Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

TANGA RAHA- Sehemu ya Thelathini na Nne ( 34 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

“Tena ngoja nikawaonyeshe kaburi lamke wangu muda kidogo umekwenda”
Tukasimama na tukatoka nje na kuzunguka upande wa pili wa nyumba na gafla nikaanza kumuona Rahma akianza kubadilika sura yake baada ya kuiona picha iliyo wekwa juu ya kaburi la mke wa Mzee Ngoda

ENDELEA
“Huyu ndio mke wangu ambaye alinifanyia mambo mengi ya ajabu sana”
Rahma akapiga magoti taratibu na kuitazama picha kwa kwa umakini huku akiifuta futa vumbi na mimi nikajikutana nikiikazia jicho kwani picha iliyo kuwepo pale inafanana sana na Olvia Hitler ambaye siku zote ninaamini ni shetani ambaye alikuwa akinifwatilia
“Baba huyu ni mke wako?”
“Ndio na nimezaa naye mtoto yule mmoja”
Nikataka kuuliza jina lake ni nani ila kwenye msalaba ulio tengenezwa ukanipa jina kamili ambalo ni Olvia Abdukarim,kajasho kembamba nikahisi kina nimwagika kwenye uso wangu huku kwa mabali mapigo ya moyo yakienda kasi kiasi
“Huyu dada mimi mbona kama ninamjua”
Rahma alizungumza na kutufanya sote tumtizame na mimi wasiwasi ukazidi kunijaa na kujikuta nikikishindwa hata kuzungumza

“Umemonea wapi?”
“Sikumbuki ni wapi nimemuona ila hata majuzi nilikuwa naye ila sikumbuki ni wapi?”
“Utakuwa umeota huyu mke wangu nilimuua miaka miine ya nyuma”
“Labda watu wanafanana na pia alinielezea mambo mengi sana ila ahaaa siyakumbuki”
 Nikamtazama Rahma jinsi anavyo ishika shika picha  iliyopo kwenye kaburi hata hamu ya kuitazama ikaniishia
“Jamani mimi nipo ndani”
Nikaondoka taratibu huku nikiwaacha wakiendelea kuzungumza kuhusiana na maisha ya mke wa Mzee Ngoda,Amani yote ikatoweka moyoni mwangu ila nikaanza kujifariji kimya kimya kutokana nina pete mkononi ambayo alinipa Yudia.Wakaingia na kunikuta nikiwa nimejilaza kwenye kochi na Rahma akajiusha na kunikalia kwenye mapaja yangu
“Tutaumizana bwana”


Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Maboresho Katika Application ya Mpekuzi..... Download Upya Kwenye Simu yako Kupata Habari Zetu Haraka

$
0
0
Kuna Maboresho Mapya Yamefanyika Hatika Application Yetu ya Mpekuzi. Maboresho hayo yamelenga kukufanya upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile Magazeti kuliko ilivyo sasa.

Chakufanya, Ingia PlayStore, Download Upya Application yetu

Tumekurahisishia; 

Rais Magufuli Aita Wawekezaji....Adai Tanzania ni Salama na Hakuna Maandamano

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa walitumia njia ya amani ya Tanzania kuwashawishi wawekezaji waje nchini Tanzania na kuwekeza kwa kuwa ni nchi ambayo hana hata maandamano.

Magufuli amesema hayo leo Machi 19, 2018 wakati akizungumza na wafanyabiashara na wawekezaji mbalimbali katika mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara Ikulu jijini Dar es Salaam.

"Kuna miradi tumeanza ambayo nafikiri inajenga uchumi wa nchi yetu, bomba la mafuta hili ambalo uwekezaji wake ni zaidi ya dolla bilioni tatu itazalisha ajira zaidi ya watu elfu 15 wale wengine ni wengi zaidi kina mama lishe na kadhalika ni nafasi yenu wafanyabiashara na wawekezaji mkatumia hiyo nafasi ili tusiwe wasindikizaji.

" Tukatumia faidi ya nchi yetu kuwa salama na amani na ile ilikuwa pointi kubwa sana kwamba Tanzania wala hakuna matatizo, wala hakuna maandamano wala nini

"Njooni  muwekeze huku na watu wamekuja hiyo kampuni ya Total inajenga bomba ambalo linapita kwenye wilaya zaidi ya 84 ile ni faidi kubwa kwa watu wanaolewa hiyo ni nafasi kubwa" alisema Magufuli

Rais Magufuli Alivyotatua Kero ya Mizigo wa Mmiliki kiwanda cha mvinyo Papo kwa Papo!

$
0
0
Rais John Magufuli ameagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuruhusu chupa za mvinyo zilizozuiliwa bandarini kwa  sintofahamu ya masuala ya kodi

Akizungumza leo Jumatatu Machi 19, Rais Magufuli ameitaka TRA kumpa mmiliki wa kiwanda cha mvinyo cha Dodoma chupa zake kwa kodi ya bei iliyoinunulia.

“Haya TRA mpeni chupa zake za mvinyo kwa kutoza kodi ile anayodai amenunulia chupa hizo,” ameagiza.

Akiwasilisha kero hiyo, mwakilishi wa kiwanda hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Minde, amesema chupa zake zimekwama bandarini kwa sababu anadaiwa kodi kubwa kuliko uhalisia wa aliyonunulia bidhaa hiyo.

Amesema ingawa amewaonyesha risiti lakini wamekataa kumpa mzigo huo, kwa sababu kodi anayodaiwa ni kubwa.

Amri Ya Mahakama Iliyotolewa Leo Kuhusu Nabiii Tito

$
0
0
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma, James Karayemaha ameagiza Tito Machibya (Nabii Tito) kufikishwa mahakamani ili kuendelea na kesi yake au apate maelezo kamili ya kwanini mtuhumiwa huyo hafikishwi mahakamani.

Hakimu Karayemaha ametoa maagizo hayo leo Machi 19, 2018 baada ya kuelezwa kuwa Nabii Tito hakufikishwa mahakamani kwa kuwa bado anaendelea kupatiwa matibabu ya ugonjwa wa akili unaomkabili kwenye kituo cha magonjwa ya akili Hospitali ya Mirembe mkoani hapa.

Nabii Tito hakuweza kufika mahakamani jana kuendelea na kesi yake ikiwa ni mara ya pili kutokana na maelezo kutoka kwa maaskari magereza kuwa hayupo mahabusu bali yupo Hospitali ya Mirembe kitengo cha magonjwa ya akili akiendelea na matibabu.

“Mheshimiwa, Tito bado yupo kwenye kitengo cha Bloodmore Mirembe anaendelea na matibabu ya ugonjwa wa akili hajaletwa mahabusu,” amesema askari magereza mmoja ambaye hakutaja jina lake.

Hata hivyo Hakimu Karayemaha hakuridhika na majibu hayo na kuagiza Nabii Tito kufikishwa mahakamani hapo kuendelea na kesi yake au kama kuna ulazima wa kutofika mahakamani basi apelekewa maelezo rasmi yanayomkwamisha mtuhumiwa kufika mahakamani.

