Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Makonda Kula Sahani Moja na Vigogo Waliogoma Kupima DNA....."Tusijaribiane, Mimi sio Mtoto Wenu"

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa atahakikisha anawashughulikia kwa mujibu wa sheria na mamlaka aliyonayo, wanaume wanaokataa kuitikia wito wa kufika katika ofisi zake kujibu tuhuma za kutelekeza watoto na kupima vina saba (DNA).

Akizungumza kupitia TBC1, Makonda amesema kuwa wanaokataa wito huo wakidhani kuwa hadhi yao ni muhimu zaidi wanapaswa kufikiria tena kwani bahati nzuri watu hao  wanamfahamu hata kabla hajawa mkuu wa mkoa.

“Yoyote anayekaidi wito wa Ustawi wa Jamii ambao wako chini yangu, achilia mbali kwamba anakuwa amefanya kosa kwa mujibu wa sheria, kwa mamlaka tu niliyonayo mimi nakutia ndani,” alisema.

“Yaani na bahati mbaya niwaambie tu Watanzania, kwangu sheria ina nafasi kubwa sana kuliko hadhi unayojitengenezea ambayo kimsingi huna kama umeamua kutelekeza mtoto. Tusijaribiane,” aliongeza.

Mkuu huyo wa mkoa alieleza kuwa anayetunisha misuli ya kutoitikia wito anapaswa kufikiria kuwa kama anaweza kumuondoa mtu kwenye mkoa huo anapoona anahatarisha usalama na kuvunja amani, itakuwaje kwa hilo la mtu kumtelekeza mtoto.

Alisema kuwa awali, wanasiasa waliokuwa wanajinasibu kuwa hawahusiki na kinachoendelea na kwamba ni mpango wa kuchafuana kisiasa wameanza kuwa wapole baada ya kuona mama na watoto waliowatelekeza wakijitokeza na kuzungumza hadharani.

Akizungumzia hatua anazoweza kuwachukulia watu hao, Mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa baada ya Ustawi wa Jamii na dawati la wanawake la Polisi kukamilisha kazi ya kuwaita wanaolalamikiwa kukamilika, watampa ripoti ya walioitikia wito na waliokataa pamoja na hatua walizofikia na ndipo waliokaidi watajua wigo wa mamlaka yake.

“Nikiambiwa haya mashauri yamebaki hayajashughulikiwa kwa sababu walioitwa wamegoma kuja… sasa hapo ndipo utaelewa Makonda ni Mkuu wa Mkoa, mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama au  ni mtoto wako unayeweza kumuendesha kama unavyoweza kuchezea sharubu za Simba aliyelala,” alisema.

Miongoni mwa watu maarufu wanaotakiwa kufika katika ofisi za mkuu huyo wa mkoa ni Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ambaye analalamikiwa na mwanamke mwenye umri wa miaka 31 kuwa ni mtoto wake aliyemtelekeza. Mama mzazi wa mtoto huyo pia alifika katika ofisi hizo na kueleza kuwa anachosema mwanaye ni kweli kwamba baba yake ni mzee Lowassa.

Mwingine aliyeguswa na sakata hilo ni mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa ambaye naye amekataa kufika ofisi za mkuu wa mkoa na kumtaka mwanamke anayedai kuwa alizaa naye na kumtekeleza afike katika ofisi za bunge ataonana naye.

Msigwa alisema kuwa endapo itathibitika kuwa ni mwanaye yuko tayari kuacha ubunge.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

TEMBELEA KATIKA BLOG YETU HAPA>>>;

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Mbunge Chadema apigwa 'Stop ' kuchangia bungeni Baada ya Kulitaja Jina la Rais

$
0
0
Mwenyekiti  wa Bunge, Mussa Zungu, amemzuia Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Upendo Peneza, kuchangia bungeni baada ya kuendelea kulitaja jina la Rais wakati wa kuchangia kwake licha ya kukatazwa kufanya hivyo.

Upendo alikuwa akimhusisha Rais na kuzuiwa kwa maandamano nchini na matangazo ya moja kwa shughuli za chombo hicho cha kutungwa sheria, yaani ‘Bunge Live’.

Kutokana na mbunge huyo kumtaja Rais katika mchango wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, aliomba kutoa taarifa ya kukiukwa kwa kanuni za 68(1) na 64(1) za Bunge akieleza kuwa Rais anawakilishwa na mawaziri ndani ya Bunge kwa mujibu wa Katiba.

“Na kanuni hii ya 64 inatukumbusha kwamba, haturuhusiwi kuzungumza mwenendo wa Rais na hasa anapokuwa katika madaraka ndani ya ofisi yake,” alisema.

Mhagama pia alisema hawatakiwi kuzungumza jina la Rais kutaka kushawishi namna ya kutoa uamuzi na kwamba kama Peneza anaona kuna shida azungumze na wawakilishi wake.

Akitoa majibu ya mwongozo huo, Zungu alisema kuwa jina la Rais halipaswi kutajwa kwa dhihaka, halaumiwi wala hatakiwi kusemwa kama alivyofanya Peneza.

Alimtaka mbunge huyo kuuliza utendaji wa mawaziri kwa kuwa kanuni inawataka wabunge kutohoji utendaji wa Rais ndani ya Bunge.

“Jina la Rais halitumiwi kwa namna ulivyokuwa unalitumia na kwa hiyo, nayafuta maneno yote kwenye hansard (kumbukumbu rasmi za Bunge),” alisema.

Hata hivyo, baada ya kupewa nafasi ya kuendelea kuchangia, Peneza aliendelea kusema juu ya kauli za Rais.

Kutokana na hali hiyo, Mhagama alisimama tena kutaka kutoa taarifa lakini Zungu alimzuia akisema: “Natumia kanuni ya 73 ukae chini hutazungumza tena.”

