Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wanafunzi Arusha watumbukia shimoni na Kufariki Dunia

$
0
0
Wanafunzi wawili wakazi wa Olkeryan jijini Arusha wamefariki dunia baada ya kutumbukia kwenye shimo lililokuwa likitumika kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya mchepuko inayotoka Ngaramtoni kuelekea Moshono.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo jana  Jumatano Aprili 11, 2018 aliwataja wanafunzi hao kuwa ni Hadija Hans aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la pili Shule ya Msingi Olkeryan na Christina Kivuyo mwanafunzi wa darasa la tano Shule ya Msingi Mt Meru.

Mkumbo alisema Hadija alikuwa akipita karibu na  shimo hilo hilo Jumanne  saa 11;30 jioni na kutumbukia na kwamba Kivuyo alipokwenda kwa nia ya kumsaidia naye  alitumbukia katika shimo hilo na wote kufariki dunia.

Amesema baada ya tukio hilo wafanyakazi wanaojenga barabara hiyo kwa kushirikiana na wananchi na polisi walienda eneo la tukio na kukuta miili ya wanafunzi hao, ambayo waliipeleka Hospitali ya Mt Meru.

Aunty Ezekiel Awataka Wasanii Wenzake Waache Kumlilia Kanumba

$
0
0
Muigizaji wa Bongo movie Aunty Ezekiel amefunguka na kuwaasa wasanii wenzake wa Bongo movie waache kumlilia msanii mwenzao Steven Kanumba na badala yake waenzi kazi zake.

Steven Kanumba alikuwa msanii wa Bongo movie ambaye alikuwa ni mfano wa kuigwa na kila msanii kwani uwezo wake wa kuigiza na ubunifu uliweza kwa kiasi kikubwa kuifikisha tasnia hiyo mbali.

Ikiwa zimepita siku kadhaa tangu tasnia hii ikumbuke siku ya kifo chake ambayo inaitwa Kanumba Day, Aunty Ezekiel amefunguka na kusema sasa kuomboleza kifo chake tu kumetosha.

Kwenye mahojiano aliyofanya na gazeti la Ijumaa, Aunty Ezekiel amesema kuwa  mara nyingi wasanii wanapoadhimisha kumbukumbu ya kifo chake, wanakuwa wanalia au wengine wanasononeka mara kwa mara hiyo inakuwa inazidi kurudisha tasnia nyuma badala yake wasanii wakaze buti waweze kufika alipokuwa amefika yeye.

"Najua wazi uchungu upo lakini inabidi tuache sasa kulia badala yake tujitahidi kufikia pale alipotuacha ili tuzidi kusonga mbele maana tukisema kulia kila siku hatuwezi kufika tunapotaka hata siku moja”.

Lowassa agoma kupimwa DNA

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema hamtambui mwanamke aliyejitambulisha juzi kama binti yake aliyetelekezwa na kwamba hatapoteza muda kwenda kupimwa vinasaba (DNA), kama msichana huyo alivyotaka.

Kwa mujibu wa mazungumzo na Gazeti la Nipashe, Lowassa ambaye kwa sasa ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), alisema kuwa kinachofanyika kwenye zoezi hilo ni siasa.

Msichana huyo aliyejitambulisha kwa jina la Fatuma alijitokeza hadharani juzi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kudai kutelekezwa na Lowassa ambaye alisema ni baba yake, kwa kuambiwa na mama yake mzazi.

"Wewe unamwamini kweli huyo msichana? Angekuwa mwanangu kweli ningeshamchukua muda mrefu, kwanza wala simjui naona siasa zinaingizwa hapo," alisema.

Alipoulizwa kama yuko tayari kupimwa DNA ili ukweli ujulikane, Lowassa alijibu "Kupima DNA huo ni upuuzi. Yaani nipoteze muda wangu kwenda kufanya upuuzi huo? Siko tayari."

Msichana huyo ni miongoni mwa mamia ya wanawake waliojitokeza kuanzia Jumatatu kuitikia wito wa Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda.

