Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Viongozi wengine wa upinzani wakamatwa na Polisi Kigoma

$
0
0
Mjumbe wa Kamati Kuu, na Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Sheria ya ACT Wazalendo, Wakili Thomas Msasa amekamatwa na polisi mjini Kigoma

Tarifa ya kukamatwa kwake imetolewa na Mbunge wa Kigoma Ujiji Zitto Kabwe, na kusema kwamba sababu ya kukamatwa ni  kuwatetea Madiwani, viongozi na wanachama wa chama hicho waliokuwa wamekamatwa na Jeshi la Polisi hapo jana.

Zitto Kabwe amesema wakili Msasa alikwenda polisi kama wakili wa Madiwani wawili wa ACT Wazalendo, diwani wa kata ya Kipampa, ndugu Mussa Mgongolwa, pamoja na diwani wa kata ya Kigoma, ndugu Hussein Kalyango, aliyekuwa mgombea udiwani kata ya Mwanga, ndugu Winston Mogha, katibu wa ngome ya vijana ya ACT Wazalendo mkoa, ndugu Masabo, pamoja na wanachama na wafuasi mbalimbali wa ACT Wazalendo wa mkoa wa Kigoma, ambao walikamatwa hapo jana.

Kwa upande wa msemaji wa chama hiko Ado Shaibu amesema mpaka sasa upande wa jeshi la Polisi hawajatoa taarifa rasmi juu ya sababu ya kukamatwa kwa watu hao, na kwamba wanasheria wao wanashughulikia suala hilo na utaratibu wa dhamana.

Isome hapa taarifa yote aliyoandika Zitto Kabwe.

Muhimbili Yataja idadi ya watoto waliozaliwa leo Pasaka

$
0
0
Jumla ya watoto 7 wamezaliwa siku ya leo Aprili Mosi, 2018, ambayo ni sikukuu ya pasaka, katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam.

Taarifa hiyo imetolewa na ofisi ya mahusiano ya hospitali ya Muhimbili, ambapo imeeleza kwamba watoto hao waliozaliwa wanne ni wa kike, huku wakiume wakiwa watatu, na wazazi sita wakiwa wamejifungua kawaida na mmoja kwa upasuaji.

Mama na watoto hao wote wapo salama na wanaendelea vizuri hospitalini hapo.

Kauli ya CHADEMA Baada ya Halima Mdee Kukamatwa na Polisi Leo

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kimeamua kumpelekea daktari wa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee ili aweze kumcheki na kuwathibitishia Jeshi la Polisi kuwa Halima ni mgonjwa na wala hakuwa na nia ya kukimbia kuripoti Polisi.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano ya Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema.

"Halima Mdee bado anashikiliwa na Jeshi la Polisi wa kituo cha 'Centro' Jijini Dar es Salaam mpaka hivi sasa japokuwa amewaeleza ukweli kwamba ametoka kwenye matibabu na kuwaonesha vyeti vyote vya hospitali lakini bado wanaendelea kumshikiria", amesema Mrema

Pamoja na hayo, Mrema ameendelea kwa kusema "mpaka sasa hivi hatua tulizozichukua ni kumpeleka daktari wake ili aende kumcheki na kuwathibitishia Polisi kuwa Halima kweli ni mgonjwa pia wanasheria wa chama wataelekea kituoni hapo muda si mrefu".

Halima Mdee ni miongoni mwa viongozi wa Chadema wanaotuhumiwa na Jeshi la Polisi kufanya maandamano yasiyokuwa na kibali kipindi cha uchaguzi mdogo wa marudio katika jimbo la Kinondoni

Askofu Shoo: Wanaopotosha Ukweli Waraka Wa Maaskofu KKKT Ni Wajinga

$
0
0
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Fredrick Shoo, amesema wale wote wanaojaribu kupotosha ukweli wa waraka wa maskofu kwa kuupaka matope ni wajinga.

Askofu Shoo ametoa kauli hiyo leo katika Usharika wa Moshi Mjini Dayosisi ya kaskazini, mkoani Kilimanjaro wakati akitoa salamu za Pasaka katika ibada maalumu ya kusherekea sikukuu hiyo.

Amesema kumekuwa na baadhi ya watu wakiwamo wanasiasa ambao wamekuwa wakitumia nguvu nyingi kupotosha waraka  wa maaskofu hao na kulipaka kanisa matope kwa malengo yao binafsi jambo ambalo halipendezi na kwamba watu hao ni wajinga.

“Wapo wanaotumia nguvu nyingi kutaka kupotosha ujumbe wa waraka wa maaskofu na wamekuwa wakilipaka kanisa matope ili waweze kurejea katika waraka ule, watu hawa naweza kuwaita ni wajinga lakini pamoja na hilo nataka wakayatafakari na kama wanaona kuna hatua za kuchukua wachukue.

“Kanisa limekuwa linapata kejeli za aina mbalimbali kutoka kwa watu hao na kuwatuhumu kuwa maskofu walifikia maamuzi ya kuandika waraka huo kutokana na sababu za kimaslahi kwa maana ya sadaka makanisani kupungua jambo ambalo si la kweli.

