Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Aunty Ezekiel Ajibu Tuhuma za Kuazima Nguo kwa Wema Sepetu

$
0
0
Mwanadada Aunty Ezekiel amefunguka na kujibu tuhuma zilizokuwa zikimkabili kuhusu tabia yake ya kuazima nguo kwa rafiki yake wa karibu Wema sepetu , tuhuma ambazo zimekuwa zikisambaa katika mitandao kila kukicha.

Aunty Ezekiel  amesema kuwa nguo wanayosema ameazima zilishonwa mbli na yeye ndiye  aliyekuwa wakwanza  kuvaa nguo hiyo lakini anashangaa sana watu wanapokuja na kumtuhumu kuhusu swala hilo.

Hata hivyo Aunty anasema kuwa bado kwao sio shida kuvaliana nguo kwa sababu ni marafiki hivyo ni swala la kawaida.

"Kwanza kuazima nguo sio shida kwetu kwa sababu ni rafiki yangu lakini cha ajabu ni kwamba nguo wanayoizungumzia wao zimefanana wala hakuna aliyenda kugonga hodi kwa mwenzake."-Alijibu Aunty

Wawili hao wamekuwa marafiki kwa muda mrefu sasa ingawa hapo katikati walikuwa wakionekana kutokuwa pamoja lakini sasa ivi mapenzi yamerudi na kuwa mapya kabisa.

Askofu anusurika Kukatwa mapanga kanisani

$
0
0
Askofu  Wilberforce Luwalira wa Kanisa la Roma la Mtakatifu Paulo, Namirembe nchini Uganda  alinusurika kifo baada ya Herbert Kadu (35), kuibuka ghafla kanisani akiwa ameshika panga na kumkimbilia nalo madhabahuni wakati ibada ya Pasaka ikiendelea.

 Tukio hilo la aina yake lilitokea juzi nchini Uganda wakati Askofu Luwalira akiendesha ibada ya Pasaka kanisani hapo.

Ujumbe wa video fupi uliosambaa jana kwenye mitandao ya kijamii unaonyesha ibada hiyo ikiendelea,  ghafla Kadu akiwa amebeba panga alianza kumkimbilia eneo la madhahabuni alikokuwa askofu huyo.

Kabla ya kumfikia askofu huyo, Kadu alijaribu kuruka kizingiti kilichotenganisha eneo la madhabahu na waumini na katika jitihada hizo alianguka na kukamatwa na wasimamizi na waumini ndani ya kanisa hilo.

Kijana huyo alijaribu kuruka kizingiti ili kwenda kwa askofu ambaye wakati huo alikuwa amesimama na msaidizi wake wakiendelea na ibada, na baada ya kuruka alidondoka upande wa madhahabu.

Wasaizidi wa askofu huyo walimdhibiti kijana huyo na kumbeba kumwondoa ndani ya kanisa hilo ili asitekeleze kusudio lake.

Taarifa zilizopatikana kanisani hapo zilisema kijana huyo aliwasili kanisani hapo akiendesha gari aina ya 'kipanya' Super Custom na kuegesha lango kuu la kuingilia kanisani hapo.

“Alipoingia alimpiga mlinzi wa getini na kuingia kwa nguvu kanisani na alikaa kanisani muda mrefu hadi ibada ilipokaribia kuisha ndipo alipojaribu kwenda madhabahuni,” shuhuda alisema katika video hiyo.

Taarifa ilisema baadaye askari walimkamata na kumpeleka kituo cha polisi Namirembe kwa mahojiano.

Habarika Masaa 24......Pakua Upya Application Yetu Tukuhabarishe Usiku na Mchana

$
0
0
==>Pakua Upya Application yetu tukuhabarishe masaa 24 usiku na mchana.

Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya Mpekuzi Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Maboresho Mapya Yamefanyika ili kukufanya upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile kuliko ilivyo sasa.

App ya zamani ilikuwa na tatizo kubwa la kuchelewa kufunguka, kuchelewesha habari na muonekano wake haukuwa wa kiwango kinachostahili.

Chakufanya, Ingia PlayStore, Download Upya Application yetu  MPYA. Ukishaipakua hii Mpya, ya zamani ifute tu.

NB: App mpya ina Icon ya Njano

Tumekurahisishia;

Hatima ya Akina Mbowe na Wenzake Kujulikana Leo

$
0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wengine watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, leo watafika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ukamilishaji wa masharti ya dhamana waliyopata mwishoni mwa wiki iliyopita.