Makonda alitaka wanawake waliotelekezewa watoto na waume zao wafike ofisini kwake kwa siku tatu kuanzia Jumatatu, kwa ajili ya kuzungumza na wanasheria, maofisa wa ustawi wa jamii na askari polisi wa Dawati la Jinsia. Siku hizo zitaisha kesho baada ya kuongezwa.

Akizungumza na vyombo vya habari juzi, Fatuma alisema yuko tayari kupima vinasaba na Lowassa ili kuthibitisha kama kweli ni baba yake na kwamba alimtafuta kwa muda mrefu bila mafanikio.

"Nilipeleka barua Ikulu kuomba kuonana na baba (Lowassa) kipindi akiwa Waziri Mkuu (2006-2008) lakini niliitwa mimi na mama katika klabu ya Mamba iliyopo Kinondoni," alisema Fatuma.

"(Hapo) alikuja mwanaume akiwa kwenye gari lenye vioo vyeusi akatuhoji mimi na mama, akaondoka hakutupa majibu yoyote hadi leo."

Kuhusu madai hayo, Lowassa alisisitiza kuwa kama kweli angekuwa mtoto wake asingesita kumchukua.

"Wala simjui, anasema ameshindwa kuniona wakati ana miaka 31, wewe unaamini kweli ameshindwa kuniona? Mbona wewe umenitafuta na umenipata na unaongea na mimi kwenye simu," alisema Lowassa.

"Hizo ni siasa zinazolenga kuchafuana."

Pia katika maelezo yake, Fatuma alidai kuwa aliwahi kukutana na mtoto wa Lowassa aitwaye Fred na alimwahidi kumsaidia lakini hadi sasa amekuwa kimya.

Magufuli Asema Bila Uimara wa Kikwete Asingekuwa Rais

$
0
0
Rais John Magufuli amekumbushia jinsi ambavyo msimamo na uimara wa rais mstaafu, Jakaya Kikwete ulivyomuwezesha kuingia Ikulu mwaka 2015.

Akizungumza jana Ikulu jijini Dar es Salaam katika hafla ya ufunguzi wa taasisi ya Jakaya Kikwete, Rais Magufuli alisema kuwa hataacha kumshukuru kila wakati wanapokutana bila kujali.

“Kwako Kikwete napenda kukuahidi kuwa nitaendelea kukushukuru kila tutakapokutana, ukichukia, ukifurahi mimi nitakushukuru kwa sababu wewe ndiye uliyesimama imara mpaka leo hii mimi ni Rais,” alisema rais Magufuli.

Aidha, alitambua mchango wa Kikwete katika kuleta maendeleo ikiwa ni pamoja na ubora wa miundombinu uliofanyika wakati wa akiwa rais. 

Alisema rais huyo mstaafu katika awamu yake alifanya mengi ikiwa ni pamoja na kujenga shule za kata, barabara na hospitali.

Alipongeza pia uanzishwaji wa taasisi ya Jakaya Kikwete ambayo imejikita katika masuala ya afya, vijana na utawala bora. 

Rais Magufuli aliahidi kuwa serikali yake itaiunga mkono taasisi hiyo kwani ina tija katika sekta zote inazohusika nazo.

Akizungumzia taasisi yake, Kikwete alisema kuwa pamoja na mambo mengine, imelenga kuwasaidia vijana kuwapa mafunzo ili wawe na elimu, wazalendo na wenye maadili mema wakitumia akili na nguvu zao kujiletea maendeleo.

Shirika la Ndege nchini(ATCL) limeondolewa katika mfumo wa malipo wa Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga(IATA) kutokana na madeni

$
0
0
Shirika la Ndege nchini ATCL limeondolewa katika mfumo wa malipo wa Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga IATA kutokana na kukabiliwa na madeni na sasa limetiliana saini ya makubaliano ya miaka mitano na Kampuni ya Ndege ya HAHN Air kuuza tiketi za Air Tanzania.

