Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mbowe na Viongozi Wenzake Kula Sikukuu ya Pasaka Gerezani

0
0
Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Wilbard Mashauri amesema baada ya kusikiliza hoja zilizowasilishwa na upande wa Serikali na utetezi katika kesi inayowakabili viongozi wa Chadema, akiwemo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe washtakiwa hao wafikishwe mahakamani hapo Aprili 3, 2018.

Amesema siku hiyo washtakiwa watasaini bondi ya Sh20 milioni na wakiwa huru ndipo utaratibu wa kukata rufaa wa upande wa mashtaka utafanyika.
 
 “Nikitoa dhamana wakati washtakiwa hawapo haina maana zoezi zima lisimame.Leo washtakiwa hawajafikishwa mahakamani na nimetoa masharti ya dhamana, hivyo kutoa dhamana na  washtakiwa wakiwa bado hawajasaini ilo zoezi bado halijakamilika.

“Hivyo kwenye hatua ya sasa ni mapema mno kwa upande wa mashtaka kuwasilisha hoja za kukata rufaa wakati bado mchakato haujakamilika.

“Mahakama inatoa remove order waje mahakamani April 3,2018 na wadhamini wao ili waje kukamilisha masharti ya dhamana.”  Amesema Hakimu Mashauri.

Kufuatia uamuzi huo, viongozi hao watakula Sikukuu ya Pasaka wakiwa mahabusu. Sikukuu hiyo inasherehekewa kuanzia kesho hadi Jumatatu.

Awali, Hakimu Mashauri alieleza dhamana kwa washtakiwa hao iko wazi, jambo ambalo lilipingwa na upande wa Serikali.

Washtakiwa hao walitakiwa kila mmoja kuwa na wadhamini wawili ambao watasaini hati ya dhamana ya Sh20 milioni na kuwa na barua kutoka kwa viongozi wao ama wa vijiji au mtaa, ambao watapaswa kuwa na nakala za vitambulisho vyao.

Hakimu alisema kwa asiyeridhika na uamuzi huo ana haki ya kukata rufaa.

Katika mvutano wa kisheria, mmoja wa mawakili wa viongozi hao, Peter Kibatala alipinga taarifa ya rufaa iliyotolewa na wakili wa Serikali.

Kibatala aliiomba mahakama kutekeleza amri yake ya dhamana kwa kuwasainisha washtakiwa bondi ya Sh20 milioni kila mmoja katika tarehe ambayo inaona inafaa na baada ya hapo ndipo ipokee taarifa ya Serikali ya kukata rufaa.

Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi alidai kuwa hilo ni suala la kisheria kwa kuwa taarifa ya rufaa ikishawasilishwa mahakamani na kupokewa, mahakama husika itakuwa imefungwa mikono kuongea chochote kuhusiana na taarifa hiyo kwa maelezo kuwa itakuwa imeingia katika kumbukumbu za mahakama.

Serikali Yawasamehe Roma Mkatoliki na PretyKind, Wafutiwa Adhabu

0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe na Naibu wake, Juliana Shonza, leo wametangaza kufuta adhabu ya kufungia wasanii wa  muziki wa Kizazi Kipya, Roma Mkatoliki na Suzan Michael maarufu kama Pretykind.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi ya Wizara hiyo jijini Dar es salaam Waziri Mwakyembe amesema kuwa muda wowote kuanzia sasa Roma Mkatoliki atakuwa huru kufanya shughuli zake za muziki kama ilivyokuwa awali kwa sharti moja la kukamilisha taratibu za kujisajili BASATA.

Kwa upande mwingine, Roma Mkatoliki ambaye naye aliongozana na Waziri Mwakyembe amesema kuwa hata kama ameachiwa huru lakini wimbo wake wa kibamia ataviomba vituo vya redio na runinga kutocheza wimbo huo.

Mwanzoni mwa mwezi Machi serikali kupitia Wizara ya Habari ilitangaza kumfungia miezi sita msanii Roma Mkatoliki kutojihusisha na masuala ya muziki kwa kukaidi amri ya kubadilisha baadhi ya mashairi ya wimbo wake wa Kiba100.

Suzan Michael maarufu kama Pretykind naye alipewa nafasi ya kuongea na wanahabari ambapo alitoa pongezi kwa serikali kwa kumfundisha malezi mema na kuwaasa wasanii wenzake kuwa na tabia nzuri.

