Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

VIDEO: Kauli ya Kwanza ya Freeman Mbowe Baada ya Kuachiwa kwa Dhamana

0
0
Mwenyekiti wa (CHADEMA) Mhe. Freeman Mbowe amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya kuachiwa huru yeye pamoja na viongozi wengine sita wa CHADEMA na kusema kuwa walipokuwa magerezani wameshuhudia mengi na watayaweka wazi karibuni.

Mbowe amesema hayo alipokuwa nje ya Mahakama ya Hakimu mzaki Kisutu baada ya kukamilisha masharti dhamana ambapo kila mmoja alitakiwa kuwa na wadhamini wawili pamoja na kusaini bondi ya shilling Million 20.

"Leo mahakama imetupa ruksa ya dhamana na tunaanza dhamana yetu siku ya leo kwa mashtaka ambayo yananikabili mimi na wenzangu, tumekuwa gerezani Segerea kwa siku saba mimi na wenzangu na tunamshukuru Mungu tuko salama mimi na wenzangu na tumewaona Watanzania wengi zaidi ya elfu mbili ndani ya gereza la Segerea ambao wengi wao haki yao imecheleweshwa

"Kwa hiyo tunasema ni haki iliyominywa, tutazungumza mengi tuliyoyaona Segerea na baadaye tutatoa taarifa rasmi ya chama kuhusiana na kesi hii" alisema Mbowe

==>Msikilize hapo chini

Mwigulu alitaka Jeshi la Polisi kuwa wakali

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amelitaka Jeshi la Polisi kuwa wakali kwa watu wanaofanya mzaha pindi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto ili kuweza kuokoa maisha ya watanzania yanayopotea kila kukicha kwenye ajali.

Waziri Mwigulu ametoa kauli hiyo leo katika Mkutano wa 11 wa kikao cha Bunge cha kwanza kinachoendelea kufanyika katika mkoa wa Dodoma wakati alipokuwa anajibu swali ya nyongeza la Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga aliyetaka kusikia tamko la serikali kuhusiana na faini zinazotozwa na askari wa barabarani pindi wanapowakamata madereva wa magari badala ya kuwapa elimu elekezi.

"Sisi kama Wizara ya Mambo ya Ndani na Jeshi la Polisi kutoza faini au kukusanya faini sio kipaumbele chetu ila kipaumbele chetu ni maisha ya watanzania. 

"Tunapobaini kuwepo uzembe mwingi barabarani ndipo tunapoamua kutoza faini kwa hiyo kama watanzania watazingatia na kuwa waangalifu kwamba wamebeba dhamana kubwa ya maisha ya wenzao katika vyombo vyao moto hili suala la faini litakuwa limeisha", amesema Waziri Mwigulu.

Pamoja na hayo, Waziri Mwigulu ameendelea kwa kusema "Nitoe rai kwa Jeshi la Polisi kuendelea kuwa wakali pindi watu wanapofanya mzaha, huku wakiwa wamebeba abiria ili kuokoa maisha yanayotokana na ajali nyingi zinazotokea barabarani, na jambo hili ninalo lisemea ni kwa vyombo vya moto vyote kuanzia magari ya abiria na binafsi pamoja na bodaboda. 

"Nalisisitiza hili kwasababu tumeshuhudia vifo vikiwa vimetokea pindi tunapoenda katika eneo la tukio unakuta gari limekwisha andikiwa faini kutokana na kutembea mwendokasi".

Kwa upande mwingine, Waziri Mwigulu amesema ajali za barabarani zimepungua kwa asilimia 43 hadi kufikia Disemba 2017 ambapo katika kipindi cha mwaka 2016 jumla ya ajali 9,856 zilizosababisha vifo 3,256 na majeruhi 2,128 na mwaka 2017 ajali 5,310 ambazo zilisababisha vifo 2,533 na majeruhi 5,355 wakati kipindi cha Januari hadi Februari mwaka 2018 zimetokea ajali 769 zilizosababisha vifo 334 na majeruhi 698 ambapo katika kipindi hicho wahanga 1583 wakilipwa fidia takribani Bilioni  7 kutoka makampuni mbalimbali ya bima.

Rais Magufuli Aagiza changamoto za Kuunganishiwa umeme Zimalizwe

0
0
Rais John Magufuli ameiagiza Wizara ya Nishati na Wakala wa Umeme Vijijini (Rea) kuondoa changamoto za kawaunganishia nishati hiyo wananchi.

