Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mama aliyejifungua mapacha wawili wenye baba tofauti

0
0
Katika hali ya kushangaza huko nchini Uganda, wanaume wawili na watu wengine wamejikuta kwenye mshangao baada ya kukuta wote wawili ni baba wazazi wa watoto wawili mapacha.

Inaelezwa kuwa wanaume hao waliingia kwenye mgogoro siku za hivi karibuni kila mtu aking’ang’ania kuwa baba mzazi wa mapacha hao, na ndipo walipoamua kwenda hospitali ili kupima kipimo cha DNA.

Hatahivyo matokea ya daktari yalionesha kuwa wanaume hao wote wawili ni baba halali wa mtoto mmoja wa mapacha hao, yaani kila mmoja ana mtoto mmoja kati ya mapacha hao.

Inaeelezwa kuwa wanaume hao Joseph Baseka Sengendo, 25, na Patrick Ssegane, 30, wamezaa na Rashida Nakabugo, ambapo Sengendo anatajwa kuwa mume wa ndoa wa mwanamke huyo.

Wanaume hao wanasemekana kuwa ni ndugu.

Katibu wa Bunge Azungumzia Ajali ya Wabunge 6

0
0
Katibu wa Bunge, Steven Kagaigai amesema chombo hicho cha dola kinafuatilia kwa ukaribu ajali ya wabunge sita iliyotokea jana usiku, Machi 29, 2018 mkoani Morogoro.

Kagaigai amesema baada ya kupokea taarifa hizo wamefanya mawasiliano na uongozi wa Hospitali ya Morogoro na walishauriwa kuwahamishia Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

“Ndiyo taarifa hizo ninazo, wamepata ajali huko Morogoro, tayari tumeshafanya taratibu za kuwapeleka Muhimbili kwa huduma zaidi na ofisi yetu inawajibika kwa kila hatua,” amesema Kagaigai.

Wabunge hao ambao wote ni kutoka Zanzibar ni Haji Ameir Haji (Makunduchi), Khamis Ali Vuai (Mkwajuni), Bhagwanji Maganlal Meisuria (Chwaka), Makame Mashaka Foum (Kijini), Juma Othman Hija (Tumbatu).

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya March 31

Mambo 13 Aliyosema Tundu Lissu baada ya Bombadier kuachiwa huuko Canada

0
0
Mbunge wa Singida, Tundu Lissu amesema ameona taarifa ya Msemaji wa Ikulu, Gerson Msigwa, kwamba ndege aina Bombardier iliyokuwa imezuiliwa Canada inakuja nchini.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Lissu ameandika baadhi ya mambo ambayo angependa baadhi ya watu wanaodai kuwa alitumwa kipindi cha nyuma alipokuwa anazungumzia kushikiliwa kwa ndege hiyo Canada wafahamu.

 ==>>Hii ni kauli yake
Nimeona taarifa ya Msemaji wa Ikulu, Gerson Msigwa, kwamba Bombardier yetu iliyokuwa imezuiliwa Canada inakuja. .

Kufuatia taarifa hiyo, baadhi ya watu wamedai mitandaoni kwamba kuletwa kwa ndege hiyo ni pigo na aibu kwa mawakala wa mabwanyenye waliosababisha ndege yetu kushikiliwa Canada.

Mimi nauliza: Hivi 'mawakala wa mabwanyenye' waliosababisha ndege yetu ikamatwe Canada ni akina nani hasa??? .
Here are some basic facts: .

1) Mwaka 2003, kampuni ya Sterling Construction and Engineering Ltd. (SCEL), ilivunjiwa mkataba wake wa ujenzi wa Barabara ya Bagamoyo. Mkataba huo ulivunjwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

2) Baada ya kuvunjwa kwa mkataba, SCEL ilishtaki Serikali ya Tanzania kwenye Mahakama ya Usuluhishi ya International Chamber of Commerce, London. Tunaambiwa baadhi ya hearings, au zote, zilifanyikia Dar Es Salaam. .

