Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Majambazi Yafunga Barabara na Kuteka Magari Pwani...Mawili Yatiwa Mbaroni

$
0
0
JESHI la polisi mkoani Pwani, linawashikilia watu wawili wanaodaiwa kuwa ni majambazi kati ya kundi la majambazi zaidi ya sita ambao waliteka magari na kupora mali mbalimbali za watu eneo la Kwang’andu ,Mbwewe barabara ya kuelekea Wami.

Kamanda wa polisi mkoani Pwani,(ACP) Jonathan Shanna alisema tukio hilo limetokea machi 24 saa 8.30 mchana .


Akizungumzia tukio hilo la unyanga’anyi wa kutumia silaha ,alieleza majambazi zaidi ya sita waliteka magari kwa kukata mti kwa msumeno kisha kuziba barabara na kuvamia magari mbalimbali ya wananchi kisha kuwapora mali zao na kuharibu baadhi ya magari yao.

Aidha kamanda Shanna alisema, watuhumiwa wawili wapo mbaroni kupisha uchunguzi.Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Saidi Salim (26) na Nyangwesa Nyangwesa.


Kamanda Shanna aliwataja na wananchi /wasafiri walioharibiwa na kuporwa mali zao akiwemo Peter Kilango, ambae aliporwa simu aina ya techno C9 na gari lake kuharibiwa kioo cha mbele upande wa dereva.

Viatus Bahati aliporwa Lap Top Dell, Usd 900.00 , shilingi 700,000 na pochi yenye document mbalimbali na Imail Meshileki alieporwa simu aina ya Tecno ,na sh .800,000 na gari lake  T.953 BXN Toyota Prado ambayo waliiharibu kioo cha nyuma.

Kamanda Shanna alimtaja mwingine ni Jackson Omary aliyeporwa Tsh.70,000 na begi lenye nguo mbalimbali na Denis Mwavano aliporwa simu Tecno C9.

Jeshi la polisi mkoani humo limekemea vitendo vya kiuhalifu na kuteka magari kwani kwa kufanya hivyo watakula nao sahani moja ,na wale waliofanikiwa kukimbia wataendelea kusakwa

Watu 17 Watambuliwa Kati Ya 26 Waliofariki Katika Ajali Mkuranga

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi,Mkuranga
WATU 17 kati ya 26 waliofariki dunia katika ajali ya barabarani iliyotokea Mkuranga Mkoani Pwani ,wametambuliwa majina yao ambapo hatua inayoendelea ni kuwakabidhi kwa ndugu zao kwa ajili ya mazishi.
 
Aidha watu wengine kumi wamejeruhiwa na wamekimbizwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu.
 
Ajali hiyo imehusisha  gari  ndogo ya abiria aina ya Toyota Hiace yenye namba za usajili T.676 DGK inayofanya safari zake Kimanzichana – Mbagala Rangi na gari nyingine aina ya Lori.
 
Mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Mkuranga, Stephen Mwandambo alisema amepokea maiti 25 na majeruhi hao ambapo majeruhi mmoja alifariki njiani wakati wakipelekwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
 
Mganga mkuu huyo aliwataja waliofariki na kutambuliwa majina yao ni 17 kati ya 26 waliofariki kuwa ni pamoja na  Selemani Guli (36) mkazi wa Kongowe,Modesta Sheleli (24 ) mkazi wa Vianzi,Doreen Selemani Seleli (5), sheila Hamad Mkuba ( 8 )mkazi wa Vianzi na Mariam Hussein Sadik (15 )mkazi wa Mwarusembe.
 
“Nassoro Hamis( 48) mkazi wa Jaribu Mpaka, Asha Athumani (24)mkazi wa Songosongo ,Nasma Athuman 22 Songosongo Mwanahawa Athuman (52),Mohammed Saidi (25) mkazi wa Njopeka na Mwajabu Jongo (20)mkazi wa Njopeka”;
 
Dokta Mwandambo aliwataja wengine ni Mwarami Mbunju(37) mkazi wa Mkamba na Abisaalom Uloga (25)mkazi wa Kimanzichana ,Kijongo Kibwana Jongo(26 )anakaa Jaribu Mpakani na Recho Japhet (16),Mariam Selemani (36)mkazi wa Mbagala  na Melania Kapatwa (38)mkazi wa Jaribu Mpakani. 
 
Inasemekana majeruhi waliopelekwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili wengine wamekatika viongo mbalimbali vya mwili.
 
Aidha dokta Mwandambo alisema wanakabiliwa na changamoto ya kipimo cha X-ray hali inayosababisha kushindwa kuwafanyia uchunguzi majeruhi .
 
Changamoto nyingine inayowakabili ni chumba cha kuhifadhia maiti kuwa kidogo kwani kina uwezo wa kuhifadhi maiti sita hivyo maiti 26 zipo nje ya uwezo wao.
 
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia machi 25 mwaka huu katika eneo la Kitonga kata ya Mwalusembe wilaya ya humo.
Chanzo cha ajali inadaiwa mwendo kasi wa dereva wa lori katika kilima na kusababisha ajali hiyo mbaya.
 
