Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Bulaya Apelekwa Mahakamani Kuunganishwa na Akina Mbowe

0
0
Mbunge wa Bunda Mjini (Chadema), Ester Bulaya amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kuripoti kituo kikuu cha polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Bulaya amepelekwa Kisutu leo Jumatatu Aprili 16, 2018 ambako ameungana na viongozi wengine wa chama hicho wanaosubiri kesi dhidi yao kutajwa.

Hivi karibuni mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche alifikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashtaka matatu na kuachiwa kwa dhamana.

Heche aliunganishwa na viongozi wengine wa chama hicho wanaokabiliwa na mashtaka ya kuchochea chuki wanayodaiwa kuyatenda Februari 16, 2018 katika maeneo ya viwanja vya Buibui na Barabara ya Kawawa wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Viongozi wengine wa Chadema ambao wamesharipoti mahakamani ni naibu katibu mkuu (Bara), John Mnyika; mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee; mwenyekiti Kanda ya Serengeti, John Heche; mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa; katibu mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji; na mweka hazina wa Bawacha, Esther Matiko.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ambao wamefika mahakamani ni mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na naibu katibu mkuu (Zanzibar), Salum Mwalimu.

Kwa mara ya kwanza washtakiwa walifikishwa mahakamani Machi 27, 2018.

Polisi Warushiana Risasi...Mmoja Afariki

0
0
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), ambaye alikuwa lindo, jana alfajiri aliwashambulia mwenzake, raia na kutishia kumfyatulia risasi mkuu wake nje ya benki ya CRDB jijini hapa na jitihada za kumdhibiti zikasababisha kifo chake.

Jeshi la Polisi limeahidi kutolea ufafanuzi tukio hilo mara baada ya kukamilisha uchunguzi wake.

Wakisimulia jinsi tukio hilo lilivyokuwa, wananchi wanaoendesha shughuli zao jirani na benki hiyo iliyo Tarafa ya Ngamiani, walisema mashambulizi ya risasi yalianza saa 11.30 alfajiri baada ya kusikika kelele ya msichana eneo la kuegeshea magari ya benki hiyo.

Walisema kelele hizo zilisababisha mmoja wa askari aliyekuwa zamu kuzunguka kushuhudia nini kinaendelea, ndipo akamkuta askari mwenzake aliyekuwa naye zamu akiwa na msichana, huku msichana huyo akipiga kelele.

Kwa mujibu wa mashuhuda hao, askari aliyefahamika kwa jina la Valerian Temba alimyang’anya mwenzake silaha aliyokuwa ameshika na kisha kumfyatulia risasi iliyomjeruhi mguuni.

“Mara askari waliokuwa wakilinda benki ya NMB ya jirani wakakimbilia eneo la tukio, lakini nao wakatishiwa kupigwa. Ndipo wakampigia simu mkubwa wao wa FFU ambaye alikuja haraka na kukuta tafrani hiyo, ”alisema mtu aliyejitambulisha kwa jina la Charles Mathias.

Shuhuda huyo alisema wakati tafrani hiyo ikiendelea, askari walizungushia kamba eneo lote la benki ya CRDB kama ishara ya kuzuia watu wasipite kwa kuwa Temba alikuwa ameelekeza bunduki akitishia kuua yeyote ambaye angemsogelea.

Mashuhuda hao walisema, mkuu wao FFU aliwasili na kumsihi askari huyo kusalimisha silaha lakini hakufanikiwa.

“Yule askari alisisitiza kuwa angemuua hata yeye (mkuu wake) endapo angemfuata,” alisema

Mashuhuda hao wameeleza kuwa askari huyo alianza kurusha risasi hovyo zilizoharibu magari na baadhi ya nyumba za jirani, ndipo askari wenzake walipoamua kumdhibiti ili asisababisha madhara zaidi.

Inadaiwa kuwa askari wenzake walifyatua risasi na moja ikamjeruhi na alifariki baadaye wakati akipata matibabu.

Baadhi ya wakazi wa eneo hilo, walisema waliposikia milio ya risasi walidhani ni sehemu ya mazoezi ya polisi ambao Jumamosi walikuwa wakiadhimisha Siku ya Familia.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe alisema atatolea maelezo ya tukio hilo mara baada ya jeshi la polisi kukamilisha uchunguzi kwa mujibu wa taratibu za kijeshi.

“Watu wanaeleza wanavyoona, lakini niseme tu kwamba fanyeni subira hadi tutakapokamilisha uchunguzi kama ambavyo taratibu za kijeshi zilivyo. Nitawaeleza kila kitu hakuna kitakachofichwa,” alisema Bukombe.
 
Credidt: Mwananchi

Baba amrusha mwanaye wa mwaka mmoja kutoka juu ya paa

0
0
Mwanaume mmoja kutoka nchini Afrika Kusini ameingia kwenye headlines za vyombo vya habari duniani kwa kitendo alichokifanya cha kushangaza baada ya kumtupa mtoto wake kutoka juu ya bati la nyumba yake.