3) Mwezi December 2009 na baadae June 2010, Arbitral Tribunal ya ICC ilitoa uamuzi kwamba Serikali ya Tanzania ilivunja mkataba wa SCEL bila uhalali wowote na kuamuru Serikali kuilipa SCEL takriban USD milioni 25, na riba ya 8% kwa mwaka kuanzia tarehe ya hukumu hadi tarehe ya malipo ya mwisho. .

4) Kwa sababu tunazostahili kuambiwa , deni la SCEL halikulipwa kwa miaka saba hadi SCEL walipoenda kwenye Supreme Court of Quebec, Canada, na kupata amri ya mahakama kuikamata Bombardier .

5) Baada ya kusikia Bombardier imekamatwa, Waziri wa Mambo ya Nje, Dr. Augustine Mahiga, na Balozi wetu Canada, Jack Zoka, walitumwa kwenda Toronto kufanya mazungumzo na SCEL juu ya namna ya kujinasua na balaa hili. Waziri Mahiga na Balozi Zoka waliiomba SCEL isitoe habari za Bombardier kukamatwa hadharani. .

6) Tarehe 18 August, 2017, baada ya kupata nyaraka mbali mbali zinazohusu kukamatwa kwa Bombardier , nilitoa taarifa za kukamatwa ndege hiyo kwa waandishi wa habari Courtyard Hotel, Dar Es Salaam. .

7) Kesho yake tarehe 19 August, Kaimu Msemaji wa Serikali, Zamaradi Kawawa, alithibitisha kukamatwa kwa Bombardier  na kutulaumu sisi wapinzani kuwa ndio tuliosababisha ndege yetu ikamatwe Canada. .

8) Licha ya Serikali kukiri ukweli wa maneno yangu, tarehe 20 August, nilikamatwa na askari polisi walioniambia hawajui kosa langu ila wanatekeleza 'maagizo kutoka juu.' Nililazwa mahabusu Central Police Station hadi kesho yake nilipopelekwa kwa Mkemia Mkuu ili kupimwa mkojo. Nilipokataa kupimwa mkojo nilirudishwa mahabusu hadi kesho yake tarehe 22 August nilipoachiliwa huru bila kupelekwa mahakamani. .

9) Alfajiri ya tarehe 26 August, 2017, ofisi za kampuni ya Mawakili ya IMMA Advocates ya Dar Es Salaam, zilishambuliwa kwa mabomu na 'watu wasiojulikana.' Miaka ya nyuma, IMMA Advocates waliwahi kuwa mawakili wa SCEL. Hadi leo hakuna mtu aliyetuhumiwa au kukamatwa na kushtakiwa kwa kuhusika na shambulio hilo la kigaidi. Na hadi sasa Jeshi la Polisi halijatoa taarifa yoyote ya uchunguzi wa shambulio hilo.

10) Tarehe 7 September, 2017, siku kumi na moja baada ya shambulio la mabomu dhidi ya IMMA Advocates, ikawa zamu yangu kushambuliwa kwa risasi za submachine guns na 'watu wasiojulikana.' Nilijeruhiwa vibaya sana, lakini Mungu ni mwema sikufa. Hadi ninapoandika maneno haya, hakuna mtu hata mmoja aliyetuhumiwa au kukamatwa na kushtakiwa kwa kuhusika na shambulio hilo la kigaidi dhidi yangu. Na hadi sasa Jeshi la Polisi halijanihoji mimi wala dereva wangu kuhusiana na shambulio hilo na wala halijatoa taarifa yoyote ya uchunguzi wa shambulio hilo. .

11) Kwa kipindi chote tangu  alipovunja mkataba mwaka 2003 hadi tarehe 18 August, 2017, nilipozungumzia hadharani suala la kukamatwa kwa Bombardier Canada, Serikali ya Tanzania, haikuwahi kuwaambia Watanzania kwamba tunadaiwa mabilioni na SCEL kwa sababu ya kuvunja mkataba na baadae kushindwa kesi. .