“Nimeamini kuwa mtuhumiwa yupo Mirembe kwa kuwa aliyetoa maelezo hayo ni askari magereza, lakini nataka April 5 afike mahakamani kuendelea na kesi yake au nipate taarifa rasmi za kwanini hafiki mahakamani, nataka aripoti siku hiyo si inakuja kutajwa tu,” amesema Karayemaha.

Hata hivyo askari magereza huyo amesema kuwa tangu mahakama ilipoamuru Nabii Tito afanyiwe vipimo vya kujua kama ana ugonjwa wa akili mwezi Februari mwaka huu, bado mtuhumiwa huyo hajamaliza siku za uchunguzi wa vipimo hivyo, kwa hiyo bado yupo Mirembe na hayupo mahabusu kwenye Gereza la Isanga.

Kesi ya Nabii Tito imeahirishwa hadi April 5 mwaka huu itakapotajwa tena.

Rais Magufuli Kazungumzia uwekezaji mpya utakaoajiri Watanzania zaidi ya 4000

$
0
0
Rais John Magufuli ameeleza kuwa siku za hivi karibuni atakutana na Wakurugenzi Watendaji wawili kutoka nchi za Ujerumani na Demark ambao watakuja kufanya uwekezaji nchini.

 Kauli hiyo ameitoa leo Machi 19, 2018 wakati wa mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara, uliobeba maudhui ya ‘Tanzania ya Viwanda na Ushiriki wa sekta binafsi nchini.’

Rais Magufuli ameeleza kuwa watakuja kufanya uwekezaji wa kiwanda kipya cha Petroli Kemikali (Petrol Chemical Plant) ambacho kitakuwa na thamani ya Dola za Marekani Bilioni 1.92 ambayo ni sawa na takriban Shilingi za Kitanzania Trilioni 4.56.

Ameeleza kuwa kiwanda hicho kinatarajiwa kutoa ajira kwa Watanzania zaidi ya 4000 katika eneo la Kilwa kwaajili ya kutengeneza mbolea ambayo itauzwa ndani pamoja na nje ya nchi kwa kutumia gesi iliyopo nchini.

Lowassa Aikubula Hoja ya Mkapa Kuhhusu Elimu.....Asema Ilikuwa ni Sera Yake na Ipo Katika Ilani yya CHADEMA

$
0
0
Waziri Mkuu za zamani, Edward Lowassa amemueleza Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa kwamba kauli yake aliyoitoa juzi akitaka kuwepo kwa mjadala wa kitaifa kujadili hali ya elimu nchini ilikuwa ajenda yake tangu alipokuwa CCM.

Lowassa ametoa kauli hiyo jana Machi 19, 2018 katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa na msemaji wake, Aboubakar Liongo.

Katika taarifa hiyo, Lowassa ambaye alijiunga Chadema mwaka 2015 baada ya jina lake kukatwa katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM kusaka mgombea wake wa urais katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015, amesema suala la elimu pia lipo katika ilani ya uchaguzi ya Chadema.

Juzi jioni katika hafla ya kumuaga Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Profesa Idris Kikula, Mkapa alisema kuna janga katika elimu nchini na kushauri kuitishwa kwa mdahalo wa wazi utakaoshirikisha makundi yote ya jamii kwa ajili ya kujadili suala hilo.

Katika taarifa yake hiyo, Lowassa amesema amesoma na kusikia taarifa ya Mkapa akitaka kuwepo kwa mdahalo wa kitaifa kuhusu kushuka kwa elimu nchini.

“Nimefurahi kuwa Mkapa ameliibua suala hili kwani hiyo ilikuwa ni ajenda yangu ya kwanza tangu nikiwa ndani ya CCM na nje ya CCM. Pia Ilani ya uchaguzi ya Chadema, elimu ndio ilikuwa ajenda kuu na tulisema tutaita mjadala wa kitaifa kuhusu elimu na kuangalia wapi tumekwama na nini kifanyike,” amesema Lowassa.

Lowassa amedai ajenda hiyo sio ya CCM na hawataweza kuisimamia kwa sababu wanataka kuendelea kutawala,ila  hawataki Taifa lililoelimika vizuri na linaloweza kuhoji.

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO 0754372325/ 0689013109/ 0620806813 

HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Waziri Mkuu Atoa Maagizo kwa Mawaziri Nchi 9 Kuhusu Magonjwa Yasiyoambukiza

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema mapambano ya magonjwa yasiyoambukiza yatafanikiwa endapo sekta nyingine mbali na afya zitashirikishwa.

Majaliwa ameyazungumza hayo jana wakati akifungua mkutano wa 65 wa mawaziri wa afya wa Jumuiya za nchi za Mashariki, Kati na Kusini mwa bara la Afrika uliowashirikisha mawaziri kutoka nchi tisa.

Alisema kutokana na ongezeko la magonjwa hayo, nchi hizo zinapaswa kuangalia namna ambavyo zitatatua ongezeko hilo ili kupunguza gharama.

"Ili kuepuka  kutumia gharama kubwa katika kutibu magonjwa haya juhudi za makusudi zinapaswa kuchukuliwa ikiwemo kushirikisha sekta nyingine katika kutatua changamoto zilizopo lakini zaidi ni kuelimisha jamii kubadili mfumo wa maisha," alisema Majaliwa.

Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia (WB), Dk Paolo Belli alisema nchi hizo kwa sasa zinatakiwa kutumia teknolojia mpya ili kupata matokeo mapya katika magonjwa mbalimbali ikiwemo magonjwa yasiyoambukiza, TB na vifo vya wajawazito na watoto.

Aidha, amezishauri nchi hizo kuangalia uwezekano wa kupunguza matumizi ya tumbaku kwa kuwa  yanasababisha madhara kwa watu wengi ikiwemo gharama za kutibu magonjwa mengi yatokanayo na madhara ya tumbaku.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP) Kumpandisha Mahakamani IGP Sirro, DCI na AG

$
0
0
Mahakama Kuu nchini  imetoa wito wa kuwaita DCI, IGP na AG kufika mahakamani siku ya Jumatano ya tarehe 21 kujibu kesi ya kutomfikisha mahakamani Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi  (TSNP) Abdul Nondo.

Taarifa za wito huo zimetolewa na Wakili wa Mwanafunzi huyo wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Wakili Jebra Kambole.

Kambole amesema "Wito umetolewa  Mahakama kuu mbele ya Jaji Rehema Sameji. kwamba DCI, IGP na AG wanapaswa kufika mahakamani 21/03/2018 kujibu kesi ya Abdul Nondo".

Kambole amesema washitakiwa katika kesi hiyo itakayosikilizwa Jumatano ni ; IGP  Sirro ambaye ameitwa kwasababu yeye ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini hivyo vituo vyote na polisi wapo chini yake lakini bado Nondo amekuwa hapatikani katika vituo vya polisi.

Aidha Kambole amesema kuwa katika jalada lililofunguliwa, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), naye kahusishwa kwa sababu mara ya mwisho Nondo alipokelewa na yeye alipofikishwa Dar es salaam kutoka Iringa na kwamba alimchukua kama muathirika wa tukio la utekwaji na siyo mshtakiwa.

Hata hivyo Kambole amesema ameshafanya jitihada nyingi za kutaka kuonana na mteja wake lakini hadi sasa juhudi zake hazijafua dafu.

