Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Polisi: Diamond Amehojiwa na Kupewa Dhamana

$
0
0
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema msanii Naseeb Abdul maarufu Diamond Platinumz jana Jumatatu Aprili 16 alishikiliwa na polisi kwa ajili ya mahojiano kufuatia kusambaza picha zisizo na maadili.

Mambosasa amesema  kuwa Diamond alihojiwa na kupewa dhamana jana Jumatatu huku uchunguzi zaidi ukiwa unaendelea na utakapokamilika ataitwa tena polisi.

“Alihojiwa jana na akapewa dhamana, upelelezi unaendelea,” amesema Mambosasa.

Leo katika kipindi cha maswali na majibu bungeni, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amesema polisi inamshikilia msanii huyo na Nandy ambao kwa nyakati tofauti wanadaiwa kusambaza picha sisizo na maadili kwenye mtandao.

Wasanii hao wanadaiwa kusambaza picha hizo kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram.

HESLB Kuanza Kupokea Maombi Ya Mikopo Mwezi Ujao .........Yawakumbusha waombaji kuandaa nyaraka muhimu

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuwataarifu wananchi kuwa inatarajia kuanza kupokea maombi ya mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2018/2019 kuanzia wiki ya kwanza ya mwezi ujao (Mei, 2018) baada ya kukamilishwa kwa maboresho makubwa ya mfumo wa uombaji kwa njia ya mtandao.

Maboresho ya mfumo wa maombi
Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru (pichani) amesema katika taarifa yake leo (Jumanne, Aprili 17, 2018) kuwa maombi yote yatapokelewa kwa njia ya mtandao (www.olas.heslb.go.tz) ambao umefanyiwa maboresho na Kituo cha Kompyuta cha Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UCC-UDSM).

Aidha, Bw. Badru amesema dirisha hilo la litafunguliwa sambamba na kutangazwa kwa mwongozo wa kina utakaotoa utaratibu wa kuwasilisha maombi, tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi, sifa na vigezo vitakavyotumika katika kuchambua na kutoa mikopo kwa mwaka ujao wa masomo unaotarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2018.

“Tunawasihi wale wote wanaotarajia kuomba mkopo wa elimu ya juu kusoma kwa makini mwongozo tutakaoutoa kwa vyombo vya habari na tovuti mwanzoni mwa mwezi Mei, 2018 na kuuzingatia,” amesema Bw. Badru.

Bw. Badru amefafanua kuwa wito wa Bodi ya Mikopo umetolewa kutokana na uzoefu wa miaka iliyopita ambapo waombaji wa mikopo waliwasilisha maombi yao bila kuzingatia mwongozo uliotolewa na kusababisha baadhi ya wanafunzi kukosa mikopo.

“Mwaka jana, kwa mfano, zaidi ya waombaji 10,027 kati ya waombaji zaidi ya 61,000 hawakuambatisha nyaraka muhimu kama vyeti vya kuzaliwa au hata vile vya vifo vilivyothibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kama tulivyoelekeza,” amesema.

Nyaraka muhimu zinazohitajika
Nyaraka nyingine muhimu ambazo waombaji mikopo wanapaswa kuziandaa ni pamoja na nakala za vyeti vya kitaaluma za kidato cha nne, sita na stashahada ambazo zimethibitishwa na Kamishna wa Viapo yaani Wakili au Hakimu.

Aidha, wanafunzi waombaji wenye ulemavu au wenye wazazi wenye ulemavu wanapaswa kuwa na barua zinazothibitisha ulemavu huo kutoka kwa Mganga Mkuu wa Mkoa, Wilaya au Kituo cha Afya cha Serikali;

Bw. Badru ameongeza kuwa wanafunzi ambao walifadhiliwa katika masomo yao ya Sekondari au Stashahada (Diploma) wawe na barua za uthibitisho wa udhamini huo kutoka katika taasisi zilizogharamia masomo yao.

Maafisa wa HESLB kutoa elimu mikoani.
Katika hatua nyingine, Bw. Badru amesema mwaka huu maafisa wa Bodi ya Mikopo watatembelea mikoa mbalimbali ili kukutana na waombaji mikopo kwa lengo la kuwaelimisha waombaji mikopo kuhusu taratibu sahihi za kuwasilisha maombi yao ya mikopo kwa njia ya mtandao. Ratiba na maeneo itakapofanyia mikutano hiyo itatangazwa mwanzoni mwa mwezi Mei, 2018.

HESLB ilianza kazi rasmi mwaka 2005 ili, pamoja na majukumu mengine, kutoa mikopo ya elimu ya juu kwa watanzania wahitaji na wenye sifa na kukusanya mikopo iliyoiva ambayo ilitolewa na Serikali tangu mwaka 1994/1995.

Imetolewa na:
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
DAR ES SALAAM
Kwa ufafanuzi: +255 (0) 757 500800.