Inaelezwa kuwa mwanaume huyo ambaye ana umri wa miaka 38 nyumba yake ilitakiwa kubomolewa na polisi kutokana na kuishi katika makazi ‘haramu’ na katika kufanyika kwa zoezi hilo aliamua kupinga nyumba yake kubomolewa kwa kutishia kumtupa mtoto wake.

Mwanaume huyo alipanda juu ya nyumba yake akiwa amemshikilia mtoto wake huyo wa kike wa mwaka mmoja na pindi askari alipomsogelea alimwachia mtoto huyo na bahati nzuri alidakwa na moja ya maaskari waliokuwa eneo hilo.

Mtoto huyo anaripotiwa kutojeruhiwa na mwanaume huyo amekamatwa na kufunguliwa kesi ya jaribia la kuua.

Abdul Nondo Aitaka Tanzania iige Kenya

0
0
Mwenyekiti wa mtandao wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Tanzania (TSNP), Mahmud Abdul Nondo amefunguka na kuitaka serikali ya Tanzania kuiga serikali ya nchini Kenya ambayo imeweza kutoa taulo za kike kwa wanafunzi wote wa kike waliopo mashuleni.

Abdul Nondo amesema kuwa yeye anaamini kuwa serikali ya Tanzania pia inaweza kufanikisha jambo hilo kwa kuwa wanafunzi wengi wa kike wanakosa kufika mashuleni kipindi ambacho wapo kwenye siku zao na kuathiri masomo yao.

"Bado tunaamimi hata Serikali ya Tanzania, inao uwezo mkubwa saana wa kutoa sanitary pads (taulo) bure kwa wanafunzi wa kike dada zetu, kwani takwimu zinaonesha hedhi huchangia kiasi kikubwa wanafunzi hawa kukosa masomo. Kutokana na gharama za manunuzi hasa kijijini.Hoja hii ilipelekwa bungeni na Mbunge wa viti maalumu Upendo Peneza, ila haikujadiliwa aliambiwa kuwa hakufuata utaratibu"

Abdul Nondo aliendelea kusema atashauriana na viongozi wake wa TSNP kuangalia namna wanavyoweza kufanya ili wabunge ambao wanaguswa na jambo hilo wasichoke kuliwasilisha bungeni.

"Nitashauriana na viongozi wenzangu wa TSNP kuangalia namna tunavyoweza kufanya suala hili kama Agenda kubwa zaidi, na kuendelea kufanya ushawishi kwa wabunge ambao wanaguswa na jambo hili ili wasichoke kuliwasilisha bungeni kwa Mara nyingine. 

"Ili serikali ijumuishe mpango huu wa kutoa pads bure katika Sera yake ya elimu bure. Ili wanafunzi hawa wapate haki yao kikamilifu ya kupata elimu kama Kenya imeweza hata Tanzania, tunaweza fanya hivi pia kwa manufaa ya dada zetu hawa" Abdul Nondo

Ripoti ya CAG yaondoka na meneja kitengo cha bahari

0
0
Meneja kitengo cha bahari na maeneo tengefu, Dk Milali Machumu amesimamishwa kazi ikielezwa kuwa ameshindwa kukisimamia ipasavyo.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amesema mbali na kumsimamisha kazi, amevunja bodi ya wadhamini ya kitengo hicho na ameagiza Dk Machumu achunguzwe.

Mpina amesema hayo leo Jumatatu Aprili 16, 2018 alipozungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma akitoa ufafanuzi wa kasoro zilizoainishwa katika taarifa ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2016/17 zinazohusu wizara hiyo.

 “Kwa mamlaka niliyonayo kulingana na sheria ya kitengo cha hifadhi za bahari na maeneo tengefu, Namba 29 ya mwaka 1994 nanatoa maelekezo yafuatayo
  1.  Namsimamisha kazi Meneja wa kitengo cha bahari na maeneo tengefu (MPRU) Dr Milali Machumu mara moja kwa kushindwa kusimamia ipasavyo kitengo hiki, pamoja na kumsimamisha kazi pia atachunguzwa
  2.  Ninavunja Bodi ya wadhamimi mara moja na kuisuka upya
  3.  Ninamwagiza Katibu mkuu wa Uvuvi katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuunda kamati ya uchunguzi kuhusu utendaji kazi wa Meneja"

Ikulu: Hatuna Taarifa na Tuzo ya Rais Magufuli Kutoka Ghana

0
0
Mkurugenzi  wa Kitengo cha Mawasiliano ya Rais, Gerson Msigwa amesema Ikulu haina taarifa kuhusu tuzo aliyoshinda Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznia, Dkt. John Magufuli nchini Ghana, kama Kiongozi Bora Barani Afrika.

Msigwa ameeleza kwamba, inafahamika utaratibu wa tuzo yoyote lazima mtu anayetunukiwa apewe taarifa rasmi, lakini mpaka sasa hawajapokea taarifa yoyote kutoka kwa waandaaji wa tuzo hizo, hivyo hawajui lolote kama ni kweli au la!

