Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Okoa Ndoa Yako, Biashara Yako, Kazi Yak,o Mpenzi Wako..... Onana Na Dr Mfaume Mzee Mwenye Uwezo Wa Kukutatulia Magonjwa Na Matatizo

0
0
Je unaupungufu wa nguvu za kiume au maumbile madogo ya kiume?

 SHAFTI POWER; ni dawa itokanayo na mizizi na magamba ya mitishamba. Hutibu matatizo matatu kwa pamoja
 1 kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka 
2 kuwahi kufika kileleni kabla ya mpenzi au mke wako
3 kulegea kwa misuli na uume kusinyaa na mda mwingi uume kuanguka ukiwa bado unaendelea na tendo, DAWA HII ITAKUPA UWEZO WA KURUDIA TENDO ZAIDI YA MARA TATU NA UTACHELEWA KUFIKA KILELENI

MWIMALA MIX NO 2 ;ni dawa ambayo hurefusha uume saiz upendayo ...inch 5 , 6,7,8 na unene sm 1-5 .Dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hadhina madhara yoyote

NINI KINACHOCHANGIA KUWA NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO?
 1 kufanyia tohara ukiwa na umri mkubwa
3 msongo wa mawazo 
4 ngiri na korodani kuvimba 
5 vidonda vya tumbo 
6 maumivu ya mgongo na kiuno 
7 mfumo wa mahisha 
8 presha, kisukali na magonjwa ya moyo 

TUNATO TIBA YA KISUKALI,KORODANI KUVIMBA VIDONDA VYA TUMBO UZAZI KWA WANAWAKE NA WAUME .Tunarudisha Mali iliyoibiwa, kudhibiti jini chuma ulete kwa wanaopata pesa na ujui ziendako.
 
KWA SHIDA NA MAGONJWA WASILIANA NAMI .Ofisi ipo mbagara Zakhemu .Kwa wateja wa mikoani mtatumiwa huduma utakayo pia tunatibu kwa njia ya simu au piga simu no 0789234653 .WOTE MNAKARIBISHWA

Diamond Ajilipua......Amtumia Ujumbe Mzito Naibu Waziri Kwa Kuwafungia Wasanii

0
0
Msanii wa muziki Bongo, Diamond amefunguka kuhusu kufungiwa kwa nyimbo zake mbili ‘Waka na Hallelujah’ kwa kueleza kuwa ni kitu ambacho hakiwezi kumpunguzia chochote na hakiwezi kujenga muziki wa Tanzania.

Muimbaji huyo ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa yupo tayari kupigania muziki wake kwa lolote lile na iwapo kuna sehemu ambayo wao kama wasanii wanaenda kinyume ni jambo la kuelekezana.

“Suala si kufungia tu nyimbo, mimi ukinifungia nyimbo hainipunguzii kitu nikienda nje naenda nai-perform ukiwa hutaki sinaondoka tu naenda nchi nyingine, kwa hiyo ni kukaa tuzungumze, tuelekezane lakini tusifanye kama kukomoana, hapana, tufanye katika mazingira ambayo yatasaidia sanaa ikue." Alisema Diamond na kuongeza;

"Huwezi kumfungia mtu kama roma kwa miezi sita,unajua kuwa anachangamoto gani?umeshawahi kutaka kuzitatua?

"Unanifungia nyimbo zangu umeshawahi kuchangia nini katika muziki wangu , utamnunulia tiffah wewe pampers?

"Simuogopi mtu hata kaka jela mimi nitaenda kwa ajili ya kuukomboa muziki .ntaitetea bongo fleva kwa sababu naijua kuliko anavyoijua yeye anaetufungia , sio unakuja unafungia bila hata kufanya research, anakuja na atatuacha sisi hapa."

Diamond ambae anaonekana kujiamini kuwa hata iweje lazima atasimama kwa ajili ya bongo fleva, anasema kuwa wala hajali kwa sababu hajapata taarifa rasmi juu ya kufungiwa kwa nyimbo zake zaidi ya kuziona habari katika mitandao ya kijamii.

Rais Magufuli Awafumbua Macho Wafanyabiashara Nchini Kuhusu Fursa za Masoko ya Ndani

0
0
Rais John Magufuli amewatajia  wafanyabishara nchini mambo mawili muhimu akiwataka kutumia fursa za masoko ya ndani ili kukuza ajira na kupunguza uagizaji wa bidhaa kutoka nje.

Akizungumza  jana Jumatatu Machi 19, 2018 katika mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara Ikulu Dar es Salaam, Dk Magufuli alisema mfanyabiashara yeyote atakayekutana na vikwazo katika uwekezaji huo atoe taarifa mapema na atachukua hatua kwa mteule wake aliyehusika.

Alitoa mfano wa fursa ya kuzalisha sare za wanafunzi na majeshi nchini. 

“Tukisema kwa mfano sare zote za wanafunzi kuanzia darasa la kwanza hadi la saba, kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita zizalishwe na viwanda vyetu vya ndani au tukaanza kuzalisha viatu vya Jeshi, tutashindwa nini,”alisema Rais Magufuli.

Alisema Kiwanda cha Mwatex kitakapoanza kuzalisha sare hizo za wanafunzi, itasaidia kulinda soko la ndani, kuongeza uzalishaji wa zao la pamba na kukuza ajira kwa wakulima.

