahakamani kwenye ile kesi yetu inayojumuisha watu 9”

“Kimsingi ukiangalia ni sharti gumu kwani nature ya kazi zetu inatutaka kusafiri kwenda kujenga chama, hivyo tunashindwa ila kwa vile ni amri ya mahakama lazima tutekeleze kwani ndio inatenda haki,” -Dr. Mashinji.

Pia Dr. Mashinji amesema kama mahakama itaridhia kuwaondolea sharti hilo itawasaidia sana.

Benki Ya Kilimo Tanzania Kufungua Ofisi Za Kikanda Kwa Awamu

$
0
0
Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma
Serikali imeeleza kuwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) inatekeleza Mpango wa Miaka Mitano (2017- 2021), wa kusogeza huduma karibu na wateja kwa kuanzisha ofisi za Kikanda katika Kanda ya Kaskazini, Kusini, Kati, Ziwa, Nyanda za Juu Kusini na Zanzibar kwa awamu.

Hayo yameelezwa Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), wakati akijibu maswali ya msingi ya Mbunge wa Viti Maalumu Mhe.  Jacqueline Msongozi (CCM), aliyetaka kujua lini Serikali itapeleka Benki ya Kilimo katika Mkoa wa Ruvuma ili wananchi waweze kukopeshwa.

Aidha, Mhe. Msongozi alitaka kufahamu utayari wa Serikali kupunguza riba ya mikopo wanayokopeshwa Wakulima katika Benki hiyo.

Akijibu maswali hayo, Dkt. Ashatu Kijaji alisema kuwa  hadi kufikia Juni 30, 2018  Ofisi ya Kanda ya Kati, Dodoma, itakuwa imefunguliwa ambayo pia itakuwa ni Makao Mkauu ya Benki hiyo.

 “Baada ya ufunguzi wa ofisi ya Kanda ya Kati kukamilika Benki Itafanya uchambuzi wa fursa zilizopo Kikanda na hivyo kuchukua hatua na taratibu za kufungua ofisi nyingine kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha”, alisema Dkt. Kijaji.

Alisema kuwa Benki hiyo inatoa mikopo kwa kutumia mfumo wa makundi, kundi la kwanza wakulima wadogo wadogo kwa riba ya asilimia 8- 12, kundi la pili la miradi mikubwa ya kilimo kwa asilimia 12 – 16 kwa mwaka na kundi la mwisho ni mikopo ya ushirika ambapo riba yake inaendana na hali ya soko la matumizi ya mkopo.

Kuhusu kupunguza riba kwa wakopaji, Dkt. Kijaji alibainisha kuwa majadiliano ya kiwango cha riba yanaweza kufanyika kulingana na historia ya mkopaji.

Waziri Mkuu Kuzindua Mradi Wa Kuongeza Uwezo Wa Kuhifadhi Nafaka Tanzania Jumamosi 21 Aprili 2018

$
0
0
Na Mathias Canal, NFRA-Dodoma
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) Tarehe 21 Apili 2018 atakuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa kuongeza uwezo wa uhifadhi wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) katika dhifa itakayofanyika kwenye viwanja vya Ofisi za Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula zilizopo Mtaa wa Kizota eneo la Viwanda Mjini Dodoma.

Mradi huo utagharimu Dola za Kimarekani Milioni 55, ambao ni mkopo wa masharti nafuu kutoka Serikali ya Poland ikiwa ni sehemu ya kiasi cha Dola milioni 110 kilichotolewa kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, mikataba ya ujenzi ilianza kutekelewa tarehe 9 Disemba 2017 ambapo Mradi huo utatekelezwa na kampuni mbili za Kandarasi kutoka Poland ambazo ni (Feerum S.A na Unia Araj Realizacje Sp.o.o) huku msimamizi wa mradi ni Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa waandashi wa habari na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Bi Vumilia L. Zikankuba ameeleza kuwa Mradi huo utahusisha ujenzi wa vihenge vya kisasa, maghala ya kisasa, ujenzi wa ofisi na kutekelezwa katika maeneo nane ambayo ni (Babati)-Manyara, Dodoma, Makambako-Njombe, Mbozi-Songwe, Shinyanga, Songea-Ruvuma, Sumbawanga-Rukwa na Mpanda-Katavi. 

