Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Chombo cha Anga cha China Tiangong-1 Chaanguka Pacific

0
0
CHOMBO cha anga za juu cha China, Tiangong-1 kimemeguka na kuvunjika vipande vipange wakati kikikatiza anga la dunia maeneo ya bahari Kusini mwa Pacific leo Jumatatu, ikiwa ni miaka saba tangu kiliporushwa angani mwaka 2011 kufanyia majaribio ya teknolojia ya kuunganisha vyombo mbalimbali anga za juu na vyombo vya kuzunguka kwenye mzingo wa dunia.

Tiangong-1 ni sehemu ya juhudi za China za kuunda kituo cha anga za juu kitakachokuwa kinadhibitiwa na binadamu katika anga za juu kufikia mwaka 2022.

Wataalamu wa anga za juu wa Marekani wamesema wametumia teknolojia ya kufuatilia mzingo wa dunia kuthibitisha kuingia ardhini kwa Tiangong-1. Mtaalamu wa anga za juu Jonathan McDowell kutoka Chuo Kikuu cha Harvard ameandika kwenye Twitter kwamba huenda chombo hicho kimeanguka Kaskazini Magharibi mwa Tahiti.

Wataalamu walitatizika kubaini hasa ni wapi chombo hicho kingeanguka. Idara ya anga za juu ya China ilikuwa awali imekadiria kimakosa kwamba chombo hicho kingeanguka karibu na Sao Paulo, Brazil muda mfupi kabla ya chombo hicho kuingia anga ya dunia.

Shirika la Anga za Juu la Ulaya (ESA) lilisema mapema kwamba uwezekano mkubwa ni kwamba chombo hicho cha Tiangong-1 kingeanguka baharini.

Imeelezwa kuwa, chombo hicho kiliacha kufanya kazi tangu Machi 2016 japo kwa kawaida Tiangong kilifaa kusitisha shughuli yake ya kuizunguka dunia kwa utaratibu na mpangilio fulani. Tiangong ni chombo kilichokuwa na urefu wa mita 10 (futi 32) na uzani wa zaidi ya tani 8 na ni kikubwa zaidi ya vyombo vyote vilivyoundwa na binadamu ambavyo vimewahi kuanguka kutoka anga za juu.

Lengo lilikuwa kutumia vifaa vinavyokipa chombo hicho msukumo kukielekeza hadi maeneo ya mbali yasiyo na watu (Bahari ya Kusini). Lakini kabla ya hilo kufanyika, ghafla hitilafu ya mfumo wa kukidhibiti ulikikumbwa na wataalamu wa China wakashindwa kukidhibiti.

Mashirika 13 ya anga za juu ya mataifa mbalimbali, yakiongozwa na Shirika la Anga za Juu la Ulaya (ESA), yalifuatilia njia ya Tiangong na kujaribu kuiga tabia yake kadiri kilivyokaribia kuingia ndani ya anga ya dunia huku kikiendelea kuizunguka. Tiangong maana yake ni ‘Kasri la Mbinguni’

Bombardier ya tatu Iliyokuwea Canada kutua nchini leo Jioni

0
0
Ndege ya tatu aina ya Bombardier Dash 8 Q400 itawasili na kupokewa nchini leo Jumatatu Aprili 2,2018 saa 10:00 jioni.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbasi katika mtandao wa kijamii wa Twitter amesema hayo.

Ndege hiyo pamoja na nyingine mbili zilizopo nchini ni utekelezaji wa mpango wa Serikali katika kulifufua Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).

Ndege hiyo awali ilitarajiwa kuwasili nchini Julai mwaka jana ikiwa ni miongoni mwa zingine mbili zenye uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 70 ambazo zinaendelea kutoa huduma nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi amekaririwa na gazeti la Serikali la Habari Leo akisema ndege hiyo iliondoka Canada tangu Ijumaa Machi 30,2018.

“Tofauti na ndege kubwa zinazoweza kusafiri moja kwa moja, ndege hii italazimika kusimama kwenye vituo kadhaa katika nchi itakazopitia kabla ya kuwasili muda wowote kesho (leo)” alikaririwa Matindi na gazeti hilo.

Wasafi TV Ya Diamond Iko Hewani....Channel 122 Azam TV

0
0
Kituo kipya cha runinga cha Wasafi TV leo Aprili 02, 2018 kimeanza kurusha matangazo yake mubashara kupitia ving’amuzi mbalimbali kikiwemo cha Azam TV.

Akithibitisha taarifa hizo, Diamond Platnumz ambaye ndiye mmiliki na muanzilishi wa kituo hicho, amesema kuwa matangazo hayo yameanza kuonekana kuanzia leo na kwa watumiaji wa king’amuzi cha Azam, Wasafi TV itapatikana namba 122 .