Wabunge wengine waliochangia walitaka Wakala wa Barabara Vijijini (Tarura), kuongezewa mgawo wa fedha za bajeti kwa kuwapa nusu ya fedha za Wakala wa Barabara (Tanroad) ili kutimiza majukumu yake ipasavyo.

Mbunge wa Lulindi, Jerome Bwanausi (CCM), alisema kama Tarura haijaongezewa bajeti yake, utakuwa ni wakala ambao umeanzishwa lakini haujaleta tija.

“Sasa hivi wakala huu umeazima watumishi kutoka halmashauri, wapewe watumishi wao na fedha kwa ajili ya matengenezo ya barabara ili ziweze kupitika,” alisema.

Mbali na Mbunge huyo wabunge wengine waliochangia sula hilo ni pamoja na Magdalena Sakaya (Kaliua-CUF), Livingstone Lusinde (Mtera- CCM), Fred Mwakibete (Busokelo-CCM) na Maftaha Nachuma (Mtwara Mjini - CUF).

Okoa Ndoa Yako Sasa : Je Umepungukiwa Na Nguvu Za Kiume Au maumbile Au Mpenzi Wako Hakutimizii Utakacho?

$
0
0
Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sabubu ya kutokuwa na nguvu za kiume au uume wako mdogo dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA;
 1 KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA YA MWENZI WAKO
2 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA 
3 UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE 
4 KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

MAKAKANUA; HII NI dawa ya maumbili madogo...hufusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba, dawa za uzaz,Mi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo 

FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU. KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA. piga simu 0743362017. 0789234653 DR AGU

Monalisa ambwaga Lupita Nyong'o baada ya Kuibuka Mshindi wa Tuzo ya Msanii Bora wa Kike Afrika

$
0
0
Mrembo na muigizaji mkongwe kwenye tasnia ya filamu nchini Yvonne Cherrie maarufu kama 'Monalisa'  ameibuka mshindi kwenye tuzo za 'The African Prestigious Awards' nchini Ghana akimbwaga mpinzani wake Lupita Nyong'o.

Katika tuzo hizo zilizotolewa usiku wa kuamkia leo huko jijini Accra nchini Ghana Monalisa ametwaa tuzo katika kipengele cha 'Best African Actress'. Kwa mujibu wa tuzo hizo Monalisa sasa ndiye muigizaji bora wa kike barani Africa.

Monalisa amethibitisha ushindi wake kupitia mtandao wa 'Instagram' ambapo amepandisha picha akiwa na tuzo yake na kuandika ujumbe huu ''Tumeshindaaaaaaa narudi home na Tuzo za kutosha.Ahsante Watanzania,Nawapenda mno''.

Kwa ujumbe huo wa Monalisa unaashilia huenda pia kuna tuzo nyingine wameshinda Watanzania ambao walikuwa wanawania vipengele mbalimbali katika tuzo hizo kubwa za filamu nchini Ghana.

Watanzania wengine waliokuwa wanawania ni King Majuto kipengele cha Mchekeshaji Bora Afrika, Vicent Kigosi kipengele cha msanii Bora wa Kiume Afrika na Mpiga picha Mahiri Moiz Hussein katika kipengele cha Mpiga Picha Bora Afrika.

Dogo Janja Aikingia Kifua Video ya Uchi ya Nandy.......Awachana Wasanii kwa Madai kuwa ni Wanafiki, Hawana Umoja

$
0
0
Ikiwa zimepita takribani siku mbili tokea mrembo Nandy kuomba radhi kutokana na video yake ya faragha kusambaa mitandaoni, msanii Dogo Janja ameibuka na kudai wasanii hawana umoja na wanafiki huwa wanafurahi sana kuona mwenzao amepatwa na majanga ili mradi apotee katika tasnia.

Dogo Janja ametoa kauli hiyo usiku wa kuamkia leo Aprili 15, 2018 kupitia ukurasa wake maalumu wa kijamii na kusema anahisi anaweza kuchukiwa leo hii na wasanii wenzake ila ni lazima yeye aongee ukweli ili mradi donda ndugu liliopo katika muziki limepone.

"Wasanii sisi ni ma-snichi sana aise, baada ya hii ishu ya Nandy ndio nimepata uhakika. Wakati wa ishu ya Roma nilianza kuliona jinsi kwenye makundi pembeni watu kibao walikuwa wanafurahi tena maneno kibao kama atakoma, amezoea huyo. Jana na juzi nimekaa na watu wasanii wakubwa tu na wote walikuwa wanasema bora limemtokea Nandy hili angalau spidi za 'show' zitapungua", amesema Dogo Janja.

Pamoja na hayo, Dogo Janja ameendelea kwa kusema.... ..."bora BASATA ingemfungia miezi 6 apotee kidogo, walikuwa wanapiga stori kama utani ila moyoni nimefikiria sana. Wasanii tuache roho mbaya, wote sisi masikini tunahangaikia ugali. Tukipata ajali kazini, tusiombeane mabaya tutafute amani".

Kwa upande mwingine, Dogo Janja amewashauri wasanii wenzake wawe na moyo wa upendo kwa wenzao na waache tabia ya kufurahia matatizo wanayowapata wakiwa kazini.

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO 0754372325/ 0689013109/ 0620806813 

HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Ludovick Utouh Akosoa hatua ya serikali kutoa majibu juu ya taarifa za ukaguzi wa hesabu

$
0
0
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mstaafu, Ludovick Utouh, amekosoa hatua ya serikali kutoa majibu juu ya taarifa za ukaguzi wa hesabu zinazotolewa na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu (NAOT).

Amesema hoja za ukaguzi hazitolewi na mkaguliwa bali mwenye mamlaka ya kufanya hivyo ni CAG mwenyewe baada ya kuridhishwa na utekelezaji wa mapendekezo yake.

Mapema wiki hii, serikali ilianza kujibu hoja za ukaguzi za CAG kutokana na taarifa ya ukaguzi wa taasisi za umma, huku ikisisitiza kuwa inafanya hivyo kwa kuwa imepewa jukumu hilo kikatiba.

