Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

TANGA RAHA- Sehemu ya Arobaini na Tatu ( 43 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Nikaanza kushangulia huku nikiruka ruka juu, nikaanza kupiga hatua nikiondoka baharini huku nikiwa nimejawa na furaha sana.Gafla nikasutkisha nikastukia nikirushwa juu na nikiwa angani nikalishuhudia joka likiwa limeufumbua mdomo wake, huku likiningojea niingie ndai ya kinywa chake.Nikaanza kurudi chini kwa kasi kubwa huku nikipiga kelele nyigi na moja kwa moja nikaingia ndani ya mdomo wa joka

ENDELEA
Kwa, haraka nikachomo mshale ulipo kwenye podo langu nililo livaa mgongoni, Nikiwa ninaendela kushuka katika tumbo la mwili wangu, huku nikiwa nimeibana pumzi yangu.Nikaukita mshale wangu kwenye tumbo la joka hili na kuanza kuuchana mwili wake huku nikimshale wangu kwenye tumbo la joka hili na kuanza kuuchana mwili wake huku nikiwa ninaendelea kushuka nao chini hadina kumfanya joka hili kuanza kubingiria bingiria huku maji mengi, ya bahari yakiwa yanakingia mwilini mwake
Wingi wa maji unao ingia mwilini mwa joka, yakanifanya niweza kupata nafasi ya kutoka nje ya joka hili ambalo bado linaendela kutapa tapa kwenye maji huku likitoa ukelele mkali.Jokaa likaanza kufutuka huku likiwa moto mkali, Kwa bahati mbaya likanipiga kikumbo, kwa kutumia mkia wake kilichorusha mbali na eneo alilo kuwepo na kunitoa nje ya bahari na kwabahai mbaya nikangukia kwenye kisiki cha mti wa mkono, na kutulia tuli huku giza zito likitawala macho yangu

  ***
 “Eddy......Eddy”
Kwa mbali niliisikia sauti ya Rahma ikiniita,nikayafumbau macho yangu taratibu na kukutana  na mwanga mkali ulio nipiga kwenye macho yangu, huku nikiwa, nimelala kwenye kitanda nikipelekwa nisipo pajua na pembeni yangu akiwepo Rahma naye akionekana akitembea huku machozi yakimwagika.Kila ninapojaribu kuyafumbua macho yangu, nikajikuta nikiona maruweruwe hata watu wanao kisukuma kitanda nilicho kilalia sikuweza kuwaona vizuri.Nikajikuta nikitawaliwa tena na giza kwenye macho yangu, na sikuelewa kilicho endelea.

Macho yangu yakaanza kupata mwangaza tena wakuona mwanga, nikajaribu kuyapitisha pitiasha kwenye kila kona ya chumba na kufanikiwa kutambua kuwa hapa nilipo ni hospitalini.Pembeni ya kitanda changu, kuna meza ndogo, na juu yake imejaa maua mengi pamoja na kadi nyingi, sikujua ni nani aliye ziweka, kwenye mkono wangu wa kushoto nimechomekwa mrija unaodondosha maji taratibu kwenye mishipa yangu.Tumboni kwangu kumefungwa bandeji lililo kaza, lililo zunguka sehemu nzima ya tumbo hadi mgongoni.Nikaiona kadi moja iliyo andikwa maandishi makubwa kwa kalamu ya wino
(Eddy tunakupenda sana endelea kuugua pole,MUNGU atakuponya)

Nikaunyoosha mkono wangu na kuchukua moja ya kadi na kulifungua ndani na kukuta maandishi yanayo nitakia mimi kuugua pole.Mlango ukafunguliwa na akaingia nesi akiwa amevalia mavazi mazuri.Baada ya kuniona akaachia tabasamu pana
“Habari yako kaka Eddy?”
“Salama mambo?”
“Salama, karibu tena duniani”
“Duniani kivipi?”
“Ni story ndefu, ila kwa muda huu pumzika kwanza”
“Sawa, ila Rahma wangu yupo wapi?”
“Amekwenda kupata chakula cha mchana”
“Kwani nesi, hapa nipo wapi?”
“Upo hospitali ya mkoa, Bombo”
“Sawa, ila ninaomba kama una namba ya Rahma mpigie”
“Usijali kwa hilo, kaka yangu”

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 67 na 68 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA-
ILIPOISHIA  

Tukiwa katika hali ya kutambulishana, alama nyekundu kwenye hichi chumba iliyo kwenye ukuta ikaanza kupiga.
“Nini?”  
Nilimuuliza Mariam kwa wasiwasi, aliye anza kuchomoa bastola yake.
“Kuna meli ya maharamia wa Kisomali wanao teka meli za mizigo inatusogelea, sasa leo hawa wameingia choo cha kike”
Mariam alizungumza huku akitoka katika chumba hichi na kuniacha na hawa manahodha ambao nao pia kila mmoja akaanza kuchomoa bastola yake tayari kwa mashambulizi ambayo kwa haraka haraka yanaonekana ni mashambulizi makubwa, kwa maana kila mmoja yupo tayari kufa au kupona.