“Kanisa linasitikika sana, tunaposema jambo la kweli na jambo linalohusu maisha ya Watanzania wote, halafu kunatokea watu chache ambao naweza kuwaita wajinga wanakebehi na kusema eti kwa sababu sadaka zimepungua kanisani sisi sadaka hazijapungua kwani wakristo wanajitoa sana na hatujapungukiwa na kitu ila tunasema yale tunayoyaamini,” amesema.

Askofu Shoo amesema anafahamu kuwa kupitia waraka ule maaskofu wa kanisa hilo watabatizwa majina ya aina mbalimbali na kwamba hizo ni jitihada za kujaribu kuuzima ukweli ulipo katika wataka huo na wao hawajali kuhusu hilo bali watasimamia ukweli zaidi.

“Najua tutaitwa majina mengi maaskofu na hizo ni jitihada za upotoshaji wa ule ukweli ulipo katika waraka na tukumbuke hili si jambo la hivi hivi tu…. kwani kwa wakati mmoja mabaraza ya  maaskofu wa makinsa makubwa mawili nchini kukaa na kutoa waraka ambao una ujumbe ulioshabihiana si kitu cha kawaida mimi nasema kuna kitu Mungu anataka kutuambia kupitia ujumbe ule tutafakari hili kama taifa,” amesema.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 73 na 74 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA-
0657072588
ILIPOISHIA  
Livna aliendelea kuzungumza naneno ambayo yalizidi kukasirisha Mariam ambaye ninatambua kwamba ana nipenda. Taratibu Mariam akapiga hatua mbili mbele  na kuniacha mimi nyuma.
“Mari…..”
Kwa jicho alio nitazama nalo Mariam nilijikuta nikinyamaza kimya, Mariam akaachia msunyo mkalia na kumsogelea Livna sehemu alipo simama.
“Sipambani kwa ajili ya huyu mwanaume, ila ninapambana kwa ajili ya uhuru wangu”
Mariam baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo, akamtandika Livna kichwa kizito cha pua, na kumfanya ainame chini huku akitoa mlio wa maumivu, kitendo kilicho pelekea wasichana wota hawa kuanza kutushambulia kwa hasira kali.

ENDELEA
Nikazidi kujitahidi kadri ya uwezo wangu kuhakikisha ninawahimili hawa wasichana wenye mafunzo makubwa ya kupambana, kila nilivyo jaribu kadri ya uwezo wangu, nilijikuta nikishindwa kabisa, kipigo ambacho ninakipata mfululizo kikanifanya taratibu kuanza kuishiwa nguvu na kuanguka chini, kwa macho yaliyo jaa ukungu wa damu inayo nimwagika kutoka kwenye baji la uso baada ya kuchanwa na kitu chenye makali, nikamuona jinsi Mariam naye akipokea kipigo kikali hadi akaanguka chini na kuulia kimya. Msichana moja pasipo kuwa na huruma, akanikanyaga kichwani mwangu kwa kiatu chake chenye ncha kali na kujikuta giza jingi likinitawala kwenye mfumo wa kuona, taratibu mawasiliano ya ubongo na mwili yakakatika.
                                                                                                          ***
    Mlio wa mashine ambayo sifahamu ni mashine ya nini, nikaanza kuisikia kwenye masikio yangu. Taratibu nikafumbua macho yangu, ukungu mzito uliopo kwenye macho yangu sikuweza kuona chochote katika chumba hichi, nikazidi kujitahidi kuyafumbua macho yangu, kwa sekunde kadhaa nikaanza kuona baadhi ya vitu ambavyo taratibu nikaanza kuvigundua kwani si mara yangu ya kwanza.
Taa mbili za mwanga mweupe zilizo juu ya chumba hichi, zikanifanya niweze kuyaona mandhari ya chumba hichi ambacho nimegundua ni hospitalini.
Mashine ya kugemea iliyopo pembeni yangu iliyo unganishwa na mtungi wa hewa ya oksijeni, vikazidi kunihakikishia kwamba eneo nililopo ni hospitalini. Kadri muda ulivyo zidi kwenda ndivyo macho yangu yalivyo weza kuona mandhari ya chumba hichi ambacho sijamuona mtu yoyote.
Nikiwa katika hali ya kufukiria ni kitu gani kilicho pelekea mimi kuwa katika hali hii, mlango wa hichi chumba ukafunguliwa na akaingia nesi wa kike aliye valia mavazi meupe ya kupendeza.

“Karibu duniani”
Nesi huyo alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.
“Nipo wapi?”
“Upo sehemu moja isiyo na jina”
“Isiyo na jina?”
“Yaa ila mimi sio mzungumzaji mkubwa katika hilo, ila yupo ambaye atazungumza”
Nesi huyo akatoka chumba humu, huku kwa mara kadhaa akinitazama kitandani nilivyo laa. Nesi huyu mwenye asili ya kiafrika amenifanya nianze kuwaza mambo mengi sana akilini mwangu, na kitu kingine ambacho kinanichanganya ni yeye kuwa na uwezo wa kuzungumza Kiswahili. Nikaendelea kulala kwenye hichi kitanda huku nikitafakari mambo mengi sana kwenye maisha yangu. Baada ya lisaa moja akaingia mwana mama mrefu aliye valia gauni jeusi pamoja viatu virefu. Ana umbo lililo jengeka vizuri kwa mazoezi huku makalio yake ni makubwa kiasi. Akatembea kwa hatua za taratibu hadi pembeni ya kitanda changu, huku akinitazama usoni mwangu akiwa na tabasamu pana.