Hata hivyo, bado haijajulikana kama Wasafi TV itapatikana kwenye ving’amuzi vingine zaidi ya Azam TV.

Tangazo la Kusimamisha Ujenzi Katika Maeneo Yanayozunguka Mjiwa Serikali

Waziri Mkuu Aitaja Mikoa Minne Inayoongoza kwa Utoro wa Wanafunzi

0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameitaja mikoa ya Tabora, Geita, Mtwara na Shinyanga kuwa inaongoza kwa utoro wa wanafunzi wa sekondari.

Waziri mkuu pia ameitaja mikoa ya Rukwa, Geita, Tabora, Singida na Simiyu kuwa inaongoza kwa utoro wa wanafunzi wa shule za msingi.

Majaliwa ambaye pia ni mbunge wa Ruangwa ameitaja mikoa hiyo leo Jumatatu Aprili 2,2018 akizindua mbio za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa Magogo mkoani Geita.

Mbio za Mwenge zitakazohitimishwa Oktoba 14,2018 mkoani Tanga zinaongozwa na kauli mbiu “Elimu ni ufunguo wa maisha, wekeza sasa kwa maendeleo ya nchi yetu.”

Majaliwa amesema Mkoa wa Tabora unaongoza kwa asilimia 9.7 ya wanafunzi watoro wa sekondari ukifuatiwa na Geita (asilimia 8.1), Mtwara (asilimia 6.1) na Shinyanga (asilimia 6.3).

Kwa shule za msingi, Rukwa inaongoza kwa asilimia 3.2, ukifuata Geita (asilimia 3.1), Tabora (asilimia 2.9), Singida (asilimia 2) na Simiyu (asilimia 2).

“Kwa jumla utoro wa wanafunzi wa sekondari ni mkubwa kuliko shule za msingi. Naikumbusha mikoa yote niliyoitaja kuhamasisha wananchi wakiwamo wazazi na walezi kuhusu umuhimu wa elimu na mahudhurio endelevu shuleni kwa kutumia utaratibu wa sheria zilizowekwa,” amesema Majaliwa.

Wema Sepetu: Sioni Wivu Diamond Kumkumbatia Hamisa Mobeto

0
0
Wakati habari zilizopo mjini kwa sasa ni tukio la mwanamitindo Hamisa Mobetto na msanii wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ’Diamond’ kuteka tukio la utoaji tuzo za filamu za Sinema Zetu International Film Festival Award (SZIFF), kwa mrembo Wema Sepetu yeye kaichukulia kawaida.

Diamond na Mobeto katika tuzo hizo zilizofanyika jana ukumbi wa Mlimani City , walikwenda kama wageni waalikwa, walichaguliwa kukabidhi tuzo kwa mshindi wa kipengele cha ‘Best Original Music’ ambayo ilikwenda kwa filamu ya Safari ya Gwalu.

Katika kipengele hicho watu walikuwa wanasubiri kwa hamu kuona namna gani Wema ataweza kukabidhiwa tuzo na wawili hao, kwa kuwa filamu yake ya ‘Heaven Sent’ ilikuwa ni mojawapo iliyokuwa ikishindanishwa lakini bahati ndiyo hivyo haikuwa yake.

Akizungumzia namna alivyochukulia  kitendo cha Mobetto na Diamond kufika eneo hilo na kuweza kukabidhi tuzo, Wema ambaye aliwahi kuwa mpenzi wa Diamond miaka kadhaa iliyopita na hivi karibuni kuelezwa kwamba wamerudiana, amesema kitendo hicho kwake amekichukulia kawaida kwa kuwa Mobetto na Diamond ni mtu na mzazi mwenzake.

“Wee ulitaka nichukuliaje labda, Mobetto na Diamond hawa ni wazazi jamani , ulitaka nikasirike au,halafu isitoshe mimi sina uhusiano wa kimapenzi na Diamond  bali ni washkaji tu na siyo kama watu wanavyosema,”amesema Wema.

Kuhusu hatua yake ya kupata tuzo mbili ya msanii bora wa kike na chaguo la watu (People’s Choice Award) kupitia filamu yake ya ‘Heaven Sent’, Wema amesema amefurahi kuona majaji wameweza kuona kipaji alichonacho.

Pia, aliahidi kuendelea kuwapa mashabiki wake kazi nzuri na kuwaondoa hofu wadau wa filamu waliokuwa wanasema kuwa bongo movie imekufa kuwa siyo kweli bali ilikuwa imelala tu.