Machi 27, Mbowe na wenzake walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na makosa nane, ombi lao la dhamana likaahirishwa uamuzi kwa siku mbili ili Hakimu akajiridhishe.

Alhamisi, Hakimu Wilbard Mashauri alikubali ombi la dhamana licha ya washitakiwa kutokuwepo mahakamani siku hiyo kutokana na gari la kuwatoa mahabusu ya Gereza la Segerea kuharibika.

Mbali na Mbowe (56), washitakiwa wengine ni Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (52), Mbunge wa Kibamba John Mnyika (37), Mbunge wa Musoma Mjini, Esther Matiko (41), Katibu Mkuu, Vincent Mashinji (45) na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu (39).

Hakimu Mashauri alisoma masharti ya dhamana kuwa ni washtakiwa kujidhamini kwa hati ya maneno ya Sh. milioni 20, wadhamini wawili kwa kila mshtakiwa wanaotoka taasisi zinazotambulika watakaosaini hati yenye thamani hiyo ya fedha.

Aidha, itakuwa ni mara ya kwanza kwa Mbowe na wenzake kukaa gerezani kwa siku saba.

Katika kesi ya msingi, ilidaiwa kuwa Februari 16, mwaka huu katika Barabara ya Kawawa eneo la Mkwajuni Wilaya ya Kinondoni, kwa pamoja washtakiwa na wenzao zaidi ya 12, walifanya mkusanyiko na kukaidi amri halali ya ofisa wa Jeshi la Polisi, Gerald Ngiichi na kusababisha kifo cha Akwilina Akwiline na askari polisi wawili Konstebo Fikiri na Koplo Rahim Msangi kujeruhiwa.

Shtaka la tatu, ilidaiwa katika siku ya tukio la kwanza katika viwanja vya Buibui vilivyopo Kinodnoni, Mbowe wakati akiwahutubia wakazi wa Kinondoni, alitamka maneno ya uchochezi kuwa "Ninapozungumza hapa kiongozi wetu wa kata ya Kinondoni Hananasif yupo mochwari... Amekamatwa na makada wa CCM kwa msaada wa vyombo vya ulinzi na usalama... Wamemnyonga, wamemwua halafu sisi tunaona ni jambo la kawaida... Tunacheka na polisi... Tunacheka na CCM", alinukuliwa kwamba alitoa maneno hayo ya kuleta chuki na uchochezi kwa Watanzania.

Pia shtaka la nne ambalo ni kosa la uchochezi na kusababisha chuki miongoni mwa jamii, Jamhuri imedai Februari 16, mwaka huu katika mkutano wa umma uliofanyika viwanja vya Buibui wilayani Kinondoni Dar es Salaam, Mbowe alifanya uchochezi na kusababisha chuki kinyume na sheria kwa kutamka yafuatayo:

"Tumejipa kibali cha kutangulia mbele ya haki... haiwezekani wanaume wazima na akili zetu na wake zetu na watoto wetu tukafanywa ndondocha.. hii ni nchi ya ajabu. Mimi leo nipo hapa kulinda taifa... kule Afrika Kusini Jacob Zuma amelazimishwa kujiuzulu... Robart Mugabe wa Zimbabwe kang'olewa, kang'olewa Waziri Mkuu wa Ethiopia... juzi ameondoka kwa people's power. Magufuli ni mwepesi kama karatasi".

Katika shtaka la tano la uchochezi wa uasi linalomkabili Mbowe peke yake, inadaiwa katika tarehe na maeneo hayo, alihutubia mkutano wa hadhara akiwa na nia ya kupandikiza chuki na dharau kwa Watanzania dhidi ya uongozi wa kisheria uliopo madarakani kwa kusema "Nitaongoza mapambano nchi hii kwasababu tumechoka kuuawa... matokeo ya Watanzania 100 watakaokufa wataleta haki katika taifa hili. Wangapi wapo tayari kuchukua bei hiyo?"