“Habari yako kijana”
Mama huyu alizungumza kwa Kiswahili fasaha kabisa hadi mimi mwenyewe nikabaki nimemkodolea macho tu.
“Habari yako kijana?”
“Ahaa salama tu”
“Kwanza nina furaha kukuona ukiwa upo hai”
Mama huyu alizungumza huku  akivuta kiti na kukiweka pembeni ya kitanda, kisha akakaa huku ananitazama usoni.
“Hapa ni wapi?”
“Upo Afrika kusini”
“Afrika kusini!!!!”
Nilijikuta nikishangaa, nikajaribu kukaa kitaki kitandani ila nikajikuta nikiwa nimeshindwa kutokana na maumivu makali ya kichwa.

TANGA RAHA- Sehemu ya Arobaini na Sita ( 46 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

“Siipendi siasa, na sidhani kama ninaweza kuwa mbunge”
“Je kuna ukweli wowote kwamba wewe umepandikizwa roho ya nyoka?”
Swali la muandishi huyu wa habari likanifanya niiname chini ya meza kwani nilijikuta nikikasirika sana jambo ambalo taratibu nikanza kuhisi mabadiliko kwenye mwili wangu, ubaridi mkali ukaanza kunitawala, huku ukiambatana na mikono yangu kuanza kubadilika jambo lililo anza kuniogopesha

ENDELEA
Nikastukia nikifunikiwa na taulo mgongoni, kuangalia vizuri nikamkuta ni Rahma ndio amenifunika na taulo ambalo limelowana maji, kidogo nikaanza kujihisi vizuri hata ubaridi mkali na mabadiliko kwenye mikono yangu vikaanza kuputea taratibu hadi nikarudi kwenye hali yangu ya kawaida
“Unajisikiaje mume wangu?”
Rahma aliniuliza kwa sauti ya chini ya kunong’oneza sana, ambayo sio rahisi kwa mtu yoyote kusikia

“Nipo powa”
“Twende basi ukapumzike ndani”
“Sawa”
“Jamani wapendwa Mr kidogo hali yake sio nzuri sana, ninawaomba mummpe muda kidogo, na mahojiano yataendelea jioni kwenye tafrija ndogo niliyo waandaliaa”
Rahma alizungumza na waandishi wa habari, taratibu akaninyanyua kwenye kiti, tarataibu tukaanza kuelekea ndani, Rahma kwa utaratibu akanilaza kitandani na kuniwashia feni lililopo pembeni ya kitanda changu
“Eddy vumilia, mume wangu”
“Mbona imekuwa hivi, sielewi?”
“Mume wangu pumzika kwanza nitakujibu baadaye”
Rahma alianza kunibembeleza taratibu, akaniacha na kwenda nje kuendelea na maandalizi ya tafrija fupi aliyo iandaa, nikaanza hihisi harufu ya tofauti ndani ya chumba changu, na taratibu nikaanza kunyanyuka kitandani mwangu, huku nikiongozwa na pua zangu, kunusa ni wapi harufu hiyo inapo tokea.Nikaanza kusikia vikopo vya kuwekea ,afuta vilivyopo bafuni vikianguka,

“Ni nini?”
Nilijiuliza kwa maana ndani kwat hakuna panya wala paka anayeweza kufanya uharibifu kama huo.Nikaendelea kutembea kwa umakini hadi bafuni na kukuta vikopo vyote vya mafuta na sabuni zikiwa chini, harufu nayo sikuihisi ndani mwangu tena.Nikaanza kuokota kimoja baada ya kingine, nikiwa nimeinama nikastukia kuiona miguu ya mwanake nyuma yangu, kupitia kioo kilichopo mbele yangu ikiwa inavuja damu nyingi, nikasimama na kugeuka na kukutana na binti wa miaka kama kumi na nane akiwa anavuja damu mwili mzima
Macho yake ameyatoa kiasi kwamba anaonekana kubanwa na kitu kwenye koo lake,
“Ni…nisa..idie”
Alizingumza kwa shida sana kiasi kwamba nikabaki nikiwa nimeshangaa kwani sikujua ameingiaje ingiaje ndani kwet na istoshe sikujua ni kitu gani kilicho mpata
“Wewe ni nani?”
“Ni…saaa iii..dieee”
Aliendelelea kuzungumza kwa shida sana, nikajaribu kuuinua mkono wangu ili nimpe, nikajihisi uzito mkubwa sana kutoka kwenye mkono wangu


Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Askofu Malasusa aonya Watanzania kuhusu amani......akemea chuki, visasi

$
0
0
Watanzania wameaswa kuondoa roho za chuki na visasi, badala yake waishi kwa amani kwa sababu wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
 
Hayo yamesemwa leo Jumapili Aprili mosi 2018 na Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania ( KKKT),  Alex Malasusa wakati wa adhimisho la ibada ya Pasaka katika Kanisa la Azania Front jijini Dar es Salaam.
 
Dk Malasusa amesema Watanzania wanapaswa kufungua masikio na kusikia agizo la Mungu ili kulinda amani.
 