Mahakama Kutoa Maamuzi Kesi ya Mbowe na Wenzake May 15

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, inatarajia May 15,2018 kutoa uamuzi wa kesi ya kufanya maandamano na mkusanyiko usio halali inayowakabili viongozi 9 wa CHADEMA akiwemo Freeman Mbowe kama iende Mahakama Kuu ama laa.

Hatua hiyo inatokana na mvutano wa hoja za kisheria zilizotolewa jana na Wakili wa utetezi, Peter Kibatala kisha kujibiwa leo na Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri.

Katika majibu yake Wakili Nchimbi ameiomba mahakama hiyo kutupilia mbali hoja za utetezi zilizotolewa na Kibatala kwa sababu zitapelekea ucheleweshaji wa shauri hilo pasipokuwa na sababu za msingi.

Nchimbi amedai kuwa katika mazingira ya mwenendo wa kesi hiyo toka ilipoanza hadi leo hakuna swali lolote la msingi lililoibuliwa na upande wa utetezi ambalo linajikita na uvunjifu ama ukiukwaji wa haki ya kikatiba.

“Nasema hivyo kwa sababu ukiangalia msingi wa hoja zilizowasilishwa na upande wa utetezi jana zimejikita katika mashtaka yanayowakabili washtakiwa” -Nchimbi

Alibainisha kuwa ukiangalia mlolongo wa hati ya mashtaka ni hati ambayo washtakiwa wamesomewa mashtaka zaidi ya mara moja ama mbili ikiwamo jana na washtakiwa waliyasikia mashtaka, wakayaelewa ndiyo maana wakaenda mbele wakayakanusha.

“Kama kweli washtakiwa waliona mashtaka haya siyo halali, hati ya mashtaka ilitolewa mapema hoja zilizowasilishwa na upande wa utetezi zingewasilishwa kabla washtakiwa hao hawaja enterpre,” -Nchimbi.

Nchimbi amedai kuwa washtakiwa wamefunguliwa kesi ya jinai wakati walikuwa katika mkutano halali wa kampeni ya uchaguzi mdogo na kwamba kuwafungulia mashtaka hayo ni uvunjifu wa haki ya kikatiba, alisisitiza kuwa ni rai ya upande wa mashtaka kwamba yote yaliyoongelewa na upande wa utetezi hayawezi kuitwa ni maswali ya kikatiba ambayo yangeilazimu mahakama kupeleka kesi hiyo Mahakama Kuu.

“Hakuna suala la kikatiba hapa na ukiendelea kufuatilia hoja za utetezi hawajashambulia vifungu vya kisheria vilivyotumika kuwashtaki washtakiwa hao, hivyo hoja zao hazina mashiko.” -Nchimbi

Baada ya kutolewa kwa hoja hizo,Wakili Kibatala aliiaambia mahakama kuwa mchakato wa kijinai ni mchakato mtakatifu ambao haukukusudiwa kuwashtaki watu ambao wanatekeleza majukumu yao kikatiba.

Kibatala alisisitiza kuiambia mahakama kuwa wanataka kwenda Mahakama Kuu ili kupata tafsiri ya je ni kweli mtu akiwa anatekeleza majukumu yake ya kikatiba ashtakiwe kijinai.

Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi May 15,2018 kwa ajili ya kutoa uamuzi kama kesi hiyo iende Mahakama Kuu ama lah.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu bara na Mbunge wa kibamba John Mnyika.

Mbunge wa Tarime mjini Esterher Matiko, Katibu wa chama hicho Dk  Vicenti  Mashinji, Mbunge wa Kawe Halima Mdee, mbunge wa Tarime vijijini, John Heche na mbunge wa bunda, Ester Bulaya.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na jumla ya mashtaka 12 katika kesi ya jinai namba 112 ya mwaka 2018 ikiwamo kula njama, kufanya mkusanyiko usio halali kinyume cha sheria na kuendelea kufanya mkusanyiko usio halali ama maandamano yaliyosababisha kifo cha Akwilina.

Nape Nnauye Ahoji Kuhusu Soko la Mbaazi Bungeni.......Serikali Yajibu Soko ni Baya, Watanzania Waitumie Kula Maana ni Chakula Kizuri

$
0
0
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye ameuliza serikali imefikia wapi kutafuta soko la Mbaazi baada ya msimu uliopita matatizo ya soko kushusha bei kutoka Tshs 2,000 mpaka 150. Amesema serikali iliahidi Bungeni kuwa itahakikisha inahangaika kupata soko la kuaminika la zao hilo.

Nape amesema sasa ni msimu wa kilimo hicho, kama bado hali haieleweki wananchi washauriwe waachane na mbaazi na badala yake wajikite kwenye mazao mengine ambayo yana soko la uhakika.

Akijibu swali hilo naibu waziri wa kilimo, Eng. Stella Manyanya amemjibu kuwa ni kweli hakukuwa na hali inayoridhisha kwenye soko la mbaazi na ni kutokana na wadau waliokuwa wanategemewa sana ilikuwa ni India.

