Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

TANGA RAHA- Sehemu ya Thelathini na Nane ( 38 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Jini la kiume ambalo ninaongea naye akaniishika mikono na gafla kufumba na kufumbua nikajikuta nikiwa katika anga na sikuamini macho yangu baada ya kuukuta mji mzima wa Tanga ukiwa umetawaliwa na damu nyingi lizilizo tapakaa maeneo mbalimbali ikiashiria watu wengi wametafunwa na majini yangu.

ENDELEA
Nikabaki nikihamaki kwani hali ilizidi kuwa mbaya,watu walikimbizama hovyo kuyaokoa maisha yao.Jini aliye nishika akanishusha juu ya gorofa moja la bandari.Kwa kutumia uwezo wa fimbo nilio nao nikaamaru majini wote kutulia,Wakatutii kwani maamlaka niliyo nayo juu yao yamezidi kuongezeka.Wakalizunguka eneo ambalo mimi nipo wakisubiri nini nifanye.
“Nani aliye waamuru kufanya huu upuuzi wakati niliwaachia kwa roo njema?”
Niliwauliza kwa ukali na majini wote wakaa kimya
“Aliye jijua kuwa amefanya tukio la kumla au kumdhuru binadamu yoyote ambaye ni mwema akae upande wangu wa kushoto”

Majini wakajigawa hadi mimi mwenyewe nikashangaa kwa jinsi wanavyo nisikiliza kwa umakini wa hali ya juu.
“Mkuu sisi ni wachache kati ya wale ambao wametekwa na wanadamu wenye nguvu zinazo endana na wewe.”
Jini mmoja alizungumza kwa sauti nzito akiwa katika kundi la majini walio watafuna watu.
“Hiyo sio mada niliyo nayo,nimeuliza ni kwanini mumewala watu wasio na hatia?”
“Mkuu wezetu ambao wametekwa walipandikizwa roho ambazo ni mbaya ndio maana wakawala watu na sisi tulio nusurika tukajua tumeruhusiwa kuwala watu ndio maana hata sisi tukawala”
Nikaangalia chini na kuona jinsi ukimya wa sehemu tuliyopo ulivyo tulia,Magari mengi yaliacha milango wazi huku mengine yakiwa yameangushwa na kuwashwa moto.
“KUMBUKA KUNA WATU WANAHITAJI MAJINI ILI KUYATUMIA KATIKA KAZI ZAO ZA KICHAWI NA WAGANGA,KUWA MAKINI NA HAO WATU.”

Sauti ya taratibu ilisikika masikioni mwangu,na ninauhakika hakuna jin lolote aliye weza kuisikia
“Sasa nifanye nini?”
“UNATAKIWA KUWAREJESHA KWANZA HAO 250 KAMA WALIVYO KISHA UANZE LILE AGIZO LA KWANZA ULILO PEWA.”
“Nitawarudisha vipi?”
“CHAGUA WAFUASI KUMI,NANE WAAMRISHE WAENDE KWENYE KILA KONA YA DUNIA WAKIWA WAWILI WAWILI,KISHA WAWILI WABAKI KATIKATI YA MKOA WAKO”
“Sijakuelewa,hao nane waende pende za dunia mzima au kwa huu mkoa tuiopo?”
“KWEENYE DUNIA,WANAKWENDA KUZUIA KUBADILISHWA KWA WEZAO,NA ENDAPO WEZAO WAKIBADILISHWA ZAIDI WATAWEZA KUKUANGAMIZA KWA MAANA WANAJUA SIRI ZAKO ZOTE”
“Sawa ila wewe sijajua ni nani?”
“MIMI UTANIJUA,NI KIONGOZI WAKO NILIYE AGIZWA KUFANYA KAZI HII”


AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 57 na 58 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA 

Nikaona gari tatu za ikulu ambazo anatembelea raisi zikiwa zimesimamishwa kwenye maegesho huku walinzi walio valia suti nyeusi wakiranda randa kika eneo.  Nikamuona Babyanka akitoka kwenye mlango wa jumba hili la kifahari, akamuita mmoja wa walinzi na kuzungumza naye kisha akageuza kuchwa chake na kutazama sehemu nilipo na macho yetu yakakutana jambo lililo mfanya Babyanka kuchomoa bastola yake na kuanza kufyatua risasi kadhaa kueleka sehemu nilipo.

ENDELEA
Nikajiachia na kwenye ukuta na kutua chini kwa umakini wa hali ya juu, nikaanza kukimbia kwa kasi kuelea kwenye mti nilipo iacha pikipikia. Nikafanikiwa kufika, nikashuhudia gari mbili za ikulu zikitoka nje ya geti hilo kwa kasi sana jambo lililo nifanya niiwashe pikipiki yangu kwa haraka na kuondoka eneo hili kwa kasi huku, huku gari hizo kutoka ikulu zikinifwata kwa nyuma. Sikuwa na namna ya kufanya zaidi ya kukatiza vichochoro na nikafanikiwa kupotezana na gari  hizo kwa umbali mkubwa.

Sikuwa na namna ya kuendelea kuwepo katika eneo hili la Tegeta, moja kwa moja nikarudi hadi Sinza kwa mama Marima, pikipiki nikaisimamisha pikipiki sehemu nilipokuwa nimemsimamisha dereva bodaboda. Nikaanza kutembea kwa miguu huku nikiwa makini, gari langu nikalikuta nje likiwa kama nilivyo liacha hapakuwa na tofauti yoyote.
Nikainga ndani na kumgongea mama Marim dirishani kwake. Nikamsikia akifungua mlango wa chumbani kwake, kisha akaufungua mlango wa mbele katika hii nyumba. Tukaingia chumba kwa mama Marim na akafunga milango yote.
“Vipi?”
Mama Marim aliniuliza huku akinitazama usoni.
“Wale wasichana wanafanya kazi chini ya raisi, na muda wowote wanaweza kurudi hapa, inanibidi kuondoka eneo hili”
“Usiku huu?”