Simanzi zimetawala katika wilaya hiyo ,ambapo mbunge wa jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega ,aliishukuru serikali ya wilaya chini ya mkuu wa wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga kwa juhudi zake za kusaidia majeruhi na marehemu kupelekwa hospitalini .
 
Ulega alitoa pole kwa wafiwa na majeruhi na kuwaasa madereva waache kuendesha kwa mwendo kasi kwani husababisha ajali zembe.
 
“Naishukuru pia hospitali ya wilaya kwa juhudi zao baada ya kupokea marehemu na majeruhi kuhangaikia kuokoa maisha yao.” alieleza Ulega.

Breaking News: Mwenyekiti UVCCM Taifa Atengua Uteuzi wa Jokate Mwegelo

$
0
0
Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM), imetengua uteuzi wa nafasi ya Kaimu Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa Umoja huo iliyokuwa ikiongozwa na  Jokate Mwegelo .

Jokate aliteuliwa Aprili mwaka jana na Kamati hiyo kukaimu kwa muda kabla ya kamati hiyo kufanya uchaguzi.

Kaimu Katibu Mkuu Taifa wa Umoja Shaka Hamdu amekiri Jokate  kutenguliwa kwa nafasi hiyo leo Machi 25,  2018 kupitia vikao vya Kamati vilivyokutana kwa mujibu wa kanuni na taratibu za UVCCM.

“Kwanza ifahamike Jokate aliteuliwa kukaimu kwa utaratibu wa UVCCM  na ameondolewa kwa utaratibu, ni kama alikuwa kwenye majaribio,” amesema Shaka.

Shaka amesema utaratibu wa kujaza nafasi hiyo utafanyika hapo baadaye kupitia vikao vya umoja huo.

Uteuzi wa Jokate kuwa Kaimu Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipkizi, ulionekana kutaka kuivuruga jumuiya hiyo baada ya kuibuka mjadala kwa viongozi na wanachama wakidai uteuzi huo haukufuata kanuni na taratibu za umoja huo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya March 26

Tazama Video Mpya ya Linex - I'M SORRY

$
0
0
Tazama Video Mpya ya Linex - I'M SORRY

==>Ipakue hapo chini

Audio: Nay Wa Mitego (Mr Nay) – Amsha Popo

$
0
0
Audio: Nay Wa Mitego (Mr Nay) – Amsha Popo

Wanafunzi Vyuo Vikuu Watajwa Kuongoza kwa Matusi Mitandaoni

$
0
0
Serikali imesema wanafunzi wa vyuo vikuu wanaongoza  kutukana na kutumia lugha zisizo na maadili kwenye mitandao ya kijamii.

Angalizo hilo limetolewa na naibu waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha  Jumamosi Machi 24, 2018 katika hafla fupi ya uzinduzi wa Unilife Compus iliyopo Mkoa wa Kilimanjaro uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Mwenge na kuvikutanisha vyuo vikuu vyote vya mkoa huo.

Alisema  yapo mambo matatu ambayo yanachangia wanafunzi kutofanya vizuri, yakiwamo matumizi mabaya ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), anasa na starehe zilizopitiliza na kujiingiza kwenye siasa ambazo zinawanyima fursa ya kusoma vizuri.

“Serikali imebaini mambo yanayochangia kufifisha na kudidimiza jitihada za elimu tunayoitoa kuonekana bure. Kuna vitu ambavyo siyo vizuri  vinaendelea katika vyuo vyetu, ndizo changamoto tunatakiwa kukabiliana nazo. Chuoni unaweza kutengeneza au kuharibu maisha yako,” alisema.

Naye mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira alisema  wanafunzi wengi hawataki kujifunza  kwa kutumia muda vizuri kwa kusoma vitabu.

"Tunabaki kuwa waigaji wa dhana za wenzetu wa magharibi, hatutaki kujifunza vitu vipya bali vilevile vya wenzetu vinatumika hadi leo. Wasomi wa Tanzania tunajishusha kwa sababu ya kushindwa kuleta mawazo mapya kwenye sekta ya elimu na afya," alisema  Mghwira.

Askofu Shoo Asema Kanisa Halitakubali Kuzibwa Mdomo......Aeleza Maaskofu KKKT Walivyofunga Kabla ya Kutoa Waraka Huo

$
0
0
Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Fredrick Shoo ameonya kwamba asitokee kiongozi yeyote nchini wa kisiasa au serikali ambaye atajaribu kuwazuia na kuwaziba midomo viongozi wa dini kutekeleza wajibu wao wa kukemea na kuonya juu ya maovu yanayoendelea hapa nchini.

Dk. Shoo ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, pia amesema kamwe kanisa halitanyamaza kimya kwa wanasiasa wenye tabia ya kutumia nafasi zao kuligawa taifa vipande vipande.