Eng. Stella amesema mbaazi ni chakula kizuri chenye protini na watanzania wanaweza kula badala ya kuwategemea watu wa maeneo mengine. 

Amesema biashara ni ushindani na kila watu wanahakikisha wanakidhi soko lao la ndani, upande wa Tanzania wanaendelea kutafuta soko lakini wakati huo huo wanaendelea kusisitiza watu wapende kutumia mbaazi.

Amesema Dodoma Mbaazi inauzwa mpaka 1,800 kwa kilo na soko la Dar es Salaam kwenye supermarket inauzwa mpaka 2,400 hivyo tusitegemee soko mpaka kutoka nje kwani hata ndani ya nchi bado kuna watu wanaweza kula mbaazi yeye akiwa mmojawapo pia inategemewa hata mashule yanaweza kutumia wakati masoko yanaendelea kutafutwa.

Makamu Wa Rais Akutana Na Prince William Jijini London

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kufanya mazungumzo na Prince William katika jumba la Kifalme la Buckingham Palace.

Makamu wa Rais alimweleza Prince William kuwa Tanzania inatambua mchango wake katika kuzuia ujangili wa wanyama pori na Serikali ya Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbali mbali ya kupambana na kuzuia ujangili ingawa bado hatujawa na tekinolojia yenye uwezo wa wa kutambua na kuona wanyama wote lakini tumeendelea kuimarisha ulinzi wa wanyama pori.

Kwa upande wake Prince Williams alimuahidi Makamu wa Rais kusaidia katika kuboresha ulinzi wa wanyama pori kwa kutumia teknolojia ya hali ya juu na pia Prince William amemualika Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano unaohusu masuala ya Wanyapori unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu jijini London.

Makamu wa Rais Mhe. Samia yupo nchini Uingereza kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa nchi za jumuiya ya Madola.

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume

$
0
0
Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni Sado 3 Mix Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

Sado 4 Mix; Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI DR. ULIMWENGU BINGWA Anapatikana dar magomeni moroco hotel
SIMU NO; 0759 030343 / 0622790494

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Waziri Mkuchika Ammwagia Sifa Zito Kabwe...."Wewe ni Kijana Msomi, Endelea Na Uzando Huohuo"

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amefunguka na kumpongeza Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe kwa kuendelea kumpigania diwani wa CCM Simon Kanguye ambaye amepotea kwa kutekwa toka mwaka jana.

Zitto Kabwe alihoji bungeni juu ya kupotea kwa Simon Kanguye ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri Kibondo ambaye anadaiwa kutekwa miezi 9 sasa na hafahamiki wapi yupo hivyo alihitaji vyombo vya usalama viweze kuweka wazi jambo hilo ili wajue kama ameshakufa ili waweke matanga au kama wao wanamshikilia.

Kufuatia taarifa hiyo serikali kupitia kwa Waziri Mkuchika ndipo ikaweka wazi kuwa jambo hilo lipo chini ya jeshi la polisi lakini alitumia nafasi hiyo kumpongeza Zitto Kabwe kwa kuweza kufuatilia jambo hilo ili hali diwani huyo ni mwanachana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

"Navyomuelewa Zitto Kabwe alivyo msomi, kijana anayeipenda nchi yake tena ana akili simuoni Zitto anahamasisha watu kuchukua sheria mkononi bali yale maneno aliyaweka tu kutuhimiza watu wa serikali jamanii eehh fanyieni kazi, na sisi tumelipokea.

" Ila suala la kupotea kwa diwani huyo lilisharipotiwa polisi na uchunguzi unaendelea na tena hapa nampongeza ndugu yangu Zitto Kabwe, huyu diwani anayemtetea tumtafute mpaka tumpate wala siyo wa chama chake cha ACT Wazalendo bali ni diwani wa CCM.

" Hii inaonyesha jinsi alivyomzalendo, anavyopenda haki itendeke kwa kila mtu... sasa uendelee hivyo hivyo mdogo wangu Zitto usiyumbe kwenye mengine endelea hivyo hivyo" alisisitiza Mkuchika

Viongozi wa CHADEMA wakamatwa na Polisi

$
0
0
Viongozi wawili wa Baraza la la Wazee Taifa la CHADEMA, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Morogoro usiku wa kuamkia leo Aprili 17, 2018 ambapo mpaka sasa haijafahamika kusudio la kukamatwa kwao.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje Chadema, John Mrema wakati alipokuwa anazungumza na mwandishi wa habari hizi na kuwataja viongozi hao waliokamatwa kuwa ni dereva Proaches Urassa na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Jimbo la Morogoro Kusini Mzee Daniel Banzi.

"Jambo la kusikitisha ni kuwa jana usiku Polisi walivamia walikokuwa wamelala Viongozi na kuwakamata baadhi yao ambao walikuwa kwenye ziara ya kukutana na wazee kwenye vikao vya ndani. 

"Hakuna maelezo ya maana yanayotolewa zaidi ya Polisi kusema ni ukaguzi wa kawaida, ila ukweli ni kwamba kila wanapoonekana viongozi wa CHADEMA Polisi wanawakamata", amesema Mrema.