Akizungumza na wanahabari huko Zanzibar, Mkurugenzi wa ATCL Mhandisi Ladislaus Ernest Matindi, amesema wamelazimika kuingia kwenye makubalianao na kampuni hiyo ili wasikose baadhi ya huduma za malipo ya tiketi.

"Tuna madeni, sikumbuki yalifikia kiasi gani lakini ni madeni makubwa ambayo yalilazimisha kusimamishwa uanachama au kufungiwa huduma hizi mpaka tutakapokuwa tumelipa hayo madeni.

"Kubwa zaidi ilikuwa ni sisi kuwa katika mfumo wa shirikisho wa mashirika ya ndege dunia IATA ambayo ndo mfumo wa uuzaji na utawanyaji wa Tiketi. Maana mabadilishano ya pesa au kupeleka pesa kutoka shirika moja kwenda lingine hufanyika kwa kutumia huo mfumo wa IATA. Hii tunaanza kufanya ni kupitia kwakweli mgongoni kwa mtu.

"Hawa ni wanachama ambao wamepewa leseni ya kutoa huduma kwa mashirika ambayo hayapo kwenye mfumo wa IATA. Lazima tulipe madeni yetu tuliyonayo AITA ni mabilioni 'ni pesa nyingi kwa kweli' ili tuweze kurudi kwanza kwenye mfumo wa kukusanya pesa" Amesema Mhandisi Ladislaus Ernest Matindi. 

==>>Msikilize Hapo Chini

Waziri: ''TFF haipo juu ya Serikali....Tunawajibu wa Kuisimamia"

$
0
0
Serikali kupitia kwa Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo  Juliana Shonza imesema Shirikisho la soka nchini TFF limesajiliwa chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano hivyo shughuli zake zote zipo chini ya serikali.

Mh. Shonza ameyasema hayo jana wakati akjibu swali la mbunge wa Singida Mjini Mussa Ramashani Sima ambaye alihoji kuhusu mamlaka ya Waziri katika kusimamia kazi za TFF ikiwemo mapato na matumizi ya shirikisho hilo kutokana na katiba ya TFF kutoruhusu kuingiliwa na serikali.

''TFF pamoja na viongozi wake wote, wanapaswa wanalazimika na hivyo wanatambua mamlaka ya Waziri, kwasababu katiba ya TFF inatambua kuwa TFF ni chombo cha mpira ambacho kimesajiliwa chini ya sheria ya Baraza la Michezo ya 1967 na marekebisho yake ya mwaka 1971'', alisema Shonza.

Aidha Mbunge Mussa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa Singida amemuomba Waziri kuhakikisha wanaibana TFF ili ipeleka mpango kazi kwenye vyama vya mikoa ili kujua matumizi ya pesa za ruzuku zinazotolewa kwa shirikisho hilo.

Urusi Yaapa Kuyatungua Makombora ya Marekani Iwapo Itaishambulia Syria....Trump Awabeza, Asisitiza Lazima Yapigwe

$
0
0
Baada ya balozi wa Urusi huko Lebanon kusema kuwa majeshi ya Russia yatatungua makombora yoyote yatakayo lenga Syria, Rais wa Marekani Donald Trump amesema Jumatano kuwa Russia iwe tayari, “ kwani makombora hayo yatapigwa nchini Syria,”

“Hamtakiwi kuwa washirika wa Mnyama Anaeuwa kwa kutumia Gesi ya sumu wananchi wake wenyewe na anafurahia!” Trump amesema hayo katika ujumbe wa Twitter wakati Washington ikiendelea kupima namna ya kulishughulikia madai ya shambulizi hilo la silaha za kemikali.

Urusi imesema makombora ya Marekani yanatakiwa kuwalenga “magaidi” na sio “serikali halali” ya Syria.

Msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov pia amesema Jumatano kuwa pande zote zinazohusika katika mgogoro wa Syria wanatakiwa kujizuilia na vitendo ambavyo vitalisambaratisha eneo hilo.