Pia, amewaagiza wakuu wa taasisi mbalimbali za umma kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuepuka gharama wanazoisababishia Serikali na kuchelewesha maendeleo kwa wananchi.

Hayo ameyasema leo Jumatatu Aprili 3, 2018 wakati akizindua kituo cha kufua umeme cha Kinyerezi II 240MV CCPP jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli amesema kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu gharama za kuunganishiwa umeme hivyo hatua za haraka zinahitajika kuchukuliwa.

"Wizara ya Nishati na Rea hakikisheni mnaongeza kasi ya kuunganishiwa umeme, yapo malalamiko machache machache ya wafanyakazi kuomba rushwa, yashughulikiwe hayo," amesema Rais Magufuli

Kuhusu malalamiko ya taasisi kucheleweshewa baadhi ya huduma amesema hilo linamkera na hataki kulisikia tena.

Amesema taasisi za Serikali zinatakiwa kufanya kazi kwa karibu hasa tunapotekeleza miradi mikubwa ya Taifa, tusicheleweshane.

"Mawaziri, wakurugenzi, wenyeviti wa bodi msiache kuwasiliana ninyi kwa ninyi, kama unaona unakwamishwa na taasisi nyingine, mambo kama haya nikisikia huwa yananiudhi, lugha ya mitaani yananiboa kweli kweli. Shirikianeni kwani mnawacheleweshea wananchi maendeleo," amesema Rais Magufuli.

Amesema kuwa umeme wa uhakika unachagiza kutekeleza Tanzania ya Viwanda kwani kwa sasa mahitaji ya nchi ni megawati karibu 1,40O lakini uzalishaji umefikia megawati 1515.3,"Bado tunahitaji umeme wa kutosha na tuongeze uzalishaji."

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Sakata la Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo Laibuka Bungeni

0
0
Mbunge CUF, Dkt. Suleiman Ally Yussuf amefunguka na kuhoji ni sababu zipi zilizopelekea mpaka Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo kuwekwa mahabusu ya Polisi kwa kipindi kirefu bila ya kufikishwa Mahakamani kusomewa mashtka

Dkt. Suleimani amehoji hayo leo (Aprili 3, 2018) katika Mkutano wa 11 wa kikao cha Bunge cha kwanza kinachoendelea kufanyika katika mkoa wa Dodoma wakati alipokuwa anauliza swali ya nyongeza kwenda kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ambapo alitaka kufahamu uhalali wa Jeshi la Polisi juu ya kuwashikilia watuhumiwa.

"Wako watu wengi wanaowekwa mahabusu ya Polisi kwa zaidi ya siku 15 bila ya kupelekwa Mahakamani akiwemo mwanafunzi Abdul Nondo. Nataka nijue ni sheria gani ambayo inatumika au inatumiwa na Jeshi la Polisi kuwaweka watu mahabusu ya Polisi zaidi ya muda huo mrefu bila ya kupelekwa Mahakamani", amehoji Dkt. Suleiman.

Aidha, katika kujibu hoja hiyo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema polisi ni chombo kilichoundwa kwa mujibu wa katiba na sheria na linatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba.

"Polisi wana mamlaka kisheria kutuhumu, kukamata, kuhoji na kuweka watuhumia mahabusu kwa muda ulioruhusiwa kisheria endapo itabainika kuwa kuna viashiria au taarifa ya kuhusika katika kutenda kosa la jinai. 

"Kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utendaji zinazoongoza Jeshi la polisi inapobainika askari amembambika kesi kwa sababu zozote zile huchukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu ikiwemeo kufukuzwa",amesema Waziri Mwigulu.

Pamoja na hayo, Waziri Mwigulu ameendelea kwa kusema "kwa kuwa jambo la kiusalama ni kipaumbele, kwa mtuhumiwa na rai wengine waliosalia, Jeshi la Polisi hutumia wajibu wake waliopewa wa kulinda usalama wa raia kwa kuweza kuhakikisha kwamba linatimiza majukumu yake na huku likiwaacha watu wakiwa salama kabisa".

Kwa upande mwingine, Waziri Mwigulu hakuweza kujibu suala lolote kuhusu Nondo kama jinsi lilivyo hojiwa na Mbunge Sulleiman juu ya uhalali wa Jeshi la Polisi kumuweka kijana huyo zaidi ya siku 15 mahabusu ya polisi.

