Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

TANGA RAHA- Sehemu ya Arobaini na Tano ( 45 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Nikabaki nikiwa nipo kimya, kama nimemwagiwa maji ya baridi, swali la kwanza kujiuliza kichwani ni mbinu gani waliyo itumi hadi mimi leo nipo hai.Nikiwa ninaendelea kuliwazia ninalo liwaza nikamuona Olvia Hitler akiwa amesimama nyuma ya Rahma huku macho yake yakimwagikwa na machozi ya damu

ENDELEA
Nikabaki nikiwa nimeduwaa, pasipo kuzungumza kitu chochote, Olvie akaanza kutingisha kichwa taratibu huku machozi ya damu yakiendelea kumwagika kwa wingi, akauinua mkono wake mmoja na kuanza kuniita taratibu, hapa ndipo nilipoiona mkono wake ukiwa umejaa damu nyingi.
“Walipo niambia kwamba umekufa, ikanilazimu kufanya kitu ambacho kingeurudisha uhai wako, kutokana sikuhitaji uweze kupotea kiurahisi maishani mwangu, wakati bado sijaisha nawe vya kutosha”
Hata Rahma alicho kizungumza sikukitilia maanani kwa maani macho, na akili yangu zote zilikuwa zipo kwa Olvia aliye simama nyuma ya mke wangu Rahma.Olvia Hitler akaunyanyua mkono wake wa pili juu na kuendelea kuniita kwa ishara kiasi kwamba nikazidi kuchanganyikiwa kwa vitendo vyake

“Niliamua kwenda, India kwa wanganga wanao tumia nguvu za kienyeji.Ambapo kuna mganga mmoja ambaye ni maarufu sana aliweza kunisaidia sana, hadi akaurudisha uhai wako”
Nikayahamishia macho kwa Raham, kisha nikayarudisha tena macho yangu kwa Olvia Hitler
“Mganga yule, alikupandikiza roho ya nyoka, na kila katikati ya mwaka na mwisho wa mwaka nilazima ugeuke kuwa.......”
Rahma alisita kidogo kuzungumza kitu anacho kizungumza na nikabaki nikiwa nimemtazama kwa umakini
“Utageukuwa kuwa nyoka mkubwa, na ninatakiwa kukupa watu wawili, uwale ili uweze kuongeza maisha ya kuishi la sivyo utakufa kabisa na nitakukosa mume wangu”
Rahma alizungumza huku akimwagikwa na machozi, nikaanza kujitazama kiungo kimoja baada ya kingine kwa maana sikuamini kama hapa mimi nilipo nimekuwa na pumzi ya nyoka.Olvia Hitler akapiga hatua moja nyuma kisha akasogea hatua nyingine moja kushoto, hapo ndipo nikamshuhudia utumbo wake ukiwa umechomoza nje, na ameushika na mkono mmoja ili usiguse chini
“Eddy”


AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 71 na 72 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA-
0657072588
ILIPOISHIA 
Baba alizungumza, wasichana hao wakanishika mikono, na kuanza kuondoka na mimi, huku baba akinikonyeza. Tukaingia kwenye moja ya chumba kilicho puliziwa manukato mazuri sana, huku kukiwa na kitanda kikubwa pamoja na sofa kubwa.
Wasichana hawa wakanisukuma kitandani na kuanza kunivua nguo moja baada ya nyingine hadi nikabaki kama nilivyo zaliwa. Wakaanza kuninyonya jogoo wangu huku mikono yao ikiwa inakatiza sehemu mbalimbali za mwili wangu. Nikiwa katika raha hii ambayo kila mwanaume huipenda, akaingia baba akiwa na kipande cha sigara mkono, nikataka kujifunika shuka kutokana na aibu.
“Endelea nahitaji kuona jinsi unavyo....msichana”
Kauli ya baba ikanifanya tubaki tumetazamana, kama kawaida yake akanikonyeza kuzidi kuniruhusu niwashuhulike wasichana hawa wenye hamasa kitandani.

ENDELEA
Wasichana hawa wakawa kama wamezidishiwa kasi ya kucheza ya jogoo wangu, kila mmoja akawa na utaalamu wake wa kunyonya jogoo wangu. Kwa macho ya kuiba nikamuona jinsi baba anavyo tingisha kichwa akikubaliana na mapigo ya mabinti hawa wanao hitaji kupata sifa mbele ya bosi wao. Nikashusha pumzi nyingi, kisha nikanyanyuka na kushuka kitandani huku jogoo wangu akiwa amesimama.
“Baba swezi kufanya hivi mbele yako?”
“Kwanini?”
“Baba umeona wapi mtoto akifanya mapenzi mbele ya baba yake”

Baba akanitazama usoni jinsi ninavyo zungumza kwa msisitizo, akanyuka kwenye sofa alilo kalia na kuanza kupiga hatua za taratibu hadi sehemu nilipo simama.

Bavicha kula Pasaka mahabusu na kina Mbowe

$
0
0
Viongozi wa Baraza la Vijana Chadema (Bavicha) kesho watasherehekea Sikukuu ya Pasaka kwa kuwatembelea viongozi wa chama hicho waliopo magerezani.

Mwenyekiti wa Bavicha, Patrick Ole Sosopi ataongoza msafara wa viongozi wa baraza hilo watakaokwenda Segerea kumtembelea Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe na wenzake.

Amesema wamefikia uamuzi huo kwa lengo la kwenda kuwatia moyo na kuwa nao pamoja.

Amesema viongozi wengine watakwenda Mbeya kwa ajili ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na Katibu wa Chadema, Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga.

"Tunataka kusherehekea nao Pasaka na kuwafahamisha kuwa chama kinaendelea, hatuwezi kurudishwa nyuma wala kutetereshwa,"amesema.

Ole Sosopi pia amewataka vijana wa baraza hilo kuwa tayari kupambana kwa ajili ya chama.

Amesema; "Kuna mambo mengi yanaendelea na tunafahamu wazi kuna ajenda ya kutaka kukifuta Chadema, sasa nawaambia hakuna namna chama hiki kitafutwa, tupo imara na tunazidi kuimarika,'

“Vijana kazi yetu ni kulinda chama na kazi hiyo tutaifanya kwa nguvu zote bila woga, hatutaogopa kufa," amesema.

Profesa Kitila asema maudhui ya waraka wa maaskofu hayaakisi wajibu na msingi wa kanisa

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo amemwandikia barua Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Askofu Frederick Shoo akitoa maoni yake binafsi kwa kanisa hilo kuhusu maudhui ya waraka wa maaskofu wa kanisa hilo uliotolewa hivi karibuni.

Waraka wa maaskofu 27 wa KKKT ulitoka hivi karibuni na ulitarajiwa kusomwa katika makanisa yote ya kilutheri Machi 25, 2018.