Saa kadhaa baadae, Jeshi la Urusi lilisema kuwa litayaweka majeshi yake huko Douma, eneo ambako shambulizi la kemikali linashukiwa kutokea Jumamosi ambalo liliuwa watu wasiopungua 40. Urusi imesema majeshi yake yataendelea kuhakikisha usalama wa mji huo.

Syria imeeleza tishio la Marekani kwamba itashambulia kwa makombora kuwa ni “shinikizo la kivita lisilo na maana,” shirika la habari la serikali ya Syria limesema.

Umoja wa Mataifa na washirika wake kadhaa wameelekeza lawama kwa majeshi ya Syria kuwa yanahusika na mauaji hayo, wakati Syria na Urusi  wamekanusha kuwa majeshi ya Rais Bashar al-Assad yalihusika na shambulizi hilo la kemikali.

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Jim Mattis amesema kuwa Marekani bado inafanya tathmini ya kintelijensia juu ya shambulizi hilo lililotokea Syria. “Tunakaa tayari kuchukua hatua za kijeshi mbalimbali iwapo zitakuwa zinaafikiana na maamuzi ya rais,” amesema Jumatano.

Deni matibabu India lamshtua CAG.....Aitahadharisha Serikali Kuendelea Kukopa

$
0
0
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad, ameishauri serikali kufuatilia kwa makini kupaa kwa deni la matibabu ughaibuni.

Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kuwasilisha bungeni mjini hapa ripoti yake ya ukaguzi ya mwaka 2016/17, Prof Assad alisema ukaguzi wake kuhusu gharama za matibabu ughaibuni ulibaini ongezeko kubwa la deni kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika hospitali za India.

Alisema deni hilo limepanda kutoka kiasi cha Sh. bilioni 28.6 kilichoripotiwa Juni 30, 2017 hadi Sh. bilioni Sh. 45.73 kufikia Desemba 31, 2017 licha ya serikali kuweka masharti kwa wananchi kwenda kutibiwa kwenye hospitali za nje ya nchi.

“Ongezeko hili ni asilimia 60.71 kwa kipindi kifupi, ni jambo linalohitaji serikali kulifuatilia kwa makini ili kupunguza mzigo wamadeni na kuhakikisha kuwa hospitali husika zinalipwa kwa wakati,” alisema.

Kuhusu Deni la Taifa, Prof. Assad alisema limeongezeka kwa Sh. trilioni 5.04 katika kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Juni 2016 hadi Juni 2017.

Alibainisha kuwa hadi kufikia Juni 30, 2017, deni hilo lilikuwa Sh. trilioni 46.08 likipanda kutoka Sh. trilioni 41.03 lilivyokuwa Juni2016, ikiwa ni ongezeko la Sh. trilioni 5.04 (asilimia 12).

Alisema kuwa kati yake, deni la ndani ni Sh. trilioni 13.33 na deni la nje ni Sh. trilioni 32.75.

Prof. Assad alisema kiasi cha Sh. trilioni 4.58 hakikujumuishwa katika Deni la Taifa kutokana na kutojumuishwa kwa madeni ya mifuko ya pensheni pamoja na dhamana ambazo masharti yake yalikiukwa.

CAG Assad alibainisha vigezo vitatu vinavyotumika kupima uhimilivu wa Deni la Taifa akibainisha kuwa uwezo wa nchi kulipa riba ya deni ulikuwa umefikia karibu mwisho, lakini mwaka huu wametumia kigezo cha GDP kulingana na deni hilo.

”Kwa kutizama kigezo hicho, tumesema ni himilivu, lakini kama nilivyosema siyo busara kutizama kipengele hicho na kusema tunaweza kukopa kwa sababu tulishawahi kukopa tukapunguziwa mkopo,” alisema.

”Kwa hiyo, mimi rai yangu ni lazima tuwe waangalifu katika ukopaji wetu. Deni la Taifa linapimwa kwa namna nyingi, na zipo namna tatu kubwa; ya kwanza ni ile ya kuangalia deni kulinganisha na Pato la Taifa, lakini pia ujue kwamba unachotakiwa kufanya ni kuangalia malipo ya mbele ulinganishe na thamani ya fedha ya sasa.