Abdul Nondo anashikiliwa na jeshi la polisi tanguMachi 7, ambapo awali aliripotiwa kupotea kusikojulikana na kesho yake kujikuta Iringa, ambapo Kamanda wa Polisi  Kanda Maalumu, Lazaro Mambosasa amesema mpaka sasa wanamshikilia Nondo kwa ajilili ya upelelezi na watakapokamilisha watamfikisha mahakamani.

Ni Dr. Chief Malunde Pekee Anaetibu Nguvu Za Kiume Na Kumtuliza Umpendae Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
"NI DR. CHIEF MALUNDE PEKEE ANAETIBU NGUVU ZA KIUME NA KUMTULIZA UMPENDAE KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI"
-baada ya kujichimbia katika nchi za kiarabu kwa zaidi ya miaka (10)sasa amewasili nchini na dawa za tiba asilia.
 
1/NGOLO 3 POWER-ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, ina ubora wa hali ya juu wa kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wasiojiweza kufanya tendo la ndoa, inaimarisha misuli iliyolegea na kusinyaa, inarutubisha mbegu za kiume na kukufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15-25 kuwa na hamu na tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila kuchoka, inarefusha uume inchi 5-8 na kunenepesha hadi cm 4 kwa wenye maumbile madogo, dawa hii imeboreshwa na hutibu matatizo haya kwa muda mfupi tu.
 
2/MAGOYE MVUTO- dawa hii ina uwezo mkubwa sana kumvuta na kumtuliza aliekuacha awe mpenzi, mme/mke itamfanya akutafute mwenyewe ndani ya masaa 3tu na kukutimizia mahitaji yako kwa haraka na kumfunga asiwe na mtu mwingine.
 
3/SUPER LUBEJA- ni dawa ya kushepu umbo no.8 mguu wa bia, kuongeza hips, na makalio kwa muda wa siku 5tu unapata saizi uipendayo, kuondoa makovu, chunusi, harufu mbaya ya mwili michirizi, kupunguza tumbo na maziwa kwa siku 6tu.
 
4/NG'WESHI MIX- ni dawa ya biashara ya kupata wateja wengi, kusafisha nyota, kurudishwa kazini na kupandishwa cheo, kurudisha mali iliyoibiwa au kudhurumiwa.
 
PIA TUNATIBU MAGONJWA SUGU KAMA: vidonda vya tumbo, ngiri, chango na uzazi kwa kina mama: (dawa zote hazina madhara kwa mtumiaji) HUDUMA HIZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO: TUNAPATIKANA DSM BUGURUNI SHELI AU PIGA SIM NO_ 0763-181099.

Waziri Tizeba, Mpina Matatani kwa Kutohudhuria Mkutano wa Rais IKULU

$
0
0
Waziri wa Kilimo, Dk Charles Tizeba na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina pamoja na Makatibu wao wameshindwa kuhudhuria mkutano wa 11 wa baraza la taifa la Biashara uliofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam na kuendeshwa na Rais Dkt Magufuli.

Katika mkutano huo Rais Magufuli aliwahitaji mawaziri hao ili waweze kutoa ufafanuzi kuhusu maswala ambayo yameibuliwa na wafanyabiashara, lakini mawaziri hao pamoja na Makatibu wao hawakufika licha ya kuwa walialikwa na kupaswa kuwepo kwenye mkutano huo.

Kufuatia kutokuwepo kwa viongozi hao, Rais Magufuli alimuuliza Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa) kama waliweza kuwaalika mawaziri hao na ndipo Waziri Mkuu alipojibu kuwa walipata mualiko na walipaswa kuwepo kwenye mkutano huo ingawa hakukuwa na taarifa yoyote ya wao kutokuwepo wala kutuma wawakilishi wao.

"Kwa hiyo wa Kilimo na Mifugo mawaziri na Makatibu wakuu wote hawapo?............Wao sio wajumbe wa mkutano huu? Alihoji Rais Magufuli ndipo Mawaziri Mkuu aliibuka na kutoa majibu kwa Rais Magufuli.

"Mawaziri wote wanaoguswa na sekta za uwekezaji na "kusupport" uchumi wetu wa viwanda, kilimo ni "facilitater" (msimamizi) wa viwanda na Mifugo naye pia ni wa viwanda walikuwa wapaswa kuwepo hapa kwa sababu walishapewa taarifa wote"

Hotuba ya Rais wa TFF alipozungumza na wahariri wa habari za michezo Jumatatu Machi 19-2018

$
0
0
Naomba nianze kwa kumshukuru mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukutana mahali hapa siku ya leo tukiwa wazima wa Afya,

Lakini pia nichukuwe nafasi hii kuishukuru Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dr.Joseph Pombe Magufuli kwa ushirikiano mkubwa ninaoupata katika uendeshaji wa mpira wa miguu, nimekuwa karibu sana na Serikali kuhakikisha juhudi zetu za kuendeleza mpira zinafanikiwa kwa kasi kubwa sana na mafanikio ya ujio wa Rais wa FIFA ni kielelezo cha karibuni kuonyesha ushirikiano mkubwa tunaoupata toka kwa Serikali hasa Waziri mwenye dhamana ya michezo Mh.Dr,Harrison Mwakyembe na timu yake.

Lakini niwashukuru kwa nafasi ya kipekee ndugu zangu Waandishi wa Habari kwa kazi kubwa mnayoifanya kuhabarisha umma kuhusu habari za mpira wa miguu,Pia pongezi zenu kwa kazi nzuri mliyoifanya wakati wa ujio wa FIFA, mlifanya kazi kubwa sana kutangaza ziara ya Rais wa FIFA, mmetupa heshima kubwa sana.

Ndugu zangu, leo nitaongelea mambo makubwa mawili ili waTanzania wapate kufahamu kinachoendelea katika mchezo wa mpira wa miguu hapa nchini.

Moja nitaongelea kuhusu mambo ambayo tumeyafanya kwa kipindi cha miezi saba nilichokuwepo madarakani lakini la pili ni mambo yanayoendelea sasa hivi kwenye Shirikisho.

MAMBO AMBAYO TUMEYAFANYA KWA MIEZI SABA TOKA TUINGIE MADARAKANI

HALI NA SHUGHULI ZA TAASISI
Kwa Mazingatio ya Utekelezaji Makini na wa Maendeleo wa Shughuli za Taasisi Tulitambulisha Muelekeo na Dira ya TFF ambapo Kazi iliyo Mbele yetu ni Kuzitoa na Kuimarisha Utambuzi na Utekelezaji wake. Sasa ni wakati Tunajiandaa Kutoa baadhi ya Mipango yetu na kutoa Dira za Utekelezaji wake. Pamoja na Mipango hiyo Bado TFF tumekuwa Tukitekeleza Shughuli za Mpira katika Mgawanyiko wake na labda kwa kifupi kugusia Miongoni mwake.

Mashindano.
Tumeendesha mashindano mbalimbali kwa ufanisi mkubwa yakiwemo mashindano ya Azam Sports Federation Cup, Ligi ndogo ya Wanawake kwa ajili ya kupata timu za kupanda daraja,Ligi Kuu ya Wanawake hatua ya makundi na hatua ya nane bora inayoendelea,Mashindano ya soka la ufukweni kwa timu za vyuo vikuu,Mashindano ya  kimataifa ya soka la ufukweni yajulikanayo COPA DAR ES SALAAM.