Baada ya mradi kukamilika Wakala utakuwa umeongeza uwezo wa kuhifahi kwa 250,000 MT zaidi (vihenge vya kisasa 190,000MT na maghala 60,000 MT) jambo ambalo litakuwa chachu na mafanikio yenye tija katika kuunga mkono Juhudi za utendaji wa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli.

Kupatikana kwa Mradi huo nchini ni jitihada za Serikali ambazo zitapelekea ukuaji wa uchumi nchini na kuchangia kuwezesha Tanzania ya viwanda ambapo kutawezesha maghala ya Wakala kuweza kuhifadhi akiba ya Chakula ambayo itaendana na mahitaji halisi ya dharura kulinganisha na ongezeko la watu nchini.

Hifadhi ya Chakula inayohitajika kukidhi mahitaji ya dharula kwa miezi mitatu ni zaidi ya tani 500,000 ukilinganisha na tani 150,000 iliyokuwa inahitajika miaka ya 2008 Wakala ulipoanzishwa.

Aidha, Zikankuba alisema kuwa technolojia itakayotumika katika ujenzi wa vihenge vya kisasa, itawezesha Wakala kupunguza gharama za uendeshaji; kuhifadhi chakula kwa muda mrefu zaidi; kupunguza upotevu wa zao la mahindi baada ya kuvuna (posthaverst loss), kuongeza soko la mahindi nchini na kuimarisha usalama wa nafaka inayohifadhiwa kwa kudhibiti sumukuvu (Aflatoxin) kwa mahindi yaliyohifadhiwa. Jitihada hizi zinalenga katika kuimarisha uwezo wa Taifa katika kuimarisha usalama wa chakula nchini.

Serikali Imewataka Wadau Wa Uwekezaji Kuacha Kulalamika Na Badala Yake Watoe Ushauri

$
0
0
NA Mahmoud Ahmad, DODOMA
SERIKALI imewataka wawekezaji na wadau mbalimbali kuachana na tabia ya kulalamika serikali na badala yake watoe ushauri kwa serikali ni jinsi gani ya kutatua changamoto mbalimbali.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Biashara Viwanda na Uwekezaji, Charles Mwijage.

Mijage alitoa kauli hiyo jana wakati  alipokuwa akifungua mkutano wa wadau na wawekezaji wa pamba,bidhaa za nguo na mavazi katika ukumbi wa mikutano wa Hazina mjini hapa.

Alisema pamoja na kuwepo kwa changamoto mbalimbali zinazokabiliana na wizara hiyo lakini ni wakati wa wadau kutoa maoni yao ya kuishauri serikali pamoja na kuisaidia ili iweze kufanikiwa badala ya kuendelea kulalamika.

Hata hivyo alisema kwa kuzingatia kuwepo kwa sera ya serikali ya viwanda ni wakati sasa wa waekezaji kujenga viwanda ambavyo vitaweza kuzalisha malighafi ambazo zinazalishwa nchii badala ya kuuza malghafi hizo nje na kununua bidhaa zinazozalishwa nje ya nchi.

Akizungumzia zao la pamba alisema kwa kuwa wananchi na wakulima wamehamasishwa zaidi kulima pamba katika maeneo ya ukanda wa pamba ni lazima pamba inayozalishwa nchini isiuzwe nje ya nchi na badala yake ichakatwe na kuzalisha nguo na nyuzi ambazo zinaweza kutumiwa na kuzalisha bidhaa bora.

Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro,Siriel Mchembe,  ameitaka serikali kuhakikisha inaweka mikakati ambayo inaeleweka kwa lengo la kujua soko la pamba pamoja na bei ambayo itakuwa inamanufaa kwa wakulima.

Akichangia katika mkutano huo mkuu huyo wa wilaya ambaye alikuwa amemwakilisha mkoa wa Morogoro, alisema kwa sasa wananchi wamehamasishwa zaidi kulima zao la pamba na kufikia hatua ya kuachana na kilimo cha mahindi hivyo wanatakiwa kuhakikishiwa kama pamba yao itakuwa na soko la uhakika.

“Kwa sasa wakulima wamehamasishwa sana kulima pamba imefikia hatua wapo wakulima ambao wameachana na kulima mahindi wakijua kuwa pamba itakuwa na bei nzuri, sasa ikitokea pamba ikaa haina soko au kuonekna ni chafu je wakulima hao tutawaambia nini” alihoji mkuu huyo wa wilaya.