“Yaaa usiku huu”
Mama Marim hakuwa na kitu cha kuzungumza ziidi ya kukubaliana na kile ambacho nilikuwa nimekikusudia, nikaanza kuvaa mwili wa plastiki unao nifanya niwe na muonekano wa mwamake, nilipo hakikisha nimemaliza kuvaa gauni langu, nikatoka nje nikiwa na funguo ya gari, nikafungua nyuma ya gari kwenye buti. Nikafungua begi la pesa, nikatoa kibunda kimoja cha dola kisha nikafunga na kurudi ndani.
“Chukua hizi pesa hakikisha unafungua biashara itakayo kusaidia maisha yako, sihitaji urudi kwenye hoteli kuendelea na ile kazi ya kuzalolishwa na watoto wadogo”
Mama Mariam akazitazama pesa zangu ninazo mpatia huku macho yakimtoka. Nikamshikisha pesa hizo mkinoni kisha nikachukua nguo zangu za kiume nilizo kuwa nimezivaa nikazikunja vizuri na kuzishika mkononi.
“Dany siamini kama ninaweza kupata pesa nyingi kiasi hicho”
“Ndio uamnini, mimi kwa sasa sina muda wa kuendelea kukaa hapa ninaondoka”

“Sawa Dany asante sana”
“Nitaendelea kumtafuta Marim sawa”
“Sawa Dany nashukuru”
Nikamiga busu la mdomo mama Marim, kisha nikabeba kila kilicho kuwa changu na kutoka nje, nikaingia kwenye gari langu na kuondoka. Japo ni usiku sikuwa na sehemu ya kueleka zaidi ya kutafuta sehemu nitakapo simamisha gari langu na kupumzika hadi itakapo timu asubuhi. Nikafika kwenye moja ya msitu maeneo ya Mbezi Temboni, nikasimamisha gari langu na kuzima taa kisha nikaikunjua siti yangu kidogo kisha nikalala.   
    Mtetemesho wa simu yangu niliyo iweka pembeni mwa siti ya gari, ndio ukanistua, nikafumbua macho yangu, nikaichukua kwa mkono wangu wa kushoto na kukuta ni mama ndio anaye nipigia.
“Shikamoo mama”
“Marahaba, sasa upo wapi?”
“Nipo kwenye moja ya msitu nimepumzika”
“Nina habari mbaya”
Ikanibidi kukaa vizuri kwenye siti yangu huku nikijiandaa kuisikiliza hiyo habari mbaya.

“Habari gani hiyo mama?”
“Kuna kikosi maalumu kutoka nchini Somalia leo, kimeingia kwa siri nchini Tanzania, na kina mpango wa kutekeleza tukio la kigaidi katika uwanja wa taifa wa mpira na mechi itakuwa ni Simba na Yanga”
Nikashusha pumzi kwa maana ni moja ya tukio ambalo sikuwa nalo kabisa katika mipango yangu
“Ila mama hiyo sio kazi yangu”
“Natambua sio kazi yako, ila tazama ni watu wangapi watakao poteza maisha yao pasipo kuwa na hatia na hichi wanacho kuja kukifanya leo ni ulipizaji kisasi kwa wezao walo uwawa kipindi kile kwenye dhiara ya raisi”
“Mungu wangu, sasa mama mimi nina anzia wapi?”
“Nakutumia picha za vijana hao watakao jitoa muhanga leo katika uwanja wa taifa. Wapo vijana wanne, ukiweza kuwatambua picha zao basi unaweza kufanikisha swala hilo la kuwaokoa maelfu ya watanzania”

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota, Mvuto wa Biashara na Mapenzi

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi 

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

NACTE yavifungia udahili vyuo 163

$
0
0

 Baraza la Taifa la Elimu na Ufundi (Nacte) limezuia vyuo 163 kudahili wanafunzi katika kozi mbalimbali ngazi ya astashahada na shahada, baada ya kukutwa na upungufu ikiwako kutokuwa na walimu wenye sifa.

Akizungumza leo, Machi 23 na waandishi wa habari, Mkuu wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Nacte, DK Annastella Sigwejo amesema walifanya uhakiki kwa vyuo 459, kati ya hivyo 296 ndivyo vimekidhi vigezo vya kutoa elimu kwa kiwango kinachotakiwa.

"Kutokana na hali hiyo hivyo ndivyo vinaruhusiwa kudahili wanafunzi kwa ajili ya kozi mbalimbali ngazi ya astashahada na stashahada kwa muhula wa udahili wa Machi na Aprili mwaka huu.”

Amesema licha ya kwamba vyuo vilivyosajiliwa viko 580 waliamua kujiridhisha kwa kuvifanyia uhakiki ambapo walifanikiwa kuhakiki vyuo 459.

Nacte wanawashauri wanafunzi kuhakikisha wanajiridhisha kuwa wanaomba kujiunga kwenye vyuo vilivyokidhi vigezo.

Mkuu wa Kitengo cha Udahili, Twaha Twaha amesema kuwa majina ya vyuo vilivyoruhusiwa kudahili yamewekwa kwenye tovuti ya Nacte.

"Hivyo Nacte inashauri waombaji wa udahili kujiridhisha kwa kuangalia hiyo orodha iwapo chuo anachokitaka kinaruhusiwa kudahili,"amesema Twaha.

Wolper:Sijawahi Kuachwa na Mwanaume Hata Siku Moja

$
0
0
Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Jacqueline Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa hajawahi hata siku moja kuachwa na wanaume.

Kumekuwa na stori nyingi Za kimbea mtandaoni ambazo zinaongelea kufeli kwa mahusiano ya Wolper na wanaume mbali mbali anaokuwa nao kwenye mahusiano.

Kiukweli kabisa Wolper ni moja kati ya watu waliokuwa na bahati mbaya kwenye mahusiano inawezekana ikawa pia ni wanaume ambao anachagua kuwa nao.

Kwa mwaka Jana pekee Wolper alikuwa kwenye mahusiano na wanaume watatu tofauti ambao ni Harmonize, Brown na Engine.

Lakini hivi sasa Wolper anaweka wazi kuwa mahusiano yake kuvunjika sio yeye mwenye makosa na wala hajawahi kuachwa yeye ndio anaacha kwenye mahusiano.

Wolper amefunguka hayo kwenye mahojiano aliyofanya na The playlist ya Times FM ambapo ameongea Mengi zaidi:

"Kiukweli kabisa naamini kuwa hakuna siku ambayo Ex wangu hata mmoja ambaye ameshawahi kuja kuniongelea vibaya Kwenye Interview yoyote kwaiyo kama ningekuwa na matatizo wangekuwa wanakuja kuniongelea vibaya kwaiyo mimi na wao ndio tunajua ukweli kuwa nani ana matatizo  

"Lakini pia sipendi sana kuongelea maex ila kikubwa ambacho kipo kwangu sipendi ujinga na sipendi kuonekana mpumbavu kwa sababu mimi ni mzuri najiamini natafuta hela yangu napenda kazi yangu na napenda kuheshimiwa kwaiyo kama ukinizingua nakufuta na by the way sijawahi kuachwa”.