Hata hivyo, hakusita kutoa shukurani kwa mashabiki zake ambao amesema ni  kati ya watu ambao waliweza kushiriki kumpigia picha hadi kuhakikisha anapata ushindi huo.

Rais Magufuli Kuweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa RADA Mchana Huu

0
0
Rais John Magufuli leo mchana Aprili 2,2018 anaweka jiwe la msingi la ujenzi wa mfumo wa rada za kuongoza ndege.

Mfumo huo wa rada za kuongozea ndege unajengwa katika vituo vinne vya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA); Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA); Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwanza na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe.

Ujenzi unafanywa na Kampuni ya M/S Thales Las France SAS ya nchini Ufaransa ukigharimu Sh67.3 bilioni fedha zinazotolewa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Hamza Johari amesema leo Jumatatu Aprili 2,2018 kuwa ujenzi utakamilika ndani ya miezi 18.

Amesema mradi huo utasaidia kurahisisha huduma za utafutaji na uokoaji kunapotokea ajali za ndege.

Johari amesema pia utaiwezesha nchi kukidhi viwango na miongozo ya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO) na kujenga imani ya watumiaji wa anga ya Tanzania.

Tayari wageni wamewasili eneo la uzinduzi wakiwamo mawaziri, wabunge, mabalozi na wananchi.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewasili akiongozana na msanii wa muziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul maarufu Diamond.

Mkutano Wa Kumi Na Moja Wa Bunge Kuanza April 3 Na Kumalizika Juni 29 Mwaka Huu Mjini Dodoma


Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO 0754372325/ 0689013109/ 0620806813 

HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Mke wa zamani wa Nelson Mandela Afariki Dunia

0
0
Winnie Mandela, mke wa zamani wa Nelson Mandela, ambaye pia alipigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini amefariki dunia akiwa na miaka 81. Habari za kifo chake zimethibitishwa na msaidizi wake.

Winnie alizaliwa mnamo 26 Oktoba mwaka 1936, na ingawa yeye na mumewe - Nelson Mandela - walitalikiana mapema miaka ya 1990, Winnie Madikizela Mandela kama alivyofahamika rasmi alisalia kutoa mchango katika maisha ya Bw Mandela.

Msemaji wa familia Victor Dlamini amesema kupitia taarifa kuwa: "Amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu, ambapo amekuwa akiingia na kutoka hospitalini mara kwa mara tangu mwanzo wa mwaka.

"Alifariki mapema Jumatatu adhuhuri akiwa amezungukwa na familia na wapendwa wake."

Askofu mstaafu na mshindi wa tuzo ya Nobel Desmond Tutu amemsifu kama "ishara kuu ya vita dhidi ya ubaguzi wa rangi," kwa mujibu wa AFP.

Winnie alikuwa na miaka 20 hivi pale alipojipata katika siasa.

Alisomea kazi ya utoaji huduma za kijamii na haraka aliyazoea maisha ya kuwa mama na mwanasiasa.

Katika kipindi chote cha miaka 27 mumewe alipokuwa gerezani bila matumaini ya kuachiwa huru kutokana na hukumu ya kifungo cha maisha jela alichopewa mwaka 1964, Bi Winnie alilazimika kubeba jukumu la ulezi wa watoto na pia kuendeleza kampeni za kisiasa kutaka mashujaa wa kupigania nchi yao waachiwe huru hasa mumewe.

"Kamwe hatutapoteza matumaini na watu wangu hawatapoteza matumaini kamwe, bila shaka tunatarajia kwamba kazi itaendelea," alisema wakati huo.

Kutokana na hayo Bi Winnie Mandela alilazimishwa kusalia tu huko Brandford katika jimbo lao la Orange Free katika miaka ya 70 baada ya operesheni mojawapo za kupambana na ubaguzi wa rangi zilizokuja kujulikana zaidi kama the Soweto Uprising.
Bi Mandela (pichani mwaka 1988) alihusika makubwa kukabiliana na utawala wa ubaguzi wa rangi Haki miliki ya picha Reuters
Image caption Bi Mandela (pichani mwaka 1988) alihusika makubwa kukabiliana na utawala wa ubaguzi wa rangi

Kama ilivyomtokea mumewe, Bi Winnie alifungwa gerezani, na hata kuwekwa katika kizuizi cha pekee yake ambacho ni mojawapo ya vifungo vigumu zaidi gerezani vinavyowaathiri wafungwa kisaikolojia.

Lakini baada ya kuachiwa kwake mtindo wa mapambano yake dhidi ya ubaguzi wa rangi ulianza kupata sifa mbaya hasa pale alipoonekana kuendekeza tabia ya kuwavisha tairi shingoni wale waliolengwa kwa tuhuma za usaliti na kisha kuwachoma moto.