12) Msemaji wa Ikulu, Gerson Msigwa, na kabla yake Msemaji wa Serikali, Abbas, hawajasema, hadi sasa, ni kwa nini Bombardier yetu ilikuwa imezuiliwa Canada. Hawajasema kama ni kweli au la kwamba ndege yetu ilikuwa imezuiliwa kwa sababu ya  kuvunja mkataba kimakosa .

13) Nafurahi kusikia taarifa za kuachiliwa kwa ndege yetu. Nitafurahi zaidi tukiambiwa Bombardier hiyo imeachiliwa kwa masharti gani, kwa vile tulikuwa tunadaiwa karibu USD milioni 40 zilizotokana na kuvunja mkataba na Serikali kushindwa kesi na SCEL.

Nawatakieni Pasaka njema.

Askofu Nzigilwa Awataka Waumini Kuacha Malumbano Waione Pepo

0
0
Askofu Msaidizi wa jimbo Katoliki la Dar es Salaam, Eusebius Nzigilwa amewataka waumini kuwa na moyo wa huruma hasa katika kipindi hiki cha kukumbuka mateso ya Yesu Kristo na kuondoa malumbano ili waweze kuiona pepo.

Akihubiri katika misa ya Ijumaa Kuu jana Machi 30, iliyofanyika katika Kanisa ka Bikira Maria Mama wa Huruma, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam alisema wawe tayari kusamehe kwa wote waliowakosea na kuondoa visasi na vinyongo ambavyo vinaweza kuharibu maisha yao.

“Katika kipindi hiki cha kukumbuka mateso ya Yesu Kristo, tunapaswa kukumbuka matendo ya huruma ambayo yatazidi kutuongezea imani na kuondoa visasi na malumbano katika jamii na familia zetu.

“Wakristo tunatakiwa kujifunza kukaa kimya na kuepusha maneno na kumgeukia Kristo ili uweze kumueleza shida zako, jambo ambalo linaweza kukusaidia ukaikuta huruma yake.

“Kila mmoja anapomuangalia Yesu msalabani anapaswa kusema yesu dhambi zangu zimekuhukumu kwa sababu alikuhumiwa katika mazingira ya uonevu,” alisema.

Aidha, Askofu Nzigilwa alisema watu wanapaswa kumuonea huruma mtu anayeteseka na kamwe hawashiriki kwa ajili ya kusababisha mateso Kwa mwingine na kwamba kila mmoja anapaswa kuweka azimio la kuwa mtetezi kwa wanaoonewa na kamwe wasinyanyase mtu au kumtendea mabaya.

“Kila binadamu anateseka kwa namna tofauti ili kupimwa imani yake kama ipo imara, hivyo basi wanapaswa kuwa wavumilivu wa moyo na kumkimbilia Mungu ili iwe sehemu ya ukombozi,” alisema.

Askofu Chengula: Chagueni viongozi wasio na ubinafsi na Ambao Hawatawaongoza kwa Woga

0
0
Wakristo kote nchini wametakiwa kujipanga kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2019 wa madiwani na wenyeviti wa serikali za mitaa na viongozi wa vitongoji kwa kumchagua mtu asiyewafanya waishi kwa kuogopaogopa.

Kauli hiyo imetolewa jana Machi 30 na Mhashamu Askofu Evarist Chengula alipokuwa akiongoza ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika kitaifa katika kanisa Katoliki la Bikira Maria wa Fatma lililopo Mwanjelwa mjini Mbeya.

Akihutubia katika ibada hiyo Mhashamu Chengula alisema ujumbe uliotolewa na maaskofu siku kadhaa zilizopita ulikuwa haumlengi mtu fulani bali uliwalenga wanafiki wanaodai ni Wakristo lakini hawana imani ya Kikristo ili waweze kubadilika na kuwa watu wema.

“Ujumbe wa mwaka huu tunasema hakuna maana kusikiliza kila kitu tu, badala yake tufikiri kabla ya kutenda.