Rais Trump na Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Obama Watishiana Kutwangana Ngumi

$
0
0
Rais wa Marekani, Donald Trump ameamua kuweka wazi kuwa amechoshwa na kauli za vitisho kutoka kwa aliyewahi kuwa makamu wa Rais nchini humo wakati wa utawala wa Barack Obama, Joe Biden.

Trump amesema amechoshwa na kauli za vitisho juu yake zinazotolewa na mwanasiasa huyo mkongwe nchini Marekani kutoka chama cha Democratic na kuweka wazi kuwa haogopi chochote kwani anamjua toka enzi ni mtu asiyekuwa na nguvu kimwili na kiakili.

“Mpuuzi Joe Biden anajifanya kama mtu mwenye nguvu. Ukweli ni kwamba ni mtu dhaifu kimwili na kiakili mbaya zaidi anatishia kunipiga kwa mara ya pili hii. Nadhani hanijui vizuri nitamsambaratisha mara moja na kurudi nyumbani akilia njia nzima. Usipende kutishia watu.“ameandika Trump kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Jumanne Machi 20, 2018 Joe Biden akiongea na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Masuala ya siasa cha Miami akisema kuwa kama wangekuwa wanasoma naye sekondari angemchakaza kwa masumbwi Rais Donald Trump.

“Wananiuliza ninauwezo wa kufanya mdaharo na Trump, nawajibu hapana. Natamani kama tungekuwa sekondari ningempeleka kwenye eneo la kufanyia mazoezi nimchakaze kwa makonde mazito. Haiwezekani Rais wa nchi awachezee wanawake kwa kuwatomasa halafu aje aombe radhi hadharani eti alifanya makosa, hapa chama cha Republican kilichemsha,“amesema Joe Buddeni kwenye video hiyo iliyowekwa kwenye mtandao wa facebook wa chuo hicho.

Joe Biden anatajwa kuwa ndiye atakayekuwa mgombea wa urais mwaka 2020 kupitia tiketi ya chama cha Democratic na atashindana na Rais Trump kama atapita kwenye kura za maoni kwenye uchaguzi huo.

Hasheem Thabeet Amkumbuka Ex Wake Jokate Mwegelo

$
0
0
Mwanamichezo anayecheza mpira wa kikapu ‘basketball’ nje ya nchi, Hasheem Thabit amemkumbuka aliyekuwa mpenzi wake mrembo Jokate kwa kumpa Zawadi siku ya birthday yake.

Hasheem alijzolea umaarufu baada ya kuanza kucheza basketball katika ligi ya NBA nchini Marekani miaka ya nyuma. Hivi sasa Hasheem anacheza basketball nchini Japan.

Hasheem na Jokate walikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa zaidi ya miaka mitatu na baadae kuweka wazi kuwa wameachana lakini Siku chache zilizopita ilikuwa ni birthday ya Jokate na Hasheem alimpa zawadi ya maua rose.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram Jokate alianika zawadi hiyo aliyopewa na Ex boyfriend wake na kuandika maneno ya shukrani:

Ni Dr. Chief Malunde Pekee Anaetibu Nguvu Za Kiume Na Kumtuliza Umpendae Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
"NI DR. CHIEF MALUNDE PEKEE ANAETIBU NGUVU ZA KIUME NA KUMTULIZA UMPENDAE KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI"
-baada ya kujichimbia katika nchi za kiarabu kwa zaidi ya miaka (10)sasa amewasili nchini na dawa za tiba asilia.
 
1/NGOLO 3 POWER-ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, ina ubora wa hali ya juu wa kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wasiojiweza kufanya tendo la ndoa, inaimarisha misuli iliyolegea na kusinyaa, inarutubisha mbegu za kiume na kukufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15-25 kuwa na hamu na tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila kuchoka, inarefusha uume inchi 5-8 na kunenepesha hadi cm 4 kwa wenye maumbile madogo, dawa hii imeboreshwa na hutibu matatizo haya kwa muda mfupi tu.
 
2/MAGOYE MVUTO- dawa hii ina uwezo mkubwa sana kumvuta na kumtuliza aliekuacha awe mpenzi, mme/mke itamfanya akutafute mwenyewe ndani ya masaa 3tu na kukutimizia mahitaji yako kwa haraka na kumfunga asiwe na mtu mwingine.
 
3/SUPER LUBEJA- ni dawa ya kushepu umbo no.8 mguu wa bia, kuongeza hips, na makalio kwa muda wa siku 5tu unapata saizi uipendayo, kuondoa makovu, chunusi, harufu mbaya ya mwili michirizi, kupunguza tumbo na maziwa kwa siku 6tu.
 
4/NG'WESHI MIX- ni dawa ya biashara ya kupata wateja wengi, kusafisha nyota, kurudishwa kazini na kupandishwa cheo, kurudisha mali iliyoibiwa au kudhurumiwa.
 
PIA TUNATIBU MAGONJWA SUGU KAMA: vidonda vya tumbo, ngiri, chango na uzazi kwa kina mama: (dawa zote hazina madhara kwa mtumiaji) HUDUMA HIZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO: TUNAPATIKANA DSM BUGURUNI SHELI AU PIGA SIM NO_ 0763-181099.

Okoa Ndoa Yako, Biashara Yako, Kazi Yak,o Mpenzi Wako..... Onana Na Dr Mfaume Mzee Mwenye Uwezo Wa Kukutatulia Magonjwa Na Matatizo

$
0
0
Je unaupungufu wa nguvu za kiume au maumbile madogo ya kiume?

