Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ni Dr. Chief Malunde Pekee Anaetibu Nguvu Za Kiume Na Kumtuliza Umpendae Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
"NI DR. CHIEF MALUNDE PEKEE ANAETIBU NGUVU ZA KIUME NA KUMTULIZA UMPENDAE KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI"
-baada ya kujichimbia katika nchi za kiarabu kwa zaidi ya miaka (10)sasa amewasili nchini na dawa za tiba asilia.
 
1/NGOLO 3 POWER-ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, ina ubora wa hali ya juu wa kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wasiojiweza kufanya tendo la ndoa, inaimarisha misuli iliyolegea na kusinyaa, inarutubisha mbegu za kiume na kukufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15-25 kuwa na hamu na tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila kuchoka, inarefusha uume inchi 5-8 na kunenepesha hadi cm 4 kwa wenye maumbile madogo, dawa hii imeboreshwa na hutibu matatizo haya kwa muda mfupi tu.
 
2/MAGOYE MVUTO- dawa hii ina uwezo mkubwa sana kumvuta na kumtuliza aliekuacha awe mpenzi, mme/mke itamfanya akutafute mwenyewe ndani ya masaa 3tu na kukutimizia mahitaji yako kwa haraka na kumfunga asiwe na mtu mwingine.
 
3/SUPER LUBEJA- ni dawa ya kushepu umbo no.8 mguu wa bia, kuongeza hips, na makalio kwa muda wa siku 5tu unapata saizi uipendayo, kuondoa makovu, chunusi, harufu mbaya ya mwili michirizi, kupunguza tumbo na maziwa kwa siku 6tu.
 
4/NG'WESHI MIX- ni dawa ya biashara ya kupata wateja wengi, kusafisha nyota, kurudishwa kazini na kupandishwa cheo, kurudisha mali iliyoibiwa au kudhurumiwa.
 
PIA TUNATIBU MAGONJWA SUGU KAMA: vidonda vya tumbo, ngiri, chango na uzazi kwa kina mama: (dawa zote hazina madhara kwa mtumiaji) HUDUMA HIZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO: TUNAPATIKANA DSM BUGURUNI SHELI AU PIGA SIM NO_ 0763-181099.

Okoa Ndoa Yako, Biashara Yako, Kazi Yak,o Mpenzi Wako..... Onana Na Dr Mfaume Mzee Mwenye Uwezo Wa Kukutatulia Magonjwa Na Matatizo

$
0
0
Je unaupungufu wa nguvu za kiume au maumbile madogo ya kiume?

 SHAFTI POWER; ni dawa itokanayo na mizizi na magamba ya mitishamba. Hutibu matatizo matatu kwa pamoja
 1 kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka 
2 kuwahi kufika kileleni kabla ya mpenzi au mke wako
3 kulegea kwa misuli na uume kusinyaa na mda mwingi uume kuanguka ukiwa bado unaendelea na tendo, DAWA HII ITAKUPA UWEZO WA KURUDIA TENDO ZAIDI YA MARA TATU NA UTACHELEWA KUFIKA KILELENI

MWIMALA MIX NO 2 ;ni dawa ambayo hurefusha uume saiz upendayo ...inch 5 , 6,7,8 na unene sm 1-5 .Dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hadhina madhara yoyote

NINI KINACHOCHANGIA KUWA NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO?
 1 kufanyia tohara ukiwa na umri mkubwa
3 msongo wa mawazo 
4 ngiri na korodani kuvimba 
5 vidonda vya tumbo 
6 maumivu ya mgongo na kiuno 
7 mfumo wa mahisha 
8 presha, kisukali na magonjwa ya moyo 

TUNATO TIBA YA KISUKALI,KORODANI KUVIMBA VIDONDA VYA TUMBO UZAZI KWA WANAWAKE NA WAUME .Tunarudisha Mali iliyoibiwa, kudhibiti jini chuma ulete kwa wanaopata pesa na ujui ziendako.
 
KWA SHIDA NA MAGONJWA WASILIANA NAMI .Ofisi ipo mbagara Zakhemu .Kwa wateja wa mikoani mtatumiwa huduma utakayo pia tunatibu kwa njia ya simu au piga simu no 0789234653 .WOTE MNAKARIBISHWA

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Kilichoendelea LEO baada ya IGP, AG na DCI kuitwa Mahakamani Kesi ya Nondo

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imepanga Aprili 4, 2018 kusikiliza maombi ya Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSGN), Abdul Nondo.

Nondo ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Iringa.

Uamuzi huo umetolewa leo Machi 21, 2018 na  Jaji  Rehema Samuje wakati shauri hilo lilipofikishwa mahakama hapo kwa ajili ya kutajwa.

Hatua hiyo inatokana na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu(THRDC), Kituo  cha Sheria na Haki   za Binadamu(LHRC) na Mtandao wa Wanafunzi Tanzania(TSNP) kuomba mambo matatu ikiwemo Nondo kupewa dhamana.

Jaji Sameja ameutaka upande wa Jamhuri kujibu hoja za utetezi dhidi ya Nondo, Machi 26, 2018.