Katika waraka huo maaskofu walizungumzia  Katiba mpya, uchumi, siasa na jamii.

“Katika kutoa maoni yangu kuhusu Waraka huo, ninalenga mambo makubwa mawili ambayo ni pongezi kwenu, na pili ni mtazamo wangu juu ya baadhi ya masuala yaliyomo katika Waraka huo,” amesema Kitila katika barua yake aliyoisaini Machi 29 mwaka huu.

Pamoja na kuwapongeza maaskofu hao, Kitila ameandika katika barua yake kuwa maudhui yaliyowekwa katika waraka wa maaskofu hao, hayaakisi hadhi na wajibu wa msingi wa kanisa.

“Kama ambavyo mmekuwa mkitufundisha siku zote, na vile tusomavyo katika Biblia Takatifu, ninafahamu kuwa kazi za msingi za kanisa ni zile ambazo Bwana wetu Yesu Kristo alizifanya alipokuwa duniani,”amesema.

Kitila ambaye ameandika barua hiyo kama muumini wa KKKT, amesema anakubaliana na mengi maaskofu waliyogusia katika Waraka huo akiamini yamefundisha na kuponya roho za waumini kwa kiasi kikubwa.

Hata hivyo, alichambua hoja katika maeneo matano zilizoibuliwa na maaskofu hao na kusema ni sahihi lakini akatahadharisha kuwa ni muhimu kwa kanisa kujiepusha na kuonekana lipo upande fulani katika mijadala ya kitaifa inayogusia jamii.

“Kwa kufanya hivyo, mtaepusha migawanyiko isiyo ya lazima kwa waumini ndani ya kanisa na wananchi kwa ujumla.” Amesema.

Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa kanisa kupima kwa umakini mkubwa uzito wa kila neno kabla ya kutoa kauli katika umma.

“Ni hatari kwa Kanisa kutoa kauli inayosababisha maumivu na mifarakano badala ya kuponya.”

Mpiga picha wa Diamond ajibu kufukuzwa WCB

$
0
0
Baada ya Mpiga Picha wa Diamond Platnumz ‘Kifesi’ kutangaza kuacha kazi hiyo, kumeibuka stori kuwa Kifesi amefukuzwa kazi kitu ambacho amekikanusha vikali.

Kifesi amesema taarifa zinazodai kuwa amefukuzwa kazi hazina ukweli wowote na kilichotokea ni maamuzi yake binafsi.

“Hapana sijawahi kuachishwa kazi, kama niliachishwa basi niliachishwa pasipo kupewa taarifa, ninachofahamu nimechukua maamuzi haya na ni kitu ambacho nilikuwa nimepanga kufanya kutoka siku nyingi, so jana nikasema i think it right time to do this,” Amesema Kifesi

Pia amejibu kuhusu kuingilia masuala ya Diamond na Zari ndiko kumepelekea hayo, Kifesi amejibu; “Kumtetea zari sijaanza leo, ukiangalia Instagram kuna posti za zamani nilikuwa nafanya hivyo lakini ni suala gumu kulielezea”.

Dada wa Diamond, Ema Platnumz baada ya kusikia taarifa za Kifesi kuacha kazi, kwenye moja ya post Instagram ali-comment; “Acha uongo Kifesi umefukuzwa kwa kuacha kazi na kufuatilia maisha ya bosi wako yametushinda sie wee mtu baki utaweza”.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya April 1

TFF Hatimaye Yasikiliza Rufaa Ya Wambura Sasa Yasubiri Maamuzi Ya Kamati Ya Maadili Kutoa Hukumu

$
0
0
 Ile rufaa inayomhusu aliyekuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Michael Richard Wambura, imesikilizwa jana kwa pande zote mbili kukutana katika makao makuu ya shirikisho hilo yaliyopo mitaa ya Karume, Ilala.

Kwa mujibu wa Wakili wa Wambura,Emmanuel Muga, amesema pande zote mbili zimemaliza vizuri kikao hicho na mambo yamekwenda sawia, kinachosubiriwa tu sasa ni maamuzi ya Kamati ya Maadili kutoa hukumu.

Muga ambaye anamtetea Wambura, ameeleza TFF wamesikiliza kwa umakini utetezi wa Wambura vilevile TFF nao wakizungumza ya kwao kuhusiana na mustakabali mzima wa kesi hiyo.

Wambura alikata rufaa kupinga kufungiwa kujihusisha na soka baada ya TFF kumfungia kwa madai ya kufanya ubadhirifu wa fedha za shirikisho hilo pamoja na makosa mengine.

Kamati ya Maadili itakaa na kuandaa rasmi na majibu ya hukumu juu ya rufaa hiyo iliyosikilizwa jana Jumamosi.

Mama aliyejifungua mapacha wawili wenye baba tofauti

$
0
0
Katika hali ya kushangaza huko nchini Uganda, wanaume wawili na watu wengine wamejikuta kwenye mshangao baada ya kukuta wote wawili ni baba wazazi wa watoto wawili mapacha.

Inaelezwa kuwa wanaume hao waliingia kwenye mgogoro siku za hivi karibuni kila mtu aking’ang’ania kuwa baba mzazi wa mapacha hao, na ndipo walipoamua kwenda hospitali ili kupima kipimo cha DNA.

Hatahivyo matokea ya daktari yalionesha kuwa wanaume hao wote wawili ni baba halali wa mtoto mmoja wa mapacha hao, yaani kila mmoja ana mtoto mmoja kati ya mapacha hao.

Inaeelezwa kuwa wanaume hao Joseph Baseka Sengendo, 25, na Patrick Ssegane, 30, wamezaa na Rashida Nakabugo, ambapo Sengendo anatajwa kuwa mume wa ndoa wa mwanamke huyo.

Wanaume hao wanasemekana kuwa ni ndugu.

Katibu wa Bunge Azungumzia Ajali ya Wabunge 6

$
0
0
Katibu wa Bunge, Steven Kagaigai amesema chombo hicho cha dola kinafuatilia kwa ukaribu ajali ya wabunge sita iliyotokea jana usiku, Machi 29, 2018 mkoani Morogoro.

Kagaigai amesema baada ya kupokea taarifa hizo wamefanya mawasiliano na uongozi wa Hospitali ya Morogoro na walishauriwa kuwahamishia Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

“Ndiyo taarifa hizo ninazo, wamepata ajali huko Morogoro, tayari tumeshafanya taratibu za kuwapeleka Muhimbili kwa huduma zaidi na ofisi yetu inawajibika kwa kila hatua,” amesema Kagaigai.