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 75 na 76 )

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA-

ILIPOISHIA  

Nilipo hisi ninaweza kufa kwa kumwagiwa maji haya yenye nguvu, nikajigeuza na tumbu langu nikalielekezea kwenye ukuta, nikawaachia mgongo ambao wakaendelea kuushambulia kwa maji hayo nyenye nguvu hadi nikaishia wanguvu kabisa na kujikuta nikilala chini. Walipo niona nimelegea kabisa, wakanicha na kuufunga mlango wa chumba hichi cheye maji mengi na kunifanya nilale hapa chini huku machozi yakinimwagika na kujiuliza ni kitu gani kinacho endelea kwneye maisha yangu ya hivi sasa.

ENDELEA
Taratibu nikajinyanyua huku mwili wangu ukiwa umejawa na maumivu makli sana yaliyo tokana na kumwagiwa maji yenye nguvu. Nijajarubu kusimama ila mwili mzima ukakosa nguvu, sikuwa na jinsi zaidi ya kuendelea kukaa hapa chini. Haukupita muda mwingi, mlango ukafunguliwa wakaingia wasichana wanne ambao  ni tofauti kabisa na wale ambao walinimwagia maji. Wasichana hawa ambao miili yao imejengeka kwa misuli kama wanaume, wakanifwata na kuninyanyua, wakaanza kuniburuza
na kunitoa nje ya chumba hichi.

Wakanipitisha katika kordo ambayo ina vyumba vingi vya wafungwa na vina mageti ya vyuma. Karibia wafungwa wote ambao wapo ndani ya vyumba vyao waliendelea kunitazama kwa umakini huku wengi wao wakionekana kunikasirikia sana. Mlango wa chumba kimoja ukafunguliwa. Wakanisukumia ndani ya chumba hichi chenye hewa nzito sana. Nikaanguka  chini huku nikiwa nina hema sana. Nikastukia nikiwa nimeguswa mgongoni, taratibu nika na kumtazama aliye nishika. Nikakuta ni yule kijana wa kiharabu ambaye alinikaribisha katika kiti cha pembeni alicho kuwa amekikaa.
”Pole”
Alizungumza huku  akinitazama usoni mwangu, taratibu akanipa mkono wake, akaninyanyua huku akinitazama usoni mwangu. Taratibu akanisaidia kunikalisha kitandani, nikakitazama chumba hichi chenye vitanda viwili ambavyo vina vitanda vya juu na chini ambavyo vijajulikana kwa jina la double deka.

“Hivi hapa ni wapi?”
Niliuliza huku nikihema sana.
“Kusema kweli mimi bado sijaelewa hili eneo, mimi nilitekwa tu na kujikuta nikiwa humu ndani ya hili gereza”
“Una muda gani hadi kuwemo kwenye hili gereza?”
“Ni mwaka sasa, ni siku nyingi sana nimetekwa, sifahamu kama familia yangu ina hali gani?”
“Na kwenye hichi chumba unaishi na nani?”
“Tulikuwa watatu, ila wawili wamesha kufa kwenye yale mapambano kwenye ule ulingo. Yaani hili gereza kwa haraka haraka hii ni sehemu ya kifo, mtu anaingia ila hakuna ambaye anaweza kutoka”
Taratibu nikashusha pumzi huku nikiutazama mlango ulio tengenezwa na nondo. Kusema kweli nilisha ingia kwneye magereza kadhaa kama mtembezi, hata gereza nililo kuwa nimefungwa miezi kazaa iliyo pita lina nafuu tena kubwa sana, kwa maana nilifungiwa tu kwenye chumba kimoja ila hili lina mchanganyiko mkubwa wa watu wa kila aina na karibia asilimia tisini na tisa ya watu wa humu ndani ya hili gereza wana roho mbaya sana.