Wizara ya Mambo ya Nje yasisitiza hakuna maandamano Aprili 26

0
0
Kumekuwa na taarifa kwenye mitandao ya kijamii zinazosambazwa na watu wasioitakia mema nchi, zinazotishia usalama wa raia na mali zao. Taarifa hizo zimewatia hofu baadhi ya raia wa kigeni na wanadiplomasia wanaofanya kazi na kuishi hapa nchini.

Taarifa hizo zimekuwa zikidai kuwa kutakuwa na maandamano yatakayofanyika tarehe 26 Aprili 2018 na zinawaonya raia wa kigeni wasiende Zanzibar katika kipindi cha Sikukuu ya Pasaka na sherehe za Muungano kwa sababu za kiusalama.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawahakikishia wanadiplomasia na raia wote wa kigeni wanaofanya kazi na kuishi nchini na wananchi kwa ujumla kuwa, waendelee na shughuli zao ikiwemo kusafari kutoka eneo moja kwenda jingine bila ya hofu yeyote kwa kuwa hakuna dalili zozote za uvunjifu wa amani, usalama na utulivu wa nchi.Vyombo vya usalama vipo makini vinatekeleza majukumu yake ipasavyo kuhakikisha kuwa matukio yote ya uhalifu yanadhibitiwa kabla ya kuleta madhara kwa umma. 

Hivyo, Wizara inawaomba wanadiplomasia, raia wa kigeni wanaoishi nchini na wananchi kwa ujumla kuzipuuza taarifa hizo. Wananchi waendelee kushirikiana kwa karibu na Serikali yao kupata taarifa sahihi kutoka vyanzo vinavyoaminika badala ya kutegemea propaganda za watu wanaotumia mitandao ya kijamii kwa maslahi binafsi. 

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 29 Machi 2018

Ajali ya Basi Yaua Watano Kagera

0
0
Watu watano wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya basi moja kati ya manane yaliyokuwa yakisafirisha wakimbizi kutoka kambi ya Nduta wilayani Kibondo mkoani Kigoma kuelekea nchini Burundi kupinduka.

Ajali hiyo imetokea leo Machi 29,2018 katika Kijiji cha Kasharazi wilayani Ngara mkoani Kagera saa 10:00 jioni.

Taarifa zinasema ajali imetokea eneo la K9 lenye mteremko na kona kali baada ya kupata hitilafu ya mfumo wa breki na kisha kuligonga lingine lililokuwa mbele na baadaye kupinduka.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Agustino Olomi akizungumzia ajali hiyo amesema miili ya waliofariki dunia bado haijatambuliwa pamoja na idadi ya majeruhi.

Amesema waliofariki dunia ni wanawake watatu na wanaume wawili. Kati yao yupo mkazi wa Kasharazi aliyekuwa akiendesha baiskeli ambaye basi lilimwangukia.

Mmoja kati ya madereva waliokuwa katika msafara huo, Raymond Revocatus amesema kila basi lilikuwa na wastani wa abiria 65.

Baadhi ya majeruhi wamepelekwa katika Hospitali ya Murugwanza wilayani Ngara kwa matibabu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya March 30

Msemaji wa Serikali: Hatujazuia Serikali Kukosolewa, Bali Misingi ya Maadili Ifuatwe

0
0
SERIKALI imesema haijazuia vyombo vya habari kukosoa utekelezaji wa sera, mikakati na programu zake na badala yake imewataka kuzingatia miiko na maadili ya taaluma hiyo yaliyoanishwa na sheria za kimataifa.

Hayo yamesemwa jana Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi wakati wa uzinduzi wa Awamu ya 25 ya utafiti wa sauti ya wananchi iliyotolewa na taasisi ya Twaweza.

Dkt. Abbasi alisema kumekuwepo na mkanganyiko mkubwa kuhusu dhana  ya uhuru wa habari, hatua inayosababisha baadhi ya vyombo vya habari kuandika na kutangaza taarifa mbalimbali ambazo zimekuwa zikikiuka misingi ya sheria za nchi.

“Wapo baadhi ya watu wamekuwa wakifikiri dhana ya uhuru ni kusema chochote na kutumia lugha ya kejeli, hivyo ripoti hii ya utafiti tumeweza kuwa na wataalamu mbalimbali waliokuwa wakitoa mada na kujadili kwa kina misingi na miiko ya uhuru wa habari” alisema Dkt. Abbasi.