“Kesi ya msingi itakuja kusikilizwa April 4 lakini upande wa Jamhuri mnatakiwa kuja kujibu hoja za upande wa wawasishaji maombi,” alisema Jaji Sameja.

“Pia upande wa wawasilishaji maombi mnapaswa kuwasilisha maombi ya nyongeza Machi 27, mwaka huu.”

Machi 19, 2018 THRDC, LHRC na TSNP  waliwasilisha maombi namba 49, 2018  Mahakama Kuu kutaka itoe amri kwa Jeshi la Polisi kumpeleka mahakamani Nondo.

Wakili wa Nondo, Jebra Kambole  amedai maombi hayo yalifunguliwa dhidi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo wapeleka maombi wanaiomba mahakama kutoa amri ya kuletwa mahakamani kwa mwanafunzi Nondo au kumuachia kwa dhamana kwani ameshikiliwa na polisi kwa muda mrefu bila sababu za msingi kutolewa.

Hata hivyo, kwa sasa Nondo amenyimwa dhamana na mahakama mjini Iringa ambayo inataka kujiridhisha na usalama wake.

TANGA RAHA- Sehemu ya Thelathini na Sita ( 36 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

“Hujui kuwa wewe ndio chanzo cha haya yote”
Nikabaki nikiwa ninamtazama Rahma huku nikikosa la kunzungumza na sikjua nimwambie nini juu ya kitu anacho dai mimi ni chanzo

ENDELEA
“Rahma unaposema kuwa mimi ni chanzo sijakuelewa una maana gani?”
“Eddy tambua ya kuwa kila ulilolkuwa ukilifanya haya ndio matokeo yake”
Moja kwa moja nikaanza kuhisi Rahma ameingundua tabia yangu ya zamani,ikanibidi niibadilishe mada kuepukana na mizozo ya kelele.
“Fanya basi upike msosi baby ninanjaa?”
“Sawa mume wangu ila hiyo mada tutazungumza baadaye vizuri”

“Mume wangu unanichekesha sana”
Rahma alizungumza nyuma yangu na kunifanya nigeuke na kumtazama
“Kwa nini?”
“Kwa maana wewe unajing’ang’aniza kupanda juu ya huo mti wakti unauona ni mkubwa na tangu kule ndani niliikuwa nikikuangalia jinsi unavyo paramia parami”Rahma alizungumza huku akicheka

“Kinacho kuchekesha wewe haswa ni nini?”
“Ninakucheka wewe unaye nga’angana kuapanda hapo”
Nikamtazama Rahma kwa macho ya umakini na kujikuta nikiachia msunyo ulio mnyamazisha kuchela
“Baby jamani mbona unanisunya?”
“Nenda ndani kaniletee maji ya kunywa”
“Sawa mume wangu au umechukia nilivyo kucheka?”
“Hapana”
Rahma akanisogelea na kunibusu shavuni na kuondoka kwa mwendo wa madoido,Sehemu niliyo simama nikaanza kuhisi mtetemeko ulio nifanya nitazame chini kwa muda.Nikajaribu kupakanyaga nikasikia mlio unao ashiria chini yangu kuna shimo.Nikaanza kuyasogeza majani mengi ya mti yaliyo kauka na nikakuta mfuniko ulio tengenezwa kwa chuma na niimara sana na juu yake ukiwa na mnyororo chakavu ulio unganika kwa pamoja

“Kuna nini hapo?”
Rahma aliniuliza huku akiwa ameshika jagi lenye maji pamoja na kikombe
“Humu ndani sijui kuna nini,ila ninahisi kuna viu muhimu sana”
“Mmmmm hembu”
Rahma akapiga hatua hadi sehemu niliyopo mimi na akanyaga mfuniko kama nilivyo ukanyaga mimi kwa kutumia mguu kisha akanitazama machoni.
“Baby iseje kukawa na madudu ya ajabu ikala kwetu?”
“Madudu gani?”
“Madudu tuu ya ovyo ovyo”
“Hakuna kitu.....Fanya hivi nenda kule jikoni kalete kile kijishoka kilicho ning’inizwa pale ukutani"
“Sawa”

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 53 na 54 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA   
ILIPOISHIA 
Monica akaondoka na kuingia jikoni, nikachukua simu na kumpigia mama.
“Nimeipata”      
“Ok kuna video ninakutumia, ipitie kisha uniambie tuisambaze au laa”
“Sawa mama unaitumia kwenye nini?”
“Kwenye emal yako”
“Ok”
Nikakata simu, kwa bahati nzuri hii sehemu kuna huduma ya inteenet ya bure, hazikupita hata dakika mbili email kutoka kwa mama ikaingia, nikaifungua email hiyo kisha video hiyo. Video hii inaonyesha K2 akiwa katika moja ya jengo kubwa ambapo humo ndani kuna kiwanda cha kutengeneza madawa ya kulevya jambo lililo nifanya nibaki nimeduwaa nisijue ni nini cha kufanya.
  