TANGA RAHA- Sehemu ya Arobaini na Saba ( 47 )

0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
Akaingia kwenye moja ya chumba na mimi nikaingia pasipo kubisha hodi, gafla macho yangu yakakutana na Regina akiwa mtupu kama alivyo zaliwa huku mwili wake ukiwa umejaa maji, akionekana kutoka kuoga, nikatazama kila kona ya chumba na sikumuona binti ambaye nilikuwa ninamfatilia, Regina hakuonekana kushangaa wala hukuficha sehemu zake za siri, zaidi akabaki akiwa ametabamu na kuanza kupiga hatua za kunifwata, gafla nikastukia mlango ukifunguliwa nyuma yangu na nilipo geuka nikakutana na Rahma akiwa anatushangaa

ENDELEA
*Eddy ndio unafanya nini hapo?”
Rahma alizungumza huku akinitazama kwa hasira,
“Kwani wifi wewe, unatuona tunafanya nini?”
Regna alimuuliza swali Rahma, ambalo likazidi kumkasirisha Rahma
“Koma wewe, sijazungumza na wewe, nimemuuliza mume wangu”
“Ndio unijibu sasa, umetukuta tumesimama unababaika, ungenikuta nimemuweka kifuani mwangu si ndio ungekufa”
Regna alizungumza kwa dharau wala sikujua ujasiri kama huu ameutolea wapi, Rahma akanipiga kikumbo, nikastukia akimvaa Regna na kumuangusha chini, na kuanza kupigana, nikabaki nikiwa ninashangaa, sikujua hata nifanye kitu gani, Regna akamgeuza Rahma na kumkalia tumboni mwake, na kuanza kumtandika vibao vya mashavu, Rahma naye hakubaki nyuma, akajikakamua hadi akafanikiwa kumuweka Regna chini ambaye yupo uchi, na kuanza kunzaba makofi ya hasira.Nikamkimbilia Rahma na kumuwahi mikono yake, na kumchomoa mikononi mwa Regna

“Rahma, tulia mke wangu, mbona unataka kuleta aibu kwa wageni waliofika hapa”
Nilizungumza huku nikiendelea kumshikilia Rahma kwa nguvu
“Niache nimkomeshe huyo malaya wako”
Rahma alizungumza huku akijikakamua kutoka mikononi mwangu
“Malaya mwenyewe, hivi unadhani utaweza kuwa peke yako, na ninakuambia ni lazima nimchukue huyo mume wako, kwanza mwanamke mwenyewe huna kizazi, unadhani mume wako ataendelea kukaa na mwanamke tasa kama wewe? Uyooooo”
Maneno ya Regna yalizidi kunishangaza kwa maana si kawaida ya mtu anaye jitambua kuzungumza mambo kama hayo

“Eddy niachie, nimfundishe adabu huyu malaya, hawezi kunvunjia adabu ndani ya nyumba yangu”
“Rahma tulia, ninakuomba utulie mke wangu”
“Unamtetea huyo malaya wako eheee, niache sasa”
Nikastukia Rahma akinipiga kisukusuku cha tumbo na kujikuta nikimuachia, akamvamia Regna na kumuangusha chini, kwa haraka nikafunga mlango, kuepuka watu wa nje kusikia kitu kinacho endelea ndani ya chumba.Rahma akazishika nywele nyingi za Regna na kuanza kukibamiza kichwe chake kwenye kwenye sakavu yetu ya kisasa, Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio baada ya kumuona damu zikiwa zinasambaa chini, zikitoea kwenye kichwa cha Regna.Kwa haraka nikavuta Rahma kwa nguvu zangu zote na kumzuia kuendelea kumpigiza Regna kichwa chake chini

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 4


Rais Magufuli amteua Mkemia Mkuu wa Serikali mpya

0
0
Rais John Magufuli amemteua Dk Fidelice Mafumiko  kuwa Mkemia Mkuu wa Serikali.

Uteuzi huo wa Dk Mafumiko umeanza  Jumanne Aprili 3, 2018.

Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu,  Gerson Msigwa imeeleza kuwa kabla ya uteuzi huo, Dk Mafumiko alikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW).

Dk Mafumiko anachukua nafasi ya Profesa Samuel Manyele ambaye amemaliza muda wake.

Spika Ndugai amerejea kutoka kwenye matibabu

0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amerejea jana Aprili 3, 2018 akitokea nchini India alikokwenda kwa ajili ya kupata matibabu miezi miwili.

Taarifa iliyotolewa katika ukurasa wa Twitter wa Bunge la Tanzania imesema “Spika Ndugai amepokelewa na Mbunge wa Viti Maalum, Mama Salma Kikwete na Wabunge wengine.”

Heche Ang’ang’aniwa Polisi....... Kufikishwa Mahakamani Leo

0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, linamshikilia Mbunge wa Tarime Vijini, John Heche (Chadema), kwa tuhuma za kushindwa kuripoti polisi kama alivyotakiwa na jeshi hilo.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amethibitishwa kushikiliwa kwa mbunge huyo tangu jana.