“Hatuna taarifa ya tuzo hiyo, tunavyojua ni kwamba mtu yeyote anayetunukiwa tuzo lazima apewe taarifa rasmi kutoka kwa watoaji, sasa hatujapata taarifa yoyote mpaka sasa, nasikia ndio tuzo ambazo kina Monalisa wameshinda, lakini hatujapokea taarifa rasmi kuhusu tuzo hiyo, hivyo siwezi nikaizungumzia”, amesema Msigwa.

Tuzo hiyo ambayo imetajwa kuwa ameshinda Rais Magufuli, imetolewa jana Jumapili, Aprili 15, 2018 jijini Accra, Ghana, ambapo pia Watanzania wengine katika tasnia ya filamu waliibuka washindi akiwemo Yvone Chery ‘Monalisa’ na Vincent Kigosi ‘Ray’.

David Kafulila apangua hoja zote za Zitto Kabwe kuhusu ripoti ya CAG

0
0
MAONI YA DAVID KAFULILA KUHUSU RIPOTI YA CAG NA MSIMAMO WA ACT.
1.    Baada ya Chama Cha ACT kutoa tamko lao kwa kina Jana kuhusu Ripoti ya CAG kwa hesabu za 2016/17, nimeulizwa na wadau wengi kuhusu maoni yangu kufuatia tamko hilo wakihusianisha na msimamo wangu  kwamba serikali ya awamu ya tano ni tofauti sana na hivyo kutaka kunisikia maoni yangu kufuatia kilichoitwa madudu yaliyobainishwa katika uchambuzi wa chama cha ACT kuhusu serikali hii kwa mujibu wa ripoti hiyo.

Kwanza niwapongeze  ACT kwa kuunguza bongo hata kutoka na tamko lililosababisha mjadala wa masuala muhimu kwa Taifa. Binafsi naamini kwamba Ripoti za CAG ni kioo kwa Serikali na Mamlaka zake,nakwasasa ni kioo kwa vyama vya siasa pia, ndio sababu serikali huzipa uzito wa kipekee kwa kuchukua hatua haraka na hivyo kutoa somo kwa vyama vya siasa kufanya hivyo pia.Hivyo nawapongeza ACT kuipa joto hoja ya CAG ili tujadili na kubadilishana mawazo kwa maslahi ya Taifa.

Katika hoja ya 7, ACT wanasema ” Kwa ujumla Serikali imepata hati Chafu.Taarifa ya CAG ya ukaguzi wa kwanza wa makusanyo na matumizi ya kibajeti ya Serikali ya awamu ya tano, imeonesha kuwa , kwa ujumla , Serikali ya Jamhuri ya Muungano imepata hati Chafu , kwakuwa Hesabu Jumuifu za Taifa ( Consolidated Accounts ) zimepata Hati ISIYORIDHISHA ( Chafu).”

UKWELI nikwamba  Nimesoma Ripoti hiyo yenye kurasa 434, sikukuta mahala CAG ameandika kwa kigezo chochote kwamba Serikali kwa ujumla imepata hati Chafu.Nikajaribu kusoma mijadala kutafuta nani ameweza kutoa Rejea ya ni wapi CAG kasema hilo, nikakuta kwenye mjadala wa Jamiiforum, Kiongozi Mkuu wa ACT amemjibu mmoja wa waliotaka kujua ni wapi CAG kasema kwa ujumla Serikali imepata hati Chafu, katibu majibu yake, Kiongozi huyo katika majibu yake kwenye mjadala huo muda(8:09PM)  ameandika kwamba CAG amesema hilo kwenye ukurasa wa

 298. NIMERUDIA KUSOMA UKURASA HUO NENO KWA NENO HAKUNA  KITU HICHO. Ukurasa huo umeleza mapungufu ya hesabu, lakini hakuna maneno ambayo ACT inataka kuaminisha Umma kuwa yametajwa na CAG.

Inawezekana ACT baada ya kusoma maelezo hayo wakahitimisha kwamba Serikali kwa ujumla imepata hati Chafu.Hata hivyo, Mwenye Mamlaka ya kuamua madaraja ya Hati si Mwingine bali CAG kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa vya Ukaguzi wa Taasisi za Umma( ISSAIs) na Bodi ya Kimataifa ya Maadili kwa kanuni za Maadili ya wahasibu ( Kanuni ya IESBA). Hivyo sio mtu yeyote au chama au taasisi inamamlaka ya kusoma hesabu na kuzipangia daraja la Hati kama ACT wanavyotaka kufanya. Ni kwa msingi huo maneno kwamba Serikali imepata hati Chafu yanabaki kuwa kwa mujibu wa chama cha ACT na sio CAG .

2. Kwenye hoja 1, ACT wanasema Mawaziri wanafanya makosa kujibu hoja za CAG kwa waandishi wa habari na kwamba sheria ya Ukaguzi wa Umma kifungu38(1)&(2) kinaeleza Maafisa Masuuli/ Makatibu Wakuu  ndio wanapaswa kujibu hoja zilizoibuliwa na CAG tena mbele ya Kamati ya PAC&LAAC.