Azam Sports Federation cup;
Mashindano hayo kwa msimu huu 2017/18 tumeyaendesha kwa ufanisi na umakini mkubwa tofauti na huko nyuma kwa kuhakikisha upangaji wa ratiba umekuwa wa wazi usio na upendeleo wowote ule hivyo kupunguza malalamiko,jambo lingine tulihakikisha timu zote zinapata stahiki zao kwa wakati na kiwango kilichopangwa,kadiri tunavyoelekea hatua za mwisho wa mashindano tutahakikisha changamoto zote zilizojitokeza huko nyuma tunakabiliana nazo na kuzitatua ili kuhakikisha mashindano hayo yanaisha vizuri.

Ligi kuu ya Wanawake;
Mwaka huu tulianza kucheza Ligi ndogo ya Wanawake kutafuta timu za kupanda Ligi Kuu ya Wanawake katika vituo vya Dar es salaam na Dodoma,ikafuatiwa na Ligi ya Wanawake katika kituo cha Arusha na Dar es Salaam ili kupata Timu 8 za kucheza hatua ya Nane bora ya Ligi hiyo.

Katika hatua ya makundi, TFF ilizigharamia timu zote kwa asilimia 100 kuanzia malazi, usafiri, chakula, gharama za maadalizi ya timu na nauli ya kwenda na kurudi,ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya mpira wa miguu wa Wanawake kwa TFF kugharamia kwa kiwango hiki.

Katika hatua ya Nane bora ya  Serengeti Lite Women Premier League vilabu vyote vilishapewa fedha zao kwa ajili ya hatua ya kwanza ambayo imesimama kupisha maandalizi ya timu ya Taifa ya Wanawake(Twiga Stars) ambayo inajiandaa na mashindano ya kufuzu michuano ya Afrika kwa Wanawake ambapo tayari timu ya Taifa ipo kambini ikijiandaa na mchezo huo dhidi ya Zambia.

Taasisi iliendesha kwa mafanikio makubwa mashindano ya soka la ufukweni (Copa Dar es Salaam) kwa kuzialika timu za Uganda, Malawi, Zanzibar na wenyeji Tanzania bara ambazo tulizigharamia malazi, chakula na usafiri wa ndani.

PROGRAMU ZA TIMU ZA TAIFA
Toka tumeingia madarakani, tumekuwa tunafanyia kazi program mbalimbali za maendeleo ya Timu za Taifa.

Taifa Stars
Tumekuwa tukiendelea na program mbalimbali za Timu ya Taifa za kuhakikisha inafuzu Fainali za kombe la mataifa Afrika 2019.

Kuhakikisha hili Taifa Stars ilicheza na Benin, Malawi, Botswana na wiki hii tunacheza na Algeria pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) katika kalenda ya mechi za kimataifa ya FIFA.

Ili kuongeza hamasa ya wachezaji tumeongeza posho ya ndani kwa asilimia 100 na asilimia 50 kwa posho za nje.

Kilimanjaro Stars
Timu yetu ya Tanzania bara ilishiriki mashindano ya CECAFA yaliyofanyika nchini Kenya mwezi Desemba 2017, mbali na kushiriki ili ichukuwe kombe sababu nyingine ilikuwa ni kuendelea kupata mechi nyingi za kimataifa.

Timu ilicheza dhidi ya Rwanda, Kenya, Zanzibar na Libya, Tunaamini kwa wachezaji vijana waliokuwa sehemu ya kikosi hicho imewajengea uwezo katika soka la kimataifa.

Timu za Taifa za Vijana
Katika eneo hili  tumekuwa na mpango wa muda mrefu kuhakikisha vijana wa timu zetu za Taifa za miaka chini ya 23, 20, 17 na 13 zinakuwa na maandalizi bora na kwa kuanzia toka tuingie madarakani tumekuwa na kambi za timu za vijana kila mwezi kwa kuwakutanisha siku 14 za mazoezi na kuwatafutia mechi za kirafiki za kimataifa.

Timu ya U23
Timu ya Taifa chini ya miaka 23 ambayo ni kikosi cha pili cha timu ya Taifa kimeshaitwa kambini mara kadhaa na tumethibitisha kushiriki mashindano ya Olimpiki ambayo fainali zake zitafanyika nchini  Japan, lengo ikiwa ni kuhakikisha tunawapatia vijana hawa mechi nyingi za kimataifa ili wawe tayari.

Timu ya Vijana U20
Timu ya Vijana U20 ambapo jana ilicheza na Morocco na Jumatano itacheza na Msumbiji, ikiwa ni maandalizi ya mechi dhidi ya timu ya vijana chini ya miaka 20 ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Congo(DRC) ikiwa ni mchezo wa kufuzu fainali za Vijana Afrika chini ya miaka 20.

Timu ya Vijana U16
Timu hii nayo imekuwa ikiingia kambini kila mwezi na hata sasa hivi ninavyozungumza na nyinyi, timu hii ipo kambini ikijiandaa kwa mashindano ya CECAFA na tunafanya jitihada za kuhakikisha inapata mechi mbili za kirafiki za kimataifa kabla haijaenda Burundi.

Timu hii ndiyo ambayo itashiriki fainali za Afrika chini ya miaka 17 zitakazofanyika hapa nchini mwaka 2019.

Baada ya kutoka Burundi itakuwa na program maalum kwa ajili ya kujiandaa kwa mashindano mengine ya kufuzu AFCON U17, 2019 ambayo yatafanyika nchini mwezi Agosti ambayo lengo ni kupata mwakilishi wa CECAFA na vijana wetu watashiriki kama wenyeji. TFF imeamua kushirikisha Timu yenye Umri mdogo zaidi kwa u17 bila ya kujali Matokeo zaidi ya Ujenzi wa timu kwa kuandaa timu moja katika matukio yote haya ili kuiweka tayari kwa Mashindano ya u17 ya 2019 mwakani ambapo vijana hawa ndio watakuwa rasmi u17

Timu ya Vijana ya U13
Timu ya Vijana ya U13 katika kutafuta namna ya Kuwaimarisha vijana  hawa baada ya Utambuzi na Uteuzi wa timu imepata nafasi ya  kushiriki mashindano ya kirafiki ya vijana chini ya miaka 13 yatakayofanyika nchini Ubelgiji mwezi Agosti 2018,Tayari orodha ya kwanza ya wachezaji 69  waliopatikana katika mashindano ya shule za msingi (UMITASHUMITA) ipo TFF na idara ya ufundi inaandaa utaratibu wa kuwaita pamoja na kupata michezo ya kirafiki dhidi ya Zanzibar kwa ajili ya kupata kikosi cha pamoja cha Tanzania.

Timu ya Taifa ya Wanawake U20
Tumeanza kuandaa kikosi cha Vijana cha timu ya taifa ya Wanawake U20 ili kuwa na kikosi bora cha Twiga Stars kilichoandaliwa kwa muda mrefu na tayari ilishacheza michuano ya kufuzu fainali za vijana za Afrika chini ya miaka 20 na kutolewa na Nigeria.