Mambosasa amesema Heche alikamatwa kwa kosa sawa na lile lililokuwa likimkabili Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, ambaye pia alishindwa kuripoti polisi wiki iliyopita baada ya kwenda Afrika Kusini kwa matibabu kabla ya kukamatwa Uwanja wa Ndega wa Dar es Salaam (JNIA), usiku wa kuamkia juzi.

Aidha, Mambosasa amesema endapo taratibu zitakamilika mbunge huyo anaweza kufikishwa mahakamani leo, kuunganishwa katika kesi ya viongozi wengine wa chama hicho waliopata dhamana jana.

“Ni kama alivyoshikiliwa mwenzake Mdee naye hakuripoti, walikuja wakatakiwa kurudi wote wao hawakurudi, hakuna kosa jipya kosa lake ni kutorudi hadi wenzake wanapelekwa mahakamani,” amesema Mambosasa.

Machi 27 mwaka huu Heche alishindwa kuripoti polisi pamoja na viongozi wengine saba wa chama hicho kama walivyotakiwa na jeshi hilo akidai alikuwa na msiba.

Viongozi hao ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu wa chama hicho, Vincent Mashinji, Naibu Katibu Mkuu Bara, John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko ambao wanakabiliwa na mashtaka manane yakiwamo kuhamasisha maandamano, uchochezi na uasi.

Wafuasi 27 Wa Chadema Washikiliwa Na Polisi kwa Kufanya Vurugu Mahakamani

0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, linawashikilia watu 27 wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Chadema kwa tuhuma za kufanya fujo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakati kesi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ikiendelea mahakamani hapo.

Kwa mujibu wa Kamanda Mambosasa wanaoshikiliwa ni wanaume 20 na wanawake saba, ambao walikamatwa katika eneo la Mahakama hiyo wakifanya fujo wakati wakisubiri uamuzi wa Mahakama hiyo juu ya hatima ya dhamana viongozi hao saba wa Chadema.

“Watu hao walikuwa wanafanya vurugu katika eneo la Mahakama wakati Mahakama inaendelea, tumewashikilia na tutawafikisha mahakamani tukikamilisha taratibu,” alisema Mambosasa.

Rais Magufuli Kuzindua Ukuta Katika Migodi ya Tanzanite

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi Ijumaa hii Aprili 06, 2018 kwenye uzinduzi wa ukuta kwenye migodi ya Mirerani mkoani Arusha.

Tarehe 30 Septemba mwaka jana, Rais Magufuli aliamuru kujengwa ukuta huo kuzunguka eneo la Mererani ili kulinda madini ya Tanzanite na kuiwezesha serikali kukusanya kodi kwa urahisi.

Kajala afunguka kuongeza mtoto wa pili na mipango ya mwanae

0
0
Msanii wa filamu Bongo, Kajala Masanja amesema hatarajii kabisa kuwa mwanae, Paula ataingia katika tasnia ya burudani nchini.

Muigizaji huyo ameiambia Planet Bongo ya EA Radio mwanae ana mpango wa kuwa mwanasheria na si nje ya hapo.

“Hivi vitu industry, sijui radio, muziki, movie hapana , hayupo interest kabisa yeye kila siku anaseama anataka kuwa mwanasheria, kwa hiyo tunasubiria amalize shule tuwe na mwanasheria mkali,” amesema.

Alipoulizwa kuhusu kuongeza mtoto wa pili, alijibu; “Mungu akijalia atotokea mwingine tu soon,”.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Mwanadada Kutoka Kenya Ajitolea Kumsaidia Wema kupata Mtoto.

0
0
Ni muda mrefu sasa umepita tangu mwanadada wema sepetu akiwa analalamika na kuonyesha kiu yake ya kupata mtoto , baadhi ya watu wamekuwa wakimuonea huruma na wengine kumsema na kumtukana lakini mwanadada huyo hajawahi kuacha kuonyesha kiu yake ya kutaka kupata mtoto.

Akiongea katika chaneli ya EATV,Wema anasema “kwakweli nimekuwa nikitamani kupata mtoto hata leo kwa muda sasa tangu nikiwa na miaka 24 hadi leo nina miaka 29”

Hata hivyo moja ya warembo kutoka kenya aliyekuwa akiishi dubai anaejulikana kwa jina la 2g diva, amejitolea kumsaidia wema kupata mtoto ili kuweza kutimiza ndoto zake za muda mrefu.

