Rais Jakaya Mrisho
Kikwete alipotembelea Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa
ya Fahamu (MOI) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jana (Jumamosi)
kuwajulia hali wanahabari wawili – Ndugu Salum Mkambala wa Channel Ten
(juu) na (chini) Ndugu Margaret Chambiri wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
(NEC). (picha: Freddy Maro/IKULU).
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Gazeti la Mwananchi
Taarifa ya IKULU kuhusu habari ya "Rais Kikwete kumtembelea mfungwa, Rajab Maranda hospitalini" iliyochapishwa na gazeti la Mwananchi jana
↧
↧
Mwanaume avuliwa nguo na kuvishwa kanga na kisha kutembezwa mtaani baada ya kufumaniwa na mke wa mtu....
Jamaa aliyejitambulisha kwa jina la Salum Athuman (22), amejikuta
akivishwa kanga na kutembezwa mitaani baada ya kwenda nyumbani kwa
mwanaume mwenzake, Dastun Mkereti (26) kwa lengo la kujivinjari na mke
wa mtu, Stela Ramadhan (20), akafumaniwa.
Tukio hilo lililofunga mitaa lilijiri maeneo ya Temeke, Dar, hivi karibuni na kugeuka sinema ya bure.
Ilidaiwa kuwa jamaa huyo amekuwa
↧
Shakira asema boyfriend wake hataki ashikwe na mwanaume kwenye video, ndio chanzo cha kufanya na Rihanna
Mwanamuziki wa kike ambaye ‘hips’ zake hazidanganyi anapocheza,
Shakira ameeleza kuwa chanzo cha kufanya video na Rihanna aliyemshika
kama mwanaume ‘Can’t Remember to Forget You’, ni wivu alionao boyfriend
wake Gerard Pique.
Katika mahojiano aliyofanya na jarida la Billboard, Shakira ameeleza
kuwa mchezaji huyo wa Barcelona hataki kabisa ashikwe na mwanaume kwenye
video na kwamba ni
↧
Mkazi wa Tabora asimulia jinsi Metakelfin ilivyomgeuza kuwa Albino, Msikilize hapa akieleza ilivyokuwa
Hafidh Masokola mwenye umri wa miaka 47, mkaazi wa Tabora amedai
kuwa alitumia dawa aina ya Metakelfin miaka minne iliyopita kwa lengo la
kutibu ugonjwa wa malaria, lakini dawa hizo zilimsababishia madhara
makubwa katika ngozi yake na kumpelekea kuwa albino.
Akiongea na Sun Rise ya 100.5 Times Fm, Hafidh ambaye ni mjasiriamali
ameeleza kuwa alinunua dawa hizo ‘Pharmacy’ na kwamba
↧
Taarifa kutoka Mahakamani kuhusu ile kesi ya msanii AT na Mganga wa jadi ambaye amemshitaki msanii huyo baada ya kugoma kulipa malipo ya matibabu
Kesi ya madai iliyofunguliwa mwezi
uliopita na mganga wa jadi dhidi ya AT ambaye ni msanii wa muziki wa kizazi kipya,
leo ndo ilikua tarehe yake katika mahamaka ya mwanzo Buguruni...
Asubuhi
AT alifika mahakamani mapema na ilipofika zamu yake akaitwa na na
kusomewa shitaka na AT alikanusha...
Kesi imeahirishwa mpaka tarehe 04 April 2014, ambapo mdai ambaye ni mganga Dr sherif
↧
↧
Kwa nini Serikali mbili haziepukiki?? ...Uchumi wa Zanzibar unategemea Tanzania Bara
WAKATI Bunge Maalum la Katiba likisuasua katika kuunda kanuni za kuongoza wajumbe wake, taarifa zinaonesha katika muundo uliopo wa serikali mbili, mbali na kuimarisha umoja na mshikamano wa Taifa, pia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imekuwa ikinufaika nao kiuchumi.