Utoah ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wajibu ambayo inalenga kuhamasisha uwajibikaji na utawala bora nchini, alisema hayo jana katika semina ya siku moja ya kuwajengea uwezo wabunge wa kamati tatu za bunge, mjini hapa.

Kamati hizo ni za Hesabu za Serikali (PAC), Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na ile ya Uwekezaji Mitaji ya Umma (PIC).Alisema inaonekana sasa hivi hakuna uelewa mzuri kwa Watanzania kuhusu Ofisi ya CAG na majukumu yake.

“Ofisi ile ipo kikatiba. CAG ana jukumu la kukagua mapato na matumizi yote ya serikali na ni jukumu lake kuuambia umma wa Watanzania aliyoyaona, hivyo niseme tu kwamba kuna utaratibu wa yeye kutengeneza hoja za ukaguzi na kutoa hoja za ukaguzi,”alisema.

Alisema inaweza kutokea CAG akaridhishwa na utekelezaji wa mapendekezo yake baada ya uhakiki ndipo hoja ya ukaguzi inafutwa kwenye daftari la hoja za ukaguzi.

Aidha, alisema kuwa anatambua kamati hizo msingi wa kazi yake ni usimamizi na uwajibikaji. Kutokana na jukumu hilo, kuna umuhimu wa kuelewa fika katika ripoti zenyewe kitu gani kinazungumzwa na kuna umuhimu wa kufanya hivyo.

“Madhumuni ya mafunzo haya ni taasisi hii kujitambulisha rasmi kwa kamati za bunge zinazoshughulika na usimamizi na uwajibikaji wa serikali ambapo ndio jukumu kubwa la taasisi yenyewe hii,”alisema Utoah.

Alisema katika semina hiyo watazungumzia pia mambo ya uwajibikaji yaliyojikita kwenye ripoti ya CAG.

Naye Mwenyekiti wa PIC, Raphael Chegeni, alisema taasisi hiyo ina watu waliobobea kwenye masuala ya usimamizi wa fedha na itawawezesha kujua namna ya kusimamia serikali.

“Pia kutambua sisi tuna mchango gani wa kuhakikisha rasilimali za taifa zinatumika vizuri. serikali ya awamu ya tano imejikita kuhakikisha kunakuwa na matumizi mazuri ya rasilimali fedha,” alisema.

Alisema serikali imewekeza zaidi ya Sh. trilioni 48 hivyo ni lazima ipate mrejesho kwenye uwekezaji wake.

Naye, Mwenyekiti wa PAC, Naghenjwa Kaboyoka, alisema mafunzo hayo yatawasaidia kuwajengea uwezo na kutambua wajibu wao.

Alisema kamati ndiyo kiungo kati ya Bunge na serikali kwa ajili ya kuona fedha za umma zinatumikaje na maofisa masuhuli wanahojiwa vipi.

“Hizi hoja za CAG zikishaletwa bungeni zinakabidhiwa, PAC ndiyo inakaa na kuchambua na kuwaita maofisa masuhuli kutoa majibu ya hoja za CAG kwa kamati kutokana na fedha walizopewa.

“Sasa kazi ya CAG anaenda kufanya uhakiki mara baada ya kuwasilishwa majibu ya hoja husika ili kama hoja inafungwa ndiyo inafungwa au kama haifungwi tunaendelea,”alisisitiza.

Mabasi ya Mwendokasi yasitisha huduma jijini Dar

$
0
0
Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, (UDART) imesitisha huduma zake kwa baadhi ya njia kuanzia saa 11:00 alfajiri tarehe 15/04/2018 kutokana na kufungwa kwa Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kwa sababu ya mafuriko yaliyosababisha maji kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi.

Aidha, kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Kimara – Morroco, Kimara – Magomeni Mapipa, na Gerezani – Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa.

Hata hivyo, Kampuni hiyo kupitia kwa mkuu wa kitengo cha mawasiliano, Deus Bugaywa imeomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Ufafanuzi wa SUMATRA kuhusu kupanda kwa nauli za mabasi ya mikoani

$
0
0
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imekanusha taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii juu ya uwepo wa nauli mpya zilizopangwa na mamlaka hiyo kwa safari za mabasi yaendayo mikoani.

Taarifa hizo zilizosambazwa mitandaoni zimedai kuwa, uwepo wa nauli hizo mpya za mabasi ya mikoani zimekuja kufuati kupanda kwa gharama za mafuta (dizeli na petroli).

Taarifa iliyotolewa na SUMATRA jana Aprili 14 kwenda kwa abiria, watoa huduma na umma kwa ujumla, imeeleza kuwa, hakuna nauli mpya zilizotangazwa na SUMATRA kwa sasa. 

Aidha, wadau wanakumbushwa kuwa, viwango vya nauli kwenda maeneo mbalimbali ya nchi vinaweza kupatikana katika tovuti ya mamlaka hiyo ya www.sumatra.go.tz

Aidha, viwango hivyo vya nauli vinaweza kupatikana kupitia ujumbe mfupi wa maandishi kwa kuandika neno Nauli (acha nafasi), sehemu unapoanzia safari (acha nafasi), sehemu unapokwenda. Kwa mfano, Nauli Dar Tanga, kisha tuma ujumbe huo kwenda namba 15200.

Kilichosababisha CHADEMA, CCM Wapewe Hati yenye Mashaka na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)

$
0
0
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad amevishika pabaya vyama vikuu vya siasa nchini CCM na Chadema baada ya kuhoji matumizi ya zaidi ya Sh19 bilioni.

Ripoti hiyo ya ukaguzi wa hesabu iliyoishia Juni 30, 2017 iliyowasilishwa bungeni wiki hii, inaonyesha kati ya vyama 19 vilivyopata usajili wa kudumu, tisa havikuwasilisha taarifa za fedha wakati sheria inataka viwasilishe ifikapo Septemba 30 kila mwaka.