UKWELI Nikwamba Mawaziri wangejibu hoja za CAG mbele ya Kamati za PAC& LAAC wangekuwa wamevunja Sheria hiyo, lakini Mawaziri kueleza Waandishi wa Habari maoni yao au hatua wamezokwisha kuchukua  kuhusu Ripoti ya CAG haijakatazwa popote kwenye sheria hiyo kwani wanahabari sio kamati ya PAC wala LAAC kama ilivyotajwa katika sheria hiyo.Ndio sababu tamko hilo hilo la ACT, pamoja na kujua kwamba Ripoti hiyo haijaanza kufanyiwa kazi na Kamati za PAC& LAAC ,  ACT wamepongeza Serikali kuanza kuchukua hatua hadharani kufuatia Ripoti hiyo. Hivyo walichokipongeza ndicho wanachokihoji tena kwenye tamko hilo hilo.

3.Kuhusu kinachoitwa upotevu wa 1.5trilioni. Kwa mujibu wa ACT nikwamba kwakuwa kwenye ukaguzi wa matumizi imeonekana kiasi kilichotolewa ni trilioni 23.8..wakati kwenye makusanyo kilichopatikana ni trilioni 25.3 .hivyo kuna upotevu wa 1.5trilioni.

UKWELI ni kwamba kwamba ACT ilipaswa kuweka hoja hii katika mfumo wa swali badala ya kuhitimisha kwani hata CAG hakuna mahala amehitimisha  kuwa kuna upotevu wa trilioni1.5. Nasema walipaswa kuuliza kwasababu Mimi baada ya kusoma Hotuba ya Bajeti 2017/18, kwenye eneo la Mapitio ya Bajeti ya 2016/17 ambayo ndio hesabu zake zimekaguliwa, Waziri wa Fedha kwenye Hotuba yake alibainisha wazi kwenye Paragrafu ya 2 kipengele cha mapitio ya matumizi  kwamba Kati ya Pesa za miradi ya maendeleo kutoka nje( trilioni trilioni 3.047).Kuna kiasi cha Pesa hizo   Matumizi yake hayakupitia mfumo wa malipo wa Serikali baada ya baadhi ya washirika wa maendeleo kuzipeleka moja kwa moja kwenye miradi.

Nanukuuu ” Hata hivyo ,baadhi ya fedha za nje za kugharimia miradi ya Maendeleo hazikujumuishwa kwenye matumizi  kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kuchelewa kupata thamani halisi ya vifaa vilivyopelekwa moja kwa moja kwenye miradi kutokana na baadhi ya washirika wa Maendeleo kuendelea kupeleka fedha moja kwa moja bila kupitia mfumo wa malipo wa Serikali”

Katika msingi huo ni wazi fedha ambazo hazikutolewa kupitia mfumo wa malipo wa Serikali CAG asingeweza kuziona na hivyo kujitokeza kwa tofauti ya makusanyo na fedha iliyolipwa sio jambo la kushangaza katika mazingira hayo.Najua Serikali inaweza kueleza hili kwa takwimu zaidi.

4.    Hoja kwamba Serikali imetekeleza Bajeti kwa asilimia 68% huku Bajeti ya Serikali za mitaa ikitekelezwa kwa asilimia 51ni utekelezaji hafifu nadhani ingekuwa vema kama ACT wangefanya ulinganisho.waseme kiasi hicho ni kidogo kulinganisha na miaka gani. Kwani navyojua miaka michache iliyopita Bajeti ya Serikali za mitaa ilitekelezwa mpaka kwa asilimia35%.
Hivyo utekelezaji huu wa asilimia 51 % ni hatua kubwa  hata kama haitoshi kwakuwa haijafika asilimia100%.

5. Kwamba  ACT wanasema Madeni ya nyuma yaliyolipwa bila idhini ya bunge ni madeni hewa, Nadhani ACT wangetafuta msamiati tofauti kwani madeni hewa ni Yale yasiyokuwepo, lakini kama yamehakikiwa kuwa ni madeni halali hayawezi kuitwa madeni hewa.

6. Kwamba CAG hakukagua ATCL hivyo nikasoro kwa CAG,  nadhani ibaki kama walivyoshauri kwamba ukaguzi ujao CAG aone haja ya kukagua lakini huwezi kumlaumu kutokagua kwa hoja tu manunuzi ya ndege yalifanyika katika mwaka huo wa fedha uliokaguliwa 2016/17 kwani hakuna mwaka CAG alikagua mashirika yote. laiti ingekuwa yamekaguliwa mashirika yote likaachwa ATCL kulikuwa na uhalali wa kuhoji kulikoni.

7. Hoja kwamba Matumizi ya Serikali yanapangwa na Ikulu siku hizi badala ya Serikali ni tuhuma nzito, ingawa kwakuwa wameitoa bila uthibitisho wowote ni ngumu kwa mtu makini kuipa uzito sawia na hivyo  inakosa uzito na kuonekana kama vijembe vya kisiasa tu.
8. Hoja kwamba namna serikali inavyokopa ndani kupitia minada ya dhamana za Serikali inasababisha Benki za biashara kuvutiwa zaidi kuikopesha serikali badala ya sekta binafsi na hivyo kufanya biashara isichangamke ni hoja inayohitaji mjadala mpana.