Alisema kuwa dhana ya uhuru wa habari ipo katika sheria mbalimbali za kimataifa iliyoanishwa katika misingi ya haki na wajibu, na hivyo ni wajibu wa wadau mbalimbali kuwawezesha wananchi na vyombo vya habari nchini kuweza kuelewa dhana hiyo.

Aliongeza kuwa Serikali imeendelea kuongeza wigo mpana wa uanzishaji wa vyombo vya habari nchini ikiwemo kutoa idadi kubwa ya leseni za uanzishaji wa vituo vya redio hususani katika maeneo ya vijijini, hatua inayolenga kuwawezesha wananchi kuweza kupata taarifa mbalimbali za umma.

Kuhusu taarifa ya utafiti huo, Dkt. Abbasi alisema Serikali itatumia taarifa ya ripoti ya utafiti huo kupata mrejesho na kuainisha maeneo yote ili kuchambua hoja na kuweza kuangalia maeneo yenye changamoto ili kuweza kuboresha mfumo wa utoaji na upatikanaji wa taarifa za Serikali kwa wananchi.

Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alisema Serikali tayari imetoa maelekezo kwa Maafisa Habari na Mawasiliano wa Taasisi zote za umma nchini kuweka utaratibu wa kutoa taarifa zake kwa umma kwa kuwa suala la utoaji wa taarifa si utashi na badala yake ni utekelezaji wa matakwa ya sheria.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze alisema katika utafiti huo uliohusisha jumla ya watu 1500, ulionyesha kuwa wananchi wana imani na taarifa na imani zinazotolewa na Viongozi Wakuu wa Serikali ikiwemo Rais ikifuatiwa na Waziri Mkuu.

Kajala Masanja Akana Kutoka Kimapenzi na Chege

0
0
Msanii wa filamu nchini Kajala Masanja amefunguka na kuweka wazi kuhusu tetesi zinazosambaa kuwa sasa anatoka kimapenzi na msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka kiumeni Chege Chigunda.

Kajala akiomgea kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio amekana kuhusu kutoka kimapenzi na msanii huyo na kudai kuwa hakuna jambo kama hilo na

"Mama yangu mzazi hakuna kitu kama hicho si mmeona Chege kapata mtoto juzi tu hapa, yaani mimi sina hata namba yake ya simu na haiwezi kutokea kitu kama hicho"alisisitiza Kajala

Mbali na hilo Kajala amewatakia kheri wanawake wote maarufu ambao wanakaribia kuolewa siku za karibuni na kusema kwake yeye badobado kwani anaamini mume mwema anatoka kwa Mungu hivyo atakapompata huenda na yeye ndiyo akafanya maamuzi hayo ya kuolewa sasa.

Mkuu wa Jeshi, Waziri wa Mambo ya Ndani Kenya Wahukumiwa Kwa Kuidharau Mahakama Sakata la Miguna

0
0
Mahakam nchini Kenya imewapiga faini waziri wa mambo wa mambo ya ndani Fred Matiang'i na mkuu wa jeshi la polisi Joseph Boinnet baada ya wawili hao kudharau amri yake kuhusu kumuachia mwanasiasa wa upinzani Miguna Miguna

Waziri wa mambo ya ndani wa Kenya na Inspekta Janerali Mkuu wa Polisi wamepigwa faini kwa kuidharau mahakam siku ya Alhamisi, kwa kushindwa kutii agizo la jaji kumuachia mwanasiasa wa upinzani, katika hukumu iliochochea zaidi mgogoro kati ya mihimili miwili ya dola.

Jaji wa mahakama Kuu George Odunga amesema maafisa hao wawili waandamizi serikalini "walidhihirsha tabia isiyotarajiwa katika zama hizi za kikatiba," - katika ukaripiaji usiokifani kwa maafisa wa juu serikalini.

Waziri wa mambo ya ndani Fred Matiang'i, na inspekta Jenerali Mkuu wa Polisi Joseph Boinet wametozwa kila mmoja shilingi za Kenya 200,000, sawa na dola za Marekani 1,985, kutokana na ushiriki wao katika kumzuwia mwansiasa wa upinzani Miguna Miguna wiki hii.