Wabunge hao ambao wote ni kutoka Zanzibar ni Haji Ameir Haji (Makunduchi), Khamis Ali Vuai (Mkwajuni), Bhagwanji Maganlal Meisuria (Chwaka), Makame Mashaka Foum (Kijini), Juma Othman Hija (Tumbatu).

Waziri Mkuu Awaomba Viongozi Wa Dini Wapiganie Na Kuilinda Amani

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaomba viongozi wa dini popote walipo wahakikishe wanaipigania na kuilinda amani kwa kila hali ikiwa ni pamoja na kupambana na viashiria vya uvunjifu wa amani.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana (Jumamosi, Machi 31, 2018) kwenye Mkutano Mkuu wa BAKWATA uliofanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma, ambapo amesisitiza kuwa ni muhimu wasaidizi wa Mufti wakasimamia suala hilo.

“Dini ni taasisi muhimu sana kwa maisha yetu ya kila siku ndio maana Serikali inaheshimu na kuzitambua dini zote kutokana na mchango wake mkubwa katika amani ya nchi yetu. Niwaombe viongozi wangu popote mlipo muilinde amani yetu”

Waziri Mkuu amesema amani ni miongoni mwa neema kubwa sana kwa binadamu na ndio maana wote wanamtambua Mwenyezi Mungu, hivyo wasiruhusu mtu au kikundi chochote kujaribu kuchafua na kuharibu amani iliyopo nchini.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewasisitiza viongozi Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) wahakikishe kuwa chombo hicho kinaendelea kuwaunganisha waislamu bila ya kujali makabila yao, rangi zao au madhehebu yao.

Waziri Mkuu amesema Mufti wa Tanzania Sheikh Aboubakar bin Zubeiry ambaye ndiye kiongozi wa Waislamu nchini mara zote amekuwa akisisitiza jambo hilo na kuwataka waislamu popote walipo watambue kuwa hicho ni chombo chao.

“Ni muhimu sana kwa ninyi wasaidizi wa Mufti mlio kusanyika hapa muhakikishe mnalisimamia hili katika maeneo yenu. Katika hili napenda kuwahakikishia kuwa Serikali yenu iko pamoja Mheshimiwa Mufti kutekeleza nia hiyo njema.”

Amesema ahadi ya Rais Dkt. Magufuli ni kuwa Serikali anayoiongoza ipo tayari kusikiliza maoni, ushauri na  mapendekezo yeyote kutoka kwa viongozi wa dini . ‘Milango iko wazi saa zote ‘

Ameongeza kuwa yeye si mtaalamu sana kama walivyo Masheikh hao lakini anakumbuka maneno ya Mwenyezi Mungu ndani ya Qur’ani sura Al Imran aya ya 103 yanayosema “ Shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote na wala msifarakane”

Mkutano huo umehudhuriwa na  Sheikh Mkuu wa Mufti wa Tanzania Sheikh Zubeir, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, wajumbe wa Baraza la Ulamaa, Masheikh na viongozi wa BAKWATA wa mikoa na wilaya zote Tanzania.

Jeshi la Polisi lamkamata Halima Mdee Airport akitokea Afrika Kusini kwenye matibabu

$
0
0
Jeshi la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee.

Mdee amekamatwa leo alfajiri uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea nchini Afrika Kusini inakoelezwa alilazwa kwa matibabu.

Meya wa Ubungo, Boniface Jacob amethibitisha  kukamatwa kwa Halima Mdee ambapo amesema; "Ni kweli amekamatwa leo Saa 9 alfajiri  Airport, akitokea Afrika Kusini alipokuwa amelazwa kwa matibabu na sasa yupo Central."

Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) huenda akaunganishwa na vigogo wengine sita akiwamo Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe katika kesi inayowakabili.

Vigogo hao wengine tayari wamekwisha kupandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, Dar es Salaam na kusomewa mashtaka nane.

Kukamatwa kwa Mdee kunafikisha watuhumiwa saba kati ya nane  ambao wamekwisha kuhojiwa mwingine ambaye bado na huenda anatafutwa na jeshi hilo ni mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche.

Isome HAPA Barua ya Profesa Kitila Mkumbo Kwenda kwa Mkuu wa Kanisa la KKKT Ikipinga Waraka Wao

$
0
0
Baba Askofu Dkt. Fredrick Shoo,
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)
S. L. P. 3033
ARUSHA.

Mheshimiwa Baba Askofu, Shalom!

YAH: MAMBO MATANO AMBAYO HAYAPONYI KATIKA WARAKA WA MAASKOFU WA KKKT

Jina langu ni Kitila Mkumbo, muumini katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), ambalo wewe ndiye mkuu wake. Kikazi, mimi ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Dodoma. Kitaaluma, mimi ni mhadhiri mwandamizi katika Saikolojia na Elimu nikiwa na cheo cha Profesa mshiriki katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mheshimiwa Baba Askofu, kwa unyenyekevu mkubwa nimeamua kukuandika barua hii ili kutoa maoni yangu binafsi kwa kanisa unaloliongoza kupitia kwako kuhusu maudhui ya waraka uliotolewa na waheshimiwa maaskofu wa KKKT siku ya Jumamosi tarehe 24 Machi 2018. Waraka huo ulitarajiwa kusomwa katika makanisa siku ya Jumapili tarehe 25 Machi 2018. Katika kutoa maoni yangu kuhusu waraka huo, ninalenga mambo makubwa mawili ambayo ni pongezi kwenu, na pili ni mtazamo wangu juu ya baadhi ya masuala yaliyomo katika waraka huo.

Mheshimiwa Baba Askofu, kwa dhati kabisa ninawapongeza sana kwa kujali na kwa utayari wenu katika kuzungumzia na kuchambua kwa kina mambo muhimu ya kijamii, kisiasa na kiuchumi yanayogusa moja kwa moja uhai na haki za kibinadamu za waumini wa KKKT na Watanzania kwa ujumla. 

Aidha, ninawapongeza sana kwa ujasiri na kwa kutumia vizuri nafasi zenu katika kanisa na jamii ya Watanzania katika kuyatolea kauli mambo yanayogusa masilahi mapana ya nchi yetu. 

Kupitia waraka huo, mmetimiza ipasavyo majukumu yenu ya msingi kwa jamii. Binafsi ninaamini kuwa pamoja na kwamba ninyi ni viongozi wa kiroho, bado mnayo nafasi kubwa katika kuchangia maendeleo ya nchi yetu kisiasa, kijamii na kiuchumi kwani mambo yote hayo yana uhusiano wa moja kwa moja na afya ya kiroho.

Mheshimiwa Baba Askofu, mbali ya pongezi hizo, nina maoni kwenu ninyi viongozi wetu wa kiroho katika mambo kadhaa yaliyobainishwa kwenye waraka, ambayo ninaona kuwa maudhui yake hayaakisi hadhi na wajibu wa msingi wa kanisa. 