"Kwa 'mikufu yetu' tutaikomboa nchi hii," alizoea kusema.

Mambo yalizidi kumwendea mrama kutokana na matendo ya baadhi ya walinzi wake katika kile kikundi kilijulikana kama the Mandela United Football Club.

Walipatikana kuhusika katika kitendo cha kumteka nyara na kumuua kijana mmoja mwenye umri wa miaka 14 aitwae Stompie Moeketsi -kwa tuhuma za kwamba alikuwa akitoa siri kwa maadui zao.

Japo Bi Winnie Mandela aliepuka hukumu ya kifungo jela - baadaye tume ya ukweli na maridhiano iliyoongozwa na askofu Desmond Tutu, iliyokuwa inachunguza ukweli kuhusu matendo tata katika vita dhidi ya ubaguzi wa rangi na kutafuta maridhiano, ilimpata Bi Mandela na hatia ya kutowajibika kisiasa wala kimaadili wakati wa kitendo hicho.
ANC leader Nelson Mandela and wife Winnie raise fists upon his release from Victor Verster prison, 11 February 1990 in Paarl Haki miliki ya picha AFP
Image caption Nelson na Winnie Mandela baada yake kuachiliwa huru Februari 1990

Licha ya misukosuko hiyo Bi Mandela alibaki kuwa mtu muhimu sana katika siasa za Afrika kusini na kuwa mwakilishi muhimu waa wanawake waliopambana kufa na kupona dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi uliokuwa unaendelezwa na Wazungu walio wachache nchini humo.

Katika siku za baada ya uhuru wa Afrika Kusini anakumbukwa zaidi kwa kuwa miongoni mwa wachache katika uongozi wa ANC waliomuunga mkono aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Thabo mbeki katika kushtumu na kulaani vikali vitendo vya kuwashambulia wahamiaji wa Kiafrika huko nchini Afrika Kusini.

KUSINI - mashambulio yaliyobadikwa jina xenophobic attack. Pia amekuwa muungaji mkono mkubwa wa kiongozi wa chama cha Economic Freedom Fighters CHA Julius Malema , kilichojimegua kutoka ANC ambacho kilimkosoa vikali rais aliyelazimika kung'atuka Jacob Zuma.

Historia ya Bi Winnie Madikizela Mandela, hadi kifo chake inabaki akikumbukwa zaidi kama mama wa taifa la Afrika kusini aliyesimama kidete dhidi ya ubaguzi wa rangi katika umri wake wote.

Tanzania Yapata Mkopo Wa Shilingi Bilioni 34 Kutoka Mfuko Wa Maendeleo Wa Abu Dhabi Kuboresha Barabara Ya Uvinza-malagarasi Kwa Kiwango Cha Lami

0
0
Benny Mwaipaja, Abu Dhabi
Tanzania imeendelea kuaminiwa na Jumuiya ya Kimataifa ambapo Mfuko wa Maendeleo wa Umoja wa Falme za Kiarabu-Abu Dhabi, umeipatia Tanzania mkopo wenye masharti nafuu wa dola za Marekani milioni 15, sawa na shilingi bilioni 34 za Tanzania, kwa ajili ya kuboresha barabara ya Uvinza hadi Malagarasi yenye urefu wa kilometa 51, kwa kiwango cha lami

Hafla fupi ya uwekaji saini wa mkataba huo imefanyika katika makao makuu ya Mfuko huo yaliyopo Abu Dhabi, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) ambapo Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-TAMISEMI, amesaini kwa niaba ya Serikali, na Mhe. Mohamed Saif Al Suwaidi Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Abu Dhabi kwa niaba ya Mfuko huo.

Akizungumza baada ya kusaini Mkataba huo, Katibu Mkuu-TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe, amesema kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa kuwa ni kiungo kikuu cha usafiri wa abiria na mizigo kutoka Bandari ya Dar es Salaam kwenda Kigoma na nchi jirani za Burundi na Kongo DRC.

Amesema kuwa uamuzi wa Serikali wa kuboresha barabara hiyo kwa kiwango cha lami umelenga kuchochea uchumi wa nchi kwa kuwezesha usafirishaji wa mazao ya wakulima pamoja na kupunguza gharama na kuongeza uwezo wa kufanya biashara na nchi hizo jirani.

“Tutabakiwa na kipande cha barabara yenye urefu wa kilometa 28 kutoka Urambo hadi Kaliua na kilometa 42 kutoka Chagu hadi Kazilambwa, barabara ambazo Serikali inaendelea kuzitafutia fedha ili kukamilisha barabara yote inayoelekea ukanda huo wa kati kutokea Dar es Salaam, Manyoni (Singida), Tabora hadi Kigoma” Alisema Mhandisi Iyombe.