Alizungumza hayo  jana kwenye ibada maalumu ya kusataafu kwa aliyekuwa Mchungaji wa Usharika wa Masama Kati, John Mshau wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro.

“Wajibu wa viongozi wa dini ni kuonya na kukemea yale mabaya yanayoendelea nchini na si vinginevyo na kwamba  asijaribu kutokea mtu yeyote kuwazuia viongozi wa dini kufanya wajibu huo kwani ni sawa na kupingana na Mungu.

“Wajibu wetu ni kuonya, kushauri, kukemea na tunatenda hivyo, asijaribu kuja mtu yeyote kutuzuia kufanya hivyo kwani neno la Mungu linasema bwana hutegemeza wenye upole na huangusha chini wenye hila, hivyo sisi kama viongozi wa dini hatutakubali kunyamaza tutasema na kukemea maovu,” amesema

Pamoja na mambo mengine, Dk. Shoo aliwaonya viongozi wote wa kisiasa nchini kuacha kutumia vyama vyao kuligawa taifa na kwamba suala hilo halitaweza kuvumiliwa na viongozi wa dini na wataendelea kusema na kuonya.

Akitolea ufafanuzi waraka ulioandaliwa na Baraza la Maaskofu 27 wa KKKT, Machi 15 Jijini Arusha alisema walifunga na kuomba Mungu kwa lengo la kupata ujumbe sahihi ili wautoe kwa waumini wa kanisa hilo na Taifa kwa ujumla na kwamba hawakukurupuka kutoa ujumbe huo.

Seriikali Yaweka Mikakati ya Kukabiliana na Maambukizi Mapya ya Virusi Vya Ukimwi

$
0
0
Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma
Serikali imesema itaendeleza mapambano ya Vita dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi kwa kuongeza kasi katika kuzuia maambukizi  mapya ikiwemo kutoa elimu kwa umma.

Akizungumza jana mjini Dodoma wakati wa warsha kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge inayoshugulikia Ukimwi na Madawa yakulevya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu mhe. Jenista Mhagama alisema kuwa dhamira ya Serikali baada ya kuanzisha mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi (ATF) ni kuhakikisha kuwa mfuko huo unajengewa uwezo ili lengo la kuanzishwa kwake litimie.

“Tayari mfuko umeweza kukusanya bilioni 279 katika kipindi kilichopita na mwaka huu bilioni 3 zimetengwa katika Bajeti na zitaingizwa katika mfuko huu ili uweze kutimiza majukumu yake kwa ufanishi na tumekuwa tukiwashirikisha wadau katika kuchangia na wamekuwa wakituunga mkono na tunaendelea kuwaomba wajitokeze zaidi  kuchangia mfuko huu ” Alisisitiza Mhagama.

Akifafanua Mhe. Mhagama alisema kuwa tayari mapendekezo kuhusu kuwepo kwa tozo maalum katika kodi yameshawasilishwa katika kamati husika kwa hatua zaidi dhamira ikiwa ni kuujengea mfuko huo uwezo wa kuwa na fedha za kutosha katika kufanikisha vita dhidi ya Ukimwi hapa nchini.

Mkakati mwingine ni ujenzi wa kituo maalum katika eneo la Mererani  Mkoani Manyara kitakachosaidia katika mapambano dhidi ya Ukimwi kwa kuwa eneo hilo ni moja ya maeneo yenye mwingiliano mkubwa wa watu kutokana na shughuli za uchimbaji madini.

Hatua nyingine ni kufanya kazi kwa kushirikiana kati ya TACAIDS  na Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya ili kuwafikia waathirika wa dawa za kulevya ambao ni moja ya makundi yanayoathika na ugonjwa wa ukimwi kwa mujibu wa tafiti mbalimbali.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.  Osca Mukasa (Mb) alisema kuwa kutengwa kwa fedha katika bajeti ya 2018/19 zitakazopelekwa katika mfuko wa kudhibi Ukimwi ni ishara nzuri kuwa serikali imeweka mkazo katika mapambano dhidi ya janga hilo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS Dkt. Leonard  Maboko alisema Tume hiyo iko katika hatua za mwisho za kukamilisha mkakati wa Nne unaolenga kuongeza  nguvu ili kufikiwa kwa malengo ya mkakati huo.

Akifafanua Dkt. Maboko alisema kuwa Tume hiyo imeandaa kampeni maalum kuhamasisha wananchi kupima ili kujijua kama wameambikizwa virusi vya ukimwi au laa hali itakayowasaidia kuchukua hatua stahiki na kwa wakati hivyo kuzuia maambukizi mapya hasa kwa vijana.

“Hapa nchini kwa mwaka kuna maambukizi mapya elfu 81,000 hivyo ni vyema tukaungana katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu kwa kuwa uwezo wa kuzuia maambuki mapya tunao”. Alisisitiza Dkt. Maboko.

Warsha kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ukimwi na Madawa ya Kulevya imefanyika mjini Dodoma leo  ikiwashirikisha wajumbe wote wa kamati hiyo, Aidha mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi (ATF) unalenga kuongeza rasilimali fedha kutoka asilimia 7 (2015) hadi asilimia 30  (2018).