Kama ambavyo mmekuwa mkitufundisha siku zote, na vile tusomavyo katika Biblia Takatifu, ninafahamu kuwa kazi za msingi za kanisa ni zile ambazo Bwana Yesu Kristo alizifanya alipokuwa duniani. Kazi hizo ni kuhubiri habari njema (injili), kufundisha waumini ambao ni sehemu ya jamii na kuponya wenye shida mbalimbali kijamii, kimwili na kiroho.

 Ninaamini kuwa ninyi viongozi wetu wa kanisa ni warithi wa kazi hizo wenye wajibu wa kuziendeleza hapa duniani. Inatarajiwa kuwa maneno na matendo yenu ndani na nje ya kanisa yatakuwa yenye mwelekeo wa kutekeleza kazi hizo ambazo matokeo yake ni uponyaji wa jamii na kuleta matumaini ya kimaisha, kiroho na kimwili.

Mheshimiwa Baba Askofu, katika waraka wenu mmetoa maoni katika maeneo 18 ambayo mmeyagawanya katika maeneo makuu matatu (jamii na uchumi; maisha ya siasa na masuala mtambuka). Kwa ujumla, ninakubaliana na mengi mliyogusia katika waraka huo na ninaamini yamefundisha na kuponya roho zetu kwa kiasi kikubwa, hasa kipingele cha tano (v) mnapozungumzia masula mtambuka pale mnaposema: “Uhai wa mtu una thamani isiyopimika. Ni wajibu usiokwepeka kuulinda na kuutunza uhai kwa vitendo halisi. Endapo uhai umepotea katika mazingira yoyote, uchunguzi huru na wa haki ufanyike na taarifa zitolewe kwa wakati muafaka ili kujenga jamii yenye imani kwa Serikali na vyombo vyake”. 

Hata hivyo, yapo maeneo matano (5) muhimu mliyoyatolea kauli ambayo, kwa maoni yangu, hayaponyi bali yanaleta mkanganyiko zaidi kwa jamii kwa kuwa hayakujengwa katika msingi wa mantiki na ushahidi wa neno la Mungu, wala kuzingatia mantiki na ushahidi wa kisayansi, ambayo siku zote yamekuwa ni msingi wa hoja za KKKT.

Mheshimiwa Baba Askofu, baada ya maelezo hayo ya utangulizi, naomba sasa niyabainishe maeneo hayo matano ambayo ninaamini kuwa mngejipa nafasi ya kutafakari kwa kina zaidi msingeyatolea kauli au mngeyatolea kauli kwa namna nyingine.

1.Kuhusu uhuru wa Bunge, Mahakama na Tume ya Uchaguzi
Mheshimiwa Baba Askofu, katika kujadili maisha ya siasa, katika hoja yenu ya nne (4), mmeeleza kwamba kuna “kubanwa na hatimaye kuelekea kupungua kwa uhuru wa Bunge, Mahakama na Tume ya Uchaguzi”. 

Maoni haya siyo mageni na yamesambaa mtaani na hasa miongoni mwa viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani. Hata hivyo, maoni kama haya yanapotolewa na ninyi viongozi wetu wakuu wa kiroho yanakuwa na mwangwi tofauti katika jamii. 

Suala hili la uhuru wa Bunge na Mahakama ni mjadala wa kudumu katika siasa duniani kote. Hii inatokana na ukweli kwamba hakuna kigezo kimoja kilichokubalika duniani kote cha kupima uhuru wa Bunge na Mahakama. Kila jamii au upande una tafsiri yake kutokana na muktadha wa nchi husika.

Mheshimiwa Baba Askofu, labda nifafanue hoja yangu kwa kutumia mfano wa Bunge. Katiba yetu ipo wazi kwamba Bunge ndicho chombo cha mamlaka ya juu (supreme) katika mihimili mitatu ya dola nchini mwetu. 

Aidha, katika mfumo wa vyama vingi, Bunge huongozwa kwa msingi wa demokrasia ya wachache wasikilizwe lakini wengi waamue. Katika Bunge letu la sasa, idadi ya wabunge wa chama kinachounda Serikali yaani CCM, ni zaidi ya theluthi mbili ya idadi ya wabunge wote. 

Hii inamaanisha kuwa, kwa mujibu wa Katiba yetu na sheria zake, kwa Bunge hili wabunge wa CCM ndiyo wenye haki ya maamuzi kutokana na idadi yao. Kwa sababu hii, kama kuna tatizo katika mfumo wa maamuzi wa Bunge letu, tatizo la msingi haliwezi kuwa kukosekana kwa uhuru wa Bunge kwa kuwa Katiba yetu imetoa uhuru wa kutosha kabisa kwa chombo hiki. Ingekuwa ni tatizo kama kuna siku Bunge lingekuwa limeamua kinyume cha matakwa na maamuzi ya walio wengi ndani ya Bunge.

2.Kuhusu wanasiasa kuhama vyama
Mheshimiwa Baba Askofu, eneo la pili ambalo nina maoni tofauti ni katika hoja yenu ya saba linalohusu maisha ya siasa. Katika eneo hili hoja yenu ya msingi ni kwamba kuna udhalilishaji wa kauli njema isemayo “maendeleo hayana chama”. Waheshimiwa Maaskofu mnadai kuwa “udhalilishaji huu unafanyika kwa njia ya kutumia fedha nyingi katika chaguzi ndogo zinazotokana na watu wanaobadili vyama ili kuleta maendeleo”. Mmeendelea kujenga hoja kwa kujiuliza, “kama maendeleo hayana chama, kwa nini mtu anajiuzulu chama fulani eti kwenda kingine?”

Mheshimiwa Baba Askofu, katika utangulizi wa waraka wenu, mmeeleza vizuri sana kuhusu umuhimu wa kudumisha mfumo wa vyama vingi. Hata hivyo, kwa maoni yangu, kauli yenu niliyoinukuu hapo juu haikuzingatia ipasavyo utamaduni unaoambatana na mfumo wa vyama vingi. 

Duniani kote, pamoja na mambo mengine, utamaduni wa mfumo wa vyama vingi huambatana na watu kuhama vyama kila wanapojisikia kufanya hivyo. Vyama vya siasa ni taasisi ambazo wanachama wake wapo huru kuingia na kutoka bila kutakiwa kujieleza kwa mtu yeyote yule ilimradi katika kufanya hivyo hawavunji sheria za nchi. 