”IMF na Benki ya Dunia (WB) kazi yao ni hiyo kuangalia data (takwimu) za kila nchi. Njia ya pili ni kuangalia mapato ya nchi dhidi ya Deni la Taifa. Kwa mfano, tunakusanya kiasi gani cha kodi? Hili ni eneo ambalo ni ‘sensitive’ zaidi, ile ya mwanzo ni kiunzi cha chini sana ndo maana unaweza kukuta nchi ina asilimia 200 kwa sababu ni kiunzi cha chini sana.

”Njia ya tatu ni kuangalia Deni la Taifa dhidi ya ‘export’ kwa sababu sehemu kubwa ya Deni la Taifa utailipa kwa fedha za nje.”Alisema mwaka huu kwa kulinganisha Deni la Taifa na GDP, deni hilo linamilika, lakini lazima nchi ambayo iliwahi kupewa nafuu ya mkopo, isikimbilie kukopakopa.

”Hatuwezi kusema tutakopa tutakopa, tutakopa kwa tahadhari kubwa kwa sababu hatutaki kurudi miaka 20 iliyopita sehemu ambayo tunataka tupewe msamaha wa madeni,” alisema.


Mmiliki Wa Mabasi Ya HBS Na Sabena Ajiua Kwa Kujipiga Risasi

$
0
0
Mmiliki wa kampuni mbili za mabasi za HBS Express na Sabena, Sultan Ahmed maarufu kama Chapa, amejiua kwa kujipiga risasi mdomoni iliyotokea kisogoni nyumbani kwake Sikonge mkoani Tabora jana.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Wilbrod Mutafungwa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo jana mkoani humo.

Kamanda Mutafungwa alisema tukio hilo lilitokea jana saa 2:30 asubuhi nyumbani kwa marehemu na kwamba chanzo cha kujiua kwake huko hakijafahamika.

"Bado tunachunguza tukio hili, amejipiga risasi mdomoni, tunachunguza chanzo cha tukio hili," alisema Kamanda Mutafungwa.

Kamanda Mutafungwa alisema marehemu Chapa pia alikuwa akimiliki kituo cha mafuta ya petroli wilayani Sikonge.

Chapa anakuwa mfanyabiashara wa pili nchini kujiua kwa kujipiga risasi katika kipindi cha mwaka mmoja baada ya Festo Msalia, muuza vinywaji kwa bei ya jumla mkoani Dodoma, kujilipua Machi mwaka jana.

Msalia alijiua kwa kujipiga risasi kichwani baada ya kukamatwa na shehena kubwa ya viroba.

Aliyekuwa Kamanda wa polisi mkoani humo wakati huo, Lazaro Mambosasa alisema marehemu aliondoka nyumbani kwake kwa kutumia gari aina ya Toyota Prado na kwenda kujipiga risasi katika eneo la Veyula, nje kidogo ya mji wa Dodoma.

Mfanyabiashara hiyo alikamatwa na shehena ya viroba Machi 3, mwaka jana.

Spika wa Bunge aogopa kuvamiwa, aweka utaratibu Mpya wa Kuingia Bungeni

$
0
0
Spika wa Bunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ametangaza rasmi utaratibu mpya wa kuingia bungeni utakaotumiwa na Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge wakati wanapokuwa wanaingia na msafara na kudai utaratibu huo unaweza kuwasaidia kiusalama zaidi. 

Spika Ndugai ametoa kauli hiyo mapema leo asubuhi wakati alipowasili Bungeni kwenye kikao cha nane, mkutano 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupitia mlango wa nyuma karibu na kiti chake ambacho anakikalia pindi anavyokuwa anaendesha shughuli za Bunge tofauti na ule mpangilio uliokuwa umezoeleka kuonekana kila uchao wa kupita kati kati ya Wabunge wote Bungeni.