“Imekuwa kawaida kila baada ya kumalizika uchaguzi mkuu tunaanza kulaumiana, Wakristo wote katika jumuiya zenu ndogo ndogo nchi nzima muanze kujipanga mnataka mtu wa aina gani, angalieni ana tabia gani na si anatoka chama fulani,” alisema Mhashamu Chengula. Amewataka wanaparokia kukaa na maaskofu na kujadili.

“Msipofanya hivyo mtarudi kule kule kwa kulaumiana. Chagueni kwa kuzingatia kila mmoja atendewe haki, apate haki na amani.” Alisema na kuongeza;

“Kila baada ya uchaguzi wanakimbizana kama sungura na mbwa maana hatuchagui anayetusaidia sisi, tunachagua chama fulani kituongoze na kitutetee badala ya kufikiri kuchagua atakayetuongoza kwa amani.”

Aliongoza: “Haina maana kutuchagulia watu fulani ambao tukiwachagua wanatuongoza kwa woga, hawa hawajajiweka wenyewe ni mimi na wewe tumewaweka, tusichague watu wenye roho ya ubinafsi.”

Alisema ujumbe huo ni kwa wote, ili waanze kujiandaa kwa sababu unafika uchaguzi wa mwaka 2019 wachague kwa kuangalia hali halisi.

“Kila mmoja akasimulie hili anapokwenda kwa sababu ni vita ya wote, kila mmoja awe makini Tanzania iwe na upendo na mshikamano kati yetu.

“Kila anayekuja kubusu msalaba huu tulioulaza hapo mbele amueleze Yesu nataka Tanzania yenye upendo,” alisema Mhashamu Askofu Chengula.

Polisi Atiwa Mbaroni kwa Kumbaka Mtoto wa Miaka 14

0
0
Askari Polisi namba H.3102 konstebo Bariki Michael (28), wa kituo cha Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi, juzi alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa akikabiliwa na shitaka la kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 14 (jina limehifadhiwa).

Michael alifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi, Erasto Phili na kusomewa shitaka linalomkabili na wakili wa serikali, Juma Maige.

Akisoma shitaka hilo, Maige alidai mshitakiwa alitenda kosa hilo Machi 14, mwaka huu saa 4:00 asubuhi eneo la Kilimani mjini Ruangwa.

Wakili huyo alidai kuwa mshitakiwa, akiwa anatambua analofanya ni kosa, alipata mwanya wa kutekeleza tendo hilo nyumbani kwa mtoto huyo, ambaye pia ni jirani yake kufuatia kubaki peke yake, ndipo akaitumia nafasi hiyo kumfuata na kumwingilia kwa nguvu.

Maige alidai kutokana na kitendo hicho, mlalamikaji alipiga kelele za kuomba msaada kutoka kwa majirani ambao walijitokeza na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo na kumpeleka kituo chao cha Polisi cha Ruangwa mjini.

Mshitakiwa alikana kosa na kupelekwa mahabusu baada ya kukosa dhamana na kesi yake imepangwa kutajwa mahakamani hapo April 12.

Wakili wa serikali Maige alisema upelelezi wa shauri hilo umekamilika.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Kiwanda Cha Nguzo Za Zege Chafungwa Kwa Kukosa Soko

0
0
KIWANDA cha kutengeneza nguzo za zege cha Hunnan Power ,mjini Kibaha Mkoani Pwani ,kimefungwa kutokana na kukosa tenda na soko , tangu uzalishaji uanze mwezi september mwaka jana.

Kutokana na hali hiyo, kiwanda hicho kimebaki gofu na kupunguza ajira kutoka wafanyakazi 30 hadi wawili kwasasa.Hayo yalibainika wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo ,alipotembelea viwanda nane vilivyoanza uzalishaji na ambavyo vipo kwenye hatua za ujenzi mjini Kibaha.