“Niwaambe Watanzania wenzangu tuwe wazalendo, tukifanya hivyo tutakuwa tumejibu hoja nyingi kwa wakati mmoja, atakayewakwamisha mniambie, mie si ndio mwenyekiti wenu? Ili kusudi nimwambie na yeye akajaribu kufanya biashara,”alisema.

Maongezi ya Rais Magufuli na Watendaji Wakuu Wa Kiwanda Cha Bia Tanzania Breweries Limited (TBL) Baada ya kukutana IKULU

TANGA RAHA- Sehemu ya Thelathini na Tano ( 35 )

0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA  

Taratibu nikafungua pazia la dirisha la sebleni na nusu nipoteze fahamu ila nikajikaza kuendelea kutazama.Kundi kubwa la watu wenye asili ya kijerumani wamewazunguka Rahma na jamaa mmoja wa kizungu huku Rahma akiwa amevalia shela la harusi huku na jamaa suti ya harusi na Rahma ameishika pete yangu aliyo itupa akitaka kumvalisha jamaa kwenye kidole kama nilicho kuwa nimekivaa mimi na nikazidi kuchanganyikiwa baada ya muongozaji wa harusi hiyo akiwa ni Olvia Hitler

ENDELEA
Taratibu nikalifunga pazia na kukaa kwenye kichi huku nikijiuliza ninacho kiona ni kwelia au ni ndoto,Kelele za ngoma zikanifanya niweze kuamini kama ni kweli kwa ujasiri mkubwa nikasimama na kuufungua mlango na kuwafanya watu wate waliopo kwenye eneo nje kunitazama kwa macho makali ambayo si ya kawaida kama ilivyo kwa sisi binadamu.Macho yao yametawaliwa na rangi ambazo si za kawaida kwa haraka haraka ninaweza kuzifananisha na mwanga wa moto wa gesi.

Rahma akabaki akinishangaa kama mtu asiye jitambua aliye kamatwa na bumbuazi kali,Nikaanza kupiga hatua mbili mbele na kuwafanya vijana wawili wa kijerumani kusimama mbele yangu na kunitazama kwa umakini kisha nao wakaanza kunisogela huku taratibu wakianza kubadilika maumbo yao kwa kutoka manyonya kama ya mbwa.Nikaanza kurudi nyuma kwa haraka na nikausukuma mlango ila kwa bahati mbaya nikaukuta mlango ukiwa umejifunga kwa ndani.

Jamaa wakazidi kunifwata na sikuwa na jinsi zaidi ya kaanza kupiga hatua za hakanyaga maua yaliyopo pembezoni mwa ukuta na kuanza kukimbia kuelekea sehemu yenye msitu,Vijana wa kijerumani naa wakanza kunikimbiza na kadri wanavyo kimbia ndivyo  miili yao ikabadilika na kuwa kama mbwa aina ya Bweha(FOX) na kuzidi kunikimbiza.Sikuwa na namna nyingine yoyote zaidi ya kuuparamia mti kwa haraka cha hadi nikakaa juu ya moja ya tawi huku nikihema na jasho jingi lilimwagika.Mwanga wa mbara mwezi ukanisaidia kuwaona jamaa wakiuzunguka mti huku wakinguruma kwa sauti za kutisha sana.Mbwa watu wakaanza kutoa vilioa vya ajabu na kadri mawingu yanavyozidi kuufunika mwezi ndivyo wao wanavyozidi kupata shida katika miili yao na ambayo ikaanza kurudi katika hali kawaida hadi wa kawa binadamu wa kawaida ila hakuna aliye kuwa na nguo miomgoni mwao

Kila kitu ambacho kinaendelea sikuwa ninaamini ni kweli na ninayo jionea,nikajilaza kwenye tawi huku nikiendela kuwatazama jamaa na wakabaki chini ya mti wakiwa wananitazama huku wakinisubiria nishuke.Masaa yakazidi kwenda na kidogo nikaanza kushindana na macho yangu kitika swala zima la usingizi na kila nipojaribu kuyafumbua kwa nguvu zagu zote ndivyo jinsi macho yalivyo zidi kunikatali nakujikuta taratibu nikiyafumba na kausingizi kakanipitia.Nikaanza kuisikia sauti kwa mbali ya Rahma ikiniita na kunilazimu kuyafumbua macho na kukuta mwanga ukiwa umetawala kila sehemu na jamaa sikuwaona,Nikashuka kwenye mti taratibu hadi ninakanyaga ardhi na Rahma akawa amefika kwenye sehemu nilipo
“Eddy ulikuwa wapi?”
Nikamtazama Rahma kwa macho makali yaliyo jaa hasira na sikumjibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kuondoka pasipo kumkibu.Nikapitiliza moja kwa moja hadi sehemu walipo kuwa wakicheza ngoma zao usiku na kuyakuta mazingira yakiwa kama jana mchana tulivyo yaacha na hapakuwa na hata jani linalo onyesha kuwa limekanyagwa.
“Eddy mume wangu si nimekuuliza ulikuwa wapi hujanijibu kitu au hujanisikia?”