 SHAFTI POWER; ni dawa itokanayo na mizizi na magamba ya mitishamba. Hutibu matatizo matatu kwa pamoja
 1 kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka 
2 kuwahi kufika kileleni kabla ya mpenzi au mke wako
3 kulegea kwa misuli na uume kusinyaa na mda mwingi uume kuanguka ukiwa bado unaendelea na tendo, DAWA HII ITAKUPA UWEZO WA KURUDIA TENDO ZAIDI YA MARA TATU NA UTACHELEWA KUFIKA KILELENI

MWIMALA MIX NO 2 ;ni dawa ambayo hurefusha uume saiz upendayo ...inch 5 , 6,7,8 na unene sm 1-5 .Dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hadhina madhara yoyote

NINI KINACHOCHANGIA KUWA NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO?
 1 kufanyia tohara ukiwa na umri mkubwa
3 msongo wa mawazo 
4 ngiri na korodani kuvimba 
5 vidonda vya tumbo 
6 maumivu ya mgongo na kiuno 
7 mfumo wa mahisha 
8 presha, kisukali na magonjwa ya moyo 

TUNATO TIBA YA KISUKALI,KORODANI KUVIMBA VIDONDA VYA TUMBO UZAZI KWA WANAWAKE NA WAUME .Tunarudisha Mali iliyoibiwa, kudhibiti jini chuma ulete kwa wanaopata pesa na ujui ziendako.
 
KWA SHIDA NA MAGONJWA WASILIANA NAMI .Ofisi ipo mbagara Zakhemu .Kwa wateja wa mikoani mtatumiwa huduma utakayo pia tunatibu kwa njia ya simu au piga simu no 0789234653 .WOTE MNAKARIBISHWA

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Makamu Wa Rais Akutana Na Mkurugenzi Mtendaji Wa Bill Gates Foundation

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 23 Machi, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation Bw. Rodger Voorhies kwenye makazi ya Makamu wa Rais, Kilimani mjini Dodoma.

Makamu wa Rais amesema amezungumza mambo mengi na Bw. Rodger hasa kwenye masuala ya afya, uwezeshaji wanawake kiuchumi, kuwatoa kwenye kilimo cha sasa na kuwaingiza kwenye kilimo biashara lakini pia kuongeza thamani ya mazao na mambo ya masoko.

Makamu wa Rais alisema wamezungumza namna ya kuwarasimisha wanawake wa vijijini na wanawake wakulima ikiwa pamoja na uwezekano wa wanawake vijijini kuweza kupata mikopo.

Aidha Makamu wa Rais alizungumzia suala zima la upatikanaji wa maji safi na salama haswa kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam ambapo mara kwa mara kumekuwa na milipuko ya magojwa ya kipindu pindu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation Bw. Rodger Voorhies alisema wamekuja kwa Makamu wa Rais kuzungumza juu ya shughuli zinazofanywa na taasisi hiyo hapa nchini haswa katika masuala ya Kilimo na Afya na Mkakati Mpya wa Kuwawezesha Wanawake Kiuchumi.

Aidha wameipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua kubwa ambayo wamepiga katika kuwajumuisha wanawake katika masuala yanayohusu Fedha.

Mwisho, Mkurugenzi huyo ameahidi ushirikiano mkubwa kwa Serikali ya Tanzania katika kutekelezaji wa miradi ya taasisi yao.

Kimataifa: Marekani yatangaza vikwazo vya kibiashara dhidi ya China....Wachina Nao Wamejibu Mapigo

$
0
0
Nchi ya China Ijumaa hii imeionya Marekani kuwa haiogopi vita vya kibiashara wakati huu ikitishia kutoza kodi ya zaidi ya dola bilioni 3 kwa bidhaa kutoka nchini Marekani katika kile kinachoonekana kujibu tangazo la rais Donald Trump kutoza kodi dhidi ya bidhaa kutoka China.

Utawala wa Beijing umetoa orodha ya bidhaa ambazo zitalengwa na kuongezewa ushuru wa hadi kufikia asilimia 25 kuanzia kwenye matunda hadi kwa nyama ya nguruwe licha ya kuwa imeshindwa kuchukua hatua zaidi na kuonesha nia ya kuwa na mazungumzo.

Hatua za hivi karibuni zimeshuhudia masoko ya hisa yakiporomoka wakati huu Marekani, ambayo inaituhumu Uchina kwa wizi wa haki miliki pamoja na hatua nyingine ambazo sio za haki dhidi ya makampuni yake, huenda ikachochea vita ya kibiashara.

"China haitaki kupigana vita ya kibiashara, lakini haiogopi kabisa vita hiyo," imesema taarifa ya wizara ya biashara ya China.

Mapema rais Donald Trump alitia saini amri ambayo itaweka ukomo kwa uwekezaji wa makampuni ya Uchina nchini humo.

"Tuna tatizo kubwa la wizi wa haki miliki linaloendelea kwa sasa," amesema rais Trump wakati akitia saini agizo hilo ambalo litajumuisha bidhaa ambazo zitatozwa ushuru wa hadi kufikia asilimia 25.

Hatua ya Trump haijachukua mara moja hatua za kuweka ushuru mpya, lakini ndani ya majuma mawili waziri wa biashara wa Marekani anatarajiwa kutangaza bidhaa zilizolengwa kwenye amri hiyo ya rais Trump.

Wakati huu rais Trump akionekana kutafuta ugomvi na mataifa yenye nguvu, utawala wa Beijing umeonya kuwa vita vya kibiashara havitamnufaisha yeyote na haitakaa kimya kuona Marekani ikitoa adhabu kwa biashara zake.

Waziri wa viwanda Wilbur Ross alisema Alhamisi ya wiki hii kuwa hatua za kulinda haki zake miliki ililenga kuifanya China ije kwenye meza ya mazungumzo na kujadiliana kutafuta njia za kudhibiti wizi huo.

Kimataifa:Viongozi wa EU watishia kuwafukuza wanadiplomasia zaidi wa Urusi

$
0
0
Viongozi wa umoja wa Ulaya wameungana kumuunga mkono waziri mkuu wa Uingereza Theresa May katika kuilaumu nchi ya Urusi kwa shambulio la sumu kusini mwa jiji la London na kukubaliana kumuitisha balozi wao wa Moscow kwa majadiliano zaidi.

Baadhi ya nchi nazo zimeanza kufikiria kuchukua hatua kama za Uingereza za kuwafurusha wanadiplomasia wa Urusi, huku nchi za Lithuania na Ufaransa zikiwa nchi za awali kuonesha kutaka kufanya hivyo.

Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May aliwaambia wenzake wa umoja wa Ulaya kuwa ni muhimu kuungana kupinga tukio la Machi 4 ambapo jasusi wa zamani wa Urusi Sergei Skripal na mtoto wake Yulia walipewa sumu iliyowaathiri mishipa ya fahamu kwenye mji wa Salisbury.

Katika mkutano wa wakuu wa nchi za umoja wa Ulaya uliofanyika jijini Brussels hapo jana, viongozi wa nchi 28 wametangaza kuiunga mkono Uingereza na kukubaliana kuwa kuna uwezekano mkubwa utawala wa Moscow ulihusika na kwamba hakuna maelezo mengine yanayoweza kupindisha ukweli.

Viongozi hao wameahidi kuchukua hatua za pamoja na waziri mkuu wa Uholanzi Mark Rutte amesema wamekubaliana kumuita balozi wao mjini Moscow kwa majadiliano zaidi.

"Baadhi ya nchi wanachama wanaangalia uwezekano wa kuwafurusha wanadiplomasia wa Urusi kwenye nchi zao au kuwatisha wanadipolomasia wao," imesema taarifa ya umoja wa Ulaya.

Utawala wa Moscow unakanusha vikali madai kuwa ulihusika kwenye shambulio la sumu la London ambapo inadaiwa kuwa sumu aina ya Novichok inayotengenezwa na nchi hiyo ndio iliyotumika.

Waziri mkuu May amewaambia viongozi wenzake kuwa ni lazima ziungane katika kuikemea nchi ya Urusi na kuonya kuwa ikiwa watafumbia macho matendo kama haya, nchi hiyo itaendelea kuwa tishio kwa miaka mingi ijayo.

Jasusi Skripal na mwane bado wako hospitalini wakipatiwa matibabu baada ya kupatikana wakiwa wamezimia kwenye bustani moja ya mapumziko licha ya polisi aliyekuwa ameathiriwa na sumu hiyo wakati akiwahudumia, jana akiruhusiwa kutoka hospitalini.

Beaking News: Lori la Mafuta Lawaka Moto na Kuua Wawili Mlima Sekenke Singida

$
0
0
Taarifa kutoka mkoani Singida ni kwamba lori la mafuta limeanguka na kuwaka moto katika eneo la Mlima Sekenke na watu wawili wameripotiwa kupoteza maisha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Deborah Magiligimba,  amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa watu wawili wamefariki, lakini bado hawajapata majina yao.

 Magiligimba amesema kwamba, ajali hiyo imetokea saa nne na nusu asubuhi milima ya Senkenke Wilaya ya Iramba barabara ya Singida - Nzega.

Gari iliyohusika kwenye ajali hiyo ni namba T167 DTC aina ya Flight liner ambayo ilikuwa na Trailer namba T 960 ALS. Hili gari ni mali ya Petromac Africa Dar es salaam.

Gali iliacha njia na kupinduka ambapo ililipuka na kusababisha moto mkubwa uliopelekea vifo vya watu wawili ambao ni wanaume.

Uchunguzi wa jeshi la Polisi wa awali baada ya kufatilia kwenye mzani wa Singida, gari ilipimwa mzani wa Singida saa moja na dk 27 asubuhi dereva alikua anaitwa Erasto Abedi Rusazi na alikuwa na tingo msaidizi wake anayeitwa Ramadhani Hashim Ramadhini wote ni Wakazi wa Tabata Dar Es Salaam.

RPC Deborah Magiligimba, ametoa wito kwa madereva watii sharia za barabarani ili kuepusha ajali.

Mahakama ya Haki za Binadamu Yawataka Babu Seya na Mwanaye Wadai Fidia

$
0
0
Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu(AfCHPR), imesema Mahakama za ndani Tanzania katika kesi ya kubaka na kulawiti iliyokuwa inamkabili mwanamuziki Nguza Viking (Babu Seya) na mwanawe Johnson Nguza (Papii Kocha) zilitenda haki kwa kiwango kikubwa na kwa upande mwingine zilikiukwa.

Aidha, kutokana na kukiukwa kwa baadhi ya haki zao hizo, mahakama hiyo imewaruhusu kuwasilisha hoja na kuainisha ni namna wanaweza kuomba fidia kulingana na haki zao ziliokiukwa ndani ya siku 30 huku upande wa Jamhuri ukitakiwa kujibu hoja hizo ndani ya siku 30.

Akitoa hukumu hiyo katika mahakama hiyo leo Ijumaa Machi 23, Kiongozi wa majaji nane waliokuwa wakisilikiza shauri hilo, Gerald Niyungeko mbele ya Rais wa Mahakama hiyo, Jaji Sylvain Ore, amesema baadhi ya haki zilizotendwa ni pamoja na kuwaachia watuhumiwa watatu kwenye kesi hiyo pamoja na kubakiza mashitaka manne kati ya 21 yaliyokuwa yakiwakabili.

“Haki zao hazikukiukwa kulingana na uamuzi uliotolewa na mahakama za ndani za Tanzania kwa kuwaachia washtakiwa wengine na kupunguza mashtaka 21 hadi manne, lakini kwa upande mwingine zilikiukwa, kwa mfano wakiwa Mahakama ya Halimu Mkazi Kisuti walikaaa mahabusu kwa siku nne bila kufahamishwa makosa yao lakini pia hawakuwa na wakili wa kuwatetea.

“Aidha, waleta maombi pia waliomba kupimwa mkojo na damu ili kuthibitishwa kama waliwaingilia wale watoto ambao upande wa jamhuri ulidai waliambukizwa magonjwa ya zinaa lakini walikataliwa.

“Kwa upande mwingine, Nguza aliomba kupimwa kama ana uwezo wa kufanya tendo la ndoa au lakini pia alikataliwa,” amesema Jaji Niyungeko.

Hata hivyo, kuhusu kupinga kifungo cha maisha, Jaji Niyungeko amesema mahakama haikujielekeza katika shauri hilo kwa sababu waleta maombi wako huru kwa msamaha wa rais hivyo haikuona sababu ya kushughulikia hilo kwani wako nje kwa mujibu wa sheria.

Babu Seya na Papii Kocha waliachiwa kwa msamaha wa rais Desemba 9, mwaka jana kutokana na kifungo cha maisha jela walichohukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Juni mwaka 2004 baada ya kumkuta na hatia ya kunajisi na kulawiti watoto 10 ambapo walikata rufaa Mahakama za juu na kugonga mwamba na hivyo kulazimika kukimbilia AfCHPR wakidai haki zao zilivunjwa.