ENDELEA  
Sikuona haja ya mimi kuendelea kukaa katika eneo hili, nilicho kifanya na mimi ni kutoka katika chumba hichi cha manahodha na kuanza kumfwata Mariam kwa nyuma.
“Ni mpango gani unafanyika?”
Nilumuuliza Mariam kwa sauti ya juu kwa maana king’ora hichi kinatoa sauti kubwa sana, na tunapishana pishana na wafanyakazi wa hii meli wakikimbia huku na kule kujipanga na mashambulizi.
“Mipango gani Dany?”
“Juu ya hawa maharamia?”
“Mipango ni kuwazuia, tukishindwa wao ndio watatuua sisi, tutafute sehemu ambayo tunaweza kujibumashambulizi yao”
Marima alizungumza huku akitembea kwa mwendo wa haraka. Tukaingia kwneye moja ya chumba cha kuhifadhia silaha. Marima akachukua  bunduki zenye uwezo zaidi ya bastola yake, hata mimi nikachangamkia uchukuaji wa silaha.

“Dany kumbuka, hii ni mali ya baba yako na wote humu ndani watakufa kwa ajili ya mali ya baba yako. Pambana na ninatambua kwamba wewe ni mpambananaji”
Mariam alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Nikatabasamu kwa maana kitu  anacho kizungumza Mariam ninakielewa vizuri. Tukatoka katika chumba hichi na kupandisha juu  kabisa ya meli na kutafuta sehemu iliyo kaa vizuri na kujificha. Hatukukaa hata dakika mbili tukaona meli boti mbili za maharamia hawa wa Kisomali zikija kwa kasi katika eneo la meli yetu.

 Nikaishika vizuri bunduki yangu huku nikiwa ninatazama boti hizo jinsi zinavyo kuja. Mariam akaanza kushambulia boti hizo, jambo ambalo lilinifanya na mimi nianze kushambila boti hizi.
Hali ya sauti katika meli hii ikabadilika kabisi, haikuwa ya king’ora kinacho lia ila ni sauti ya milio ya bunduki hizi za kila aina. Maharamia nao wakajitahidi kujibu mashambulizi, ila hali ikawa mbaya kwao kwa maana watu zaidi ya mia moja wanawashambulia wao tu.
    Boti moja ya maharamia, ikalipuka hata kabla hawajafika kwenye meli yetu. Mashabulizi yakahamia kwenye boti hii ya pili ambayo baada ya kuona mashambulizi yamezidi  kuwa makali, wao wenyewe wakaamua kugeuza na kuandoka. Watu weoye kwenye meli wakashangilia kwa furaha kutokana na ushindi ambao tumeupata.

Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) , Simon Sirro Atuma Salamu za Pasaka kwa Watanzania Wote

$
0
0
Inspekta Jenerali wa Polisi, Simon Sirro anawashukuru Wananchi kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa kwa Jeshi la Polisi  jambo ambalo limesaidia kupunguza uhalifu kwa kiasi kikubwa hapa nchini. 

Kiujumla hali ya usalama hapa nchini ni shwari na matukio  makubwa ya uhalifu wa kutumia Silaha yamepungua kwa kiasi kikubwa na jitihada za kukabiliana na makosa ya usalama barabarani zinaendelea ili  kupunguza ajali zinazosababisha vifo na majeruhi kwa raia.

Tunapoelekea kipindi hiki cha Sikukuu ya Pasaka, Jeshi la Polisi katika mikoa yote linawahakikishia wananchi kuwa limejipanga kikamilifu kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kuhakikisha kuwa sikukuu hii inasherekewa kwa amani na utulivu na hakuna vitendo vyovyote vya uhalifu vitakavyofanyika na pale vitakapojitokeza vitadhibitiwa kwa haraka.

Ulinzi utaimarishwa kwenye maeneo yote yakiwemo maeneo ya kuabudia, fukwe, sehemu za starehe na maeneo mengine ambayo yatakuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu ili kuhakikisha wananchi wote wanasherekea sikukuu hiyo katika hali ya  utulivu.

Wazazi wanatakiwa kuwaangalia watoto wao na kutowaacha kutembea peke yao bila ya kuwa na uangalizi wa karibu, pia wamiliki wa kumbi za starehe wanatakiwa  kufuata sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa kumbi hizo ikiwemo kutoruhusu disko toto na kujaza watu kupita kiasi.

Vilevile Jeshi la Polisi linawatahadharisha wale wote ambao watakuwa wakitumia barabara kuwa makini na kuzingatia Sheria za Usalama barabarani hasa kwa madereva wa magari na pikipiki kuepuka kujaza watu kupita kiasi, kubeba mishikaki, kwenda mwendo kasi, kutumia vilevi pamoja na kupiga honi hovyo.

Nawatakia Pasaka njema.