Katika shtaka la sita la uchochezi wa uasi, wakili Nchimbi aliendelea kudai, katika tarehe hiyo hiyo na maeneo hayo mkoani Dar es Salaam, Mbowe alitoa matamshi ya kupandikiza chuki na dharau kwa upande wa raia wa Tanzania dhidi ya mamlaka halali kuwa; "Hii nchi inadharaulika... imejengewa misingi wa uwoga, kwa lugha nyingine wanaume ni kama mademu, si unawaona hao wanavaa suruali, waoga, bure kabisa... juzi ametekwa kijana wetu, wanasema yupo mochuari, haki ya Mungu ingekuwa nchi nyingine Kinondoni ingekuwa majivu... Lissu amepigwa risasi machine gun na vyombo vya dola... Watanzania mnarudi nyuma... kuna mwandishi wa habari leo ana siku 86 amebebwa na vyombo vya dola... suluhu ya nchi hii haipo bungeni. Suluhu ya nchi hii ipo kwa wananchi wenyewe... lakini ili tupate suluhu hiyo... ni lazima tukubali kubeba majeneza... Inawezekana leo mnaogopa kufa... Ni bora tuwabebe wachache hata wakiwa 200 waliokufa katika ukombozi ili hatimaye nchi hii isimame kama nchi ya wanaume wengine katika dunia hii".

Katika shtaka la saba la kushawishi kutendeka kwa kosa la jinai , inadaiwa katika tarehe hiyo hiyo na maeneo hayo, Mbowe alishawishi wakazi wa Kinondoni kutenda kosa la kufanya maandamano na mkusanyiko usio halali.

Katika shtaka la nane la kushawishi utendaji wa kosa la jinai, linalomkabili mshtakiwa wa pili Msigwa, ilidaiwa katika maeneo hayo hayo Msigwa alishawishi raia na wakazi wa eneo hilo kutenda kosa la jinai kwa kutembea mbele ya umma wakiwa na silaha.

Maulid Mtulia , Dk Godwin Mollel Waapishwa Bungenii Leo

$
0
0
Naibu Spika, Tulia Ackson, leo amewaapisha wabunge wawili, Dk Godwin Mollel wa Siha na Maulid Mtulia wa Kinondoni, leo Aprili 3.

Wabunge hao wameapishwa baada ya kufanyika kwa uchaguzi mdogo katika majimbo ya Siha na Kinondoni,  baada ya wabunge wa maeneo hayo kuhamia CCM.

Mtulia, alikuwa mbunge wa Kinondoni (CUF), kabla ya kuhamia CCM na kugombea tena jimbo hilo kwa kupitia CCM.

 Kadhalika Mollel, alikuwa mbunge wa Siha, (Chadema) kabla ya kuhamia CCM na kugombea tena jimbo hilo kwa tiketi ya CCM.

Hata hivyo kiapo hicho hakikushuhudiwa na idadi kubwa ya wabunge wa upinzani ambao hawakuwepo katika kikao cha leo.

 Hili ni bunge la kumi na moja na mkutano wa kumi na moja.

Freeman Mbowe na wenzake Tayari Wako Mahakamani

$
0
0
Wanachama na viongozi wa Chadema wamekusanyika  ndani na nje ya viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kusubiri hatima ya dhamana ya viongozi wakuu wa chama hicho.

Viongozi hao, Mwenyekiti wa Taifa Freeman Mbowe na wenzake watano wanatarajiwa kuachiwa  kwa dhamana leo iwapo watatimiza masharti ya dhamana.

Masharti hayo ni  kusaini bondi ya Sh20milioni  kuwa na wadhamini wawili wenye barua kutoka ofisi za Serikali za mitaa au vijiji na kuripoti kituo kikuu cha Polisi kila Alhamisi.

Tayari Mbowe na wenzake wameshafikishwa mahakama ni tangu saa mbili asubuhi  na sasa wanasubiri shughuli za kimahakama zianze ili wakamilishe masharti ya dhamana.

Mbali ya Mbowe wengine ni Katibu Mkuu Dk  Vicent Mashinji, Manaibu Katibu wakuu John Mnyika (Bara), Salum Mwalimu (Zanzibar), Mbunge wa Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa  na Mweka Hazina wa Baraza la Wanawake wa chama hicho Ester Matiku wanakabiliwa na kesi ya jinai, wakidaiwa pamoja na mambo mengine ikiwamo kufanya  mikusanyiko na maandamano yasiyo halali.

Wamekuwa mahabusu tangu walipopandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka hayo Machi 27 mwaka huu, 2018.

LIVE: Rais Magufuli Anazindua Mtambo wa Kufua Umeme, Kinyerezi 2

$
0
0
LIVE: Rais Magufuli Anazindua Mtambo wa Kufua Umeme, Kinyerezi 2

Lowassa alivyofika Mahakamani katika kesi ya Mbowe na Viongoz Wengine CHADEMA

$
0
0
Viongozi sita wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  wameshafikishwa Mahakama ya Kisutu tangu saa mbili asubuhi.