Pamoja na hayo, Mrema ameendelea kwa kusema "mpaka sasa tumewatuma Mawakili wetu mkoani Morogoro ili waweze kujua viongozi hao walikamatwa kutokana na tatizo gani. Tunalaani kwa nguvu zote udhalilishaji huu unaofanywa dhidi ya viongozi na wanachama wetu".

Tiba ya Fangasi Sugu, Vidonda vya Tumbo, Kuondoa Chunusi na Nguvu za Kiume

$
0
0
MAKANGA 3 POWER: Hutibu nguvu za kiume dakika 10 na kupona  ndani ya siku 3. Huimarisha misuli ya uume iliyolegea, pia ipo dawa ya kurefusha uume mfupi nchi 4 handi nchi 7

Tuna tiba ya kudumu ya kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kuopata choo vizuri, busha( bila opareshen)

Pia tunatibu  kisukari, presha, muguu kuuma, fangasi sugu, vidonda vya tumbo, kupunguza unene, maziwa, kuondoa chunusi pete na cheni za bahati.

Onana na Dr. Shilindes shida zako zote zitakwisha.

Tupo Mbagala Rangi tatu:  0784460348  au 0659103360

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0766340868

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 87 na 88

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA                      
ILIPOISHIA  

Delifina alizungumza huku akisimama, nikatazama kwa mbali nikaona uwanja  wenye nyasi nzuri na kwa mbele kuna majengo yanayo waka taa.
“Hapa ndio ikulu?”  
“Ndio”
“Ni watu gani ambayo wanahitaji kukua?”
“Ni adui wa baba yangu, anaitwa Livna Livba na hii sio mara yake ya kwanza kuhitaji kuniua. Asante sana Dany na Mungu akubariki”
Delfina alizungumza akanibusu shavuni na kuondoka huku akikimbia. Taswira ya Livna amsaliti wangu ikaanza kunijia kichwani mwangu, nikajikuta nikitawaliwa na hasira kali na kwa haraka nikageuka na kuanza kurudi msituni huku nikikimbia, nikihitaji kumkamata mmoja wa watu wake nimpatie meseji atakayo ipeleka kwa bosi wake

ENDELEA
Ndani ya msitu mzima kazi yangu ni kuhakikisha kwamba ninawapata watu wa Livna Livba. Ila kadri nilivyo zidi kusonga mbele sikuweza kuona dalili yoyote ya mtu ndani ya huu msitu na nikajikuta nikitokea sehemu ya maegosho ya magari. Japo polisi na waandhishi wa habari walisha jitokeza kuchukua matukio ambayo yametokea katika hili eneo. Nikajipenyeza penyeza kwa watu ambao wamekusanyika pemebi wakitazama jinsi polisi wakifanya uchunguzi wao. Nikaanza kurudi kuelekea sehemu ambapo tulitokea kutoka kwenye ngome yetu ya Al-Shabab. Nikafanikiwa kufika salama pasipo mtu yoyote kuniona, nikawakuta Ruben na rafi yetu ambaye tulitoroka naye.

“Dany ulikuwa wapi?”
“Babu pale lile tukio lilivyo tokea, nilijibanza kwenye moja ya kona ndio muda huuu ndio ninatoka baada ya kuona mambo kutulia”
“Ahaa ilikuwa bado nusu tuingie kwa maana tulihisi ni miongoni mwa watu walio kufa”
“Ahaaa sifi  kirahisi namna hiyo”
Sikutaka marafiki zangu kuweza kufahamu kwamba kuna jambo gani ambalo nimelifanya. Tukaingia kwenye shimo letu, tukachukua tochi zetu, tukaziwasha na kuelekee sehemu ambayo inatokezea katika chumba kilichopo ndani ya ngome hii. Hatukuchukua muda sana tukafika kwenye shimo letu, akapanda mmoja mmoja. Tukafunika sehemu hii tunayo tokelezea, chumba tukakipanga vizuri, nikabadilisha nguo zangu na kuvaa nguo nilizo kuwa nimezivaa.

“Sasa waskaji?”
“Poa bwana Dany japo mambo yameharibika”
“Musijali, mukipata nafasi nyingine kama hii musisahau kunialika”
“Usijali kaka, sisi kila weakend tunatoka”
“Poa poa”
Nikafungua mlango na kutoka kaatika chumba hichi. Japo ni majira ya usiku sana ila nikajitahidi kutembea kwa kujiamini kama nipo kwenye lindo. Nikafanikiwa kufika chumbani kwangu, nikaingia, nikawasha taa kuangalia  kama usalama wa chumba kipo, kisha nikaizima na kulala kitandani. Sura ya Livna Livba kwa mara kadhaa ikaanza kunitawala kichwani mwangu, kila muda ninajaribu kufikiria ni jinsi gani ninavyo weza kumpata.