ENDELEA
Ikanibidi kuirudia tena video hii aliyo nitumia mama ambayo inaonyesha kama imerekodiwa na simu kwa maana mrekodiji mwenyewe mikono yake inacheza cheza. Uzuri wa mchukuaji video hiyo aliweza kuivuta sura K2 karibu sana.
Monica akarudi sebleni akiwa ameshika sahani yenye vipande vya kuku, akaviweka mezani huku akiitazama video hiyo.

“Huy…u si ndio yule aliye kuja kutuvamia na watu wake?”
“Ndio yeye”
“Hembu”
Monica akaigeuzia Laptop upande wake na kuitazama vizuri video hiyo, nikamuona anavyo shusha pumzi nyingi huku akinitazama usoni mwangu.
“Sasa hii video s uisambaze kwenye mitandao ajulikane kwamba yeye ni adui wa hii nchi kwa maana huu n unga kabisa wa kuvuta”
“Bado mapema, nahitaji ateseke kidogo kidogo hadi kufa kwake”
“Ila Dany hapo utakuwa unakosea, tazama maisha yetu kwa sasa yanavyo andamwa, afadhali mimi ninanafuu, wewe kila muda unatangaza kwenye vituo vya habari”
“Nimekuambia ninajua ni nini cha kufanya sawa”
Nilizungumza kwa ukali huku nikiifunga Laptop na Monica akatulia tuli. Ukimya ukatawala ndani ya chumba huku nikijaribu kuumiza akili juu ya kulipiza kisasi changu kwa K2 pamoja na kaka yake ambaye ndio raisi wa hii nchi. Monica akachukua kipande cha paja la kuku na kunilisha, sikuona hata ladha ya nyama hiyo japo ameipika vizuri sana.
“Usiku wa saa mbil tunaeleka Dar”
“Dar!!”
“Ndio, panga nguo zako na tunaondoka kama utakuwa tayari kuandamana na mimi katika hili”
“Sawa mimi sina tatizo”

Nikanyanyuka kwenye sofa na kuigia kwenye chumba, nikakisogelea kioo kilichopo humu ndani nikajitazama kuanzia chini hadi juu, nikatazama nguo za Monica alizo zimwaga kitandani pamoja na mawigi. Nikachukua moja ya gauni na kujipimisha kipimo cha mwili wangu, nikaona linananitosha.
“Ehee na hilo gauni unataka kufanya nini?”
“Nahitaji kulivaa, nataka uniweke na hili wigi”
“Hahahaaa Mungu wangu, Dany hembu acha vituko vyako”
“Vituko vya nini sasa, nahitaji kubadilika muonekano niwe mtoto wa kike, kuna watu wangu kupitia muonekano huu nitaweza kuwapata”
“Mmmm hembu livae nikuone”
Nikavua nguo zangu na kubakiwa na tisheti pamoja na boksa, nikalivaa gauni hil jeusi lililo jaa vimetometo vya dhahabu.
“Waoooo it’s so amaizing”
Monica alizungumza huku akinisogelea, akanifunga zipu kwa nyuma, kwa jinsi nilivyo nyoa upara na ndevu si rahisi mara moja kwa mtu kunigundua kwamba mimi ni mwanaume pale nitakapo vaa wigi.

==>Endelea Nayo <<Kwa Kubofya Hapa>>

Masogange augua siku ya kusomewa hukumu ya kesi inayomkabili

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeshindwa kumsomea hukumu msanii Agnes Gerald maarufu kama Masogange anayekabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya kwa sababu anaumwa, amewekewa dripu na hawezi kutembea.

Hukumu hiyo ilitarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri mara baada ya upande wa mashtaka ukiwakilishwa na Wakili wa Serikali, Costantine Kakula kuwaita mashahidi watatu kutoa ushahidi dhidi ya Masogange na kuufunga na mshtakiwa mwenyewe kujitetea.

Ilipofika saa 3:46 asubuhi leo Jumatano Machi 21, 2018 kesi hiyo iliitwa kwa Hakimu Mashauri na wakili wa Serikali, Adolf Mkini alieleza kuwa kesi ilipangwa kwa ajili ya hukumu ila mshtakiwa Masogange anayewakilishwa na wakili Ruben Simwanza hakuwapo.

Hata hivyo, mdhamini wa Masogange ambaye hakutaja jina lake alisimama na kuiambia mahakama kuwa Masogange hakufika mahakamani kwa sababu anaumwa na akawasilisha nakala za vyeti vya hospitali mahakamani hapo.

Mdhamini huyo amedai kuwa Masogange amewekewa dripu na hawezi hata kutembea.

Kutokana na hali hiyo Mkini ameiomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya hukumu. Hukumu itasomwa Aprili 3, 2018. Wakili mwingine anayemtetea Masogange ni Nehemiah Nkoko.

Masogange wakati akijitetea katika kesi hiyo aliiomba mahakama imuachie huru kwa sababu hana kosa lolote.

Masogange  ambaye anakabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam, katika utetezi wake amedai kuwa yeye hajawahi kutumia dawa za kulevya hata siku moja.