Katika ukaguzi huo, CAG anahoji matumizi ya zaidi ya Sh7 bilioni kwa Chadema na zaidi ya Sh12 bilioni kwa CCM. CAG anasema katika ukaguzi walibaini kuwa chama tawala kimeendelea kuwekeza katika kampuni nne na mikopo yenye thamani ya Sh12 bilioni.

“Hata hivyo, tumejifunza kwamba mikopo hiyo haina faida yoyote iliyoonekana imeingia kwenye chama,” anasema CAG.

Pia imebainika kuwa Sh80 milioni zilitambuliwa kama mapato ya uwekezaji katika taarifa za fedha za CCM kutoka Jitegemee Trading Company Limited lakini hazikuwa na kiambatanisho kinachothibitisha kama ni gawio au kitu kingine.

CAG anasema CCM bila kuanzisha sera, uwekezaji wa chama hicho upo katika hatari ya kutumiwa vibaya na kwamba malengo yaliyowekwa yanaweza yasifikiwe.

CAG pia amebaini kupitia ukaguzi wa taarifa za fedha za CCM kwa mwaka 2016/2017 kuwa hazina taarifa za kutosha kuhusu mikataba, masharti, kiasi na sababu za kutoa msaada wa Sh455.9 milioni kwa Radio Uhuru.

Taarifa hiyo inaonyesha kuwa menejimenti ya CCM ilikopa na kuhamisha Sh337.1 milioni kutoka akaunti ya malipo ya pensheni kwenda akaunti ya katibu mkuu wa chama na kupokewa kwa stakabadhi namba 156424. 

Hata hivyo, kiasi hicho hakijarejeshwa hadi wakati wa ukaguzi na kwamba, matokeo yake ni uwezekano wa madai ya wafanyakazi wastaafu kutolipwa kwa wakati.

CAG anasema Aprili 11, 2015 Chadema iliingia makubaliano na mwanachama wake ili awakopeshe Sh2 bilioni kwa ajili ya shughuli za chama.

Hata hivyo, anasema hawakukuta nyaraka zinazoonyesha kiasi hicho cha mkopo walichokubaliana iwapo kilitolewa na kupokewa na chama husika. 

CAG anasema katika ukaguzi, alikuta ankara ya kodi (tax invoice) yenye namba 201508226 iliyotolewa Agosti 26, 2016 ya Sh866.6 milioni ambayo ililipwa na mwanachama kwa niaba ya chama kwa ajili ya mabango ya matangazo yaliyoletwa na mzabuni M/S Milestone International Co. Ltd.

Anasema nje ya deni hilo, Sh715 milioni zililipwa kwa mwanachama kama marejesho ya fedha iliyokopwa kulipia ununuzi wa mabango bila ya kuambatishwa makubaliano ya kisheria.

Pia, anahoji matumizi ya Sh2.3 bilioni ambazo ni makusanyo ya Chadema kwa wanachama wake kwa mwaka 2014/15 na 2015/16, fedha ambazo zinadaiwa kutopelekwa benki na matumizi yake kutotolewa kwa ajili ya ukaguzi.

Ripoti ya CAG inaonyesha kuwa Chadema ilifanya ununuzi wa Sh2.1 bilioni bila ushindani; malipo ya Sh240.1 milioni yenye nyaraka pungufu; na Sh558.9 milioni ambazo ni masurufu ambayo hayakurejeshwa.

Wakati wa ukaguzi, CAG anasema alibaini vyama vinne vya Chadema (Kanda ya Magharibi), NLD, Demokrasia Makini na ADC havina daftari la mali za kudumu, hali inayosababisha ugumu wa kujua mali za chama, aina yake, gharama na sehemu zilipo, hivyo kuziachia mali za chama kwenye hatari ya kutumika vibaya.

“Kukosa daftari la mali za kudumu ni kinyume cha Sheria ya Usajili wa Vyama vya Siasa inayovitaka vyama vilivyosajiliwa kuwasilisha kwa msajili tamko la mali zote kila mwaka” anasema CAG.

“Ninashauri vyama vya siasa viwe na madaftari ya mali za kudumu ambayo yanahuishwa mara kwa mara kutokana na ununuzi au mauzo ya mali,” inasema taarifa ya CAG.

Kuhusu malipo yenye nyaraka pungufu ya Sh735.978 milioni, CAG amebaini vyama vitatu kati ya tisa vilivyokaguliwa, vina malipo yenye nyaraka pungufu kinyume cha miongozo ya kiuhasibu pamoja na kanuni Na. 86 (1) na kanuni na. 95 (4) ya Kanuni za fedha za Umma za mwaka 2001 ambazo zinaelekeza kila malipo yawe yameambatanishwa na nyaraka sahihi.

Kutokana na upungufu aliobaini, vyama vya CCM na Chadema vimepewa hati zenye shaka huku Chama cha Wakulima (AFP), ADC, Demokrasia Makini, Chama cha Kijamii, NLD, Sauti ya Umma na TLP vikipata hati mbaya.

Marekani Kuishambulia Tena Syria

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa nchi yake imejipanga na iko tayari kuishambulia tena Syria kama itarudia kufanya mashambulizi ya silaha za kemikali.

Onyo hilo la Trump limekuja baada ya Marekani, Ufaransa na Uingereza kufanya mashambulizi katika maeneo matatu ya Syria ndani ya saa 12, kwa kufyatua makombora 100.

Marekani na washirika wake hao wanadai kuwa Syria ilifanya mashambulizi ya silaha za kemikali wiki iliyopita katika eneo la Douma na kusababisha vifo vya watu wasio na hatia, kinyume cha sheria za kimataifa.