Taarifa hizo za kiuchumi, zinaungana na taarifa za kisiasa na kijamii kusisitiza umuhimu wa muundo wa Muungano wa
↧
Afrika kusini yawatimua maofisa watatu wa ubalozi wa Rwanda nchini humo......Rwanda nayo yajibu mapigo kwa kuwafukuza maofisa 6 wa ubalozi wa Afrika Kusini
SERIKALI ya Rwanda, imefukuza maofisa sita wa ubalozi wa Afrika Kusini muda mfupi baada ya nchi hiyo kuwataka maofisa watatu ubalozi wa Rwada kuondoka Afrika Kusini.
Aidha, kutokana na hatua hizo, Afrika Kusini imeanza kuangalia uwezekano wa kuvunja uhusiano wa kidiplomasia na Rwanda, kutokana na mvutano wa siku za hivi karibuni kati ya nchi hizo mbili, uliosababisha kila upande
↧
Taarifa kwa vyombo vya habari juu ya Ajira kwa Walimu wapya kwa mwaka 2013 / 2014
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI JUU YA AJIRA KWA WALIMU WAPYA MWAKA 2013/14
Jumla ya Walimu wapya 36,021 ambao wamehitimu mwaka 2013 kutoka vyuo
mbalimbali hapa nchini wataajiriwa rasmi na Mamlaka za Serikali za Mitaa
(Halmashauri) ifikapo tarehe 01 Aprili 2014. Kati ya idadi hiyo walimu
wa ngazi ya Cheti (Daraja III A) ambao hufundisha katika shule za
Msingi ni 17,928 na walimu wa shule
↧
Askofu Kakobe ampelekea Rais Kikwete ujumbe wa wazi kutoka kwa Mungu....Bofya hapa uusome
↧
↧
Uzushi mitandao ya kijamiii nchini wamkera Edward Lowassa.....Ni baada ya watu kutengeneza noti ya sh. 500 yenye picha ya Lowassa
Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa amekerwa na tabia ya
baadhi ya watu wanaosambaza uzushi katika mitandao ya kijamii kwa
kutumia jina lake.
Lowassa alisema kuna watu wanaoendeleza kusambasa
picha ya noti ya Sh500 yenye picha yake huku wakiongeza maneno mabaya
juu yake.
Katika taarifa iliyotolewa na ofisi yake, Lowassa
alisema, “Kitendo hicho siyo utani, bali ni dhihaka
↧
CHADEMA wampitisha rasmi mgombea ubunge Chalinze atakaye kabiliana na Fabian Leonard ( CUF ) na Ridhiwani Kikwete ( CCM )
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),
kimempitisha Mathayo Torongey kuwa mgombea rasmi wa ubunge kwa tiketi ya
chama hicho katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze.
Akimtambulisha mgombea huyo kwa Waandishi wa
habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri wa
Chadema, John Mrema alisema Torongey alipitishwa juzi na Sekretariati ya
chama
↧
CCM yampa jeshi la ushindi Ridhiwani Kikwete......Kamati kuu yampitisha Rasmi, Kinana kufungua kampeni....Dr. Shein kuzifunga!
KAMATI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imemteua, Ridhiwani Kikwete, kuwa mgombea katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani, unaotarajiwa kufanyika Aprili 6, mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, uzinduzi wa kampeni za CCM utafanywa na Katibu Mkuu wa chama hicho Taifa, Abdulrahaman Kinana
↧
TFF Yaiomba Radhi Serikali kwa uharibifu wa vitu katika Uwanja wa taifa uliosababishwa na vurugu za watazamaji....Yasema itailipa Serikali hasara yote iliyopatikana
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) tunalaani vikali fujo na uhabirifu wa
mali unaofanywa na washabiki viwanjani wakati mechi mbalimbali zikiwemo
zile za kimataifa na ligi za hapa nchini.
Tunaiomba
radhi Serikali kwa uharibifu wa viti uliotokea kwenye mechi ya Ligi ya
Mabingwa Afrika kati ya Yanga ya Tanzania na Al Ahly ya Misri
iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
↧
↧
Mchungaji Christopher Mtikila Achafua Hali ya Hewa Bungeni
Mchungaji Christopher Mtikila amechafua hali ya hewa bungeni, kwa kumtaka Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Pandu Kificho
amueleze ni kwanini tangu jana amekuwa akimnyima nafasi ya kuzungumza
bungeni.