Akijitetea Masogange meidai kuwa mbali ya kuwa msanii pia alikuwa ni mfanyabiashara wa nguo.

Masogange katika kesi hiyo  anadaiwa kuwa kati ya Februari 7 na 14, 2017 katika maeneo yasiyojulikana ndani ya jiji la Dar es Salaam alitumia dawa za kulevya aina ya Heroin (Diacety Imophine).

Pia anadaiwa kuwa kati ya Februari 7 na 14, 2017 alitumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam.

Waziri Mkuu Amuwaklisha Raisi John Magufuli Katika Mkutano Wa AU Rwanda

$
0
0
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa leo amemwakilisha Rais John Magufuli katika sherehe za kusaini mkataba wa kulifanya Bara la Afrika kuwa eneo huru la biashara jijini Kigali, Rwanda.

Tanzania ni miongoni mwa nchi zaidi ya 50 ziilizosaini mkataba huo, ambao umeelezwa utaongeza chachu kwa Afrika kuimarika kiuchumi.

Mkataba huo umesainiwa baada ya kukamilika kwa kamati za wataalamu zilizoshirikisha pia mawaziri wa biashara na mambo ya nje wa nchi washirika.

Mbali na mkataba huo, marais hao pamoja na wawakilishi wa nchi washirika wamesaini Itifaki ya utekelezaji wa makubaliano hayo ambayo yanatoa uhuru wa makazi, kutembea, haki ya kuishi na kufanyakazi popote Afika bila vikwazo wala vizuizi sambamba na Tamko la Kigali.

Sherehe hizo pia zimehudhuriwa na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi na Mwenyekiti wa CEO Round Table, Ally Mufuruki ambaye jana alikuwa miongoni mwa wazungumzaji katika mjadala wa uchumi na biashara.

TCRA, Mwakyembe Wamkabili Diamond

$
0
0
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kamati yake ya maudhui inafuatilia mahojiano ya mwanamuziki Nasseb Abdul maarufu Diamond aliyoyafanya katika kituo cha Redio cha Times jijini Dar es Salaam.

 Ofisa Mkuu Idara ya Utangazaji ya mamlaka hiyo, Andrew Kisaka amesema wamechukua uamuzi huo kwa kuwa mahojiano hayo yamefanyika katika kituo wanachokisimamia.

Katika mahojiano hayo, Diamond alimjibu Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza kutokana na Serikali kuzifungia nyimbo 15 mwezi uliopita, zikiwemo mbili za mwanamuziki huyo.

Kisaka amefafanua kuwa kiutaratibu wao wanaangalia zaidi chombo ambacho wamekipa leseni na kwamba, masuala mengine yatashughulikiwa na mamlaka nyingine.

Amesema suala hilo kwa sasa linafanyiwa kazi na kamati ya maudhui na kuahidi kulitolea ufafanuzi siku za hivi karibuni akiwataka wananchi kuwa na subira.

Wakati TCRA ikisema hivyo, Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amesema amesikitishwa na matamshi ya Diamond kuhusu kufungiwa kwa nyimbo hizo aliyoyatoa katika kipindi hicho.
 
“Maamuzi ya kuzifungia baadhi ya nyimbo za wasanii wawili kwa kukiuka maadili yalifanywa kwa mujibu wa sheria na si kwa utashi binafsi wa Shonza ambaye analaumiwa na Diamond,” amesema.

“Diamond atambue kuwa Serikali ina taratibu zake na maamuzi ya naibu waziri ni ya wizara. Kama vikao na wasanii tumefanya vingi sana, lakini Diamond hakuwahi kuhudhuria vikao hivyo, si wajibu wa Serikali kumfanyia kikao cha peke yake.”

Amesisitiza, “Sheria ni ya watu wote bila kujali umaarufu au nafasi ya mtu katika jamii, hivyo msanii Diamond anapaswa kutii sheria na mamlaka zilizowekwa.”

Dk Mwakyembe ameeleza kuwa sio busara kwa Diamond  kushindana na Serikali na endapo ana ushauri wowote ni vyema akawasilisha kwa njia sahihi, lakini si kumshambulia naibu waziri kwa dharau na kejeli kama alivyofanya.

“Diamond kwa mafanikio aliyoyapata katika muziki, anatarajiwa kuwa mfano bora kwa wanamuziki wenzake. Napenda kuwakumbusha wasanii wote kwamba sanaa ni kazi kama zilivyo kazi nyingine,” amesema.

“Pamoja na kuwa na kipaji hicho, wasanii wanatakiwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo inayosimamia tasnia ya sanaa kama ilivyo kwa tasnia nyingine.”

Polisi yamshikilia dereva tukio la mhasibu ubalozi Syria kujeruhiwa

$
0
0
Polisi Mkoa wa Kinondoni wanamshikilia mfanyakazi wa ubalozi wa Syria  nchini kwa tuhuma za kumjeruhi usoni mhasibu wa ubalozi huo,  Hassan Alfaouri na kumpora Euro 93,000 (Sh237milioni).