Baadhi ya wachezaji wa timu hii wamepandishwa kikosi cha wakubwa na sehemu kubwa wanacheza Ligi Kuu ya Wanawake kupitia vilabu mbalimbali.

Tutaendelea na utaratibu wa kuwaita kambini kila wakati kutakapokuwa na nafasi ili kuzidi kuimarisha kikosi.

Twiga Stars
Kikosi cha Twiga Stars kimeingia kambini kwaajili ya maandalizi ya mashindano ya kufuzu fainali za Africa kwa Wanawake zitakazofanyika nchini Ghana baadaye mwaka huu.

Twiga Stars inakabiliwa na mchezo dhidi ya Timu ya Taifa ya Zambia utakaochezwa Aprili 4,2018 Uwanja wa Taifa na marudiano kuwa Aprili 8,2018 nchini Zambia.

MAPATO NA MATUMIZI

MAPATO
Katika kipindi cha miezi Saba(7),Shirikisho limefanikiwa kukusanya kiasi cha Tzs 3,670,397,199.00 kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali  ambavyo ni pamoja na mapato kutoka kwa wadhamini Tzs 2,295,472,151 sawa na 62.5%ya mapato yote, makusanyo ya viingilio uwanjani Tzs 378,139,866 sawa na10.3%. 27.2% ilitokana na Fedha kutoka CAF na FIFA.

MATUMIZI
Katika kipindi hiki Shirikisho lilitumia kiasi cha Tzs 3,752,001,171.00. Sehemu kubwa ya matumizi yalielekezwa kwenye usimamizi wa ligi mbalimbali pamoja na kuandaa timu za taifa ambapo jumla ya Tzs 2,409,150,732 sawa na 64% ya matumizi yote zilitumika.

Asilimia 36 ya Fedha zilizobaki ilitumika kulipia madeni ya Taasisi, Kulipa mishahara ya wafanyakazi, kusaidia mikoa katika maeneo ya miundo mbinu, kuwajengea uwezo wafanyakazi pamoja na kuendesha mafunzo mbalimbali.

Kama Rais wa TFF sijapokea HOJA wala USHAURI wala MAPENDEKEZO yoyote kutoka kwa Wajumbe wangu katika Ngazi zote kuhusiana na Matumizi ya Taasisi, Nasikitika kama kuna anayedai amehoji sijui wapi kwa kuwa kama Rais sijapokea hoja yoyote wala kuwasilishwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji iliyopita ambayo Taarifa ya Kamati ya Fedha iliwasilishwa nakupokelewa na kupitishwa na Kamati ya Utendaji.

MADENI
Katika kipindi hiki,Shirikisho lilianza zoezi la kutathmini madeni iliyoyarithi kutoka kwenye Uongozi uliopita, ambapo deni hilo linafikia Tzs 2,172,000,000linalodaiwa na watoa huduma mbalimbali, wafanyakazi,wachezaji na makocha.

Asilimia kubwa ya deni hili lilitokana na malimbikizo ya deni la TRA, Workers Compensation Fund na NSSF ambalo lililimbikizwa kwa zaidi ya miaka miwili.

Shirikisho lilifanikiwa kulipa deni lote la michango ya wafanyakazi NSSF jumla ya Tzs 88,000,000 zilizokuwa hazijalipwa kipindi cha miaka miwili, na lilifanya majadiliano na Mamlaka ya Mapato Tanzania kuhusu ulipaji deni la kodi linalofikia Tzs 1,077,000,000, ambapo jumla ya Tzs 315,000,000 zimelipwa nakiasi kilichobaki tumekubaliana kitalipwa kwa awamu kadhaa mpaka deni lote litakapomalizika.

Pia shirikisho limefanikiwa kupunguza mishahara kwa wafanyakazi kutoka Tzs  85,063,092.00 mpaka kufikia 50,000,000.00 baada ya kupunguza idadi ya wafanyakazi kutoka 44 mpaka 21.

Baada ya kuingia madarakani tulifanya majadiliano na makocha wa timu za Taifa kuhusu uhalisia wa malipo yao na kufanikiwa kuokoa zaidi ya dola laki mbili(USD 200,000) kwenye mikataba yao na fedha zilizookolewa zitasaidia shughuli nyingine za mpira wa miguu.

UFUNDI
1. Kliniki iliyoendeshwa na Kocha PiaSundhage kutoka Sweden

2. Kozi ya ngazi ya awali ya makocha wa mpira wa miguu

ilifanyika katika mikoa ya Kigoma,Songwe, Lindi, Morogoro na Pwani

3. Kozi ya ngazi ya kati ya makocha wa mpira wa miguu

  Ilifanyika katika mikoa ya Kigoma mara mbili, Manyara na Morogoro.

4.Grassroot & Live your goal project

Kozi hii ilifanyika katika mikoa ya Lindi ambapo washiriki walitoka katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

 Pia kozi nyingine ilifanyika katika mkoa wa Mbeya ambapo washiriki walikuwa ni kutoka katika mikoa ya Mbeya, Njombe, Katavi, Songwe na Rukwa

Aidha hii kozi ilifanyika Kigoma na kushirikisha washiriki wa mikoa ya Kigoma na Tabora.

5.Mafunzo ya awali ya Utawala mikoani

 Kuna kozi ya utawala na masoko iliyofanyika Dar es Salaam ili kuwaongezea watu wa masoko uwezo wa kuwavutia wadhamini.

6.Mafunzo ya waamuzi

  Mafunzo ya waamuzi wa FIFA na Waamuzi wa ngazi ya juu yalifanyika mara tatu jijini Dar es Salaam.

7. Kozi ya kupandisha daraja kwa Waamuzi

Kozi hii ilifanyika mara mbili katika mikoa ya Dar es Salaam na Mwanza.

8. Ziara za Mafunzo na kubadilishana uzoefu

 Zilifanyika ziara mbalimbali za Waamuzi wetu za kubadilishana uzoefu katika nchi mbalimbali.

9. Mpango wa ugawaji wa vifaa vya vijana na mafunzo

Tulipoingia madarakani tulikuta uongozi uliopita wameshanunua mipira na imekaa stoo, katika kutekeleza azma ya maendeleo ya vijana ili tuwe na timu za Taifa imara Shirikisho limegawa mipira (100 kwa kila Mkoa) saizi 4 na 3 kwa Mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar, Mikoa imepewa vifaa vya kufundishia (cones and markers) ili vijana wapate fursa ya kuonesha na kuendeleza vipaji vyao kwa maslahi ya Mpira hapa nchini.

Uzinduzi wa zoezi hili ambalo linategemewa kuwa endelevu lilifanyika Uwanja wa Taifa Agosti 3, 2017.

Rais wa TFF aliwakabidhi wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa niaba ya Mikoa yao kwenye Kanda husika, Kwa upande wa Zanzibar Katibu Mkuu wa ZFA alikabidhiwa mipira hiyo kwa ajili ya Mikoa ya Zanzibar.

MASOKO NA HABARI
Tumeendelea kuongeza wadhamini katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha Taasisi inanufaika na bidhaa zake.Lakini pia tumeendelea kuimarisha idara ya habari kwa kuwanunulia nyezo za kufanyia kazi.