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 51 na 52 )

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA                      
ILIPOISHIA 

Nikasikia Monica akimuambia mzee huyo anahitaji hati, mzee huyo akampatia bahasha, Monica huku simu akiwa ameibana sikioni mwake, akatoa hati ya nyumba.
“Ni hati yenyewe?”
“Ndio ni hati nyenyewe?”
“Ina jina gani?”
“Raja Bahamuz”
“Ok mpatie mtoto wake”
Nilipo hakikisha Monica amekabidhiwa kila kitu nikasimama sehemu niliyo kuwa nimelala nikilifwatilia tukio hilo.
“Nyoosha mikono yako juu na bastola yako itupe pembeni”
Niliisikia sauti ya K2 nyuma yangu, jambo lililo nifanya mwili mzima kunisisimka kwa hasira kali
  
ENDELEA
Taratibu nikanyoosha mikono yangu juu, huku bastola yangu nikiitupia pembeni.
“Geuka nyuma”
Alizungumza kwa ukali, nikafanya kama alivyo hitaji niweze kufanya. Taratibu nikageuka huku nikimtazama usoni. Alipo niona ni mimi akabaki akiwa ameduwaa, macho yamemtoka, nikahisi hata nguvu za mwili zimemuishia.

“Halloo K2”  
Nilizungumza huku nikimtazama kwa macho ya dharau. Nikaitazama mikono yake nikaiona jinsi inavyo tetemeka kwa woga, nikatambua kwamba hii ndio nafasi yangu ya kuweza kumshambulia. Pasipo kufikiria kwa maya ya pili nikajituma hewani huku nikirusha teke lililo elekea maeneoa ya mikono ya K2 na bastola yake ikaangukia pembeni. Hapo ndipo K2 alipo jipanga kwa kukabiliana na mimi woga na wasiwasi ukamtoka. Akaanza kurusha ngumi za huhakikia ambazo nyingi katika hizo niliweza kuzikwepa japo kuna baadhi ya ngumi hizo zilinipiga kwenye baadhi ya mwili wangu.
‘Hakikisha unarudi na kichwa cha K2 hapa’
Kauli ya mama ikanirudia kichwani mwangu, roho ya kinyama ikaniingia moyoni mwangu. Nikaanza kujibu mashambulizi ya K2 kwa kasi kubwa na nguvu. Ngumi zangu kwa wakati huu ninaimani zimeongezeka uzito, kila ngumi niliyo mpiga iliweza kumyumbisha.

    Gafla nikaanza kusikia milio ya risasi ikitokea uwanjani, nikageuza macho yangu na kuona kundi la wana kikosi cha NSS, walio valia suti nyeusi wakija kwa kasi. Nikampiga mtama mmoja K2 na kuanguka chini, na kuanza kubingiria kwenye ngazi za uwanja huu. Kwa haraka nikaifwata bastola yangu ilipo huku nikiwa ninaruka sarakasi zilizo nisaidia sana kuweza kukwepa risasi za wezangu hawa ambao kwa sasa tumekua kama maadui.
Nilipo hakikisha bastola yangu nimeishika vizuri mkononi, sikuwa na haja ya kuanedelea kukaa katika eneo hili, kwa kupitia sehemu niliyo ingilia katika uwanja huu, ndio njia ninayo tumia kutoka. Nikashuka kwenye ukuta huo kwa haraka na kusimama nje. Nikatazama gari langu sehemu lilipo sikuliona hapo wasiwasi ndipo ulipo anza kunikabili.

“Ingia kwenye gari”
Niliisikia sauti ya Monica akizungumza pembeni yangu huku akiwa amesimamisha gari langu pembeni yangu,    nikamtazama kwa sekunde kadhaa kisha nikaingia kwenye gari, na akaliondoa kwa kasi katika eneo hili.
“Ulikuwa umekwenda wapi?”
Nilizungumza huku nikiwa ninatazama nyuma kuangalia kama kuna gari ambazi zinatufwata.
“Nilichukua gari kuliweka sawa kwa maana nilisha kuona umewekwa kwenye ulinzi”
“Ulijuaje kama ningeweza kutoroka eneo lile?”
“Unaonekena ni kijana shupavu, sio mtu wa kukamatwa kiurahisi rahisi kiasi kile, tena na mwanamke”
Manano ya Monica kidogo yakanitatanisha akilini mwangu, nikawaza labda alihitaji kuondoka na gari langu na kubadilisha mawazo yake, ubaya niliufunga mlango na kuondoka na funguo zangu.

“Funguo za gari ulizipatia wapi?”
“Nilizikuta nje ya gari zimeanguka”
Nikajipapasa sehemu nilipo kuwa nimeziweka na ni kweli sikuzioona.
“Sasa tunaelekea wapi?”
Nilimuuliza Monica ambaye yupo makini barabarani akizidi kuongeza mwendo kasi wa gari.
“Tunaelekea nyumbani kwangu”
“Ni wapi?”
“Wewe twende utapaona”
Monica hakusimamisha gari, tukafika maeneo ya Jaje, akazidi kusonga mbele kueleka maeneo ya Pangani. Katikati ya msitu akakunja kushoto mwa barabara ambapo kuna barabara ndogo inayo ruhusu gari kuweza kupita. Tukazidi kusonga mbele, kidogo wasiwasi ukaanza kunipata, bastola yangu nikaishika vizuri endapo kutatokea jambo lolote la hatari basi ninaweza kujitetea.

Naibu Waziri :Siwezi Kujibizana na Diamond

0
0
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, amesema amesikia malalamiko ya mwanamuziki Diamond lakini hawezi kumjibu kwa sababu zipo taratibu za kufuata kama anaona hajatendewa haki.

Shonza analijibu hilo ikiwa ni siku moja tangu mwanamuziki  'Diamond' amtaje waziri huyo katika malalamiko yake, akidai amekuwa akikurupuka  na kutolea mfano wa kufungia nyimbo na wasanii wakati akihojiwa na kituo cha redio cha Times.