Urusi ambao ni washirika wa Syria waliwasilisha hoja katika Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa ikitaka kitendo kilichofanywa na Marekani kulaaniwa vikali na umoja huo, ombi ambalo lilipingwa baada ya mjadala wa muda mrefu uliokuwa na maneno makali, kwa mujibu wa ripoti.

Balozi wa Urusi kwa Umoja wa Mataifa, Vassily Nebenzia alisoma nukuu ya maneno ya Rais Vladimir Putin kwa kutekeleza mashambulizi hayo bila kuzingatia sheria za umoja wa mataifa na bila kusubiri majibu ya shirika la upelelezi la umoja wa mataifa linaloshughulikia silaha za kemikali la OPCW.

Wajumbe wa OPCW wanatarajia kuzulu eneo la Douma wiki ijayo kufanya uchunguzi wa tuhuma za Syria kutumia silaha za kemikali.

Syria imekana kutumia silaha hizo na kueleza kuwa tukio hilo limefanywa na waasi kwa lengo la kuichonganisha serikali ya Syria na wananchi wake pamoja na jumuiya za umoja wa mataifa. Rais Bashar Al-Assad ameseam kuwa mashambulizi ya Marekani yanazidi kumuimarisha.

Rais Mpya Fatuma Karume Atangaza Mikakati yake TLS

$
0
0
Rais mpya wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), Fatma Karume aliyechaguliwa kwa kishindo wikendi hii, amesema katika kipindi chake atahakikisha anashughulikia zaidi suala la utawala wa sheria.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, muda mfupi baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo akipokea kijiti kutoka kwa Tundu Lissu, Fatma amesema kuwa moja kati ya suala linalolalamikiwa na wanachama wengi ni watu kushikiliwa mahabusu kwa muda mrefu bila kupelekwa mahakamani.

“Wanachama wetu wametaka tushughulikie suala la watu kushikiliwa kwa miaka mingi bila kupelekwa mahakamani. DPP anasema bado upelelezi haujakamilika. Sasa wanataka watu wasiendelee kushikiliwa kama upelelezi bado haujakamilika au wafikishwe mahakamani,” alisema.

Akizungumzia tathmini yake kwa mtangulizi wake, alisema alifanya kazi nzuri katika kipindi kifupi alichokuwa ofisini lakini pia hata baada ya kupata matatizo makamu wake aliendelea kufanya kazi nzuri pia.
 
Fatma ameahidi kutumia nafasi hiyo kuhuisha utawala wa sheria nchini na kuepuka baadhi ya viongozi kufanya kazi kwa kufuata matamko kinyume cha matakwa ya katiba.

Mwanasiasa huyo alipigiwa kura 820 akimuacha kwa mbali Ngwilimi aliyemfuatia akipata kura 363, Mwapongo kura 12 na Wasonga akipata kura 6 kati ya kura 1,195 zilizopigwa na kuhesabiwa. Kipindi chake cha urais kitakamilika baada ya mwaka mmoja.

Mama Atiwa Mbaroni Kwa Kumuua Mtoto Wake Kisa Kala Chakula cha Mdogo wake

$
0
0
Polisi wamemkamata mwanamke wa kijiji cha Sokoni wilayani Tarime, kwa kumuua mtoto wake wa miaka minane kwa kumpiga na mwiko.

Kamanda wa polisi Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe alisema tukio hilo lilitokea Machi 25 .

Mwaibambe alisema chanzo ni baada ya mtoto Debora Jomo kula chakula ambacho mama yake alikiandaa kwa ajili ya kula mdogo wake ambaye ni mgonjwa.

Alisema mtoto huyo alifariki dunia Machi 26 saa 11:00 asubuhi kutokana na kutopelekwa hospitalini.

‘’Inasikitisha sana kuona mama anaua mtoto wake tena wa kumzaa mwenyewe, mtoto alitoka shuleni akakuta chakula alikuwa na njaa na alijua aliachiwa akala,” alisema.

Naye diwani wa Sirari, Paul Nyangoko aliwataka wazazi kuangalia adhabu za kuwapa watoto kwa kuwa vipigo vikali vinaathiri afya ya mtoto na kumsabaibishia kifo.

Alisema kwenye kata yake hakuna njaa na debe la mahindi linauzwa kwa Sh7,000.

ACT Wazalendo wabaini maeneo nane hatari katika ripoti ya CAG.....Watoa mapendekezo yao

$
0
0
Leo Jumapili Aprili 15, 2018 Chama cha ACT Wazalendo kimetoa tathmini na uchambuzi wake juu ya ripoti  mpya ya Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2016/17.

==>Soma taarifa hiyo iliyotolewa leo Aprili 15, 2018 na Kiongozi wa ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini, Mhe. Zitto Kabwe.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, CAG, Prof. Mussa Assad ametoa taarifa yake ya ukaguzi wa mapato na matumizi ya fedha za umma kwa mwaka 2016/17. Kwa sasa taarifa hiyo iko wazi kwa umma, baada ya kuwa imekabidhiwa rasmi bungeni. Sisi ACT Wazalendo, tumeisoma, kuipitia na kuichambua taarifa husika, kwa lengo la kuitumia ili itusaidie kutimiza wajibu wetu wa kuisimamia Serikali, kama chama cha Upinzani bungeni.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndugu Magufuli tayari amechukua hatua za kiuwajibikaji dhidi ya baadhi ya Watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa zenye hati isiyoridhisha, hatua hii ni ya njema, ACT Wazalendo tunampongeza kwa jambo hilo. Hata hivyo, baada ya kuipitia ripoti husika, tumegundua kuwa CAG ameibua masuala mazito ambayo yana madhara makubwa kwenye mfumo mzima wa Bajeti ya Nchi kama hayatashughulikiwa. Tumewaita hapa kuyazungumzia hayo.

Maeneo 8 ya Hatari Katika Ripoti ya CAG.