UTAWALA BORA
Katika kipindi hiki cha Miezi saba nimesimamia eneo hili kwa uadilifu mkubwa, Kamati zimekuwa zinakutana kabla ya vikao vya Kamati ya Utendaji ili kuhakikisha kila mmoja anashirikishwa.

Mfano, Wakati nilipokuwa mwenyekiti wa Kamati ya Fedha,kwa miaka 4 nilikaa kikao kimoja cha Kamati ya Fedha,Katika Utawala wangu aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha ndani ya miezi saba ameitisha vikao visivyopungua vitano.

Nilimuagiza Kaimu Katibu Mkuu kuhakikisha kila Kamati ya Fedha inapohitaji kukutana ahakikishe inakutana na Mtendaji Mkuu amekuwa anatekeleza.

Na kwa sababu nafasi ya Makamu wa Raisi Kikatiba ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Mipango, basi hata mazungumzo ya Mkataba wa Udhamini wa Ligi Kuu msimu 2018/2019 yeye ndiye aliyekuwa anasimamia.

Nimekuwa nafanya hivi ili Taasisi iendeshwe kwa uwazi na kushirikisha kila mmoja,Na nimeendelea kusisitiza kuwa mapato ya matumizi ya Taasisi yatatolewa kwenye vyombo vya Habari ili yawe wazi kwa umma.

SEKRETARIETI YA TFF
Toka tuanze kuunda sekretarieti tumeajiri Wakurugenzi Watatu na Meneja mmoja na wote hawa waliajiriwa na Kamati ya Utendaji, Ofisi ya Katibu Mkuu haijawahi kuajiri mfanyakazi hata mmoja kufikia sasa.

Nafasi ambayo haijajazwa ni nafasi ya Katibu Mkuu ambako Ndugu Kidao Wilfred bado anakaimu.

Kwanza nikiri kazi nzuri inayofanywa na mtendaji mkuu aliyekuwepo katika kuhakikisha Taasisi inapiga hatua kwa kasi kila ninapokutana na watendaji wakuu wa FIFA, CAF na CECAFA wamekuwa hawasiti kunimwagia sifa kwa kuwa na sekretarieti mahiri iliyobadilika katika kufanyia kazi changamoto za Taasisi.

Raisi wa FIFA alisema anaona mabadiliko makubwa ya hatua tunazochukuwa, Lakini Katibu Mkuu wa FIFA alisema nina Sekretarieti ya Vijana wenye hali, nguvu na maono ya kuipeleka Taasisi mbele huo ndio ujumbe wao.

Nimeyasema haya kuwahakikishia nikiwa msimamizi wa sekretarieti, mambo yote ambayo Kaimu Katibu Mkuu amekuwa akiyafanya ni maelekezo yangu au utekelezaji wa maamuzi halali ya kamati ya Utendaji, Kwahiyo nichukuwe fursa hii kupongeza kasi ya sekretarieti katika kusimamia mambo mbalimbali.

 AJIRA
Katika kipindi changu cha uongozi (Kamati ya Utendaji) kwa kushirikiana na ofisi ya Katibu Mkuu tumeweza kupunguza wafanyakazi kutoka Wafanyakazi 44 tuliowakuta wakati naingia madarakani hadi kufikia 21,Ni hatua kubwa na tunafanya upembuzi makini kabla hatujaanza kuajiri watu tuwe na mahitaji stahiki.

KATIBU MKUU
Kumekuwa na maneno mengi juu ya nafasi ya Katibu Mkuu wa Shirikisho, Ndugu zangu wakati naanza kazi niliona ni muhimu nafasi hii ikaimishwe kwa mtu anayelijua shirikisho vizuri na ambaye sina shaka na uwezo wake,Sifa zote hizi alikuwanazo KIDAO WILFRED na wajumbe wa Kamati ya utendaji chombo ambacho kinahusika nakupitisha kilibariki awe Kaimu Katibui MKuu.

Kutoka nje ya Ofisi na kukaimu hii siyo mara ya kwanza,wakati Ndugu Tenga anashinda Uraisi alimuomba Bi.Lina Kessy ambaye alikuwa mtumishi wa Serikali kuwa Mratibu wa Ofisi, nafasi iliyokuwa kama Mkuu wa sekretarieti wakati huo.

Hata wenzetu wa CAF, Rais ndiye anayepeleka jina bila kujali Mchakato utakavyokuwa kwa maana wanaweza wakatangaza au wasitangaze,na hata Katiba ya TFF inahitaji Rais wa TFF atoe mapendekezo ya Katibu Mkuu ili Kamati ya Utendaji ijadili, haya yanafanyika kwa sababu Rais kama msimamizi wa Sekretarieti anafanya kazi kwa karibu sana na Katibu Mkuu hivyo FIFA wanahitaji watu hawa  wawe wanaoweza kufanya kazi kwa karibu sana,ndipo Rais wa TFF anapopewa kipaumbele cha mtu wa kufanya naye kazi kwakuwa ndio nguzo ya Taasisi kwakuwa Rais ndio mkuu wa Taasisi na Katibu Mkuu ndio mkuu wa Sekretarieti.

Lakini pamoja na yote hayo bado nilikuwa napeleka ajenda ya Ajira kwenye Kamati ya Utendaji ili kushauriana njia bora ya kupata Katibu Mkuu kwa maslahi mapana ya Mpira wa Miguu na siyo mtu.

Niwahakikishie kikao kijacho cha kamati ya Utendaji kitaamua njia sahihi ya kupata Katibu Mkuu na tutahakikisha tunakuwa na Katibu Mkuu ndani ya muda mfupi ujao.  

Mipango Mbalimbali
Tumekuwa katika Ujenzi wa Mipango Mbalimbali kama nilivyoainisha kwenye Ilani yangu ambapo Katibu Mkuu amekuwa Kiungo muhimu katika kunisaidia kwenye Ujenzi wa Mipango yangu hiyo lakini kwa bahati Mbaya Kaimu Katibu Mkuu Kidao amekuwa kwenye wakati mgumu kutokana na kuandamwa na Maneno na Vitendo vinavyolenga na kufanikisha kumkwamisha na kumkosesha mazingira bora na rahisi ya kufanyia kazi zake na hivyo imekuwa ni atahri kwa TFF kwa Baadhi ya Mipango yake kuwa inakwama kutoka Mpaka sasa na hiyo ni athari kwa Mpira wetu kwa Ujumla.

Ndugu zangu jambo la pili ambalo nimeona niligusie ni jinsi vyombo vya maamuzi vya TFF vinavyofanya kazi,

Ndugu waandishi, TFF inafanya kazi kwa mujibu wa Katiba yake ya mwaka 2013 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2015. Katiba hii inataja Kamati ya Utendaji itaundwa na Wajumbe wafuatao;

1. Rais

2. Makamu wa Rais

3. Wajumbe 13 kutoka kanda zilizotajwa ibara 32 ya katiba ambazo ni Kanda namba 1-Kagera na Geita

Kanda namba 2- Mara na Mwanza

Kanda namba 3- Shinyanga na Simiyu

Kanda namba 4- Arusha na Manyara

Kanda namba 5- Kigoma na Tabora

Kanda namba 6- Katavi na Rukwa

Kanda namba 7- Mbeya, Iringa na Songwe

Kanda namba 8- Njombe na Ruvuma

Kanda namba 9- Lindi na Mtwara

Kmada namba 10- Dodoma na Singida

Kanda namba 11- Pwani na Morogoro

Kanda namba 12- Kilimanjaro na Tanga

Kanda namba 13- Dar es Salaam

4. Wajumbe wawili wanowakilisha vilabu vya Ligi Kuu

5.Mwenyekiti wa Chama cha Soka ya Wanawake.