Wanachama na viongozi wa Chadema wamekusanyika  ndani na nje ya viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kusubiri hatima ya dhamana ya viongozi hao

Viongozi hao, Mwenyekiti wa Taifa Freeman Mbowe na wenzake watano wanatarajiwa kuachiwa  kwa dhamana leo iwapo watatimiza masharti ya dhamana.

==>>Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa  tayari yuko mahakaman kufatilia kesi hiyo ya mwenyekiti wa chama chake


Ujenzi bwawa la umeme mto Rufiji kuanza Julai

$
0
0
Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani amesema kuwa hadi kufikia Julai mwaka huu, ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme katika mto Rufiji utakuwa umeanza.

Ameyasema hayo  leo Aprili 3, wakati wa hafla ya kuzindua kituo cha kufua umeme Kinyerezi awamu ya pili.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo ni Rais John Magufuli.

Dk Kalemani amesema mradi huo wa miaka mitatu utakamilika kwa wakati.

Amesema hatua inayoendelea sasa ni kutafuta mkandarasi ambaye hadi kufikia Julai atakuwa ameshapatikana kwa ajili ya kuanza kazi.

“Sasa tunamuandalia mazingira ili akipatikana aanze kazi bila kikwazo, tumemboreshea barabara na tumeshapeleka umeme,” amesema Dk Kalemani.

Akizungumzia suala la umeme wa uhakika, Dk Kalemani amesema hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu watakuwa wamekamilisha uimarishaji wa miundombinu.

“Umeme upo mwingi wa kutosha na wa ziada, kinachofanyika sasa ni kuboresha miundombinu hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu tutakuwa tumelikamilisha hilo na umeme kupatikana wakati wote na katika majira yoyote,” amesema Dk Kalemani.

Breaking News: Agnes Masogange Ahukumiwa kwenda jela miaka 3

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu video queen, Agnes Gerald ‘Masogange’ kulipa faini ya Shilingi Milioni 1.5 ama kwenda jela miaka 3 baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Kutokana na hukumu hiyo, Wakili wa utetezi Nehemiah Nkoko amesema kuwa watalipa faini.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri amesema kuwa katika ushahidi wa kesi hiyo upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi 3, huku utetezi ukiwa na shahidi 1.

Hakimu Mashauri amesema kuwa ameridhishwa pasina kuacha shaka juu ya ushahidi wa upande wa mashtaka hasa kwa uthibitisho uliotolewa na Mkemia Mkuu wa serikali kwamba mkojo wa mshtakiwa ulikutwa na chembe chembe za dawa za kulevya.

“Kutokana na kujiridhisha na ushahidi huo, namtia hatiani mshtakiwa kwa makosa hayo ya kutumia dawa za kulevya,”-Hakimu Mashauri

Baada ya Masogange kutoa utetezi wake, Hakimu Mashauri amesema kuwa ameusikia utetezi wa mshtakiwa kwamba apewe adhabu ndogo, huku upande wa mashtaka ukitaka apewe adhabu kali.

“Nimesikiliza maelezo ya pande zote, katika kosa la kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin namuhukumu mshtakiwa kulipa faini ya Sh.Mil 1 ama jela miaka 2.

” Katika kosa la pili la kutumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam, nakuhukumh kulipa faini ya Sh.Laki 5 ama jela miezi 12,”  amesema Hakimu Mashauri.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

PICHA: Halima Mdee Alivyofikishwa Mahakamani Leo

$
0
0
Mbunge wa Kawe Halima Mdee leo April 3, 2018 amefikiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi, ameomba kufanya marekebisho ya hati ya mashtaka ili kumuunganisha Mbunge huyo.

 Mdee alikamatwa juzi katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere(JNIA) akitokea Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa.

 Awali, viongozi sita wa Chadema, akiwamo Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, walisomewa mashtaka manane, yakiwamo ya uchochezi na kuhamasisha maandamano.

Lakini Mdee hakujumuishwa katika hati hiyo ya mashtaka  na hivyo Wakili Nchimbi ameiomba leo Aprili 3, kumuunganisha Mdee katika kesi hiyo.

Viongozi hao walitakiwa kuwa huru kwa dhamana tangu Machi 29 lakini wakaendelea kubaki mahabusu   baada ya kushindwa kusaini bondi ya Sh20 milioni.