Ameushukuru Mfuko huo kwa kuendelea kuiamini Serikali na kutoa mkopo huo wenye masharti nafuu baada ya kufanya hivyo hivi karibuni kwa kutoa mkopo mwingine wa dola milioni 57, uliofanikisha kuboreshwa kwa barabara ya Kidahwe hadi Uvinza yenye urefu wa kilometa 77 kwa kiwango cha lami.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Abu Dhabi, Mhe. Mohamed Saif Al Suwaidi, kwa upande wake, amesema kuwa Mfuko huo uko tayari kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.

Amefafanua kuwa mradi huo ambao mkataba umesainiwa mjini Abu Dhabi, utakuwa ni wa nne kufadhiliwa na Mfuko wake Tangu uhusiano wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Tanzania uanzishwe mwaka 1977, ukiwemo mradi wa kuendeleza kiwanda cha Sukari cha Kagera, Mradi wa Maji Vijijini huko Viwani Zanzibar na Mradi wa kuboresha barabara ya Kidahwe hadi Uvinza kwa kiwango cha lami.

Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk  amesema kuwa kusainiwa kwa mkataba huo ni kiashiria cha kukubalika kwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli, katika kuwaletea wananchi wake maendeleo ya haraka na kuungwa mkono na Jumuiya ya Kimataifa.

“Hatua hii ni uthibitisho wa mahuasiano mazuri ya kihistoria na kidugu kati ya Tanzania na Umoja wa Falme za Kiarabu uliodumu kwa muda mrefu tangu mwaka 1977” Alisisitiza Mhe.Mbarouk

Mhe. Mbarouk amebainisha kuwa kukamilika kwa barabara hiyo ya Uvinza hadi Malagarasi kutachochea maendeleo ya kiuchumi na mapinduzi ya viwanda kwa kuunganisha shughuli za kiuchumi kama vile kilimo na maliasili pamoja na kukuza utalii.

Ni Marufuku Kuoa bila taarifa

0
0
SERIKALI ya Kijiji na Kata ya Nsalala Tarafa ya Itwangi Shinyanga Vijijini, imetunga sheria ya kutokomeza mimba na ndoa za utotoni, kwa kumtaka mwananchi anayetaka kuoa ama kuozesha kutoa taarifa kwa uongozi wa kijiji.

Lengo la marufuku hiyo ni ili kijiridhisha kama anayeolewa siyo mwanafunzi au msishana chini ya umri wa  miaka  18.

Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki na Mwenyekiti wa Kijiji cha Nsalala, Sandeko Machungo, kwenye mdahalo wa kutoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia ndani ya jamii kupitia mitandao ya kijamii, ulioandaliwa na Shirika la Kivulini linalotetea haki za watoto na wanawake kwa ufadhiri wa shirika la OXFAM la Uingereza.

Alisema viongozi wa Serikali ya kijiji mara baada ya kupata elimu ya ukatili wa kijinsia kupitia mashirika mbalimbali, wameona ni vyema wakatunga sheria ndogo kijijini ya kuzuia wananchi kuoa amakuozesha bila ya kutoa taarifa kwenye uongozi huo kwa lengo la kutokomeza tatizo la mimba na ndoa za utotoni.

“Kwenye kijiji changu tumetunga sheria, hakuna mwananchi kuoa ama kuozesha bila ya kuuona uongozi wa kijiji, tutafuatilia taarifa za mtu anayetaka kuolewa kama hayupo chini ya umri wa miaka 18 na siyo mwanafunzi, kwa kuangalia cheti cha kuzaliwa ama kadi ya klinini ndipo tunatoa ruhusa,” alisema Machungo.

Aliongeza sheria hiyo waliitunga mwaka jana na wananchi wamekuwa wakifanya hivyo, na tangu ianze kufanyakazi hakuna changamoto tena ya ndoa za utotoni kijiji humo wala mimba kwa wanafunzi.

Kwa mujibu wa Machungo, kila mwananchi amekuwa mlinzi wa mwezake na atakaye bainika kwenda kinyumena sheria hiyo kijiji kitamshughulikia.

Taarifa Toka Ofisi ya Waziri Mkuu Baada ya Kuzindua Mbio za Mwenge

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa mikoa ya Tabora, Geita, Mtwara na Shinyanga ambayo inaongoza kwa utoro wa wanafunzi kwa shule za sekondari wahamasishe umuhimu wa elimu na mahudhurio endelevu shuleni.