"Dunia ina mambo mengi, dunia ina kelele nyingi, fungua masikio na usikilize Mungu anakwambia nini na Roho Mtakatifu akikwambia nenda ukashuhudie atakuongoza kufuata yale uliyoyasikia yapate kutendeka katika maisha yako," amesema Dk Malasusa.
 
Amesema binadamu hapaswi kuishi kwa huzuni na manung'uniko, wala kukata tamaa katika maisha yake.
 
"Kuna watu wamezaliwa kuwapelekea wenzao hofu, lakini sisi Wakristo tumezaliwa na kuagizwa kuwaletea watu matumaini na kuhubiri amani," amesema Dk Malasusa.
 
Amesema wasije kutokea watu wakavuruga amani kwa kuwa itakuwa ni vigumu kuirejesha, hivyo Wakristo wanapaswa kusimamia maandiko katika kuhubiri amani na si kusikiliza maneno kutoka sehemu tofauti.
 
"Ndiyo maana tunafuatwa na kuambiwa tuhubiri amani kwa sababu wanaamini dini zina nguvu katika kuhubiri amani na rahisi waumini kuyasikiliza kama ilivyo kwa maandiko," amesema Dk Malasusa.

Halima Mdee kufikishwa mahakamani Jumanne Aprili 3

$
0
0
Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, anatarajia kufikishwa mahakamani Jumanne Aprili 3, kuungana viongozi wengine wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), akiwamo Mwenyekiti wake Freeman Mbowe, wanaoshtakiwa kwa makosa manane yakiwamo uchochezi, kuhamasisha maandamano na uasi.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema hayo leo na kuongeza kuwa mbunge huyo amekiuka masharti yaliyomtaka kuripoti kituo cha polisi pamoja na viongozi wengine saba wa chama hicho kabla ya kufikishwa mahakamani.

Halima alikamatwa leo Jumapili Aprili Mosi, saa tisa alfajiri katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), alipokuwa akirejea nchini akitokea Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu.

Aidha, alipoulizwa ni kwanini Halima amekamatwa wakati mawakili wake walikuwa wakitoa taarifa zake, Mambosasa amesema: “hayo ni maneno tu, anafahamu taratibu zikoje, anafahamau sheria zinasemaje kwa sababu wanatunga wenyewe huko bungeni hilo si suala la kujadili na mimi, asubiri atajibu hayo mahakamani.

Mambosasa amesema hayo muda mchache baada ya Chadema kulitaka Jeshi la Polisi kumpatia dhamana Mbunge ili aweze kuendelea na matibabu.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje ya chama hicho, John Mrema amesema licha ya kwamba Mbunge huyo kuwa mgonjwa ambaye hivi punde ametoka hospitali, lakini pia dhamana ni haki yake na lawama zote zitakuwa juu yao endapo afya ya mbunge huyo itatetereka.

“Hadi mchana wa leo Aprili Mosi, Jeshi la Polisi limeendelea kumshikilia Katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam na hajapatiwa dhamana pamoja na daktari wake kuwathibitishia polisi kuwa Mheshimiwa Halima ni mgonjwa.

“Tunasikitishwa na kulaani kitendo hiki cha polisi kuendelea, kumshikilia mgonjwa ambaye alikuwa amelazwa hospitalini, , tumetuma mawakili daktari wake lakini hawajafanikiwa mwisho, Jeshi la Polisi litawajibika kwa Watanzania endapo afya ya Halima Mdee ikitetereka au ikidhoofu zaidi na lawama zote zitakuwa juu yao,” amesema Mrema

Askofu Masangwa Akerwa Na Manabii Wa Uongo Wanaotoza Waumini Fedha Kuwaombea

$
0
0
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Kati, Dk. Solomon Masangwa amewataka waumini wa kanisa hilo kusimama katika imani zao wasidanganywe na manabii wa uongo wanaotoza waumini fedha.

Aidha amewataka waumini wa kikristo nchini kuishi kwa kuzingatia imani ya dini hiyo ili kuishi maisha yanayompendeza Mungu.

Dk. Masangwa ameyasema hayo leo Jumapili Aprili Mosi, mjini hapa alipokuwa akihubiri katika Ibada ya Pasaka iliyofanyika katika Usharika wa Mjini Kati Arusha na kuongeza kuwa kuna baadhi ya waumini ambao amewataka kuacha tabia ya kutanga tanga katika dini ambapo wamekuwa wakidanganywa na watu wanaojiita manabii na mitume.

“Kwanini mnakubali kudanganywa, siku hizi kuna watu wanajiita manabii, mitume na mnaenda kwao tena kwingine mnalipa kiingilio hata laki moja ili kumuona nabii au mtume,kwanini mdanganywe na mnasahau kusimama katika imani zenu,mnasahau ukombozi umepatikana kwa kifo na kufufuka kwa Yesu,” amesema.

Pamoja na mambo mengine, Askofu Masangwa amekemea vitendo vya uovu vinavyoendelea nchini ikiwamo mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi na wizi.

“Baadhi ya waumini wamekuwa wakitaka kuishi maisha mazuri, biashara zao kukua kwa kasi ambapo wengine wanajihusisha na imani za kishirikina zinazowafanya kujiingiza katika vitendo viovu.