‘Au  atakuwepo hapa Somalia?’
Nilijiuliza maswali mengi. Matumaini yakaanza kunijaa moyoni mwangu kwa maana tayari nimesha gundua njia ambayo inaweza kunisaidia kutoka katika hii kambi pasipo watu wengine kunistukia, kumshuhulikia Livna Livba kisha nitafwatia na K2 hawa ndio wanawake ambao ni maadui zangu wakubwa chini ya hili juu. Hadi kuna pambazuka kichwa changu kimesha panga mipango ya kipelelezi ya chini chini, kuhakikisha ninampata adui yangu mmoja baada ya mwengine.

“Ni muda wangu sasa”
Nilizungumza huku nikijinyoosha viungo vyangu, nikaanza kufanya mazoezi madogo madogo ndani ya chumba changu. Nilipo hakikisha nipo vizuri, ndio nikatoke nje kuelekea kwenye mazoezi ya kikundi.
“Jana usiku ulikuwa wapi?”
Mwalimu wangu wa mazoezi aliniuliza kwa sauti ya chini sana pasipo mwajeshi mwengine kusikia. Kidogo nikastuka ila akili yangu sasa hivi nimesha iweka katika hali ya kuweza kupanga na kupangua matatizo kwa ustadi wa hali ya juu.
“Nilikuwa kwa Ruben”

Ndalichako Aijibu Ripoti ya CAG

$
0
0
Waziri wa Elimu na mafunzo ya Ufundi, Joyce Ndalichako, amesema anaitumia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali kama changamoto na chachu ya kuendelea kufanya kazi nzuri.

 Ndalicho ameyasema hayo leo Aprili 17 wakati akijibu hoja za ripoti ya CAG iliyosomwa wiki iliyopita bungeni.

 Wiki iliyopita mawaziri wanane walifanya mkutano na waandishi wa habari wakijibu hoja za ripoti ya CAG.

“Serikali ya awamu ya tano kwenye suala la udhibiti haina utani kila mtu ameona kazi ambayo imefanyika, tunapopata ripoti ya CAG, inatupa chachu ya kuendeleza na kazi nzuri inayofanywa na serikali ya awamu ya tano,” amesema

Amesema kama CAG alivyoshauri, watafanyia kazi mapendekezo ya CAG na pia watawachukulia hatua watendaji wanaotumia vibaya fedha za umma.

Ndalichako alizungumzia hoja ya CAG kuhusu ukusanyaji hafifu wa fedha za mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu na akasema, tangu serikali ya awamo ya tano iingie madarakani, kumekuwa na ongezeko la ukusanyaji wa madeni hayo.

“Taarifa ya CAG 2015/16 hadi 2016/17    inaionyesha kuwa makusanyo yameongezeka kutoka Sh28bilioni hadi Sh 116bilioni. Hilo ni ongezeko la asilimia 300. Takwimu hazidanganyi,” amesema

Hata hivyo amesema bado makusanyo hayo hayatoshelezi na ameitaka  Menejimenti ya Bodi ya Mikopo kuhakikisha ukusanyaji wa mikopo unaimarishwa.

Serikali kuhamia Dodoma kwaongeza bajeti ofisi ya makamu wa rais

$
0
0
Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria imesema katika bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) mwaka 2017/18 kuna ongezeko la fedha lililotokana na gharama za kuhamisha watumishi wa ofisi hiyo kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma, kwamba ongezeko hilo ni zaidi ya fedha zilizoidhinishwa na Bunge.

Akisoma taarifa ya kamati hiyo kuhusu utekelezaji wa bajeti ya ofisi hiyo kwa niaba ya mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohamed Mchengerwa,  mbunge wa Viti Maalum (CCM), Amina Mollel amesema katika mwaka wa fedha 2017/18  ofisi binafsi ya makamu wa rais ilitengewa Sh4.9bilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

Amesema hadi kufikia Februari 2018, ofisi hiyo ilipokea Sh5bilioni sawa na asilimia 103 ya bajeti ya matumizi ya kawaida, ikiwa ni ongezeko la asilimia tatu.

“Kiasi hicho kiliongezeka kutokana na gharama za kuhamisha watumishi wa ofisi ya makamu wa Rais kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma,” amesema.

Amebainisha kuwa pia ofisi hiyo mwaka 2017/18 ilitengewa Sh8.2bilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida, kwamba hadi kufikia Machi 2018 ofisi hiyo ilipokea Sh10.5bilioni sawa na asilimia 128 ya bajeti ya matumizi ya kawaida, ikiwa ni ongezeko la asilimia 28 zaidi ya fedha zilizoidhinishwa na Bunge.

“Uchambuzi huu unaonyesha kumekuwa na mwenendo mzuri na wa kuridhisha kuhusu upatikanaji  wa fedha kwa ofisi ya makamu wa rais. Maoni ya kamati ni kwamba hali hii ya upatikanaji wa fedha kwa wakati inatakiwa kuendelea na kuzingatiwa na Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19,” amesema Mollel.