“Kwa ujumla utoro wa wanafunzi wa Sekondari ni mkubwa zaidi kwa Mikoa husika kuliko shule za msingi. Nitumie nafasi hii kuikumbusha Mikoa niliyoitaja kuhamasisha wananchi wakiwemo wazazi, walezi na wanafunzi wenyewe kuhusu umuhimu wa elimu na mahudhurio shuleni.”

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumatatu, Aprili 02, 2018) wakati akizindua mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2018 katika uwanja wa Magogo mkoani Geita. Kaulimbiu ya mbio za mwenge kwa mwaka huu ni ‘Elimu ni ufunguo wa maisha, wekeza sasa kwa maendeleo ya Taifa letu.’

Waziri Mkuu amesema dhamira ya Serikali kupitia kaulimbiu hiyo ni kuwashirikisha wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo kuwekeza katika elimu na kuzalisha rasilimali watu yenye ujuzi na stadi zitakazowezesha kuchochea mapinduzi ya viwanda ili nchi iwe ya uchumi wa kati ifikapo 2025.

Akizungumzia kuhusu utoro kwa shule za sekondari nchini, Waziri Mkuu amesema mkoa wa Tabora ndio unaongoza kwa utoro kwa kuwa na silimia 9.7,

Geita asilimia 8.1, Mtwara asilimia 6.4 na Shinyanga asilimia 6.3.

Kuhusu utoro wa wanafunzi wa shule za Msingi nchini, Waziri Mkuu amesema mkoa unaoongoza ni wa Rukwa kwa asilimia 3.2, Geita asilimia 3.1, Tabora asilimia 2.9, Simiyu asilimia 2.0 na Singida asilimia1.9.

Amesema mikoa yenye kiwango kikubwa cha utoro wa wanafunzi na kuacha shule ihakikishe mahudhurio yanadhibitiwa shuleni ili kuhakikisha wanafunzi wote wanaoandikishwa wanahudhuria, wanasoma na kuhitimu ngazi husika.

“Ukitaka kuleta maendeleo ya uchumi ulio imara, ukitaka kujenga jamii inayo heshimu na kufuata misingi ya uwajibikaji na ubunifu, ukitaka kujenga Taifa lenye amani na utulivu, lazima uwekeze zaidi katika elimu”.

“Kwa hiyo, uwekezaji katika elimu haumaanishi tu kuhakikisha watoto wetu na Watanzania kwa jumla wanapata haki yao ya msingi bali ni kuweka misingi imara itakayo liwezesha Taifa na mtu binafsi kufikia hatua bora ya maisha”.

Waziri Mkuu amesema ili kuhakikisha Taifa linafikia viwango bora vya elimu, Serikali ya awamu ya tano inyoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli, imedhamilia kuboresha elimu katika ngazi zote nchini, kuanzia Elimu ya Awali hadi Elimu ya Juu.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema kuwa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu zitaendelea kuhimiza mapambano dhidi ya rushwa kwa sababu bado ipo na inaendelea kuwa ni adui wa haki na kudhoofisha jitihada za Serikali za kuimarisha uchumi, kuimarisha huduma za jamii na Utawala bora.

Amesema athari zinazotokana na vitendo vya rushwa huwaathiri watu wa kawaida zaidi na kuendelea kubaki wanyonge katika jamii, hivyo Serikali itaendelea kupambana na vitendo vya rushwa bila kuchoka mpaka jamii itakapoachana na vitendo hivyo vya kidhalimu.

Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bibi Jenista Mhagama alisema Mwenge wa Uhuru utakimbizwa umbali wa takribani kilomita 103,440.7 kwa siku 195 katika mikoa yote 31 nchini na halmashauri za wilaya 195.

Alisema kazi hiyo itafanywa na vijana sita kutoka Tanzania Bara na  Zanzibar ambao wameandaliwa kikamilifu ili kuhakikisha wanaendelea kuwakumbusha Watanzania historia ya falsafa ya Mwenge wa Uhuru, kufikisha kwa ufasaha ujumbe wa mwaka huu na kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo kwa umakini.

Bibi Jenista alisema mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018 zinaongozwa na Bw. Charles Kabeho kutoka mkoa wa Dar es Salaam akishirikiana na Bw. Issa Abasi Mohamed (Kusini Pemba), Bi. Agusta Safari (Geita), Bw. Ipyana Mlilo (Tanga), Bw. Dominick Njunwa (Kigoma) na Bi. Riziki Hassan Ali (Kusini Unguja).

Naye, Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo - Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Ali Abeid Karume alisema atahakikisha ujumbe wa Mwenge wa Uhuru unawafikia wananchi wote pamoja na kupita katika miradi yote ya maendeleo iliyopangwa.