Alisema mkoa huo unadhamira ya kuwa ukanda wa Viwanda vinavyozalisha bidhaa mbalimbali lakini endapo soko litakuwa hakuna ,wawekezaji watakata tamaa.

Alisema mkoa una viwanda vinavyotengeneza nguzo za zege viwili ikiwemo Hunnan Power /Kibaha na East Africa infrastructure engineering Ltd kilichopo Fukayosi /Bagamoyo ambavyo vinahofiwa kushindwa kuendelea kuzalisha kwasababu ya bidhaa zake kukosa wateja.

"Katika ziara hii tumebaini changamoto ya kiwanda cha Hunnan Power kukosa masoko na tenda huko shirika la umeme (Tanesco ),hawajapata tenda mara tatu 

"Hali hiyo imesababisha kiwanda hicho kufungwa, hakizalishi ,mashine zimefungiwa ndani ,kiwanda kimezungukwa nyasi ,kimekuwa gofu na ajira hakuna" suala hili linaangusha juhudi za rais John Magufuli ,Mkoa na serikali"alisema mhandisi Ndikilo.

Mhandisi Ndikilo alieleza, wawekezaji wanajitoa kuunga mkono na kuitikia wito wa serikali kujenga viwanda lakini baadhi vinakumbana na changamoto ya ukosefu wa soko la uhakika.Aliahidi kuzungumza na waziri mwenye dhamana na mkoa utafuatilia ili waziri wa nishati aweze kusaidia suala hilo.

Mkuu huyo wa mkoa aliitakaTanesco kuangalia kwa jicho la tatu tatizo hilo na kuangalia namna ya kutoa tenda ili kuokoa kuinua viwanda hivyo.

Mhandisi Ndikilo alitaja changamoto nyingine alizofikishiwa kwenye ziara hiyo,kuwa ni umeme,maji barabara na vibali kutoka TFDA.Aliwasihi viongozi wa wilaya ,halmashauri kuandika barua moja kwa moja kwa taasisi husika watatue matatizo hayo ili kuwavutia wawekezaji .

"Official communication itasaidia kuliko kusumbua sana hawa wawekezaji ,,itakuwa rahisi kufanya ufuatiliaji na kuzibana taasisi husika na kuzisukuma zifanye utekelezaji " alisisitiza.

Awali akitoa taarifa ya kiwanda cha Hunnan Power ,mkalimani wa kiwandani hapo, Suleiman Ramadhani alisema kiwanda kilianza ujenzi Jan 2017 na kuanza uzalishaji September 2017 na kimegharimu dollar milioni mbili na hakijawahi kuuza hata nguzo moja.Alisema kiwanda hakifanyi kazi tangu Jan mwaka huu kwakuwa kinategemea tenda na soko .

Suleiman alielezea kuwa ,wenye viwanda wanahitaji kujenga kiwanda kingine katika eneo hilo lakini wanashindwa kwasasa hadi hapo watakapopata wateja .Mhandisi wa udhibiti wa mapato Tanesco mkoani Pwani ,Fabian Rukiko ,alisema hawajawahi kutumia nguzo za zege mkoani hapo hadi hapo itakapohitajika.

Alikishauri kiwanda hicho kujitangaza kupitia kitengo cha mauzo na masoko kwani itasaidia kufanya ufuatiliaji na kushirikiana na wadau wakubwa watakaoweza kununua bidhaa hiyo muhimu ambayo inadumu kwa kipindi kirefu.Mwezi Novemba 2017, waziri wa Nishati Dk.Merdard Kalemani alitembelea kiwanda cha nguzo za zege kilichopo Fukayosi na alilitaka shirika la umeme Tanesco kutumia nguzo zinazozalishwa nchini kwenye ujenzi wa miradi mikubwa.

Nanukuu":"baada ya serikali kupiga marufuku uingizwaji wa nguzo za umeme toka nchi za nje na kuruhusu wawekezaji kutengeneza nchini, sasa umefika wakati TANESCO ianze kutumia nguzo za zege kuanzia Desemba 2017 kwenye miradi mikubwa";alisema.