Orodha ya Vyuo/Taasisi Zinazoruhusiwa Kufanya Udahili wa Wanafunzi Wapya 2018

$
0
0
Na Jina la Chuo/Taasisi

1 Agency for Development of Education Management (ADEM) – Mbeya Campus
2 AMO Training Centre - Bugando
3 Arafah Teachers' College - Tanga
4 Archbishop John Ramadhan School of Nursing - Korogwe
5 Ardhi Institute - Tabora
6 Ardhi Institute Morogoro - Morogoro
7 Arusha Institute of Business Studies - Arusha
8 Arusha Lutheran Medical Centre School of Nursing - Arusha
9 Arusha Technical College - Arusha
10 Assistant Medical Officers Training College -Mbeya
11 Bagamoyo College of Arts (TaSUBa) - Bagamoyo)
12 Bagamoyo School of Nursing - Bagamoyo
13 Bariadi Teachers College - Bariadi
14 Berega School of Nursing - Kilosa
15 Besha Health Training Institute - Tanga
16 Bishop Nicodemus Hando College of Health Sciences - Babati
17 Borigaram Agriculture Technical College - Dar es Salaam
18 Bugando School of Nursing - Nyamagana
19 Bulongwa Health Sciences Institute - Makete
20 Bulongwa Training Institute - Makete
21 Bustani Teachers’ College - Kondoa
22 Butimba Teachers College - Nyamagana
23 Capital Teachers’ College - Dodoma
24 Centre for Educational Development in Health Arusha
25 Centre for Foreign Relations - Dar-es-Salaam
26 Coast Teachers College - Kibaha
27 College of Business and Management - Dar es Salaam
28 College of Business Education - Dar-es-Salaam
29 College of Business Education - Dodoma
30 College of Business Education – Mwanza Campus
31 Dabaga Institute of Agriculture - Kilolo
32 Dar es Salaam School of Journalism - Dar es Salaam
33 Dar-es-Salaam Institute of Technology - Dar-es-Salaam
34 Dar-es-Salaam Maritime Institute - Dar-es-Salaam
35 Dodoma Institute of Development and Entrepreneurship – Dodoma
36 Eastern Africa Statistical Training Centre - Dar-es-Salaam
37 Eastern and Southern African Management Institute - Arusha
38 Ebonite Institute of Education - Dar es Salaam
39 Eckernforde Teachers' College - Tanga
40 Elijerry Training Centre - Muheza
41 Faraja Health Training Institute - Moshi
42 Fisheries Education and Training Agency (FETA) Mbegani - Bagamoyo
43 Fisheries Education Training Agency (FETA) - Nyegezi
44 Forest Industries Training Institute (FITI) - Moshi
45 Forestry Training Institute (FTI) Olmotonyi - Arusha
46 Future World Business College - Dar es Salaam
47 Geita School of Nursing - Geita
48 Habari Maalum College - Arusha
49 Heri Nursing School - Kigoma
50 Horticultural Research and Training Institute – Tengeru Arusha
51 Huruma Health Training Institute - Rombo
52 Igabiro Training Institute of Agriculture - Muleba
53 Ilasi Training Institute - Mbozi
54 Ilembula Institute of Health and Allied Sciences - Njombe
55 Ilonga Teachers’ College - Kilosa
56 Ilula Nursing School - Kilolo
57 Institute of Accountancy Arusha - Arusha
58 Institute of Adult Education - Dar-es-Salaam
59 Institute of Adult Education – Mwanza
60 Institute of Finance Management - Dar-es-Salaam
61 Institute of Finance Management - Mwanza Campus
62 Institute of Judicial Administration - Lushoto
63 Institute of Procurement and Supply - Dar-es-Salaam
64 Institute of Rural Development and Planning - Dodoma
65 Institute of Rural Development and Planning – Mwanza Campus
66 Institute of Social Work - Dar-es-Salaam
67 Institute of Tax Administration - Dar-es-Salaam
68 Institution of Construction Technology – Morogoro
69 International Film Angels Training School – Dar-es-Salaam
70 Isimila Nursing School - Iringa
71 Kabanga School of Nursing - Kasulu
72 Kahama College of Health Sciences - Kahama
73 Kairuki School of Nursing - Dar es Salaam
74 Kaliua Institute of Community Development -Tabora
75 KAM college of Health Sciences - Dar es Salaam
76 KAPS Community Development Institute - Mufindi
77 Karagwe Institute of Allied Health Sciences - Karagwe
78 Karatu Health Training Institute - Karatu
79 Karume Institute of Science and Technology - Zanzibar
80 Kasulu Teachers College - Kasulu
81 Katoke Teachers College - Muleba
82 Katoro Teachers College - Bukoba
83 KCMC AMO General School Moshi - Moshi
84 KCMC AMO Ophthalmology School - Moshi
85 KCMC School of Physiotherapy - Moshi
86 Kibaha College of Health and Allied Sciences - Kibaha
87 Kidugala Teachers College - Njombe
88 Kilacha Agriculture and Livestock Training Institute - Moshi
89 Kilema College of Health Sciences - Moshi
90 Kilimanjaro Agricultural Training Centre - Moshi
91 Kilimanjaro Institute of Technology and Management - Dar es Salaam
92 Kilimanjaro International Institute for Telecommunications, Electronics and Computers (KIITEC) - Arusha
93 Kilimanjaro Modern Teachers' College - Moshi
94 Kilimanjaro School of Pharmacy - Moshi
95 Kilombero Agricultural Training and Research Institute (KATRIN) - Kilombero
96 King’ori Teachers’ College - Arusha
97 Kirinjiko Islamic Teachers' College - Same
98 Kisanga Teacher’s College - Dar es Salaam
99 Kisongo Teachers' College - Arusha
100 Kiuma Nursing School -Tunduru
101 Kiuma Teachers College - Tunduru
102 Kizimbani Agricultural Training Institute - Zanzibar
103 Kolandoto College of Health Sciences - Shinyanga
104 Korogwe Teachers College - Korogwe
105 Landmark Institute of Education Sciences and Technology – Geita
106 Livestock Training Agency - Mpwapwa
107 Livestock Training Agency (LITA) - Dar es Salaam
108 Livestock Training Agency (LITA) - Morogoro
109 Livestock Training Agency (LITA) Mabuki - Misungwi
110 Livestock Training Agency Buhuri Campus - Tanga
111 Livestock Training Agency Kikulula - Karagwe
112 Livestock Training Agency Tengeru Campus –Arusha
113 LUA Teacher’s College - Dar es Salaam
114 Lugala School of Nursing - Ulanga
115 Lugalo Military College of Medical Sciences - Dar es Salaam
116 Lugarawa Health Training Institute - Ludewa
117 Mabughai Community Development Technical Training Institute - Lushoto
118 Machame Health Training Institute - Moshi
119 Makambako Institute of Health Sciences - Makambako