Akizungumza leo Jumatano Machi 21, 2018 kamanda wa polisi mkoani humo, Jumanne Muliro amesema tukio hilo lilitokea Machi 19, 2018 saa nane mchana eneo la Shule ya Msingi Oysterbay, jijini Dar es Salaam.

Amesema siku hiyo, mhasibu huyo akiwa katika gari na dereva wake wakielekea Benki ya Azania tawi la Mazdu House lililopo mtaa wa Samora wakipeleka fedha hizo, walipofika mtaa wa Zambia dereva huyo alianza kuendesha gari taratibu.

Amesema baada ya kupunguza mwendo, alisimama  na kuzima gari ghafla walitokea watu watatu; mmoja kati yao alikuwa na kipande cha nondo mkononi  na kuingia katika gari hilo na kumtaka mhasibu huyo awape fedha.

Muliro amebainisha kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa tukio hilo lilipangwa na baadhi ya wafanyakazi wa ubalozi wasio waaminifu, akiwamo dereva huyo ambaye wakati uporaji ukiendelea, hakutoa msaada wowote.

"Walivyoona anakawia kutoa fedha walimjeruhi usoni kwa kipande cha nondo, walimshusha dereva kwa nguvu na kuondoka na gari hilo,” amesema.

Amesema baada ya tukio hilo, polisi walianza msako  na kuikuta gari hiyo ikiwa imetelekezwa Msasani Bonde la Mpunga.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi yya Marchh 22

Waziri Ummy Awashauri Wananchi Kwenda Vituo Vya Tiba Haraka Pindi Wanapogundua Dalili Za Ugonjwa Wa Dengue

$
0
0
NA WAMJW-DAR ES SALAAM.
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amewashauri wananchi kwenda vituo vya tiba haraka mara baada ya kugundua kuwa wana dalili za ugonjwa wa dengue.

Hayo ameyasema wakati alipotoa tamko juu ya kuingia kwa ugonjwa wa dengue hapa nchini mara baada ya kufunga Mkutano wa 65 wa Jumuiya ya Mawaziri wa Afya wa Nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini ECSA jana  jijini Dar es salaam.

“Kuna dalili za Ugonjwa Dengue zikiwemo homa ya ghafla, kuumwa kichwa hususan sehemu za macho, maumivu ya viungo na uchovu. Dalili hizi huanza kujitokeza kati ya siku 3 hadi 14 tangu mtu alipoambukizwa virusi vya homa ya Dengue hivyo Wizara inashauri kuwa wananchi wasiwe na hofu, bali mara tu wanapoona dalili za ugonjwa waende katika vituo vya tiba " alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Wakati mwingine dalili za ugonjwa huu zinaweza kufanana sana na dalili za malaria hivyo basi wananchi wanaaswa kuwa, wakipata homa wahakikishe kuwa wanapima ili kugundua kama wana vimelea vya malaria au Dengue, au sababu nyingine, ili hatua stahiki zichukuliwe.

Waziri Ummy amesema kuwa ili kujikinga na ugonjwa huo ni lazima Kuangamiza mazalio ya mbu kwa kufukia madimbwi ya maji yaliyotuama au nyunyuzia dawa ya kuua viluwiluwi vya mbu kwenye madimbwi hayo pamoja na Kujikinga na kuumwa na mbu kwa  kuvaa nguo ndefu muda wote hasa nyakati za mchana.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Wizara itaendelea Kuimarisha ufuatiliaji wa magonjwa nchi nzima kwa kutumia mfumo uliopo wa ukusanyaji wa taarifa (IDSR), ambapo tunaendelea kupata taarifa za kila siku juu ya mwenendo wa ugonjwa huu na Kutoa elimu kwa jamii kupitia vyombo vya habari.

Mbali na hayo Waziri Ummy amesisitiza kuwa  hakuna vikwazo vyovyote vilivyowekwa kwa ajili ya wasafiri wanaoingia na wanaotoka nchini na  Wizara itaendelea kushirikiana na wadau na sekta mbalimbali katika kufuatilia na kudhibiti ugonjwa huo.

Homa ya Dengue ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyoenezwa na mbu wa aina ya Aedes ambao ni weusi wenye madoa madoa meupe yenye kung’aa.

Amber Lulu: Simpendi Baba Yangu Hata KIdogo Na Wala Sitaki Kumuona

$
0
0
Video vixen maarufu aliyegeukia sanaa ya Bongo fleva Amber Lulu amekiri kuwa amemtosa Baba yake mzazi na hataki hata kumuona.

Amber Lulu amefunguka hayo wakati anaelezea changamoto alizozipitia katika maisha yake baada ya Baba yake mzazi kuwakimbia na kumuacha yeye kama mtu pekee ambaye alitakiwa kuiangalia familia yake hasa mama yake ambaye alikuwa mgonjwa.