Waziri huyo amesema hayupo tayari kumjibu Diamond  ingawa wasanii wanapaswa kuelewa kuwa hakuna aliye juu ya sheria hata kama msanii mkubwa namna gani.

"Aliyewafungia wasanii si Shonza bali ni mamlaka na kama mlivyoona safari hii hadi Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeingilia kati suala hilo, sasa mtu anaporusha tuhuma kumlaumu Shonza atakuwa hanitendei haki. Isitoshe ofisi zetu zipo wazi anayeona ameonewa afuate taratibu katika kudai haki yake na si kulalamikia pembeni," amesema Waziri Shonza.

Kuhusu kutoitwa kwa wasanii kabla ya kufungiwa kwa nyimbo zao Shonza amesema hilo waulizwe Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) maana ndio wenye kujua sababu na kwa baadhi ambao aliwaita ameeleza kuwa ni kutokana na kupewa maagizo ya kubadilisha nyimbo zao na kuwahi kukiri makosa lakini wakashindwa kutekeleza.

Katika mahojiano hayo na redio Times, Diamond alielekeza mashambulizi zaidi kwa Waziri Shonza na kudai kwamba amekuwa akifanya maamuzi yake kwa kukurupuka akisahau kwamba viongozi hawana mchango wowote kwao na pia wamekuwa wakiziumiza familia zao.

Februari 28 TCRA iliandika barua kwa vituo vya redio na televisheni ikiviagiza visitishe kuonyesha nyimbo 15 za wasanii kadhaa kutokana na kuwa na maudhui ambayo yanaenda kinyume na maadili na kanuni za Huduma za Utangazaji(Maudhui) 2005.

Nyimbo hizo na jina la msanii aliyeimba  kwenye mabano ni  Hallelujah na Wakawaka (Diamond), Kibamia (Roma Mkatoliki), Pale Kati patamu, Maku (Makuzi) na Mikono Juu (Ney wa Mitego), Hainaga Ushemeji(Manifongo), I am Sorry JK(Nikki Mbishi.

Nyingine ni Chura (Snura) na Nimevurugwa (Snura), Tema mate tumchape(Madee), Uzuri wako(Jux), Nampa papa(Gigy Money), Nampaga(Baranaba) na Bongo Bahati mbaya(Young D).

Kisa Cha Mwanamke Aliye Bakwa Na Sokwemtu Wa Kichawi Kwa Sababu Ya Usaliti Wa Mapenzi.

0
0
IMESIMULIWA NA   DOKTA. MUNGWA KABILI
0744  000  473

Tukio hili lilitokea  mwaka  1994  katika  kijiji  kimoja kilichopo  katika  mkoa mmoja uliopo  magharibi  mwa  Tanzania.

                   CHANZO   CHA   KUBAKWA   :
Chanzo  cha   tukio  hili  ni  usaliti  ulio fanywa na  binti  huyo  dhidi ya  mwanaume  ambae  aliwekeza  muda, afya, mali na  pesa  zake  kwa  mwanamke  huyo  mrembo  akitumaini kuwa  kwa  kufanya  hivyo  atapata  nafasi  ya  kumuoa  mwanamke huyo  aliyetikisa  kijiji  kwa  uzuri  wake  lakini  badala  yake  mwanamke  huyo  akaishia  kumsaliti   na  kutaka  kuolewa  na  mwanaume  mwingine.

HISTORIA   FUPI  YA  BINTI  HUYU NA  JINSI  ALIVYO  INGIA  KATIKA  UHUSIANO  NA  MWANAUME WAKE  WA  KWANZA.
Binti huyo  mrembo  alizaliwa mwaka  1975  katika  kijiji  kicho. Alianza   darasa  la  kwanza  mwaka 1983  na  kuhitimu  darasa  la  saba  mwaka  1989  akiwa  na umri wa  miaka  kumi  na  nne.

Hakufanikiwa  kuchaguliwa  kuendelea  na  masomo  ya  sekondari na  wazazi  wake  kwa  kuwa  hawakuwa  na  uwezo  wakampeleka  kwa  shangazi  yake  aliye  kuwa  anaishi  wilayani ili aweze kujifunza  kushona cherehani.

Hii ilikuwa ni  mwanzoni  kabisa  mwa  mwaka wa 1990.

Mwaka 1992  akiwa  amesha hitimu  mafunzo  yake  na  sasa  akawa anapata  uzoefu  wa  kazi  ya  kushona , binti huyo alikutana  na  kijana  mmoja na  kuanzisha  nae urafiki  ulio  zaa  mapenzi na  baadae  uchumba.

Kijana  huyu  alikuwa na  umri  wa miaka thelathini. Alitoka  katika kijiji  jirani  na  anacho toka  binti  huyu.

Kijana  huyu  alikuwa  anajishughulisha  na  kilimo ambacho  alikifanya  kijijini  kwao  na  hapo  senta   alikuwa  anajishughulisha  na  biashara  ya  genge.

Kijana  huyu  ingawa  hakuwa  tajiri  lakini  pesa ya  chakula  ilikuwa  haimpigi  chenga.

KIJANA  ANATAMBULISHWA  NYUMBANI KWAO  BINTI
Mwaka 1993  mwanzoni   kijana  huyu  alienda  kwao  na  huyo  binti  kwa  ajili  ya  kujitambulisha rasmi  ambapo posa  yake  ilikubaliwa.