TRA Yazindua Utoaji Wa Vitambulisho Kwa Wafanyabiashara Wadogo

$
0
0
Na Veronica Kazimoto,-Dar es Salaam,
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  jana imezindua rasmi utoaji wa vitambulisho vya Wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi ikiwa ni pamoja na Wamachinga.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi huo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo Charles Kichere alisema kuwa, utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo unatokana na marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015 yaliyofanywa na Bunge la Bajeti la Mwaka wa Fedha 2017/2018 ambapo moja ya marekebisho hayo ni kuwatambua na kuwapatia vitambulisho maalum wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi.

“Baada ya marekebisho ya Bunge la Bajeti la Mwaka wa Fedha 2017/2018, zoezi hili la kuwatambua wafanyabiashara wadogo lilianza kutekelezwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania  kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kama vile Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) pamoja na Idara ya Uhamiaji”, alisema Kichere.

Kichere alieleza kwamba, TRA  kwa kushirikiana na wadau hao, ilianza kutekeleza jukumu hilo kwa kuutambua Umoja wa Wamachinga wa Kariakoo jijini Dar es Salaam na kufanikiwa kuwapatia vitambulisho vya Taifa na Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) ambapo leo hii baadhi yao wamepatiwa vitambulisho maalum vya wafanyabiashara wadogo kama ishara ya uzinduzi wa utoaji wa vitambulisho hivyo.

Aliongeza kuwa,  zoezi la kutambua vikundi mbalimbali vya wafanyabiashara wadogo na kuwapatia Kitambulisho cha Taifa na Namba ya Utambulisho wa Mlipa kodi linaendelea kufanyika nchi nzima na kubainisha kuwa, ili wafanyabiashara wadogo waweze kupata vitambulisho hivyo maalum,  wanatakiwa kujiunga katika vikundi vinavyotambuliwa kisheria na Serikali, kuwa na Kitambulisho cha Taifa, kuwa na Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi ya kikundi alichojiunga nacho pamoja na kuchangia shilingi 10,000.

“Zoezi la kuwatambua wafanyabiashara wadogo linaendelea kufanyika nchi nzima na vitambulisho maalum vinavyotolewa kwa  wafanyabiashara hao vitadumu na kutumika kwa kipindi cha miaka mitatu (3). Maelezo ya mfanyabishara mdogo yaliyopo kwenye kitambulisho hicho maalum ni pamoja na jina na picha ya mfanyabiashara, jina la eneo analofanyia biashara, Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi na Sahihi ya mfanyabiashara husika”, Alifafanua Kichere.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam Mhe. Sophia Mjema aliishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Rais John Pombe Magufuli kwa kuwatambua wafanyabiashara wadogo ili waweze kupiga hatua kiuchumi kutoka daraja la chini hadi la kati na hatimaye kuweza kuchangia maendeleo ya nchi kupitia ulipaji wa kodi mbalimbali.

“Lakini kwanza naomba nimshukuru Mhe. Rais wetu John Pombe Magufuli kwa hii ndoto yake ya kuwasaidia wanyonge waliokuwa wanafanya biashara ndogo ndogo kutambulika na Serikali na kisha waondoke katika hali ya daraja la chini na kufikia daraja la kati.  Nafurahi kuwaeleza kwamba, ndoto ya Mhe. Rais wetu imetimia”, alisema Mjema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Shirikisho la Wamachinga wa Kariakoo jijini Dar es Salaam Steven Lusinde alisema kuwa, wamefurahishwa na azma ya Serikali ya kuwatambua wafanyabiashara walio kwenye sekta isiyo rasmi kwa kuwa wamekuwa na hamu ya kuchangia maendeleo ya Taifa kwa muda mrefu.

“Sisi wamachinga tumekuwa na hamu kubwa sana ya kuchangia Taifa letu kwa sababu tunaamini chochote tunachokiona katika nchi hii bila sisi kuchangia hakiwezi kwenda”, alieleza Lusinde.

Moja ya majukumu ya Mamlaka ya Mapato Tanzania ni kukusanya mapato ya Serikali sambamba na kutoa elimu kwa walipakodi na watanzania kwa ujumla ili kuongeza uhiari wa ulipaji kodi na kuongeza mapato ya Serikali ambayo yanahitajika katika kuleta maendeleo ya nchi pamoja na wananchi wake.

Kenya Na Tanzania Wahakiki Mpaka Wa Kimataifa wa Tanzania Na Kenya

$
0
0
Na Rehema Isango, Tarime, Mara
Timu za watalaamu wa upimaji ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Tanzania na taasisi za usimamizi wa Ardhi nchini Kenya zimekutana wilayani Tarime mkoani Mara kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa kazi ya kuhakiki na kuimarisha mpaka wa Kimataifa baina ya nchi hizi mbili.

Mapema mwezi Machi, Naibu Waziri wa Adhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula alitangaza azma  ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanza  kuimarisha mipaka yake kwa nchi jirani za Kenya na Uganda baada ya ziara yake ya kukagua mpaka wa Tanzania na Kenya katika Mbuga ya Wanyama ya Taifa ya Serengeti iliyopo mkoani Mara.