Brela yatoa miezi sita kampuni kuhakiki taarifa mtandaoni

$
0
0

 Ili kuhakikisha huduma zote zinatolewa kidigitali, Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) umetoa miezi sita kwa wamiliki wa kampuni kuhakiki taarifa zao kwenye mfumo mpya kwa njia ya mtandao, vinginevyo hawatapata huduma wanazostahili.

Agizo hilo linazihusu kampuni 200,000 zilizosajiliwa kabla ya Februari mosi mwaka huu baada ya mfumo huo kuanza kutumika Januari 4.

Ofisa mtendaji mkuu wa Brela, Frank Kanyusi alisema mpaka sasa ni kampuni 200 pekee zimesajiliwa kwenye mfumo huo na kufafanua kuwa, hakuna kampuni itaweza kufanya lolote kwani mifumo yote ya Serikali inaangalia ripoti ya Brela kabla ya kumhudumia mteja.

“Kama hujahakiki taarifa na kuingia kwenye mfumo wa mtandao, hakuna chochote unachoweza kufanya kwa kuwa hata mamlaka nyingine kama (Mamlaka ya Mapato Tanzania) TRA lazima zije kwetu kujiridhisha kuhusu kampuni fulani. Hivyo, iwapo haijasajiliwa haitapata huduma,” alisema.

Kwenye mfumo huo, mmiliki wa kampuni anaweza kufanya mabadiliko yoyote kwa njia ya mtandao, hivyo kupunguza gharama ya kusafiri kutoka mikoani mpaka Dar es Salaam zilipo ofisi za wakala huo.

“Sasa hivi chochote kinafanyika mtandaoni, tukijiridhisha tunaingiza kwenye nyaraka zetu kama hatujaridhika tunawasiliana na mhusika,” alisema Kanyusi.

Alisema kinachotakiwa kampuni kujisajili kwenye mfumo huo ni namba ya ulipajikodi, namba ya mlipakodi ya kila mkurugenzi, vitambulisho vya uraia vya wakurugenzi na wenye hisa ndani ya kampuni.

Tangu mfumo huo uanze kufanya kazi, Kanyusi alisema umerahisisha utoaji huduma. “Tumeshaanza kupata mrejesho kutoka kwa mawakala wa alama za biashara, wanasema umewaondolea usumbufu na umewarahisishia utendaji wao tofauti na ilivyokuwa awali wakati kazi zilipokuwa zikifanyika kwenye karatasi,” alisema.

Muda wowote kuanzia sasa, Brela inatarajia kuzindua utoaji leseni daraja A na B kwa njia ya mtandao, huku ikiwa imejiwekea malengo ya kusajili zaidi ya kampuni 50 kwa siku kupitia mfumo huo.

Kanyusi alisema Brela ndiyo mlango wa kurasimisha biashara hivyo inaweka mazingira rahisi ya kuanzisha biashara na kuvutia wawekezaji.

“Tunafahamu zitakuwapo changamoto za hapa na pale kwenye mfumo huu mpya ila ninaamini tutafika, wenye kampuni wazivumilie watakazokumbana nazo ila wasajili kampuni zao,” alisema.

Mfumo huo unaotumiwa na Brela unaziunganisha mtandaoni taasisi muhimu za Serikali zinazohusika na usimamizi wa biashara, ili kuokoa muda kwa wahusika kuzifuata kwenye ofisi zilizopo maeneo tofauti.

Kanyusi alisema faida nyingine za mfumo huo ni kupunguza gharama na muda wa kusajili na kuanzisha biashara nchini. Kabla ya kuanza kuutumia mfumo huo, Brela ilienda kujifunza kwenye mataifa mbalimbali kuhusu ufanisi wake ikiwamo Vietnam unakotumika kwa miaka mingi.

Mwasisi wa CHADEMA Mzee Victor Kimesela afariki dunia

$
0
0
Victor Kimesera, mmoja wa waasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa anapatiwa matibabu. 
 
Uongozi wa juu wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini umesema umepokea kwa mshituko taarifa ya msiba huo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, Kimesera alifariki dunia usiku wa kuamkia juzi.

“Chadema tumepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za msiba huu. Tumeondokewa na moja ya nguzo muhimu za ustawi wa chama chetu ambaye amekuwa katikati ya mapambano tangu aliposhiriki kuasisi chama hiki hadi umauti ulipomkuta akiwa mtendaji wa chama makao makuu,” Mbowe alisema katika taarifa hiyo.

“Kimesera maarufu kama VPK kama tulivyozoea kumuita, ametutoka katika kipindi ambacho mchango wake ungehitajika sana, hasa wakati huu ambapo taifa letu linapita katika mkwamo mkubwa wa kisiasa.

Atakumbukwa zaidi kwa namna alivyojitolea kwa hali na mali kupigania haki, demokrasia na maendeleo nchini na kipekee katika Jimbo la Kiteto mkoani Manyara.”