1. Mawaziri Wanavunja Sheria ya Ukaguzi. Tunaomba kutoa angalizo na muongozo wa kisheria juu ya hadaa inayofanywa na Serikali juu ya kinachoitwa “Majibu ya Mawaziri juu ya Ripoti ya CAG”. Kisheria Mikutano hii ya Mawaziri na wanahabari inayoendelea ni kinyume na Sheria ya Ukaguzi ya Umma, kifungu cha 38(1) na (2), ambacho kinaelekeza waziwazi kuwa Maafisa Masuuli ndio wanapaswa kujibu hoja za ukaguzi zilizoibuliwa na CAG, tena majibu husika hupaswa kuletwa mbele ya Kamati za Bunge za PAC na LAAC. Kwa utaratibu wa kawaida wa kiwizara, maafisa masuuli ni Makatibu Wakuu wa Wizara na si Mawaziri.

2. 6% ya Fedha zilizokusanywa na Serikali hazijulikani zilizokwenda. Katika ukaguzi wa Bajeti ya mwaka 2016/17, ambayo ni Bajeti ya kwanza ya Serikali ya awamu ya tano, CAG ameonyesha kuwa kati ya Bajeti ya shilingi 29.5 trilioni iliyoidhinishwa na Bunge, Serikali iliweza kukusanya shilingi 25.3 trilioni tu kutoka vyanzo vyote vya kodi, vyanzo visivyo vya kodi, mikopo ya ndani na nje, na misaada ya wahisani na washirika wa maendeleo. Serikali ilishindwa kukusanya kiasi cha shilingi 4.2 trilioni, sawa na 15% ya Bajeti yote ya mwaka 2016/17. Jambo la kushtusha na linalohitaji majibu ya Serikali ni kwamba, CAG amegundua kuwa katika fedha zote zilizokusanywa, shilingi 25.3 trilioni, ni shilingi 23.8 trilioni tu ndio zilitolewa kwa ajili ya mishahara ya watumishi, matumizi mengine, matumizi ya maendeleo na kulipa madeni yatokanayo na amana za serikali na riba, shilingi 1.5 trilioni zilizobaki hazijulikani zimekwenda wapi. Fedha hii ambayo matumizi yake hayajulikani ni sawa na 6% ya Fedha zote zilizokusanywa mwaka huo. Matrilioni haya ambayo Serikali imeyapoteza ni zaidi ya mara mbili ya Bajeti ya Wizara ya Maji ya mwaka husika (672 bilioni).

3. Bajeti ya Tanzania haina Hadhi (Credibility) tena. Taarifa ya CAG inaonyesha kuwa Bajeti inayopitishwa na Bunge haina Hadhi (Credibility) tena, kwani kuna matumizi makubwa ya nje ya Bajeti kinyume na ilivyoidhinishwa na Bunge. Kwa mfano, CAG ameonyesha kuwa Bunge lilitoa Kibali kwa Serikali kukopa mikopo ya ndani yenye thamani ya TZS 5.4 trilioni lakini Serikali ilikopa zaidi ya kiwango kilichoidhinishwa kwa 10%, ambapo zilikopwa shilingi 5.9 trilioni, yaani bilioni 500 zaidi ya ukomo wa kukopa uliotolewa na Bunge. Haya ni matusi makubwa kwa Bunge, yanaondoa hadhi ya bajeti inayopotishwa na Bunge.

4. Heshima na Hadhi ya Bunge letu vinaondolewa. Kazi Kuu ya Bunge ni kuidhinisha Bajeti inayoletwa bungeni na Serikali, mara baada ya mjadala. Kwa sasa heshima na hadhi ya Bunge vinaondolewa kutokana na Bajeti iliyopitishwa kutokutekelezwa, hasa kwa kiasi cha fedha zilizoidhinishwa na bunge kwaajili ya miradi ya Maendeleo kutokutolewa. Taarifa ya CAG imeonyesha kuwa, kwa ujumla, ni 68% tu ya Bajeti ya Maendeleo ndio ilitekelezwa, hali ni mbaya zaidi kwa upande wa Serikali za Mitaa, ambapo ni 51% tu ndiyo ilitekelezwa.

5. Mabilioni ya Fedha za Watanzania yametumika kulipa Madeni ambayo hayakuidhinishwa na Bunge. Taarifa ya CAG imeonyesha pia kuwa Serikali ilitumia zaidi ya shilingi 219 bilioni, kulipa madeni ya nyuma. Lakini matumizi hayo hayakuwa sehemu ya Bajeti iliyoletwa na Serikali na kuidhinishwa na Bunge. Hivyo madeni hayo ni hewa, na ulipwaji wake ni matumizi nje ya Bajeti iliyopitishwa na Bunge.

6. TRA Wametoa Takwimu za Uongo za Mapato ya Kodi ya zaidi ya shilingi 2.2 trilioni. Taarifa ya CAG imeonyesha, kwa mwaka wa fedha wa 2016/17, Mamlaka ya Mapato nchini, TRA ilituhadaa kwa kutangaza kuwa imekusanya fedha zaidi kuliko uhalisia wake. Kati ya kiasi cha shilingi 15.1 trilioni ambazo TRA ilitutangazia kuwa imezikusanya kwa mwaka 2016/17, shilingi 2.2 trilioni hazikuwa za TRA. Kimsingi fedha hizo si makusanyo ya kodi, bali TRA walizikusanya tu kama wakala wa asasi, taasisi na wakala nyengine za Serikali. Makusanyo halisi ya fedha za kodi yalikuwa ni shilingi 12.9 trilioni tu. Uongo huu wa TRA kutangaza hata mapato yasiyo yake umepelekea kutokea kwa shilingi 325 bilioni ambazo zilihesabiwa mara mbili (double accounting) kwenye Hesabu Jumuifu za Taifa, na hivyo kuchafua hesabu za Taifa na kuondoa uhalali wake kitakwimu. Pia taarifa ya CAG imeonyesha kuwa TRA hudanganya makusanyo wanayotangaza kila miezi mitatu.