Mahakama nchini Kenya imekuwa katika msuguano na mhimili wa utawala tangu ilipobatilisha ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa Agosti 2017.

Miguna Miguna, mwanasiasa maarufu lakini asiechaguliwa kutoka muungano wa upinzani wa NASA, alijipatia umaarufu baada ya kufukuzwa nchini mwezi uliopita, na jaribio lake la kurejea Kenya wiki hii limeshuhudia nchi hiyo ikiingia katika sarakasi za kisiasa.

Wakati Miguna alipozuwiwa kwenye uwanja wa ndege kuhusiana na mgogoro wa uhamiaji, mahakama kuu iliwaamuru mara mbili, waziri wa mambo ya ndani Fred Matiang'i, mkuu wa jeshi la polisi Joseph Boinnet na kamishna mkuu wa idara ya uhamiaji kumfikisha mahakamani.

Mvutano kati ya mihimili mikuu miwili
Vita vinavyozidi kati ya serikali na mahakama - tangu mahakama ya juu kabisaa ilipobatilisha ushindi wa rais Uhuru Kenyatta mwaka uliopita -- vimeshuhudia maafisa wa serikali wakipuuza amri kadhaa za mahakama.

Kufukuzwa kwa kwanza kwa Miguna kulikuja baada ya kukamatwa kwa tuhuma za uhaini kutokana na kushiriki kwake katika tukio la kujiapisha kwa Raila Odinga, aliesisitza kuwa yeye ndiye alikuwa mshindi halali wa uchaguzi wa mwaka uliopita.

Wizara ya mambo ya ndani ya Kenya inasema Miguna alipoteza uraia wake kwa kuchukuwa uraia wa Canada miaka kadhaa iliopita -- wakati ambapo uraia wa nchi mbili ulikuwa hauruhusiwi.

Mwezi Februari, mahakama iliiamuru serikali kumruhusu Miguna arejee, na kumpatia hati mpya ya kusafiria au imruhusu aingie nchini kwa kutumia hati yake ya Canada, wakati akisubiri kusikisiliza shauri la kutetea uraia wake wa Kenya.

Hata hivyo, Miguna alipowasili siku ya Jumatatu, alikataa kuomba visa ya miezi sita, kuingia kwa kutumia hati yake ya Canada au kujaza fomu za kuhalalisha uraia wake.
"Alikataa kusaini nyaraka za kuingia nchini na kuzichana. Alisalia hapa kwa siku mbili na kila zilipopelekwa kwake alitukaripia kwamba yeye ni Mkenya," alisema afisa uhamiaji kwa sharti la kutotajwa jina.

Polisi wamalizia hasira kwa waandishi
Siku ya Jumatatu, polisi wa uwanja wa ndege waliwashambulia na kuwajeruhi waandishi kadhaa wa habari waliokuwa wanaripoti sakata hilo katika tukio lililorekodiwa na kulaaniwa na kamati ya kuwalinda waandishi habari.

Katika taarifa kutoka Dubai, Miguna alisema alizuwiwa chooni kwa siku mbili katika uwanja mkuu wa ndege wa Kenya, na kudai kuwa maafisa walimuangusha chini na kumpiga sindano yenye vitu visivyoeleweka na kumsababishia kupoteza fahamu.

Tukio hilo limekuja wiki kadhaa baada ya maridhiano ya kushtukiua kati ya Odinga na Kenyatta kufuatia msimu wa mgumu wa uchaguzi. Karibu watu 100 waliuawa, wengi wao na jeshi la polisi, wakati wa machafuko ya uchaguzi, kulingana na mashirika ya haki za binadamu.

Credit:DW

Jeshi la Polisi latoa onyo kwa Madereva kipindi cha Sikukuu

0
0
JESHI la Polisi mkoani Pwani limewaasa madereva hususani wa mabasi yanayofanya safari za mikoani ,kuacha kufanya mbwembwe wakati wakiwa barabarani na kutumia vileo katika kipindi hiki cha sikukuu za Pasaka ili kuepusha ajali zembe.

Aidha jeshi hilo limetoa onyo kali kwa wale wenye nia ya kutenda uhalifu kwenye kipindi hicho .