120 Malya College of Sports Development - Kwimba
121 Mamire Teachers' College - Babati
122 Mamre Agriculture and Livestock College - Wanging’ombe
123 Mandaka Teachers’ College - Moshi
124 Mary Queen Technology College - Morogoro
125 Mbalizi Polytechnic College - Mbeya
126 Meteorological Training Cntre - Kigoma
127 Military Aviation School – Ngerengere
128 Mineral Resources Institute - Dodoma
129 Ministry of Agriculture Training Institute - Mbeya
130 Ministry of Agriculture Training Institute (MATI) Ilonga - Kilosa
131 Ministry of Agriculture Training Institute (MATI) Mtwara - Mtwara
132 Ministry of Agriculture Training Institute Igurusi -Mbeya
133 Mirembe School of Nursing - Dodoma
134 MISO Teachers College - Mufindi
135 Mkolani School of Nursing and Midwifery - Mwanza
136 Monduli Teachers' College - Monduli
137 Montessori Teacher Training College - Mtwara
138 Montessori Teachers' Training Centre - Lushoto
139 Montessori Training Centre - Mwanza
140 Moravian Teachers Training College - Mbeya
141 Morogoro Teachers College - Morogoro
142 Moshi Teachers’ College - Moshi
143 Mpuguso Teacher Training College - Tukuyu
144 Ms Training Centre for Development Cooperation - Arusha
145 Mt. Maria Goretti Agriculture Training Institute - Kilolo
146 Mtwara (K) Teachers College - Mtwara
147 Mtwara (U) Teachers College - Mtwara
148 Mtwara Clinical officers training Centre - Mtwara
149 Mtwara Nursing Training College (MNTC) - Mtwara
150 Mufindi Teachers College - Mufindi
151 MusomaUtalii College - Tabora
152 Muyoge Health Science and Management College - Mafinga
153 Mvumi Institute of Health Sciences - Dodoma
154 Mwambani School of Nursing - Songwe
155 Mweka College of African Wildlife Management - Moshi
156 Nachingwea Teachers College -Nachingwea
157 National College of Tourism (NCT), Temeke Campus - Dar es Salaam
158 National College of Tourism, Bustani Campus - Dar es Salaam
159 National Institute of Transport - Dar-es-Salaam
160 Nazareth College of Education - Mbinga
161 Ndala Teachers’ College - Nzega
162 Ndolage School of Nursing - Bukoba
163 New Mafinga Health and Allied Institute - Mafinga
164 Newala School of Nursing - Mtwara
165 Njombe Health Training Institute - Njombe
166 Njombe School of Nursing - Njombe
167 Njuweni Institute of Hotel, Catering and Tourism Management - Kibaha
168 Nkinga Institute of Health Sciences - Igunga
169 Northern Highlands Teachers’ College - Moshi
170 Operating Theatre Management School - Mbeya
171 Paradigms College of Health Sciences - Dar es Salaam
172 Paradise Business College - Sumbawanga
173 Peramiho School of Nursing - Songea
174 Primary Health Care Institute - Iringa
175 Richrice Teachers College - Geita
176 Rubya Health Training Institute - Muleba
177 Rungemba Teacher College - Iringa
178 Rungwe International College of Business and Entrepreneurship Development - Rungwe
179 School of Optometry – KCMC - Moshi
180 Sengerema Clinical Officers Training Institute - Sengerema
181 Shaalika Institute of Science and Technology - Same
182 Shinyanga Teachers College - Shinyanga
183 Shirati College of Health Scinces - Rorya
184 Shiwanda Teachers College - Mbozi
185 Singachini Teachers' College - Moshi
186 Singida Health Laboratory Assistants School - Singida
187 Songe Teachers’ College - Kilindi
188 Songea Teachers College - Songea
189 Sr. Dr. Thekla Nyangao School of Nursing - Mtwara
190 St Aggrey College of Health Science - Mbeya
191 St. Alberto Teachers College - Musoma
192 St. Bakhita Health Training Institute - Nkasi
193 St. Bernard Teachers’ College - Singida
194 St. Francis Technical College – Dar es Salaam
195 St. Gaspar School of Nursing - Itigi
196 St. John College of Health Science - Mbeya
197 St. Magdalene School of Nursing - Misenyi
198 St. Mary’s Teachers College - Dar es Salaam
199 St. Monica Teachers College - Iringa
200 St. Rock College of Early Education - Korogwe
201 Sumve School of Nursing - Kwimba
202 Sunrise Teachers College - Mbozi
203 Suye Health Institute – Arusha
204 Tanzania Correctional Training Academy - Dar es Salaam
205 Tanzania Geommological Centre – Arusha
206 Tanzania Institute of Accountancy - Dar-es-Salaam
207 Tanzania Institute of Accountancy – Mbeya Campus
208 Tanzania Institute of Accountancy - Mwanza Campus
209 Tanzania Institute of Accountancy – Singida Campus
210 Tanzania Peoples Defence Force ICT Centre - Dar es Salaam
211 Tanzania Police School - Moshi
212 Tanzania Police Staff College - Kidatu
213 Tanzania Regional Immigration Training Academy - Moshi
214 Tanzania Training Center for International Health (TTCIH) - Ifakara
215 Tengeru Community Development Training Institute - Arusha
216 The Mwalimu Nyerere Memorial Academy - Dar-es-Salaam
217 The Mwalimu Nyerere Memorial Academy - Zanzibar
218 Triple J Institute of Social Studies – Arusha
219 Tumaini Jipya Medical Training School - Mafinga
220 Tusaale Business and Planning College – Mafinga
221 Tusaale Teachers College - Mufindi
222 Unique Academy - Dar-es-Salaam
223 University Computing Centre - Dodoma
224 University of Dar es Salaam Computing Centre - Arusha
225 University of Dar es salaam Computing Centre - Mbeya Campus
226 University of Dar es Salaam Computing Centre - Mwanza
227 Ununio Institute of Professionals - Dar es Salaam
228 Vector Control Training Centre - Muheza
229 VETA Kipawa ICT Centre - Dar es Salaam
230 Vikindu Teachers College - Mkuranga
231 Visele Live-Crop Skills Training Centre - Mpwapwa
232 Waama Lutheran Teachers’ College - Mbulu
233 Wami International College of Business Management - Morogoro
234 Water Development and Management Institute - Dar-es-Salaam
235 Wesley College – Mwanza
236 Yohana Wavenza Health Institute - Songwe
237 Zanzibar College of Business Education - Zanzibar
238 Zanzibar Law Resource Centre - Zanzibar
239 Zanzibar Police College - Zanzibar
240 Zanzibar School of Journalism and Media Studies - Zanzibar