Labda nikupeni mifano michache katika kupanua uelewa wa jambo hili. Katika nchi ya jirani Kenya viongozi wote wakuu katika siasa za Kenya wamewahi kuhama vyama mara nyingi. Rais wa sasa wa Kenya ameshahama na kubadili vyama mara nne. Kiongozi nguli wa upinzani Raila Odinga ameshahama na kubadilisha vyama mara sita. Huko nchini Uganda kiongozi maarufu wa upinzani nchini humo Kiiza Besigye alikuwa katika chama kimoja na Rais Museveni, lakini alihama na kuanzisha chama chake.

Pengine unaweza ukasema tabia za kuhama vyama zipo Afrika tu. Hapana. Muasisi wa kuhama vyama duniani ni Winston Churchil, ambaye ndiye anayeshikilia rekodi ya kuwa waziri mkuu bora nchini Uingereza. Huyu alihama kutoka chama cha Conservative na kujiunga na chama cha Liberal. Baadaye tena alirudi katika chama cha Conservative na hatimaye kuchaguliwa kuwa waziri mkuu. 

Ukienda nchini Marekani wapo wanasiasa maarufu 21 waliowahi kuhama vyama vyao. Kwa mfano, rais wa zamani wa Marekani Ronald Reagan alikuwa mwanachama wa chama cha Democrat, lakini alihamia chama cha Republican na baadaye akaja kuwa rais wa nchi hiyo. 

Alipoulizwa kwa nini alihama alijibu kuwa “I didnt leave the Democratic Party. The party left me” (Sikukiacha Chama cha Democrat. Chama ndicho kilichoniacha). Wanasiasa wengine maarufu waliowahi kuhama vyama vyao nchini Marekani ni pamoja na Condoleeza Rice, Elizabeth Warren, Hillary Clinton na Theodore Roosevelt. Rais wa sasa wa Marekani, Donald Trump alishahama vyama mara tatu na hadi mwaka 2001 alikuwa mwanachama wa chama cha Democrat.

Mheshimiwa Baba Askofu, nimetoa mifano yote hii katika kujaribu kupanua uelewa wenu kuhusu tabia za wanasiasa katika mfumo wa vyama vingi duniani kote. Hata hivyo, jambo hili halipo katika siasa tu. Wewe unafahamu vizuri kuwa hata katika dini watu hubadili dini na madhehebu yao. Sembuse vyama vya siasa? 

Aidha, katika nchi yetu tumeshakuwa na chaguzi ndogo nyingi zinazotokana na wabunge na madiwani ama kuhama vyama vyao au kufukuzwa katika vyama vyao tangu mfumo wa vyama ulipoanza, na chaguzi zote hizo husababisha gharama kubwa. Sasa ninajiuliza kwa nini Kanisa limeumia sana na chaguzi za kipindi hiki? Kuna nini?

3.Kuhusu mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu
Mheshimiwa Baba Askofu, hoja ya tatu ambayo nayo pia ningependa kuitolea maoni ipo katika eneo la tatu la waraka wenu, ambayo ni kuhusu upatikanaji wa mikopo ya elimu ya juu. Katika hoja hiyo mmeeleza kwamba, “uwezeshwaji wa vijana kupata mikopo ya elimu ya juu uwe shirikishi na usiokuwa na ubaguzi kati ya wanafunzi wa vyuo binafsi na wale wa serikali; sayansi na sanaa; wazazi maskini na wenye nafasi; waliosoma shule binafsi na wale wa shule za Serikali”. 

Kwa ufahamu wangu ni kwamba kimsingi kila mkopo lazima uwe na vigezo. Msingi mkubwa wa mikopo inayotolewa kwa wanafunzi wa elimu ya juu hapa nchini ni kile kinachofahamika kama means testing, ambapo Bodi ya Mikopo huchambua maombi ya mikopo kwa kuzingatia, pamoja na mambo mengine, uwezo wa wazazi wa wanafunzi. Hivyo, mnaposema pasiwe na tofauti katika utoaji wa mikopo, mlitaka kumaanisha nini hasa?

Ni vizuri kukumbushana kuwa kuanzishwa kwa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kulitokana na Serikali kushindwa kugharamia wanafunzi wote wanaodahiliwa katika elimu ya juu. Kwa sababu hii, njia pekee ilikuwa ni kuja na vigezo ambavyo vingewaondoa wale ambao wana uwezo wa kujilipia. 

Katika mazingira haya, sio sahihi, kwa mfano, kusema kuwa hata mtoto wa mzazi mwenye wadhifa kama wangu naye apate mkopo. Aidha, kanisa haliwezi kueleweka linapotaka mtoto aliyesomeshwa na mzazi wake katika Shule ya Sekondari Feza au International School of Tanganyika naye apate mkopo wa serikali.

Aidha, kila nchi duniani ina vipaumbele vyake vya mahitaji kutokana na wakati na mazingira. Kwa wakati na mazingira ya nchi yetu kwa sasa tunahitaji zaidi wataalamu katika fani za sayansi kuliko sanaa. 

Ni kwa sababu hii Serikali inawekeza zaidi katika kusomesha wanafunzi katika fani za sayansi kuliko sanaa. Huu ndiyo msingi wa Serikali kuwapa kipaumbele wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi kuliko wale wanaosoma masomo ya sanaa.

Kwa maoni yangu, jukumu la kanisa katika suala hili lingekuwa ni kuiasa serikali kuepuka ubaguzi katika mikopo kwa misingi ya dini, itikadi za siasa na ukabila ambapo bahati nzuri ubaguzi huo haupo. 

Ubaguzi katika mikopo ya elimu ya juu kwa misingi ya uwezo wa wazazi na aina ya shule ambayo mtoto alisoma (binafsi au umma) hauepukiki. Kwa maoni yangu, kuna haja pia kuangalia kama bado ni muhimu kutoa kipaumbele kilicho sawa kati ya wanafunzi wanaodahiliwa katika vyuo vikuu vya umma na wale wanaodahiliwa katika vyuo vikuu vya binafsi. 

Huo pia unaweza ukawa aina nyingine ya ubaguzi unaokubalika katika utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu, hasa katika mazingira ambayo vyuo vya umma vina nafasi ya kutosha ya kudahili wanafunzi wote wenye sifa za kujiunga na elimu ya juu.

4.Katiba Mpya
Mheshimiwa Baba Askofu, katika waraka wenu mmetoa pia maoni kuhusu umuhimu na uharaka wa kupatikana kwa Katiba mpya. Hii ni hoja kubwa inayogusa Taifa letu kwa muda mrefu. Sote tunatambua utashi na ujasiri aliouonyesha Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne wa kuruhusu mchakato huu uanze, pamoja na kwamba haikuwa ajenda ya msingi na kipaumbele katika chama chake. Kwa hiyo, ninaunga mkono kanisa kulitolea kauli jambo hili kubwa na muhimu kwa Taifa letu.