MAMA  WA BINTI  APATA  MARADHI YA  FIGO
Mwaka  1993  mwishoni, mama  wa binti  huyo aligundulika kuwa na  maradhi  ya  figo  ambapo  ilihitajika  figo  moja ili  kuokoa uhai  wa  mama  huyo.

MCHUMBA  WA BINTI  ANAJITOLEA  KUTOA  FIGO  YAKE
Taarifa  za kuhitajika  figo  moja  ili  kuokoa  maisha  ya  mama  yake zilimchanganya  sana  binti  huyo  kama  zilivyo  wachanganya  wana  familia  wengine.

Hawa  kuwa  na  budi  Zaidi  ya kufanya utaratibu  ili  mama yao  apate figo moja.  Katika  kufanikisha  hilo, ndugu  na jamaa wa mama  wa  binti  wakaanza  kufanya  utaratibu  wa  kutafuta  mtu katika  familia au ukoo ambae anaweza  kujitolea  kutoa  figo  yake.

Jamaa  yeye  mwenyewe  bila  hata kuombwa na  binti  alimwambia  binti kuwa yupo tayari  kutoa  figo  kwa ajili  ya  mama  ake.

Jambo  hili  lilimshangaza  sana  binti na  alipo ijulisha  familia  yake  walishangaa  kuona  upendo  wa  ajabu  ulio onyeshwa  na  kijana  huyo.
 
Taratibu  zikafanyika  na  ikaonekana  kitaalamu  kwamba  figo ya  jamaa  inafaa, basi  jambo  hilo  likafanyika  kwa  mafanikio makubwa.

BINTI   ANAPATA  MCHUMBA MWINGINE
Katika hali ya kushangaza, wakiwa  bado  katika  uchumba, binti  huyo  alikutana  na mwanaume mwingine  ambae  alionekana kuwa  na  uwezo  mkubwa  sana  kuliko  mchumba  wa  binti  huyo.

Hii  ilikuwa mwanzoni  mwa mwezi wa Juni  mwaka 1994.

Mwanaume  huyu  mpya, alikuwa  msomi, na  mwenye uwezo  mkubwa  kifedha  ambae alikuwa anafanya  kazi kwenye  shirika  moja  la  kimataifa  ambalo lilikuwa  na  ofisi  yake  katika  wilaya  kinacho  patikana  kijiji  alichoishi  binti huyu.

Kwa nguvu  ya  pesa aliyo  kuwa nayo, jamaa aliweza kufanya  mipango  ya  kujitambulisha  nyumbani kwao na  binti  haraka haraka  na ikapangwa siku  rasmi ya kwenda kutoa  mahari nyumbani kwao na binti.

JAMAA  ANAPATA  TAARIFA  ZA  BINTI  KUPATA  MCHUMBA  MWINGINE ..
Familia  ya  binti  hawakutaka  jambo  hili lijulikane na mchumba  wa binti  huyo  hivyo  walipanga  kufanya  jambo  hilo  haraka  haraka  na  kwa siri  kubwa  sana.

Lakini hata  hivyo, duniani  hakuna  siri  ya  watu wawili, wapo wasamaria  walio kuwa  wanajua  kuhusu  uchumba  kati  ya  binti  na  jamaa  huyo  na  ambao  hawakufurahishwa  na mpango  wa  familia  ya  binti  kumuozesha  binti  huyo  kwa  mwanaume  mwingine, na hivyo  kwenda kumjulisha  jamaa.

Jamaa  hakuamini  na  alichanganyikiwa  sana na  aliunganisha  dot  kati  ya  maelezo  aliyopewa  na  mabadiliko  ya  tabia  na  kimuonekano  kutoka  kwa  binti  na  familia  ya  binti.

Binti  alianza  kuonekana  akiwa anavaa  mavazi  mazuri  kuliko  kiasi  cha pesa  alichokuwa  anampa.  Akapunguza  heshima  na  mawasiliano  kwa jamaa.  Baba  na  mama wa  binti  nao  wakaanza  kumbadilikia  jamaa. Kwa mfano  alikuwa  akiomba  binti amsindikize  mjini  anakataliwa  bila  sababu  ya  msingi, tofauti  na  ilivyo  kuwa  awali.

Pia  akashangaa  kumuona  binti  anauza  duka kubwa bila  kujua  duka  ni  la  nani, achilia  mbali  kumtaarifu jamaa.

Mambo  haya  yalimchanganya  sana  jamaa  na  kumuumiza  moyo  mno.

Mtu mmoja  wa  karibu na  jamaa  akamwambia  pengine binti  na  familia  yake  wamekubadilikia  kwa  sababu  unachelewesha  ndoa, fanya  mipango  ya  ndoa  haraka  na  bila shaka  mambo  yatakuwa  mazuri kama zamani.

MPANGO  WA  JAMAA  UNAKATALIWA NA  BABA  WA  BINTI.
Jamaa  akamchukua  mshenga  wake, wakaenda  hadi  kwa  baba  wa  mchumba  wake  na  kumueleza  kwamba  sasa  anataka  afanye mpango  ili  yeye  na  binti  huyo  wafunge  ndoa  haraka  iwezekanavyo  lakini  kwa  mshangao  wake, baba  wa  binti  akamwambia  ngoja  awashirikishe  wanandugu  kwanza. Jambo  hili  lilimtia  hasira sana  jamaa.