Katika taarifa yake hiyo, Mbowe alisema kwa sasa chama kupitia ofisi ya Katibu Mkuu kinashirikiana na familia ya marehemu kuhusu taratibu mbalimbali za msiba huo na ratiba ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam zitatolewa baadaye. 

Boko Haram wawaonya wasichana waliowaachia kutorudi shule

$
0
0
Kundi la kigaidi la Boko Haram limewaonya wasichana zaidi ya 100 lilowateka na kuwaachia hivi karibuni kuhakikisha hawarejei tena shuleni kuendelea na masomo.

Kundi hilo ambalo moja kati ya itikadi zake ni kupinga elimu yenye mfanano na ile ya magharibi, liliwateka wasichana hao Februari 19 katika shule ya bweni eneo la Dapchi nchini Nigeria.

Jumla ya wasichana 110 walitekwa na kundi hilo, watano walifariki walipojaribu kutoroka na mmoja ameendelea kushikiliwa kutokana na msimamo wake wa kutobadili dini.

Wasichana waliorejeshwa kutokana na makubaliano kati ya kundi hilo na Serikali ya Nigeria wamewekwa chini ya uangalizi maalum wakifanyiwa uchunguzi wa afya zao.

ATCL Yasitisha Safari za Songea- Dar es Salaam

$
0
0
Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) itasitisha safari kati ya Dar es Salaam na Songea kuanzia Machi 31, mwaka huu, kutokana na ubovu wa njia ya kurukia ndege katika uwanja wa Songea.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Ladislaus Matindi, safari hizo zitarudishwa baada ya kukamilika kwa matengenezo makubwa ya uwanja huo yanayotarajiwa kuanza hivi karibuni.

“Kusitishwa kwa safari za Songea kutaathiri pia safari za Mtwara kwa kipindi kifupi kutokana na sababu za kibiashara wakati ATCL ikitathmini njia mbadala ya kuhudumia kituo hiki peke yake,” imesema taarifa.

Alisema ATCL inawaomba radhi wateja wake kwa usumbufu utakaojitokeza kutokana na uamuzi huo kwani usalama wa wateja ndio kipaumbele cha kampuni hiyo.

Mwadhama Kadinali Polycarp Pengo AMEUKANA Waraka wa Pasaka wa MAASKOFU wa Kanisa katoliki

$
0
0
Mwadhama Kadinali Polycap Pengo amesema hakuwa anajua kama kuna waraka utatolewa kuhusu kwaresma na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania huku akisema waraka huo una mazuri mengi japo umechanganya dini na siasa.

Kadinali Pengo ameyasema hayo wakati akiadhimisha ibada ya Jumapili ya matawi huko Bagamoyo katika tamasha la vijana.

"Katika wiki chache zilizopita watu wamekuja kwangu wakaniuliza unaionaje ile barua ya Maaskofu kuhusu Kwaresma mwaka huu? Ninazungumzia hilo na wala mtu asiende aka-quote kitu kingine ndio maana nataka kusema wazi kabisa:-

"Barua ile ijapokuwa hata jina langu mnaliona limeandikwa pale kwamba na mimi ni mmoja wa waandishi au watamkaji...mimi nimeipokea, baadhi yenu mmeshaipokea.

" Kwahiyo sioni namna gani mimi naweza kuwa mwandishi au mhubiri kwenu wa ile barua ambayo imetungwa labda na maaskofu...naamini na baadhi ya maaskofu lakini mimi mwenyewe hata nilikuwa sijaiona, hata nilikuwa sijaambiwa kuna kitu cha namna hiyo kinakuja.

"Tuelewane vizuri, ninaposema hivi sitaki kusema ile barua ni mbaya. Moja tu ni kwamba barua nzima imechanganya vitu viwili; Mwalimu angekuwepo angepiga kelele Maaskofu msichanganye Dini na Siasa. 

"Angepiga kelele sana kuhusu waraka huu katika nyakati zake. Na hilo nawambia sina hofu, muende mkamwambie mtu yeyote nimesema hivi. Ndio wala msione aibu, najua labda hata wengine mmekunja nyuso, kunjeni tu lakini huo ndio msimamo wangu.

"Zipo sehemu katika waraka huo zinazochanganya Dini na Siasa na si kazi ya maaskofu ni kazi yenu wanasiasa mkiwa ni wa CHADEMA, mkiwa ni wa CCM lakini haiwezi kuwa kazi yangu mimi. 

"Siwezi kwanza nikaanza kuchambua na ku-criticize Serikali katika mambo yaliyo yake; sikupewa mamlaka hayo. Na kwanini niwe padri mpaka nikubali kuwa Askofu na huku kumbe wito wangu ni siasa? 

"Itakuwa namsaliti hata yule aliyenipa wito huu. Tuchambue yale yanayohusu imani yetu katika ule waraka. Yale ambayo moja kwa moja yanahusu imani yetu Katoliki na tuyashike tuyazingatie kwa dhati kabisa.