“Kwanini mnakwenda kukata viungo vya albino au kumrusha mwenzao au kuiba, unakwenda kutafuta hirizi ili biashara ishamiriili maisha yawe mazuri mnasahau Yesu ni  bwana wa mabwana, Mungu ndiye anayetoa uwezo na nguvu za kuwa tajiri, mtegemeeni si waganga,” amesema.

Askofu Banzi: Tuwaheshimu Marehemu, Tusiwafunge Kwenye Viroba

$
0
0
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga, Mhashamu Anthony Banzi ameitaka jamii kuiheshimu miili ya marehemu kwa kuwapa maziko ya heshima badala ya kuwafunga kwenye viroba na kuwatupa kwenye maji.

Amesema jambo ambalo si zuri machoni kwa wanadamu na kwa Mwenyezi Mungu na pia inakiuka utamaduni wetu kama Watanzania ambapo ameitaka jamii kubadilika kwa vitendo vya namna kwani vinaondoa utu wao.

Ameyasema hayo leo Jumapili Aprili Mosi, wakati akitoa salamu za Pasaka kwa waumini wa kanisa hilo kwenye misa iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Anthony wa Padua, Chumbageni Jijini Tanga.

“Lazima tuwaheshimu marehemu katika nchi yetu, pengine tunataka kuwa na utamaduni tofauti wafu wengi tunaambiwa wameokotwa ndani ya viroba kwenye maji na kuzikwa, je hali hii inatupeleka wapi kama taifa” Tujitafakari kwa jambo hilo.

“Kama unavyoheshimika ukiwa mzima, marehemu pia wanapaswa kuheshimika hata wanapokuwa wamefariki kwa kuhifadhiwa mahali ambapo hawawezi kuonekana tena,” amesema.

Aidha, amewataka viongozi ambao wanajukumu la kulinda usalama wa nchi, kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani na utulivu ambayo ni tunu tulioachiwa na waasisi wa taifa hili.

“Mara nyingi tumesikia raia wema wametoa taarifa ya kukamatwa wahalifu hivyo ni jukumu la waliochaguliwa kutazama usalama wao kwa lengo la kuwawezesha kutimiza majukumu mengine ya kimaendeleo,” amesema Askofu Banzi.

Askofu Manase: Kila Kanisa Likitoa Waraka Wake Taifa Halitakalika

$
0
0
Askofu Mkuu wa Makanisa ya Babtisti Tanzania, Mchungaji Arnold Manase amewataka viongozi wa dini kushauri kwa namna njema bila kutabiria nchi mambo mabaya kwani ubaya huenea haraka kuliko wema.

Aidha, amesema kila dhehebu nchini likisimama na kutoa waraka wake taifa halitakalika.

Askofu Manase ameyasema hayo leo Jumapili Aprili Mosi, jijini Arusha wakati akitoa salam kwenye Ibada ya Pasaka katika Kanisa la Jerusalem Babtisti lilipo Ngarenaro mjini Arusha.

Kupitia Ibada hiyo, Askofu Manase amewaomba wadau wa amani nchini, ikiwamo Serikali kukaa na wadau ili kujadili mustabali wa taifa.

“Tunahitaji kuomba amani ya Mungu itawale, kama ambavyo Yesu Kristo alivyotuachia amani yake.

“Tukiwa kama viongozi wa dini kama kuna mambo tunaweza kushauri basi tuyashauri kwa namna njema tusitabirie nchi mambo mabaya Kwani ubaya unaenea haraka kuliko wema, nawasihi tuhubiri amani,” amesema Askofu Manase.

Pamoja na mambo mengine, Askofu Manase katika Ibada hiyo ameongoza maombi kuomba hekima kwa viongozi wa Serikali, madhehebu yote nchono ili hekima ya Yesu Kristo ikatawale kwenye mioyo yao.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya April 2


Mwenge wa Uhuru kuwashwa leo

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa mkoa wa Mwanza baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza Aprili 1, 2018 akiwa njiani kwenda Geita
 ************
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Aprili 2,2018 atawasha Mwenge wa Uhuru mkoani Geita.

Sherehe za kuwashwa Mwenge zinatarajiwa kuanza saa moja asubuhi hadi saa tano asubuhi katika kiwanja cha Magogo mjini Geita.

Mwenge wa Uhuru ambao utakimbizwa mkoani Geita kwa siku sita  utakabidhiwa mkoani Kagera Aprili 7,2018.

Mbio za Mwenge ambazo kauli mbiu kwa mwaka huu ni ‘Elimu ni ufunguo wa maisha, wekeza sasa kwa maendeleo ya Taifa zitahitimishwa Oktoba 14,2018 mkoani Tanga.

Waziri Mkuu Israel Alipongeza Jeshi kwa Kuwaua Wapalestina

$
0
0
Serikali ya Marekani imeweka kipingamizi juu ya muswada ulioletwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UN) Jumamosi ukitaka uchunguzi ufanyike juu ya Israeli kutumia risasi za moto dhidi ya Wapalestina walioshiriki katika maandamano katika Ukanda wa Gaza, kwa mujibu wa maelezo ya mwanadiplomasia wa Baraza hilo ambaye alilifahamisha shirika la habari la Ufaransa.

Vyombo vya usalama vya Palestina vimesema kwamba sio chini ya watu 15 waliuwawa Ijumaa na majeshi ya Israeli na zaidi ya watu 750 walitupiwa risasi za moto.