Naye mkuu wa mkoa wa Mara Adam Kigoma Malima alisema haiweze, Mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya pamoja na wetendaji wengine wakaishi kwa kulalamika badala ya kutafuta suluhusho.

Alisema suala la uwepo wa viwanda unatakiwa kuwa na mikakati ya pamoja nadala ya kuishi kwa malalamiko na kukosa ufumbuzi na maazimio ya pamoja na kwa hali hiyo haiwezekani pakawepo na maendeleo.

Serikali Yatolea Ufafanuzi Ulipaji Wa Pensheni Wastaafu Wa Shirika La Posta Na Simu

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma
Serikali imeeleza kuwa haiwezi kuhamisha jukumu la kulipa pensheni ya Wastaafu wa Shirika la Posta na Simu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwenda kwenye mojawapo ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa kuwa zoezi la kuunganisha Mifuko ya Pensheni halijakamilika.

 Hayo yamesemwa Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Ludewa Mhe.  Deo Ngalawa (CCM), aliyetaka kufahamu, lini Serikali itakuwa tayari kuhamisha jukumu la kuwalipa Wastaafu wa  lililokuwa Shirika la Posta na Simu la Afrika Mashariki kwenye moja wapo ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji alisema kuwa Serikali kupitia Shirika la Posta  inaendelea na jukumu la kuwalipa pensheni ya kila mwezi Wastaafu wa shirika hilo.

“Uamuzi wa kuhamisha au kuendelea na utaratibu wa sasa utatolewa baada ya zoezi la kuunganisha mifuko ya pensheni kukamilika”, alisema Dkt. Kijaji.

Katika maswali ya nyongeza Mhe. Ngalawa alihoji kwakuwa Shirika la Posta limekuwa likisuasua katika kujiendesha na miongoni mwa mambo yanayosababisha ni ulipaji wa pensheni za Wastaafu hao, Serikali haioni ni wakati wa kulitua mzigo Shirika hilo na kuchukua jukumu hilo.

Mhe. Ngalawa alieleza kuwa  kuanzia mwaka 2015  malipo ya pensheni kwa Wastaafu yalipanda kutoka Sh. 50,000 hadi Sh. 100,000 lakini kuna baadhi ya Wastaafu hawajabadilishiwa pensheni zao. Alitaka kujua lini Serikali itabadilisha pensheni hizo ili ziwe sawa kwa wote.

Dkt. Kijaji alisema kuwa  baada ya Shirika la Posta  kulipa Wastaafu huwasilisha madai yake Hazina na Serikali imekuwa ikirejesha fedha  hizo kwa wakati na hakuna madai ya ziada.

Alifafanua kuwa Serikali kupitia Mifuko yote ya Hifadhi ya Jamii imekuwa ikilipa ongezeko la pensheni kwa Wastaafu kwa wakati, na kukiri kuwa Wastaafu wachache wamekuwa wakipeleka kesi za kutoongezewa pensheni zao kutokana na sababu mbalimbali.

Dkt. Kijaji alisema kuwa Hazina imekuwa ikipokea malalamiko hayo na kuyashughulikia, ametoa wito kwa Wastaafu wote yenye malalamiko wafike Hazina ili waweze kusaidiwa.

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume

$
0
0
Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni Sado 3 Mix Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

Sado 4 Mix; Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI DR. ULIMWENGU BINGWA Anapatikana dar magomeni moroco hotel
SIMU NO; 0759 030343 / 0622790494

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Okoa Ndoa Yako Sasa : Je Umepungukiwa Na Nguvu Za Kiume Au maumbile Au Mpenzi Wako Hakutimizii Utakacho?

$
0
0
Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sabubu ya kutokuwa na nguvu za kiume au uume wako mdogo dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA;
 1 KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA YA MWENZI WAKO
2 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA 
3 UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE 
4 KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

MAKAKANUA; HII NI dawa ya maumbili madogo...hufusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba, dawa za uzaz,Mi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo 

FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU. KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA. piga simu 0743362017. 0789234653 DR AGU

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0766340868

DPP alifunga jalada la kesi ya mauaji ya Akwilina

$
0
0
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Biswalo Mganga amesema, jalada la kesi ya aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini amelifunga rasmi.