Katika moja ya video zilizovuja mtandaon zikimuonyesha dada huyo akiongea anasema kuwa ” wema sepetu darlin suluhisho tunalo, may be unaenda kuwa mama soon”

Repoa yatoa tahadhari kuhusu uchumi wa nchi

0
0
Taasisi ya Utafiti Repoa imetoa tahadhari ikisema licha ya juhudi zinazoendelea katika mageuzi ya kiuchumi, Serikali inapaswa kushughulikia vikwazo vilivyopo ili kukabiliana na ushindani wa masoko nje ya nchi.

Mkurugenzi mtendaji wa taasisi hiyo, Dk Donald Mmari alisema jana kuwa, pamoja na Serikali kushughulikia ukuaji wa uchumi kwa miaka 15 iliyopita, tafiti mbalimbali zinaonyesha viwango vya tija katika sekta nyingi ziko chini.

“Lakini pia hata ushindani wake ukilinganisha na nchi nyingine bado hauridhishi, Tanzania inao uwezo wa kujiweka katika nafasi kubwa zaidi kiuchumi duniani kutokana na upatikanaji wake katika jiografia, wingi wa rasilimali za asili, utulivu wa kisiasa na kijamii,”alisema.

Baadhi ya vikwazo alivyotaja katika mkutano wa waandishi wa habari ni pamoja na upatikanaji wa nguvu kazi yenye afya, ujuzi na elimu, miundombinu rafiki ya biashara na uwekezaji.

Wachumi kutoka taasisi mbalimbali, NGO, viongozi, wasomi, wahisani na watunga sera wametajwa kushiriki warsha itakayofanyika leo na kesho itakayojikita katika uzalishaji wenye tija na ushindani katika utandawazi.

Warsha hiyo itaongozwa na katibu mtendaji wa Shirikisho la Forodha la Kusini mwa Afrika (Sacu), Pauline Mbala huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.).

Masuala yatakayojadiliwa yatajikita kwenye mabadiliko ya mfumo wa uchumi hususan katika umuhimu wa kufahamu misingi ya uzalishaji wenye tija na ushindani katika utandawazi na masoko

Mtafiti mwandamizi katika taasisi hiyo, Dk Blandina Mlama alisema ni umuhimu pia kuwekeza katika mnyororo wa thamani kupitia sekta zinazoajiri Watanzania wengi.

Hotuba Ya Upinzani Yakwaa Kisiki Bungeni

0
0
Hotuba ya Kambi ya upinzani kuhusu bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu, haitasomwa bungeni baada ya kambi hiyo kuchelewa kuiwasilisha.

Hayo yameelezwa leo, Aprili 4 na Naibu Spika Dk Tulia Ackson dakika chache kabla ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, kusoma bajeti yake.

“Kwa maelekezo yaliyotolewa na Spika Ndugai, kwa kambi ya upinzani ni kuwa upinzani wanatakiwa kuwasilisha hotuba yao siku moja kabla ya bajeti kusomwa bungeni ili kuondokana na matatizo ya kuchelewa kuzipata hotuba hizo,” amesema Dk Ackson

Waziri Majaliwa leo anawasilisha bungeni mapitio na mwelekeo wa kazi za Serikali na makadirio ya mapato na matumizi ya fedha za ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge, kwa mwaka wa fedha 2018/2019 mjini Dodoma.

Mahakama Kutoa Maamuzi Kesi ya Wema Sepetu April 23

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Aprili 23, 2018 itatoa uamuzi kama Wema Sepetu  na wenzake wawili kama wana kesi ya kijibu au la.

Uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi watano wa upande wa mashtaka na kuufunga ushahidi wao.

Machi 23, 2018 upande wa utetezi uliwasilisha hoja katika Mahakama hiyo ili waone washtakiwa hao hawana kesi ya kujibu.

Mbali na Wema, wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ya kutumia dawa za kulevya ni Angelina Msigwa  na Matrida Seleman Abbas.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.
 
Inadaiwa  kuwa  Februari 4, 2017 katika makazi ya Wema huko Kunduchi Ununio  washtakiwa hao walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.

Wema anadaiwa kuwa Februani Mosi, 2017 katika  eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam, alitumia dawa za kulevya  aina ya bangi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images