Nasema hivyo kwasababu kwenye awamu ya nne tulilalamika kwamba Serikali ilikuwa inakopa ndani kwa mfumo huo  lakini kwa riba juu sana mpaka zaidi ya asilimia17% mwaka 2015  kwa TBs za Sik182&365 na hivyo hoja ikawa ni kwamba Benki zinapoteza hamu ya kukopesha sekta binafsi na hata kuongeza riba zaidi kwa kulinganisha na riba ambayo Benki huvuna inapoikopesha serikali( kwasababu Benki zinajua Serikali ni Risk free).

Ni kwasababu hiyo tukawa tunajenga hoja bungeni serikali isikope kwa riba ya juu katika masoko ya dhamana ili Benki za biashara ziwe na hamu ya kukopesha sekta binafsi na kwa riba nafuu.

Kitu ambacho Serikali hii imetekeleza, kwamba kwasasa Serikali inakopa kwenye mfumo huo wa TBs kwa riba ya asilimia 5% kwa TBs za siku365 na riba ya  kwa TBs za siku182.Hii inathibitisha wazi dhamira ya serikali kutozivutia Benki za biashara ziikopeshe n badala yake zijielekeze kwenye sekta binafsi kwani riba zinayopata sasa kwa kuikopesha Serikali ni pungufu kwa zaidi ya asilimia 300% kulinganisha na mwaka 2015.

9. Mwisho nihitimishe kwa kuipongeza Serikali kwa namna  imevyofanikiwa kutekeleza kilichokuwa kilio cha Bunge la 9&10 kuhusu misamaha ya kodi ambapo kwa miaka10 mabunge hayo yalipigania misamaha ishuke mpaka asilimia1% ya pato la Taifa ikitolewa mifano ya nchi wanachama Afrika Mashariki kama kigezo( misamaha yake ilikuwa asilimia1% ya Pato la Taifa). Miaka miwili yote ya Serikali hii, misamaha ya kodi ni asilimia1% kutoka asilimia2 % mpaka asilimia3% ya pato la Taifa kabla ya awamu hii( Kwa mujibu wa Ripoti hii ya CAG).

Aidha ufanisi wa TRA katika kukusanya kodi tangu mwaka 2016 upo juu kuliko miaka mingi kama inavyojieleza kwenye Ripoti ya CAG ukurasa wa 31&32. Ambapo imebainishwa kwamfano, mwaka 2013/14 makadirio ya makusanyo ya kodi  yalikuwa billion10,320 lakini ikakusanywa bilioni 9289 , sawa na pungufu ya bilioni 1031, Mwaka 2014/15 Makisio ilikuwa kukusanya billion11262 lakini ikakusanywa billion9919 sawa na pungufu ya billioni1343. Lakini Mwaka wa Kwanza wa awamu ya tano, hesabu za 2015/16 , Makadirio yalikuwa billioni12363 lakini makusanyo yakafika billion12464 sawa na ziada ya billion101 na hata mwaka 2016/17 ambapo makisio yalikuwa juu kuliko mwenendo wa awali kwa kuwekwa billioni 15105 lakini bado makusanyo yalifika billioni14271 sawa na pungufu ya billioni834,pungufu ambayo bado ni kidogo kulinganisha na miaka iliyotangulia.( Rejea Ripoti ya CAG ukurasa31&32).

Niwashukuru watanzania wote mliohitaji kusikia maoni yangu.
David KAFULILA
Leo Aprili16,2018.

RC Makonda ataka shule zifungwe kwa masaa 72

0
0
Mkuu wa Dar es salaam, Paul Makonda ameziomba Mamlaka za Elimu kufunga shule kwa siku mbili kufuatia mvua zinazoendelea katika jiji hilo.

RC Makonda ameyasema hayo leo wakati akikagua maeneo mbalimbali yaliyoathirika na mvua zinazoendelea kunyesha katika mkoa wa Dar es salaam.

“Nimeziomba Mamlaka za elimu kufunga shule kwa siku mbili, hadi tutakapowaambia siku ya Jumatano kulingana na hali itakavyokuwa kwasababu mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mengi yamejaa mengi kwa hali hii sio salama,” amesema RC Makonda.

Hata hivyo Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini,  TMA, imesema mvua kubwa zitaendelea kunyesha mpaka mwezi Mei, mwaka huu, hivyo imewataka watu kuchukua tahadhari mapema.

Pia TMA imeeleza kuwepo kwa vipindi vifupi vya mvua kubwa katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Morogoro, Dar es salaam, Pwani, Tanga, Lindi, Mtwara, Pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba, Kagera, Geita, Mwanza, Mara, Shinyanga, Simiyu, Kigoma, Tabora, Katavi, Kilimanjaro, Arusha, na Manyara.

”Kwa Tarehe 16/04/2018 Kuna muendelezo wa tahadhari na Agalizo la Matarajio ya kuwepo kwa vipindi vifupi vya mvua kubwa”.

Okoa Ndoa Yako Sasa : Je Umepungukiwa Na Nguvu Za Kiume Au maumbile Au Mpenzi Wako Hakutimizii Utakacho?