7. Serikali kwa ujumla imepata Hati Chafu. Taarifa ya CAG ya Ukaguzi wa kwanza wa makusanyo na matumizi ya kibajeti ya Serikali ya awamu ya tano, imeonyesha kuwa, kwa ujumla, Serikali ya Jamhuri ya Muungano imepata Hati Chafu, kwa kuwa Hesabu Jumuifu za Taifa (consolidated accounts) zimepata Hati ISIYORIDHISHA (Chafu). Sababu za kutolewa Hati hii kwenye taarifa ya CAG ni pamoja na fedha kutumika kinyume na mafungu yaliyopangwa na Serikali yenyewe, kupotea kwa shilingi 1.5 trilioni, TRA kutangaza mapato ambayo si yake kuwa ni yake na hivyo kupelekea ‘double accounting‘ (kuhesabiwa mara mbili kwa fedha) kwenye mapato. Hesabu Jumuifu za Taifa ndio Hazina ya Taifa, kupata Hati Chafu ni hatari sana kwa mustakabali wa Taifa.

8. CAG hajakagua Ununuzi wa Ndege. Licha ya kuwa taarifa hii ya CAG ni taarifa bora sana kwa maudhui na uchambuzi, kuna mambo kadhaa ambayo CAG ameyaacha, ikiwemo Ununuzi wa Ndege za Shirika la Ndege Nchini, ATCL ambao kwa sehemu umefanyika mwaka wa fedha 2016/17.

Mapendekezo: Baada ya kusoma taarifa hiyo ya CAG na kuyaanisha maeneo hayo 8, sisi ACT Wazalendo tuna mapendekezo yafuatayo:

1. Tunawaomba Wenyeviti wa Kamati za Bunge za PAC na LAAC kufikisha suala Mawaziri kuzungumza kwenye vyombo vya habari kujibu ripoti ya CAG kwa Spika wa Bunge, ili Spika amjulishe Waziri Mkuu juu uvunjifu huu wa sheria unaofanywa na Mawaziri wa Serikali ya Awamu ya Tano, wakiwemo Mawaziri wazoefu wa taratibu za kibunge kama Waziri William Lukuvi na Waziri Harrison Mwakyembe. Mawaziri hawa wanafanya ‘spinning’ (hadaa) ili kuficha madudu ambayo CAG ameyaibua. Tunawaasa waache jambo hili, na wafuate sheria.

2. Tunaisihi Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, PAC kuomba kibali cha kukutana haraka na kuagiza Ukaguzi Maalumu wa shilingi 1.5 trilioni ambazo zimepotea na Serikali ya Awamu ya Tano imeshindwa kuzitolea maelezo kutoka kwenye makusanyo ya mwaka 2016/17. Hii ni mara ya kwanza kwenye historia ya nchi yetu kwa Serikali kukusanya fedha, kutozigawa kwenye Wizara, Idara, Wakala na Mikoa, kutoonekana matumizi yake na CAG kushindwa kuzikagua. PAC itimize wajibu wake haraka iwezekavyo. Wakati huu ukaguzi huu unafanyika, kama ilivyofanyika kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa waliopata Hati Isiyoridhisha, Rais amsimamishe kazi Katibu Mkuu Hazina na Mlipaji Mkuu wa Serikali, kwa kushindwa kusimamia vema Fedha za Umma na kupelekea Hesabu Jumuifu za Taifa (consolidated accounts ) kupata Hati isiyoridhisha ili kupisha uchunguzi huu.

3. Tunalishauri Bunge litake maelezo ya kina ya Serikali kuhusu kukopa bilioni 500 zaidi ya Serikali yenyewe ilivyoomba na kuidhinishiwa na Bunge. Ni matarajio yetu kuwa Bunge litachukua hatua dhidi ya Serikali kwa kukiuka Sheria ya Bajeti ambayo inakataza kabisa Serikali kukopa zaidi ya kiwango kilichoidhinishwa na Bunge. CAG ameonya katika Taarifa yake kwa kusema yafuatayo kuhusu jambo hili “sehemu kubwa ya mtaji wa mabenki unakuwa umefungwa kwenye fedha walizokopesha serikali kwa muda mfupi na muda mrefu; na matokeo yake, riba ya kukopesha kwa watu binafsi inakuwa kubwa na gharama za maisha zinakuwa juu”. Ukopaji wa namna hii unafanya UCHUMI KUSINYAA kwani unaondoa fedha kwenye mzunguko na kushusha uzalishaji.

4. Tunalishauri Bunge liiwajibishe Serikali kwa kutoheshimu Bajeti ambayo Bunge lilipitisha. Bunge linapaswa kulinda hadhi na heshima yake kwa kuhakikisha fedha za maendeleo linazozipitisha zinapelekwa kama ilivyopangwa. Bunge lisipofanya hivyo litaendelea kudharaulika. Spika wa Bunge asimame imara kulinda Mhimili wa Bunge dhidi ya uvunjifu wa sheria wa Serikali kwenye masuala ya Fedha za Umma, hasa wakati huu ambao CAG ameonyesha Fedha nyingi zimetumika kinyume na utaratibu huku fedha za maendeleo zilipitishwa na Bunge zikiwa hazipelekwi.

5. Ni imani yetu kuwa Bunge litawawajibisha wote waliohusika katika malipo ya madeni ambayo hayakuidhinishwa na Bunge letu. Madeni haya pia yanapaswa kujulikana ni yepi kwani CAG anaonyesha kuwa Wizara ya Ujenzi ndiyo imelipa zaidi madeni ya namna hii ambayo hayakuwa kwenye bajeti. Utaratibu wa namna hii ukiachwa bila kuchukua hatua, utatoa mwanya wa fedha za umma kupotea tu bila maelezo yoyote.