"Utaratibu huu unafaida nyingi, wakati mwingine mnaweza mkawa na hasira tunapopita hapa katikati mkaturukia", amesema Ndugai
 
Spika Ndugai amesema ingawa haimo kwenye kanuni, lakini mabadiliko hayo yanafanyika ili kuendana na nchi nyingine zilizoendelea.

Aidha, Spika Ndugai amesema mlango mkuu wa kuingia Bungeni watautumia kupita endapo kutakuwa na ugeni wa kitaifa kama vile Rais na kufunga au kufungua Bunge na sio vinginevyo.

Leo ni Kumbukumbu ya Kifo cha Edward Moringe Sokoine.......Tazama Hapa Alichokiandika Rais Magufuli

$
0
0
Ikiwa leo ni Kumbukumbu ya Kifo cha aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Edward Moringe Sokoine aliyefariki dunia Aprili 12, 1984 kwa ajali ya gari, eneo la Dakawa nje Kidogo ya Mji wa Morogoro, Rais Dkt. John Magufuli amefunguka na kueleza alivyomfahamu kiongozi huyo enzi za uhai wake na mchango wake katika Taifa letu.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Magufuli amesema;

“Katika siku kama ya leo tarehe 12 Aprili 1984 nikiwa Mpwapwa JKT nikitumikia jeshi langu “Oparesheni Nguvukazi” tukatangaziwa kifo cha marehemu Edward Moringe Sokoine, ilikuwa siku ya majonzi shujaa huyu niliyemjua na kumshabikia ikawa siku yake ya mwisho.

“Wakati tunapoazimisha siku kama hii ya kifo chake, watanzania tuige mfano wake kwani alikuwa msema kweli, asiyeogopa, mpiga vita rushwa,ufisadi, unyonyaji,mzalendo wa kweli na aliyechukia rasilimali za watanzania kuibwa.

“Marehem Sokoine hatasahaulika katika historia ya Tanzania, ni wito wangu kwa watanzania tumuige na kumuishi. Ni rai yangu pia tumuenzi kwa kujenga umoja wetu , kupiga vita rushwa na kuchapa kazi . Mungu aiweke roho ya marehemu Edward Moringe Sokoine mahala pema peponi,” amesema Magufuli.

Mbunge aihoji serikali nafasi ya Zanzibar katika Jumuiya za Kimataifa

$
0
0
Naibu wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa,Dkt. Susan Kolimba amesema kuwa serikali imekua ikihakikisha serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inashiriki kikamilifu masuala yote ya Kimataifa.

Kolimba ameyasema hayo leo Bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swala la Mbunge wa Wingwi, Juma Kombo Hamad aliyehoji; "Je, Zanzibar ina nafasi gani katika Jumuiya za Kimataifa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?"

“Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na mabadiliko yake masuala ya mambo ya nje yapo chini ya mamlaka ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

"Serikali imekua ikihakikisha serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inashiriki kikamilifu masuala yote ya Kimataifa masuala hayo ni pamoja na ziara za viongozi na mashirika mbalimbali za Kimataifa zinazofanyika hapa nchini, ziara zinazofanywa na viongozi wa Kitaifa kwenye nchi mbalimbali , mikutano ya mashirika na Taasisi za Kimataifa na kikanda na mikutano ya pande mbili na Zanzibar kuwa mwenyeji wa mikutano ya Kimataifa,” amesema Dkt. Kolimba.

“Aidha viongozi mbalimbali wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wamekuwa wakiongoza ujumbe wa nchi kwenye mikutano mbalimbali ya Kimataifa kwa mfano kwa mwaka 2017/018 serikali ya mapinduzi ya Zanzibar imeshiriki katika mikutano ipatayo 11 ya mashirika na Taasisi mbalimbali za Kimataifa.”

Waziri asema hakuna upendeleo uteuzi wa mabalozi

$
0
0
Tanzania ina mabalozi 40 duniani kote na kati ya hao, wanaotoka Zanzibar wako tisa, sawa na asilimia 22.5 ya mabalozi wote nchini.