"Lakini yale ya kuanza kusema Serikali ya awamu ya 5 inagandamiza uhuru inafanya nini...wewe Askofu uhuru wa kisiasa umeujua wapi? Umeujuaje? Na mambo ya ndani ya kisiasa huyajui na bado uje kutamka...nadhani tumeelewana.

"Yapo yaliyo mema mazuri kabisa katika waraka ule ingawaje sikujuia kama yameandikwa lakini siwezi kukataa yaliyo mema kwa sababu sikujua. 

"Yanaendelea kuwa mema mpaka kesho na keshokutwa. Lakini yale ambayo yanachanganya Dini na Siasa hayo siwezi kuyakubali. 

"Nyerere alifanya indoctrination kubwa mno kwa watu wa umri wetu. Mtu huwezi ukathubutu na ukalala salama usiku. Watu wa umri wangu ukichanganya dini na siasa utaota vitu vya ajabu utakosa usingizi(vicheko)

"Sasa ninyi vijana ninalotaka ni hili kwamba na ninyi mkichanganya dini na siasa muote vitu vibaya kama hivyo..muote vitu vibaya kabisa hata muone mnachungulia kaburi katika ndoto. 

"Sisi sio wanasiasa tunahitaji wanasisia mtuendelee wale tunaokuwa wito huo. Wale tunaotaka kuwa mama wakuu, mababa padri, maaskofu. Fuateni wito kulingana na misimamo yake ya kiimani."

Hatimaye Mahakama Yakubali Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo Apewe Dhamana

$
0
0
Hakimu mkazi mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, John Mpitanjia amesema dhamana ya Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo ipo wazi.

Nondo amefikishwa mahakamani  hapo leo  Jumatatu asubuhi Machi 26, 2018.

Mpitanjia amesema dhamana ipo wazi na Nondo anatakiwa kudhaminiwa na watu wawili ambao ni wakazi wa Iringa, mmoja awe mfanyakazi wa Serikali, na wanatakiwa waweke bondi ya shilingi milioni 5 pamoja na kuwa na mali isiyohamishika.

Kwa sasa wakili wa Nondo, Jebra Kambole anashughulikia dhamana ya mwanafunzi huyo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Nondo anatuhumiwa kwa makosa mawili. Kosa la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa Ubungo na kusambaza kwa kutumia mtandao wa WhatsApp kuwa yupo hatarini.

Shtaka la pili ni kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa umma mjini Mafinga alipokuwa akitoa taarifa katika kituo cha Polisi Mafinga kuwa alitekwa na watu wasiojulikana jijini Dar es Salaam na kupelekwa Kiwanda cha Pareto cha Mafinga.

Alifikishwa  mahakamani hapo saa tatu asubuhi akiwa kwenye gari la Polisi kisha kupelekwa katika mahabusu ndogo mahakamani hapo na kuingizwa katika chumba cha mahakama saa 3:45 asubuhi. Kesi imeahirishwa hadi Aprili 4, 2018.

Mara ya kwanza Nondo alipofikishwa mahakamani kuliibuka mkanganyiko kwa kisheria kuhusu dhamana baada ya upande wa mashtaka kuomba asipewe kwa maelezo kuwa bado maisha yake yapo hatarini.

Rais Magufuli Awataka Maaskofu Wahubiri Ujenzi wa Viwanda

$
0
0
Rais John Magufuli amewataka maaskofu badala ya kuhubiri mambo mengine, wahubiri kuhusu ujenzi wa viwanda vya dawa nchini ili Tanzania isinunue dawa nje ya nchi.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Machi 26, 2018 katika hafla fupi ya ugawaji wa magari 181 ya Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kwa ajili ya kusambaza dawa maeneo mbalimbali nchini inayofanyika eneo la Keko, jijini Dar es Salaam.

Amesema kununua dawa nje ya nchi kunasababisha nchi kupoteza Sh500bilioni.

“Asilimia 94 ya dawa zinanunuliwa nje ya nchi, ni asilimia sita tu ya dawa zinanunuliwa ndani,” amesema.

Amesema Rais Magufuli na kuwapongeza MSD kwa kufanya kazi nzuri na ya kizalendo.

Amesema kupatikana kwa magari hayo kumeifanya MSD kuwa na magari 213 kutoka magari 32 waliyokuwa nayo awali.

Atiwa Mbaroni Kwa Kuwabaka wanawake na Kuwapiga Picha za Uchi

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limemkamata mkazi wa mjini humo, Mabula Mabula maarufi Six kwa tuhuma za uporaji wa simu kwa kutumia pikipiki, kubaka na kuwapiga picha za utupu wanawake kisha kuzisambaza mitandaoni.

Akizungumza leo Jumatatu Machi 26, 2018, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ulrich Matei amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa baada ya makachero, kikosi cha kupambana na uhalifu  mitandaoni pamoja na kikosi cha kupambana na ujambazi, kumfuatilia kwa ukaribu.