Akizungumza na waandishi wa habari na baadhi ya maofisa wa jeshi hilo ,kuhusiana na operesheni za kaguzi hizo ambazo ni endelevu ,na kutoa salamu za Pasaka ,kaimu kamanda wa polisi ,mkoani Pwani ,(SSP) Abdi Issango ,alisema madereva wafuate sheria za usalama barabarani bila kushurutishwa .

Amesema wanafanya operesheni ya kukagua madereva wa mabasi hayo na kufanikiwa kuwakamata madereva 29 kwa makosa ya mwendo kasi na kulipita gari la mbele sehemu isiyoruhusiwa (wrong overtaking).

Pamoja na hayo ,Issango alielezea madereva 22 walikamatwa kwa kosa hilo na madereva saba walikamatwa kwa kosa la mwendo kasi .

Alibainisha dereva mmoja alipewa onyo kutokana na kosa lake ,madereva watano waliadhibiwa kwa kulipishwa faini ,na madereva 23 watafikishwa mahakamani kuweza kujibu mashtaka yanayowakabili .

"Katika operesheni hii ,dereva wa kampuni ya basi la Super Feo lenye namba za usajili T.754 DML linalofanya safari zake kati ya Dar es salaam -Songea ,Peter Augustino (38) mkazi wa Makambako "

" Yeye tutamfikisha mahakamani kwa makosa mawili ya kulipita gari la mbele sehemu isiyoruhusiwa  na kuendesha gari akiwa ametumia kileo ambapo baada ya kumpima alikutwa akiwa na kilevi 26.8mg/ml.":;alisema Issango.

Kwa mujibu wa Issango machi 28 mwaka huu jeshi hilo limeendesha msako katika maeneo mbalimbali katika mkoa huo na kufanikiwa kukamamata watuhumiwa 21 wakiwa na bangi kete 155 sawa na gramu 77.5.

Alisema huko Mapinga wilayani Bagamoyo ,walimkamata Wilson Jengua akiwa na mtambo mmoja wa kutengeneza pombe ya moshi(gongo) , "Mbali ya mtambo huo ,tumekamata pombe hiyo lita 62 " alifafanua Issango.

Issango ambae pia ni kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Pwani, alieleza watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu mashtaka dhidi yao .

Aliwasihi wahalifu wenye mawazo ya kufanya uhalifu kipindi cha Pasaka wabadili mawazo hayo, kabla ya hatari kwani jeshi hilo limejipanga kikamilifu kupambana na uhalifu wa aina yoyote.

Urusi Nayo Imejibu Mapigo.....Wanadiplomasia 60 wa Marekani Watimuliwa, Ubalozi Wafungwa

0
0
Urusi imewafukuza wanadiplomasia 60 wa Marekani, na kufunga ubalozi uliopo St Petersburg ikiwa ni majibu kwa kitendo cha Marekani kuwafukuza wanadiplomasia wa Urusi juu ya shutuma ya Uingereza kuhusu kuhusika kwa Urusi katika shambulio la jasusi wa zamani wa Urusi Sergei Kripal na binti yake huko Uingereza.

Hatua hiyo ilitangazwa na waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov. Zaidi ya nchi ishirini zimewafukuza wanadiplomasia wa urusi nchini mwao katika kuunga mkono Uingereza.

Miongoni mwa nchi hizo ni Marekani ambapo mapema wiki hii iliwatimua wanadiplomasia 60 wa urusi kuondoka Marekani.

Katika kujibu hilo Urusi imewatimua wanadiplomasia 58 kutoka Moscow na wawili kutoka mji wa Yekaterinburg, chombo cha habari cha Interfax kiliripoti.

Lavrov alisema kuwa nchi nyingine zilizowafukuza Warusi wasubiri majibu kwa vitendo.

Ameongeza kuwa Ubalozi wa Marekani umepewa taarifa juu ya hatua hiyo kama majibu kwa Marekani kwa kuwatimua wanadiplomasia wake na kusimamisha ubalozi ulioko St. Petersburg.

Baada ya hatua hiyo msemaji wa Marekani amesema kuwa Urusi haina nia ya kuwa na uhusiano mzuri na nchi nyingine, na hivyo Marekani ina haki ya kuchukua hatua nyingine dhidi ya Urusi.

''Urusi imeamua kujitenga zaidi yenyewe, tunaangalia maamuzi ya kuchukua'' Heather Nauert aliwaambia waandishi wa habari.
 