0
0
Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sabubu ya kutokuwa na nguvu za kiume au uume wako mdogo dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA;
 1 KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA YA MWENZI WAKO
2 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA 
3 UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE 
4 KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

MAKAKANUA; HII NI dawa ya maumbili madogo...hufusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba, dawa za uzaz,Mi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo 

FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU. KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA. piga simu 0743362017. 0789234653 DR AGU

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume

0
0
Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni Sado 3 Mix Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

Sado 4 Mix; Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI DR. ULIMWENGU BINGWA Anapatikana dar magomeni moroco hotel
SIMU NO; 0759 030343 / 0622790494

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO 0754372325/ 0689013109/ 0620806813 

HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Tiba ya Fangasi Sugu, Vidonda vya Tumbo, Kuondoa Chunusi na Nguvu za Kiume

0
0
MAKANGA 3 POWER: Hutibu nguvu za kiume dakika 10 na kupona  ndani ya siku 3. Huimarisha misuli ya uume iliyolegea, pia ipo dawa ya kurefusha uume mfupi nchi 4 handi nchi 7

Tuna tiba ya kudumu ya kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kuopata choo vizuri, busha( bila opareshen)

Pia tunatibu  kisukari, presha, muguu kuuma, fangasi sugu, vidonda vya tumbo, kupunguza unene, maziwa, kuondoa chunusi pete na cheni za bahati.

Onana na Dr. Shilindes shida zako zote zitakwisha.

Tupo Mbagala Rangi tatu:  0784460348  au 0659103360

Ni Dr. Chief Malunde Pekee Anaetibu Nguvu Za Kiume Na Kumtuliza Umpendae Kwa Kutumia Dawa Za Asili

0
0
"NI DR. CHIEF MALUNDE PEKEE ANAETIBU NGUVU ZA KIUME NA KUMTULIZA UMPENDAE KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI"
-baada ya kujichimbia katika nchi za kiarabu kwa zaidi ya miaka (10)sasa amewasili nchini na dawa za tiba asilia.
 
1/NGOLO 3 POWER-ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, ina ubora wa hali ya juu wa kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wasiojiweza kufanya tendo la ndoa, inaimarisha misuli iliyolegea na kusinyaa, inarutubisha mbegu za kiume na kukufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15-25 kuwa na hamu na tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila kuchoka, inarefusha uume inchi 5-8 na kunenepesha hadi cm 4 kwa wenye maumbile madogo, dawa hii imeboreshwa na hutibu matatizo haya kwa muda mfupi tu.
 
2/MAGOYE MVUTO- dawa hii ina uwezo mkubwa sana kumvuta na kumtuliza aliekuacha awe mpenzi, mme/mke itamfanya akutafute mwenyewe ndani ya masaa 3tu na kukutimizia mahitaji yako kwa haraka na kumfunga asiwe na mtu mwingine.
 
3/SUPER LUBEJA- ni dawa ya kushepu umbo no.8 mguu wa bia, kuongeza hips, na makalio kwa muda wa siku 5tu unapata saizi uipendayo, kuondoa makovu, chunusi, harufu mbaya ya mwili michirizi, kupunguza tumbo na maziwa kwa siku 6tu.
 
4/NG'WESHI MIX- ni dawa ya biashara ya kupata wateja wengi, kusafisha nyota, kurudishwa kazini na kupandishwa cheo, kurudisha mali iliyoibiwa au kudhurumiwa.
 
PIA TUNATIBU MAGONJWA SUGU KAMA: vidonda vya tumbo, ngiri, chango na uzazi kwa kina mama: (dawa zote hazina madhara kwa mtumiaji) HUDUMA HIZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO: TUNAPATIKANA DSM BUGURUNI SHELI AU PIGA SIM NO_ 0763-181099.

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0766340868

Mpina Awataka Wawekezaji Wa Viwanda Vya Punda Kuongeza Bei

0
0
Na John Mapepele, Dodoma
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amewataka wawekezaji wa viwanda vya kuchinja Punda nchini kupandisha bei ya kununua wanyama hao badala ya shilingi laki mbili ya sasa kwa punda mmoja ili kudhibiti utoroshaji wa mifugo nje ya nchi ambapo inakadiriwa kuwa zaidi ya mifugo elfu kumi inatoroshwa mipakani kwa siku kwenda nje ya nchi inakonunuliwa kwa bei ya juu.

Akizungumza leo baada ya kufanya ziara ya kushitukiza katika Kiwanda cha Punda cha Hua Cheng Limited kilichopo nje kidogo ya mji wa Dodoma alichokifungua hivi karibuni, Waziri Mpina alisema bei hiyo haiendani na gharama halisi ya ufugaji wa Punda hali inayowafanya wafugaji kuwatorosha mifugo na kulikosesha taifa mapato makubwa.

Alisema ili punda aweze kufikia hatua ya kuchinjwa inachukua kiasi cha miaka miwili ambapo gharama zake za ufugaji zinakuwa juu ukilinganisha na bei ya shilingi laki mbili anayouzwa kwa wenye viwanda vya punda nchini.