Hata hivyo, baadhi ya hoja zenu na lugha iliyotumika katika kuwakilisha hoja hiyo haiponyi bali inaligawa kanisa na nchi kwa ujumla. Kwa mfano, mnaposema kuwa “tunaisihi Serikali ya Awamu ya Tano kurejea mchakato wa upatikanaji wa KATIBA MPYA ya wananchi iliyopendekezwa na wananchi kupitia Tume ya Warioba”, mlitaka kumaanisha nini hasa? 

Ninauliza hivi kwa sababu ninafahamu kuwa mchakato wa kuunda Katiba mpya ulikuwa umevuka ngazi ya Tume ya Warioba na kufikia ngazi ya Bunge la Katiba, ambapo Bunge lilipitisha kwa kura ya wengi. 

Kilichokwama katika mchakato huo ni kura ya maoni ya wananchi kutokana na kukosekana kwa maridhiano mapana ya kijamii baada ya baadhi ya wawakilishi katika Bunge la Katiba kususa kuhudhuria vikao vya Bunge hilo. 

Ninafahamu pia kuwa kanisa na dini zingine ziliwakilishwa kikamilifu katika Bunge hilo. Wawakilishi wa kanisa sio miongoni mwa wabunge waliosusia Bunge la Katiba, ikimaanisha kuwa kanisa liliridhia mchakato hadi mwisho na ni sehemu ya jamii waliokubaliana na rasimu iliyopitishwa na Bunge hilo.

Sababu za msingi za mchakato wa Katiba kukwama ni kutokana na kukosekana kwa mwafaka na maridhiano ya kitaifa. Kwa sababu hii mchakato wa Katiba mpya umebaki ukielea. Sasa katika mazingira haya ni hatari sana kwa ninyi viongozi wetu wakuu wa kiroho kuchukua upande mmojawapo katika mgawanyiko huo uliotokea. 

Kwa maoni yangu, kwa upande wenu kama kanisa ingetosha kutoa wito wa kurejewa kwa mchakato wa Katiba mpya na kutoa wito wa mchakato huo kuzingatia maridhiano ya kitaifa. 

Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wa Sauti za Wananchi yaliyotolewa mwezi Oktoba 2017, maoni ya wananchi yamegawanyika katika makundi manne kuhusu upatikanaji wa Katiba mpya. Kuna kundi la Watanzania linalotaka mchakato uanze upya. Kuna kundi jingine linalotaka turejee kwa Tume ya Warioba. 

Lipo kundi linalotaka tumalizie mchakato kwa kwenda katika kura ya maoni. Lakini pia wapo Watanzania wanaosema hakuna haja tena ya Katiba mpya. Makundi yote haya ni ya Watanzania na bila shaka miongoni mwao ni waumini wa KKKT. Hivyo, ninyi viongozi wetu mnapoongelea suala hili kwa namna ya kuhimitisha (conclusive) mnajiweka katika mazingira ya kuchochea mgawanyiko badala ya kuleta umoja na uponyaji.

5.Kuhusu Serikali kutoendeshwa kwa ilani ya vyama
Hoja yenu nyingine katika eneo la maisha ya siasa ni kuhusu nafasi ya ilani ya vyama katika kuendesha nchi na Serikali. Katika hoja yenu hii mmenena ya kuwa, “Taifa haliongozwi na ilani za vyama. Serikali haiongozwi na ilani za vyama. Serikali huongozwa na Katiba, sheria, kanuni na mapokeo mema (misingi na tunu za Taifa)”.

Baba Askofu, niruhusu nikupeni elimu ya siasa kidogo kuhusu jambo hili. Duniani kote inajulikana kuwa chama kinachopata ridhaa ya kuunda serikali hupewa dhamana ya kutekeleza ahadi ambazo chama hicho kilizitoa katika uchaguzi. 

Ndiyo kusema, vyama vinapoingia kushindana katika uchaguzi hushindania fursa ya kuunda serikali ili vitekeleze yale ambayo vinaamini ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa husika. Kwa hivyo, msingi wa sera za serikali iliyopo madarakani ni ilani ya chama tawala iliyosheheni ahadi za chama hicho wakati wa uchaguzi. 

Ndiyo kusema mara chama kinaposhinda uchaguzi na kuunda serikali ahadi zake zilizopo ndani ya ilani hugeuka kuwa ajenda za maendeleo za Taifa hilo. Ndiyo maana ahadi za CCM za uchaguzi wa mwaka 2015 ni sehemu muhimu ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano.

Kwa hiyo serikali huongozwa na vyombo vikubwa viwili katika kuendesha nchi. Chombo cha kwanza ni ilani ya chama tawala ambayo hutekelezwa kama sehemu ya ajenda za maendeleo ya Taifa husika. 

Chombo cha pili ni Katiba, sheria, kanuni na miongozo mbalimbali ambayo hutolewa na vyombo mbalimbali vya dola. Katiba, sheria na kanuni ni nyenzo za utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya Taifa, ikiwemo ilani ya chama tawala.

Hadi hapo utaona kuwa hamkuwa sahihi hata kidogo kuwahubiria waumini wa KKKT na Watanzania kwa ujumla kuwa Serikali haiendeshwi kwa ilani za vyama. Ukweli ni kuwa ilani ya chama tawala ni nyenzo na ajenda muhimu ya kuendesha serikali katika nchi zote zinaendeshwa kidemokrasia na kwa kufuata utawala wa sheria. 

Marekani, kwa mfano, leo wanajenga ukuta wa kuitenga Marekani na Mexico ili kudhibiti wahamiaji kutoka Mexico. Hii ilikuwa ni moja ya ahadi kubwa za Rais Donald Trump na chama chake cha Republican wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2016. Baada ya Donald Trump kushinda uchaguzi na kuunda serikali ahadi hii sasa ni ajenda ya Taifa la Marekani.

Mheshimiwa Baba Askofu, nihitimishe barua yangu kwa kurudia tena pongezi za dhati kwa kuandaa Waraka ambao umegusa masuala nyeti yanayohusu nchi yetu. Hata hivyo, upo umuhimu kwa kanisa kujiepusha kadri inavyowezekana kuonekana lipo upande fulani kwenye mijadala ya kitaifa inayogusa jamii pana yenye mitazamo kinzani. 

Kwa kufanya hivyo, mtaepusha migawanyiko isiyo ya lazima kwa waumini ndani ya kanisa na wananchi kwa ujumla. Ushauri wangu ni kwamba ili kanisa lionekane linaendeleza kazi za msingi zilizoanzishwa na Bwana wetu Yesu Kristo, ni muhimu sana kufanya utafiti na uchambuzi wa kina wa jambo lolote kabla ya kulitolea kauli hadharani.