Wapalestina walizika maiti za watu wao Jumamosi, huku waombolezaji wakitangaza kulipiza kisasi.

Waziri Mkuu wa Israeli Benjamini Netanyahu aliyapongeza majeshi ya Israeli ambayo yalitupa risasi dhidi ya Wapalestina.

“Hongereni askari wetu,” waziri mkuu alisema katika tamko la serikali. “Israel inachukua hatua thabiti na kwa azma ya kulinda uhuru wake na usalama wa wananchi wake.”

Wapalestina walikuwa katika siku ya maombolezo ya kitaifa Jumamosi.

Shirika la habari la Associated Press (AP) limeripoti Jumamosi kuwa mmoja wa waandishi wake walishuhudia Wapalestina wawili, katika matukio mawili tofauti, ambao walikuwa wakitembea karibu na mpaka wa eneo lenye uzio la Ukanda wa Gaza linalotenganisha Israeli kutoka kwa Wapalestina. Wanajeshi wa Israeli waliwatupia risasi na kuwapata Wapalestina hao miguuni.

Katika tukio jingine, kijana wa miaka 16 ameiambia AP yeye alitupa mawe kuelekea katika mpaka huo siku ya Ijumaa na kutupiwa risasi zilizolenga miguu yote miwili. Kijana huyo alikuwa hospitali akitibiwa wakati mguu mmoja umefungwa bendeji na mwengine umetiwa vyuma, wakala wa habari wameripoti.

Credit: Voa

Jinsi Ya Kuandaa Na Kutayarisha Lishe Maalumu Ya Kuongeza Na Kunenepesha Mwili

$
0
0
Kama umekonda  na  kudhoofika  mwili  kutokana  na  sababu  mbalimbali  kama  vile kuugua  magonjwa  na  maradhi  mbalimbali  au  kupatwa  na  msongo  mawazo, basi  fuata  maelekezo  yafuatayo  ili  upate  kujua  namna  ya  kuandaa  na  kutayarishe  lishe  maalumu  ya  asili  itakayo  kusaidia kunenepa  na  kurejesha  afya  ya  mwili  wako  katika  hali  yake  ya  kawaida.

MAHITAJI:
1.    Dawa  Lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili

2.   Asali  ya  tende

3.   Ufuta

4.     Ukwaju

5.    Kitunguu  swaumu

6.   Giligiliani

7.    Juisi  ya  Komamanga na  Asali

MATAYARISHO  NA  MATUMIZI
Matumizi  ya  lishe  hii, yame  gawanyika  katika  awamu  kuu  mbili. Awamu  ya  kwanza, itachukua  siku thelathini  na  awamu  ya  pili  itachukua  siku  thelathini pia.

Katika  awamu  ya  kwanza , mgonjwa  atatumia  DAWA  LISHE  YA  KUNENEPESHA  MWILI, ASALI  YA  TENDE  NA  UFUTA  na  awamu  ya  pili, mgonjwa  atatumia   UKWAJU, KITUNGUU  SWAUMU, GILIGILIANI  na  JUISI  YA  KOMAMANGA  & ASALI  kwa  kufuata  utaratibu  utakao  elezwa  hapo  chini.

AWAMU   YA   KWANZA
SIKU   THELATHINI  ZA  KWANZA

Mahitaji

1.   Dawa  lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili

2.   Ufuta

3.   Asali  ya  Tende  (   Dates  Syrup )

MATAYARISHO  , MAELEKEZO  NA  MATUMIZI
1.   Dawa –Lishe  ya  Kunenepesha  Mwili

Chukua  vijiko   vitatu vikubwa  vyenye  dawa  yako, kisha  changanya  na  maji  nusu  lita halafu chemsha  hadi  itokote, Ikiisha  tokota, ipua  acha  ipoe  kidogo kisha  tumia  kunywa  pamoja  na  machicha  yake.  Utafanya  hivyo  mara  mbili  kwa  siku  asubuhi  na  jioni  kwa  muda wa  siku  thelathini.

2.   Ufuta : Matayarisho : Chukua  vijiko  vikubwa  vinane  vyenye  ufuta, kisha  changanya  na  lita  moja  na  nusu  ya  maji. Kama  hauna  tatizo  na  sukari, unaweza  kuongeza  na  sukari  kiasi ili  kuipa  ladha.  Ikisha  tokota, ipua iache  ipoe  kiasi  kisha  tumia  kula  ufuta wote  pamoja  na  supu  yake  ama  juisi  yake. Utafanya  hivyo mara  mbili  kwa siku  asubuhi  na  jioni  kwa  muda  wa  siku  thelathini.

(N.B:   KAMA  UNA  NAFASI,  BADALA  YA  KUTUMIA  VIJIKO  VINANE  TU VYA  UFUTA  KWENYE LITA  MOJA  NA  NUSU  YA  MAJI, WEWE  TUMIA  ROBO KILO  YA  UFUTA  KWENYE  LITA  TATU  YA  MAJI, CHEMSHA  HADI  ITOKOTE,  IACHE  IPOE, KISHA  TUMIA  KULA . FANYA  HIVYO  MARA  MBILI  KWA  SIKU  ASUBUHI NA  JIONI  KWA  MUDA  WA SIKU  THELATHINI )

2.   ASALI  YA  TENDE
3.   Tumia  kula  vijiko vikubwa  vinne  vya  tende  mara  mbili  kwa siku  asubuhi  na  usiku   kwa  muda  wa  siku  thelathini. Yaani  asubuhi  kula  vijiko  vikubwa vinne  na  usiku  kula  vijiko  vikubwa vinne  vya  asali  ya  tende.