Shilole Apangua Tuhuma za Kuivujisha Video ya Uchi ya Nandy

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Shilole amefunguka kuhusu tuhuma za kuvujisha video ya utupu ya Nandy na Bill Nas, na kusema kwamba hahusiki na hajawahi kuona picha yoyote ya wawili hao wakiwa faragha.

Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Shilole amesema post aliyoweka insta kuhusu kuwa na picha za faragha za wawili hao alikuwa anatania, lakini ukweli ni kwamba hana picha yoyote na hajawahi kuona picha yoyote kabla.

Akiendelea kutoa utetezi wake Shilole amesema hahusiki kwenye kuvujisha video hiyo, isipokuwa inawezekana kuna mtu alikuwa nayo akapata kisingizio baada ya Shilole kupost ili aonekane ni yeye aliyevujisha.

“Hamna kitu kama hicho, mimi nilileta mzaha na nilitania tu, ni kama vile unamwambia mtu tuone kama kesho utaamka, kesho mtu anakufa kweli unaonekana ndiye wewe, kumbe watu walikuwa na mambo yao tayari, lakini kiukweli sihusiki, sijawahi kuziona nimetania, hiyo ni mtu ametembea na link au mtu alikuwa anatafutia sababu”, amesema Shilole.

Hivi karibuni baada ya video ya utupu ya Nandy na Bill Nas kuvuja mtandaoni, watu wengi wamekuwa wakimtuhumu Shilole wakiamini ndiye kavujisha, baada ya kusema kwamba ana picha nyingi za faragha za wawili hao, kwenye ukurasa wake wa instagram.

Serikali Yaeleza Utekelezaji Hoja Za CAG Sekta Za Afya Na Elimu

$
0
0
Serikali imesisitiza kuwa hakuna hoja ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika sekta zote na hususani sekta za Afya na Elimu ambayo haitatekelezwa ili kuhakikisha azma ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inafikiwa ipasavyo.

Ahadi hiyo imetolewa mjini hapa leo na Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia walipozungumza na waandishi wa habari kueleza utekelezaji wa hoja za CAG katika sekta zao.

Waziri Ummy: Tunakagua Deni la Wagonjwa Nje
Akieleza utekelezaji wa hoja mbalimbali katika sekta ya Afya, Waziri Ummy ameeleza kuwa Wizara ya Afya, baada ya kupata taarifa ya CAG kuhusu kuongezeka kwa deni la matibabu ya wagonjwa wanaopata rufaa nje ya nchi, imeamua kufanya uchunguzi wa kina wa kitabibu na kihasibu kujua usahihi wa deni hili ili kuchukua hatua madhubuti.

Aidha, amesisitiza kuwa Wizara imekubaliana na ushauri wa CAG wa kuhakikisha Serikali inaendelea kuboresha utoaji wa huduma za kibingwa hapa hapa nchini nchini ili kupunguza gharama. Waziri Ummy ameeleza hatua mbalimbali zilizochukulia kutekeleza agizo hilo ikiwemo kuanza kutolewa hapa nchini huduma za upasuaji wa moyo, upandikizaji wa figo, uwekaji wa vifaa vya usikivu na matibabu ya magonjwa ya mifupa na mishipa ya fahamu.

Kwa upande wa huduma za kibingwa katika maradhi ya saratani, Waziri Ummy alisema tatizo kubwa lililopo sasa ni huduma za kiwango cha juu cha kupima ugonjwa huo ambazo hazipatikani sehemu nyingi za Afrika. Hata hivyo alisema katika mwaka mmoja ujao Tanzania itamaliza tatizo hilo kwani Serikali imetenga Shilingi bilioni 14.5 mwaka ujao wa fedha kununua mashine ya kupima saratani (PET-CT-SCAN)

Kuhusu uingizwaji wa bidhaa zenye thamani ya Dola za Marekani Milioni 1.94 kwa kutumia vibali vya kughushi, Waziri Ummy amesema wameshachukua hatua za haraka kupitia Bodi ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuwabaini wote waliohusika na tayari baadhi wameshakabidhiwa kwenye vyombo vya dola huku TFDA ikichukua hatua za kujiunga na mfumo wa TRA ili kutambua nyaraka zisizo halali.

“Wizara yangu itahakikisha kuwa maoni yote ya CAG yanaendelea kufanyiwa kazi kwa haraka zaidi ili kuhakikisha hakuna senti ya wananchi katika sekta ya afya inatumika kinyume na matarajio,” alisema Waziri Ummy.

Prof. Ndalichako: Tunakichunguza Kitengo cha Manunuzi
Akizungumzia maeneo kadhaa ya sekta ya elimu, Waziri Ndalichako amekubaliana na hoja mbalimbali za CAG hasa katika eneo la ucheleweshaji wa ujenzi wa miradi mbalimbali ya elimu ikiwemo ucheleweshaji wa mradi wa ujenzi wa shilingi bilioni 4.6 katika Chuo cha Ualimu Ndala.