Amber Lulu ameongelea uhusiano aliokuwa nao na Baba yake mzazi ambapo amekiri katika umri mdogo alianza kushika majukumu mazito ya kuielea familia yake hivyo ilimbidi ajiingize katika biashara mbali mbali ili aweze kupata pesa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Clouds Fm, Amber Lulu aliongea haya kuhusiana na changamoto alizozipitia:

"Kipindi hiko nilikuwa bado niko shule lakini ilikuwa likizo hata ya wiki mbili nilikuwa nakuja Dar kufanya kazi maana tulikuwa tunahitaji pesa na mama Yangu alikuwa mgonjwa na ndio baba alikuwa kashatukimbia, nakumbuka msanii alikuwa anaitwa Pasha alinitumia kwenye video yake akanilipa shilingi elfu hamsini ambayo sikutumia hata senti nikaenda kumpa Mama yangu ambaye alikuwa anahitaji lakin moja na nusu ya matibabu”.

Lakini Pia Amber Lulu ameongelea uhusiano wake na Baba yake mzazi ambaye alimkimbia:

"Wanasema mzazi ni mzazi lakini mimi Baba yangu alinitelekeza kaja kunitafuta nilivyotoa wimbo wangu wa Watakoma alafu ananiomba hela kusema kweli aliniumiza kwa sababu hajanitafuta kama miaka kumi halafu anakuja kunitafuta kwa sababu anataka hela , dah kusema ukweli simpendi baba yangu hata kidogo na sitaki hata kumuona”

Fatma Karume Ajitosa Kumrithi Tundu Lissu Urais TLS

$
0
0
Wakili wa kujitegemea, Fatma Karume amejitosa kumrithi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kwa kugombea urais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), utakaofanyika Aprili 14, mwaka huu.

Lissu, ambaye aliteuliwa kugombea nafasi hiyo lakini ameshindwa kukidhi matakwa ya kamati kutokana na fomu ya uteuzi iliyowasilishwa kwa sekretarieti hiyo.

Kwa mujibu wa sheria mpya, Lissu hataweza kugombea tena nafasi hiyo kwani kifungu cha nane cha sheria hiyo, kinamzuia mtu ambaye ni kiongozi wa chama chochote  cha siasa, kuongoza chama hicho.

Katika kinyang’anyiro hicho, Fatma atachuana na Godwin Mwapongo, Godfrey Wasonga na Godwin Ngwilimi huku nafasi ya umakamu wa rais ikiwa na mgombea pekee, Rugemeleza Nshalla na Mweka Hazina akiwa Sadock Magai.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi wa chama hicho, Dk. Kibuta Ongwamuhana, uchaguzi wa rais utatanguliwa na viongozi wa kanda utakaofanyika kila mkoa kuanzia Machi 27, mwaka huu.

Wakizungumzia uchaguzi huo baadhi ya mawakili wamesema wanamtabiria Fatma ushindi wa kishindo kutokana na kuwa na kariba inayofanana na Lissu.

“Fatma atashinda kwa sababu anapenda mtu mwenye ‘tension’ na ni mtu mwenye kujiamini anaweza akaitetemesha serikali na wanasheria wanapenda hivyo,” amesema mawakili wa kujitegemea ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Wakili mwingine alisema ingawa sheria hiyo inamkataza Lissu kugombea ambapo walipanga kumchagua tena mwaka huu lakini Fatma anaweza kuziba pengo la Lissu.

Ajali Ya Lori Yaua 7 Kigoma

$
0
0
Watu saba wamefariki dunia katika ajali ya gari aina ya Scania iliyotokea katika Kijiji cha Mkongoro, Barabara ya Manyovu Wilaya ya Kigoma Vijijini.

Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, Martin Otieno amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni dereva kushindwa kuimudu gari kwenye mteremko.

Amesema ajali hiyo imetokea jana Jumatano Machi 21, saa tatu asubuhi katika Mlima wa Kasagamba ambapo lori lenye namba T741AAB  lilianguka na kusababisha vifo vya watu saba akiwamo dereva wa gari hiyo aliyefahamika kwa jina la Siri Hamis (43) mkazi wa Singida pamoja na utingo wake aliyefahamika kama Ramadhani Saidi (23).

“Katika gari hiyo walikuwa wamebeba mizigo na watu wanne mmoja mwanamke na watatu wanamume ambapo wengine waliofariki na majina yao hayakufahamika mara moja.

“Ajali hiyo pia imesababisha kifo cha mwanafunzi aliyefahamika kwa jina la Eliakimu Samsoni (15 ), aliyekuwa akitembea kwa miguu kuelekea shuleni na gari hilo kumgonga akiwa anatembea,” amesema Kamanda Otieno.

Boko Haram yawaachia huru wanafunzi wa kike Nigeria

$
0
0
Serikali ya Nigeria imethibitisha kuwa wengi kati ya wanafunzi wa kike 110 waliokuwa wametekwa na kikundi cha Boko Haram zaidi ya mwezi mmoja uliopita wameachiwa Jumatano asubuhi.

Shirika la habari la AFP limeripoti kuwa wasichana hao waliletwa katika mji wa Dapchi ulioko upande wa Kaskazini mwa Nigeria wa Jimbo la Yobe baada ya wale waliokuwa wanawashikilia kuwarejesha katika msafara ulioandamana na magari 9.