Urusi imekataa kuhusika kwa namna yoyote na jaribio la mauaji kwa jasusi wake wa zamani. Kripal bado yupo katika hali mbaya hospitalini lakini Binti yake anaendela vizuri na ameondoka katika hali ya hatari.

Kutokana na kuhusishwa kwa Urusi na tukio hilo mapema Uingereza ilisema kuwa hawatatuma mawaziri wake pamoja na familia ya Malkia kushiriki kombe la dunia.

Itakumbukwa kuwa mwaka 1986 Rais wa Marekani Ronald Reagan aliwatimua wanadiplomasia 80 wa Urusi.

Na mwaka 2016 uongozi wa Barack Obama uliwafukuza wanadiplomasia 35 kutokana na kudukua chama cha Democratic.

Credit:BBC

Magari ya wagonjwa na polisi Yapigwa marufuku barabara za mabasi yaendayo haraka (BRT)

0
0
Wakati uongozi unaosimamia barabara za mabasi yaendayo haraka (BRT), ukipiga marufuku magari ya wagonjwa na polisi kutumia barabara hizo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema watalazimika kuzitumia barabara hizo wakati wa dharura.

Barabara za mabasi yaendayo haraka zimejengwa kwa ajili ya kutoa huduma zake kwenye barabara za Morogoro na Kawawa.

Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari imesisitiza kuwa hakuna chombo chochote cha moto kitakachoruhusiwa kupita katika barabara hizo zaidi ya mabasi ya mwendokasi.

Akifafanua zaidi taarifa hiyo, mkurugenzi wa wakala wa mabasi hayo (Dart), Ronald Lwakatare alisema ni kweli magari ya wagonjwa hayaruhusiwi kupita katika barabara hizo mpaka ruhusa ya polisi wa usalama barabarani.

Katika kusimamia sheria za barabara hizo, alisema zipo kanuni na taratibu mbalimbali ikiwamo sheria za barabarani, halmashauri na nyinginezo.

“Ieleweke kwamba ni marufuku kutumia barabara hizo na mtu yeyote, kwani zimetengenezwa kwa ajili ya magari hayo tu na kama ikatokea likapita basi iwe ni kwa ruhusa ya polisi wa usalama barabarani ambao wao wanajua ni muda gani na sababu gani ya kuyaruhusu magari mengine yapite,”alisema Lwakatare.

Pia mkurugenzi huyo alisema tayari Rais (John Magufuli) alishatoa maagizo ya magari yafanywe nini inapobainika kutumia njia hizo na kuwataka wanachi kuwa makini ili kuepuka kuingia katika matatizo yatakayowapotezea mali na muda wao bila sababu za msingi.

Taarifa hiyo imeeleza pia kuwa magari ya vyombo vya ulinzi na usalama yanapopita katika barabara hizo, huchangia kwa kiasi kikubwa magari ya watu binafsi kufanya hivyo.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa kuanzia jana hakuna gari lolote litakaloruhusiwa kupita kwenye barabara hizo na kwamba hata magari ya wagonjwa hayaruhusiwi kwa kuwa yana utaratibu wake uliozoeleka sehemu zote duniani.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa kuna baadhi ya magari ya wagonjwa hasa yanayotokea mjini kwenda Kimara yamekuwa yakitumia barabara hizo bila kubeba abiria kwa kigezo cha kupitisha wagonjwa.

Jana, Mambosasa alisema anawaunga mkono BRT, lakini polisi itatumia barabara hizo endapo watakuwa na dharura.

“Kama hatuna dharura tutapita barabara za kawaida. Lakini tukiwa na dharura tutapita barabara zote,”alisema Kamanda Mambosasa.

Ndege Tanzania aina ya Bombardier Q400 iliyokuwa imezuiliwa nchini Canada imekwishaondoka kuja nchini

0
0
Kwa Mujibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Gerson Msigwa amesema Ndege ya Tanzania iliyokuwa inashikiliwa nchini Canada imeshaondoka nchini humo na inarejea Tanzania.