Prof. Ndalichako amekiri kuwa kuna tatizo ndani ya Kitengo cha Manunuzi wizarani kwake. Kufuatia hali hiyo, ameagiza uchunguzi kuhusu ufanisi wa Kitengo hicho ambao utakamilika mwishoni mwa mwezi huu na amesisitiza kuwa hatasita kuchukua hatua kali dhidi ya watakaobainika kuchelewesha miradi muhimu ya maendeleo.

Kwa upande wa changamoto mbalimbali katika utoaji na ufuatiliaji wa madeni ya mikopo ya Elimu ya Juu, Prof. Ndalichako ameeleza hatua mbalimbali ambazo Serikali imezichukua ikiwemo kuteua Mkurugenzi Mkuu mpya wa Bodi ya Mikopo na kuunda Bodi mpya Agosti mwaka jana; mabadiliko ambayo yameleta mageuzi katika kupunguza muda wa wanafunzi kupata mikopo na vile vile kuongezeka makusanyo ya madeni ya mikopo.

“CAG alionesha kuwa miaka ya nyuma Bodi ilikuwa inakusanya kati ya Shilingi bilioni 32 na 48 za madeni ya mikopo. Lakini tangu iingie Serikali ya Awamu ya Tano na mabadiliko yaliyofanyika, ukusanyaji umeongezeka hadi shilingi bilioni 116 mwaka 2016/17 na mwaka huu wa fedha hadi kufikia Machi, 2018 kiasi cha Shilingi bilioni 132.20 ambazo ni sawa na asilimia 101 ya lengo la mwaka 2017/18,” alisema na kuongeza:

“Nakiri pia kwamba huko nyuma kulikuwa na udhaifu katika kuwatambua wadaiwa sugu. Hivi sasa kazi inafanyika ambapo Bodi ya Mikopo imeongeza idadi ya kuwatambua wadaiwa sugu kufikia 147,231 mwaka 2017/18 kutoka wadaiwa sugu 48 tu waliobainishwa awali ambapo kati ya waliobainishwa jumla ya wadaiwa 42,213 wameshaanza kulipa madeni yao ya mikopo.”

Waziri Ndalichako ametumia fursa hiyo kusisitiza kuwa Wizara yake pia imewaagiza wataalamu na viongozi wote wa taasisi zilizo chini yake kuhakikisha kuwa wanapitia neno kwa neno taarifa ya CAG ili kuhakikisha maeneo yote yenye changamoto yanafanyiwa kazi.

Kesho katika mfululizo wa mawaziri kueleza utekelezaji wa hoja za CAG itakuwa ni zamu ya Wizara ya Nchi (Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira) na Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Imetolewa na:
Dkt. Hassan Abbasi,
Mkurugenzi, Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 18

Waziri Profesa Makame Mbarawa Afanya Ziara Ya Kushtukiza Shirika La Posta Tanzania Kukagua Utendaji

$
0
0
WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mh. Profesa Makame Mbarawa (MB)  jana  tarehe 17 Aprili, 2018 amefanya ziara ya kushtukiza Makao Makuu ya Shirika la Posta Tanzania.

Mhe. Profesa Mbarawa ametembelea  Makao Makuu ya Shirika la Posta Tanzania kwa lengo la kukagua utendaji na uendeshaji wa shughuli mbalimbali za Posta, katika ziara hiyo Mhe. Waziri aliongozana na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Shirika la Posta Luteni Kanali mstaafu Dr. Haruni Kondo.

Katika ziara hiyo Mhe. Waziri alitaka kujionea matumizi ya mifumo ya kielektronik na namna ambavyo Shirika limejipanga kuitumia mifumo mbalimbali ili kusimamia utendaji kwa ukaribu.

Mhe. Waziri Mbarawa alitembelea idara ya Fedha, Idara ya Barua na Logistiki, Idara ya Sheria, Idara ya Masoko na pia alikagua mifumo  udhibiti wa gharama za mafuta na mwenendo wa magari ya Shirika yanayosafiri kati ya  Dar es salaam na mikoani.

Katika ziara hiyo Mh. Waziri ameitaka menejimenti ya Shirika kusimamia utendaji kazi na kuzingatia weledi na matumizi ya mifumo ya kielektroniki na kufanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia kasi ya Serikali ya awamu ya tano na kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

Mhe. Waziri alitoa msisitizo wa kufanya kazi kwa bidii ili kuongeza ufanisi na kukuza tija kwa kila Idara ndani ya Shirka la Posta. Waziri amemwaagiza Kaimu Postamasta Mkuu Hassan Mwang’ombe kufuatilia utendaji wa kila idara na kupata taarifa za mara kwa mara ili kuimarisha utendaji wa shirika.

Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Shirika la Posta alimshukuru Waziri Mhe. Mbarawa kwa kutembelea Shirika la Posta na kuahidi kuwa maagizo yote na maelekezo aliyoyatoa atayasimamia kikamilifu ili kuleta tija na Ufanisi zaidi.