Maalim Seif Apigwa Marufuku Mwanza

0
0
CHAMA cha Wananchi (CUF) mkoani Mwanza kimempiga marufuku Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad kutofanya mikutano na vikao vya kisiasa katika wilaya za Nyamagana na Ilemela zilizoko jijini hapa.

Hatua hiyo ya kumpiga marufuku Maalim Seif aliyesimamishwa uongozi na Baraza Kuu la Uongozi la CUF Taifa, imetolewa katika tamko la pamoja la viongozi katika wilaya za Ilemela za Nyamagana mkoani Mwanza.

Viongozi hao waliongozwa na Mwenyeviti wa CUF wa Wilaya ya Nyamagana, Salum Mkumbukwa aliyekuwa ameambatana na wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa, Martha Haule na Zainabu Ally.

Walidai kuwa wamesikia kuwa Maalim Seif anawasili jijini Mwanza kwa siri kupitia mwavuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kwa lengo la kuhudhuria kongamano moja la chama cha siasa linalotarajiwa kufanyika hivi karibuni katika wilaya za Nyamagana na Ilemela akiwa na lengo la kukutana na wanachama wa CUF, jambo ambalo uongozi halina tija kwa wakati huu wakati akiwa amesimamishwa uongozi.

Viongozi hao walisema wamemwandikia barua Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na wakuu wa wilaya za Nyamagana na Ilemela kupinga ujio wake.

Mpiga picha wa Diamond ‘Kifesi’ aacha kazi WCB, atoa sababu mbili kubwa

0
0
Mpiga picha wa msanii Diamond Platnumz na WCB kwa ujumla, Kifesi ameamua kuachana na kazi hiyo.

Kifesi ameeleza kuwa muda aliyofanya kazi WCB wa takribani miaka mitano unatosha ila kilichomsukuma zaidi kuacha kazi ni kutaka kujiajiri na kuwa karibu na Mungu wake kwani kazi aliyokuwa anaifanya ilimbana zaidi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Kifesi ameandika;

"Leo ikiwa ni siku takatifu na siku ya ibada kwangu ni siku nilioamua kufanya maamzi yatayobadili maisha yangu, nimeamua rasmi kuacha kazi kama mpiga picha wa Diamond na mwajiriwa wa WCB.. 

"Well It’s insane to be leaving a stable job u love But that’s reality for me naacha kazi kwa mtu alikuwa zaidi ya Rafiki kwangu, naacha kazi ambayo ni ndoto ya vijana wengi out there but to me..i see miaka yngu 4/5 ya kufanya kazi hapa inatosha niachie nafasi kwa vijana wengine nimeamua kufata moyo wangu.

"Ni uamzi niliokua nao karibu mwaka sasa but kama ilivyo kwa waajiriwa wengi is so hard kufanya maamzi ya kuacha kazi but IN ORDER TO GROW WE NEED TO MAKE CHANGE.. Naacha kazi to pursue my Dreams life ikiwamo kujiajiri mwenyewe. Naacha kazi ili nipate muda mwingi wa kuwa flexible nitumie muda wangu mwingi ku-unleash my potential for excellence.  reason ya mwisho na kubwa zaid kwangu.

"Naacha hii kazi ili niwe karibu zaidi na Mungu wangu kwa imani yangu kama Mkristo nilikua nafanya kazi katika lifestyle na mazingira ya kazi yasiyompendeza Mungu, ilinibidi kujihusisha na mziki, kwenda kwenye matamsha ya mziki, kwenda maeneo ya starehe kutokua na muda wa kwenda kanisani sababu ya kazi at the end we need to choose GOD over everything, sifa, umaarufu na fahari yote ya Dunia vitanifaidia nini endapo nitaukosa ufalme wa Mungu.