Hayo ameyasema leo Aprili 20, 2018; Ikulu jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari huku akionya watu wanaovunjua amani kutofumbiwa macho wakiwamo waandishi wa habari.

Amesema jeshi la polisi linapotumia nguvu kuzuia maandamano, haliwezi kushtakiwa au hata kukitokea vurugu na kusababisha mauaji huwezi kulishtaki jeshi.

”Katika maandamano yale ya watu zaidi ya 200, huwezi kubaini nani amehusika na kumpiga risasi Akwilina na mwili wake haukutolewa risasi yoyote.”

Alipoulizwa kuhusu askari waliokamatwa baada ya kutokea kwa tukio hilo, Biswalo amesema, “kama jalada nimelifunga, kwa hiyo askari wale nao wameachiwa huru hawana hatia.”

Mkurugenzi huyo amesema moja ya jukumu lake ni kuhakikisha amani inakuwapo,”na niseme tu kuwa, mimi sina chama cha siasa, si mwanasiasa, kwa hiyo sitamvumilia mtu awe mkubwa wala mdogo, nitamshughulikia.”

“Na wanaosema wataandamana, waambieni wasifanye hivyo kwani wakiandamana watakwenda kuwasilimulia familia yake,” amesisitiza Biswalo

Pia, amevionya vyombo vya habari ambavyo vinavyoweza kuchangia uvunjifu wa amani, hatua zitachukuliwa hivyo kuvitaka kuwa makini na kutimiza wajibu wao kwa kufuata misingi ya taaluma yao.

Polisi waua majambazi wanne Pwani

$
0
0
Majambazi wanne wameuawa  na polisi asubuhi ya leo Ijumaa Aprili 20, wakati wakijaribu kupora Kisarawe mkoani Pwani.

Kabla ya kuuawa yalitokea majibizano ya risasi kati yao na askari Polisi.

Imedaiwa majambazi hao wametokea jijini Dar es Salaam na walikuwa wanatumia gari lenye namba za kibalozi hatua iliyosababisha askari wa usalama barabarani kutowahisi chochote kwani gari hizo sio rahisi kusimamishwa ovyo.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, ambaye pia ni Mwenyekiti Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani Pwani, Evarist Ndikilo amethibitisha tukio hilo.

SAD NEWS: Agness Masogange Afariki Dunia

$
0
0

Mwanamitindo na video queen marufu bongo Agnes Gerald maarufu kama Masogange, amefariki dunia jioni ya leo April 20 alipokuwa amelazwa katika hospital ya Mama Ngoma akipatiwa matibabu

Akithibitisha taarifa ya kifo hicho Daktari Rama Ngoma wa hospitali ya Mama Ngoma, amesema Agnes amefariki dunia kwa tatizo la pneumonia na upungufu wa damu jioni hii, na alikuwa amelazwa hospitalini hapo kwa muda wa siku nne mpaka kifo kilipomkuta.

Tayari mwili wake umeshatolewa hospitali ya Mama Ngoma, na kwa mujibu wa muigizaji Steve Nyerere umepelekwa hospitali ya Taifa ya muhimbili.

Agnes Masogange alikuwa maarufu baada ya kuonekana kwenye video kadhaa za bongo ikiwemo Masogange ya Belle 9.


Hivi karibuni, Masogange alihukumiwa kulipa faini ya Sh 1.5 milioni  na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya kukutwa na hatia ya kutumia dawa za kulevya aina ya heroin.

Alibainika kutumia dawa hizo kati ya Februari 7 na 14, 2017.

Mwili wa marehemu Agness Masogange ulivyowasili Muhimbili

$
0
0
Mwili wa aliyekuwa Video Vixen Agnes Gerald (Masogange) ulishatolewa katika Hospitali ya Mama Ngoma na kupelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kuhifadhiwa kabla ya kutangazwa kwa ratiba za mazishi.

Uteuzi alioufanya Rais Magufuli muda huu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Msalika Robert Makungu kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora.

Bw. Makungu anachukua nafasi ya Dkt. Thea Ntara ambaye amestaafu.