IMETOLEWA NA:
OFISI YA KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)
TAREHE : 20 Machi, 2018

Waziri Mkuu Aridhishwa Na Mradi Wa Ujenzi Wa ‘Termina lIII'

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea mradi wa ujenzi wa jengo la tatu la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) na kwamba ameridhishwa na maendeleo yake.

Mradi wa ujenzi wa jengo hilo umefikia asilimia 70 na unatarajiwa kukamilika Juni 2019 na utakuwa na uwezo wa kuegesha ndege kubwa 24 kwa wakati mmoja, pamoja na kuhudumia abiria milioni sita kwa mwaka na kuwa na.

Waziri Mkuu ambaye ametembelea mradi huo leo (Ijumaa, Machi 23, 2018) amesema amefarijika na maendeleo ya ujenzi wa mradi huo pamoja na kukuta Watanzania wengi wakishiriki katika kazi za ujenzi.

“Serikali imejiimarisha katika kuboresha usafiri wa anga, ambapo kukamilika kwa jengo hili kutachangia ongezeko la ndege kubwa nyingi kutua nchini. Pia sekta ya utalii nayo itaimarika kwa kuwa watalii wanaoingia nchini wataongezeka.”

Amesema mbali na ujenzi wa jengo hilo, pia Serikali inaendelea kuvikarabati viwanja mbalimbali vya ndege nchini kikiwemo cha Musoma, Iringa, Kilwa Masoko, Lake Manyara, Lindi, Moshi, Njombe, Tanga, Simiyu, Singida na Songea ili kuboresha huduma za usafiri wa anga nchini.

Akisoma taarifa za ujenzi wa mradi Mkurugenzi wa Miradi wa TANROADS, Mhandisi Christianus Ako amesema mradi huo umeajiri wafanyakazi 1,400 kwa sasa na wanatarajia kuongeza watumishi na kufikia 1,800.

Pia wanatarajia kufanya majaribio ya kwanza ya mifumo na vifaa vya umeme kuanzia Julai, 2018 kwa kuwa tayari utekelezaji wa kazi kubwa za ujenzi wa mradi huo zimefanyika.

Tamko La Waziri Wa Afyaummy Mwalimu Kuelekea Maadhimisho Ya Siku Ya Kifua Kikuu Duniani Machi 24 – Leo Mjini Dodoma

$
0
0
Na WAMJW-Dodoma.
# Kifua Kikuu(TB) ni ugonjwa wa kuambukiza unaoongoza kwa kusababisha vifo vingi Duniani.

# Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani(WHO) inakadiriwa kuwa zaidi ya watu milioni 10.4 huugua Kifua Kikuu kila mwaka Duniani na Milioni Moja kati ya hao ni watoto wenye umri chini ya miaka 15.

# Tafiti nyingi zinaonesha kuwa karibia theluthi moja ya Watanzania tayari wamepata maambukizo ya Kifua Kikuu na wanaishi na vimelea mwilini mwao.

# Kauli mbiu ya mwaka huu inasema *” Viongozi Tuwe Mstari wa Mbele Kuongoza Mapambano ya Kutokomeza TB.”*

#Nchini Tanzania kila mwaka jumla ya watu 160,000 wanakadiriwa kuwa na ugonjwa wa Kifua Kikuu.

# Nitoe wito kwa viongozi wa ngazi zote kuifanya vita dhidi ya TB kuwa agenda muhimu na ya kipaumbele.

# Napenda kuwakumbusha TB inatibika na kupona kabisa, dawa zake zinatolewa bure na zinapatikana sehemu zote nchini katika vituo vya Umma na Binafsi.

# Serikali imechukua hatua mbalimbali kukabiliana na tatizo la Kifua Kikuu nchini ikiwemo kuimarisha uchunguzi na ugunduzi wa Kifua Kikuu katika Vituo vya Afya.

# Serikali na wadau mbalimbali tunaendelea na utekelezaji wa kampeni za uhamasishaji na upimaji wa Wananchi katika maeneo ya migodi, makazi duni kwenye miji mikubwa, magereza na shule za bweni.

# Pia Serikali imezindua dawa mpya za TB za watoto ili kuhakikisha zinakidhi matakwa ya Shirika la Afya Duniani ( WHO), dawa hizo mpya ni za watoto za mseto ( RHZ/RH) zilizoboreshwa na  tayari zimeshawasili nchini na tumeanza kuzisambaza kwenda Mikoani na Halmashauri zote nchini.

# Nawaagiza waganga wafawidhi wote wa hospitali na vituo vya huduma kuhakikisha watoto wote wanaoanza shule za bweni wanafanyiwa uchunguzi wa TB kikamilifu kabla ya  kuanza masomo.

#Ni marufuku kwa Madaktari  kujaza fomu za uchunguzi wa Afya bila kupima wanafunzi husika. Kufanya hivyo ni kuliangamiza kwa makusudi Taifa  kwa uzembe ambao hauwezi kuvumilika.

# Serikali inatambua umuhimu wa ushirikishwaji wa jamii katika mapambano ya kutokomeza TB.

#Mpaka sasa takribani watoa huduma1530 kati ya 5000 katika ngazi ya jamii ambao wamepata mafunzo ya muda mfupi ya Kifua Kikuu wanawezeshwa ili kuibua wagonjwa wa TB na kuwafuatilia watoto wanaopata matibabu katika maeneo yao.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya March 24

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images