Hayo yameelezwa leo Aprili 12 bungeni na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Suzan Kolimba.

Dk Kolimba amesema uteuzi wa mabalozi hufanywa kwa weledi mkubwa kwa kuangalia uwezo wa mtu.

Alikuwa akijibu maswali ya nyongeza ya Mbunge wa Baraza la Wawakilishi (CCM), Jaku Hashim Ayoub aliyetaka  kujua Tanzania ina mabalozi wangapi wanaotoka Zanzibar huku mbunge wa Viti Maalum kutoka Zanzibar (Chadema) Mariam Msabaha akihoji kwa nini mabalozi kutoka Zanzibar wanapelekwa nchi za Uarabuni pekee.

Lakini Serikali ilikanusha madai kuwa mabalozi wanaoteuliwa kuwakilisha Tanzania wakitokea Zanzibar, wanapelekwa Uarabuni tu.

Dk Kolimba amesema hakuna upendeleo wa aina yoyote katika kuwapanga mabalozi bali kinachotazamwa ni namna ambavyo mhusika atasaidia kujenga mahusiano mema na mataifa husika.

Spika Ndugai amtaka Bashe kuachana na umaarufu wa Mitandaoni na Badala Yake Afuate Kanuni za Bunge

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amewatahadharisha wabunge wanaokusudia kupeleka hoja binafsi kuacha kutafuta umaarufu mitandaoni badala yake wafuate kanuni za bunge.

Ndugai ameyasema hayo leo Aprili 12 na kumtaja mbunge wa Nzega mjini, Hussein Bashe kuwa ni mfano wa wabunge hao ambao hutoa taarifa ya kusudio la kupeleka hoja binafsi lakini ghafla wanaanza kutangaza hoja zao mitandaoni.

"Wabunge wengine nawashauri mfuate kanuni na mfano ni Bashe, mnataka umaarufu tu wakati mnatakiwa kufanya lobbying (ushawishi) kwanza ili hoja zenu ziungwe mkono." amesema Ndugai.

Spika aagiza mwandishi Pascal Mayalla na Wahariri wa gazeti la Raia Mwema wahojiwe kwa kulidhalilisha Bunge

$
0
0
Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge, inatarajia kuwahoji mwanahabari Paschal Mayallah na wahariri wa gazeti la kila wiki, la Raia Mwema kwa madai ya kuchapisha habari inayodhalilisha bunge, Aprili 9 wiki hii.

Hayo yameelezwa leo Aprili 12 bungeni na Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyesema kuwa habari iliyochapishwa Aprili 9 ilidhamiria kuchafua hadhi ya bunge.

Hayo yamekuja baada ya mbunge wa Ulanga (CCM), Goodluck Mlinga kuomba mwongozo wa Spika juzi Aprili 9, akihoji iwapo habari iliyoandikwa na gazeti hilo yenye kichwa cha habari “Bunge linajipendekeza?” haidhalilishi bunge.

Spika Ndugai leo Aprili 12, ameliambia bunge kuwa mwandishi huyo na wahariri watatakiwa kuhojiwa na kamati hiyo ya bunge.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

Tiba ya Fangasi Sugu, Vidonda vya Tumbo, Kuondoa Chunusi na Nguvu za Kiume

$
0
0
MAKANGA 3 POWER: Hutibu nguvu za kiume dakika 10 na kupona  ndani ya siku 3. Huimarisha misuli ya uume iliyolegea, pia ipo dawa ya kurefusha uume mfupi nchi 4 handi nchi 7

Tuna tiba ya kudumu ya kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kuopata choo vizuri, busha( bila opareshen)

Pia tunatibu  kisukari, presha, muguu kuuma, fangasi sugu, vidonda vya tumbo, kupunguza unene, maziwa, kuondoa chunusi pete na cheni za bahati.

Onana na Dr. Shilindes shida zako zote zitakwisha.

Tupo Mbagala Rangi tatu:  0784460348  au 0659103360

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images