Machi 29,  Hakimu Wilbard   Mashauri aliamuru kuwa viongozi hao wafikishwe mahakamani leo na kusaini bondi hiyo ndipo suala la rufaa lifanyiwe kazi. 



==>Usisahau ku install App yetu upate habari zetu kwa wepes zaid << Bofya hapa>>

UPDTES: Mbowe na Viongozi wengine CHADEMA Wametimiza Masharti ya Dhamana.....Halima Mdee Kasomewa Mashitaka Mawili

$
0
0
Viongozi 6  wa Chadema wakiongozwa na Mwenyekiti wao Freeman Mbowe wametimiza masharti ya dhamana Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Washtakiwa hao walitakiwa kila mmoja kuwa na wadhamini wawili ambao watasaini hati ya dhamana ya Sh20 milioni na kuwa na barua kutoka kwa viongozi wao ama wa vijiji au mtaa, ambao watapaswa kuwa na nakala za vitambulisho vyao.

Mbunge wa Kawe, Halima Mdee  yeye amesomewa mashtaka mawili ya kufanya mkusanyiko usio halali na kuendelea na mkusanyiko huo, kutotii amri iliyowataka kutawanyika na kusababisha vurugu iliyosababisha kifo cha Akwilina Akwilini na askari kujeruhiwa. 

==>Endelea Kutufuatilia

Usisahau ku install App yetu upate habari zetu kwa wepes zaid << Bofya hapa>>

BREAKING: Halima Mdee Naye Kapata Dhamana kwa Bondi ya Milioni 20

$
0
0
Mbunge wa Kawe Halima Mdee leo April 3, 2018 alifikiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  na kuunganishwa na  akina Freeman Mbowe

Mdee  yeye alisomewa mashtaka mawili ya kufanya mkusanyiko usio halali na kuendelea na mkusanyiko huo, kutotii amri iliyowataka kutawanyika na kusababisha vurugu iliyosababisha kifo cha Akwilina Akwilini na askari kujeruhiwa.

Baada ya kusomewa mashitaka hayo, Mahakama imempa  dhamana kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili watakaosaini kwa maandishi bondi ya Sh milioni 20 na kuripoti mara moja kila wiki.

Mahakama  imesema haiwezi kumnyima mshtakiwa dhamana kwa sababu aliruka dhamana ya polisi maana  polisi ni taasisi nyingine na mahakama ni taasisi nyingine, hivyo ikampatia dhamana mshtakiwa kwa masharti tajwa hapo juu.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Ni Dr. Chief Malunde Pekee Anaetibu Nguvu Za Kiume Na Kumtuliza Umpendae Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
"NI DR. CHIEF MALUNDE PEKEE ANAETIBU NGUVU ZA KIUME NA KUMTULIZA UMPENDAE KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI"
-baada ya kujichimbia katika nchi za kiarabu kwa zaidi ya miaka (10)sasa amewasili nchini na dawa za tiba asilia.
 
1/NGOLO 3 POWER-ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, ina ubora wa hali ya juu wa kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wasiojiweza kufanya tendo la ndoa, inaimarisha misuli iliyolegea na kusinyaa, inarutubisha mbegu za kiume na kukufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15-25 kuwa na hamu na tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila kuchoka, inarefusha uume inchi 5-8 na kunenepesha hadi cm 4 kwa wenye maumbile madogo, dawa hii imeboreshwa na hutibu matatizo haya kwa muda mfupi tu.
 
2/MAGOYE MVUTO- dawa hii ina uwezo mkubwa sana kumvuta na kumtuliza aliekuacha awe mpenzi, mme/mke itamfanya akutafute mwenyewe ndani ya masaa 3tu na kukutimizia mahitaji yako kwa haraka na kumfunga asiwe na mtu mwingine.
 
3/SUPER LUBEJA- ni dawa ya kushepu umbo no.8 mguu wa bia, kuongeza hips, na makalio kwa muda wa siku 5tu unapata saizi uipendayo, kuondoa makovu, chunusi, harufu mbaya ya mwili michirizi, kupunguza tumbo na maziwa kwa siku 6tu.
 
4/NG'WESHI MIX- ni dawa ya biashara ya kupata wateja wengi, kusafisha nyota, kurudishwa kazini na kupandishwa cheo, kurudisha mali iliyoibiwa au kudhurumiwa.
 