Uteuzi wa Bw. Makungu unaanzia tarehe 20 Aprili, 2018 na tarehe ya kuapishwa kwake itapangwa baadaye.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
20 Aprili, 2018

Diamond, Wema Sepetu, Steve Nyerere wamlilia AGNESS MASOGANGE

$
0
0
Leo April 20,2018 simanzi kubwa imetawala kwenye tasnia ya muziki wa Bongo Fleva kupoteza video vixen maarufu Agnes Gerald “Masogange” na kwa upande wa mastaa ambao wameonyesha kuguswa na msiba huu ni pamoja na wanamuziki na waigizaji akiwemo Wema Sepetu, Diamond Platnumz,  Steve Nyerere, na wengine.

Aslay Isihaka ameweka picha ya Masongange na kuandika, “Dah mbele yako nyuma yetu sister, safari yetu moja innalillah wainnailah raajiun,”

Huku Naseeb Abdul maarufu ‘Diamond Platnum’ akiweka picha ya mishumaa na maneno, “Rest in paradise Agnes.”

Rajab Kahali ‘Harmonize’ ameweka picha ya Masongange na kusema, “God’s plan  R.I.P. Aggy.

Naye Steven Mengere 'Steve Nyerere’ ameweka picha tatu tofauti za Masogange na kuzungumzia kifo hicho akianza kwa kusema;

“Nimepokea taarifa ya kifo chako kwa mshtuko mkubwa sana. Masogange amka mama Masogange. Staki kuamini.”

Mcheza filamu, Wema Sepetu ameweka picha ya Masongange ikiambatana na maneno, “Innah lillah wa innah illah rajiun... Dah...!


Walichokiamua wasanii Bongo Movie Usiku Huu Kuhusu Mazishi ya Agness Masogange

$
0
0
Wasanii mbalimbali wa filamu na wa bongo fleva, wamekutana katika viwanja vya Leaders Club usiku huu  ili kujadiliana kuhusu utaratibu wa mazishi ya msanii anayepamba video za muziki (video queen), Agness Gerald maarufu Masogange.

Steve Nyerere amesema kuwa, Masogange anatarajiwa kuzikwa Mbeya na kuwa mwili utasafirishwa Jumapili wiki hii na kuzikwa Jumatatu.

Miongoni mwa wasanii waliofika Leaders leo ni pamoja na Chopa wa Mchopanga, Irene Uwoya aliyeambatana na mume wake, Dogo Janja na aliyekuwa mtangazaji wa Clouds Media Group, Zamaradi Mketema.

Kamati ya awali iliyoundwa, imemchangua Mchopanga kuwa katibu na Zamaradi kukusanya michango.

“Lakini tukipata taarifa kutoka kwa ndugu tutajua msiba utagharimu shilingi ngapi kwa sasa mahitaji makubwa ni mabasi mawili kwa ajili ya kusafirisha mwili, maturubai, vyakula na maji,” amesema Nyerere.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya April 21

Benki ya Dunia yakubali kushirikiana na Serikali kutafuta ufumbuzi wa mafuriko Dar es Salaam

$
0
0
Benki ya Dunia (WB) imekubali kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kukabiliana na athari za mafuriko zinazosababishwa na mvua kubwa zinazonyesha kila mwaka katika Jiji la Dar es Salaam na kuleta madhara makubwa hususan katika eneo la Jangwani jijini humo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) wakati akizungumza na ujumbe wa Benki ya Dunia ulioongozwa na Mkurugenzi wa Benki hiyo kwa nchi za Tanzania, Somalia, Burundi na Malawi Bi. Bella Bird, katika mikutano ya kipupwe inayoendelea mjini Washington DC.

Dkt. Mpango amesema kuwa Benki ya Dunia imekubali kusaidia kukabiliana na mafuriko katika bonde la mto Msimbazi hasa katika eneo la  kutoka Magomeni Mapipa kwenda Faya  na tayari Benki hiyo imeanza  zoezi la kutafiti eneo la Jangwani ili kuweza kuangalia namna nzuri ya kugharamia uboreshaji wa  mifereji katika bonde la mto Msimbazi ili kumaliza kero hiyo kwa wananchi wa Dar es Salaam.