Hatua ya  uhakiki na uimarishaji wa alama za mipaka ya mikataifa inatokana na mpaka huu kuwa wa siku nyingi na haukuwa wazi katika maeneo mengi pia baadhi ya alama hizo kuharibiwa, kung’olewa au kuchakaa na hivyo kusababisha Serikali pande zote kushindwa kusimamia kwa ufanisi shughuli za mipakani, rasilimali za nchi pamoja na ulinzi na usalama.

Katika uimarishaji wa alama hizo za mipaka hivi sasa, kutaongezwa alama mpya ndogo zinazoonana kwa umbali wa mita 100  pamoja na kubainisha eneo la ardhi huru kwa kila upande wa nchi (buffer  zone).

Mpaka kati ya Tanzania na Kenya una jumla ya urefu wa Kilommita 760 kuelekea bahari ya Hindi ambapo awamu ya kwanza ya kazi ya uimarishaji mpaka  inayofanyika hivi sasa itahusisha urefu wa Kilomita 238 kutoka kando ya Ziwa Victoria mkoani Mara hadi Ziwa Natron mkoani Arusha.

Baadaye, kazi ya uhakiki na uimarishaji wa mipaka itaendelea katika mikoa ya Kilimanjaro na Tanga na kisha itafanyika katika maeneo yote yanayohusika na  mipaka ya kimataifa nchini.

Uimarishaji wa mipaka ya kimataifa nchini umefanyika mara ya mwisho mwaka 1975 kwa kurudishia alama  ambazo ziliondolewa na kuongeza  nyingine mpya kwa kuzingatia alama zilizopo.

Mbali na Kenya nchi nyingine zinazopakana na Tanzania ni; Msumbiji, Malawi, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Burundi, Rwanda, Uganda pamoja na visiwa vya Komoro na Shelisheli.

Mwanza: Mwanaume Amuua Mkewe na Yeye Kajinyonga Hadi Kufa

$
0
0
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la John Mtemi (23) amejinyonga baada ya kumuua mke wake Casta Edward kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amesema tukio hilo lilitokea  Machi 26 saa sita  mchana katika Kijiji Mahaha,  Kata ya Shishani wilayani Magu.

Kamanda Msangi amesema tukio hilo limegundulika  baada ya mwenye nyumba waliyokuwa wakiishi Daudi Philipo kupita nje ya nyumba hiyo na kuona damu zikiwa zimechuruzika nje ya mlango wa nyumba waliyokuwa wakiishi wanandoa hao.

“Polisi wamekuta mwili wa mwanamke upo mlangoni lakini ilionekana michirizi ya damu kutoka chumbani, na polisi walipoingia chumbani walikuta mwili wa mwanaume ukining’inia kwenye waya wa umeme,” amesema Msangi.

Amesema  chanzo cha mauaji bado hakijafahamika licha ya kudaiwa kuwa wanandoa hao walikuwa wakiishi kwa amani bila ugonvi wowote na kwamba uchunguzi bado unaendelea.

Miili ya marehemu imehifadhiwa Hospitali ya Wilaya ya Magu kwa ajili ya uchunguzi na ukikamilika itakabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya mazishi.

Kamanda huyo amewataka wana ndoa kutojichukulia sheria mkononi na kuomba wananchi waendelee kutoa taarifa za uhalifu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya March 29


Times FM Waomba Radhi kwa Kauli za Msanii Diiamond

$
0
0
Kituo cha Redio Times cha jijini Dar es Salaam kilichorusha mahojiano ya  mwanamuziki Diamond Platnumz kimeomba radhi kwa kauli tata zilizozua mjadala nchini.

Taarifa hiyo iliyowekwa  katika mtandao wa kijamii wa Instagram, ilisema imeamua kuomba radhi kutokana na kauli tata alizotumia msanii huyo wakati akihojiwa katika kipindi cha Play List kinachoongozwa na mtangazaji Omary Tambwe.

Taarifa hiyo ilieleza kwamba siku hiyo Diamond alialikwa katika kipindi hicho  kwa ajili ya kupongezwa kwa kumpa tuzo maalumu nyota wa mchezo kwa mchango wake kwenye muziki na  kutoa ajira kwa vijana.

Jingine ni kutangaza lugha ya Kiswahili kupitia muziki na kupeperusha bendera ya Tanzania kupitia sanaa ya muziki na kutoa albamu yake mpya ya ‘A Boy From Tandale ‘  ambapo kituo hicho kilimtaja kama msanii bora wa kiume, msanii bora wa kimataifa kwa kuvunja rekodi na  msanii mwenye ushawishi zaidi na pia kumpatia tuzo maalum (Plaque).

“Kwa namna ambayo haikutarajiwa , mwanamuziki huyo alitumia kauli  tata dhidi ya Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Juliana Shonza katika mahojiano hayo.
 