Aidha, ni muhimu kwa kanisa kupima kwa umakini mkubwa uzito wa kila neno kabla ya kutoa kauli katika umma. Ni hatari kwa kanisa kutoa kauli inayosababisha maumivu na mifarakano badala ya kuponya. Ili kuepuka kauli za namna hii, ni vizuri kila mara kanisa na viongozi wetu mkajenga hoja zenu kwa kuzingatia mantiki na ushahidi wa kiinjili unaopatikana ndani ya Biblia Takatifu, na/au mantiki na ushahidi wa kisayansi unaopatikana kupitia tafiti na tafakuri pana na shirikishi.

Mheshimiwa Baba Askofu, Bwana Yesu Asifiwe.
Kwa heshima na taadhima ninaomba kuwasilisha.
Dodoma
Alhamisi 29 Machi 2018.

Mambosasa: Silaha Iliyomuua Akwilina Haijajulikana, Bado Tunaendelea Kuchunguza

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum jijni Dar es salaam, Lazaro Mambosasa, ameelezea hatua inayoendelea kuchukuliwa juu ya askari polisi sita waliokuwa wameshikiliwa kutokana na kifo cha mwanafunzi wa NIT Akwilina Akwilin, aliyeuawa kwa risasi mapema mwaka huu

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es salaam, Kamanda Mambosasa amesema polisi hao bado wapo kwenye uchunguzi kubaini ni nani anahusika, kwani mpaka sasa hakuna ushahidi wa moja kwa moja wa kuweza kumbaini.

“Wale walipokamatwa tulieleza bayana kwamba upelelezi unafanyika ili kujua ni nani ambaye ametenda kosa lile, bado suala la upelezi linaendelea.

"Yapo maelekezo yaliyotolewa ambayo tunaendelea kufuatilia ili kuja kubaini, ikumbukwe silaha moja ambayo haijajulikana ni ipi ndio ilikwenda ikamgusa Akwilina, lakini kama ulivyojua askari walikuwa ni wengi lakini pia kulikuwa hakuna ushahidi kwamba yupi aliyekuwa ametenda hivyo, kwa hiyo uchunguzi bado unaendelea”, amesema Kamnda Mambosasa.

Ikumbukwe kwamba mnamo Februari 17, mwaka huu, mwanafuzi wa chuo cha usafirishaji jijini Dar es salaam Akwilina Akwilini alifariki dunia baada ya kupigwa risasi ambayo inaaminika ilitoka kwa mmoja wa askari waliokuwa wakitawanya maandamano ya wafuasi wa chadema, huku yeye akiwa kwenye daladala akipita njia.

Wabunge sita wapata ajali, mmoja alazwa ICU

$
0
0
Wabunge sita wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamepata ajali ya gari jana usiku Machi 29, 2018 mkoani Morogoro wakati wakitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam.

Baada ya kutokea ajali hiyo saa 2 usiku katika barabara kuu ya Morogoro-Dodoma eneo la Bwawani, wabunge hao waliumia maeneo mbalimbali ya miili yao na kukimbizwa hospitali ya Mkoa wa Morogoro.

Wabunge hao ambao wote ni kutoka Zanzibar ni Haji Ameir Haji (Makunduchi), Khamis Ali Vuai (Mkwajuni), Bhagwanji Maganlal Meisuria (Chwaka), Makame Mashaka Foum (Kijini), Juma Othman Hija (Tumbatu).

Mganga mfawidhi hospitali ya rufaa Mkoa wa Morogoro, Dk Rita Lyamuya amesema majeruhi hao walipokelewa saa 3 usiku na kupatiwa huduma za awali.

"Jana tumepokea majeruhi sita walioumia sehemu mbalimbali na mmoja wao alilazimika kulazwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu (ICU) lakini hali yake inaendelea vizuri,” amesema.

“Leo asubuhi tayari tumewapa rufaa kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi  zaidi.”

Dk Rita amesema Kimbe na May ndio wameumia zaidi, kupata maumivu makali.

Profesa Kitila asema maudhui ya waraka wa maaskofu hayaakisi wajibu na msingi wa kanisa

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo amemwandikia barua Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Askofu Frederick Shoo akitoa maoni yake binafsi kwa kanisa hilo kuhusu maudhui ya waraka wa maaskofu wa kanisa hilo uliotolewa hivi karibuni.

Waraka wa maaskofu 27 wa KKKT ulitoka hivi karibuni na ulitarajiwa kusomwa katika makanisa yote ya kilutheri Machi 25, 2018.

Katika waraka huo maaskofu walizungumzia  Katiba mpya, uchumi, siasa na jamii.

“Katika kutoa maoni yangu kuhusu Waraka huo, ninalenga mambo makubwa mawili ambayo ni pongezi kwenu, na pili ni mtazamo wangu juu ya baadhi ya masuala yaliyomo katika Waraka huo,” amesema Kitila katika barua yake aliyoisaini Machi 29 mwaka huu.

Pamoja na kuwapongeza maaskofu hao, Kitila ameandika katika barua yake kuwa maudhui yaliyowekwa katika waraka wa maaskofu hao, hayaakisi hadhi na wajibu wa msingi wa kanisa.

“Kama ambavyo mmekuwa mkitufundisha siku zote, na vile tusomavyo katika Biblia Takatifu, ninafahamu kuwa kazi za msingi za kanisa ni zile ambazo Bwana wetu Yesu Kristo alizifanya alipokuwa duniani,”amesema.

Kitila ambaye ameandika barua hiyo kama muumini wa KKKT, amesema anakubaliana na mengi maaskofu waliyogusia katika Waraka huo akiamini yamefundisha na kuponya roho za waumini kwa kiasi kikubwa.

Hata hivyo, alichambua hoja katika maeneo matano zilizoibuliwa na maaskofu hao na kusema ni sahihi lakini akatahadharisha kuwa ni muhimu kwa kanisa kujiepusha na kuonekana lipo upande fulani katika mijadala ya kitaifa inayogusia jamii.

“Kwa kufanya hivyo, mtaepusha migawanyiko isiyo ya lazima kwa waumini ndani ya kanisa na wananchi kwa ujumla.” Amesema.

Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa kanisa kupima kwa umakini mkubwa uzito wa kila neno kabla ya kutoa kauli katika umma.

“Ni hatari kwa Kanisa kutoa kauli inayosababisha maumivu na mifarakano badala ya kuponya.”


Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO 0754372325/ 0689013109/ 0620806813 

HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Ni Dr. Chief Malunde Pekee Anaetibu Nguvu Za Kiume Na Kumtuliza Umpendae Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
"NI DR. CHIEF MALUNDE PEKEE ANAETIBU NGUVU ZA KIUME NA KUMTULIZA UMPENDAE KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI"
-baada ya kujichimbia katika nchi za kiarabu kwa zaidi ya miaka (10)sasa amewasili nchini na dawa za tiba asilia.
 