6. Mwenyekiti wa Kamati ya Tiba

7. Wajumbe wawili wa kuteuliwa na Rais wa TFF.

Rais wa TFF amepewa nafasi za kuteua wajumbe wawili wa kamati ya Utendaji ili kumsaidia kufanya kazi na watu ambao wanajua muelekeo wake lakini ambao anaamini watamsaidia kwenye maeneo mbalimbali katika Taasisi.

Kamati ya Utendaji inafanya kazi na vyombo mbalimbali ambavyo ni Kamati ndogondogo, Bodi ya Ligi na Kamati za Kisheria pamoja na Kamati za Uchaguzi.

Kamati Ndogondogo;
  1.     Fedha na Mipango
  2.     Mashindano(Kamati ya Tuzo na Soka la Ufukweni)
  3.     Ufundi na Maendeleo
  4.     Vijana
  5.     Wanawake
  6.     Waamuzi
  7.     Katiba, Sheria, na Hadhi za wachezaji.
  8.     Tiba
  9.     Ukaguzi (ambayo yenyewe ni kama Kamati huru)
    Kamati za Kisheria;
  1.    Nidhamu
  2.     Rufani ya Nidhamu
  3.     Maadili
  4.     Rufani ya Maadili
Kamati za Uchaguzi;
  1.     Uchaguzi
  2.     Rufani ya Uchaguzi
Ufanyaji wa kazi wa Kamati hizi umeelezewa katika Katiba ya TFF kwa maana Kamti za Kisheria zinajitegemea huwa haziingiliwi kwenye maamuzi yake.Ingawa vikao vyake vyote huwa vinaratibiwa na ofisi ya Katibu Mkuu.

Kwahiyo maamuzi ya Kamati hizi huwa ni ya kujitegemea hivyo watu wote ambao wamekuwa wanahukumiwa na Kamati hizi ni vyema wakawa wanajua utaratibu wa Kamati zinavyofanya kazi.Na mimi binafsi nimeendelea kuheshimu Kamati zifanye kazi bila kuingiliwa na mtu yoyote vile.

Ndiyo maana wakati nachaguliwa niliahidi kusimamia Taasisi kwa uadilifu mkubwa bila kumuonea aibu mtu yeyote, wala kumuogopa mtu na hii ni katika kuunga mkono juhudi za Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ya kupambana na uchafu  wa aina zote katika serikali,Nami nimeamua kusafisha Taasisi kama nilivyoahidi wakati wa Kampeni za uchaguzi ulioniweka madarakani,niseme wazi hakuna mtu asiye muadilifu atabaki katika mpira,Na nimpongeze  Kaimu Katibu Mkuu wangu kwa kusimamia kwa ujasiri mkubwa usimamiaji wa maagizo yote halali ya Kamati mbalimbali,Amekuwa anasimamia bila uoga bila kujali anavyosakamwa kwangu linanipa faraja sana.

Tumekuwa tunachukuwa hatua katika kila eneo tumeshaanza kuchukuwa hatua kwa wizi wa Mapato ya milangoni, kuna viongozi wamefungiwa,hatukuishia hapo tayari viongozi walioghushi leseni za usajili wamefungiwa,Hiyo yote ikiwa ni kuonesha sina masihara hata kidogo kwenye kuhakikisha mpira unakuwa sehemu ya watu waadilifu.

FIFA walituma Timu ya Uchunguzi(Investigation Team) kuangalia yale yote yaliyofanyika toka mwaka 2013 mpaka mwaka 2017,Timu ilikaa nchini kwa takribani wiki mbili ikifanya kazi kwa karibu na Ofisi ya Katibu Mkuu,Yaliyogundulika yameacha doa kubwa na walitoa Ripoti na Maelekezo ya mambo ya kuyafanyia kazi na ya kuchukulia hatua.

Masharti yote haya yaliambatana na kuzuiwa kwa fedha zetu za miradi nia na wenzetu wachache, Lakini tumekosa pesa zinazoitwa Operation Cost ikiwa ni shinikizo la Dola Milioni Tatu ambazo tulipaswa kulipwa toka mwaka 2015-2018.

Karibia nchi zote Duniani zimenufaika kwa kupata pesa hizi, isipokuwa Tanza kuhakikisha tunatekeleza masharti ya FIFA, Hivyo tulipopata ripoti tumeamua kutekeleza kwa asilimia mia moja maagizo yote ya FIFA. Haya yanayotokea ni Miongoni mwa Matokeo ya Utekelezaji wa Taarifa za Wakaguzi wa TFF na Wakaguzi na Timu ya Uchunguzi kutoka FIFA. Jambo hili limepitia Hatua stahiki kwa Mujibu wa Taratibu zinazohusiana na Taarifa za kiUkaguzi na wahusika wameshirikishwa ipasavyo na Utetezi wao walipeleka kwenye Kamati husika ya Ukaguzi miezi iliyopita baada ya kutakiwa kufanya hivyo kwa mujibu wa taratibu.

Niseme tu unaposafisha Taasisi kuna gharama zake TFF inahitaji Kuungwa Mkono zaidi kwa Hatua Madhubuti inazochukua za Kujisafisha na Kusonga Mbele.

Katika VITA hii ya Kupambana na Udhalimu kwenye Mpira wetu Hatutarudi Nyuma, Tutapambana bila hofu wala woga almuradi Hakuna dhulma wala Uonevu wala Upendeleo kwa yeyote. Na Nitoe wito kama kuna Kiongozi au Mdau yoyote anayejua ana Pesa za TFF kinyume cha Utaratibu Natoa WITO Ajisalimishe Mwenyewe.

Ahsanteni kwa kunisikiliza naamini mtaniunga mkono ili kuusogeza mbele Mpira wa Tanzania.

Mwisho niwakumbushe TFF inaendelea na maandaalizi ya Matayarisho wa AFCON U 17,2019 .Timu ya ukaguzi ya CAF itakuja mwezi wa Tano, tumekuwa tunalifanyia kazi kwa ukaribu  na serikali kuhakikisha changamoto za viwanja vitavyochezea mashindano pamoja na viwanja vya mazoezi vinakuwa tayari kwa wakati.Tutaendelea kulitolea ufafanuzi kila wakati.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Wafungwa Kupewa Mafunzo Ya Ujasiriamali Huko Gerezani Ili Kuwasaidia Kubaini Fursa Mbalimbali za Kiuchumi

$
0
0
Na Lucas Mboje, Jeshi la Magereza;
Jeshi la Magereza limetiliana saini makubaliano na Asasi ya TECHNOSERVE katika kuendesha  mafunzo ya ujasiriamali kwa wafungwa vijana wenye umri wa kati ya miaka 18 hadi 30 waliopo magerezani katika Mikoa ya nyanda za juu Kusini ikiwemo Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe, Ruvuma, Katavi na Rukwa.