“Tumewaeleza Benki ya Dunia  changamoto hii ambayo imekuwa inajirudia kila mara na kusababisha upotevu wa maisha ya watu, kusababisha kufungwa kwa barabara, watu kushindwa kwenda kazini na wanafunzi kushindwa kwenda shule, hivyo wameonesha nia ya kumaliza kero hii kwa wananchi,” alisema Dkt. Mpango.

Amesema kuwa baada ya timu ya Benki ya Dunia kumaliza kufanya kazi yao kwa kushirikiana na Manispaa ya jiji la Dar es Salaam, Serikali inaamini njia ya kudumu itapatikana na kuondokana na tatizo hilo la mafuriko ya mara kwa mara katika eneo la Jangwani.

Siku ya Malaria Kitaifa kufanyika wilayani Kasulu, Kigoma

$
0
0
Tanzania inatarajia kuungana na nchi zingine duniani kwenye kuadhimisha siku ya Malaria Duniani ambayo ufanyika April 25 kila mwaka.

Maadhimisho hayo ya kitaifa yatafanyika wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma huku Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii akitarajiwa kuzindua ripoti ya hali ya Malaria nchini.

Akiongea jijini Dar es Salaam, Waziri Nyoni ambaye ni Mkurugenzi wa Miradi kutoka VectorWorks alisema kutakuwa na shamra shamra mbali mbali kuanzia tarehe 22 April kabla ya kufikia kilele cha maadhimisho hayo.

VectorWorks ni mradi wa miaka mitano wa kupamba na malaria hapa nchini umefadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani (USAID) kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti malaria na kuratibiwa na John Hopkins Center for Communications.

“Sisi kazi yetu ni kuhakikisha hali ya ugonjwa wa malaria inapungua. Kwa sababu hiyo, tumekuwa na zoezi endelevu la kugawa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu kwa kila kaya hapa nchini. Vile vile, tunatumia vituo vya afya kuwafikia walengwa wakuu ambao ni akinamama waoenda kliniki na watoto wenye umri chini ya mwaka mmoja,” alisema Nyoni.

Akina mama wanaonza kliniki ni lazima wapatiwe chandarua chenye dawa ya muda mrefu bure. Hii njia bora ya kujikinga na mbu waenezao malaria. Vile vile tunafanya kazi kwa kushirikiani na Serikali kupitia Wizara ya Afya kitengo cha kupamba na Malaria nchini ambao wamekuwa wakipuliza dawa yenye viatilifu kwenye maeneo yenye masalia ya mbu.

 “Tumepiga hatua kubwa kupunguza malaria hapa Tanzania kwa hivyo natoa wito wangu kwa kila Mtanzania kuhakikisha analala kwenye chandarua kwenye dawa ya muda mrefu,” aliongeza Nyoni.

Wanaume Waliokaidi Wito Wa Rc Makonda Kukamatwa Jumatatu

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amesema wanaume wote waliokaidi wito wa kufika ofsini kwake baada ya kupigiwa simu na kutumiwa barua za wito watakamatwa na Jeshi la Polisi kuanzia siku ya jumatatu ya April 23.
 
RC Makonda amesema ifikapo siku ya Jumapili majina ya wanaume waliokaidi wito yatafikishwa kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Lazaro Benedict Mambosasa kwaajili ya utekelezaji.
 
Aidha RC Makonda ameongeza siku nyingine tano kwaajili ya kusikiliza kesi zilizowasilishwa ofisini kwake na kufanya idadi ya kufikia siku 15.
 
Pamoja na hayo RC Makonda amesema ataunda kamati ya wanasheria na maafisa ustawi wa jamii kutoka serikalini na taasisi binafsi kwaajili ya kufanya uchambuzi wa ukubwa wa tatizo na mapendekezo ya kisheria kisha kuwasilishwa wizara husika kisha kuwasilishwa Bungeni.
 
Hata hivyo RC Makonda amesema ifikapo April 25 na 26 atatoa ripoti ya mwelekeo dhidi ya mateso waliyokuwa wakipata kinamama na watoto waliotelwkezwa. 
 
RC Makonda amesema Zoezi la kusikiliza kinamama waliotelekezwa limekuwa na mafanikio makubwa ambapo zaidi ya wananchi 17,000 walifika ofsini kwake ambapo hadi sasa kinamama 7,000 wamesikilizwa na wanaume 1,200 wamekubali kwa maandishi kutunza watoto wao na wengine wamepimwa DNA.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images