Msigwa ameandika hayo kupitia ukurasa wakwe wa mtandao wa kijamii wa Twitter

Pia Msigwa ameongeza kuwa Ndege 3 kubwa, Mbili aina ya Bombardier CS300 kutoka Canada na Moja Boeing 787-8 Dreamliner kutoka Marekani zitawasili baadae mwaka huu


"Ndege yetu aina ya Bombardier Q400 iliyokuwa imezuiliwa nchini Canada ilikwishaondoka Canada kuja Tanzania. Aidha, ndege kubwa nyingine 3 (2 Bombardier CS300 kutoka Canada & 1 Boeing 787-8 Dreamliner kutoka Marekani) zitawasili baadaye mwaka huu. Nawatakia Ijumaa Kuu njema."-Msigwa

Kamanda Mambosasa atoa tahadhari kwa wananchi Msimu Huu wa Sikukuu

0
0

Kamanda wa Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es salaam, Lazaro Mambosasa amesema wamejipanga vizuri katika kuimarisha hali ya usalama nchini katika sikukuu hii ya Pasaka na kudai atakayethubutu kufanya vitendo vya kiharifu atachukuliwa hatua kali.

Kamanda Mambosasa ameeleza hayo leo (Machi 30, 2018) wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam na kusema kulingana na uzoefu waliokuwa nao wamejipanga kuimarisha usalama kwa hali ya juu ili wananchi waweze kusherehekea kwa amani na utulivu.

"Jeshi la Polisi litahakikisha wananchi wa Dsm wanasherehekea sikukuu hii kwa amani na utulivu na kwa kuwa uzoefu unaonesha kwamba mara nyingi katika sherehe kama hizi watu wenye nia ovu wanajiandaa kufanya vitendo vya kiharifu ikiwa na pamoja na kufanya ujambazi ili kujipatia vipato kwaajili ya kusherehekea sikukuu", amesema Mambosasa.

Pamoja na hayo, Mambosasa ameendelea kwa kusema "baada ya kulijua hilo Jeshi la Polisi tumejipanga vizuri, kwamba hakuna mtu yeyote atakayeweza kupata fursa ya kufanya lolote katika uvunjifu wa sheria, tumeimarisha doria lakini tunaendelea na misako maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam katika mikoa yote mitatu na wilaya zote za kipolisi 11".

Kwa upande mwingine, Kamanda Mambosasa amesema hayo yote yanafanyika kwa lengo la kuimarisha hali ya usalama katika siku kama hizi za sikukuuu.

Jeshi la Polisi latoa ripoti kifo cha Akwilina

0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum jijni Dar es salaam, Lazaro Mambosasa, ameelezea hatua inayoendelea kuchukuliwa juu ya askari polisi sita waliokuwa wameshikiliwa kutokana na kifo cha mwanafunzi wa NIT Akwilina Akwilin, aliyeuawa kwa risasi mapema mwaka huu

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es salaam, Kamanda Mambosasa amesema polisi hao bado wapo kwenye uchunguzi kubaini ni nani anahusika, kwani mpaka sasa hakuna ushahidi wa moja kwa moja wa kuweza kumbaini.

“Wale walipokamatwa tulieleza bayana kwamba upelelezi unafanyika ili kujua ni nani ambaye ametenda kosa lile, bado suala la upelezi linaendelea.

"Yapo maelekezo yaliyotolewa ambayo tunaendelea kufuatilia ili kuja kubaini, ikumbukwe silaha moja ambayo haijajulikana ni ipi ndio ilikwenda ikamgusa Akwilina, lakini kama ulivyojua askari walikuwa ni wengi lakini pia kulikuwa hakuna ushahidi kwamba yupi aliyekuwa ametenda hivyo, kwa hiyo uchunguzi bado unaendelea”, amesema Kamnda Mambosasa.

Ikumbukwe kwamba mnamo Februari 17, mwaka huu, mwanafuzi wa chuo cha usafirishaji jijini Dar es salaam Akwilina Akwilini alifariki dunia baada ya kupigwa risasi ambayo inaaminika ilitoka kwa mmoja wa askari waliokuwa wakitawanya maandamano ya wafuasi wa chadema, huku yeye akiwa kwenye daladala akipita njia.

Idriss Sultani Amchokonoa Wema Sepetu

0
0
Mrembo Wema Sepetu ametoa sababu ni kwanini kila mara anapenda kuposti picha za watoto tofauti tofauti katika ukurasa wake wa Instagram.

Ameeleza hayo baada ya kufanya hivyo na baadae mugizaji Idris Sultan kumwambia; si uanzishe tu nursery.