Ripoti za vyombo vya habari zimesema wasichana watano kati ya hao walikufa wakati wakisafirishwa, lakini afisa wa serikali wa jimbo la Yobe amesema hili bado halijaweza kuthibitishwa.

Waziri wa Habari wa Nigeria Lai Mohammed amesema kuachiwa kwa wasichana hao mapema asubuhi “bila masharti” kulitokana na “juhudi za kisiri” zikisaidiwa na “baadhi ya marafiki wa nchi hiyo.”

“Wasichana 91 na mvulana mmoja wameelezewa kuwa wameachiwa. Hayo ndio yaliyojiri,” amewaabia waandishi.

“Wengi kati ya wasichana hao, wengi wa wanafunzi hao walioachiwa huru hawakuletwa wote sehemu moja. Waliachwa njiani na wao wenyewe walirudi majumbani kwa wazazi wao.

Vyanzo vya habari nchini Nigeria vimetoa habari kuwa wakazi wa eneo la Dapchi walikuwa wanafurahia kuachiwa kwa watoto hao.

Wazazi ambao hapo awali walikuwa wanamsiba kwa kutekwa kwa vijana wao hivi sasa wanasheherekea kurudi kwao.

Mbowe Atoa Waraka: Kuna Njama Kubwa Imepangwa Dhidi Yetu

$
0
0
Waraka Maalum wa Freeman Aikaeli Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa Hai kwa Taifa

Leo tarehe 22 Machi 2018, mimi na viongozi wenzangu waandamizi wa Chadema tumetakiwa tena kuripoti Polisi.

Tunaokabiliwa na usumbufu huu ni pamoja na: Mhe Vincent Mashinji (Katibu Mkuu), Mhe. John John Mnyika, Mb na Naibu Katibu Mkuu Bara, Mhe. Salum Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu, Zanzibar; Mhe Halima J. Mdee, Mb, Mwenyekiti wa Bawacha, Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu, Mhe. John W. Heche, Mb, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Serengeti (Mara, Simiyu na Shinyanga) na Mjumbe wa Kamati Kuu; Mhe. Esther N. Matiko, Mb, Mwenyekiti wa Bawacha Mkoa wa Mara na Mweka hazina wa Bawacha Taifa.

Tuna taarifa pia ya kusudio la kumuunganisha Mhe. Peter Msigwa, Mb, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Nyasa (Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa) na Mjumbe wa Kamati Kuu katika shauri hili.

Historia ya wito:
Kwa muda wa wiki tano sasa, kufuatia sintofahamu kadhaa zilizojitokeza katika uchaguzi wa marudio wa Jimbo la Kinondoni, Dar es Salaam na Siha, Kilimanjaro, tumekuwa tukisumbuliwa kuripoti Polisi kila wiki kwa mashtaka ambayo hayajawahi kuwekwa bayana.

Katika kampeni na chaguzi hizi, palijitokeza mambo mengi ya ukiukwaji wa Haki za binadamu, ukiukwaji wa sheria za uchaguzi, matumizi mabaya ya madaraka ya kiserikali, udhalilishaji na unyanyapaa dhidi ya Vyama vya Upinzani, mauaji na mateso kwa viongozi wa vyama vya Upinzani na hata Wananchi wasio na hatia.

Wakati nenda rudi hii ikiendelea, tuna taarifa (asante teknolojia) kuwa zinapangwa njama mahususi za kutubambikia viongozi wa Chadema kesi za Mauaji au Uhaini ili kuhalalisha azma ya Watawala kutuweka mahabusu kwa muda mrefu, wakidhani kwa kufanya hivyo watakuwa wamefanikisha kufifisha na hata kuua kabisa uwepo wa Upinzani katika Taifa.

Jitihada hizo ni pamoja na kujaribu kuhusisha viongozi, wanachama na wapenzi wa chama chetu na tuhuma aidha za Kigaidi, Mauaji na hata Uhujumu wa Uchumi.

"Viongozi" hawa, wasaidizi na washirika wao wamejazana matumaini hewa kuwa vuguvugu la mabadiliko na uhitaji wa demokrasia ya kweli na vita dhidi ya udikteta katika taifa hili litazimwa kwa "kuwaficha, kuwapoteza na hata kuwaua" viongozi wa Chadema na wanaharakati wengine wanaoamini katika uhalisia huu.

Naam, njama hizi zaweza kuua baadhi, kujeruhi baadhi na hata kupoteza kadhaa! Lakini kamwe, hazitazima njozi za Watanzania wema kupigania haki na ustawi katika nchi yao.

Naamini kwa kuzima uongozi wa Chadema uliopo leo, siyo tu kutaruhusu kuchipua kwa kasi kwa uongozi mbadala, bali pia kutaamsha ari ya taifa kuongeza juhudi katika harakati ili hatimaye kutokomeza  uongozi wa kiimla katika nchi yetu.