Aidha alisema kumekuwa na utoroshaji mkubwa wa mifugo wanaokadiriwa kufikia takribani 1,614,035 kwa mwaka unaofanyika kwenye mipaka ya nchi yetu ambapo takribani shilingi bilioni 32.28 zinapotea kama ushuru na takribani shilingi bilioni 24.21 zinapotea kutokana na kodi ya mapato ambayo ingelipwa kwa nyama ambayo ingeuzwa hapo nchini.

Aidha Mpina ameunda tume ya wataalam kutoka Wizarani kwa ajili ya kuja kufanya tathmini kama kiwanda hicho kimetimiza masharti yote yaliyotolewa na Serikali baada ya kukifungua Februari mosi mwaka huu ambapo alisema ikibainika kuwa kiwanda hakijakidhi masharti yaliyotolewa na Serikali kitachukuliwa hatua kali zaidi za kisheria ikiwa ni pamoja na kukifungia kufanya kazi zake.

Aliyataja baadhi ya masharti yaliyotolewa na Serikali wakati wa kukifunga kiwanda hicho Julai 2017 kuwa ni pamoja na kuwa na ranchi za punda, kuboresha kosaafu za Punda nchini, kuunda na kuingia mikataba na vikundi vya wafugaji wa Punda na kuwa na Punda wasiopungua mia tatu katika eneo la kuhifadhia mifugo kabla ya kuchinjwa ili kuwa kuhakikisha kwamba mifugo wanaangaliwa kwa wiki mbili kabla ya kuchinjwa ili wawe katika ubora wa kimataifa.

Waziri Mpina alisema uwekezaji wa aina hiyo wa kuongeza thamani ya mazao ya mifugo ni moja ya vipaumbele vya wizara yake kwa sasa ili kuchochea kwa kasi kufanikisha azma ya Tanzania ya viwanda.

Aidha aliwahakikishia wawekezaji wa kiwanda hicho kuwa endapo watakuwa wamekamilisha masharti atawapa kibali cha kudumu ambapo pia atawaongezea idadi ya kuchinja Punda kutoka punda 20 wa sasa ili vijana wengi wapate ajira na kiwanda kiweze kuchangia zaidi katika mapato ya Serikali.

Mpina aliwahimiza wawekezaji hao kuhakikisha wanawasaidia wafugaji katika kuongeza uzalishaji, kupambana na maradhi, upatikanaji wa maji na malisho kwa
mifugo.

Alisema idadi ya punda waliopo nchini ni 520,000 tu hivyo juhudi za makusudi zinahitajika kuongeza uzalishaji.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda hicho Xun Long Go alimshukuru Waziri Mpina kwa kufungua kiwanda hicho ambapo amesema hadi sasa kiwanda kimezalisha na kuuza tani 224 za nyama ya Punda kwenda nchini China na Vietinam ambapo pia tani 52 za ngozi ya Punda ilizalishwa na kuuzwa kuanzi mwezi Februari, 2018.

Alisema kiwanda hicho kimeajiri watanzania 55 ambapo hadi sasa kina punda 88 katika maeneo ya Chalinze na Zuzu mkoani Dodoma.

Kaimu Mkurugenzi wa Uzalishaji Mifugo na Masoko wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Lucia Chacha aliutaka uongozi wa kiwanda hicho kwa kubuni mbinu za kuwasaidia wafugaji kwa kuwapatia elimu bora zaidi ya ufufaji wa punda ili waweze kuwazalisha kwa wingi zaidi kuliko ilivyo sasa

Hivi sasa Tanzania ina viwanda viwili tu vya kuchinja na kuuza nyama ya punda ambavyo ni kiwanda cha Punda cha Huacheng Limited kilichopo nje kidogo ya mji wa Dodoma na Kiwanda cha Fang Hua kilichopo Shinyanga ambavyo vyote vimepewa kibali cha kuchinja Punda 20 kwa siku kila kimoja.

Taarifa Muhimu Toka Makao ya Jeshi- JWTZ

0
0
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo (kushoto) akimvisha cheo Luteni Jenerali Paul Massao baada ya kupandishwa cheo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika hafla iliofanyika leo tarehe 16 April, 2018 Makao Makuu ya Jeshi, Upanga jijini Dar es Salaam.

Tume ya Uchaguzi yapata pigo....Watatu Wajiuzulu kwa Mpigo

0
0
Tume huru ya Uchaguzi nchini Kenya IEBC imepata pigo kubwa baada ya watumishi wake watatu kuacha kazi kwa mpigo, huku wakilaumu uongozi wa Tume hiyo

Wafanyakazi hao ambao ni Kaimu Mwenyekiti Consolata Nkatha Maina, Kamishna Margaret Mwachanya na Paul Kurgat wamejiuzulu wadhifa wao na nafasi zao za kazi ndani ya tume hiyo, huku wakisema kwamba Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati ameshindwa kuongoza.

“Kwa muda mrefu sana na mara nyingi mno, mwenyekiti wa tume ameshindwa kuwa na mkono thabiti na imara, badala yake chini ya uongozi wa Chebukati, bodi ya tume imekuwa mahali pa kutembea kwa habari zisizo za ukweli, misingi ya kutokuaminiana na kujitafutia sifa binafsi. 