“Uongozi wa Times unaomba radhi kwa Wizara, Naibu Waziri, TCRA, Basata pamoja na umma kutokana na kauli hiyo ya Diamond kwani Times haikuwa dhamira yetu kwa sintofahamu hiyo na tumekuwa tunafanya jazi kwa kuzingatia sheria na taratibu za utangazaji,” imesema taarifa hiyo.
Add caption

Tamko la CHADEMA kuhusu Viongozi wao Kulazwa Mahabusu

$
0
0
Kamati Kuu ya chama hicho jana Jumatano, Mach 28 ilikutana  na  kutoa  msimamo wake  ambapo walidai kuwa hawapo tayari kuendelea  kuonewa.  

Juzi Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na viongozi wenzake  walifikishwa mahakamani na kuswekwa rumande baada ya kunyimwa dhamana,

Baadhi ya viongozi wa Chadema waliozungumza ni pamoja na Makamu mwenyekiti wa Chadema, Profesa Safari, Godbless Lema na John Mrema, ambapo mkutano huo pia ulihudhuriwa na Wajumbe wa Kamati Kuu akiwemo Edward Lowassa, Fredrick Sumaye na Meya Boniface Jacob.

Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Prof. Abdallah Safari alisema tukio la kunyimwa dhamana na kupelekwa rumande kwa viongozi hao ni uonevu kwani dhamana ni haki ya mtuhumiwa anapokamatwa.

“Licha yaa jitihada za mawakili wetu kuwatetea viongozi wetu lakini wamewanyima dhamana. Tumemwandikia barua Jaji Mkuu kumwambia mbona kila tunapokamatwa linapofika swala la dhamana tunakataliwa? Jaji Mkuu kajibu kirahisi sana eti kateni rufaa,” alisema Prof. Abdallah Safari.

Kwa upande wake, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema kwamba anafahamu kuwa upo mkakati wa kuwafunga Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe pamoja na viongozi wengine waliowekwa mahabusu tangu jana.

“Huo mchezo wanaotaka kufanya waendelee nao, wamewanyima dhamana ili kesi iendeshwe haraka na wawafunge kama alivyofanyiwa Sugu. Tunajua vikao vyao na nia yao. Wakitaka tusema, ukiogopa kufa utakufa.

“Sisi tutaweka mambo mengi hadharani, sina uhakika kama Mwenyekiti wetu kesho(leo) atapewa dhamana. Hapa tulipofika hatuwezi kuendelea kuishi kwa hofu. Hii vita si ya Chadema, hii ni vita ya demokrasia, Akwilina hakuwa mwanachama wa Chadema lakini aliawa, sasa nafikiri inatosha.

“Baada ya kutoka mahakamani kesho(leo) tutakutana na kuamua iwapo tufungulie maji na tuanike kila kitu kwa sababu hatuna namna. Yeyote aliyehusika tutamuanika,” alisema Lema.

TANESCO yakanusha taarifa inayodai kuwa huduma ya mauzo ya LUKU itapatikana katika Ofisi za TANESCO pekee

Taswira ya Vijana Tanzania (TAVITA) Yalaani Wanasiasa Wanaochochea Uvunjifu wa Amani

$
0
0
Taswira ya Vijana Tanzania (TAVITA) imelaani vikali uchochezi unaofanywa na baadhi ya wanasiasa kupitia mitandao ya kijamii dhidi ya Serikali ya Awamu ya tano.

Akizungumza jana  jijini Dar es Salaam, Katibu wa TAVITA Otieno Peter alisema Serikali ya awamu ya tano imefanya mambo mengi kama vile kuanzisha miradi mikubwa kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania na kurejesha nidhamu kwa watumishi wa umma.

Pia imejikita katika kusimamia rasilimali za nchi, kuhimiza uwajibika na kukomesha vitendo vya rushwa.Hivyo inasikitisha kuona baadhi ya watu wakitumia muda wao mwingi kuchochea uvunjifu wa amani badala ya kuelimisha jamii na endapo amani itapotea itakua imeharibu dira ya nchi yetu.

Ameviomba vyombo vya habari kutumia kalamu zao katika kuelimisha kuhusu masuala ya maendeleo kwa maslahi ya Taifa.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa taasisi hiyo Shabani  Mwanga amewataka wananchi kutokubali taarifa zinazotolewa kwa ajili ya kuharibu taswira njema ya nchi kwani hao wanaofanya hivyo wanataka kuvuruga amani ya nchi iliyopo.

"Kamwe tusikubali kuyumbishwa na mawakala ambao wanatumia saa 24 kutoa taarifa za kupaka matope ili kuharibu taswira njema ya taifa letu,"amesema .

Ameongeza taasisi ya Taswira ya Vijana Tanzania ipo tayari kupambana kwa hali yoyote na watu hawa wanaotaka kuchafua amani ya nchi na kwamba wapo tayari kuunga mkono juhudi za Rais Dk. John Magufuli kwa maendeleo ya taifa.