Jecha Salim Jecha Ang'atuka Tume ya Uchaguzi Zanzibar

$
0
0

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha amemaliza muda wake wa majukumu ya tume hiyo kwa kipindi cha miaka mitano kilichoanzia Aprili 30,2 013 hadi Aprili 29, 2018 ambapo yeye na wajumbe wa tume hiyo wamekabidhi ripoti yao ya kazi.

Akitoa taarifa yake kwa Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein, Jecha amesema kuwa tume inaamini kwamba, mafanikio yaliyopatikana wakati wa utekelezaji wa majukumu yake hasa ya kiuchaguzi yalitokana na ushirikiano wa wadau mbalimbali na wananchi kwa jumla.

"Ndani ya miaka mitano tume imeweza kuendesha jumla ya chaguzi ndogo nne, zikiwemo chaguzi ndogo tatu za Udiwani na chaguzi moja ya uwakilishi pamoja na kusimamia uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25,2015 na ule wa marudio yake Machi 20, 2016. Tume imefanya mapitio ya majimbo ya uchaguzi na kubadilisha mipaka ya majimbo ya uchaguzi, majina ya majimbo na kuongeza idadi ya majimbo kutoka 50 hadi 54", ameeleza Jecha.

Pamoja na hayo, Jecha ameendelea kwa kusema "Tume imeweza kufanya uandikishaji wa wapiga kura kwa awamu mbili na kuliendeleza daftari la kudumu la wapiga kura sambamba na kuendesha programu mbalimbali za elimu ya wapiga kura kupitia vyombo vya habari, mikutano ya wadau, uchapishaji wa vipeperushi, majarida na makala mbalimbali".

Aidha, Mwenyekiti huyo amemueleza Dkt. Shein kuwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar imechaguliwa kuwa kiongozi wa Uchaguzi Mkuu wa nchini Congo utakaofanyika mwezi Disemba mwaka huu.

Kwa upande wake, Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein ameipongeza Tume hiyo kwa kutekeleza vyema majukumu yake ndani ya miaka mitano kwa kuendesha chaguzi zote .

"Tume hii inastahiki pongezi kwa kuifanikisha vyema kazi waliyopewa ikiwa ni pamoja na kuendesha chaguzi zote ukiwemo uchaguzi Mkuu, chaguzi ndogo na ule uchaguzi wa marudio ambazo zote hizo zilifanywa kwa ufanisi mkubwa", amesema Dkt. Shein.

Wajumbe wa tume hiyo ambao wamemaliza muda wao ni Mwenyekiti mwenyewe Jecha Salim Jecha, Jaji Abdul-hakim Ameir Issa, Balozi Omar Ramadhan Mapuri, Nassor Khamis Mohammed, Ayoub Bakari Hamad, Haji Ramadhan Haji na Salmin Senga Salmin ambao wote hao waliapishwa rasmi  Mei,4, 2013.

Neema yaja kwa watumishi wa umma

$
0
0
SERIKALI imetangaza neema kwa watumishi wa umma 4,812 baada ya jana kubainisha kuwa kuna fursa za mafunzo 659 zitakazotolewa na Serikali ya China.

Fursa hizo za mafunzo zimejikita kwenye maeneo ya kipaumbele cha taifa yaliyoainishwa katika Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano (2016/17-2020/21).

Katika mkutano wake na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari na Elimu ya Bunge mjini hapa jana, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk. Laurean Ndumbaro, alisema mafunzo yamejikita kwenye uhandisi wa viwanda, mawasiliano na usafirishaji.

Dk. Ndumbaro pia alisema mafunzo hayo yatajikita kwenye kilimo, elimu, afya, biashara na uchumi, Tehama na utawala bora.

Alisema gharama za mafunzo hayo zitagharamiwa na Serikali ya Watu wa China kuanzia usafiri wa ndege kwenda na kurudi, malazi, chakula na ada.

"Serikali, waajiri watatakiwa kuwawezesha watumishi walio chini yao kuomba na kuhudhuria mafunzo hayo kulingana na sheria, kanuni na taratibu za utumishi," alisema Dk. Ndumbaro.

Gigy Money Ahofia Kupotea Kwenye Gemu

$
0
0
Msanii wa Bongo fleva Gift Stanford maarufu kwa Jina la usanii kama Gigy Money aliyetamba na kibao chake cha Nampa papa amehofia kupotezwa katika gemu ya Bongo fleva kipindi hiki ambacho ni mjamzito.

Gigy Money ameibuka baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu huku hali hiyo Ikiwa imesababishwa na kuwa mjamzito hivyo kukiri kuwa anashindwa kufanya kazi nyingi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Gigy Money ameongelea hofu yake ya kusahaulika kutokana na kuwa kimya na kuandika ujumbe mfupi uliosindikizwa na picha zake mpya:

"Hapa mjini nikisema siposti msije mkanisahau bure nipo kiranja wa mashangingi hali ni mbayaaa hali ni teteee”.


Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images