Hafla ya kutiliana saini makubaliano hayo imefanyika katika Ofisi za Makako Makuu ya Jeshi la Magereza jijini Dar es Salaam na Asasi ya TECHNOSERVE iliwakilishwa na Afisa wake Bw. Monsiapile Kajimbwa.

Akizungumza baada ya kutiliana saini makubaliano hayo, Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa amesema kuwa mafunzo hayo ya ujasiriamali yatawapa uwezo wafungwa wa kubaini na kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi ikiwemo uwezo wa kubuni na kuandaa mipango ya biashara.

“Mafunzo haya yatawanufaisha sana wafungwa waliopo magerezani katika mikoa hiyo kwani yatawajengea uwezo wa kujitambua pamoja na kujipatia vipato halali badala ya kutenda uhalifu katika jamii.” Alisema Jenerali Malewa.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yatafanyika katika Chuo cha Ufundi cha Magereza Ruanda kilichopo Mkoa wa Mbeya ambapo wafungwa watajifunza nadharia na vitendo katika dhana nzima ya ujasiriamali ikiwemo stadi za utengenezaji sabuni, ushonaji, useremala, ufumaji sambamba na uandaaji wa mipango ya kibiashara.

Meneja Mkazi wa Asasi ya TECHNOSERVE, Bw. Monsiapile Kajimbwa amesema kuwa hatua ya kutiliana saini makubalino hayo ni kuimarisha ushirikiano kati ya Asasi yake na Jeshi la Magereza katika kutoa mafunzo kwa wafungwa ili waweze kupata ujuzi kupitia program hiyo.

Dira ya Jeshi la Magereza ni kuwa Jeshi la kurekebisha wahalifu lenye utaalam wa hali ya juu linaloendeshwa katika kanuni na viwango vilivyowekwa Kitaifa na Kimataifa.

Viwanda HEWA Vya Sukari Vyamkera Rais Magufuli

$
0
0
Rais John Magufuli amesema matokeo ya uchunguzi uliofanywa na kamati yake teule yamebaini kuwapo viwanda hewa vilivyokuwa vinaagiza sukari ya viwandani.

Amesema Machi 15, mwaka huu amepokea ripoti hiyo yenye idadi ya viwanda 30 huku viwanda vinane tu ndiyo vikibainika kuwa na taarifa za kweli katika uagizaji wa sukari.

Kampuni hizo nane ni ASB, Nyanza Bottlers, Bonite Bottlers Ltd, Bakhresa Group of Companies, Kazman Group, Lakailo Company, ANB Group na Kampuni ya Super ASB.

Rais Magufuli alibainisha hayo jana wakati wa Mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) uliofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, yeye akiwa mwenyekiti wake.

"Niliunda kamati maalum ya kufuatilia suala la uagizaji wa sukari kutoka nje, nimepokea ripoti Machi 15, mwaka huu (Alhamisi)," alisema Rais Magufuli. "Kilichobainika humo kinasikitisha sana, kampuni zaidi ya 22 zilikuwa zinaagiza sukari kwa manufaa yao."

Rais Magufuli alisema kamati hiyo imebaini kuwa kampuni hizo 22 zilikuwa zinaagiza sukari kuliko mahitaji yao halisi waliyokuwa wanayahitaji.

Rais Magufuli alitolea mfano wa kampuni ya Iringa Food Products iliyokuwa imeagiza tani 300 wakati mahitaji yake ni tani 190.

Alisema kuna kampuni ya Dabaga ilikuwa inaagiza  tani 2,000 wakati mahitaji halisi ni tani 1,600. Alisema kuna viwanda vimekuwa vikiagiza sukari ya viwandani lakini huibadilisha kuwa ya matumizi ya binadamu badaye.

Sukari ya viwandani kutoka nje ya nchi ina unafuu mkubwa wa kodi ya forodha kulinganisha na ile ya kawaida.

Mwenyekiti huyo wa TBNC alitoa takwimu hizo ikiwa ni malalamiko yake kwa sekta binafsi ambayo awali ilikuwa imeorodhesha kero mbalimbali za upande wa serikali zilizopo katika biashara na uwekezaji nchini.

Rais Magufuli alisema kuna baadhi ya viwanda bado havijajengwa lakini wamiliki wake wamekuwa wakiagiza hadi tani 500 na kueleza kuwa wahusika wote waliobainika wataandikiwa barua.

"Kuna kiwanda kinaitwa Maisha Bottlers kiliagiza tani za sukari 7,000 kikieleza kiko Mbeya," alisema mwenyekiti huyo, "lakini kamati (ya uchunguzi) imeenda Mbeya, imekitafuta, haijakiona."Hii ripoti nitamkabidhi Waziri Mkuu aipitie na achukue hatua."

Alisema suala la sukari limekuwa likiwaweka watu wengi matatani wakiwamo mawaziri wa tangu utawala wa Rais wa tatu, Benjamini Mkapa (1995-2005).

Alisema mahitaji ya sukari nchini ni tani 590 kwa mwaka, ambapo tani 455 ni kwa matumizi ya nyumbani na tani 135 kwa matumizi ya viwandani.

Aliongeza kuwa kwa sasa kuna upungufu wa tani 130 kwa sukari ya kula na tani 135 kwa matumizi ya viwandani.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Mange Kimambi Ampa Makavu Wemasepetu Kisa Diamond

$
0
0
Mwanaharakati wa siasa mtandaoni Mange Kimambi ameibuka na kumwagia matusi mazito msanii wa Bongo movie Wema Sepetu baada ya kuzua maneno maneno jana kwenye mtandao wa Instagram.

Siku ya jana Wema alishika headlines za mitandao ya kijamii baada ya kuposti posti kadhaa zilizoamsha tetesi kuwa amerudiana na Diamond na alizidi kuzua maneno baada ya kuonekana akiwa na Esma huku wakiitana wifi.

Sio siri kuwa Wema na Mange wapo kwenye bifu kali tangu Wema afanye uamuzi wa kurudi CCM mapema mwaka jana akitokea Chadema na hata kuanzisha urafiki na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam jambo ambalo halikumfurahisha Mange.

Siku ya jana Mange amemtolea povu zito Wema na kumtuhumu anatumika kuleta drama zake na Diamond ilimradi wazime amsha amsha za maandamano na kudai amegeuzwa Jinga na familia ya Diamond.

Kupitia ukurasa wake Instagram, hili ndio povu la Mange kwa Wema:

"...........Wema mj***ga sana, mtu gani kutwa anatafuta attention za watu kwa mambo ya kijinga? Forever my wii my foot mbona Bi. Tukinao alivyokuwa nao mbona hawakukuita forever my wii? 

"Yamewashinda kwa mganda ndio wamelikumbuka jinga lao. Janamke j*nga halikui from CEO wa Endless Fame to mfanyakazi wa Wasafi Tv? 

"Seriously wenzake wanasonga mbele lenyewe linarudi nyuma. Halafu hata halijistukii linaongea proudly kabisa “Sasa Diamond anaenda kuwa bossi wangu” from kuwa CEO mpaka kuwa mfanyakazi wa Diamond kama wakina Kifesi?”.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images