TUKIO   LA  BINTI  KUBAKWA  NA  SOKWE  MTU.
Ilikuwa ni  mwezi  Desemba  1994. Siku  hii ilikuwa  ni  siku  ambayo mwanaume mpya, mshenga  wake, baba ake, dada  zake  na  baadhi  ya ndugu  zake  walikuwa  wameenda   nyumbani kwao na  binti huyo kwa  ajili  ya  kutoa  mahari  rasmi.

Wakati  taratibu  za  kutambulishana  zikiwa  zinaendelea, lilitokea  kundi  kubwa  la  sokwe mtu  kutoka  kwenye  msitu  wa  miti  uliokuwa karibu  na nyumba  yao na huyo  binti.

Kundi hili  la  sokwe mtu  wasio  wa kawaida  liliingia ndani  hadi mahali  walipokuwa   wamekaa  familia za  pande  zote  mbili  yani upande wa binti na  upande wa mwanaume na kuzua  taharuki kubwa.

 Sokwe  mtu  mmoja   aliingia hadi  mahali  alipokuwa amekaa  binti  huyo, akamshika na  kutoka  nae  nje  sehemu  ya  uwazi   ambapo  alimchania  nguo  zake  na  kuanza  kumbaka.

Binti  na  wanafamilia  walibaki wanapiga  kelele za  kuomba  msaada  lakini  kelele  zao  hazikumzuia  sokwe mtu  huyo kuendelea  kumbaka binti  huyo.

Kelele za  wanafamilia zili washtua  wanakijiji ambao  mamia  kwa  mamia  walikuja  katika  eneo  la  tukio  kuona  kunani.

Walipofika  katika  eneo la  tukio  walikuta  sokwemtu  akiwa anambaka binti  huku ndugu na jamaa  wa binti  huyo  pamoja  na ndugu  na  jamaa  wa mwanaume  aliye taka  kumtolea  mahari  binti  huyo  wakiwa  wanajaribu  kupambana  na  sokwe huyo  pamoja  na sokwe  wale  wengine  bila  mafanikio.

Wanakijiji  walivyo  kuja  wakaongeza  nguvu  na  wazee  wakimila  wa  kijiji na  kuanza  kupambana  na  wale sokwemtu  ambao walikimbia  na  kupotelea  msituni.

Wakati  huo huo  sokwe  aliyekuwa anambaka  yule  binti  alikuwa tayari  ameshamaliza  kufanya  tendo na yeye  akakimbia  na  kupotelea  msituni  kimiujiza.
 
Binti  huyo  ambae  kwa  wakati  huo  alikuwa anagaa  gaa  kwa  maumivu  makali  uwanjani hapo   alichukuliwa na wazee  wa  kimila  kwa  ajili  ya  kupewa  huduma  ya  kwanza na kufanyia  matambiko.

MATOKEO   YAKE
·Yule mwanaume  aliekuja  kumchumbia  yule  binti  aliondoka na  hakurudi  tena  wala  hakutaka  kusikia  chochote  kuhusu  mwanamke  huyo.  Asingeweza  kuishi  na mwanamke  ambae amebakwa  na  sokwemtu  huku yeye,wanafamilia  yake  na  kijiji  kizima  wakishuhudia.
  • Binti  alijiua
  • Familia  ya  nzima  ya  binti  huyo ilinyanyapaliwa.
  • Mama wa  binti  aliwehuka na  kutoweka  kijijini hapo
  • Mdogo  wa  binti  alikimbilia  kwa  shangazi  yake kule wilayani lakini  haikumchukua  muda  mrefu nay eye  alijiua
  • Baba  wa  binti  aliwehuka  na  kufa miaka  miwili  baadae.

FUNZO :  USALITI  KATIKA  MAPENZI   IWE  UMEFANYWA  NA  MWANAMKE  AU  MWANAUME NI  MBAYA  SANA, UNAWEZA  KUKULETEA  MADHARA  MAKUBWA  KAMA MADHARA  YALIYO  ITOKEA  FAMILIA  YA  BINTI  HII.

CHANZO  KIKUU  CHA  USALITI  KATIKA MAPENZI  NI TAMAA. WACHA TAMAA  TAMAA  MBAYA  SANA.

Katika  siku  zijazo  nitaandika  Makala  nikielezea  kwa  kina  jinsi  wachawi  wanavyo weza kutengeneza  sokwe mtu  wa  kichawi  kwa  kwa  ajili ya  kuwatumia  kulipa  kisasi  dhidi ya  wasaliti  katika  mapenzi  pamoja na  kinga  ya  kuzuia  kudhuriwa  na  uchawi  kama  huu.

IMESIMULIWA  NA  DOKTA MUNGWA  KABILI…..0744 000 473.

Mchungaji Awalambisha Viatu Waumini wake Ili Wapate Baraka za Miujiiza

0
0
Mchungaji mmoja kutoka Nigeria (39), Andrew Ejimadu wa kanisa la Christ Freedom Ministries amezua gumzo mtandaoni baada ya ku-post picha zake katika mtandao wa Facebook wakati wa kuabudu mitandaoni.

Nabii huyo ameshangaza maelfu ya watu baada ya kuonyesha picha za waumini wa kanisa lake wakibusu na kulamba viatu vyake akidai kuwa kwa kufanya hivyo watapata baraka na miujiza.

Nabii huyo aliweka picha hizo katika ukurasa wake na kuandika.“Nimebariki miguu yako, nimeosha nyayo zako.”

“Kitu cha kwanza kesho asubuhi, ikiwa utaandika Amen na ushirikishe ujumbe huu, kuna mtu atakupigia simu na miguu yako itakubeba hadi huko kuchukua zawadi maalum. Watu wengi watakosa hilo, jaribu,” Andrew Ejimadu.