"Nimeamaua ku-drop kila kitu i just want to be happy, do my works live my life and have time with God, ukimchagua Mungu hata hivi vingine atakuongezea najua kutakua na changamoto nyingi, Up and downs but Mungu He knew me before was born aliahidi ukimchagua yeye he will open the doors atatufnya kuwa kichwa na siyo mkia.

"Mwisho nashukuru familia yote ya WCB  kwa kuwa na mimi for all these years was great working with u.. but zaidi nimshukuru Diamond kwa muda wote niliofanya nae kazi since chini mpaka sasa, nimefnya kazi kwa mapenzi, bidii na uaminifu mkubwa kwangu haukua boss bali rafik na nilkua rafiki wa kweli kwako a will always appreciate mchango wako kwangu.. Tusameheane pale tulipowahi kukoseana we are just humans, hatutakuwa pamoja kikazi but nina imani tutaendelea kuwa marafiki. God bless you, uzidi kufika unapopenda kufika, GOD Bless me.. God bless my next Hustles #happysabbathDay

Utakumbuka Siku chache zilizopita, March 28, 2018 mara baada ya aliyekuwa Baby Mama wa Diamond Platnumz, Zari The Boss Lady kupata dili la kuwa balozi wa bidhaa za Softcare Diapers, Kifesi alitupa lawama kwa Diamond kwa kumuacha Zari kwa kudai alikuwa ni mwanamke wa Baraka aliyepewa na Mungu.

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO 0754372325/ 0689013109/ 0620806813 

HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Ni Dr. Chief Malunde Pekee Anaetibu Nguvu Za Kiume Na Kumtuliza Umpendae Kwa Kutumia Dawa Za Asili

0
0
"NI DR. CHIEF MALUNDE PEKEE ANAETIBU NGUVU ZA KIUME NA KUMTULIZA UMPENDAE KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI"
-baada ya kujichimbia katika nchi za kiarabu kwa zaidi ya miaka (10)sasa amewasili nchini na dawa za tiba asilia.
 
1/NGOLO 3 POWER-ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, ina ubora wa hali ya juu wa kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wasiojiweza kufanya tendo la ndoa, inaimarisha misuli iliyolegea na kusinyaa, inarutubisha mbegu za kiume na kukufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15-25 kuwa na hamu na tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila kuchoka, inarefusha uume inchi 5-8 na kunenepesha hadi cm 4 kwa wenye maumbile madogo, dawa hii imeboreshwa na hutibu matatizo haya kwa muda mfupi tu.
 
2/MAGOYE MVUTO- dawa hii ina uwezo mkubwa sana kumvuta na kumtuliza aliekuacha awe mpenzi, mme/mke itamfanya akutafute mwenyewe ndani ya masaa 3tu na kukutimizia mahitaji yako kwa haraka na kumfunga asiwe na mtu mwingine.
 
3/SUPER LUBEJA- ni dawa ya kushepu umbo no.8 mguu wa bia, kuongeza hips, na makalio kwa muda wa siku 5tu unapata saizi uipendayo, kuondoa makovu, chunusi, harufu mbaya ya mwili michirizi, kupunguza tumbo na maziwa kwa siku 6tu.
 
4/NG'WESHI MIX- ni dawa ya biashara ya kupata wateja wengi, kusafisha nyota, kurudishwa kazini na kupandishwa cheo, kurudisha mali iliyoibiwa au kudhurumiwa.
 
PIA TUNATIBU MAGONJWA SUGU KAMA: vidonda vya tumbo, ngiri, chango na uzazi kwa kina mama: (dawa zote hazina madhara kwa mtumiaji) HUDUMA HIZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO: TUNAPATIKANA DSM BUGURUNI SHELI AU PIGA SIM NO_ 0763-181099.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Mbowe Atuma Salamu Toka Gerezani

0
0
Viongozi sita wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe, wamewataka Watanzania na wanachama wao wasiogope kwa sababu katika kupigania haki, demokrasia, amani na ustawi wa nchi lazima wapatikane watakaoumia kwa ajili ya wengine.