"Taasisi imesababishwa kutoweza kufanya uamuzi, kuvuja nyaraka za ndani ili kutumikia malengo binafsi na kufuata maslahi binafsi, yote ambayo ni kinyume na sheria iliyowekwa ambayo inasimamia mwenendo wa uongozi wa tume na wafanyakazi”, wamesema wafanyakazi hao ambao miongoni mwao yumo Kaimu Mwenyekiti wa Tume.

Hivi karibuni Mwenyekiti wa Tume hiyo Wafula Chebukati amempa likizo ya lazima Mkurugenzi wa Tume Ezra Chiloba bila sababu maalum, huku wengi wakilaumu kitendo hicho, wakisema kuwa Chebukati anaendesha Tume kwa maslahi yake binafsi.

IEBC imekuwa ikilaumiwa kwa matukeo ya uchaguzi wa mwaka 2017 wa viongozi wa Kenya, ambao pia ulisababisha kufutwa kwa matokeo ya Urais, kwa uchaguzi wa Agosti 8, 2017.

Toka Twitter: Ushauri wa Waziri January Makamba kwa wasanii na vijana maarufu

0
0
Ujumbe huu umeandikwa leo na Waziri January Makamba katika ukurasa wake wa Twitter ikiwa ni ushauri kwa wasanii na vijana maarufu. 

Ushauri huu umechukuliwa na wengi wa watumiaji wa mitandao ya Twitter na Instagram kama muhimu kwa wasanii hasa baada ya kuibuka kwa matendo yasiyoakisi taswira njema kwa jamii kwa siku za karibuni. 

Ujumbe huo umeandikwa kwa lugha ya Kiingereza lakini tafsiri isiyo rasmi ni:

“Kwa wadogo zangu maarufu wa kike na wa kiume: umaarufu unabeba majukumu. Ushike kwa makini. Umaarufu unaweza kudumu kwa dakika 15 watu tukafurahi na kukuona muhimu – kisha maisha yakaendelea. Umaarufu pia unaweza kudumu milele, ukafa kimwili lakini jina lako lisife. Umaarufu pia unaweza kudumu na kufikia kiwango cha kukuharibu na kukuondoa kwenye mstari.”

Mmojawapo ya wasanii waliojibu ujumbe huo Twitter ni Vanessa Mdee ambaye ameshukuru

PICHA: Msaidizi wa Rais, Kanali Mlunga Akaribishwa Rasmi Ikulu

0
0
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa amemkaribisha Ikulu Msaidizi wa Rais Magufuli Kanali Mlunga. 

Kanali Mlunga amechukua nafasi ya Mbaraka Mkeremy aliyepandishwa cheo na kuwa Brigedia Jenerali.
Gerson Msigwa akimuagaMbaraka Mkeremy aliyepandishwa cheo na kuwa Brigedia Jenerali.

Mkuchika ageuka mbogo Bungeni: "Mimi nitafanya kazi gani wewe ukiniamulia"

0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Mkuchika amefunguka na kusema kuwa atawachukulia hatua watumishi wa serikali ambao wanazuia barua za watumishi wengine hasa walimu wanaotaka uhamisho zisimfikie yeye au Katibu au Waziri Mkuu.

Mkuchika amesema hayo bungeni na kudai kuwa yapo malalamiko ya baadhi ya walimu kushindwa kuhama kutokana na viongozi wao kuzuia barua zao zisifike kwake au viongozi wengine ambao wana mamlaka.

"Sasa naomba kulieleza bunge hili tukufu mwenye mamlaka ya kumkatalia uhamisho ni yule anaye andikiwa barua

"Wewe uliyeandikiwa pale kupitia kwa kiswahili sanifu kabisa, wakishasema kupitia kwa wewe si muamuzi wa mwisho, peleka barua kwa mwajiri ili mwajiri apate kuamua

"Mimi natembelea mikoani nimepata kupita mkoa mmoja naambiwa hii ofisi yetu haijapitishwa barua ya mtu kuhama hata moja, mimi nasema mimi ndiyo Waziri wa Utumishi wa Umma, nikimbaini kuna kiongozi wa utumishi anakataa kupitisha barua isinifikie mimi, isimfikie Katibu Mkuu Kilimo, isimfikie Waziri Mkuu nitamshughulikia mwa mujibu wa sheria na taratibu

"Nitafanya hivyo kwa sababu mtu huyo amejichukulia madaraka ambayo si yake,  hukuandikiwa wewe barua halafu wewe ndiye unaamua sasa mimi niliyejuu nitafanya kazi gani kama wewe unaniamulia" alihoji Mkuchika

Mbali na hilo Mkuchika amesema kuwa zoezi la kuajiri sasa linatarajiwa kuendelea baada ya zoezi la uhakiki wa vyeti feki kukaribia kukamilika na kusema serikali itaendelea na kutoa ajira mpya.

"Tutaendelea na ajira mpya kama nilivyosema 50,200 wa mwaka jana na mwaka ujao serikali imejipanga kuajiri 49,000" alisema Mkuchika
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images