Mwaka 2016, Mchungaji Ejimadu alipamba vichwa vya habari na kushikiliwa na polisi nchini Zambia yeye na kaka yake, Cleopasa Ejimadu kwa kosa la kumbaka binti mdogo mwenye umri wa miaka 14 ambaye alikwenda kwenye makazi yao kwa ajili ya uponyaji na kupata ushauri WA kiroho.

Rais Magufuli Kawapa Siku 7 Mawaziri Wake

0
0
Rais Dkt. John Magufuli ametoa wiki moja kwa Mawaziri kufanyia kazi changamoto na maoni yaliyotolewa na wafanyabiashara katika mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara ili kuweza kutatua kero zao.

Amewataka Mawaziri kuandika maelezo yenye majibu ya changamoto na maoni hayo na kuwasilisha kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ili serikali ifanyie kazi na kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji hapa nchini.

Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa baraza hilo ametoa maagizo hayo jana wakati akihitimisha mkutano huo ambao wafanyabiashara na wawekezaji kutoka sekta mbalimbali walipata nafasi ya kueleza maendeleo ya shughuli zao, changamoto zinazowakabili na mapendekezo ya kuimarisha biashara na uwekezaji hapa nchini.

Miongoni mwa changamoto zilizoweza kuwasilishwa katika mkutano huo ni pamoja na utozaji wa kodi unaoathiri biashara na uwekezaji, urasimu wa taasisi za serikali, udhibiti wa bidhaa za kutoka nje ya nchi zinazoathiri uzalishaji wa bidhaa za ndani, uwepo wa sheria na kanuni kandamizi kwa biashara na uwekezaji na utendaji usioridhisha kwa baadhi ya maafisa wa Serikali.

“Nataka kuwaambia kwa dhati kabisa, serikali ninayoiongoza haiwachukii wafanyabiashara, inawapenda na itawaunga mkono, kama nilivyowaambia huko nyuma huu ndio wakati wenu wa kufanya biashara, fanyeni biashara zenu na lipeni kodi, hizi changamoto tumezipokea na tutazifanyia kazi”, alisema Dkt. Magufuli.

Kwa upande mwingine, Rais Magufuli ametoa wito kwa wafanyabiashara hao kuhakikisha wanashiriki katika miradi mikubwa anayotekelezwa na serikali ikiwemo ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge), mradi wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stieglers’ Gorge), mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta la kutoka Hoima – Uganda hadi bandari ya Tanga – Tanzania, na amewataka wafanyabiashara wanaofanya vitendo vya udanganyifu katika kodi na uingizaji wa bidhaa wabadilike.

Waziri Mkuu Atoa Milioni 5 Kwa Mjasiriamali Mlemavu

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemkabidhi Bibi Tecla Hamidu ambaye ni mlemavu wa miguu sh. milioni tano ili aweze kuongezea katika mtaji wake.

Ametoa fedha hizo leo (Jumanne, Machi 20, 2018) ikiwa ni katika kutimiza ahadi yake aliyoitoa Februari 22, 2018 kwenye Mkutano wa Sita wa Wamiliki wa Viwanda na Watumiaji wa simbomilia (barcodes).

Waziri Mkuu alitoa ahadi hiyo baada ya Bibi Tecla ambaye ni mjasiriamali anayejihusisha na ushonaji wa bidhaa mbalimbali zikiwemo nguo kumuomba amchangie sh. 500,000 ili aweze kuongezea mtaji wake.

Wakati akimkabidhi fedha hizo, Waziri Mkuu amesema kwamba anatarajia zitamsaidia katika kuongeza  mtaji wake, hivyo atazalisha bidhaa nyingi zenye ubora unaohitajika katika masoko ya ndani na nje.

Kwa upande wake, Bibi Tecla alimshukuru Waziri Mkuu kwa msaada huo na ameahidi kuzitumia fedha hizo kama ilivyo kusudiwa.

“Nashukuru kwa msaada huu kwani kuna watu wanakopa sh. laki mbili ili waongeze mitaji, lakini mimi leo nimepewa milioni tano bure na kiongozi wetu,”

Amesema licha ya kukabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa masoko anaamini tatizo hilo litakuwa historia baada ya kuwa na mtaji wa kutosha kwani atakwenda kuzalisha bidhaa zenye ubora zaidi.

Millen Amtole Povu Shabiki Kuhusu Mtoto Wake.

0
0
Mwanamitindo Millen Magese amejikuta akiongea kwa hasira na uchungu baada ya moja ya mashabiki zake kumsema na kumwambia kuwa kwa mavazi anayomvalisha mtoto wake ni kama anataka kumuu kwa kumnyonga,.

Mwanamitindo huyo ambae amepata mtoto wake hivi karibuni baada ya kukaa kwa muda mrefu bila kupata mtoto kutokana na ugonjwa aliokuwa nao ambao kwa wanawake wengi unasababisha ugumba aliongea na kusea kuwa kwa muda mrefu sana amekuwa akitafuta mtoto huyo kwaio hawezi kufanya kitu kama icho.