Ujumbe huo wameutoa wakiwa ndani ya Gereza la Segerea, Dar es Salaam jana ikiwa ni siku moja imepita baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuamuru viongozi hao wafikishwe mahakamani Aprili 3, mwaka huu ili kutimiza masharti ya dhamana zao baada ya juzi kudaiwa kushindwa kufikishwa kutokana na gari kuwa bovu.

Ujumbe huo wa Mbowe na viongozi wenzake ulitolewa jana na Mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini na kada wa chama hicho, Dk. Makongoro Mahanga, waliopata muda wa nusu saa kuzungumza mambo mbalimbali na viongozi hao.

Selasini na Mahanga waliweka ujumbe huo katika akaunti zao za mtandao wa Facebook, pamoja na mambo mengine walisema wamewaona viongozi na haya ndiyo maneno yao: ‘Tuko imara, tuko vizuri. Wapelekeeni wenzetu ujumbe huu. Msiogope. Taifa linatutegemea. Chadema ndiyo pekee itakayobadilisha uonevu unaofanywa na watawala kwa Watanzania na kuwahakikishia demokrasia, amani ya kweli, haki na maendeleo. Tukiwa waoga tutakuwa wasaliti wa matamanio hayo ya Watanzania.’

“Wamesema pia wamepata muda mzuri wa kupumzika na kufanya retreat (tafakari ya kina. Tumemkuta Mbowe akiwa na Biblia mkononi. Amesema amesoma na karibu anamaliza Injili zote. Pia yeye pamoja na Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini leo (jana) wataadhimisha ibada ya Ijumaa Kuu kwa kuwashirikisha mahabusu na wafungwa wote wao kama watumishi wa neno la Mungu.”

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Bavicha wasema upo mpango wa kuifuta Chadema

0
0
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema, (Bavicha) Patric Ole Sosopi, amesema Serikali ya awamu ya tano ina lengo la kuifuta Chadema.

Akizungumza leo, Machi 31, katika mkutano na wanahabari uliofanyika katika ofisi za chama hicho, Sosopi amesema, wapo watu wanaotumwa na Serikali kuichafua Chadema na kupata sababu ya kukifuta chama hicho.

“Tumewapuuza kwa muda mrefu, tukiamini vyombo vitachukua hatua dhidi yake lakini kwa kuwa wanamtuma anaendelea kuwa salama,” amesema.
 
Amesema Chadema inawahakikishia Watanzania kuwa jitihada za kuifuta Chadema hazitafanikiwa na hakuna yeyote atakayeifuta Chadema.

Dogo Janja akubali kuwa ‘Video Queen’ katika video ya Nikki Mbishi

0
0
Takribani wiki mbili zilizopita Dogo Janja aliingia katika headlines hasa katika stori za kidaku mara baada ya kutokea katika video ya ngoma yake ‘Wayu Wayu’ akiwa na muonekana wa kike.

Kitendo hicho kilizua mjadala mpana kiasi katika music industry kwa hapa Bongo. Sasa Rapper Nikki Mbishi hajawa nyuma katika hilo, kupitia ukurasa wa twitter Nikki ameandika; Dogo Janja ni “VIDEO QUEEN” .

Baada ya tweet hiyo Dogo Janja amejibu; Chupa Lako Ukinihitaji Onana Na Management bei yangu SIO GHALI SANA.

Jibu hilo linaweza kutafsiriwa kuwa Dogo Janja yupo tayari kufanya hivyo katika video ya Nikki au msanii yeyote ila kinachotakiwa ni kuonana na menejimenti yake kwa ajili ya malipo kitu ambacho mwishoni amesisitiza sio ghali.

Madee ambaye anafanya kazi na Dogo Janja kupitia Tip Top Connection anatajwa kuwa ndiye alimpatia Janjaro idea ya video hiyo. Madee alikaririwa akisema idea hiyo alitaka kuitumia katika video yake ila hakuwa na wimbo wa kutoa hivi karibuni ndipo akaitoa kwa dogo Janja.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images