Mchungaji Mtikila alisimama ghafla na kusema: Mwenyekiti kwanini
unaninyima haki yangu ya kuzungumza, nataka kujua kwanini unaninyima
haki ya kuzungumza. Kuzungumza ni haki yangu.
↧
Mh. Samwel Sitta achukua fomu ya kugombea uenyekiti wa bunge la katiba
Mgombea
Uenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samuel Sitta akipokea Fomu kutoka
kwa Ofisa wa Bunge Bi. Lidya Mwaipyana. Katikati ni Mjumbe wa Bunge
Maalum la Katiba na Mbunge wa Nzega, Dk Hamisi Kigwangala.
Mhe. Sitta
akionesha fomu aliyochukua leo. Kushoto ni Mhe. Dk Kigwangala na kulia
ni Mjumbe wa Bunge hilo Bw. Paul Makonda. (picha zote: Hassan
Silayo/MAELEZO).
↧
Taswira mbalimbali kutoka Bunge la Katiba mjini Dodoma Leo
Wajumbe
wa Bunge Maalum la Katiba, William Lukuvi (kulia) akizungumza ,
Anna Abdallah (katikati) na Tundu Lisu wakizungumza , Bungeni Mjini
Dodoma Machi 11, 2014.
Wabunge wa Bunge Maalum la Katiba Kabwe Zitto na Ibrahim Lipumba wakiteta Bungeni Mjini Dodoma Machi 11, 2014.
Mwenyekiti
wa Muda wa Bunge Maalum la Katiba, Pandu Kificho akiongozwa kutoka
kwenye
↧
Mahakama yawaruhusu Basil Mramba na Daniel Yona kwenda kutibiwa nje ya nchi
MAHAKAMA
ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imewaruhusu kwenda
kutibiwa nje ya nchi Mawaziri Waandamizi wa zamani, Basil Mramba na
Daniel Yona wanaokabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na
kuisababishia Serikali hasara ya Sh. bilioni 11.7 kwa kutoa msamaha wa
kodi baada ya kusikiliza maombi yao leo.
Uamuzi
huo umetolewa leo mahakamani hapo na Jaji John
↧
↧
Samuel Sitta ateuliwa kuwa Mwenyekiti wa kudumu wa Bunge la katiba baada ya kupata ushindi wa kura 487
Samuel Sitta ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa kudumu wa Bunge la katiba
kwa kupata jumla ya kura 487 kati ya kura zote 563 zilizopigwa na
wawakilishi wa bunge hilo....
Miongoni
mwa changamoto alizoziahidi kuzishughulikia ni pamoja kulifanya bunge
hili kuwa bunge la viwango na kuahidi kutumia muda mfupi zaidi kwenye
bunge hili la Katiba sambamba na kuwashughulikia wanaotaka muungano
↧
Taarifa ya CUF: Zanzibar ilimtegemea nani kabla ya kuungana na Tanganyika?
THE CIVIC UNITED FRONT (CUF- Chama Cha Wananchi)
Office of the Secretary General
Party Headquarters,
P.O. Box 3637, Zanzibar, Tanzania
E - mail: cufhabari.co.uk
Homepage: www.cuftz.org
Our Ref:
CU/HQ/KR/HUM/181
Date: 11/03/2014
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Ukweli utaendelea kubaki ulimwenguni kwamba Zanzibar ni Nchi iliyokuwa
huru tangu asili na zama, ambayo ikitegemea
↧
Bodaboda, Bajaji na biashara holela zapigwa marufuku katikati ya jiji la Dar
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam Saidi Mecki Sadiki akizungumza na waandishi wa
habari leo jijini Dar es salaam kutoa agizo kwa viongozi na watendaji
wa jiji la Dar es salaam kuhakikisha kuwa wanawaondoa na kuwachukulia
hatua za kisheria wanaovunja sheria za jiji kwa kuendesha shughuli
mbalimbali katika maeneo yasiyoruhusiwa.
Kamanda
wa Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamishna (CP)
↧
More Pages to Explore .....