Balozi Karume ametumia fursa hiyo kuwapongeza Rais Dkt. Magufuli pamoja na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein kwa jitihada zao za kudumisha amani, utulivu, kuwaletea wananchi maendeleo bila ya ubaguzi pamoja na kupambana na maadui wanaotaka kudhoofisha maendeleo nchini.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, APRILI 02, 2018.

Makonda 'Awashitaki' Kwa Rais Magufuli Wanaoingia Dar na Kutoa Matamko ya Kichochezi

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam amewashtaki kwa Rais Magufuli baadhi ya watu (hajawataja kwa majina) kwa kudai kuwa wanaingia ndani ya mkoa wa Dar es salaam na kutangaza uchochezi.

Mh. Makonda amewasilisha mashtaka hayo kwa Rais leo wakati alipokuwa akiweka jiwe la msingi la  ujenzi mradi wa kuongozea ndege katika vituo vinne hapa nchini.

Mh. Makonda amemuambia Rais Magufuli kwamba kuna watu wanaingia ndani ya mkoa wa Dar es salaam na kutangaza uchochezi hivyo yeye kama kiongozi wa mkoa wanajaribu kuangalia utaratibu mzuri wa kisheria watolee matamko katika mikoa yao.

Aidha amesema kwamba "Mh. Rais Tumesikia sikia huko kwingine ila sisi kwetu hakuna waraka. Hakuna waraka popote pale ulipopita. Watu wamemwabudu bwana na mwokozi wao na Tumeungama dhambi zetu kupitia kufa kwake msalabani, tumefufuka naye na tunaendelea kufanya kazi kikamilifu".

Mbali na hayo Mku huyo wa Mkoa ameweka wazi kwamba wakazi wa Mkoa wa Dar es salaam wamesherehekea sikukuu ya Pasaka salama salimini kwani wananchi wametambua thamani ya amani.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya April 3

Pwani Kujenga Viwanda Vitatu Vya Madawa Na Baadhi Ya Vifaa Tiba

0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Kibaha
SERIKALI mkoani Pwani, imeitikia wito wa serikali ya awamu ya tano ya kujenga viwanda vya madawa na baadhi ya vifaa tiba ambapo inatarajia kuwa na viwanda hivyo vitatu hali itakayoondoa adha ya kuagiza madawa nje ya nchi .
 
Aidha imekemea tabia inayofanywa na baadhi ya wawekezaji ya kutoa ajira kwa watu kutoka nje ya nchi na kuwabania fursa hiyo wanaPwani ama watanzania .
 
Akielezea masuala ya uwekezaji na ajira ,wakati wa ziara yake ya kutembelea viwanda mjini Kibaha ,mkuu wa Mkoa wa Pwani,mhandisi Evarist Ndikilo alisema Viwanda vya madawa vitawezesha kuokoa mamilioni ya fedha yaliyokuwa yakitumika kununulia madawa nchi jirani na nje.
 
Alieleza viwanda vitatu vinajengwa Mkoani Pwani ikiwemo Kairuki Pharmaceuticals industry Ltd ,Zinga pharmaceuticals ambacho kitajengwa kwa ubia na waislael na kipo mbioni kuanza kujengwa na Bahari pharmaceuticals .
 
“Tunaikitia wito wa rais Dk.John Magufuli ,lakini pia tangu kipindi cha nyuma tumejipanga kujenga viwanda hivyo ,kupitia ziara hii tunawathibitishia wananchi tunaunga  mkono kauli ya serikali yetu”alifafanua Ndikilo.
 
Pamoja na hayo ,mkuu huyo wa mkoa alieleza ,zipo fursa mbalimbali  za uwekezaji  lakini vijana na wazawa wanashindwa kukimbilia fursa hizo.
Ndikilo alisema wazazi na vijana bado hawajatambua kujipanga kukuza elimu na ujuzi wao kwa ajili ya kujipatia ajira kirahisi.
 
Alitoa rai kwa wawekezaji ,kuacha kuwanyima ajira wazawa na watanzania ambao wanaujuzi na sifa za kufanya kazi .
 
” Haiwezekani tunajenga viwanda vingi lakini vijana ,waTanzania na wanaPwani hawanufaiki na ajira zinazopatikana,haikubaliki”alisisitiza Ndikilo.
 
“Sidhani kama Pwani ama Tanzania nzima haina wenye sifa na ujuzi,hivyo aliwataka wawekezaji hao watoe kipaombele kwa watanzania wenye uwezo .
 
Ndikilo alisema amepokea taarifa uwekezaji wa standard gauge eneo la Soga hawatoi ajira hata ya udereva jambo ambalo analichunguza na atakapopata uhakika watachukua hatua zinazostahili.
 