( HABARI  NJEMA  KWA  WATEJA  WETU  NI  KWAMBA, ASALI  YA  TENDE  SASA  INAPATIKANA  MOJA  KWA  MOJA  DUKANI   KWETU . UTAPATIWA  DAWA  LISHE  PAMOJA  NA  ASALI  YA  TENDE  UTAKAYO  ITUMIA  KWA  MUDA  WA  SIKU  THELATHINI  KWA  UTARATIBU  WA  MAELEKEZO  HAYO  HAPO  JUU )
AWAMU   YA  PILI
Awamu  ya  pili  ya  lishe  hii, itaanza  baada  ya  kukamilika  kwa  siku  thelathini  za  kutumia  dawa  lishe, ufuta  pamoja  na  asali  ya  tende. Kama  ilivyo  kuwa  kwa  awamu  ya  kwanza, awamu  ya  pili  pia  itachukua  muda  wa  siku  thelathini

MAHITAJI, MATAYARISHO   NA  MATUMIZI

1.  UKWAJU
Matayarisho na  Maandalizi
Chukua ukwaju  kiasi  cha  robo kilo , weka  kwenye  maji  kiasi  cha  lita  moja, ongeza pilipili  manga kiasi cha  kijiko kimoja kidogo  ( tea spoon ) halafu ongeza sukari  vijiko  vitatu vikubwa, ongeza karafuu  ya unga  kijiko kimoja kidogo, pamoja  na hiriki vijiko  vikubwa  viwili.

Ukisha  fanya  hivyo, chemsha  hadi  mchanganyiko  wako  utokote. Ukisha  tokota, ipua  na  kuchuja  kisha  weka  kwenye  chombo  kisafi.

MATUMIZI :
Tumia  kunywa  mchanganyiko  huu kila  siku  asubuhi  baada  ya  kunywa  chai. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo.

2.   JUISI   YA  KOMAMANGA  NA  ASALI
Matayarisho  na  Matumizi

Tayarisha  juisi  ya  komamanga  kiasi  cha  nusu  lita, changanya  na asali ya  kawaida  vijiko vikubwa    vinane, kisha  ongeza  chumvi kijiko kidogo( tea spoon)

Koroga  mchanganyiko  wako  halafu  tumia  kunywa. Utafanya  hivyo  mara  moja   kwa  siku kwa  muda  wa  siku thelathini.

Matunda  ya  makomamanga  yanapatikana  masokoni, ingawa  mara  nyingi  hupatikana  kwa  uchache. Kama  utabahatika  kupata matunda  mengi, basi  unashauriwa  kuyachukua  kwa  wingi  na  kuyahifadhi, sehemu  salama ili usipate  usumbufu  wakati  wa  kutumia  tiba  yako.

Mbali  na  kutumika  katika lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili, tunda  la  komamanga, linasaidia  kuondoa  harufu  mbaya  ya  kinywa. Kwa  kuondoa  harufu  mbaya  ya  kinywa, kula  walau  tunda  moja  la  komamanga  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo. Utapata  matokeo  mazuri . ( HII  ITAWASAIDIA  ZAIDI  WALE  AMBAO  TATIZO  LAO  LA  KUTOKWA  NA  HARUFU  MBAYA  YA  KINYWA  LIMEANZIA  KINYWANI  NA  SIO  TUMBONI

ALTERNATIVE (MBADALA )  WA JUISI  YA  KOMAMANGA  ILIYO  UNGWA  NA  ASALI.

Kama  utashindwa  kupata makoma manga, basi  utafanya  kama  ifuatavyo :

KITUNGUU  SWAUMU
Chukua punje  nne  za  vitunguu  swaumu, zitwange kisha  tia  kwenye  maji nusu lita halafu ongeza  juisi  ya  ndimu  moja  au  limao  moja kisha  chemsha hadi mchanganyiko  wako  uchemke.

Matumizi :  Tumia  hivyo kila  siku  usiku baada  ya  kula  chakula cha  usiku. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku  thelathini mfululizo.

AU
Vile vile , mbadala  mwingine wa  kutumia  juisi  ya komamanga  iliyo  changanywa  na  asali, unaweza  kutumia  JUISI  YA  GILIGILIANI  kwa  kufuata  utaratibu  ufuatao :

JUISI   YA   GILIGILIANI
MATAYARISHO   NA   MATUMIZI YA  JUISI  YA  GILI GILIANI

Chukua giligiliani  fresh, kisha zi -blend ( ZISAGE ) ili  kupata  juice  yake  kiasi  cha  robo  lita.

 Ndani  ya  juisi  yako  ya  giligiliani, kamuliamo ndimu fresh moja, halafu  ongeza  chumvi  kiasi robo  kijiko  kidogo ( tea spoon), koroga  kisha  tumia  kunywa.  Utakunywa  usiku  baada  ya  kula  chakula  cha  usiku. Utafanya  hivyo mara   moja  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo.