1/NGOLO 3 POWER-ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, ina ubora wa hali ya juu wa kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wasiojiweza kufanya tendo la ndoa, inaimarisha misuli iliyolegea na kusinyaa, inarutubisha mbegu za kiume na kukufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15-25 kuwa na hamu na tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila kuchoka, inarefusha uume inchi 5-8 na kunenepesha hadi cm 4 kwa wenye maumbile madogo, dawa hii imeboreshwa na hutibu matatizo haya kwa muda mfupi tu.
 
2/MAGOYE MVUTO- dawa hii ina uwezo mkubwa sana kumvuta na kumtuliza aliekuacha awe mpenzi, mme/mke itamfanya akutafute mwenyewe ndani ya masaa 3tu na kukutimizia mahitaji yako kwa haraka na kumfunga asiwe na mtu mwingine.
 
3/SUPER LUBEJA- ni dawa ya kushepu umbo no.8 mguu wa bia, kuongeza hips, na makalio kwa muda wa siku 5tu unapata saizi uipendayo, kuondoa makovu, chunusi, harufu mbaya ya mwili michirizi, kupunguza tumbo na maziwa kwa siku 6tu.
 
4/NG'WESHI MIX- ni dawa ya biashara ya kupata wateja wengi, kusafisha nyota, kurudishwa kazini na kupandishwa cheo, kurudisha mali iliyoibiwa au kudhurumiwa.
 
PIA TUNATIBU MAGONJWA SUGU KAMA: vidonda vya tumbo, ngiri, chango na uzazi kwa kina mama: (dawa zote hazina madhara kwa mtumiaji) HUDUMA HIZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO: TUNAPATIKANA DSM BUGURUNI SHELI AU PIGA SIM NO_ 0763-181099.

Rais Magufuli aungana na Wakristo kuadhimisha misa ya Pasaka Kanisa la Mt. Joseph Jijini Dar es Salaam

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 01 Aprili, 2018 ameungana na Wakristo wote Tanzania katika maadhimisho ya Misa Takatifu ya sikukuu ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Joseph, Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Misa hiyo imeongozwa na Paroko Msaidizi wa Parokia ya Mtakatifu Joseph Padre Venance Tegete.

Akizungumza baada ya kukaribishwa na Padre Tegete kutoa salamu, Mhe. Rais Magufuli amewatakia Watanzania wote heri ya Pasaka na ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kuishi kwa amani na upendo huku wakishiriki ipasavyo katika ujenzi wa Taifa.

“Kifo na ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo ukafufue matendo yetu, tuendelee kuijenga amani yetu, upendo wetu na tujenge maendeleo ya Watanzania wote, kwani Kristo alifundisha upendo miongoni mwetu.

“Kwa hiyo Baba nakushukuru sana kwa kuongoza Misa hii, naomba ufikishe shukrani zangu kwa Kardinali Pengo, Maaskofu wote na Watanzania wote tuendelee kusimama pamoja ili kulijenga Taifa letu” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli aliongozana na Mkewe Mhe. Mama Janeth Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU.
Dar es Salaam
01 Aprili, 2018

Miguna Miguna Amtupia Lawama Raila Odinga

$
0
0
Mwanasiasa wa upinzani nchini Kenya, Miguna Miguna amemtupia lawama Raila Odinga kwa kushindwa kumsaidia kuingia nchini humo. 

Amesema Odinga hapaswi kukaa akifurahia Pasaka wakati mtu aliyemuapisha kuwa rais "anauawa" na watu waliomwibia ushindi katika uchaguzi.

Katika taarifa yake aliyoituma kutoka Dubai, Falme za Kiarabu alikosafirishwa kwa nguvu na serikali, Miguna Jumamosi alimshutumu Odinga kwa kufanya karamu na watesi (wa mwanasheria huyo).

“Raila Odinga hawezi na hapaswi kukaa akifurahia Sikukuu ya Pasaka na wadhalimu huku mtu aliyesimamia kiapo chake cha kuwa rais wa watu “anauawa” na walewale waliomwibia ushindi katika uchaguzi uliopita na ambao wameua na kuwatia vilema wafuasi wake,” alisema.

Ingawa waziri mkuu huyo wa zamani hajatoa maoni yoyote hadharani kuhusu kuondolewa nchini kwa Miguna na kusafirishwa hadi Dubai, alijaribu kumwokoa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta Jumatatu jioni.

Ripoti zinaonyesha Odinga aliondoka kwenye uwanja wa ndege baada ya juhudi za kutafuta ufumbuzi, ikiwemo ya kumpigia simu Rais Uhuru Kenyatta, kugonga ukuta.

Serikali, vyanzo vinasema, ilisisitiza kwamba Miguna lazima asalimishe pasipoti yake ya Canada kabla ya kuruhusiwa kuingia nchini.

Raila ambaye ni kiongozi wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM) na ambaye amekubali kushirikiana kufanya kazi na serikali ya Kenyatta kwa ajili ya uponyaji wa nchi na umoja, alihudhuria kwa muda kusikiliza kesi juu ya uraia wa Miguna katika Mahakama Kuu.

Miguna amewahimiza wafuasi wake kumtaka Raila achukue hatua kwa sababu mateso yote anayopata ni matokeo ya kiapo alichomsimamia.

Pia amewataka wafuasi wake kuandamana na kuishinikiza serikali kuheshimu amri za mahakama na imruhusu kurejea nyumbani.

“Kusanyeni makundi makubwa ya watu waandamane, pigeni kelele na mdai kwamba haki zangu za kuzaliwa, kikatiba na kisheria ziheshimiwe na zizingatiwe,” alisema.

“Waheshimu amri za mahakama; nirejeshewe pasipoti yangu ya Kenya au nipewe mpya; ulinzi na usalama wangu uwepo.”

"Naomba kuokolewa kutoka Dubai, niruhusiwe kuondoka kwa usalama na kuingia kwenye nchi nilikozaliwa ya Kenya bila kukawia,” alisema.

"Mzaliwa wa Kenya hawezi kuzuiwa kuingia kwenye nchi aliyozaliwa. Sijawahi kuukana uraia wangu. Mahakama zimethibitisha na zimetambua uraia wangu."

Dk Miguna pia aliomba apatiwe huduma ya matibabu haraka akidai kemikali aliyodungwa wakati anasafirishwa inazidi kuathiri afya yake.

“Ni lazima nimwone dokta au tabibu na nifanyiwe vipimo vya kujua aina ya kemikali,” alisema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images