Akihojiwa mara baada ya kukamatwa, Mabula ameeleza mbinu anazotumia ikiwa ni pamoja na kujifanya askari polisi, kuwakamata wanawake nyakati za usiku, kuwasingizia makosa mbalimbali na kuwapeleka maeneo yenye giza na kuwabaka.

Mtuhumiwa huyo ameyataja maeneo anayofanyia matendo hayo kuwa ni Msamvu Relini na kwamba amekuwa akitumia mapanga kuwatisha wanawake hao na kuwapiga picha za utupu na baadaye kutishia picha hizo kuzituma kwenye mitandao ya kijamii.

“Hizo picha huwa nawapiga kwa kutumia simu zao na anayekataa kunipa hela huwa naondoka na simu yake na kisha natuma hizo picha kwenye mitandao iliyopo kwenye simu hizo, baada ya hapo simu naiuza napata hela,” amesema mtuhumiwa huyo.

Katika  mahojiano na polisi, mtuhumiwa huyo amemtaja mwezake mmoja Ramadhani Salumu maarufu Miondoko mkazi wa Manispaa ya Morogoro kuwa ndio mnunuzi wa simu hizo za wizi.

Katika msako huo polisi wamefanikiwa kumkamata Salumu na kwamba wote watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.

Alichokisema Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Kuhusu Serikali Kuwafungia Wasanii

$
0
0
Ikiwa zimepita siku kadhaa tangu Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza kutangaza adhabu ya kumfungia kutoshiriki kazi za sanaa kwa kipindi cha miezi sita msanii Roma Mkatoliki pamoja na kufungia baadhi ya nyimbo za wasanii wengine, Leo March 26, 2018 Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Kheri James akiwa katika mkutano na wanachama mkoani Dodoma alionesha hisia zake za kutopendezwa na maamuzi hayo.

“Viongozi wanaoshughulika na masuala ya sanaa na utamaduni wasiifanye kazi hii kama kazi ya uhakimu bali waifanye kama kazi ya Ualimu kwa kuwafundisha watu namna ya kufanya”- amesema James na kuongeza;

“Serikali ya CCM imeahidi ajira kwa vijana, Vijana wameamua kujiajiri kwenye sanaa. Walimu wetu ni kuwawezesha kwenye sanaa na sio kuwakatisha tamaa kwahiyo tusitumie kigezo cha sheria na taratibu kuwaangamiza watu ambao tungeweza kuwaelimisha na wakafanya vizuri zaidi.
 
“Leo tuna wasanii ambao wameitangaza nchi yetu vizuri na wanalipa kodi kwa kazi zao sasa leo tunakwenye kupoteza mabalozi wazuri na walipakodi kwa makosa madogo ambayo yanaweza kurekebishwa na tukaendelea kufanya vizuri. Kama tutaaendelea kuwaacha vijana wakiangamizwa kwa kitu kinaitwa kanuni na taratibu za sheria basi hakuna kijana atakayebaki hapa”

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 63 na 64 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA-
ILIPOISHIA 

Nikafika katika hoteli ya Serena, walinzi wa getini walipo ona namba za gari langu hawakuhitaji kulikagua sana, nilicho kifanya ni kipita na kulisimamisha kwenye maegesho ya magari. Nikaacha bastola moja chini ya siti ya gari, nikajiweka vizuzri kofia yangu, hata sura yangu haikuonekana vizuri.
Nikashika kitasa cha mlango wa gari langu, kabla sijaufungua nikamuona K2 akitoka na mzee niliye mfwata wakaingia naye kwenye gari kisha wakaanza kuondoka jambo lililo nifanya nibaki nimeduwaa nisijue ninaanzia wapi kwa maana gari si chini ya nne zimeongozana na gari la K2 na zote zinatoka katika ofisi za N.S.S(Nation Securty Service)

ENDELEA  
Taratibu nikawasha gari langu na kuanza kuzifwatilia gari hizo huku nikiwa nimeziacha kwa umbali mrefu kidogo. Nikatoa simu mfukoni na kumpigia Babyanka ambaye alisha iingiza namba yake kwenye simu yangu.

“Ndio Dany?”
“Dili limeharibika”
“Kwa nini?”
“Kipindi ninafika tu, nimekuta K2 anatoka na mzee yule wa Kimarekani”
“Ohoo Gody sasa inakuwaje?”
“Hapo ndio ninaumiza kichwa kufikiria ninafanyaje kwa maana wana msafara wa gari kama nne hivi na zote zimetoka katika kitengo cha N.S.S.
“Mmmm kwa sasa wanaelekea maeneo ya wapi?”
“Maeneo ya Mwenge”
“Mwenge Mwenge…..”
“Hembu usikate simu nimpigie mama atushauri juu ya hili swala tufahamu ni nini cha kufanya”
“Sawa”
Nikaingiza namba ya mama kwa haraka kisha nikampigia, simu ya mama haikumaliza hata sekunde tano kuita ikapokelewa.
“Mama kuna tatizo”
“Tatizo gani?”
“Huyu mkuu wa watu wanao husika katika kuibinafsisha nchi yupo mkononi mwa K2 na hapa ninavyo zungumza nimeongozana nao na sifahamu wanampelekea wapi?”
“Upo eneo gani?”