PIA : Jenga  utaratibu  wa  kuwa  unakula    giligiliani kwa wingi. Hakikisha  katika  kila  mlo  wako, inakuwepo  mboga  ya  giligiliani  pembeni.

VITU   VINGINE VYA   KUZINGATIA..
Pamoja na kutumia  lishe  hii  ya  asili  kwa  kufuata  utaratibu  huo  hapo  juu, unashauriwa  kuzingatia  matumizi  ya  vyakula  vifuatavyo:

TANGAWIZI
Jenga  tabia  ya  kuwa  una tumia  tangawizi, kila  mara  upatapo  nafasi.  Utaratibu  wa  jinsi  ya  kutayarisha  tangawizi ni  kama  ifuatavyo :

Chukua kipande  kimoja  cha  tangawizi, kisha  kitwange  halafu ongeza  vikombe  viwili vya  maji  vyenye  ujazo  wa  milimita  mia  mbili  na  hamsini ( 250 mills). Chemsha pamoja  kisha ongeza  maziwa  kiasi cha  robo lita  na  sukari ili kupata  ladha.  Fanya  hivi  kila  mara  uapatapo  nafasi. Ukiweza kufanya  hivyo walau  mara  mbili  kwa  siku, itakuwa  vizuri  zaidi.

  AU  chukua  kipande  kimoja  cha  tangawizi, kitwange kisha  chemsha pamoja  na  chumvi nusu  kijiko  kidogo  kwenye  maji kiasi  cha  nusu   lita  halafu tumia  kunywa  kikombe  kimoja  nusu  saa  kabla  ya  kula  chakula chako  cha  asubuhi, mchana  na usiku.

HIRIKI
Jenga utaratibu  wa  kuwa  unakunywa  mara  kwa  mara  chai  iliyo  changanywa  na  hiriki.

MACHUNGWA
Jenga utaratibu  wa  kuwa  unakula  machungwa kwa  wingi,  kwa  kadri utakavyo  weza. Unashauriwa  kuwa  unachanganya na  chumvi  kidogo  pamoja  na  pilipili  manga.

KWA  MAHITAJI  YAKO  YA  DAWA-LISHE  YA  KUNENEPESHA  & KUONGEZA  MWILI  PAMOJA  NA  ASALI  YA  TENDE.

Kwa  mahitaji  yako  ya  DAWA-LISHE ya  kuongeza & kunenepesha  mwili, pamoja  na  asali  ya  tende, fika  katika  duka  la  NEEMA  HERBALIST.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM, jirani  na  SHULE  YA  MSINGI   UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA  0766 53 83 84.

Kwa wateja  wetu  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam, ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  dukani  kwetu  Ubungo, tunayo  huduma  ya  kuwapelekea  dawa  mahali  walipo ( HOME & OFFICE  DELIVERY  )

Kwa wateja  waliopo  nje  ya  mkoa   wa  Dar  Es  Salaam,  watatumiwa  dawa  kwa  kutumia  mabasi  mbalimbali.

Kwa  wateja  waliopo  Zanzibar, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti.

Kwa  wateja  waliopo  ughaibuni, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

Na kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee  kila  siku  katika  blogu  yetu :

Waziri Mkuu: Mwanza Endeleeni Kusajili Wanunuzi Wa Pamba

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza viongozi wa mkoa wa Mwanza kuendelea na usaji wa wanunuzi wa zao la pamba na wawape fursa ya kuchagua maeneo wanayotaka kununua pamba.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumapili, Aprili 01, 2018) alipozungumza na viongozi mkoa wa Mwanza baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege  wa Mwanza akiwa njiani kuelekea mkoani Geita.

Waziri Mkuu leo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za kuwasha mwenge wa Uhuru zitakazofanyika mkoani Geita. Kauli mbiu ya mbio za mwenge kwa mwaka huu ni ‘Elimu ni ufunguo wa maisha, wekeza sasa kwa maendeleo ya Taifa letu.’

Waziri Mkuu alisema wakati viongozi hao wakiendelea na usajili wa wanunuzi wa pamba ni vema wakawapa nafasi ya kuchagua maeneo watakayohitaji kukunua kwa sababu yanaweza kurahisishia usafirishaji.

Hata hivyo, Waziri Mkuu aliwasisitiza viongozi hao kuendelea kusimamia na kufuatilia maendeleo ya zao hilo kwa umakini zaidi ili kuweza kubaini changamoto zitakazojitokea na kuzipatia ufumbuzi kwa wakati.

Alisema kutokana na mwenendo wa hali ya hewa mwaka huu wakulima wa zao la pamba wanatarajiwa kuvuna pamba nyingi, hivyo ni vema ukatengenezwa utaratibu utakaomrahisishia mkulima kutoa mazao shambani na kufikisha mnadani.

Waziri Mkuu alisema utaratibu huo wa kutoa mazao shambani na kupelekwa mnadani kwa wakati ni muhimu kwa sababu utasaidia katika kulinda pamba ili isipoteze ubora wake.

Zao la pamba ni miongoni mwa mazao matano ya biashara ambayo Serikali imeamua kuyapa kipaumbe kwa kuyafuatilia kuazia hatua za awali za utayarishaji wa mashamba, pembejeo pamoja na uuzaji. Mengine ni korosho, chai, kahawa na tumbaku.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, APRILI 02, 2018.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images