Umoja Wa Rudisha Uzalendo (RUTA) Waandaa Maandamano ya Kupongeza Juhudi Za Rais Magufuli

$
0
0
WAKAZI wa Jiji la Dar es Salaam  kupitia Umoja wa Rudisha uzalendo Tanzania (RUTA) umepongeza juhudi za Rais Dk.John Magufuli na watendaji kazi wake katika kusukuma gurudumu la maendeleo nchini huku wakitangaza kufanya maandamano ya amani Aprili 12 mwaka huu.

Hayo yameelezwa jana  na Mratibu wa umoja huo Charles Masele  jijini Dar es Salaam ambapo alisema  kuwa wananchi wengi wamevutiwa na wanaunga mkono juhudi za Rais Magufuli, hivyo katika kumpongeza wameandaa maandamano ya amani yatayohusisha watu wa itikadi zote yatakayofanyika Aprili 12 mwaka huu kuanzia Karume hadi viwanja vya Mnazi mmoja kuanzia saa moja hadi saa tano asubuhi .

Wakizungumza zaidi  wadau hao walisema hawana budi kuunga mkono juhudi za Rais kwani huduma nyingi zimeboreshwa zikiwemo miundombinu, afya hasa kwa akina mama na elimu ambayo hutolewa bure, pia mikopo ya elimu ya juu ambayo hutolewa kwa wanafunzi wa hali ya chini.

Aidha wameeleza utiifu wa Rais na watendaji wake wa serikali na taasisi binafsi kwa namna wanavyothamini na kuhudumu kwa haki na usawa hivyo wameona ni vyema kumuunga mkono na kumuombea.

Pia umoja huo umewataka vijana na watu wa kada mbalimbali kuunga mkono juhudi hizo kwani zinafanywa kwa maendeleo ya kizazi cha sasa na baadaye.

Mimi Mars: Sitaki Kuolewa na Mwanaume Mpare

$
0
0
Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘Papara’ Mimi Mars ambaye pia ni mdogo wa staa wa Bongo fleva Vanessa Mdee, amefunguka na kuweka wazi kuwa hataki Kuolewa na mwanaume kabila la Wapare.

Mimi Mars amesema kuwa hategemei na wala hataki kuolewa na mwanaume kutoka katika kabila la wapare kwa sababu yeye mwenyewe ni mpare na kuna baadhi ya tabia za wapare anazijua na hazimpendezi.

Kwenye mahojiano na Enews ya East Africa Tv, Mimi Mars pia ametaja Makabila mengine kama wachaga ambayo nayo amekiri hatorudia Tena kuwa nao:

"Kutokana na mimi mwenye kuwa ni Mpare kwa hiyo tabia za wanaume wa kipare ninazifahamu vizuri halafu wanasema mafahari wawili hawezi kukaa zizi moja, hivyo najua tutashindwana tu kwasababu wote tunajisikia, wabahili 'so' tukikaa wawili 'type' hiyo mambo yatakuwa magumu", amesema Mimi Mars.

Pamoja na hayo, Mimi ameendelea kwa kusema; "inanibidi nitafute kabila ambalo tofauti na mimi ndio maana sitoweza kuwa kabila hilo ila sio kwa ubaya ila mimi mwenyewe tu nimesema sitoweza.

Lakini pia Mimi Mars ameweka wazi kuwa kwa sasa hana mpenzi  na yupo single:

Mwigulu Awaponza Wanafunzi Sita Udsm, Walimwa Barua Ya Onyo

$
0
0
Wanafunzi sita wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), wamelimwa barua za onyo kwa kuhamasisha maandamano kinyume cha sheria.

Wanafunzi hao wanadaiwa kuhamasisha maandamano kutaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ajiuzulu kutokana na kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Aquilina Akwilini, aliyeuawa kwa risasi Februari mwaka huu.

Katika barua yake ambayo imesainiwa na Makamu Mkuu wa Chuo (Taaluma), Profesa David Mfinanga, kwenda kwa wanafunzi hao ambao wamekataa majina yao yasitajwe, imesema onyo hilo ni la mwisho na endapo wataendelea kujihusisha na vitendo hivyo watasimamishwa masomo mara moja kulingana na kipengele 14(xi) wakati mashtaka dhidi yake yakiandaliwa na kushughulikiwa.

“Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, umepata taarifa kuwa wewe ni miongoni mwa wanafunzi wanaojihusisha na vitendo kinyume cha sheria ndogo ndogo za wanafunzi wa Chuo Kikuu ya mwaka 2011, hususan makosa yaliyoainishwa kwenye vipengele 4.2(vxiii), 4.2(xix) na 4.2(xxvi).

“Vitendo hivyo visivyokubalika ni pamoja na kupanga na kuhamasisha maandamano kinyume cha sheria, kujihusisha na vitendo vinavyokishushia hadhi chuo kwa kuanzisha kikundi/vikundi visivyoruhusiwa dhidi ya wanafunzi wenzako, serikali na viongozi wa nchi.