6.TRA kwa makusudi, na kwa lengo la kufanya hadaa walitangaza kiwango kikubwa zaidi cha makusanyo kuliko kiwango ilichopaswa kutangaza kuwa imekusanya. Tunatarajia kuwa Bunge litaitaka TRA iombe radhi Watanzania kwa upotoshaji huo ilioufanya na kutaka wote waliohusika kwenye hadaa hii wawajibike. Pia tunawasihi TRA kuzingatia weledi wa kazi yao kwa kutangaza makusanyo yao tu, na kuacha fedha za taasisi na asasi nyengine kama VETA, TPA, Bodi ya Mikopo nk (ambazo TRA huzikusanya kama Wakala wa taasisi hizo) zitangazwe na wahusika wenyewe.

7. Tunaishari Serikali kurejesha utaratibu wa kupanga matumizi ya kila mwezi ya fedha za umma kwa Hazina, na kuacha utaratibu wa sasa wa Ikulu kupanga matumizi ya kila mwezi. Utaratibu huu wa sasa unamuexpose (unamweka kwenye mazingira hatari) Rais, hasa kutuhumiwa kwa ufisadi na kukiuka sheria iwapo kuna makosa ya upotevu wa fedha kama haya ambayo CAG ameyaibua katika taarifa yake na kupelekea hesabu jumuishi za Serikali kupewa Hati Chafu. Tunashauri pia kuachwa kwa mfumo wa Rais wetu kutamka kugawa Fedha kinyume kabisa na Bajeti iliyopitishwa na Bunge.

8. Ni matarajio yetu kuwa katika ripoti ya mwakani ya CAG, Taifa litapata wasaa wa kuona ukaguzi wa ununuzi wa ndege za shirika la ndege la Taifa, ATCL na ukaguzi wa manunuzi ya kandarasi ya ujenzi wa kiwanja cha ndege cha Chato. Ni muhimu sana kwa CAG kuona mambo yanayosemwa na umma na kuchukua hatua za ukaguzi kwani yeye ndiye mlinzi wa fedha za umma.

Hitimisho
ACT Wazalendo tunawasihi Wabunge wote bila kujali vyama vyao kutekeleza wajibu wao wa kuisimamia Serikali. Wabunge tusipotekeleza wajibu wake nchi yetu itaangushwa na matumizi mabovu ya nje ya Bajeti na ya kinyume cha sheria. Ni dhahiri, kwa dalili hizi zilizoonyeshwa na taarifa ya CAG, kuwa Wabunge tusipoisimamia na kuidhibiti Serikali ya awamu ya tano, Nchi itafilisika kutokana na maamuzi ya hovyo, yasiyo ya kibajeti, yanayoenda kinyume na kanuni za kifedha na kiuchumi, na yasiyozingatia sheria za Nchi yetu.

Sisi ACT Wazalendo tutaendelea kuichambua taarifa hii ili kuibua masuala zaidi. Haya tuliyoyaeleza leo ni machache sana, hatujagusia kabisa mapungufu kwenye deni la Taifa, kulinganisha na mambo mengi ambayo CAG ameeleza. Tunawahimiza Wabunge na Wananchi kwa ujumla kusoma taarifa ya CAG kwa ukamilifu. Taarifa ya mwaka huu ina hoja nzito kuliko wakati mwingine wowote ule. Haijawahi kupata kutokea Serikali ya Nchi kulidgarau Bunge letu kama ilivyo kwa kiwango kilichoonyeshwa na taarifa ya mwaka huu ya CAG.

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume

$
0
0
Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni Sado 3 Mix Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

Sado 4 Mix; Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI DR. ULIMWENGU BINGWA Anapatikana dar magomeni moroco hotel
SIMU NO; 0759 030343 / 0622790494

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kongwa afariki dunia baada ya gari lake kuangukiwa na lori la mafuta

$
0
0
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kongwa, Izengo Ngusa, amefariki asubuhi ya leo Aprili 15 kwenye ajali ya gari,

Taarifa zilizotufikia zinasema gari dogo alilopanda Mkurugenzi huyo, lenye namba za usajili T619 DMA aina ya Toyota Crown Athlete, liliangukiwa na lori lililobeba mafuta,

Ajali hiyo imetokea eneo la Mbande Makaravati mkoani Dodoma.

Mange Kimamhi Akerwa na Kitendo cha Mdogo wake kwenda kwq RC Makonda

$
0
0
Kufuatia mdogo wake Mange Kimambi kufika Ofisini kwa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kwa ajili ya kusuluhisha mgogoro wake wa kutelekeza mtoto Mange amesema kuwa hajafurahishwa na kitendo hicho.

Amesema kuwa amechukizwa na kitendo hicho cha mdogo wake kufika ofisini kwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda, ambapo ameandika kwenye ukurasa wake Instagram ataifufua kesi ya mirathi iliyoamuliwa mwaka 2016.

Aidha, katika hatua nyingine Mange ameituhumu familia yake kwa kuuza machimbo ya urithi ya kokoto kwa bei ndogo yaliyopo Tegeta jijini Dar es salaam bila kupewa taarifa wala kutumiwa mgao wake.

“Nilikuwa tayari niishi vibaya ila nyinyi muishi vizuri ndio maana sikuwasumbua na mali za baba yetu, Mgao wangu wa machimbo ya kokoto mliyouza muanze kunitafutia. Mlidhani sijui? Kweli mnadhani sijapewa habari za nyinyi kuuza machimbo yetu ya kokoto? Nilikuwa najua Ila niliamuwa kukaa kimya sababu nawapenda na bila nyinyi kwenye maisha yangu nahisigi siwezi kuishi ila labda nahitaji kujifunza kuishi bila nyinyi,”ameandika Mange kwenye ukurasa wake wa Instagram

Hata hivyo, amesema kuwa mpaka sasa hajachukua chake kwani hadi leo ni miaka 12 sasa imepita tangu jaji awagawanye mali za urithi
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images