“Tunaelekea Mwenge huku”
“Mwalimu”
“Kumbe Babyanka yupo”
“Ndio mwalimu, mimi nipo nyumbani ila unaonaje kama tukazi control trafick Light?”
“Wazo zuri, Dany munatokea upande gani?”
“Upande wa huku Morocco”
“Ok nafungulia gari zinazo toka Mlimani kuelekea Mbezi  Beach, nitawasimamisha hapo kwa dakika kum na tano, Dany hakikisha kwamba hii kazi unaifanya vizuri”
“Sawa mama”
“Dany mimi ninaelekea ofisini”
“Sawa”
Nikakata simu na nikaiweka pembeni, nikaanza kuyapita magri yaliyopo mbele yangu hadi gari za N.S.S. Lengo langu kubwa ni kuiwahi foleni na ninahitaji gari langu kuwa la kwanza. Kama nilivyo panga nivyo ilivyo kuwa. Nilipo fika tu kwenye foleni taa za kusimamisha magari upande wetu zikawaka na kufanya magairi yote kusimama.

TANGA RAHA- Sehemu ya Arobaini na Moja( 41 )

$
0
0
 AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Radi nyingi zikaanza kutawala kwenye anga huku mawingu mazito ya mvua yakikusanyika kwa kasi.Ndani ya dakika kadhaa mvua kubwa iliyoongozana na radi kali ikaanza kunyesha.Nikatafuta sehemu ya kujibanza pembezeni ya ukuta ili kuacha mvua ipite
Nikiwa nimeuegemea ukuta niskastukia nikikabwa shingo kwa nguvu na mkono ulio tokeza kwenye ukuta nilio uegeme huku mkono huo ukiwa na kucha ndevu za kutisha

ENDELEA
Cha kwanza kukiwahi ni kuishika shingo yangu kwa haraka na kuanza kuminyana na kiganja hiki kilicho ikamata shingo yangu,nikafanikiwa kujinasua kwenye kiganja,kitendo cha kugeuka nyuma nikakikuta kikimalizikia kuingia ndani ya ukuta.Nikataka kuondoka ila ujasiri mkubwa ukauvaa mwili wangu,nikarudi nyuma hatua chache na kuiangalia jinsi nyumba hii ilivyo kuanzia juu hadi chini.Ni nyumba inayoonekana kujengwa miaka mingi ya nguma,kwani hata kuta zake ni zile zilizo jengwa kipindi cha ukoloni.Nikiwa ninaendelea na uchunguzi wangu wa macho nikaanza kuzisikia sauti za watu wakingong’oneza ndani ya ukuta ambao nilikuwa nimeuegemea.

Kila ninapojaribu kuitafsiri hii lugha siipatii jibu kwa maana,kinacho zungumza hakieleweki ila watu hao wanazungumza kwani wanaonekana wanamambishano ya wao na wao.Nikazunguka upende wa pili wa nyumba na kukuta milango na madirisha vikiwa vimefunga,gafla taa zilizokuwa zinawaka nje zote zikazima gafla na kiza kinene kikatawala kila eneo,huku mvua iliyo andamana na radi zikiendelea kurindima kwa kasi ya ajabu.Nikaanza kuondoka taratibu,hatua chache kutoka nyumba ilipo nikasikia jina langu likitajwa ndani kwa sauti ya juu na kunifanya nigeuke nikiwa na mshangao mkubwa

Nikatamani kurudi nyuma ila nikaanza kuondoka,kila ninapopiga gatua moja mble ndioyo sauto ya mtu anaye liita jina langu huku akilia ikizidi kuongezeka.Nikayaziba masikio yangu na kwenda mbele zaidi ila nikajikuta saut inayo niita ikizidi kongezeka.Wasasiwasi mwingi ukaanza kunitawala,niakageuka na kuanza kurudi sehemu ilipo nyumba,hadi ni nafika mlango ukafunguka na wala sikumuona mtu aliye ufungua mlango zaidi ya giza nene lililo tawala ndani ya nyumba.

“Njoo”
Sauti ambayo ilikuwa ikiniita ikaanza kuniiomba niingie ndani.Nikajitazama kuanzia juu hadi chini na kuanza kupiga hatua za taratibu na kuingia ndani,gafla mlango ukafunga kwa nyuma na nikaanza kuhisi vitu vikianza kunishika shika mwilini mwangu.Sikuwa na budi zaidi ya kuanza kupiga mayowe ya kuomba msaada,ujanja wote ukaniishia.Gafla taa za chemli zipatazo nne zikawaka kwenye kona zote za chumba.Sikuamini kuona watu wengi wakiwa wamerundikana kwenye nyumba hii ambayo kwa ndani haina vyumba kama nyumba nyingine.Watu ambao wapo humu ndani wanavuja damu kwenye miili yao

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images