“Kwa barua hii unatakiwa kuacha mara moja vitendo hivi na endapo utakaidi utakuwa umejiongezea makosa mengine kama yalivyoainishwa kwenye sheria ndogo ndogo za wanafunzi wa chuo vipengele vilivyotajwa,” imesema sehemu ya barua hiyo.

Barua hiyo pia imetumwa nakala kwa Makamu Mkuu wa Chuo, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo (Taaluma), Naibu Makamu Mkuu wa Chuo (Utafiti), Mwanasheria Mkuu wa Chuo na Kaimu wa Baraza na Mkurugenzi wa Shahada za Awali kwa kumbukumbu.

Akizungumzia barua hiyo, mmoja wa wanafunzi waliopewa barua hiyo amesema barua hizo wamechukua polisi Kituo cha Chuo Kikuu, baada ya kupigiwa simu Machi 14, wakitakiwa kuchukua barua hizo lakini hawakuweza kwa sababu walikuwa wamefunga chuo.

“Kwanza hatukujua wameandika nini, tulipigiwa simu na polisi wa kituo kicho kwamba tukachukue barua zetu tulipoenda tukapewa hizo,” amesema mwanafunzi huyo.

Aidha, amesema barua hizo zimekosewa kwa sababu wao hawakuhamasisha maandamano lakini pia sheria hizo ndogo ndogo zinatoa adhabu kama hiyo kwa mwanafunzi aliyetenda kosa ndani ya chuo.

“Wamekosea hawajataja tulihamasisha maandamano hayo wapi, sisi hatujawahi kufanya maandamano ndani ya chuo sheria hizo zinasema endapo mwanafunzi atatenda kosa ndani ya chuo, hazizui kufanya mwanafunzi kufanya maandamano kitendo cha kusema sisi tulifanya maandamano si kweli.

“Sisi tulifanya mkutano na waandishi wa habari tukasema Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ajipime. Kwa kifupi tumeshachukua hadi kufikia Machi 20, wote tulikuwa tumeshachukua barua zetu na tumejipanga kuzijibu,” amesema.

Hata hivyo, mwanafunzi huyo amesema kuna uwezekani Mwenyekiti wa Mtandai wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo naye yake ilikuwapo isipokuwa imeondolewa baada ya kusimamishwa masomo kutokana na kesi ya kutoa taarifa za uongo kwenye mitandao ya kijamii na kudanganya kutekwa inayomkabili.

Mahakama yatishia kuwafunga IGP, Waziri Mambo ya Ndani

$
0
0
Mahakama Kuu nchini Kenya imewataka Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Waziri wa Mambo ya Ndani na Kamishna wa Uhamiaji kufika mahakamani leo kujitetea kwanini wasifungwe jela au kulipa faini kwa kuidharau Mahakama.

Jaji wa Mahakama Kuu, George Odunga alisema kuwa maafisa hao wakuu Serikalini walifanya kosa la kuidharau mahakama kwa kukataa wito wa kumfikisha mahakamani hapo mwanasheria Miguna Miguna, Jumatano wiki hii.

Jaji huyo amesema kuwa Mahakama haiwezi kuchezewa na Serikali na haitaruhusu hilo lifanyike kwani ndicho chombo cha haki.

Miguna alishikiliwa na Polisi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta alipojaribu kurejea nchini humo akitokea nchini Canada alikopelekwa kwa nguvu kwa madai ya kutokuwa raia wa Kenya.

Serikali inadai Miguna aliyekuwa anatuhumiwa kwa uhalifu wa kushiriki zoezi la kumuapisha Raila Odinga kama ‘Rais wa Watu’, alipinga uraia wake mwaka 1988, madai ambayo mwanasheria huyo ameyapinga. Miguna anadai ni raia wa kuzaliwa wa Kenya mwenye uraia pia wa Canada lakini hajawahi kuukana uraia wa nchi hiyo kama inavyodaiwa.

Hata hivyo, mbali na tishio hilo la Mahakama kwa viongozi hao wa vyombo vya usalama, jana usiku Miguna alisafirishwa bila hiari yake hadi Dubai.

Mahakama imewahi kuamuru Muguna aachiwe huru na kama kuna madai yoyote anapaswa kufikishwa mahakamani na sio vinginevyo.

Download Upya Application Yetu Ya mpekuzi .....Ile Ya Zamani Tutaifuta

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya Mpekuzi Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Maboresho Mapya Yamefanyika ili kukufanya upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile Magazeti kuliko ilivyo sasa.

App ya zamani ilikuwa na tatizo kubwa la kuchelewa kufunguka, kuchelewesha habari na muonekano wake haukuwa wa kiwango kinachostahili.

Chakufanya, Ingia PlayStore, Download Upya Application yetu  MPYA. Ukishaipakua hii Mpya, ya zamani ifute tu.