PIA TUNATIBU MAGONJWA SUGU KAMA: vidonda vya tumbo, ngiri, chango na uzazi kwa kina mama: (dawa zote hazina madhara kwa mtumiaji) HUDUMA HIZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO: TUNAPATIKANA DSM BUGURUNI SHELI AU PIGA SIM NO_ 0763-181099.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Rais Magufuli aitaka Tanesco kupunguza bei ya umeme

$
0
0
Rais John Magufuli amelitaka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuanza kufikiria kupunguza bei ya umeme kwani nchi inatarajia kuwa na umeme mwingi.

Rais ameyasema hayo leo Aprili 3, wakati wa uzinduzi wa kituo cha kuzalisha umeme cha Kinyerezi awamu ya pili.

Amesema miradi yote ya umeme ukijumlisha na wa Stiegler Gauge itafikia megawati 5000 hivyo wataibana  Wizara ya Nishati ianze kufikiria kupunguza bei ya umeme.

“Muanze kufikiria namna ya kushusha bei ya umeme, mmeanza vizuri muendelee na utaratibu huo.

“Nchi ina vyanzo vingi vya kuzalisha umeme, maji , jua, upepo, makaa ya mawe, hata nyuklia, kwa sababu tunayo madini ya uranium yanayoweza kuzalisha umeme kwa nyuklia, kwa umeme wote huo hakuna haja ya kuwa na bei ya juu, ”amesema Magufuli.

Amefafanua kuwa anayetaka kuwekeza bila kukomoa aje, lakini siyo wawekezaji wababaishaji.

Ameeleza kuwa nchi itakuwa na umeme wa kutosha,  wa uhakika na kwa gharama nafuu.

Magufuli pia alizitaja sababu za bei ya nishati hiyo kuwa ya juu ni kutokana na umeme mwingi kuzalishwa kwa kutumia mafuta (dizeli), huku baadhi ya mikataba kuwa mibovu na ya ovyo.

Ameeleza takwimu zilizofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) mwaka 2015/16 zinaonyesha asilimia 36.6 ya Watanzania ndiyo wameunganishiwa umeme.

Kesi ya Mbowe na Viongozi Wengine wa CHADEMA Kusikilizwa April 16

$
0
0
Upande wa mashtaka wa kesi inayowakabili viongozi saba wa Chadema, akiwemo Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe ameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iruhusu kesi hiyo isikilizwe kwa haraka, ikiwezekana jambo hilo kuanza kesho.

Wakili huyo wa Serikali, Faraja Nchimbi  amesema msingi wa  maombi hayo ni kutokana nai upelelezi kukamilika.

Amesema sababu nyingine ni kwamba washtakiwa wengi katika kesi hiyo ni wabunge na kwa kuwa kesi hiyo inavuta watu wengi ni vema ikasikilizwa haraka.

"Kwa hiyo tunaomba kama ikiwezekana kesho mchana tuendelee na usikilizaji wa awali ili sisi upande wa mashtaka tuweze kuwasilisha kile tulicho nacho,” amesema Nchimbi.

Hata hivyo, wakili wa upande wa utetezi,  Peter Kibatala amepinga mapendekezo hayo akieleza kuwa ndiyo kiongozi wa jopo la mawakili wa utetezi, kesho atakuwa na kesi nyingine Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi na kesho kutwa pia atakuwa na kesi nyingine.

Amesema Aprili watakuwa na semina za mawakili ambazo ni za lazima kwa kuwa bila kupata alama zinazohitajika kutokana na semina hizo, leseni yake haiwezi kuhuishwa.

Vilevile, amesema kuanzia Aprili 13 watakuwa na mkutano wa mawakili wote jijini  Arusha na akapendekeza usikilizwaji wa awali  wa kesi hiyo ufanyike Aprili 16.

Katika uamuzi wake, Hakimu Wilbard Mashauri amekubaliana na mapendekezo ya upande wa utetezi na akaamuru usikilizwaji wa awali ufanyike April 16, 2018.

Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi tarehe hiyo, itakapoitwa kwa ajili ya usikilizwaji wa awali.

Mbali ya Mbowe viongozi wengine walioachiwa kwa dhamana ni Katibu Mkuu Dk  Vicent Mashinji, Manaibu Katibu Wakuu John Mnyika (Bara), Salum Mwalimu (Zanzibar), Mbunge wa Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa,  Mweka Hazina wa Baraza la Wanawake wa chama hicho Ester Matiku  na mwenyekiti wa baraza hilo, Halima Mdee.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images