Mrembo huyo aliyekuwa Miss Tanzania mwaka 2006 hakukawia kujibu comment hiyo ya Idriss, ni kama alichokozwa alivyoijibu kwa haraka;

"Dah… mbona ningekuwa nae wa kwangu ningekuwa nampost all the time… ni kwasababu tu sina wangu… so i post every baby dat melts my heart…Since i don’t have one to call my owm… ila ningekuwa nae mbona ungeni-unfollow… Smh…

Utakumbuka mwaka 2016 Idris na Wema walikuwa katika mahusiano ya kimapenzi na ilifikia hatua wakaeleza kuwa wanatarajia kupata watoto mapacha, hata hivyo baadae ilikuja kuripotiwa kuwa ujauzito huo kuharibika.

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO 0754372325/ 0689013109/ 0620806813 

HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Wabunge sita wapata ajali, mmoja alazwa ICU

0
0
Wabunge sita wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamepata ajali ya gari jana usiku Machi 29, 2018 mkoani Morogoro wakati wakitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam.

Baada ya kutokea ajali hiyo saa 2 usiku katika barabara kuu ya Morogoro-Dodoma eneo la Bwawani, wabunge hao waliumia maeneo mbalimbali ya miili yao na kukimbizwa hospitali ya Mkoa wa Morogoro.

Wabunge hao ambao wote ni kutoka Zanzibar ni Haji Ameir Haji (Makunduchi), Khamis Ali Vuai (Mkwajuni), Bhagwanji Maganlal Meisuria (Chwaka), Makame Mashaka Foum (Kijini), Juma Othman Hija (Tumbatu).

Mganga mfawidhi hospitali ya rufaa Mkoa wa Morogoro, Dk Rita Lyamuya amesema majeruhi hao walipokelewa saa 3 usiku na kupatiwa huduma za awali.

"Jana tumepokea majeruhi sita walioumia sehemu mbalimbali na mmoja wao alilazimika kulazwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu (ICU) lakini hali yake inaendelea vizuri,” amesema.

“Leo asubuhi tayari tumewapa rufaa kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi  zaidi.”

Dk Rita amesema Kimbe na May ndio wameumia zaidi, kupata maumivu makali.

Ni Dr. Chief Malunde Pekee Anaetibu Nguvu Za Kiume Na Kumtuliza Umpendae Kwa Kutumia Dawa Za Asili

0
0
"NI DR. CHIEF MALUNDE PEKEE ANAETIBU NGUVU ZA KIUME NA KUMTULIZA UMPENDAE KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI"
-baada ya kujichimbia katika nchi za kiarabu kwa zaidi ya miaka (10)sasa amewasili nchini na dawa za tiba asilia.
 
1/NGOLO 3 POWER-ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, ina ubora wa hali ya juu wa kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wasiojiweza kufanya tendo la ndoa, inaimarisha misuli iliyolegea na kusinyaa, inarutubisha mbegu za kiume na kukufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15-25 kuwa na hamu na tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila kuchoka, inarefusha uume inchi 5-8 na kunenepesha hadi cm 4 kwa wenye maumbile madogo, dawa hii imeboreshwa na hutibu matatizo haya kwa muda mfupi tu.
 
2/MAGOYE MVUTO- dawa hii ina uwezo mkubwa sana kumvuta na kumtuliza aliekuacha awe mpenzi, mme/mke itamfanya akutafute mwenyewe ndani ya masaa 3tu na kukutimizia mahitaji yako kwa haraka na kumfunga asiwe na mtu mwingine.
 
3/SUPER LUBEJA- ni dawa ya kushepu umbo no.8 mguu wa bia, kuongeza hips, na makalio kwa muda wa siku 5tu unapata saizi uipendayo, kuondoa makovu, chunusi, harufu mbaya ya mwili michirizi, kupunguza tumbo na maziwa kwa siku 6tu.
 
4/NG'WESHI MIX- ni dawa ya biashara ya kupata wateja wengi, kusafisha nyota, kurudishwa kazini na kupandishwa cheo, kurudisha mali iliyoibiwa au kudhurumiwa.
 
PIA TUNATIBU MAGONJWA SUGU KAMA: vidonda vya tumbo, ngiri, chango na uzazi kwa kina mama: (dawa zote hazina madhara kwa mtumiaji) HUDUMA HIZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO: TUNAPATIKANA DSM BUGURUNI SHELI AU PIGA SIM NO_ 0763-181099.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images