NB: App mpya ina Icon ya Njano

Tumekurahisishia; 

Mwanamke Aliyemwaga Machozi Mbele ya Rais Magufuli Afungwa Jela Miezi Mitatu

$
0
0
Mahakama ya Mwanzo Usambara mkoani Tanga imemhukumu kwenda jela miezi mitatu Swabaha Shosi ambae alishawahi kushika headlines kwa kulia mbele ya Rais Magufuli wakati wa maadhimisho ya siku ya sheria February 2, 2017.

Hakimu wa Mahakama hiyo Khadija Kitogo amemtia hatiani kwa kuingia eneo lisiloruhusiwa kisheria.

Swahaba alifikishwa Mahakamani hapo August 9, 2017 akikabiliwa na shtaka la kuingia Chongoleani ambako hakuruhusiwi Raia kuingia.

Mahakama ilielezwa kuwa aliingia katika eneo lililokuwa limetengwa kwa ajili ya ujio Rais Magufuli na Yoweri Museveni walipokwenda kuzindua mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda mpaka Hoima.

Swahaba alikana mashtaka hayo na kujitetea kuwa alikanyaga eneo wakati akiandaa eneo kwa ajili ya kuwauzia chakula waliodhuria uzinduzi huo na kwamba hakuwa peke yake walikuwa wengi.

Hakimu Kitogo akitoa hukumu hiyo amesema baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mahakama imemkuta na hatia ya kuvunja sheria ya Makosa ya jinai.

“Ninampa adhabu ya kwenda jela miezi mitatu ili iwe fundisho kwa wengine wanaovunja sheria kwa kuingia maeneo yasiyoruhusiwa”

China yasema Korea Kaskazini Imekubali kuondoa silaha za nyuklia

$
0
0
China imesema kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amethibitisha katika ziara yake ya siri huko Beijing kuwa yuko tayari kuondosha silaha za nyuklia katika rasi ya Korea na kushiriki katika mazungumzo yatakayo zishirikisha Korea Kusini na Marekani.

Shirika la habari la China Xinhua, lililoweka picha za kiongozi wa Korea Kaskazini akiwa na Rais wa China Xi Jinping, limeripoti kuwa Kim na mkewe Ri Sol Ju walifanya ziara ya kiserikali Beijing kuanzia Jumapili hadi Jumatano, na alihudhuria karamu maalum katika ukumbi wa Great Hall of the People akiwa na Xi na mkewe Peng Liyuan.

Wakati wa mkutano wao viongozi hao wawili walisisitiza umuhimu wa kuendeleza umoja wa karibu kati ya China-Korea Kaskazini ambao ulikuwa umeingiliwa na mvutano juu ya Pyongyang kukaidi na kuendeleza jaribio la silaha za nyuklia na makombora ya balistika.

Xi alikuwa amewafiki vikwazo vizito vilivyokuwa vimewekwa chini ya usimamizi wa Marekani ili kumshinikiza Kim kurejea tena katika mazungumzo na kuacha kutumia vitisho vya programu yake ya nyuklia ikiwa ni suluhisho la kumaliza vikwazo vya kiuchumi, kuongeza misaada na kuwahakikishia usalama wao.

Katika miezi michache iliyopita, Kim alibadilisha msimamo wake wa kukataa mazungumzo alipotangaza Korea Kaskazini ni taifa lenye silaha za nyuklia.

Baadae alibadilisha msimamo huo na kupunguza mvutano kwa kusimamisha majaribio ya nyuklia na makombora, kuiacha nchi yake kushiriki katika michezo ya Olympic huko Korea Kusini na kuwa tayari kufanya mazungumzo ya suala la nyuklia pamoja na Rais wa Korea Kusini Moon-Jae-in ambao umepangwa kufanyika April, na mkutano mwengine na Rais wa Marekani Donald Trump unaotarajiwa kufanyika May 2018.

Kim amemwambia Xi kuwa yuko tayari kutafuta ufumbuzi wa “suala al kuondoa nyuklia” muda wa kuwa Korea Kusini na Marekani “watakuwa tayari kushiriki katika juhudi hizi kwa nia njema, kuweka mazingira ya amani na utulivu, wakati akichukua hatua za kusukuma mbele mazungumzo hayo na kufikia muwafaka ili kufikia amani,” kwa mujibu wa Xinhua.

Mbowe na Viongozi Wengine wa CHADEMA Wafikishwa Tena Mahakamani

$
0
0
Viongozi sita wa Chadema wamefikishwa leo saa 2 asubuhi katika Mahakama ya Kisutu kwa ajili ya kusikiliza uamuzi wa dhamana yao, huku ulinzi ukiimarishwa katika eneo hilo.

Kesi hiyo inatajwa leo Machi 29, ambapo Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard, Mashauri atatoa uamuzi kama washtakiwa hao watapata dhamana au hawatapata.

Wakati viongozi hao wakifikishwa mahakamani, Jeshi la Polisi limeimarisha ulinzi kuzunguka viunga vya mahakama ya Kisutu.

Katika lango kuu la kuingia mahakamani hapo, polisi waliovalia kiraia walifanya ukaguzi kwa kila anayeingia na kutoka na kuwazuia baadhi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images