Taifa lina msiba! Wanasiasa, wanaharakati, wanahabari na hata wasanii wanateswa, wanafungwa, wanajeruhiwa na wengine kuuwawa! Wafanyabiashara na wawekezaji wa ndani na nje wanalia! Viongozi wa dini wanachanganyikiwa! Wakulima, wafugaji na wavuvi wako hoi! Hata watoto na wanafunzi nao ni tishio kwa watawala!

Taifa limejazwa hofu. Wengi hawasemi, lakini wanataabika rohoni. Wanaisubiri fursa iwavyo vyovyote vile.

Nguvu, majeshi na silaha zao, magereza na mifumo kandamizi haziwezi kuwa suluhu ya uimla huu. Tuimarishwe badala ya kufifishwa.

Hatukimbii!! Tuko tayari kwa lolote, popote!

Shime Watanzania! Msitulilie! Lilieni watoto wenu na Taifa la kesho.

Na iwe vyovyote iwavyo! Damu, mateso, dhihaka dhidi ya maisha yetu iwe chachu ya dhati katika kutafuta Tanzania aliyoikusudia Mwenyezi Mungu yenye kusimamia haki, demokrasia, usawa, utu na ustawi kwa wote!!

Aluta Continua!!!
Freeman Aikaeli Mbowe

Roma: BASATA Nipunguzieni Adhabu Mtaniua Njaa

$
0
0
Siku chache baada ya Naibu Waziri wa Habari Sanaa, Michezo na Utamaduni, Juliana Shonza kusema wasanii waliofungiwa nyimbo zao wanatakiwa kufuata taratibu kama wana malalamiko, msanii wa Bongo Fleva, Ibrahim Musa maarufu  Roma Mkatoliki amesema alifuata taratibu hizo lakini amegonga mwamba.

Roma ameyasema hayo jana Jumatano Machi 21, 2018  katika mahojiano na kipindi cha XXL kinachorushwa na kituo cha Radio Clouds, akidai kuwa  adhabu ya kufungiwa miezi sita inamuumiza na kuomba apunguziwe au kutozwa faini ili yaishe.

Machi 1, 2018  Shonza alimfungia Roma Mkatoliki kutojihusisha na tasnia ya muziki kwa kipindi cha miezi sita na kwamba msanii huyo alipopewa muda wa kurekebisha wimbo wake wa Kibamia, ameshindwa kutekeleza agizo hilo.

Katika kipindi hicho, Roma amesema tangu siku alipofungiwa alijitahidi kufanya taratibu za kumuona naibu waziri huyo kama ambavyo alitaka, ikiwemo kufunga safari hadi ofisini kwake lakini  hakufanikiwa.

Amebainisha kuwa amefungiwa wakati tayari ana shoo za kufanya na alishachukua fedha, ikiwemo  shoo ya Kili Marathon ambayo baadaye alitakiwa kurejesha fedha hizo.

 “Shoo ya Kili Marathon mimi na Stamina kupitia kundi letu la Rostam tulikuwa tumelipwa vizuri, lakini juhudi za kufanikisha ziligonga mwamba hata kwa kuomba barua kidogo ya utambulisho. Mambo kama haya yanatuharibia kuaminika tena kwa kampuni ambazo zinatupa kazi,” amesema.

Kuhusu kumuona naibu waziri  amesema, “Siku moja nilitoka hospitali nikampitia rafiki yangu Madee na Askofu nikawaambia twendeni tukamuone mheshimiwa lakini mimi sikupewa ruhusa ya kumuona. Wengine wote walipewa ruhusa, basi nikawatuma wao wafikishe ujumbe kwa sababu niliogopa kulazimisha kwa kuwa ningeonekana nafanya fujo.”

Amesema alitakiwa kupewa muda kabla ya hatua iliyochukuliwa kuliko kudhaniwa kuwa anakaidi agizo la kutakiwa kuripoti ofisi za Baraza la Sanaa la Taifa (Basata).

“Walitakiwa kujua kuwa nilikuwa na udhuru na pia hiyo ilikuwa ni mara yangu ya kwanza,” amesema na kubainisha kuwa hata kama alipigiwa simu, aliogopa kupokea kwa sababu ya uoga alionao tangu alipotekwa na watu wasiojulikana mwaka jana.

“Inaonekana Roma hajafanya kitu chochote tangu litokee jambo hilo lakini ambacho mimi sijafanya ni kuja kwenye media kusema leo nimeandika barua au vipi? Sikupewa barua kwa wakati ule nilipewa ujumbe tena kwa namba ngeni.”

Download Upya Application Yetu Ya mpekuzi .....Ile Ya Zamani Tutaifuta

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya Mpekuzi Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Maboresho Mapya Yamefanyika ili kukufanya upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile Magazeti kuliko ilivyo sasa.

App ya zamani ilikuwa na tatizo kubwa la kuchelewa kufunguka, kuchelewesha habari na muonekano wake haukuwa wa kiwango kinachostahili.

Chakufanya, Ingia PlayStore, Download Upya Application yetu  MPYA. Ukishaipakua hii Mpya, ya zamani ifute tu.

NB: App mpya ina Icon ya Njano

Tumekurahisishia; 

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images