Katika ukurasa wake wa instagram millen aliweka picha a mtoto wake ndipo alipoanza kupokea maneno ya kukera kutoka kwa mashabiki na kuamua kumjibu mmoja wapo.
Picha ya mtoto wa millen iiliyozua utata katika mitandao.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Amuua Mkewe na Kuificha Maiti Kwenye Mbuyu kwa Miaka 8

0
0
Mwanaume  mmoja aliyejulikana kwa jina Bernard Shumba mkazi wa Singida anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa kumuua mke wake miaka minane iliyopita kisha kuuficha mwili wa marehemu kwenye mbuyu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Deborah Magiligimba, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtuhumiwa baada ya kukamatwa alikiri kutenda kosa hilo na kwenda kuonyesha mwili wa marehemu aliokuwa ameuhifadhi ndani ya mbuyu ambapo jeshi hilo kushirikiana na wananchi limefanikiwa kupata mabaki yake.

Inadaiwa kuwa mnamo Julai 10, 2010 katika Kijiji cha Yulansoni Kata na Tarafa ya Kinyangiri Wilaya ya Mkalama mkoani Singida, Tabu Robert (28) ambaye kwa kabila ni Mnyiramba, mkulima wa Yulansoni, aliuawa na mume wake aitwae Bernard Shumba Siza (47), Mnyiramba na mkulima wa Yulansoni.

Baada ya Mmuhumiwa kufanya tukio hilo aliuchukua mwili wa marehemu na kwenda kuuficha kwenye mti wa mbuyu ambao una tundu kubwa na kisha aliripoti polisi kituo kidogo cha Kinampanda Mkalama kuwa mke wake ametoroka na alianza kumtafuta hadi tarehe Machi 17, 2018 ambapo taarifa zilipopatikana kuwa alimuua.

Baada ya mtuhumiwa kukamatwa na kuhojiwa alikiri kufanya kitendo hicho na kuonyesha sehemu alipouficha mwili huo Machi 18, mwaka huu majira ya saa 10:00 jioni.

Mkuu wa polisi kituo cha  Mkalama na timu yake ya makachero walifika eneo la tukio na kufanikiwa kupata mabaki ya mifupa yakiwa ndani ya mti huo. Baadhi ya mifupa imechukuliwa kwa ajili ya kupelekwa kwa mkemia wa serikali na iliyobakia ndugu wamekabidhiwa kwa ajili ya mazishi.

Credit: Global Publisher

Rais Magufuli kumuapisha IGP Mstaafu Mangu kuwa Balozi kesho

Kauli Ya Serikali Kuhusu Ofisa Ubalozi wa Syria Nchini Kushambuliwa

0
0
Baada ya kuwepo kwa taarifa kupitia mitandao ya kijamii kuhusu kushambuliwa kwa afisa wa ubalozi wa Syria nchini Tanzania na watu watatu wasiojulikana na kupigwa ikiwa pamoja na kuporwa pesa, simu na gari aliyokuwa akiitumia kwa shughuli za ubalozi.

Kufuatia taarifa hizo Msemaji Mkuu wa Serikali Dk. Hassan Abasi amefunguka na kukiri kupata taarifa hizo na kudai kuwa serikali inafuatilia suala hilo na itatoa taarifa kamili kuhusu jambo hilo.

"Umma unaarifiwa kuwa vyombo vya dola vinafuatilia taarifa za Afisa Ubalozi wa Syria nchini kushambuliwa, kuporwa. Taarifa kamili itatolewa" alisema Abasi

Aidha katika taarifa za awali zinadai kuwa afisa huyo amelazwa katika hospitali ya Agha Khan akipatiwa matibabu kufuatia shambulio hilo

Diamond Kamjibu Tena Naibu Waziri wa Habari......“Unalijua leo baada ya kukosa point sahihi?”

0
0
Baada ya Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Juliana Shonza kukataa kumjibu Diamond, msanii huyo ameibuka tena yakiwa ni masaa takribani 23 yamepita tangu alipomjia juu kupitia kipindi cha The Playlist.

Diamond ameonekana kukerwa na majibu ya Naibu Waziri Shonza ambayo amekuwa akiyatoa kuhusu kufungia nyimbo za wasanii bila ya kuwapa taarifa sahihi na kuamua kumjibu kwa mara nyingine na safari hii ametumia mtandao wa Twitter.

Kupitia mtandao wa huo Diamond ameandika:
Swala la Barua Unalijua leo baada ya Kukosa Point sahihi? Ungekuwa unajua kama taratibu sahihi ni Kuandika Barua, Mbona hukuwatumia pia Wasanii barua zakuwa unafungia kazi zao?… kwakuwa Uliyapeleka Social Media na Radio, nami nikakupelekea huko ili uenjoy Zaidi…❤

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya March 21

Mfanyabiashara wa Kinondoni Kafikishwa Mahakamani Kwa Kusafiirisha Dawa za Kulevya

0
0
Mfanyabiashara, Hariri Mohammed Hariri (45), mkazi wa Kinondoni, jana alipandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kujibu Tuhuma za kusafirisha zaidi ya gramu 214 za dawa za kulevya.
 
Akisoma hati ya mashtaka Wakili wa serikali, Clara Chalwe mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi imedaiwa Machi 2 mwaka huu huko Kinondoni Matitu ndani ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam mshtakiwa alisafirisha dawa za kulevya aina ya Heroine Hydrochloride zenye uzito wa gramu 214.11.

Hata hivyo, mshtakiwa hakuruhusiwa kujibu kitu chohote mahakamani hapo kwa kuwa Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za dawa za kulevya  isipokuwa kwa kibali kutoka kwa DPP.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika. Na imeahirishwa hadi Aprili 4 mwaka huu
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images