Aliwataka kununua vifaa vya ujenzi kama nondo ndani ya nchi ,kwani taarifa waliyompatia kwenye ujenzi wa Kairuki Pharmaceuticals industry Ltd kuwa wananunua nondo huko Uturuki .
Alisema kipo kiwanda cha Kiluwa ambacho kinatengeneza nondo zenye ubora hivyo wanunue katika viwanda vya ndani ya nchi.
 
Nae mkurugenzi  mtaalamu wa Kairuki Pharmaceuticals eng.Valency Assenga alisema ujenzi wa mradi huo ulianza machi 10 mwaka huu na mkandarasi ni Petra Construction Ltd Ltd na unatarajiwa kumalizika Novemba 2018.
 
Alielezea kazi zote zinaendelea kwani zipo hatua ya awali ya ujenzi na mpaka kukamilika ujenzi wa awamu ya kwanza kiwanda hicho kitagharimu bilioni 3.9 ” #
 
Eng .Assenga alitaja changamoto kuwa ni miundombinu ya barabara,mradi kusuasua kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha na ucheleweshwaji wa uunganishwaji wa umeme.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji huo ,Jennifer Omolo akizungumzia suala la mipango miji alisema wameanza zoezi la kupima mji muda mrefu  na wanaendelea na zoezi hilo .
 
Omolo aliwataka watu waache kujenga na kufanya biashara kiholela bila kupangwa ,na kuwashauri waone watalaamu wa mipango miji ofisi ya mkurugenzi ili  kupewa maelekezo ya kupata vibali .

Picha: Rais Magufuli Alivyoipokea Bombadiier ya Tatu na Kuweka Jiwe la Msingi Ujennzi wa Rada

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono na kushukuru  wakati akiingia katika ndege hiyo mpya ya Bombardier Q400 iliyowasili kutoka nchini Canada.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amewashika mikono marubani wawili waliokuja na ndege hiyo mpya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza mwanamuziki wa Bongo flavor Naseeb Abdul-Diamond platinum mara baada ya kuweka jiwe la msingi mfumo wa usimikaji wa Rada katika viwanja vinne vya ndege (Mwalimu Julius Nyerere-Dar es Salaam, Mwanza, KIA-Kilimanjaro na Songwe katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza mwanamuziki wa Bongo flavor Naseeb Abdul-Diamond platinum mara baada ya kuweka jiwe la msingi mfumo wa usimikaji wa Rada katika viwanja vinne vya ndege (Mwalimu Julius Nyerere-Dar es Salaam, Mwanza, KIA-Kilimanjaro na Songwe katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka jiwe la msingi mfumo wa usimikaji wa Rada katika viwanja vinne vya ndege (Mwalimu Julius Nyerere-Dar es Salaam, Mwanza, KIA-Kilimanjaro na Songwe katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli Awashangaa Maaskofu....Ahoji Kwa nn Hawakutoa Waraka Wakati wa Mauaji ya Kibiti

0
0
Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa makanisani saizi zaka zimepungua kwa kuwa mafisadi ndio walikuwa wanatoa zaka na kudai kuwa watu ambao walikuwa wamezoea kupata pesa za bure ndiyo wanapiga makelele.

Rais Magufuli amesema hayo jana  alipokuwa akihutubia uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam, wakati akiweka jiwe la msingi kwa ajili ya mradi wa kuongozea ndege katika vituo vinne hapa nchini.

"Ni uhakika pia wapo watu ambao walizoea fedha za bure za kuibia masikini wale ndio wanapiga kelele kweli.

"Nina fahamu hata makanisani zaka zimepungua kwa sababu zingine zilikuwa zinatolewa na mafisadi, lakini sisi Watanzania tusimame twende mbele .Ninawaeleza kwa dhati kwa sababu najua tulikotoka na tunakokwenda. Watendaji wangu hawa wanafanyakazi kubwa kweli" alisema Rais Magufuli

Mbali na hilo Rais Magufuli alisema kuwa nchi sasa ipo salama kutokana na jitihada za maafisa wa ulinzi na usalama na kusema anashangaa kuona watu wakati wa mauaji wa kibiti hawatoi waraka.

"Wakati wa mauaji ya Kibiti hatukuona mtu yoyote analaani, kufa kwa Kibiti ni salama hakuna hata waraka uliotoka ingawaje sipendi sana kulizungumzia hili kwa sababu nalijua wala halina msingi sana na wala halitafanikiwa na wala hakuna lolote kwa sababu serikali ipo na nimekabidhiwa na wananchi kuilinda kwa nguvu zote na ninasema kweli kweli wengine nawaangalia tu"
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images